Saturday, November 24, 2012

BALAA ZA UJANANI PART-2

Asalaam Aleiykum,

Anahadithia Ibn Abbas r.a"Kasema Bwana Mtume s.a.w""Kamilisha matano kabla hayajakufika matano"Yafanyie kazi matano hayo, kuwa makini katika mambo haya matano, jichunge sana katika kadhia hii ya mambo matano.(1)Ujana wako kabla haujakufika utu uzima,(2)Na Afya yako kabla Maradhi hayajakuvamia,(3)Utajiri wako kabla Hujafilisika,(4)Na Faragha yako kabla mambo hayaja kushughulisha,(5)Na Uhai wako kabla Mauti hayaja kuhudhuria.
Sasa hapo naya kusanya yote matano haya ili niweze kuyatia kwenye ukurasa mmoja ili upate kuyasoma kwa pamoja usije ukababaika.
Balaa za Ujana hazisemeki unaweza kuangua kilio ukikumbuka kuwa wewe ndie ulikua una andaa picknic na machupa ya ulevi, wewe ndie mwenye kuandaa ngoma za msondo na chakacha ili watu wapate kumsahau Mollah wao, wewe ndie mwenye kutembea umevaa (Backless)unaonesha watu mgongo wako. wewe ndie mwenye kuvaa kisuruali kifupi unaonesha watu mapaja yako, leo hayo yote yamepita umebaki wewe na sisi uko wapi ujana wako, Umepita kama moshi na yote ulotenda yamehifadhiwa halijafutwa hata moja, rekodi yako imetunzwa kwa umakini mkubwa na kama utabisha Viungo vitasema "Ewe kijana sisi ni mashahidi wako kwani hujaambiwa katika sura ya Yaasin aya ya 65.
" ٱلۡيَوۡمَ نَخۡتِمُ عَلَىٰٓ أَفۡوَٲهِهِمۡ وَتُكَلِّمُنَآ أَيۡدِيہِمۡ وَتَشۡہَدُ أَرۡجُلُهُم بِمَا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ"
"Siku hiyo vitafungwa vinywa vyao, Itazungumza Mikono yao na itoe Ushahidi miguu yao kwa yale waliyokua wakiyachuma".
Ajihadhari Mwanaadamu siku ile viungo vitakapo kuwa tayari kumwaga siri zake, Vitaongea na kusema kweli mimi nilikua naishi maisha yangu kama Mcheza Cinema(Actor na Actress)Nilikua siwezi mimi kutoka katika nyumba yangu ila nijipambe, nitie piko, nitengeneze kucha,na Nywele niziachie nk, ndio nitoke, hivi hivi watu watanionaje na mimi nimeumbwa sijapendeza, Mimi nilikua nawaalika waja wako ili wanitizame mimi wapate kukuasi wewe na kukusahau Mollah wangu, hivyo ndivyo nilivoutumia Ujana wangu.(1)
Na Afya ulonipa nilikua nacheza mipira masaa mawili, Nakimbia riadha,nilikua na kula na kushiba mpaka nikawa nanyanyua vyuma nimejiunga (Gym)kwa uzima wa afya ulonipa, Lakini nyumba yako ya Ibada kwangu ilikua Marfuku, Ulikua ukiniona nikicheza pachanga (Disco)mpaka chini lakini nikiitwa kusujudu nilikua na kasirika sana hassa wakati wa Alfajiri.(2)
Na Uliponifungulia Utajiri Mollah wangu mtaa ulitingishika watu wote walijua mpaka paka wangu nilimvisha kengele, Niligeuka  mimi kuwa mcheza Senema maarufu nikiji fagharisha kwa kila aina ya starehe kuanzia ujenzi wa jumba la kifahari na magari yake sikujali chochote katika maagizo yako(3)Na Wakati ulo niruzuku ukanipa nafasi ya kuwa peke yangu ili nikukumbuke wewe, Hapo ndipo nilipotafuta (Whatsup)iko wapi, Computer iko wapi, Facebook iko wapi mchezo wangu kwenye TV utaanza saa ngapi, barazani kuna nini, hivyo ndio nilivokua natumia wakati wangu wa Faragha.(4)Na jambo la (5)ni kama ilivoanza mada kuelezea hali ya Uhai kabla ya Mauti.Basi leo uko wapi Ujana uliokua unaringia ulisahau maneno ya Mollah wako katika sura ya Yaasin aya ya 68
"وَمَن نُّعَمِّرۡهُ نُنَڪِّسۡهُ فِى ٱلۡخَلۡقِ‌ۖ أَفَلَا يَعۡقِلُونَ"
Na tunayempa Umri (mrefu)tunamrejesha nyuma katika umbo, basi jee hawayatii akilini(Kuzingatia).
Leo Ujana uko wapi huwezi hata kufanya mazoezi, Afya imekimbia umegubikwa na maradhi,Kipato sasa huwezi kukipata tena, kukaa peke yako sasa unaogopa, na pazia la Uhai lishafunikwa mgeni unae mtaraji Mauti yupo njiani, Basi yale Manne(4)umeyakosa hili lilobaki la Uhai bado unalo jitahidi katika hili kabla hujenda kukutana na Mollah wako.Zidisha Ibadah na Kuomba Maghfira Asaa Mollah wako huenda akakusamehe.

Abdulla Baja


No comments:

Post a Comment