Saturday, November 10, 2012

NANI KAMA MAMA?PART-4

Asalaam Aleiykum,

Nani kama Mama?
Leo unataraji pepo huku unamtuma mama yako akuletee chai, huku unapita ukisema anamkera mkeo au mumeo, Mama akiomba pesa ya chakula unamjibu huna wakati ukitoka unakwenda kuchapa matumizi kwa mambo ya kijinga, Nyie watoto wa kike haijambo kidogo mnajitahidi kuwafanyia hisani Mama zenu ila zidisheni unyenyekevu, Enyi watoto wa kiume nyie tahadharini sana na kuwatupa mama zenu na kuwasahau, yanakufikeni madhara na fimbo ya Mwenye-enzi-Mungu inakupigeni pasi na nyinyi kujijua, Unapita kujiuliza mbona mambo hayendi, mbona sina furaha, mbona nyumba yangu haikaliki kuna nini? mbona watoto hawanisikilizi, mbona kipato changu hakitoshi, kumbe hujijui umo katika kukanusha Maneno ya Mwenye-enzi-Mungu"Ni shukuru mimi na wazazi wako wawili"huyo ndio Mama ambaye leo umemtupa, leo humtizami, huwezi hata kumtembelea una harakati nyingi. Ewe mtoto umeambiwa muhudumie mama yako unasema huna uwezo eti unamajukumu mengi, nini habari yako wewe kama ghafla utafunga kauli huwezi kusema tena, Angalau mwenzio Alqamah alipata bahati Mama yake akamridhia, sasa nini hali yako wewe kama Mama yako akikutangulia bila ya kupata Radhi zake.
Sasa nini ufanye? vipi utamshukuru Mzee wako, itabidi tukitembelee kisa cha Nabii Mussa a.s "alipomuuliza Mollah wake nani atakua Rafiki yangu peponi?"Mwenye-enzi-Mungu akamwambia nenda katika njia mtu wa mwanzo utayekutana naye huyo ndie atayekua Rafiki yako peponi, Akatoka yule Msemezwa na Mollah wake Nabii Mussa a.s akenda kwenye hiyo njia akakutana na huyo mtu akamwambia leo nataka nikufate niwe na wewe kutwa nzima, yule mtu akamjibu sawa, wakatoka wakenda sokoni akanunua chakula wakarudi nyumbani walipofika walimkuta  
Bibi mtu mzima kakaa pembeni, yule kijana akatoa vile vitu akaanza kupika alipomaliza akachukua maji akamnawisha yule bibi halafu akaanza kumlisha ikisha akampa maji na kumrudisha kwenye kitanda, huku wakati wote Nabii Mussa a.s anamuangalia alipomaliza, Nabii Mussa a.s akamuuliza huyu bibi ni nani kwako, yule mtu akamjibu huyu ni Mama yangu, Nabii Mussa a.s akasema nilikua nakuona kila unachomfanyia huyu bibi unasema maneno, ni maneno gani ulokua unasema, akajibu kila nilipokua namfanyia kitu Mama yangu nilikua nikiomba Ewe Mollah nijaalie mimi kuwa Rafiki yangu Nabii Mussa a.s huko peponi. 
Nani kama Mama?
Huyo ndio Mama na hayo ndio malipo yake, hiyo ndio maana ya hiyo pepo ipo chini za nyayo za Mama zenu, "Ni Shukuru mimi na wazazi wako wawili"Kushukuru wazazi ni kuwatendea wema, kuwadekeza, kuwapa mapenzi, kusema nao kwa upole, usiwatolee jeuri, uwatizame kwa hali na mali, ukimuona anafanya kazi kuwa wa mwanzo kumsaidia, fanya kila uwezalo mpaka mama yako afurahi moyoni na akifurahi basi utaona matatizo yote yanaondoka utaipata furaha ya Raha mustarehe kama ulivokua tumboni nakukumbusha (Connection)bado ipo inaendelea mpaka mwisho wa Uhai wenu, na katika kiungo hichi ndipo inapokaa hiyo Radhi basi fanya jitihada usije ukaikosa au kuikata, Mwenye-enzi-Mungu wape Rehma zako za Usamehevu kwa wale wazee wetu walotangulia, wape afya njema kwa wale walobakia, na uwape umri mrefu wenye manufaa ya kukumbuka wewe daima-Amin

Abdulla Baja

No comments:

Post a Comment