Saturday, November 17, 2012

KIPIMO CHA IMANI PART-2

Asalaam Aleiykum,

Nini Taqwa? Taqwa ni mapenzi, nini mapenzi, mapenzi ni njia au kivuli cha Imani, nini Imani, Imani ni msingi wa Ibadah, nini Ibadah, Ibadah ni njia au mwenendo wa kukutoa kwenye giza kwenda kwenye nuru, Kukuondoa kwenye hali ya kuto kuona kwenda kwenye kuona, Kukutoa kwenye Hamaki kwenda kwenye Huruma, Kukutoa kwenye kuadhibu kwenda kwenye kusamehe, kukutoa kwenye kusahau kwenda kwenye kukumbuka, kukutoa kwenye mazungumzo kwenda kwenye kusabihi, na mwisho kukutoa kwenye kiwiliwili kwenda kwenye Roho na hapo tena ni marejeo yetu sote kwa Mollah Muumbaji.
Sasa Ikiwa tushamaliza kuujua huo msingi hapo juu wacha tumalizie na nguzo zake ambazo sote tunazijua na kufahamu ziko sita, Katika nguzo hizi tumeambiwa tuziamini, lakini wengi katika sisi hakuna anazo ziamini ila tunazikubali, ni vizuri kukubali ndio mwanzo, lakini kinachotakiwi hapo ni kuziamini kwani kukubali tu wakati wowote unaweza kuzikataa (ndio maana wale walokaa barazani wakasema hakuna muislam hapa)ndio maana zikaitwa nguzo za Imani.Sasa chukua kipimo mwenyewe ujiulize ndani ya nafsi yako umeziamini au umezikubali ukipata jawabu ukajijua hujaamini umekubali tu Basi Nakwambia(Kama kweli mpenzi wa Mungu chupa ujiunge nami)ili utazame zaidi katika hizi Ishara ntakazo zitaja ili ujue ngapi unazo na hapo utajua kipimo cha Imani yako. Jiulize hivyo kweli mimi nina Imani?Nimeshawahi mara ngapi kuwalisha mayatima (1)Jee nimeshawahi kuwapa msaada wajane bila ya kuwatamani (2)Nini hali ya Muombaji pale anaponifata nimpe japo chakula natekeleza hilo (3)Nini hali ya Maskini jee nawafanya kuwa ndio marafiki zangu (4)Naweza kujizuia mimi nisiseme watu (5)Naweza kukaa siku mbili nisiseme uongo(6) nguzo sita namie nimetaja mambo sita lakini vipimo ni vingi sana vya hiyo Imani na kama mizani yako bado haijainuka hata kidogo kwa mambo hayo sita basi nakuomba "(Chupa ujiunge nami)"Ili tupate kuzikarabati hizo nguzo isije nyumba yako ikaporomoka kwa kukosa nguzo madhbuti.
Nguzo hizi zinafahamika uzuri kwa maandishi lakini kuna tabu kubwa kuziamini hususan kwa sisi viumbe wa kawaida ambao bado hatujaamua kuchupa, lakini kuna hii nguzo moja ambayo kidogo unaweza kujitahidi, sasa ni nguzo gani hiyo?ambayo ndio pekee inakugusa hiyo sehemu inapo kaa Imani, Nguzo yenyewe hii ya (kuamini vitabu vyake)hili la kitabu kuna wakati unachungulia ndani kutaka kujua kuna nini, angalau kidogo linakugusa pahali ukawa unakubali baadhi ya mambo, Na kama kitachomwa moto kitabu hichi unapata hasira japo kwa mbali na hamaki zinakushika, hapo angalau japo kidogo Kimizani chako kina nyanyuka, inaonesha unayo chembe ya mbegu ya Imani, Ndani ya chembe hiyo ndio mie nataka nitie mbolea ili upate kuota mti mkubwa wa Imani wenye matawi mingi.Sasa wacha tukamate nguzo hii ya kitab tutizame imesema nini na inathibitisha vipi hayo tuloyataja mwanzoni kuhusiana na kadhia hii ya Imani. Endelea-part 3

No comments:

Post a Comment