Asalaam Aleiykum,
"الٓمٓ (١) ذَٲلِكَ ٱلۡڪِتَـٰبُ لَا رَيۡبَۛ فِيهِۛ هُدً۬ى لِّلۡمُتَّقِينَ (٢) ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَـٰهُمۡ يُنفِقُونَ (٣) وَٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ وَمَآ أُنزِلَ مِن قَبۡلِكَ وَبِٱلۡأَخِرَةِ هُمۡ يُوقِنُونَ (٤) أُوْلَـٰٓٮِٕكَ عَلَىٰ هُدً۬ى مِّن رَّبِّهِمۡۖ وَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ ("٥
"Hiki ni kitab kisichokua na shaka ndani yake, ni uongozi kwa wanao mcha Mwenye-enzi-Mungu.Ambao huyaamini yasio onekana na kusimamisha sala na kutoa katika yale tulo waruzuku.Na ambao wanaamini yaliyoteremshwa kwako, na yaloteremshwa kabla yako na wanaimini (hiyo)Akhera.Hao wako juu ya uongozi utokao kwa Mollah wao, Na hao ndio wenye kuongoka."
"Aya hiyo ya pili imeanza kimaajabu"imesema hakika hichi ni kitabu ambacho hakina shaka ndani yake na ni muongozo(Kwa wapenzi)Wamchao Mungu,Maana yake kama utakifata kitab hichi (Quraan)basi ndani ya hiki kitab kuna muongozo na muongozo huu ni ule unao kukupeleka kwenye Imani, kwa hiyo ni vizuri kama unasimamisha Sala na kumpenda Mollah wako na Mtume wake basi umo katika (njia ya Uongofu)na ukikaa katika njia hii kuna siku utafunguliwa hiyo Imani.
"Aya ya tatu ikasema Ambao wanayaamini yasio onekana na kusimamisha sala na katika yale tunayo waruzuku wanayatoa"
Itabidi hapa mstahamili ili tupate kuchuma katika mti wa faida kuhusiana na hilo neno kuamini yasioonekana. Ina hadithiwa katika riwaya za hekima, kuna siku walikaa Mawalii wawili pamoja na wanafunzi wao, Ikawa walii mmoja anataka kumwambia mwenzie kitu lakini hawezi kufanya vile mbele ya wale wanafunzi, akaagiza aletewe karatasi nyeupe anataka kuandika kitu, wanafunzi wake wakamletea, akachukua kidole chake cha Shahada akawa anaandika kwenye ile karatasi alipomaliza akampa yule walii mwenzie yule walii aliikamata ile karatasi akaitizama kwa njia ya kusoma ikisha akaangua kicheko kikubwa, Walo hudhuria pale wakaona sasa mambo yamekua makubwa, ama walimu wagonjwa au kuna miujiza mikubwa imetendeka mbele yetu, wakashikilia sana wale wanafunzi kuwauliza walimu wao nini kilicho andikwa kwenye karatasi ile lakini hawakupata jawabu la swali lao, Baada ya muda kupita yule muandikaji wa ile barua mauti yaka muhitaji, yule mwenzie alobakia akawaita wale wanafunzi wote akawaambia leo nitakwambieni nini kilichoandikwa na mwenzangu siku ile, Alicho andika mwenzangu siku ile katika ile karatasi nyeupe na nyie mkawa hamuoni yale maandiko alisema maneno haya,"hawa wanafunzi wangu nimekaa nao sasa yapata miaka sita, hawanifahamu wala hawafahamu kitu, hawatizami dalili wala hawazioni, hawaelewi chochote ninacho wafundisha,utadhani macho yao yamepofuka au masikio kuzibwa, basi kama mauti yatanihitaji mimi mwanzo naomba uwape habari hii. Wale wanafunzi wakamuuliza vipi wewe uliweza kuisoma ile karatasi nyeupe isiyokua na maandishi, Akajibu kulikua hakuna miujiza wala makarama ila ilikua wakati anaandika anatumia ishara na alama za herufi kwa kidole chake na mimi nilikua naangalia kile kidole kinaandika herufi gani basi nikawa naunganisha neno, Na nyinyi wakati ule mlikua hamjui kuyatizama yasio onekana(yalo Ghaib).Na wewe ungekuwepo wakati ule ungebisha, ungeshangaa na kuamini makarama, lakini dunia yetu ya leo unamuona (Bubu na Kiziwi)wote wanazungumza kwa ishara na alama.Haya ndio matatizo yetu makubwa hatujui kutizama ishara zote Mollah wetu alotuwekea, sasa ikiwa umejipima na kujigundua bado Imani yako ni dhaifu jaribu kuangalia Ishara na Alama za Mollah wako asaa mizani yako ya Imani itapanda juu, pengine utafunguliwa kuona mambo ili izidi Imani yako na imani ikiingia sawa sawa basi halitoki tena jambo hilo la Imani mpaka mwisho wa Umri wako na utakua unaamini kama unavo liamini jua na mwezi kuwa vipo na hayo mengine utaamini hivyo hivyo, na ikisha kuingia Imani hiyo kwako kila wakati utakua wakati wa "(kusimamisha hiyo Sala)" na kama mtu atakutania tu, "kama kweli mpenzi wa Mungu chupa ujiunge nami"hapo hapo husiti au kusubiri chochote kile, sijui nyumba nitamwachia nani, gari atachukua nani, pesa za bank itakuaje, hufikiri mambo hayo kabisa ila unajiachia kama yule Darweish.Endelea part 4
No comments:
Post a Comment