Asalaam Aleiykum,
Umeagwa katika ngazi ilopita kwa kuambiwa maneno haya "Hakika Mwenye kupewa Hekima amepewa kheri nyingi sana" Nini Kheri? Kheri ni kinyume cha Shari, kama vile ilivyo (Shida na Raha)sote tunazijiua. Tahadhari sana wakati unaingia kwenye ngazi hii ya sita kwa sababu sakafu yake ya vioo, Na desturi ya Kioo ni lazima uone na uonekane, Unakwenda kwenye shughuli unajipamba kwa kujitizama kwenye kioo ili watu wakuone umependeza, kwa hiyo una kazi mbili ujione na uonekane.
Katika Ngazi hii ya sita katika hizo kheri nyingi unopewa moja yake ambayo kubwa ni hii ya kuona. Nikisema kuona usije kunishangaa na kusema mbona sote tunaona, hapana wewe huoni ila wewe unatizama, ndio maana unayakosa mambo mengi kuyaona. Hivi sasa umepanda kwenye Ghorofa ya Wacha Mungu, Upo katika Ghorofa ya Mawalii, katika ngazi hii kama hupo makini unaweza kuteremka kama utelezi mpaka ngazi ya mwanzo.
Hapa ndipo penye mtihani na mambo makubwa, Mja anafunguliwa kuyaona na kuyajua mambo kwa uwazi, Katika Ngazi hii ndio unapata Kuwaona Majini na Viumbe wengine katika maumbile yao halisi, Unakutana nao moyo kwa moyo, Hapa ndipo yanapopatikana Matibabu ya Maradhi takriban yote, Na kama Mja wa kheri basi wakija wenzio bila ya kuhitaji pesa unawatatulia matatizo yao, hapa wewe umeona bure kwanini unahitaji pesa kwa?
wakija wenzio unawaambia tatizo hili fanya hivi fanya vile utapona, hapa ndipo penye Muono wa mambo mepya kabisa, nikisema kuona nitafanya dhuluma kama sijafafanua kuona huku kukoje?.
endelea part 2
Sunday, March 30, 2014
NGAZI SABA ZA ROHO PART 2 (NGAZI 6)
Asalaam Aleiykum,
Desturi ya kuona unayoifahamu wewe ni kuchukua (Information)Nje na kuzipeleka ndani, hata hivyo mamia ya (Information)unayasahau kabla hayajafika ndani kuchambuliwa, mfano wa (Cinema)unaona Nyumba, unaona (Furniture)na kila kitu, lakini unasahau yote ila unakumbuka jambo moja nalo ni (Story)kwa hiyo utakua umeiona (Story) na yule alo (Act) kwa kufanya hivyo kuona kwako umetumia (Akili) ndio maana kila unachoona hivi sasa ni vilevile viliyopo kwenye (Memory)yako.
Na kuona kwa aina nyengine ni huku kutumia Roho(Direct communion)kuona huku kumetajwa ndani ya Quraan sura ya (Najm)aya ya 10"مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ ""Moyo haukusema Uongo uliyoyaona".
Huko ndio kuona kwa (Clear)huwezi kukadhibisha, hakuna uongo katika kuona huko, ila kuna mshangao, na kwanini ikawa kwenye Moyo? hayo tutayazungumza siku za mbele kukujulisha chini ya Moyo kuna kaa nini? Ila nitakupa kitu ukitizame(Ukicheka kama unaweza kukumbuka jitizame)kila kitu kina (Dis-appear)litizame hilo neno vizuri halafu litie maana utagundua kitu fulani, Ukicheka (Time) inapotea kwa sekunde unabakia wewe na huoni chochote, ukimaliza kucheka jiulize nani yule alocheka, hapo utagundua kumbe hata kicheko kinatokea Moyoni, na hapo hapo ndio unapo patikana huo Muono.
Kwa mara ya mwanzo unapoondolewa pazia hili au kufikia ngazi hii ya sita, utajua kumbe hapa ndio ngazi ya wale matabibu wote wa ukweli, kumbuka sio (Uchawi) sababu uchawi ni tendo linalopatikana kwenye (Akili), Lakini Utibabu unatokea kwenye Roho, Na kitokeacho kwenye Roho kimetoka kwa Mwenyewe Mollah Mkarim, (Tukawajaalia kusikia na kuona). Kuona huku anako funguliwa Mja ni hisani ya Mollah wako kukuonesha mambo yalofichikana, Ili kumkaribisha kiumbe katika ufalme wa mambo ya siri ndio pazia linaondoshwa kidogo kidogo kwa daraja yako ya Ucha Mungu, na zaidi sana hupewa wale walokwisha kuihama dunia hii wakawa hawana haja nayo japokua wako hai.
endelea part 3
Desturi ya kuona unayoifahamu wewe ni kuchukua (Information)Nje na kuzipeleka ndani, hata hivyo mamia ya (Information)unayasahau kabla hayajafika ndani kuchambuliwa, mfano wa (Cinema)unaona Nyumba, unaona (Furniture)na kila kitu, lakini unasahau yote ila unakumbuka jambo moja nalo ni (Story)kwa hiyo utakua umeiona (Story) na yule alo (Act) kwa kufanya hivyo kuona kwako umetumia (Akili) ndio maana kila unachoona hivi sasa ni vilevile viliyopo kwenye (Memory)yako.
Na kuona kwa aina nyengine ni huku kutumia Roho(Direct communion)kuona huku kumetajwa ndani ya Quraan sura ya (Najm)aya ya 10"مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ ""Moyo haukusema Uongo uliyoyaona".
Huko ndio kuona kwa (Clear)huwezi kukadhibisha, hakuna uongo katika kuona huko, ila kuna mshangao, na kwanini ikawa kwenye Moyo? hayo tutayazungumza siku za mbele kukujulisha chini ya Moyo kuna kaa nini? Ila nitakupa kitu ukitizame(Ukicheka kama unaweza kukumbuka jitizame)kila kitu kina (Dis-appear)litizame hilo neno vizuri halafu litie maana utagundua kitu fulani, Ukicheka (Time) inapotea kwa sekunde unabakia wewe na huoni chochote, ukimaliza kucheka jiulize nani yule alocheka, hapo utagundua kumbe hata kicheko kinatokea Moyoni, na hapo hapo ndio unapo patikana huo Muono.
Kwa mara ya mwanzo unapoondolewa pazia hili au kufikia ngazi hii ya sita, utajua kumbe hapa ndio ngazi ya wale matabibu wote wa ukweli, kumbuka sio (Uchawi) sababu uchawi ni tendo linalopatikana kwenye (Akili), Lakini Utibabu unatokea kwenye Roho, Na kitokeacho kwenye Roho kimetoka kwa Mwenyewe Mollah Mkarim, (Tukawajaalia kusikia na kuona). Kuona huku anako funguliwa Mja ni hisani ya Mollah wako kukuonesha mambo yalofichikana, Ili kumkaribisha kiumbe katika ufalme wa mambo ya siri ndio pazia linaondoshwa kidogo kidogo kwa daraja yako ya Ucha Mungu, na zaidi sana hupewa wale walokwisha kuihama dunia hii wakawa hawana haja nayo japokua wako hai.
endelea part 3
NGAZI SABA ZA ROHO PART 3(NGAZI 6)
Asalaam Aleiykum,
Hakika kwa Mja yoyote alopewa kuona huku basi unakua kwake ni mtihani, ambayo naogopa hata kuitaja asije Mja akadhurika au kuwadhuru viumbe wenzie, ila nakupa mfano mmoja tu halafu siendelei , katika kuona huko unaweza kupewa ukaona kiumbe mwenzio yuko katika hali ya matamanio, Na kama utafanya kitu fulani hawezi kukukatalia amri yako ya kufanya chochote, hilo ndio tatizo lenyewe, huo ndio mtihani uliyopo na mambo mengi katika ngazi hii, ndio maana hawapewi kuona huku watu wengi, ingekua balaa.
Na pazia hili pia anopewa anapewa kwa mujibu wa ukuruba wake na Mollah wake, na wako wanopewa kwa bahati itokayo kwa Mollah pia, ila hao ni wachache sana, Na wengine hupata kuchungulia tu kidogo wakajua baadhi ya mambo na wakaanza kuyatumia vibaya. Ndio utaona kupewa huku kuona mambo ya siri wengine wanageuka na kua watabiri, wanageuka kutenda makosa makubwa makubwa, na wakizuiliwa kuona huku hapo tena wanaanza kutumia viumbe wengine kama majini kuwaletea habari, na Mwenye enzi Mungu anasema katika sura ya (Mulk aya ya 5)
"وَلَقَدۡ زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِمَصَـٰبِيحَ وَجَعَلۡنَـٰهَا رُجُومً۬ا لِّلشَّيَـٰطِينِۖ وَأَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابَ ٱلسَّعِيرِ "
Kwa hakika tumeipamba mbingu (Hii ya dunia)ya karibu kwa mataa, Na tumeyafanya ili kuwapiga mashetani, Na tumewaekea tayari adhabu ya moto uwakao kwa nguvu.
Hao wanoanza kuwatuma kufanya urafiki na majini na kuanza kuwatuma ili wapate habari ndio wanaambiwa wakipanda kutaka kusikiliza wanapigwa kwa vijinga vya moto, (Hapandi mtu ngazi ya sita kwa hiyari yake mwenyewe).
Na ukiwa Mja mwema kwenye ngazi hii unapewa zaidi kuona huku mambo ya siri, Roho inafunguliwa kuona kwa upeo wa juu katika ngazi hii, na huyo muonaji unamshukia upole na ukimya katika nafsi yake, na hawi tena mwenye kuonja dhiki wala mateso, na hapo anasubiri kuipanda ngazi ya saba ambayo tutaimalizia wiki ijayo.
Hakika kwa Mja yoyote alopewa kuona huku basi unakua kwake ni mtihani, ambayo naogopa hata kuitaja asije Mja akadhurika au kuwadhuru viumbe wenzie, ila nakupa mfano mmoja tu halafu siendelei , katika kuona huko unaweza kupewa ukaona kiumbe mwenzio yuko katika hali ya matamanio, Na kama utafanya kitu fulani hawezi kukukatalia amri yako ya kufanya chochote, hilo ndio tatizo lenyewe, huo ndio mtihani uliyopo na mambo mengi katika ngazi hii, ndio maana hawapewi kuona huku watu wengi, ingekua balaa.
Na pazia hili pia anopewa anapewa kwa mujibu wa ukuruba wake na Mollah wake, na wako wanopewa kwa bahati itokayo kwa Mollah pia, ila hao ni wachache sana, Na wengine hupata kuchungulia tu kidogo wakajua baadhi ya mambo na wakaanza kuyatumia vibaya. Ndio utaona kupewa huku kuona mambo ya siri wengine wanageuka na kua watabiri, wanageuka kutenda makosa makubwa makubwa, na wakizuiliwa kuona huku hapo tena wanaanza kutumia viumbe wengine kama majini kuwaletea habari, na Mwenye enzi Mungu anasema katika sura ya (Mulk aya ya 5)
"وَلَقَدۡ زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِمَصَـٰبِيحَ وَجَعَلۡنَـٰهَا رُجُومً۬ا لِّلشَّيَـٰطِينِۖ وَأَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابَ ٱلسَّعِيرِ "
Kwa hakika tumeipamba mbingu (Hii ya dunia)ya karibu kwa mataa, Na tumeyafanya ili kuwapiga mashetani, Na tumewaekea tayari adhabu ya moto uwakao kwa nguvu.
Hao wanoanza kuwatuma kufanya urafiki na majini na kuanza kuwatuma ili wapate habari ndio wanaambiwa wakipanda kutaka kusikiliza wanapigwa kwa vijinga vya moto, (Hapandi mtu ngazi ya sita kwa hiyari yake mwenyewe).
Na ukiwa Mja mwema kwenye ngazi hii unapewa zaidi kuona huku mambo ya siri, Roho inafunguliwa kuona kwa upeo wa juu katika ngazi hii, na huyo muonaji unamshukia upole na ukimya katika nafsi yake, na hawi tena mwenye kuonja dhiki wala mateso, na hapo anasubiri kuipanda ngazi ya saba ambayo tutaimalizia wiki ijayo.
Sunday, March 23, 2014
NGAZI SABA ZA ROHO PART 1 (NGAZI 5)
Asalaam Aleiykum,
Umetokea kwenye Ngazi ya Mapenzi sasa nini kinatokea wakati Mapenzi yashajaa Moyoni, angalia nini kinatokea, tunajua chochote chenye kujaa lazima kitoke,(Maana ya kujaa nafasi hakuna tena)na mapenzi yakijaa lazima uyagawe au yatageuka sumu, yatageuka chuki, yatageuka wivu, ili kuipata salama ya mapenzi lazima (Share)hiyo ndiyo (Taqwa)kwanza unajipenda mwenyewe ikisha unapenda kilicho nje,(Ikiwa mwenyewe unajichukia vipi utapenda kilicho nje)ndio maana unapita kutangaza mpaka kupiga (msuwaki haramu)Naam na (Taqwa) yenyewe Uwapende Maskini na Mayatima, uwapende Mafukara na Viumbe wenzio Nk.
Ngazi ya 5. Unapanda ngazi hii lazima ufahamu kinachotokea katika (Ghorofa hii). Kinachotokea hapo ni Mgeni amewasili, na lazima utue mzigo wako, kwa sababu umebeba kitu Adhimu moyoni mwako, katika kitu hicho Mapenzi ukiyafungua zinamwagika zawadi za (Hekima). Kama yalivyo maua yanabeba vitu viwili muhimu(Uzuri na Harafu)Na Mapenzi vilevile yanabeba vitu viwili(Fadhila na Hekima)Na sasa yameshachanua , Na kama hujijui upo ngazi gani, basi wewe huna dawa tena.
Ngazi uliyopo hivi sasa kama ushajijua basi utakutana na aya ya 269 sura ya (Baqara) inayosema hivi:
"يُؤۡتِى ٱلۡحِڪۡمَةَ مَن يَشَآءُۚ وَمَن يُؤۡتَ ٱلۡحِڪۡمَةَ فَقَدۡ أُوتِىَ خَيۡرً۬ا ڪَثِيرً۬اۗ وَمَا يَذَّڪَّرُ إِلَّآ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَـٰبِ"
(Mwenye enzi Mungu)Humpa Hekima amtakaye, Na aliyepewa Hekima bila shaka amepewa Kheri nyingi, Na hawakumbuki ila wenye Akili.
Ndio Maana anopenda haogopi kutoa, kheri alizopewa nyingi, Zawadi imetokea Kwa Mollah wake, kajaa mapenzi mwenye hekima humkuti kucheza (Karate au Judo)kwa sababu kajaa kitu chengine kabisa(Blissful)ukenda na Magonvi anapatanisha, Na wala hachonganishi, yupo kwenye Raha ndio maana husema hata usingizi sipati, hataki kuikosa raha ya Ku (Enjoy).
Nini Hekima?
Endelea Part 2
Umetokea kwenye Ngazi ya Mapenzi sasa nini kinatokea wakati Mapenzi yashajaa Moyoni, angalia nini kinatokea, tunajua chochote chenye kujaa lazima kitoke,(Maana ya kujaa nafasi hakuna tena)na mapenzi yakijaa lazima uyagawe au yatageuka sumu, yatageuka chuki, yatageuka wivu, ili kuipata salama ya mapenzi lazima (Share)hiyo ndiyo (Taqwa)kwanza unajipenda mwenyewe ikisha unapenda kilicho nje,(Ikiwa mwenyewe unajichukia vipi utapenda kilicho nje)ndio maana unapita kutangaza mpaka kupiga (msuwaki haramu)Naam na (Taqwa) yenyewe Uwapende Maskini na Mayatima, uwapende Mafukara na Viumbe wenzio Nk.
Ngazi ya 5. Unapanda ngazi hii lazima ufahamu kinachotokea katika (Ghorofa hii). Kinachotokea hapo ni Mgeni amewasili, na lazima utue mzigo wako, kwa sababu umebeba kitu Adhimu moyoni mwako, katika kitu hicho Mapenzi ukiyafungua zinamwagika zawadi za (Hekima). Kama yalivyo maua yanabeba vitu viwili muhimu(Uzuri na Harafu)Na Mapenzi vilevile yanabeba vitu viwili(Fadhila na Hekima)Na sasa yameshachanua , Na kama hujijui upo ngazi gani, basi wewe huna dawa tena.
Ngazi uliyopo hivi sasa kama ushajijua basi utakutana na aya ya 269 sura ya (Baqara) inayosema hivi:
"يُؤۡتِى ٱلۡحِڪۡمَةَ مَن يَشَآءُۚ وَمَن يُؤۡتَ ٱلۡحِڪۡمَةَ فَقَدۡ أُوتِىَ خَيۡرً۬ا ڪَثِيرً۬اۗ وَمَا يَذَّڪَّرُ إِلَّآ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَـٰبِ"
(Mwenye enzi Mungu)Humpa Hekima amtakaye, Na aliyepewa Hekima bila shaka amepewa Kheri nyingi, Na hawakumbuki ila wenye Akili.
Ndio Maana anopenda haogopi kutoa, kheri alizopewa nyingi, Zawadi imetokea Kwa Mollah wake, kajaa mapenzi mwenye hekima humkuti kucheza (Karate au Judo)kwa sababu kajaa kitu chengine kabisa(Blissful)ukenda na Magonvi anapatanisha, Na wala hachonganishi, yupo kwenye Raha ndio maana husema hata usingizi sipati, hataki kuikosa raha ya Ku (Enjoy).
Nini Hekima?
Endelea Part 2
NGAZI SABA ZA ROHO PART 2 (NGAZI 5)
Asalaam Aleiykum,
Hekima ni Mtiririko wa Fahamu zinazotokea kusiko fahamika kwa (Mollah wetu)Usije kwenda kwa mganga kutaka kuitafuta hekima.
Nini Fahamu?Fahamu ni ujuzi wa ithbati wa jambo au mambo yenye kuthibitika, (Mfano)kama sasa hivi unavojijua uko macho, Na ukiwa umelala unakua hujijui huna Hekima, Na tafauti yako na mwenye Hekima kuwa wewe umelala lakini upo macho, Na yeye yupo macho ila keshaamka mwanzo, hiyo ndio tafauti yenu.
Huyo mwenye Hekima kapanda ngazi mapema, na wewe unaweza kupanda lakini inabidi tukuamshe mapema(Salaah Salaah)tukutikise mabega wewe amka kuna kitu Hekima na wewe ukipate, Upo kwenye ngazi ya tano umejaa mapenzi na hekima inaaanza kutumika, hutomkuta mwenye hekima kutumia maguvu, wakati wote anapata zawadi za hekima kutoka kwa Mollah wake na yeye anazitumia kwa ajili ya viumbe wenzie, kwa ajili ya kuwaita kwenye hekima, kuwashauri kwa mambo ya kheri, penye matatizo yeye huingia kuyatatua, penye ugonvi yeye huwa wa mwanzo kupatanisha, matendo yake yote yanashikana na dalili za kheri.
Katika Ngazi hii mwenye Hekima anajua kwa yakini kwamba matatizo, maradhi na madhara yote yanatokana na kwenda kinyume na mpangilio wa sheria za Mwenye enzi Mungu.
Sasa kwa kuwa keshajua anatumia muongozo utokao kwa Mollah wake, Na hiyo ndio maana ya sisi kuomba kwetu (Yaa Rabb)tupe Elimu na Hekima itokanayo kwako.
Kumbuka upo katika Ngazi ya 5 na matarajio yangu ushafahamu nini kusudio la darsa hii ya Ngazi saba za Roho. Na kama hujafahamu hizo (Ngazi)saba ni (Phase)ya Umri wako unopita au niseme mpito wa (Tabaka) la Maisha yako, Sasa kwa wale ambao wanapita katika mpito huu huku wamelala basi hata wakifikia Umri huu wa kupewa Hekima bado wao hawajui, hawataki, wabishi, hawawezi kuwacha. Na wakitaka yao basi utasikia wanakwenda kwa (Zee la Hekima)kuchukua ushauri, Unalijua nani zee la (Hekima)?ukisikia zee la hekima ni mganga, watu wengi siku hizi huko ndiko walikohamia hususan Waumini.
Sasa Mwenye enzi Mungu anatwambia nini kuhusu Mja Mwenye Hekima (Sura ya Luqman aya ya 12)
وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا لُقۡمَـٰنَ ٱلۡحِكۡمَةَ أَنِ ٱشۡكُرۡ لِلَّهِۚ وَمَن يَشۡڪُرۡ فَإِنَّمَا يَشۡكُرُ لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَنِىٌّ حَمِيدٌ
Hakika tulimpa Luqman hikma, tukamwambia Mshukuru Mwenye Enzi Mungu, Na atakaye shukuru, kwa Yakini anashukuru kwa ajili ya nafsi yake, na atakayekufuru, Mwenye enzi Mungu ni mkwasi(Alojitosheleza)asifiwaye(hana haja ya shukurani yako).
Sasa kwanini unashukuru? unashukuru kwa sababu ya kuona wewe hustahiki kwa hicho ulichopewa, lakini kwa mapenzi ya Mollah wako kakuchagua kukupa wewe, ukiligundua hilo ndio wewe una nyenyekea kwa furaha ya mapenzi kumshukuru Mollah wako kwa kukupa Fadhila na Baraka zake zinazoendelea kukushukia mpaka mwisho wa Uhai wako.
Endelea part 3
Hekima ni Mtiririko wa Fahamu zinazotokea kusiko fahamika kwa (Mollah wetu)Usije kwenda kwa mganga kutaka kuitafuta hekima.
Nini Fahamu?Fahamu ni ujuzi wa ithbati wa jambo au mambo yenye kuthibitika, (Mfano)kama sasa hivi unavojijua uko macho, Na ukiwa umelala unakua hujijui huna Hekima, Na tafauti yako na mwenye Hekima kuwa wewe umelala lakini upo macho, Na yeye yupo macho ila keshaamka mwanzo, hiyo ndio tafauti yenu.
Huyo mwenye Hekima kapanda ngazi mapema, na wewe unaweza kupanda lakini inabidi tukuamshe mapema(Salaah Salaah)tukutikise mabega wewe amka kuna kitu Hekima na wewe ukipate, Upo kwenye ngazi ya tano umejaa mapenzi na hekima inaaanza kutumika, hutomkuta mwenye hekima kutumia maguvu, wakati wote anapata zawadi za hekima kutoka kwa Mollah wake na yeye anazitumia kwa ajili ya viumbe wenzie, kwa ajili ya kuwaita kwenye hekima, kuwashauri kwa mambo ya kheri, penye matatizo yeye huingia kuyatatua, penye ugonvi yeye huwa wa mwanzo kupatanisha, matendo yake yote yanashikana na dalili za kheri.
Katika Ngazi hii mwenye Hekima anajua kwa yakini kwamba matatizo, maradhi na madhara yote yanatokana na kwenda kinyume na mpangilio wa sheria za Mwenye enzi Mungu.
Sasa kwa kuwa keshajua anatumia muongozo utokao kwa Mollah wake, Na hiyo ndio maana ya sisi kuomba kwetu (Yaa Rabb)tupe Elimu na Hekima itokanayo kwako.
Kumbuka upo katika Ngazi ya 5 na matarajio yangu ushafahamu nini kusudio la darsa hii ya Ngazi saba za Roho. Na kama hujafahamu hizo (Ngazi)saba ni (Phase)ya Umri wako unopita au niseme mpito wa (Tabaka) la Maisha yako, Sasa kwa wale ambao wanapita katika mpito huu huku wamelala basi hata wakifikia Umri huu wa kupewa Hekima bado wao hawajui, hawataki, wabishi, hawawezi kuwacha. Na wakitaka yao basi utasikia wanakwenda kwa (Zee la Hekima)kuchukua ushauri, Unalijua nani zee la (Hekima)?ukisikia zee la hekima ni mganga, watu wengi siku hizi huko ndiko walikohamia hususan Waumini.
Sasa Mwenye enzi Mungu anatwambia nini kuhusu Mja Mwenye Hekima (Sura ya Luqman aya ya 12)
وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا لُقۡمَـٰنَ ٱلۡحِكۡمَةَ أَنِ ٱشۡكُرۡ لِلَّهِۚ وَمَن يَشۡڪُرۡ فَإِنَّمَا يَشۡكُرُ لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَنِىٌّ حَمِيدٌ
Hakika tulimpa Luqman hikma, tukamwambia Mshukuru Mwenye Enzi Mungu, Na atakaye shukuru, kwa Yakini anashukuru kwa ajili ya nafsi yake, na atakayekufuru, Mwenye enzi Mungu ni mkwasi(Alojitosheleza)asifiwaye(hana haja ya shukurani yako).
Sasa kwanini unashukuru? unashukuru kwa sababu ya kuona wewe hustahiki kwa hicho ulichopewa, lakini kwa mapenzi ya Mollah wako kakuchagua kukupa wewe, ukiligundua hilo ndio wewe una nyenyekea kwa furaha ya mapenzi kumshukuru Mollah wako kwa kukupa Fadhila na Baraka zake zinazoendelea kukushukia mpaka mwisho wa Uhai wako.
Endelea part 3
NGAZI SABA ZA ROHO PART 3 (NGAZI 5)
Asalaam Aleiykum,
Ama Mwenye kukufuru "Ambaye kapewa hiyo hekima" akaanza kuitumia vyengine, akaanza kuleta ujanja ujanja, ukweli akauchanganya na uongo, basi atamkuta Mollah hana haja na Mtu huyo, Na ukitaka kumjua Mwenye hekima aliye mkweli utaangalia matendo yake yeye si mwenye kulazimisha jambo,na wala hatoi ushauri. Nini maana ya ushauri? Ushauri ni kitu huna uhakika nacho kitafaa au hakifai jaribuni, hiyo ndio maana ya kushauri, lakini hekima anatoa nasaha kwa kuwa yeye anaelewa jambo kwa uhakika, ndio maana utaona aya inofatia ya (13)Luqman anasema.
وَإِذۡ قَالَ لُقۡمَـٰنُ لِٱبۡنِهِۦ وَهُوَ يَعِظُهُ ۥ يَـٰبُنَىَّ لَا تُشۡرِكۡ بِٱللَّهِۖ إِنَّ ٱلشِّرۡكَ لَظُلۡمٌ عَظِيمٌ۬
Na Luqman alipomwambia mwanawe, Hali ya kuwa anampa Nasiha, Ewe Mwanangu usimshirikishe Mwenye enzi Mungu, maana kushirikisha ni dhuluma kubwa.
Jambo la mwanzo mwenye hekima katika ngazi hii analolijua ni (Shirk)ya aina yoyote ile kuwa ni dhulma kubwa, na Mti wa (Shirk)ni mkubwa ndio maana akmwambia mwanawe kwa tendo la kuelewa ewe mwanangu usimshirikishe Mollah wako kwa chochote kile, vipi leo unamshirikisha yule ambaye kakuumba wewe na vyote vilivyomo kwenye Ulimwengu huu, sijui unamtegemea (Boss)wako, kama si fulani nisingepata kitu fulani, hivi na vile, umekamata matawi chungu nzima ya shirk, basi kitu cha mwanzo usimshrikishe Mollah wako na chochote, na ukiona humshirikishi Mollah wako na chochote basi jua hekima ishaanaza kuteremka.
Utafikri wewe vipi yule aliyeumba mbingu na Ardhi awe na mshirika hapa Ardhini, vipi leo uwe unaamini Shetani na Mizimu ndio ilokufanya ufanikiwe, ukiwa katika Imani hizo jua bado hekima haijafika kwako, Na wala haitofika.
Kwa hiyo utagundua Mwenye Hekima ni mwenye kumtegemea Mollah wake kwa mambo yake yote, (Kumbuka na wewe upo ngazi ya 5, na hiyo tano ukiiwekea Sifuri nyuma inageuka kuwa 50)huo labda ndio Umri wako pengine ndio wakati wa kuzipata hizo Hekima, Luqman anamuusia mwanawe , hekima inatoka kwa mtu mzima kwenda kwa mtoto "Ewe"Mwanangu.
يَـٰبُنَىَّ إِنَّہَآ إِن تَكُ مِثۡقَالَ حَبَّةٍ۬ مِّنۡ خَرۡدَلٍ۬ فَتَكُن فِى صَخۡرَةٍ أَوۡ فِى ٱلسَّمَـٰوَٲتِ أَوۡ فِى ٱلۡأَرۡضِ يَأۡتِ بِہَا ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَطِيفٌ خَبِيرٌ۬
Ewe Mwanangu kwa hakika jambo lolote lile ijapokua na uzito wa chembe ya hardali(Atom)likawa ndani ya jabali, au mbinguni au katika ardhi, Mwenye Enzi Mungu atalileta(Amlipe alofanya)bila shaka Mwenye enzi Mungu ni mjuzi wa mambo yalofichikana, na mambo yalo dhahiri.
Na ukitaka ujue chochote kidogo katika thamani ya Hekima wewe jitizame kwa siku unasema uongo mara ngapi japo wa kipuuzi, ukiona husemi hata mara moja basi jijue ushajisafishia njia ya kuipata hekima. Na kuna mtihani mwengine mwepesi ukitaka kumjua miongoni mwenu kama yupo mwenye Hekima, tizama kama mpo kwenye chakula nyote mkimaliza utasikia mnasema tumeshiba, lakini mwenye hekima atanyanyuka na kusema chakula kitamu, tizama tafauti yake ya maneno hapo.
يَـٰبُنَىَّ أَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ وَأۡمُرۡ بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَٱنۡهَ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَٱصۡبِرۡ عَلَىٰ مَآ أَصَابَكَۖ إِنَّ ذَٲلِكَ مِنۡ عَزۡمِ ٱلۡأُمُورِ
Ewe Mwanangu Simamisha Sala na uamrishe Mema, Na ukataze mabaya, na usubiri yale yatakayo kusibu, hakika hayo ni katika mambo yanayostahiki kuadhimiwa.
Ewe Mja usidhani kwamba unasimamisha Sala hakitokufika kitu, uko katika Ulimwengu huu kumbuka uwe tayari kwa chochote kitachokufika, kiridhie na ukikiridhia (Ushakwenda)(Beyond)hakikugusi tena, kitagusa mwili wako, kitagusa akili yako, lakini hakikugusi wewe abadan, ukiligundua hilo basi wewe una hekima, ukilijua hilo basi wewe unaishi ndani ya hekima, Na ukiwa katika hiyo hekima basi sasa anza kuamrisha mema na kukataza mabaya, Na ukiitaka hekima ikufike sawa sawa basi Ewe Mwanangu.
وَلَا تُصَعِّرۡ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمۡشِ فِى ٱلۡأَرۡضِ مَرَحًاۖ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخۡتَالٍ۬ فَخُورٍ۬
Wala usiwatizame watu(Kwa Ujeuri wa kuwanyanyulia Pua)kwa upande mmoja wa uso, (Na)Wala usende katika Nchi kwa Maringo, hakika Mwenye Enzi Mungu hampendi kila ajivunae (Mwenye)kujifagharisha.
Huwezi kupewa Hekima ukiwa una jeuri za kuwatizama wenzio kwa kuwageuzia Shingo kwa jeuri na kuwakejeli, Na wala usijione una Utajiri au Elimu, ukaanza jeuri kumbuka utanyimwa Hekima na (Kubakia na cheo cha Babu Jinga). Na wala usitembee ukawa unatingisha Mabega kwa vyeo ulivyo navyo ili watu wajue au waulizane unamjua yule alopita, kwani kwa kufanya hivyo huwi kabisa Mtu wa Mwenye enzi Mungu, hupandi kabisa katika ngazi ya 5, Na Mollah wako si mwenye kupenda wanojifagharisha.
Ewe Mwanangu
وَٱقۡصِدۡ فِى مَشۡيِكَ وَٱغۡضُضۡ مِن صَوۡتِكَۚ إِنَّ أَنكَرَ ٱلۡأَصۡوَٲتِ لَصَوۡتُ ٱلۡحَمِيرِ
Na ushike mwendo wa katikati, na uteremshe sauti yako, bila shaka sauti ya punda ni mbaya kuliko sauti zote.
Shika mwendo wa katikati, usiwe umezama upande mmoja ukawa kila kitu haramu, unarusha mafatwa bila ya hekima yoyote, na wala usizame kwenye maasi, maana yake kuna watu wanatoka kwenye maasi moja kwa moja wanachupia dini, na wanakua wakali wao, wale wote walokuwamo kwenye dini tokea mwanzo hawafai, hawana Ibada, hapa unapewa nasaha zenye Hekima Shika mwendo wa katikati, unaujua mwendo wa katikati ni upi? ni Furaha, katikati ni Hekima, katikati ni (Blissfull). Na wala usiwe unapiga makele ovyo ovyo kama mchiriku, unazuia hata hekima kukushukia kutwa unazungumza, kila siku una hutubia, mazungumzo kwa wingi na makelele chungu nzima kama ya debe. Na unajijua kwanini unapiga makelele sana, jichunguze utagundua ni Tafrani na mambo mengi kichwani, pengine ujinga umezidi, au mgonjwa unataka upige makelele upate nafuu, ndio maana utaona mwenye machungu anapiga kelele, huwezi kuwa na hekima ikiwa litakuwepo zogo kichwani mwako, umepanda ngazi ya tano unatakiwa uwe mpole, uwe karimu, uwe mkimya na hapo tena utaona umeshakuwa Hekima, kila kitu chako kinageuka kuwa hekima na hekima ikitimia unakuwa umeshaaminiwa na Mfalme wa Mbinguni, na ukiaminiwa na Mollah wako unapewa kitu chengine ambacho tutakutana nacho ngazi ya sita. Inshaa Allah wiki ijayo.
Ama Mwenye kukufuru "Ambaye kapewa hiyo hekima" akaanza kuitumia vyengine, akaanza kuleta ujanja ujanja, ukweli akauchanganya na uongo, basi atamkuta Mollah hana haja na Mtu huyo, Na ukitaka kumjua Mwenye hekima aliye mkweli utaangalia matendo yake yeye si mwenye kulazimisha jambo,na wala hatoi ushauri. Nini maana ya ushauri? Ushauri ni kitu huna uhakika nacho kitafaa au hakifai jaribuni, hiyo ndio maana ya kushauri, lakini hekima anatoa nasaha kwa kuwa yeye anaelewa jambo kwa uhakika, ndio maana utaona aya inofatia ya (13)Luqman anasema.
وَإِذۡ قَالَ لُقۡمَـٰنُ لِٱبۡنِهِۦ وَهُوَ يَعِظُهُ ۥ يَـٰبُنَىَّ لَا تُشۡرِكۡ بِٱللَّهِۖ إِنَّ ٱلشِّرۡكَ لَظُلۡمٌ عَظِيمٌ۬
Na Luqman alipomwambia mwanawe, Hali ya kuwa anampa Nasiha, Ewe Mwanangu usimshirikishe Mwenye enzi Mungu, maana kushirikisha ni dhuluma kubwa.
Jambo la mwanzo mwenye hekima katika ngazi hii analolijua ni (Shirk)ya aina yoyote ile kuwa ni dhulma kubwa, na Mti wa (Shirk)ni mkubwa ndio maana akmwambia mwanawe kwa tendo la kuelewa ewe mwanangu usimshirikishe Mollah wako kwa chochote kile, vipi leo unamshirikisha yule ambaye kakuumba wewe na vyote vilivyomo kwenye Ulimwengu huu, sijui unamtegemea (Boss)wako, kama si fulani nisingepata kitu fulani, hivi na vile, umekamata matawi chungu nzima ya shirk, basi kitu cha mwanzo usimshrikishe Mollah wako na chochote, na ukiona humshirikishi Mollah wako na chochote basi jua hekima ishaanaza kuteremka.
Utafikri wewe vipi yule aliyeumba mbingu na Ardhi awe na mshirika hapa Ardhini, vipi leo uwe unaamini Shetani na Mizimu ndio ilokufanya ufanikiwe, ukiwa katika Imani hizo jua bado hekima haijafika kwako, Na wala haitofika.
Kwa hiyo utagundua Mwenye Hekima ni mwenye kumtegemea Mollah wake kwa mambo yake yote, (Kumbuka na wewe upo ngazi ya 5, na hiyo tano ukiiwekea Sifuri nyuma inageuka kuwa 50)huo labda ndio Umri wako pengine ndio wakati wa kuzipata hizo Hekima, Luqman anamuusia mwanawe , hekima inatoka kwa mtu mzima kwenda kwa mtoto "Ewe"Mwanangu.
يَـٰبُنَىَّ إِنَّہَآ إِن تَكُ مِثۡقَالَ حَبَّةٍ۬ مِّنۡ خَرۡدَلٍ۬ فَتَكُن فِى صَخۡرَةٍ أَوۡ فِى ٱلسَّمَـٰوَٲتِ أَوۡ فِى ٱلۡأَرۡضِ يَأۡتِ بِہَا ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَطِيفٌ خَبِيرٌ۬
Ewe Mwanangu kwa hakika jambo lolote lile ijapokua na uzito wa chembe ya hardali(Atom)likawa ndani ya jabali, au mbinguni au katika ardhi, Mwenye Enzi Mungu atalileta(Amlipe alofanya)bila shaka Mwenye enzi Mungu ni mjuzi wa mambo yalofichikana, na mambo yalo dhahiri.
Na ukitaka ujue chochote kidogo katika thamani ya Hekima wewe jitizame kwa siku unasema uongo mara ngapi japo wa kipuuzi, ukiona husemi hata mara moja basi jijue ushajisafishia njia ya kuipata hekima. Na kuna mtihani mwengine mwepesi ukitaka kumjua miongoni mwenu kama yupo mwenye Hekima, tizama kama mpo kwenye chakula nyote mkimaliza utasikia mnasema tumeshiba, lakini mwenye hekima atanyanyuka na kusema chakula kitamu, tizama tafauti yake ya maneno hapo.
يَـٰبُنَىَّ أَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ وَأۡمُرۡ بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَٱنۡهَ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَٱصۡبِرۡ عَلَىٰ مَآ أَصَابَكَۖ إِنَّ ذَٲلِكَ مِنۡ عَزۡمِ ٱلۡأُمُورِ
Ewe Mwanangu Simamisha Sala na uamrishe Mema, Na ukataze mabaya, na usubiri yale yatakayo kusibu, hakika hayo ni katika mambo yanayostahiki kuadhimiwa.
Ewe Mja usidhani kwamba unasimamisha Sala hakitokufika kitu, uko katika Ulimwengu huu kumbuka uwe tayari kwa chochote kitachokufika, kiridhie na ukikiridhia (Ushakwenda)(Beyond)hakikugusi tena, kitagusa mwili wako, kitagusa akili yako, lakini hakikugusi wewe abadan, ukiligundua hilo basi wewe una hekima, ukilijua hilo basi wewe unaishi ndani ya hekima, Na ukiwa katika hiyo hekima basi sasa anza kuamrisha mema na kukataza mabaya, Na ukiitaka hekima ikufike sawa sawa basi Ewe Mwanangu.
وَلَا تُصَعِّرۡ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمۡشِ فِى ٱلۡأَرۡضِ مَرَحًاۖ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخۡتَالٍ۬ فَخُورٍ۬
Wala usiwatizame watu(Kwa Ujeuri wa kuwanyanyulia Pua)kwa upande mmoja wa uso, (Na)Wala usende katika Nchi kwa Maringo, hakika Mwenye Enzi Mungu hampendi kila ajivunae (Mwenye)kujifagharisha.
Huwezi kupewa Hekima ukiwa una jeuri za kuwatizama wenzio kwa kuwageuzia Shingo kwa jeuri na kuwakejeli, Na wala usijione una Utajiri au Elimu, ukaanza jeuri kumbuka utanyimwa Hekima na (Kubakia na cheo cha Babu Jinga). Na wala usitembee ukawa unatingisha Mabega kwa vyeo ulivyo navyo ili watu wajue au waulizane unamjua yule alopita, kwani kwa kufanya hivyo huwi kabisa Mtu wa Mwenye enzi Mungu, hupandi kabisa katika ngazi ya 5, Na Mollah wako si mwenye kupenda wanojifagharisha.
Ewe Mwanangu
وَٱقۡصِدۡ فِى مَشۡيِكَ وَٱغۡضُضۡ مِن صَوۡتِكَۚ إِنَّ أَنكَرَ ٱلۡأَصۡوَٲتِ لَصَوۡتُ ٱلۡحَمِيرِ
Na ushike mwendo wa katikati, na uteremshe sauti yako, bila shaka sauti ya punda ni mbaya kuliko sauti zote.
Shika mwendo wa katikati, usiwe umezama upande mmoja ukawa kila kitu haramu, unarusha mafatwa bila ya hekima yoyote, na wala usizame kwenye maasi, maana yake kuna watu wanatoka kwenye maasi moja kwa moja wanachupia dini, na wanakua wakali wao, wale wote walokuwamo kwenye dini tokea mwanzo hawafai, hawana Ibada, hapa unapewa nasaha zenye Hekima Shika mwendo wa katikati, unaujua mwendo wa katikati ni upi? ni Furaha, katikati ni Hekima, katikati ni (Blissfull). Na wala usiwe unapiga makele ovyo ovyo kama mchiriku, unazuia hata hekima kukushukia kutwa unazungumza, kila siku una hutubia, mazungumzo kwa wingi na makelele chungu nzima kama ya debe. Na unajijua kwanini unapiga makelele sana, jichunguze utagundua ni Tafrani na mambo mengi kichwani, pengine ujinga umezidi, au mgonjwa unataka upige makelele upate nafuu, ndio maana utaona mwenye machungu anapiga kelele, huwezi kuwa na hekima ikiwa litakuwepo zogo kichwani mwako, umepanda ngazi ya tano unatakiwa uwe mpole, uwe karimu, uwe mkimya na hapo tena utaona umeshakuwa Hekima, kila kitu chako kinageuka kuwa hekima na hekima ikitimia unakuwa umeshaaminiwa na Mfalme wa Mbinguni, na ukiaminiwa na Mollah wako unapewa kitu chengine ambacho tutakutana nacho ngazi ya sita. Inshaa Allah wiki ijayo.
Sunday, March 16, 2014
NGAZI SABA ZA ROHO PART 1 (NGAZI 4)
Asalaam Aleiykum,
Tumepita kwenye maajabu na kuangaza kule na huku na kama umekwenda (Deep)itakua umegundua mambo mengi ambayo hayeshi na wala huwezi kuyagundua, hujui uwache lipi ushike lipi, dunia nzima ni maajabu matupu, Sasa unatamani upande ngazi ya Nne, shauku imekushika, ukifika hapa sasa unapewa msaada wa kuipanda ngazi hii kwa (Lift)unachukuliwa kama (Airport)na Ngazi ya Umeme, mara huyo unajikuta umewasili kwenye ghorofa ukaapo Moyo, Ghorofa yanapoishi Mapenzi.
Ufikapo kwenye Ngazi hii la mwanzo kabisa unakumbwa na (Khofu)kumbuka sio (Hofu) tafauti yake khofu ni afya, khofu ni furaha, na hofu ni maradhi, woga, shida balaa, Sasa kwenye Ngazi hii unakumbwa na khofu, ikisha unajaa unyenyekevu, katika Ngazi hii mapenzi unayokutana nayo ni ya kudumu, kila wakati hutaki ladha hii ikutoke, hapo ndio unapata siri ya kwanini kila kiumbe kimejaa mapenzi,sasa utakua unamuona Paka na vitoto vyake kwa njia nyengine, kuku na vitoto vyake kwa njia nyengine kabisa, utawatizama Ndege na vikinda vyake kwa mtazamo mwengine kabisa, ukishamaliza wanyama utagundua kumbe mpaka miti ina mapenzi, hata Miti nayo inahuzunika, mpenzi wake akifa au akikatwa kuwa mbao basi iangalie miti ilosalia inakua na hali gani?.
Mpaka Samaki nao wanapendana? nini hichi kitu kinachoitwa Mapenzi.
Nini Mapenzi? Mapenzi ni Miujiza, Nini Miujiza?
Miujiza ni kitu chenye kutokea au kubadilika bila ya matarijio, kumbuka umetoka kwenye Maajabu na sasa unaingia kwenye Miujiza, Na pia napenda uelewe vitu hivi vitatu (Maisha,Kifo,Na Mapenzi)vyote ni Miujiza(Mystirious)unaishi navyo lakini hujui siri yake, vyote vinatokea kinyume cha matarajio yako, Sasa kama ushaishi kwenye Maajabu nakuta utumbukie sasa kwenye Ulimwengu wa Miujiza ambao wewe huna Mamlaka nao.
Endelea Part 2
Tumepita kwenye maajabu na kuangaza kule na huku na kama umekwenda (Deep)itakua umegundua mambo mengi ambayo hayeshi na wala huwezi kuyagundua, hujui uwache lipi ushike lipi, dunia nzima ni maajabu matupu, Sasa unatamani upande ngazi ya Nne, shauku imekushika, ukifika hapa sasa unapewa msaada wa kuipanda ngazi hii kwa (Lift)unachukuliwa kama (Airport)na Ngazi ya Umeme, mara huyo unajikuta umewasili kwenye ghorofa ukaapo Moyo, Ghorofa yanapoishi Mapenzi.
Ufikapo kwenye Ngazi hii la mwanzo kabisa unakumbwa na (Khofu)kumbuka sio (Hofu) tafauti yake khofu ni afya, khofu ni furaha, na hofu ni maradhi, woga, shida balaa, Sasa kwenye Ngazi hii unakumbwa na khofu, ikisha unajaa unyenyekevu, katika Ngazi hii mapenzi unayokutana nayo ni ya kudumu, kila wakati hutaki ladha hii ikutoke, hapo ndio unapata siri ya kwanini kila kiumbe kimejaa mapenzi,sasa utakua unamuona Paka na vitoto vyake kwa njia nyengine, kuku na vitoto vyake kwa njia nyengine kabisa, utawatizama Ndege na vikinda vyake kwa mtazamo mwengine kabisa, ukishamaliza wanyama utagundua kumbe mpaka miti ina mapenzi, hata Miti nayo inahuzunika, mpenzi wake akifa au akikatwa kuwa mbao basi iangalie miti ilosalia inakua na hali gani?.
Mpaka Samaki nao wanapendana? nini hichi kitu kinachoitwa Mapenzi.
Nini Mapenzi? Mapenzi ni Miujiza, Nini Miujiza?
Miujiza ni kitu chenye kutokea au kubadilika bila ya matarijio, kumbuka umetoka kwenye Maajabu na sasa unaingia kwenye Miujiza, Na pia napenda uelewe vitu hivi vitatu (Maisha,Kifo,Na Mapenzi)vyote ni Miujiza(Mystirious)unaishi navyo lakini hujui siri yake, vyote vinatokea kinyume cha matarajio yako, Sasa kama ushaishi kwenye Maajabu nakuta utumbukie sasa kwenye Ulimwengu wa Miujiza ambao wewe huna Mamlaka nao.
Endelea Part 2
NGAZI SABA ZA ROHO PART 2 (NGAZI 4)
Asalaam Aleiykum,
(4)Ngazi ya Nne, Ngazi hii ya Nne watu wakishafika Mtu anasahau kwanini yupo kwenye ngazi hii, Na katika usahaulivu huo unatukuta Muujiza huu katika tamaa zetu za Maisha ndio unajikuta Mtu unasutwa na Quraan sura ya Fajir aya ya 20.وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
Na Mnapenda Mali pendo la kupita kiasi"
Unayageuza hayo mapenzi kwenye kitu kisichosema, kisicho hisi,unakua ugonjwa wako mapenzi ya pesa, unapenda Mali mpaka unafikia kusahau kuwa wewe umezungukwa na watu, Mali inakucheka Maskini mtizameni huyu mgonjwa, ananipenda mimi nisokua na fahamu, badala ya kumpenda mwenye fahamu anashughulika na mimi.
Nini Mapenzi? Hakuna awezaye kujibu swali hili, nani anoweza kuueleza muujizi ni nini? tunachoweza kufanya ni kuishi kwenye muujiza, kwenda karibu yake na kujiunga na huo muujiza, kupata hisia zake, hilo tu ndilo tunaweza kulitenda na ukitoka katika huo muujiza ndio unahadithia wenzio tafsiri chungu nzima, Unaanza kwa kusema Mapenzi ni Ukarimu, Ukarimu ni Uhuru, sasa wanokusikiliza wanachanganyikiwa na maneno haya, Na kama mtu ataleta ufanisi wa lugha maana yote itampita ya kufahamu Mapenzi.
Sasa yasome nini Mapenzi ujue kwa uzuri, Mapenzi ni Uhuru na hapa Wazungu wanamsemo mzuri ikiwa utazingatia, wanasema hivi (Ukimpenda Mtu Mwache aende akirudi mwenyewe kwa hiyari yake basi jua huyo ni Kipenzi chako).
Upo katika Ngazi ya 4, Soma kwa Makini ili uishi ndani ya Muujiza huu wa Mapenzi upate kujua yanakuaje, ili yatakapo kujia au kukuta ujue unayakabili vipi, Kumbuka Miujiza ipo mingi lakini muujiza wa Mapenzi lazima Roho ipite Ngazi ya 4 ili kukutana nayo, sasa yatupie macho mapenzi. uyaone yanaanza vipi?.
Kwanza kabisa Mollah wako kwa hayo Mapenzi ya Kiumbe wake kakuumba ikisha akakufanyia Ukarimu wa Uhai na kukufanya Khalifa, Halafu tena akakupa Uhuru kukuwaachia utende unavyopenda, Halafu tena akakupa ukumbusho Ewe Kiumbe changu Ukirudi kwa hiyari yako hayo ndio Mapenzi juu yangu, Ndio akasema Mollah wetu katika Quraan mimi (Nawapenda) (Surat Buruj 13-14)إِنَّهُ ۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ
"Yeye ndiye aliyeanzisha(aliyeumba)Na ndiye atakayewarejesha(tena)وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ
"Naye ni Mwingi wa Msamaha (Na)Mpenda(Viumbe vyake).
Na hiyo ndio maana ya Ibadah,kurejea kwa Mollah wako kwa Mapenzi, Na hiyo ndio Miujiza pekee (Something inside)Ndani ya Moyo wako inakutuma umtafute na kumjua Mollah wako kipenzi kwa hiyari yako, sio kwa kuogopa Moto au kuitaka Pepo.
Kuumbwa kwako Binaadamu ni Miujiza na kurejea kwako vilevile ni Kimiujiza. Unataka kujua vipi unarejea kimiujiza hudhuria kisa hichi katika Quraan ili ujue unarejea vipi?
Endelea part 3
(4)Ngazi ya Nne, Ngazi hii ya Nne watu wakishafika Mtu anasahau kwanini yupo kwenye ngazi hii, Na katika usahaulivu huo unatukuta Muujiza huu katika tamaa zetu za Maisha ndio unajikuta Mtu unasutwa na Quraan sura ya Fajir aya ya 20.وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
Na Mnapenda Mali pendo la kupita kiasi"
Unayageuza hayo mapenzi kwenye kitu kisichosema, kisicho hisi,unakua ugonjwa wako mapenzi ya pesa, unapenda Mali mpaka unafikia kusahau kuwa wewe umezungukwa na watu, Mali inakucheka Maskini mtizameni huyu mgonjwa, ananipenda mimi nisokua na fahamu, badala ya kumpenda mwenye fahamu anashughulika na mimi.
Nini Mapenzi? Hakuna awezaye kujibu swali hili, nani anoweza kuueleza muujizi ni nini? tunachoweza kufanya ni kuishi kwenye muujiza, kwenda karibu yake na kujiunga na huo muujiza, kupata hisia zake, hilo tu ndilo tunaweza kulitenda na ukitoka katika huo muujiza ndio unahadithia wenzio tafsiri chungu nzima, Unaanza kwa kusema Mapenzi ni Ukarimu, Ukarimu ni Uhuru, sasa wanokusikiliza wanachanganyikiwa na maneno haya, Na kama mtu ataleta ufanisi wa lugha maana yote itampita ya kufahamu Mapenzi.
Sasa yasome nini Mapenzi ujue kwa uzuri, Mapenzi ni Uhuru na hapa Wazungu wanamsemo mzuri ikiwa utazingatia, wanasema hivi (Ukimpenda Mtu Mwache aende akirudi mwenyewe kwa hiyari yake basi jua huyo ni Kipenzi chako).
Upo katika Ngazi ya 4, Soma kwa Makini ili uishi ndani ya Muujiza huu wa Mapenzi upate kujua yanakuaje, ili yatakapo kujia au kukuta ujue unayakabili vipi, Kumbuka Miujiza ipo mingi lakini muujiza wa Mapenzi lazima Roho ipite Ngazi ya 4 ili kukutana nayo, sasa yatupie macho mapenzi. uyaone yanaanza vipi?.
Kwanza kabisa Mollah wako kwa hayo Mapenzi ya Kiumbe wake kakuumba ikisha akakufanyia Ukarimu wa Uhai na kukufanya Khalifa, Halafu tena akakupa Uhuru kukuwaachia utende unavyopenda, Halafu tena akakupa ukumbusho Ewe Kiumbe changu Ukirudi kwa hiyari yako hayo ndio Mapenzi juu yangu, Ndio akasema Mollah wetu katika Quraan mimi (Nawapenda) (Surat Buruj 13-14)إِنَّهُ ۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ
"Yeye ndiye aliyeanzisha(aliyeumba)Na ndiye atakayewarejesha(tena)وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ
"Naye ni Mwingi wa Msamaha (Na)Mpenda(Viumbe vyake).
Na hiyo ndio maana ya Ibadah,kurejea kwa Mollah wako kwa Mapenzi, Na hiyo ndio Miujiza pekee (Something inside)Ndani ya Moyo wako inakutuma umtafute na kumjua Mollah wako kipenzi kwa hiyari yako, sio kwa kuogopa Moto au kuitaka Pepo.
Kuumbwa kwako Binaadamu ni Miujiza na kurejea kwako vilevile ni Kimiujiza. Unataka kujua vipi unarejea kimiujiza hudhuria kisa hichi katika Quraan ili ujue unarejea vipi?
Endelea part 3
NGAZI SABA ZA ROHO PART 3 (NGAZI 4
Asalaam Aleiykum,
(In loves Death does happen) Upo Ngazi ya 4 mambo yanatokezea bila ya wewe kutaka, na hali hiyo ni haki yako lazima uipate, ama ukiikataa ni shauri lako mwenyewe.Mapenzi yanatokea kwenye Moyo wako, mabadiliko kila siku yanatokea lakini kila yakitokezea wewe hupo kabisa pengine upo Dodoma, au upo kwenye Taarab, au umeketi kwenye Gumzo huna habari ya Siri hizi zinazotokea kwenye Nafsi yako.Ni kweli maneno hayo ya mwanzo Kifo kinatokezea katika hayo mapenzi ya kitu chochote, ndio maana nikasema hapo mwanzoni (Maisha, Mapenzi na Kifo)vyote ni Miujiza kwetu, bado vinatushangaza, sasa nini kinatokezea, halafu jiulize na wewe wakati mwengine hayakutokezei baadhi ya Mambo wakati pengine unasikiza dua, au umehudhuria msiba au unasikiza mawaidha nini kinatokezea?(Al-Shuara 46)"فَأُلۡقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سَـٰجِدِينَ"
"Walipinduka Wachawi wakasujudu"
Sio wachawi hata wewe wakati mwengine inakujia uwache, inakujia upinduke lakini umezidiwa na mambo, mapenzi ya kusujudu hayajafika, hata ukisujudu bado kichwa kiko ardhini, akili ipo Disco, pengine haijarudi Dodoma, au bado hujafunga hesabu.
Kwanini walipinduka, Walipinduka kutokana na (Khofu)sio Hofu, Nini tafauti yake?utaijua huko mbele, ila napenda ujue katika Mapenzi yoyote kila mpenzi ana khofu ya kumpoteza mpenzi wake, inakuaje hali hiyo, (Khofu)ni miujiza, inatokea wapi? ndio kinacho tushangaza, "katika aya za mbele Firauni" ana Nadi nitakukateni miguu na mikono ikisha nitakusulubuni" Wachawi umewafika Ukweli, Na ukweli ukikufika unakuja na mapenzi, wameshaona hakuna chengine chochote kiwezacho kuushinda ukweli huu hata kifo hakina nafasi tena hapa, Wakasema "
"قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ "
Hakuna Dhara tena, Kwa Mollah wetu sisi tutarejea.
Hiyo ndio hali ya Mapenzi, hata kifo hujali tena, sisi tumesha (Surrender)tumetulia na tuna tamaa Mollah wetu atatusamehe Makosa yetu kwani sisi tumekua wenye kusilimu.
Na hiyo ndio Maana ya Mwingi wa Rehma Mwenye Kurehemu(Mawadat wa Rahma)Lazima viwili hivi vende pamoja, (Hapa itabidi nifafanue kidogo)kwanini hapa imewapata Khofu wakarejea kwa Mollah wao,)Tunachojua Khofu ni miujiza lakini hatujui wapi unatokea, Kitu kinafanyika Nje wewe unatetemeka ndani ya Moyo, kwanini ikawa hivyo, inabidi ufahamu msemo huu, au uwatizame baina ya shujaa na mwoga(Kwa Shujaa huenda Kilio, na Kwa Mwoga huenda kicheko)kwanini isiwe (kinyume chake)kwa sababu wawili hao wote wako sawa ila tafauti yao Shujaa ana Khofu na Mwoga ana Hofu, mambo mawili tafauti, (Khofu inatokea Moyoni) na (Hofu inatoka kwenye Akili)ndio maana mmoja yuko tayari kufa na yule wapili yupo tayari kukimbia.
Ndio maana na wewe kama unajifanya Shujaa wa hapa Duniani basi kwako kitakwenda kilio siku ya malipo, na yule alokua Mwoga hapa Ulimwenguni kwake kitakwenda kicheko. Zingatia viwili hivyo utapata faida kubwa ukifahamu. Sasa panda ngazi hii ya 4 uwapende Wazazi wako, uwapende ndugu zako, uwapende maskini na mafukara na mayatima, uwapende familia yako mke na watoto zako. Ili siku hiyo itakapo kujia siku ya habari ya Khofu usiwe katika wale wenye Sura ya Kuogopa(Sura ya Ghashiyya)ila uwe katika kundi la wale wenye sura ziloneemeka. Na hayo ndio mapenzi.
Na hakuna kitu kinacho Mtisha Kiumbe kama Moto, ndio maana mtu akiona moto hata akiwa ghorofa ya Mia, yuko radhi achupe kuliko kufa kwa Moto, watizame wanyama wanavotoka mbio kwenye misitu kuukimbia moto, Na hivi ndivo yalivyo mapenzi yetu Moto mtupu, hakuna raha magonvi yametawala, baada ya kumpenda mwenzio unapenda Mali, Unapenda Haramu, unapenda Mirungi, unapenda Pombe, unapenda Disco, kila kibaya ndicho unachopenda wewe vipi leo mapenzi matamu yatatokea kwenye Moyo wako, vipi utaipanda ngazi hii ya 4 ukiwa na mizigo hiyo yote, Miujiza hii haiwezi kutokea kwenye Moyo wako, na hata ikitokezea utaona unapenda Mpira, uko Radhi upende watu kumi na moja kuliko kumpenda mmoja alokaribu yako(Mkeo).
Tupo katika Ngazi hii ya 4 ambayo Roho pengine hivi sasa ndio inapita, sasa elewa hapa ndio kwenye kufungukiwa na Moyo wa mapenzi, hapa unagundua kumbe katika mambo mengi niyafanyao yamezungukwa na mapenzi, kumbe kama sina mapenzi nakua maradhi matupu, Bila ya Mapenzi sina afya njema, hapo tena kama una ufahamu nzuri unaomba muujiza huu wa mapenzi, na vipi muujiza huu utakufikia lazima kwanza ushushe mizigo, mapenzi yanateremka daima, lakini kwako hayafiki sababu (Vipeto)ulobeba moyoni mwako ni vingi, penzi halina sehemu ya kukaa, Matatizo sio mapenzi, matatizo ni moyo wako.
Nini Ufanye? la Mwanzo kabisa anza kusamehe kwa kila alokukosea, usibebe mizigo yao ukaweka donge moyoni, kumbuka walokosa wao kwanini unaumia wewe,Pengine katika moyo wako unatamani uwe Tajiri na hilo haliwezekani, ondosha tamaa hizo, Roho inatamani mapenzi lakini moyo hautaki.
Sasa ufanye nini katika Ngazi hii ili usikose Raha za Mapenzi, Usikose kumpenda Mollah wako, Familia yako na kila Kiumbe. Itabidi hapa tukuanzishe mazoezi, Moyo unataka mazoezi ya nje na ndani, Ama ya nje nenda (Walk)tembea tembea, moyo unakwenda mbio unapata mazoezi, Na mazoezi ya Ndani ni kushituliwa yote ni sawa, ukenda mbio unapiga kwa kasi na ukishituliwa unapiga kwa kasi, kwa hiyo (Formula)ni hiyo hiyo ya kuamsha Moyo ulo lala.
Vipi utauamsha ili ujae Mapenzi, mapenzi yaanze kuteremka, la kwanza kabisa unatakiwa ulete Maghfira angalau mara 70 kwa siku kwa muda wa miezi mitatu, Ikisha ujichunguze mambo mangapi unayapenda moyoni mwako ya hesabu(Pengine unapenda Ugali nk)ya hesabu, halafu lipitie moja baada ya jengine ujiulize kwanini, ukishajua sababu yake kazi yake imekwisha hutoganda tena kulipenda utasema (Alhamdullillah)hapo moyo wako utakua (Empty)kwa jambo hilo, sasa tena huna la kufanya subiri kidogo kidogo miujiza itaanza kushuka hapo tena Moyo utaanza kujaa mapenzi ya Mollah wako na ya kijaa tu, utaanza kupenda viumbe wenzio, sala yako itakua yakukutoa machozi, Mkeo au Mumeo umekaa naye siku zote utamuona vyengine, ukikerwa utakua unacheka, na ukifurahishwa utakua unalia kwa ajili ya mapenzi na hiyo ndio(Bliss)ipate ubadilike, Na ukibadilika kwa ajili ya mapenzi nini kinatokea?
Hayo Inshaallah tutakutana nayo kwenye ngazi ya 5.
(In loves Death does happen) Upo Ngazi ya 4 mambo yanatokezea bila ya wewe kutaka, na hali hiyo ni haki yako lazima uipate, ama ukiikataa ni shauri lako mwenyewe.Mapenzi yanatokea kwenye Moyo wako, mabadiliko kila siku yanatokea lakini kila yakitokezea wewe hupo kabisa pengine upo Dodoma, au upo kwenye Taarab, au umeketi kwenye Gumzo huna habari ya Siri hizi zinazotokea kwenye Nafsi yako.Ni kweli maneno hayo ya mwanzo Kifo kinatokezea katika hayo mapenzi ya kitu chochote, ndio maana nikasema hapo mwanzoni (Maisha, Mapenzi na Kifo)vyote ni Miujiza kwetu, bado vinatushangaza, sasa nini kinatokezea, halafu jiulize na wewe wakati mwengine hayakutokezei baadhi ya Mambo wakati pengine unasikiza dua, au umehudhuria msiba au unasikiza mawaidha nini kinatokezea?(Al-Shuara 46)"فَأُلۡقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سَـٰجِدِينَ"
"Walipinduka Wachawi wakasujudu"
Sio wachawi hata wewe wakati mwengine inakujia uwache, inakujia upinduke lakini umezidiwa na mambo, mapenzi ya kusujudu hayajafika, hata ukisujudu bado kichwa kiko ardhini, akili ipo Disco, pengine haijarudi Dodoma, au bado hujafunga hesabu.
Kwanini walipinduka, Walipinduka kutokana na (Khofu)sio Hofu, Nini tafauti yake?utaijua huko mbele, ila napenda ujue katika Mapenzi yoyote kila mpenzi ana khofu ya kumpoteza mpenzi wake, inakuaje hali hiyo, (Khofu)ni miujiza, inatokea wapi? ndio kinacho tushangaza, "katika aya za mbele Firauni" ana Nadi nitakukateni miguu na mikono ikisha nitakusulubuni" Wachawi umewafika Ukweli, Na ukweli ukikufika unakuja na mapenzi, wameshaona hakuna chengine chochote kiwezacho kuushinda ukweli huu hata kifo hakina nafasi tena hapa, Wakasema "
"قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ "
Hakuna Dhara tena, Kwa Mollah wetu sisi tutarejea.
Hiyo ndio hali ya Mapenzi, hata kifo hujali tena, sisi tumesha (Surrender)tumetulia na tuna tamaa Mollah wetu atatusamehe Makosa yetu kwani sisi tumekua wenye kusilimu.
Na hiyo ndio Maana ya Mwingi wa Rehma Mwenye Kurehemu(Mawadat wa Rahma)Lazima viwili hivi vende pamoja, (Hapa itabidi nifafanue kidogo)kwanini hapa imewapata Khofu wakarejea kwa Mollah wao,)Tunachojua Khofu ni miujiza lakini hatujui wapi unatokea, Kitu kinafanyika Nje wewe unatetemeka ndani ya Moyo, kwanini ikawa hivyo, inabidi ufahamu msemo huu, au uwatizame baina ya shujaa na mwoga(Kwa Shujaa huenda Kilio, na Kwa Mwoga huenda kicheko)kwanini isiwe (kinyume chake)kwa sababu wawili hao wote wako sawa ila tafauti yao Shujaa ana Khofu na Mwoga ana Hofu, mambo mawili tafauti, (Khofu inatokea Moyoni) na (Hofu inatoka kwenye Akili)ndio maana mmoja yuko tayari kufa na yule wapili yupo tayari kukimbia.
Ndio maana na wewe kama unajifanya Shujaa wa hapa Duniani basi kwako kitakwenda kilio siku ya malipo, na yule alokua Mwoga hapa Ulimwenguni kwake kitakwenda kicheko. Zingatia viwili hivyo utapata faida kubwa ukifahamu. Sasa panda ngazi hii ya 4 uwapende Wazazi wako, uwapende ndugu zako, uwapende maskini na mafukara na mayatima, uwapende familia yako mke na watoto zako. Ili siku hiyo itakapo kujia siku ya habari ya Khofu usiwe katika wale wenye Sura ya Kuogopa(Sura ya Ghashiyya)ila uwe katika kundi la wale wenye sura ziloneemeka. Na hayo ndio mapenzi.
Na hakuna kitu kinacho Mtisha Kiumbe kama Moto, ndio maana mtu akiona moto hata akiwa ghorofa ya Mia, yuko radhi achupe kuliko kufa kwa Moto, watizame wanyama wanavotoka mbio kwenye misitu kuukimbia moto, Na hivi ndivo yalivyo mapenzi yetu Moto mtupu, hakuna raha magonvi yametawala, baada ya kumpenda mwenzio unapenda Mali, Unapenda Haramu, unapenda Mirungi, unapenda Pombe, unapenda Disco, kila kibaya ndicho unachopenda wewe vipi leo mapenzi matamu yatatokea kwenye Moyo wako, vipi utaipanda ngazi hii ya 4 ukiwa na mizigo hiyo yote, Miujiza hii haiwezi kutokea kwenye Moyo wako, na hata ikitokezea utaona unapenda Mpira, uko Radhi upende watu kumi na moja kuliko kumpenda mmoja alokaribu yako(Mkeo).
Tupo katika Ngazi hii ya 4 ambayo Roho pengine hivi sasa ndio inapita, sasa elewa hapa ndio kwenye kufungukiwa na Moyo wa mapenzi, hapa unagundua kumbe katika mambo mengi niyafanyao yamezungukwa na mapenzi, kumbe kama sina mapenzi nakua maradhi matupu, Bila ya Mapenzi sina afya njema, hapo tena kama una ufahamu nzuri unaomba muujiza huu wa mapenzi, na vipi muujiza huu utakufikia lazima kwanza ushushe mizigo, mapenzi yanateremka daima, lakini kwako hayafiki sababu (Vipeto)ulobeba moyoni mwako ni vingi, penzi halina sehemu ya kukaa, Matatizo sio mapenzi, matatizo ni moyo wako.
Nini Ufanye? la Mwanzo kabisa anza kusamehe kwa kila alokukosea, usibebe mizigo yao ukaweka donge moyoni, kumbuka walokosa wao kwanini unaumia wewe,Pengine katika moyo wako unatamani uwe Tajiri na hilo haliwezekani, ondosha tamaa hizo, Roho inatamani mapenzi lakini moyo hautaki.
Sasa ufanye nini katika Ngazi hii ili usikose Raha za Mapenzi, Usikose kumpenda Mollah wako, Familia yako na kila Kiumbe. Itabidi hapa tukuanzishe mazoezi, Moyo unataka mazoezi ya nje na ndani, Ama ya nje nenda (Walk)tembea tembea, moyo unakwenda mbio unapata mazoezi, Na mazoezi ya Ndani ni kushituliwa yote ni sawa, ukenda mbio unapiga kwa kasi na ukishituliwa unapiga kwa kasi, kwa hiyo (Formula)ni hiyo hiyo ya kuamsha Moyo ulo lala.
Vipi utauamsha ili ujae Mapenzi, mapenzi yaanze kuteremka, la kwanza kabisa unatakiwa ulete Maghfira angalau mara 70 kwa siku kwa muda wa miezi mitatu, Ikisha ujichunguze mambo mangapi unayapenda moyoni mwako ya hesabu(Pengine unapenda Ugali nk)ya hesabu, halafu lipitie moja baada ya jengine ujiulize kwanini, ukishajua sababu yake kazi yake imekwisha hutoganda tena kulipenda utasema (Alhamdullillah)hapo moyo wako utakua (Empty)kwa jambo hilo, sasa tena huna la kufanya subiri kidogo kidogo miujiza itaanza kushuka hapo tena Moyo utaanza kujaa mapenzi ya Mollah wako na ya kijaa tu, utaanza kupenda viumbe wenzio, sala yako itakua yakukutoa machozi, Mkeo au Mumeo umekaa naye siku zote utamuona vyengine, ukikerwa utakua unacheka, na ukifurahishwa utakua unalia kwa ajili ya mapenzi na hiyo ndio(Bliss)ipate ubadilike, Na ukibadilika kwa ajili ya mapenzi nini kinatokea?
Hayo Inshaallah tutakutana nayo kwenye ngazi ya 5.
Sunday, March 9, 2014
NGAZI SABA ZA ROHO PART 1 (NGAZI 3)
Asalaam Aleiykum,
Tumepita kwenye ngazi mbili za mwanzo huku tukitupiwa maua ya Fahamu, Na kama hujapanda vizuri au ulikua unapepesuka au niseme hujafahamu, basi wacha kidogo nifafanue kabla hatujapanda ngazi hii ya Tatu. Mwanzo kabisa tumeanza na maji ya Uzazi au (Baleghe)wakati ule ulipopewa Fahamu, Ikisha tukapanda ngazi ya Pili tukakutana na (Kifo)au(Mauti), Na watu wengi wanadhani huo ndio Mwisho wetu.
Kweli inaweza kuwa mwisho wako ikiwa umekwama kwenye ngazi ya kwanza(Lift)halifanyi kazi, lakini kama umepanda ngazi ya pili ikisha ukamudu kuja katika ngazi hii ya tatu, Utafahamu nini maana ya Mauti, kwanini ukawa unasisitizwa uyakumbuke mara kwa mara, nini kinatokezea yanapokukuta Mauti, hapa napenda nifahamishe yapo mauti ya aina ngapi?
Mauti yapo ya aina mbili, unategemea vipi yatakukuta, au utayafata, kukukuta yanakuja, kuyafata ni kuyakuta na kwenda (Beyond).
Yakikukuta inakua ghafla, unakua hujajitaarisha, unahisi umeonewa, kuna mambo hujamaliza, pengine hujaandika Urithi, hapo kwa ukaidi wako unakwenda lakini kwa vishindo, Machungu, Woga mkubwa wakati wa tukio hili la kutolewa (Roho).
Ukiyafata ukayajua unakwenda (Beyond)Unakua wewe Nafsi ilotulia, unapita katika Mauti kama ulivopita kwenye kufungukiwa na (Sex)au Baleghe.
Inakuaje hali hiyo Endelea part 2
Tumepita kwenye ngazi mbili za mwanzo huku tukitupiwa maua ya Fahamu, Na kama hujapanda vizuri au ulikua unapepesuka au niseme hujafahamu, basi wacha kidogo nifafanue kabla hatujapanda ngazi hii ya Tatu. Mwanzo kabisa tumeanza na maji ya Uzazi au (Baleghe)wakati ule ulipopewa Fahamu, Ikisha tukapanda ngazi ya Pili tukakutana na (Kifo)au(Mauti), Na watu wengi wanadhani huo ndio Mwisho wetu.
Kweli inaweza kuwa mwisho wako ikiwa umekwama kwenye ngazi ya kwanza(Lift)halifanyi kazi, lakini kama umepanda ngazi ya pili ikisha ukamudu kuja katika ngazi hii ya tatu, Utafahamu nini maana ya Mauti, kwanini ukawa unasisitizwa uyakumbuke mara kwa mara, nini kinatokezea yanapokukuta Mauti, hapa napenda nifahamishe yapo mauti ya aina ngapi?
Mauti yapo ya aina mbili, unategemea vipi yatakukuta, au utayafata, kukukuta yanakuja, kuyafata ni kuyakuta na kwenda (Beyond).
Yakikukuta inakua ghafla, unakua hujajitaarisha, unahisi umeonewa, kuna mambo hujamaliza, pengine hujaandika Urithi, hapo kwa ukaidi wako unakwenda lakini kwa vishindo, Machungu, Woga mkubwa wakati wa tukio hili la kutolewa (Roho).
Ukiyafata ukayajua unakwenda (Beyond)Unakua wewe Nafsi ilotulia, unapita katika Mauti kama ulivopita kwenye kufungukiwa na (Sex)au Baleghe.
Inakuaje hali hiyo Endelea part 2
NGAZI SABA ZA ROHO PART 2 (NGAZI 3)
Asalaam Aleiykum,
Kama ulivopita kwenye (Baleghe)na kwenye Mauti unapita hivyo hivyo ukiwa (Live), Ndio maana unaambiwa kumbuka Mauti, hili tukio lipo, pia litatokea, kwa hiyo wakati una Akili yako timamu kabla hujawa mgonjwa hudhuria kadhia hii, nini kinatokezea ukihudhuria unafahamu zako kikamilifu.
(3)Ngazi ya Tatu: Inatokezea (Transformation)mabadiliko makubwa, yakiambatana na maajabu makubwa, unakua (New Man) kama kweli utaipanda Ngazi hii kwa fahamu zako ukadhihiri ukweli wa (Mauti)inakujia Fahamu, kumbuka Fahamu inatokea ndani sio kwa yule (maiti)unayemuona ila (Understanding) ya kujua kumbe kinachokufa ni kiwiliwili changu, Kinachopita katika haya Mauti ni kitu chengine kabisa ambacho hakiguswi na haya Mauti, Nini hichi ambacho baada ya Mauti yangu kinabakia?.
Jee Naweza kukijua nikiwa Hai, sio mpaka nisubiri mpaka siku yangu ya kufa, Jawabu ndio,بَلِ ٱلۡإِنسَـٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَة.
Anza safari ya kukutana na Nafsi na ukikutana nayo inakupeleka katika safari ya maajabu, inakutoa katika dhiki ya Dunia na kukupeleka kwenye Raha na maajabu ya Ulimwengu huu ambayo ulikua huyajui, Na ukiingia katika Ulimwengu wa Fahamu hii ya kuijua Nafsi yako unabadilika na kuwa Mtu mwengine kabisa, unatoweka katika maisha ya kawaida na hapo tena unaanza safari ya Ulimwengu wa kushangaza nini unakutana nacho katika maajabu hayo, katika ngazi hii kila kitu unakiona kwa njia nyengine kabisa, kila jambo linajifungua tafsiri yake na kuweka wazi siri zake.
Unapokutana na Nafsi yako kitu cha mwanzo unacho gundua ni kuona kumbe huu Mwili wangu (Body) ni (Inteligence)tupu inafanya kazi bila ya mimi kuingilia, ni miujiza baada ya miujiza inatumika, una elewa kumbe mimi nimeubeba tu mwili huu, lakini unafanya kazi zake bila ya kunihitaji mimi, unasaga chakula, unasafisha damu, unajiponesha wenyewe, na unafanya kazi zake nyingi pasi mimi kuingilia, kuanzia kidole gumba mpaka utosini muujiza huu unajitosheleza wenyewe.
Hapo tena unagundua kumbe mimi nimebeba kiwanda kizima natembea nacho, Nani huyu Mwenye kujua, nani huyu mwenye kusikia,Nani huyu Mwenye kuhisi, Nani huyu anoshuhudia haya yote, Na baada ya kushuhudia mwisho anakwenda wapi huyu Shahidi?, hapo sasa ukimaliza utaanza kuangaza Nje uone nako kuna nini?,(Hakika Nafsi ni Yenye kuona) Ukiweza kuona basi na kutizama inakua Rahisi, kumbuka kuona ni (Within)Ndani, Na kutizama ni (Outer)Nje hapo utaanza kuona mengine ya mfano kama wako na mengine zaidi, Nini hayo?
Endelea Part 3
Kama ulivopita kwenye (Baleghe)na kwenye Mauti unapita hivyo hivyo ukiwa (Live), Ndio maana unaambiwa kumbuka Mauti, hili tukio lipo, pia litatokea, kwa hiyo wakati una Akili yako timamu kabla hujawa mgonjwa hudhuria kadhia hii, nini kinatokezea ukihudhuria unafahamu zako kikamilifu.
(3)Ngazi ya Tatu: Inatokezea (Transformation)mabadiliko makubwa, yakiambatana na maajabu makubwa, unakua (New Man) kama kweli utaipanda Ngazi hii kwa fahamu zako ukadhihiri ukweli wa (Mauti)inakujia Fahamu, kumbuka Fahamu inatokea ndani sio kwa yule (maiti)unayemuona ila (Understanding) ya kujua kumbe kinachokufa ni kiwiliwili changu, Kinachopita katika haya Mauti ni kitu chengine kabisa ambacho hakiguswi na haya Mauti, Nini hichi ambacho baada ya Mauti yangu kinabakia?.
Jee Naweza kukijua nikiwa Hai, sio mpaka nisubiri mpaka siku yangu ya kufa, Jawabu ndio,بَلِ ٱلۡإِنسَـٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَة.
Anza safari ya kukutana na Nafsi na ukikutana nayo inakupeleka katika safari ya maajabu, inakutoa katika dhiki ya Dunia na kukupeleka kwenye Raha na maajabu ya Ulimwengu huu ambayo ulikua huyajui, Na ukiingia katika Ulimwengu wa Fahamu hii ya kuijua Nafsi yako unabadilika na kuwa Mtu mwengine kabisa, unatoweka katika maisha ya kawaida na hapo tena unaanza safari ya Ulimwengu wa kushangaza nini unakutana nacho katika maajabu hayo, katika ngazi hii kila kitu unakiona kwa njia nyengine kabisa, kila jambo linajifungua tafsiri yake na kuweka wazi siri zake.
Unapokutana na Nafsi yako kitu cha mwanzo unacho gundua ni kuona kumbe huu Mwili wangu (Body) ni (Inteligence)tupu inafanya kazi bila ya mimi kuingilia, ni miujiza baada ya miujiza inatumika, una elewa kumbe mimi nimeubeba tu mwili huu, lakini unafanya kazi zake bila ya kunihitaji mimi, unasaga chakula, unasafisha damu, unajiponesha wenyewe, na unafanya kazi zake nyingi pasi mimi kuingilia, kuanzia kidole gumba mpaka utosini muujiza huu unajitosheleza wenyewe.
Hapo tena unagundua kumbe mimi nimebeba kiwanda kizima natembea nacho, Nani huyu Mwenye kujua, nani huyu mwenye kusikia,Nani huyu Mwenye kuhisi, Nani huyu anoshuhudia haya yote, Na baada ya kushuhudia mwisho anakwenda wapi huyu Shahidi?, hapo sasa ukimaliza utaanza kuangaza Nje uone nako kuna nini?,(Hakika Nafsi ni Yenye kuona) Ukiweza kuona basi na kutizama inakua Rahisi, kumbuka kuona ni (Within)Ndani, Na kutizama ni (Outer)Nje hapo utaanza kuona mengine ya mfano kama wako na mengine zaidi, Nini hayo?
Endelea Part 3
NGAZI SABA ZA ROHO PART 3 (NGAZI 3)
Asalaam Aleiykum,
Hapo tena utaanza kumuona Ndege kwa njia Nyengine, utajiuliza vipi anabeba Mwili wake na kupaa angani, kitu gani kinacho mfanya apae na kubakia Angani, Nini kile kilichobeba Mwili ule hapo tena ukizidi kuchambua na kutaka kuyajua, unakutana na maajabu juu ya maajabu na nitayataja machache sura ya Hajj aya ya 18."أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ يَسۡجُدُ لَهُ ۥ مَن فِى ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَمَن فِى ٱلۡأَرۡضِ وَٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ وَٱلنُّجُومُ وَٱلۡجِبَالُ وَٱلشَّجَرُ وَٱلدَّوَآبُّ وَڪَثِيرٌ۬ مِّنَ ٱلنَّاسِۖ
(Mpaka mwisho wa aya)
(Uko katika kuona)"Jee Huoni kwamba Mwenye Enzi Mungu kinamsujudia kila kilichomo Mbinguni na kilichomo Ardhini, Na Jua na Mwezi na Nyota na Milima na Miti na Wanyama na Wengi Miongoni mwa Watu".
Hapo yamesemwa maneno makubwa yanatakiwa kuzingatiwa ili yakubadilishe muono wako, ikiwa vyote vilotajwa hapo vina Sujjudu ina maana lazima katika vitu hivyo ipo (Consciousness) (Awareness)ya kumjua Mollah wake, vyote vinafanya kitendo cha (Surrender)kwa Mollah wao, vyote vimeumbwa na vinaleta heshima kwa kumjua Mollah wao, kwa ajili hiyo basi lazima vitu hivi vitakua na (Sense) ya kuhisi kama ulivo mfano wa Mti wenye kufata maji chini kwa chini hata mita mia mbili, Na milima na sauti zake za mzungumzo ya kimya kimya, na Wanyama na tabia zao zilopangika za kupumzika wanapokwisha kula, vipi wanasujjudu? lazima kwanza tujiulize nini Sujjudu(Sijda) Ni (Surrender)kujisalimisha kikamilifu, kwa heshima na kuridhia na kufahamu kuwa kila kiumbe kimeumbwa na katika kuifanya hiyo (Sijda)ni kutekeleza Utiifu wako kwa Muumba, unakwenda kwa heshima zote kuwa umefata Amri za Mollah wako, umeacha kila kitu, unakwenda ukiwa msafi na sasa unaanguka kurudi kwa Mollah wako kwa Unyenyekevu ukiwa umekubali huna tena pengine pakwenda isipokua kurejea kwa Muumba wako ukiridhi apitishe hukumu yake, (Complete)huna cha kutenda zaidi ya kushukuru kwa hisani ya kuumbwa.
Sio hizi Sijda unakwenda ushadhulumu, umekwiba, umezini umepinga amri zote za Mollah halafu unakwenda kusujjudu? hizo hazifai kabisa, kwanza acha ulonayo halafu tena ndio nenda ukaipate sijida, utaikuta sijida yako tafauti, utajikuta machozi yanakumiminika bure ndani ya sijjida, na hiyo ndio maana ya vyote vinamsujudia, vyote vimekiri, vyote havendi kinyume na Mollah wao, hulikuti Jua kuutangulia mwezi wala mwezi kutangulia Jua, vyote vina tii, Na ndio ukichunguza sana utaona Milima, Nyota , wanyama Binaadamu vyote tushajua vinakufa vilobaki viwili ambavyo pia vinatarajiwa kufa navyo ni Jua na Mwezi sasa ikiwa umepata habari hii chache ya ngazi ya Maajabu endelea kutafuta mwenyewe mengine yalosalia ambayo hayeshi katika Ulimwengu huu. Inshaallah tumepita katika ngazi hii ya maajabu, Wiki ijayo tutaingia ngazi ya Nne yenye Miujiza.
Hapo tena utaanza kumuona Ndege kwa njia Nyengine, utajiuliza vipi anabeba Mwili wake na kupaa angani, kitu gani kinacho mfanya apae na kubakia Angani, Nini kile kilichobeba Mwili ule hapo tena ukizidi kuchambua na kutaka kuyajua, unakutana na maajabu juu ya maajabu na nitayataja machache sura ya Hajj aya ya 18."أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ يَسۡجُدُ لَهُ ۥ مَن فِى ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَمَن فِى ٱلۡأَرۡضِ وَٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ وَٱلنُّجُومُ وَٱلۡجِبَالُ وَٱلشَّجَرُ وَٱلدَّوَآبُّ وَڪَثِيرٌ۬ مِّنَ ٱلنَّاسِۖ
(Mpaka mwisho wa aya)
(Uko katika kuona)"Jee Huoni kwamba Mwenye Enzi Mungu kinamsujudia kila kilichomo Mbinguni na kilichomo Ardhini, Na Jua na Mwezi na Nyota na Milima na Miti na Wanyama na Wengi Miongoni mwa Watu".
Hapo yamesemwa maneno makubwa yanatakiwa kuzingatiwa ili yakubadilishe muono wako, ikiwa vyote vilotajwa hapo vina Sujjudu ina maana lazima katika vitu hivyo ipo (Consciousness) (Awareness)ya kumjua Mollah wake, vyote vinafanya kitendo cha (Surrender)kwa Mollah wao, vyote vimeumbwa na vinaleta heshima kwa kumjua Mollah wao, kwa ajili hiyo basi lazima vitu hivi vitakua na (Sense) ya kuhisi kama ulivo mfano wa Mti wenye kufata maji chini kwa chini hata mita mia mbili, Na milima na sauti zake za mzungumzo ya kimya kimya, na Wanyama na tabia zao zilopangika za kupumzika wanapokwisha kula, vipi wanasujjudu? lazima kwanza tujiulize nini Sujjudu(Sijda) Ni (Surrender)kujisalimisha kikamilifu, kwa heshima na kuridhia na kufahamu kuwa kila kiumbe kimeumbwa na katika kuifanya hiyo (Sijda)ni kutekeleza Utiifu wako kwa Muumba, unakwenda kwa heshima zote kuwa umefata Amri za Mollah wako, umeacha kila kitu, unakwenda ukiwa msafi na sasa unaanguka kurudi kwa Mollah wako kwa Unyenyekevu ukiwa umekubali huna tena pengine pakwenda isipokua kurejea kwa Muumba wako ukiridhi apitishe hukumu yake, (Complete)huna cha kutenda zaidi ya kushukuru kwa hisani ya kuumbwa.
Sio hizi Sijda unakwenda ushadhulumu, umekwiba, umezini umepinga amri zote za Mollah halafu unakwenda kusujjudu? hizo hazifai kabisa, kwanza acha ulonayo halafu tena ndio nenda ukaipate sijida, utaikuta sijida yako tafauti, utajikuta machozi yanakumiminika bure ndani ya sijjida, na hiyo ndio maana ya vyote vinamsujudia, vyote vimekiri, vyote havendi kinyume na Mollah wao, hulikuti Jua kuutangulia mwezi wala mwezi kutangulia Jua, vyote vina tii, Na ndio ukichunguza sana utaona Milima, Nyota , wanyama Binaadamu vyote tushajua vinakufa vilobaki viwili ambavyo pia vinatarajiwa kufa navyo ni Jua na Mwezi sasa ikiwa umepata habari hii chache ya ngazi ya Maajabu endelea kutafuta mwenyewe mengine yalosalia ambayo hayeshi katika Ulimwengu huu. Inshaallah tumepita katika ngazi hii ya maajabu, Wiki ijayo tutaingia ngazi ya Nne yenye Miujiza.
Sunday, March 2, 2014
NGAZI SABA ZA ROHO PART 1 (NGAZI 2)
Asalaam Aleiykum,
Tunaendelea na upandaji wetu wa ngazi ya Kiroho tukiwa sasa tunaikurubia ngazi ya Pili ili tujue nako kuna hazina gani, tupate kufahamu nini kipo katika ngazi hii, tumeona vipi katika ngazi ya kwanza Mja anavolimbikiza Mali, Vipi anavo jisahau katika kutafuta chumo au pato la kumstarehesha hapa Ulimwenguni, tumetambua vipi vitu hivyo vinavyoziba masikio na macho yetu tukawa hatuna habari kabisa kama ipo ngazi nyengine nayo hii ya pili ambayo Mja anatakiwa aipande.
(2)Ngazi ya Pili, Katika ngazi hii kuna jambo unajulishwa kama vile ulivyojulishwa wakati wa kuvunja ungo au kubaleghe, sasa unajulishwa hili jengine, zinakujia Fahamu katika ngazi hii kwa mara ya mwanzo kabisa unakutana uso na macho na Kifo(Death) hilo ni tukio kubwa la pili kukujia katika maisha haya unayoishi katika Ulimwengu huu. Umepewa fahamu ya kwanza, sasa unapewa fahamu ya pili, mwanzo ulioneshwa maisha na sasa unaoneshwa mauti, unakutana nayo uso kwa macho, kama mwanzo ulivogundua (Sex)na sasa unagundua (Death).
Kwa bahati mbaya ufunuo huu wengi ukiwafikia wanajaribu kuukwepa, wanajitahidi kujibabaisha, wengine wanapuuza kabisa hawataki mawazo haya, Na unakuja ufunuo au fahamu hizi katika kipindi cha miaka 40, lakini wengi unawafikia kwa ukweli wa dhati katika kipindi cha miaka 49. Hapo tena utaona Mtu kidogo anaanza kubadilika anapiga (Break) analeta (Slow down) kwa wale walo bahatika, lakini wengine waloghafilika wanaendelea kulisakata(Rumba).
Ama kama ukikujia ufunuo huu na wewe uko (Aware)Umekukuta ukiwa ni kipenzi cha Mwenye enzi Mungu, hapo katika Ngazi hii unakutana na hii aya katika sura ya Fajr.
يَـٰٓأَيَّتُہَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَٮِٕنَّةُ
Ewe Nafs Ilotulia
ٱرۡجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً۬ مَّرۡضِيَّةً۬
Rejea kwa Mollah wako, hali yakuwa umeridhika, Na (Mollah)wako ameridhika na wewe.
Vipi kuridhika kwako?
Ukishapata Fahamu hizi za Umauti kinakujia kitu cha kukumbusha kuwa siku zote unahudhuria maziko lakini hakuna kitu kinachokugusa katika nafsi yako, unaona umekwenda tu, lakini hakuna chochote, mbona sitishiki, sasa nini hicho kinogusa nafsi yako katika ngazi hii ya pili?
endelea part 2
Tunaendelea na upandaji wetu wa ngazi ya Kiroho tukiwa sasa tunaikurubia ngazi ya Pili ili tujue nako kuna hazina gani, tupate kufahamu nini kipo katika ngazi hii, tumeona vipi katika ngazi ya kwanza Mja anavolimbikiza Mali, Vipi anavo jisahau katika kutafuta chumo au pato la kumstarehesha hapa Ulimwenguni, tumetambua vipi vitu hivyo vinavyoziba masikio na macho yetu tukawa hatuna habari kabisa kama ipo ngazi nyengine nayo hii ya pili ambayo Mja anatakiwa aipande.
(2)Ngazi ya Pili, Katika ngazi hii kuna jambo unajulishwa kama vile ulivyojulishwa wakati wa kuvunja ungo au kubaleghe, sasa unajulishwa hili jengine, zinakujia Fahamu katika ngazi hii kwa mara ya mwanzo kabisa unakutana uso na macho na Kifo(Death) hilo ni tukio kubwa la pili kukujia katika maisha haya unayoishi katika Ulimwengu huu. Umepewa fahamu ya kwanza, sasa unapewa fahamu ya pili, mwanzo ulioneshwa maisha na sasa unaoneshwa mauti, unakutana nayo uso kwa macho, kama mwanzo ulivogundua (Sex)na sasa unagundua (Death).
Kwa bahati mbaya ufunuo huu wengi ukiwafikia wanajaribu kuukwepa, wanajitahidi kujibabaisha, wengine wanapuuza kabisa hawataki mawazo haya, Na unakuja ufunuo au fahamu hizi katika kipindi cha miaka 40, lakini wengi unawafikia kwa ukweli wa dhati katika kipindi cha miaka 49. Hapo tena utaona Mtu kidogo anaanza kubadilika anapiga (Break) analeta (Slow down) kwa wale walo bahatika, lakini wengine waloghafilika wanaendelea kulisakata(Rumba).
Ama kama ukikujia ufunuo huu na wewe uko (Aware)Umekukuta ukiwa ni kipenzi cha Mwenye enzi Mungu, hapo katika Ngazi hii unakutana na hii aya katika sura ya Fajr.
يَـٰٓأَيَّتُہَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَٮِٕنَّةُ
Ewe Nafs Ilotulia
ٱرۡجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً۬ مَّرۡضِيَّةً۬
Rejea kwa Mollah wako, hali yakuwa umeridhika, Na (Mollah)wako ameridhika na wewe.
Vipi kuridhika kwako?
Ukishapata Fahamu hizi za Umauti kinakujia kitu cha kukumbusha kuwa siku zote unahudhuria maziko lakini hakuna kitu kinachokugusa katika nafsi yako, unaona umekwenda tu, lakini hakuna chochote, mbona sitishiki, sasa nini hicho kinogusa nafsi yako katika ngazi hii ya pili?
endelea part 2
NGAZI SABA ZA ROHO PART 2 (NGAZI 2)
Asalaam Aleiykum,
Unakwenda mazikoni unaona ni kumfukia mwenzio, ndio maana unafanya maskhara makaburini, sababu huna hisia, maziko hayakukumbushi chochote , lakini ukipata fahamu za mauti, sasa kifo kinakua kweli juu yako, Unakutana na kile kitu kinacho chukua kila kitu ulokua nacho, Mali, Mke,Mume,watoto,marafiki, kila kitu ulichoita chako kwenye Ulimwengu huu kinatoweka, Na kuchukuliwa na kifo.
Unapata kufahamu katika ngazi hii kuwa wakati wowote zamu yangu itafika, wako wapi wazee wangu, wako wapi marafiki zangu,wangapi wameshatangulia, wengi nilokua nao washatangulia chini ya Ardhi, kifo kinamchukua kila mtu, hapo tena kama Mja Mwema ulojifunga na Mollah wako unashukuru Mungu kwa yote ulofanya katika Ulimwengu huu yaliyo mema, Na yale Mabaya unajifunga kuanza kuomba msamaha(Toba).
Hapo zinakujia fikira kuwa Mollah wako kakupa nafasi na kukumbusha kadhia hii ya Mauti, unaanza kuona kadhia yote ya Vyeo, kutafuta mali, kushiriki anasa yashapitwa na wakati, linakujia wazo kuwa huna haja tena ya kutafuta (Viagra) na hivi na vile, unakumbuka kuwa Mollah wako mwanzo ndio alokupa nguvu hizo na sasa amezichukua lazima kuna mpango wake alonipangia nguvu hizo sasa zitumike vipi, Na mimi nimeridhika nafata amri zake, Nakubali wakati wowote namie Mauti yatanihudhuria, Na kwa jambo hilo mimi sina mamlaka nalo.
Kwa hiyo kuanzia hivi sasa nimeridhika na Namuachia Mollah ndio awe Muamuzi wa mambo yangu yote, kama kikija cheo au ukubwa fulani sawa, Nikipata mali sawa, nikikosa sawa, sasa nimeshagundua Mauti na kazi yake na hakuna kinacho ni shughulisha isipokua Mollah wangu. Na mimi kwa hilo nimeridhika sasa najiunga na watu wema kusubiri fadhila za Mollah wangu.
Endelea part 3
Unakwenda mazikoni unaona ni kumfukia mwenzio, ndio maana unafanya maskhara makaburini, sababu huna hisia, maziko hayakukumbushi chochote , lakini ukipata fahamu za mauti, sasa kifo kinakua kweli juu yako, Unakutana na kile kitu kinacho chukua kila kitu ulokua nacho, Mali, Mke,Mume,watoto,marafiki, kila kitu ulichoita chako kwenye Ulimwengu huu kinatoweka, Na kuchukuliwa na kifo.
Unapata kufahamu katika ngazi hii kuwa wakati wowote zamu yangu itafika, wako wapi wazee wangu, wako wapi marafiki zangu,wangapi wameshatangulia, wengi nilokua nao washatangulia chini ya Ardhi, kifo kinamchukua kila mtu, hapo tena kama Mja Mwema ulojifunga na Mollah wako unashukuru Mungu kwa yote ulofanya katika Ulimwengu huu yaliyo mema, Na yale Mabaya unajifunga kuanza kuomba msamaha(Toba).
Hapo zinakujia fikira kuwa Mollah wako kakupa nafasi na kukumbusha kadhia hii ya Mauti, unaanza kuona kadhia yote ya Vyeo, kutafuta mali, kushiriki anasa yashapitwa na wakati, linakujia wazo kuwa huna haja tena ya kutafuta (Viagra) na hivi na vile, unakumbuka kuwa Mollah wako mwanzo ndio alokupa nguvu hizo na sasa amezichukua lazima kuna mpango wake alonipangia nguvu hizo sasa zitumike vipi, Na mimi nimeridhika nafata amri zake, Nakubali wakati wowote namie Mauti yatanihudhuria, Na kwa jambo hilo mimi sina mamlaka nalo.
Kwa hiyo kuanzia hivi sasa nimeridhika na Namuachia Mollah ndio awe Muamuzi wa mambo yangu yote, kama kikija cheo au ukubwa fulani sawa, Nikipata mali sawa, nikikosa sawa, sasa nimeshagundua Mauti na kazi yake na hakuna kinacho ni shughulisha isipokua Mollah wangu. Na mimi kwa hilo nimeridhika sasa najiunga na watu wema kusubiri fadhila za Mollah wangu.
Endelea part 3
NGAZI SABA ZA ROHO PART 3(NGAZI 2)
Asalaam Aleiykum,
Mwenye Roho ilotulia hababaiki tena na Ulimwengu, hao ndio walopata ufunuo na kuweza kupanda ngazi hii ya pili bila ya matatizo, kuna wengine wao wamepuuza ufahamu huu, Umewajia lakini hawakuutaka, wanaona vifo vinatokea kwa watu wengine, kwa hiyo wacha tuendelee kuyachapa maisha, wanasahau kabisa kuipanda ngazi hii ya pili, hawakumbuki ya mwanzo sikwambii ya pili, Sasa kama ndani husikilizi Wanaadamu wanaanza kukuhimiza "wewe nenda Makaburini"kwani kifo ni mawaidha makubwa, nenda mazikoni kuna faida utaipata.
Sasa Waja wawili nyie, yule wa mwanzo na huyu wa pili wakipanda ngazi wanakutana pia na Milango miwili, mlango wa kwanza anapita huyu alosukumwa na akapanda kwa nguvu, alokua hasikilizi anayoambiwa , yeye kajaa mashaka matupu, anajiuliza hivyo "وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَٮِٕذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابً۬ا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ "
"Na walikua wakisema tutakapo kufa, na tukawa udongo na mifupa ndio (Kweli)tutafufuliwa.
Hivi ndio ilivyo watu wengi wakenda mazikoni hakuna chochote kinachotokezea, hakuna ukumbusho, watu wanabadilishana namba za simu na kuzungumza habari za zamani, ndio daima unabakia sijui marungu yapo, vipi wakikujia hao viumbe wa ajabu Malaika wanakuja na (Daftari langu) kila kitu unakitilia wasi wasi, Ukijiona upo katika hali hiyo basi jua wewe katika wale ambao somo la mauti ulikua ukilipuuza, huzitaki fahamu hizo zikikujia.
Ama kwa wale walokua wakisikiliza na kulisikia somo hili, wakawa hawalipuuzi, wao wanakwenda (Deep) wao wanajua moja kwa moja mlango wao umeandikwa "لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلۡمَوۡتَ إِلَّا ٱلۡمَوۡتَةَ ٱلۡأُولَىٰۖ"(Dukhan 56 mpaka mwisho wa aya)"Hawatayaonja Mauti ila(isipokua)mauti ya kwanza".
Moja kwa moja katika Ghorofa hii wanafungua mlango na wanakutana na mambo ya Ajabu, Wanakwenda (Beyond Death)wanakikuta kitu chengine kipya ambacho tutakuja kukijua tutakapo panda ngazi ya tatu wiki ijayo kwa kadir ya uwezo wa Mollah wetu tukiwa hai, tuone vipi Mauti yanavokuonesha mambo kiajabu.
Mwenye Roho ilotulia hababaiki tena na Ulimwengu, hao ndio walopata ufunuo na kuweza kupanda ngazi hii ya pili bila ya matatizo, kuna wengine wao wamepuuza ufahamu huu, Umewajia lakini hawakuutaka, wanaona vifo vinatokea kwa watu wengine, kwa hiyo wacha tuendelee kuyachapa maisha, wanasahau kabisa kuipanda ngazi hii ya pili, hawakumbuki ya mwanzo sikwambii ya pili, Sasa kama ndani husikilizi Wanaadamu wanaanza kukuhimiza "wewe nenda Makaburini"kwani kifo ni mawaidha makubwa, nenda mazikoni kuna faida utaipata.
Sasa Waja wawili nyie, yule wa mwanzo na huyu wa pili wakipanda ngazi wanakutana pia na Milango miwili, mlango wa kwanza anapita huyu alosukumwa na akapanda kwa nguvu, alokua hasikilizi anayoambiwa , yeye kajaa mashaka matupu, anajiuliza hivyo "وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَٮِٕذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابً۬ا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ "
"Na walikua wakisema tutakapo kufa, na tukawa udongo na mifupa ndio (Kweli)tutafufuliwa.
Hivi ndio ilivyo watu wengi wakenda mazikoni hakuna chochote kinachotokezea, hakuna ukumbusho, watu wanabadilishana namba za simu na kuzungumza habari za zamani, ndio daima unabakia sijui marungu yapo, vipi wakikujia hao viumbe wa ajabu Malaika wanakuja na (Daftari langu) kila kitu unakitilia wasi wasi, Ukijiona upo katika hali hiyo basi jua wewe katika wale ambao somo la mauti ulikua ukilipuuza, huzitaki fahamu hizo zikikujia.
Ama kwa wale walokua wakisikiliza na kulisikia somo hili, wakawa hawalipuuzi, wao wanakwenda (Deep) wao wanajua moja kwa moja mlango wao umeandikwa "لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلۡمَوۡتَ إِلَّا ٱلۡمَوۡتَةَ ٱلۡأُولَىٰۖ"(Dukhan 56 mpaka mwisho wa aya)"Hawatayaonja Mauti ila(isipokua)mauti ya kwanza".
Moja kwa moja katika Ghorofa hii wanafungua mlango na wanakutana na mambo ya Ajabu, Wanakwenda (Beyond Death)wanakikuta kitu chengine kipya ambacho tutakuja kukijua tutakapo panda ngazi ya tatu wiki ijayo kwa kadir ya uwezo wa Mollah wetu tukiwa hai, tuone vipi Mauti yanavokuonesha mambo kiajabu.
Subscribe to:
Posts (Atom)