Friday, March 1, 2013

BARUA YA MCHA-MUNGU-PART-1

Asalaam Aleiykum,

Katika darsa yetu ya leo tunasoma Barua ya Mcha-Mungu, Basi nakuomba kama una Phd, au Master's au Degree yoyote ile basi iweke pembeni, Soma Maudhui haya ukiwa mweupe moyoni(Absent)hakuna kitu, hapo unaweza kuifahamu barua hii, lakini ukija umejaa mizigo ya elimu kichwani, hapo utakosa kumfahamu Mcha-Mungu na kusudio la maneno yaliyomo kwenye barua hii. Halafu kumbuka utakapoisoma usije ukafanya makosa ya (Kutuwama)kubakia kwenye maneno, bali fanya bidii na jitihada uyapasue hayo maneno ili upate ujumbe(Massage) iliyomo kwenye hayo maneno.
Inaanza Barua hii kwa mshangazo na maajabu makubwa, Anauliza Mcha-Mungu!! Jee ushawahi kujiuliza kwanini Mlevi akilewa Anayumba(Anapepesuka)? anaendelea kwa kusema lazima iko sababu, Na tayari kila mmoja wenu ana jawabu alilo taarisha kujibu, lakini subirini na hizo jawabu ili tupate nafasi ya kuendelea na Barua ya Mcha-Mungu. "Mwenye-enzi-Mungu katuumbia waja wake kitu kiitwacho (Sense) na hizo ziko tano ambazo tulokua tunazijua, Nazo ni (1)Kutokana na ngozi tunapata hisia ya kugusa(2)Kwa ajili ya Macho tunapata kuona, (3)Kutokana na masikio tunapata kusikia,(4)Na kwa njia ya ulimi tunapata kuonja Ladha,(5)Na la Tano ni hili la pua tunapata kunusa vilo vizuri, hizo ndizo tano tunazozijua na zenye kujulikana tokea hapo kale na wagunduzi wa majambo.
Ikatajwa ndani ya kitabu kitukufu chenye maneno ya ukweli mtupu ya kwamba  "وَٱلَّذِينَ إِذَآ أَنفَقُواْ لَمۡ يُسۡرِفُواْ وَلَمۡ يَقۡتُرُواْ وَڪَانَ بَيۡنَ ذَٲلِكَ قَوَامً۬ا" sura ya Furqan aya ya 67," Na Wale ambao wanatoa(Kutumia)hawafanyi israf(fujo-Ovyo) Na wala (hawazuii kabisa)hawafanyi Ubakhili, Bali wanakuwa kati kati baina(Balance) ya hayo".
Utakapo toa usifanye israf au kuzuia kabisa ila unatakiwa uwe umekaa katikati, umefanya (Balance)ya mizani usije ukayumba, usije ukatoa sana ukafilisika au kuzuia kabisa ukawa Bakhili, Hapo Mwenye-enzi-Mungu anaitaja (Balance)ambayo tumekuja kuigundua kupitia wana sayansi miaka ya karibuni kumbe kuna (Sense)ya sita inayomuweka Binaadamu kuwa (Balance) ili asiyumbe, Na nyinyi mnalishuhudia hilo kwenye mapigano ya Masumbwi kama atapigwa mmoja wao konde la sikio likampata utamuona mpiganaji huyo anavoyumba na hana tena (Balance).
Au kama mtu atafanyiwa Operesheni ya masikio akakosewa kidogo inakua hata kusimama hawezi keshakosa (Balance)Hiyo ndio hisia ya sita katika Umbile la Mwanaadamu, hilo ndilo alotuchagulia Mcha-Mungu kutuonesha kupitia mfano wa Mlevi, tumeoneshwa mfano huo kwa sababu hiyo (Balance) ipo kwenye (Physical na Mental) na Mcha-Mungu kagundua  sisi sote tunalewa ila tunabadilisha aina ya Mvinyo, Mlevi yeye kaamua kuyumba dhahir, lakini sisi wengine tunaamua kunywa siri siri, na sote tumetajiwa ulevi wetu na mtu ajitizame yeye anakunywa nini na kama hayumbi kwa siri, kuna wengine wana chupa ya Kiburi, hebu mtizame wewe vipi mwenye kiburi anavoyumba, wengine ulevi wao zinaa, wengine mvinyo wao Mali, wengine wamelewa chopi katika kutafuta pesa, wengine wanachupa za kula Rushwa, wengine wana ulevi wa maharusi Nk, na mambo mengi ambayo yanatufanya maisha yetu iwe mfano kama vile tupo Baharini, kila mtu anayumba na atizame mtu nini yeye kinamyumbisha hata ikawa hakai katika hiyo (Siratul-Mustakim).
Jitizame kwanini (Sense)yako ya sita inakutesa, nini khasa tatizo lako, mbona huna furaha, wapi chanzo chake kinatokea na upande gani nimeelemea jee niko katikati au nimezidi sehemu nyengine,  Mbona siwezi kuweka mizani yangu ya maisha sawasawa.
Jaribu kujifanyia mitihani midogo midogo upate kujua (Balance)yako iko wapi, angalia kama mtu atakupa Msahafu na pesa nini kina kufurahisha, ukiona pesa ndio inakufurahisha basi ushajua upande gani unakuyumbisha na pata wasi wasi mkubwa, na ikiwa umepewa vyote viwili na furaha yako ikawa iko kawaida na vyote umeviridhia basi wewe ushaipata (Balance) na hapo uko sawa ikija pesa sawa, ukija Msahafu sawa basi jijue huyumbi na tayari ushaanza kupiga hatua za Ucha-Mungu, na kama hayo yote yamekushinda sasa unataka msaada endelea na Barua ya Mcha-Mungu sehemu ya Pili ili ukaone msaada gani unapewa ili upate kuweka (Sense)yako ya sita katika mstari ulonyooka na ukisha kuwa huyumbi basi hapo safari ya Ucha-Mungu ndio imeshaanza.
Kuyajua hayo Endelea-Part-2


No comments:

Post a Comment