Thursday, May 10, 2012

DALILI ZA MCHA MUNGU PART 2

Asalaam-Aleikum


Nani Mcha-Mungu?
Kabla hatujaigusa aya ya ucha Mungu wacha tuendelee kumchambua Mcha Mungu ni mtu wa aina gani.


Mcha Mungu ni mja aliyekufa kwa mapenzi ya Mollah wake wakati akiwa hai, hataki yeye sifa, wala kufanya jambo kwa malipo yoyote halei yatima kwa kuhitaji malipo, halishi maskini kwa kuhitaji aongezewe utajiri.


Zitazame sala zetu zilivo husali ila ni mwenye kuhitaji pepo au utajiri au ufanikiwe hili na lile ukichunguza sala zako zote (full of Bussines)zimejaa biashara na kama sio biashara basi unasali kwa woga usitiwe motoni.


Imani yako (empty) ukiulizwa leo unaamini nini basi utarusha ngumi kwa sababu huna (Empty) utatumia maneno kujibia imani na hivo viwili ni vitu tafauti.


Maneno yanatoka kwenye ulimi, imani inatokea kwenye (Moyo-Heart)Feeling) umesali miaka yote hata siku moja yashakutoka machozi kwa ajili ya sala yako, haiwezekani kwa sababu huna feeling hujapata kumiminikiwa na Imani hujakutana nayo imani ana kwa ana kila kitu kimo ulimini (Ndio maana bwana Mtume s.a.w"akaonesha kifuani mara tatu kuashiria
moyo")


Jitizame unajiita Mcha-Mungu hata siku moja umepata sala, ukiwa dukani au kazini unawaza kwenda kusali ukifika msikitini unawaza kazini na dukani hivi ndivo sala zetu zilivo hivi ndio ucha Mungu wetu ulivo, hatusali ila kuonesha watu kila kitu maonesho matupu, ukikataa au ukipinga ukweli hivi ndivyo tutendavyo.


Nani Mcha-Mungu?
Mcha Mungu ni yule ambaye masaa(24)yupo anaishi na Mollah wake katawaliwa na Mollah wake akivuta pumzi anamkumbuka Mollah, akisimama anamkumbuka Mollah wake, akilala anamkumbuka Mollah wake.


Ukianza kuupata ucha Mungu kweli kweli basi (Automatic) unaanza kuihama dunia hutaki tena yanakukera mambo yake, sasa unakua unaona raha kila wakati unataka uwe na kipenzi chako, (na kama nani anotaka awe mbali na Mpenzi wake) kumbuka


Mcha Mungu hana khofu yoyote anaishi katika ulimwengu yupo na wenzie kila mtu rafiki yake lakini (inside)yupo na Mollah wake hasahau hata dakika moja kumdhukuru Mollah wake.


Sasa wacha tuitizame aya ya Mcha Mungu inasemaje,

Aya hiyo ya 62 inamtaja Mcha-Mungu kuwa mtu asie na khofu vipi?.


(Hakika ya wale mawalii wa kweli kweli wa Mwenye-enzi-Mungu wale vipenzi walojitupa kwa Mollah wao wakajiweka karibu kabisa na Mollah wao hakuna khofu juu yao kabisa)


Kwa nini ikawa hivyo?
Napenda uelewe nyuma ya khofu kuna matumaini, ndio maana wewe Muumin wa kawaida hujijui itakuwaje mwisho wako, lakini kwa Mcha-Mungu jambo hilo hakuna.


Kwake kuna nini?
Ipo yakinifu (Gurantee) ithbati ya njia ya Mollah wake kwa jambo lolote ulifanyalo unaridhia chochote kile unakua kama majani, Upepo ukija unayumba nao ukenda kusini unafata ukenda kaskazini unafata, huwi kama mti unabishana na upepo ndio maana kikija kimbunga kikali mti unakatika tena hapo hakuna kinachobaki ila hugeuzwa majina ikawa hii kuni, lile gogo na kadhalika.


Naam na wala hana khofu kesho atakula nini au atavaa nini, jumba lake atalimaliza lini, afya yake ikoje huwa na Imani ikiwa Mollah wangu anaweza kumponesha Ndege alo msituni, basi atashindwa na mie ninayeishi nyumbani, 


Mcha-Mungu anafunguliwa mambo na Mollah wake akajua nini afya, na hilo ni jambo kubwa kabisa ukiweza kungundua nini afya, hata madaktari wenye elimu za kupindukia hawezi kukwambia nini afya, atakutajia maradhi ya aina yote lakini hawezi kukutamkia nini afya, ndio maana ukenda kwa Mcha Mungu akizungumza na Mollah wake upesi upesi utaona mbona nimepona mara moja imekuaje hajafanya lolote? huyo ndio mcha Mungu.


Na hana kuhuzunika katika nafsi yake fulani mbona vile mie mbona hivi, mbona sasa umeniondoshea afya umenipa maradhi yote hayo kwake huwa maridhia akipewa anaona kajaribiwa na akinyimwa pia huona kanusuriwa, hayamtoki mdomoni kwake ila maneno ya shukura.


Endelea part 3


Abdulla Baja

No comments:

Post a Comment