Saturday, November 10, 2012

NANI KAMA MAMA?PART-1

Asalaam Aleiykum,

Leo wacha nikuchukue tuingie katika Dunia ya Mama, Kwanini nikasema tunaingia, nimesema tunaingia kwa sababu dunia ya mama ni ulimwengu wa ajabu, na wanaadamu desturi zetu ukishazaliwa, ukalelewa kwa mapenzi basi unakuwa huna haja ya kutizama nyuma au kwa maana nyengine hutaki kujua mahusiano yako na wazee hawa wawili. Zawadi hii adhimu hutaki kuijua, ila unaicha iendelee (Automatic), na hiyo (automatic)huenda ikafikia pahala inaharibika, inakua haifanyi kazi tena na hapo ndipo mahusiano yako na wazee wako wawili yanaanza kutetereka.
Sasa ikifikia hali kama hiyo ndio inatubidi tutembelee tena ndani ya Quraan-aya-ya-14-Luqman, ipate kutukumbusha,
"وَوَصَّيۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ بِوَٲلِدَيۡهِ حَمَلَتۡهُ أُمُّهُ ۥ وَهۡنًا عَلَىٰ وَهۡنٍ۬ وَفِصَـٰلُهُ ۥ فِى عَامَيۡنِ أَنِ ٱشۡڪُرۡ لِى وَلِوَٲلِدَيۡكَ إِلَىَّ ٱلۡمَصِيرُ "
"Tumemuusia Mwanaadamu(Kuhusiana na kuwafanyia wema)Wazazi wako, Mama amechukua mimba(yako)kwa udhaifu juu ya udhaifu, na kumwachisha kunyonya baada ya miaka miwili,(basi)Nishukuru mimi na wazazi wako,ni kwangu mimi marejeo yenu"
Nilipoanza hapo juu nilitaja neno (Automatic)kusudio langu ni kueleza huo wasia ambao umo ndani ya jinsi(Being)yako, imeshaumbiwa ufahamu huu wa kuwafanyia wema wazee wao kama kuishi nao kwa uzuri na mapenzi, hii kwa wazee wako inakuja (Automatic)sio kwamba anakuja mtu kukuweka chini na kuanza kukupa wasia, ikiwa mtu atafanya hivyo elewa hizo ni taratibu zake au uzoefu wake, lakini wasia kutoka kwa Mollah wako unatokea ndani ya (Roho)yako ndio maana utajiona unawaonea huruma, imani, nk. Lakini aya imekwenda mbele ikakumbusha nishukuru mimi (Mollah)wako ikisha na wazee wako wawili, Hapa ndipo nikasema hebu tutizame nyuma, tuingie katika hii dunia ya Mama vipi kachukua mimba kwa udhaifu juu ya udhaifu, ukisha kuyajua hayo hapo pengine shukurani yako ya dhati itatokea moyoni.
Ili shukurani hiyo ikuporomoshe kwa maneno na vitendo, isije ukawa unaitoa shukurani hiyo huku umeshika kiuno huku unamtuma mama yako akuletee maji ya kunywa.
Nani kama Mama?
"Alikuja Mtu siku moja kwa Bwana Mtume s.a.w akamuuliza"Ewe Mjumbe wa Mwenye-enzi-Mungu, Nani Katika wanaadamu anastahiki awe kipenzi changu,(Nimfanye kuwa rafiki yangu)nimfanyie ihsani nimpe na mapenzi?Akajibu Bwana Mtume s.a.w "Mama yako,yule mtu akasema ikisha, Bwana Mtume s.a.w akasema tena Mama yako,yule mtu akasema halafu,Bwana Mtume akamwambia Mama yako, na Mara ya Nne akamwambia Baba yako.Hasemi Bwana Mtume s.a.w Ila maneno yake ni uthibitisho utokao kwa Muumba mwenyewe wa hao wanaadamu, Sasa kwanini     
Bwana Mtume s.a.w akasisitiza hususan Mama, ili upate kujua Endelea part-2

No comments:

Post a Comment