Saturday, November 17, 2012

KIPIMO CHA IMANI PART-4

Asalaam Aleiykum,

Na hapo tena  kila unacho Ruzukiwa unafanya haraka haraka kukitoa, na kumbuka kila ukitoa kwa njia ya Imani basi huku unazidishiwa kupewa ili upate kutoa tena. 
Na hao ndio walo amini yaloteremshwa kwako "Ewe Mjumbe wa Mwenye-enzi-Mungu" na yaliyo teremshwa kabla yako, yepi hayo walo yaamini ikawa ndio nguzo zao. Dalili ya nyumba, maana yake kuna mtu anaishi, Ukiona na kuutizama Ulimwengu basi una hakika yupo alouumba naye huyo Mollah wako(1)Dalili ya Hukumu ni haya matendo ya Dhanbi na Thawabu kwa hivyo ni kuamini hiyo Akhera na siku ya (Hukumu)Kiyama.(2)Kuupata huu ujumbe wa Mwenye-enzi-Mungu na ushaidi uliopo wa macho kwa kujionea na mabaki yalobakia katika historia ni kuamini Mitume yake.(3)Kuyapata maneno kama haya yenye uthibitisho na maliwazo na ukumbusho pamoja na maonyo ni kuamini Vitabu vyake.(4)Kukubali maneno ya Mollah wako na kujua kwamba utakufa na Roho yako itachukuliwa ni kuamini Malaika wake.(5)Kujua kwamba vyote viliyomo mbinguni, nyota, mwezi,jua na viliomo ardhini miti, majani, wanyama, ukiwemo na wewe mwanaadamu nyote mmekamatana ni kitu kimoja basi hiyo ndio njia ya kuamini kheri na shari vyote vinatokana na yeye Mollah wako.(6). Na huo ndio muongozo utokao kwa Mollah wako na anayepata muongozo huu unampeleka katika Imani kubwa na anakua ni mwenye kufanikiwa ndipo akiambiwa chupa kwa ajili ya Mwenye-enzi-Mungu hasubiri hata itamkwe tena ila anakua kesha hudhuria kwa Mollah wake bila ya kuchelewa.
Ukitaka kuijua Imani yako patafute wapi yanatokea machozi, wapi zinapotokea hasira,wapi inapotokea chuki, wapi zinapotokea huzuni, wapi zinapotokea huruma, wapi zinapotokea hisia ukisha pagundua hapo pahala basi subiri hapo hapo wala usichoke asubuhi na usiku wala usifanye chochote baada ya muda Mollah anajua kama kweli wewe mpenzi wake na yeye ndio atakufungulia huo mlango wa Imani, na ukiipata hiyo Imani wewe unakua hakika Miongoni mwa waloongoka.
" قَالَتِ ٱلۡأَعۡرَابُ ءَامَنَّا‌ۖ قُل لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ وَلَـٰكِن قُولُوٓاْ أَسۡلَمۡنَا وَلَمَّا يَدۡخُلِ ٱلۡإِيمَـٰنُ فِى قُلُوبِكُمۡ‌ۖ وَإِن تُطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُ ۥ لَا يَلِتۡكُم مِّنۡ أَعۡمَـٰلِكُمۡ شَيۡـًٔا‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ۬ رَّحِيمٌ "
"Walisema Waarabu (wanaoishi majangwani)Tumeamini(Wanamwambia Mtume s.a.w)sema hamjaamini, lakini semeni tumesilimu, Maana Imani haijaingia katika mioyo yenu, Na mkimtii Mwenye-enzi-Mungu na Mtume wake, hata kupunguzieni chochote katika vitendo vyenu, Hakika Mwenye-enzi-Mungu ni mwingi wa kusamehe na Mwingi wa Kurehemu. Namalizia kwa Aya hii ili upate kujijua na kuongeza juhudi na "KAMA KWELI MPENZI WA MUNGU BASI CHUPA UANZE LEO HII KUITAFUTA NA KUIJAZA HIYO IMANI"na Mollah wako atakusaidia kwa hilo Inshaallah.

Abdulla Baja


No comments:

Post a Comment