Thursday, November 1, 2012

SHAIRI LA MCHA MUNGU-PART-4

Asalaam Aleiykum,

Sauti, jamani sauti ni nyenzo kali sana sababu inapenya moja kwa moja haina kizuizi, macho unaweza ukafunga au usitizame lakini sauti hata ukiziba masikio inapenya moyoni, ndio maana wakaambiwa enyi wanawake teremsheni sauti zenu kwa kuwa zinamtoa nyoka pangoni, zinakata maini msije mkazipandisha sababu zinakwenda kukaa moyoni. Na huu moyo una sifa zote mbili za kuona na kusikia, vipi kwa wewe mwanaadamu wa kawaida kadhia hii inatokea kwako, pengine unaona kwenye nchi yako au nyumbani kwako maasi yamekithiri lakini una yapuuza, basi elewa bado yangali machoni, lakini matendo hayo yakishuka moyoni unakua huwezi kustahamili tena, sababu yanakuumiza, sasa utachukua hatua moja katika mbili hizi kama shujaa utaamua kuanza kazi ya kuyaondosha, na kama dhaifu utaona unaanza kusema chini kwa chini, bali elewa yote hayo mawili ni hijaza ilotoka kwa Mollah wako wala usifanye kazi ya kuanza kuitoa moyoni kwako kwani utakua mmoja katika hao maelfu walopotea.
Ukipata uzinduo huo wa kujua kwa moyo sasa inabidi ujiunge na wafuasi wa aya hii:Quraan-As-saff-"11"
"تُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَتُجَـٰهِدُونَ فِى سَبِيلِ ٱللَّهِ بِأَمۡوَٲلِكُمۡ وَأَنفُسِكُمۡ‌ۚ ذَٲلِكُمۡ خَيۡرٌ۬ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ"" Muamini Mwenye-enzi-Mungu na Mtume wake, na piganieni dini ya Mwenye-enzi-Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu, hayo ni bora kwenu, ikiwa mnajua."
Kwanza imeanza Imani lazima utumie huo Moyo kujaza mawili hayo, ikisha upigane kwa njia ya Mollah wako, kwanza kwa hiyo Mali yako uliyoichuma, jijue wakati wowote unaweza kufa ikarithiwa na wengine wakaifuja kwa njia ya dhanbi, basi anza mwenyewe kuitoa kwa mambo ya kheri,sio unachangia mambo ya harusi na chakacha na kukandamizwa waislam wenzio, wewe toa katika kuondosha mambo machafu, halafu na nafsi yako nenda moyoni kama alivo kwenda kugundua Mcha Mungu, nini kagundua Mcha Mungu. "Nilipogundua katika huu Moyo wangu anaweza kukaa asiye kuwa wewe, nilifanya jitihada za kujaza uongofu utokao kwako mpaka nika hakikisha hakai mwengine asiye kuwa wewe"Mcha Mungu kagundua Mapenzi yanakaa moyoni(kapewa taaluma hii)"Ukipenda nchi unaitia moyoni,ukipenda mali unaitia moyoni,ukimpenda mtu unamtia moyoni"kumbuka chochote kile unachokipenda lazima kikae moyoni na wewe kifanyie uchunguzi utakuja kugundua kama alivojua Mcha Mungu, Na wanasema wajuzi wa mambo ya lugha, huwezi kupenda viwili na mapenzi yakawa sawa, basi ukiona kitu hakimo moyoni fanya hima ukijaze katika moyo wako, na wewe ndio utachagua kitu gani kikae kwenye moyo wako.endelea part-5


No comments:

Post a Comment