Friday, March 1, 2013

BARUA YA MCHA MUNGU-PART-3

Asalaam Aleiykum,

" لَا يَسۡتَوِىٓ أَصۡحَـٰبُ ٱلنَّارِ وَأَصۡحَـٰبُ ٱلۡجَنَّةِ‌ۚ أَصۡحَـٰبُ ٱلۡجَنَّةِ هُمُ ٱلۡفَآٮِٕزُونَ"
"Hawawi sawa watu wa Motoni na Watu wa peponi, Watu wa peponi ndio wenye kufuzu".
Kwanini sasa ukatajiwa tafauti ya watu wa motoni na peponi na wewe huwajui, umetajiwa watu hao kwa sababu ushapewa ishara zao katika aya ilopita ukaambiwa wewe usiwe kama hao, hakika hao ni wenye kutenda Maasi, basi kuwa tafauti nao, usikubali kuyumba wala kuyumbishwa, na watu wa peponi ni wenye kufuzu, basi na wewe anza kuonja matunda ya peponi ungali hai kabla hujafika, ishi katika hiyo (Balance)usikope, usiibe,usizini,usiseme uongo,usidhulumu jiepushe na kila aina ya dhanbi, jikurubishe sana kwa Mollah wako hapo utapata mambo mawili la kwanza itakuteremkia (Dhikr) wakati wote utakua unamkumbuka Mollah wako na la pili itakushukia(Bliss) au (To live happy ever after).
Na aya ya 21 inatukumbusha kuhusu hii Quraan na ukweli wake na thamani ya maneno haya kwa kutwambia,
"لَوۡ أَنزَلۡنَا هَـٰذَا ٱلۡقُرۡءَانَ عَلَىٰ جَبَلٍ۬ لَّرَأَيۡتَهُ ۥ خَـٰشِعً۬ا مُّتَصَدِّعً۬ا مِّنۡ خَشۡيَةِ ٱللَّهِ‌ۚ وَتِلۡكَ ٱلۡأَمۡثَـٰلُ نَضۡرِبُہَا لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَفَكَّرُونَ"
"Lau kama tungeiteremsha hii Quraan juu ya Mlima, ungeliona ukinyenyekea (na)Kupasuka kwa khofu ya Mwenye-enzi-Mungu, Na hii ni mifano tunawapigia watu(wanaadamu)ili wafikiri".
Hapa limetajwa jambo la kushangaza, kuwa mlima ungenyenyekea na kupasuka kwa khofu ya (Mollah)wake, sasa swali la kujiuliza kwanini ukatajwa mlima, Umetajwa mlima kwa sababu kila chenye kuishi katika Ulimwengu huu basi kiko hai na kina ufahamu wake, utizame mti unaota ikisha unachomoza mizizi, ile mizizi kazi yake kupata (Nutrition)na maji kwa umbali ulokadiriwa, milima hali kadhalika, ina mungunyika na kujitengeza upya ili kuweka hiyo(Balance)(Kama nilivotaja katika mada ya Shukurani ya Uhai)tizama weye kila kiumbe kiwe kidogo au kikubwa kinavofanya kazi ya kutafuta Riziki yake kama alivo ipangia Mwenye-enzi-Mungu.
Basi Unaambiwa Utukufu wa hii Quraan, na uzito wa maneno haya lau ungejua thamani yake ungekwenda kwa tumbo kuyakiri na kuyatii maneno haya na maamrisho yake, na hiyo ndio mifano tunayopigiwa ili tupate kufikiri, Mollah wako hana haja ya kukitesa kiumbe chake, analo taka ni jambo moja fikiri tu, na ukiweza kufikri maane yake ushakumbuka, na ukikumbuka ina maana ushasita kuyumba, na ukisita kuyumba funga barua ya Mcha-Mungu sasa andika yako ili watu wapate kuisoma. Kwani na wewe Mungu kashakujaalia kuwa Mcha-Mungu.
Namuomba Mollah atuondoshee usahaulivu wa hii (Sense)ya sita na tukaanza kuyumba, atupe utulivu tusiyumbe mpaka tukawa hata katika huo Ucha-Mungu tunaongeza na (Riah)kujionesha, au tukayumba upande wa pili kuwa katika kundi la walomsahau Mollah wao na Mollah akawasahaulisha. Amin.

No comments:

Post a Comment