Saturday, March 9, 2013

ELIMU YA UCHAWI NA MASHETANI-PART 2

Asalaam Aleiykum,

Quraan Baqarah aya ya 102.

"وَٱتَّبَعُواْ مَا تَتۡلُواْ ٱلشَّيَـٰطِينُ عَلَىٰ مُلۡكِ سُلَيۡمَـٰنَ‌ۖ وَمَا ڪَفَرَ سُلَيۡمَـٰنُ وَلَـٰكِنَّ ٱلشَّيَـٰطِينَ كَفَرُواْ يُعَلِّمُونَ ٱلنَّاسَ ٱلسِّحۡرَ وَمَآ أُنزِلَ عَلَى ٱلۡمَلَڪَيۡنِ بِبَابِلَ هَـٰرُوتَ وَمَـٰرُوتَ‌ۚ وَمَا يُعَلِّمَانِ مِنۡ أَحَدٍ حَتَّىٰ يَقُولَآ إِنَّمَا نَحۡنُ فِتۡنَةٌ۬ فَلَا تَكۡفُرۡ‌ۖ فَيَتَعَلَّمُونَ مِنۡهُمَا مَا يُفَرِّقُونَ بِهِۦ بَيۡنَ ٱلۡمَرۡءِ وَزَوۡجِهِۦ‌ۚ وَمَا هُم بِضَآرِّينَ بِهِۦ مِنۡ أَحَدٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِ‌ۚ وَيَتَعَلَّمُونَ مَا يَضُرُّهُمۡ وَلَا يَنفَعُهُمۡ‌ۚ وَلَقَدۡ عَلِمُواْ لَمَنِ ٱشۡتَرَٮٰهُ مَا لَهُ ۥ فِى ٱلۡأَخِرَةِ مِنۡ خَلَـٰقٍ۬‌ۚ وَلَبِئۡسَ مَا شَرَوۡاْ بِهِۦۤ أَنفُسَهُمۡ‌ۚ لَوۡ ڪَانُواْ يَعۡلَمُونَ "
"Wakayafata yale (walozua)kuyafata mashetani, Katika ufalme wa (Nabii) Suleiman (a.s) Na hakukufuru Suleiman, bali Mashetani ndio walokufuru, Wakiwafundisha watu Uchawi(Walokuwa wanaujua toka mwanzoni) Na (elimu ya Uchawi)ulioteremshwa kwa Malaika wawili Haruta na Maruta, katika mji wa Babil(Babiloni)(Malaika hao)hawakumfundisha yoyote mpaka wamwambie, Hakika sisi ni mtihani(wa kutizamwa kwenu)basi usikufuru, Wakajifunza kwao ambayo (Katika elimu hiyo)waliweza kumfarakisha mtu na mkewe (Na mambo chungu nzima). Wala hawakua wenye kumdhuru yoyote kwa hayo ila kwa idhini ya Mwenye-enzi-Mungu. Na wanajifunza ambayo yatawadhuru wala hayatawafaa, Na kwa yakini wanaju kwamba aliyeridhi haya hatakuwa na sehemu yoyote katika Akhera, Na bila shaka ni kibaya kabisa walichouzia nafsi zao laiti wangalijua."
Naam, Nabii Suleiman a.s yeye alipewa Elimu hii lakini kupitia Mrengo wa kulia, akawa mwenye kusikia sauti, kuumiliki upepo na majini, ndipo walipomzulia kuwa yeye si mtume bali ni mchawi, ndio wakajibiwa alikua anajua elimu hiyo lakini hakukufuru, lakini walo kufuru ni Majini na watu wenyewe kwa kuwafundisha watu uharibifu na ufisadi mwengine kama vile kuchezea akili ya Mke na Mume na kuwagombanisha, wanatumia ile (Method) ya (Mind elecritical signal) na kuisambaratisha na kama kumtia mtu chuki nk, Malaika wale walotumwa walifundisha watu kwa masharti, kwanza wakiwaambia sisi tumekuja na (Mtihani)hii elimu tulo nayo ni Mtihani kwenu ukiingia umeumia, wachache sana wanovuka wakaamua kuwa (Matabibu)wa huo Uchawi, lakini wengi wenye Elimu hii lazima wakufuru, ndio maana ukiigusa elimu hii basi jiwekee wewe mtu wa  Motoni, sababu vishawishi vyake ni vikubwa na hapo ndio unapokutana na mwalimu wako Shetani.
Shetani anafanya nini? Shetani yuko jirani na elimu hii japokua si wenye kuimiliki kikamilifu lakini wanachangia sana katika kumkufurisha Mwanaadamu, Wanapendelea sana Mashetani kuwaandama wanawake kutokana na wanawake kuwa na (Energy)ya (Nagative) ya kukubali, kupokea, ukiona mtu kapanda shetani na anasema lugha nyengine basi hapo kwa wenye kujua elimu ya (Hypnotism)watanielewa na kujua nini Shetani kafanya, Wale wenye kumjua (Hypnotist)wanajua vipi anavoweza kukuamrisha ufanye kitu na ukafanya bila ya ridhaa yako, basi na Shetani hutumia njia hiyo hiyo akaanza kuwakufurisha watu na hata kuwafitini.
Usidhani Shetani pekee ni mwenye kupasua ukuta akaingia hata wanaadamu wanazo elimu hizo pale wanapofanya kitu kupotea, na wala usidhani ni uzushi wa Mtu kuonekana sehemu mbili kwa wakati mmoja hayo yote ni katika elimu hizo nilozitaja huko nyuma ni vitu vinavyo wezekana na bado vipo. Shetani anayo vile vile elimu ya kuingia na kukaa katika mwili wa binaadamu na kuupoteza kabisa katika njia za haki, na nyinyi mnoshuhudia mkawa mnastaajabu nini kimetokezea kwa mwenzetu huyu. Lakini katika yote hayo Mwenye-enzi-Mungu hakutoa elimu ya kukiangamiza kiumbe(Kufa) isipokua kwa Idhini yake, hakuna jini wala binaadamu atakae kudhuru ikiwa wewe utajitupa katika elimu ya (Qadir)ya Mollah wako, katika Elimu hii hakuna chochote chenye kudhurika au kuguswa na dhara.Yoyote yule  Anaengia katika elimu hii ya Kichawi ni lazima anakutana na Bahari ya (Numerology)au Ramli, ambayo inamuangamiza kabisa, kuna wengine wenye kutizamia kwenye maji au kioo, bahari ya elimu hii ni kubwa na mimi sina wino wa kuimaliza, dhamiri yangu ilikua ni kuonesha japo kwa uchache vipi inakua na vipi Makosa yanopatikana kwa yule anofanya na anaeomba kufanyiwa, na yule mwenye kushiriki katika Imani za mashetani ajue huko ni kuangamia kukubwa, wala hakuna msamaha, na kwa utendaji wa mambo hayo umejiharamishia mwenyewe Pepo huko Akhera, kwa hiyo kama una jamaa au rafiki au Muislam mwenzio anaeshiriki mambo haya muonee huruma na umfahamishe simambo yenye manufaa kwa maisha haya ila ni vishawishi vya kukupeleka Motoni. Namuomba Mollah atuepushe na kupenda na kuyafata mambo haya, na wenye nayo Mollah awashushie muongozo na kuwacha itikadi hizi za Kishetani na elimu isiyo na manufaa.
Amin.

1 comment: