Saturday, March 9, 2013

ELIMU YA UCHAWI NA MASHETANI-PART-1

Asalaam Aleiykum,
Leo tunaligusa somo lenye kuwagusa wengi katika jamii kuhusiana na kadhia hii ya (Uchawi na Mambo ya Mashetani)si dhumuni langu kufundisha au kutilia nguvu jambo hili, lakini nia yangu kufahamisha chanzo na madhara ya wenye kushiriki katika jambo hili hususan tukiwa tumebeba (Mabango ya  kujiita sisiWaumini)Nitaanza maudhui hii kwanza kuzungumzia (Uchawi)halafu nitagusia (Mashetani), Kwanini nikafanya hivyo, Sababu kubwa (Shetani)ni Mwalimu wa huu uchawi, kwa hiyo kwanza nimeona nitaje somo halafu ndio nimtaje (Mwalimu)wa somo hilo.
Nini Uchawi?
Kwa ujuzi wangu Uchawi ni (Inner-Science)Sayansi ya Ndani ya Upande wa pili tusiouona, Katika sayansi hii isiyo onekana ina mrengo wa kushoto ya (Ufisadi na uharibifu)na Kuna Mrengo wa kulia ambao huu ndio huo wa (Tabibu nk), Inapatikana Elimu hii kwa njia mbili ya mafundisho au ya kuingia mwenyewe kwa taaluma makhsusi ambayo inachukua muda kufanikiwa kuingia katika hii (Psychic-World)katika dunia hiyo ya sayansi ya (Uchawi),kuna dhamana maalum ya yoyote mwenye kuingia basi itabidi ajiandae kwenda (Motoni-Jahnnam)kwa sababu vishawishi vilivyomo ni vikubwa sana mwanaadamu wa kawaida ukiingia lazima upotee, na Dalili mnaziona kwa wale wenye kupata tone la elimu hii vipi wanakua katika shughuli zao za kila siku zenye kuambatana na (Shirk na Uharibifu)"Ameangamia yule anokwenda kwa wanoitwa Mganga akataka cheo au fulani adhurike".
Elimu hii ya Uchawi inaandamana na mambo mengi, makubwa katika hayo ni (Mind-Elecricity-Sound)Ukiingia katika Elimu hii unakutana na utawala au uwezo wa (Control-other's mind)unakua na uwezo wa elimu ya kuharakisha maradhi kwa wanaadamu wenzio, unakua na uwezo wa kuchezea akili za wenzio, na katika kuzidi elimu hiyo unapata sasa uwezo wa kutumia (Electricity and Air)Umeme na hewa kwa njia za kuruka, kupeleka ujumbe wako, kufanya vitu kuonekana na kupotea, na kwa ajili ya (Sound) Sauti unapata uwezo wa kuwatia maradhi wenzio kubadilisha matukio nk, hayo yote ni mambo yenye kukupeleka (Motoni).
Sasa nilipoita Sayansi ya ndani nilikua na maana ya mifano hii, kama vile vifanyavyo kazi vitu hivi, (Mind)Akili Ukiingia katika (Field)uwanja  huu jambo la mwanzo lazima ufanye ni (Shirk) kwa sababu kama unataka fulani adhurike, au yamkute mauti, au mke na mume waachane lazima ufanye (Connection)Mawasiliano na (Cosmic Mind) ambapo unatumia mawasiliano ya (Energy) nguvu maalum kusafirisha (Madhara au maradhi)yende kwa fulani, ndio maana Waganga wanataka jina na mambo mengine ili wapate kumshirikisha Mwenye-enzi-Mungu kutumia hiyo (Energy)yao ndogo kusafirisha au kugeuza mambo kutumia (Special Power)sitaki kueleza vipi na wapi hiyo (Specia Power) ipo ili asije kila mmoja wenu akataka kuwa Mganga, kwani kila Mganga mwenye kuleta madhara kashachukua dhamana ya kukaa motoni pamoja na huyo alokwenda kufanyiwa hiyo haja yake. Sasa kutokana na Ufundi huo wa uchawi anatumia mtumiaji nyenzo maalumu ya hii (Electricity signal)kusafirisha matakwa yake hata kwa mtu aliye mbali ili adhurike, sote tunajua katika Sayansi ya nje kuna kitu kinaitwa (Electrical Ray's) au mionzi inavo mponesha mtu kwa magonjwa mbali mbali, na pia sasa tunaelewa Akili (Mind)inafanya kazi kutumia hizo (Electrical-signal) kwa hiyo Wachawi wamegundua zamani elimu hiyo na wakawa wanaitumia kwa matakwa yao ya uharibifu na ufisadi.
Na hili la Tatu la (Sound) hili nalo lina mfano ule ule wa (Elecricity signal) hakika sauti ina mambo mengi mengine wenyewe mnayaona mtoto akiimbiwa nyimbo analala kwa nguvu za sauti, Wale watu wa dhikr wanajua kama likitajwa neno la (Allahu-Allah)kwa sauti moja  na kwa muda mrefu, basi inapatikana harufu ya (Ubani) na hapo ndipo ilipogundulika mti huu wa (Ubani)ikawa mpaka leo watu wakifanya visomo wanachoma ubani, kwa sababu hawana wakati wa kudhikr mpaka ikapatikana hiyo harufu ya ubani, Na ubani pia umegunduliwa una (Connection) na (Mind) unaleta utulivu, unaondosha tafrani (Dipression au stress)wewe jaribu kama una (maudhi yako fukiza ubani na moshi vuta kwenye pua utaona manufaa yake)kwenye (Brain) yote hayo yamegunduliwa kutokana na (Sound) Naitaja (Sound) kwa njia ya kheri kwa sababu katika njia ya shari ina balaa kubwa na siwezi kuzitaja hadharani, wazee wangu wa kingazija walikua na elimu hii ya (Sound)wakiita (Burdai)sijui kama mpaka leo ipo au vipi? ilikua elimu hii kama kuna mgonjwa taabani wakukatiwa tamaa basi huja wasomaji wa dua hii ya (Burdai)ilopangwa kwa mpango maalum, wanasoma wakimaliza basi ama mgonjwa anapona au ana ana aga dunia na (Kufariki), kitizamo hapo sio kisomo ni ile (Sound) au sauti wanayoitoa wasomaji ndio inayoleta matokeo, walikuwepo watu miaka ya nyuma wenye kujua elimu hii ya (Sound)wakafanya utafiti, alichukuliwa ndege akawekwa mbele ya huyu mwenye elimu hii ya kichawi, yule bwana akafanya sauti fulani ndege akaanguka na kuzimia na akafanya tena yule ndege akaamka na kuruka. hii kwa uchache ni kuonesha vipi huo Uchawi unafanya kazi zake, sasa nini Quraan inasema kuhusu kadhia hii.
Endelea Part 2

No comments:

Post a Comment