Asalaam Aleiykum
Ingekua si (Sex) ningekwenda peponi, huwezi kwenda, na wala si rahisi kuwa Mcha Mungu kwa sababu zako za (Investment) za mambo mengi, na Ucha Mungu unatakiwa (Invest) ya kitu kimoja tu nacho ni kwa ajili ya Mollah wako, lakini wapi wewe ume (Invest) kwenye Biashara, Umetia hisa kwenye Siasa, Una (share) kwenye magonvi, kwenye husda, kwenye kusema watu, kwenye vikao vya mpira, na mabaraza ya karata na pombe, Na sasa umebakia kula faida ya Riba, kwa ajili ya Hisa zako zilivyozidi kwenye dunia ya ufisadi, jiangalie sana utayajua hayo hayafichiki, sasa vipi leo utaupata Ucha Mungu.
Ucha Mungu haupatikani kirahisi kwa njia ya mdomo na maonesho, Ucha Mungu lazima ujitolee hata kufa ili uupate Ucha Mungu, Utajiuliza Ufe vipi? Unatakiwa ufe (Painful Death) inakuaje hii (Painful Death) hapa ndio mwanzo wa Darsa yetu ya leo.
Itabidi tumsikilize kwa kituo msemezwa na Mwenye enzi Mungu Nabii Musa a.s anasemaje kuhusiana na kadhia hii ya Ucha Mungu, kwa kuwa kajua nyinyi mmekwisha (Invest) sana kwenye Ulimwengu huu, ili mpate kuupata huo Ucha Mungu Mjumbe wa Mwenye enzi Mungu anasema maneno haya:Quraan sura ya Saff aya ya 10 na 11.
"يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ هَلۡ أَدُلُّكُمۡ عَلَىٰ تِجَـٰرَةٍ۬ تُنجِيكُم مِّنۡ عَذَابٍ أَلِيمٍ۬ "
Enyi Mlioamini je Nikujulisheni biashara itakayokuokoeni na adhabu iumizayo.
"تُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَتُجَـٰهِدُونَ فِى سَبِيلِ ٱللَّهِ بِأَمۡوَٲلِكُمۡ وَأَنفُسِكُمۡۚ ذَٲلِكُمۡ خَيۡرٌ۬ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ "
(Basi)Muaminini Mwenye enzi Mungu na Mtume wake, na piganieni dini ya Mwenye enzi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu, haya ni bora kwenu ikiwa mnajua.
Inashangaza hapa maneno yameanzia kwa waloamini, utajiuliza vipi waloamini watapata adhabu ya Mwenye enzi Mungu, kwa ajili ya kuyachambua maneno haya itabidi nikujulishe (Level) mbili za Imani. Ama (Level) ya kwanza ya Imani yako imekaa kwenye Akili (Mind) ambayo inakua umekubali, umeambiwa au umesikia na wewe umekubali, hiyo ndio Imani yako, sasa Nabii Musa a.s alipokutaka uamini tena kakusudia uondoke kwenye (Level) ya kwanza na uende kwenye ya pili nayo ni Moyo (Falling in Love) si umejiona ukipenda unakuaje, uko tayari hata kufa kwa ajili ya mpenzi wako, uko tayari kufanya chochote ili mpenzi aridhike, na si unajijua hujali chochote kuyafanya hayo, sasa na huo Ucha Mungu unatakiwa uwe katika hali kama hiyo kwa ajili ya Mollah wako.
Na hilo anoweza kulifanya ni Mmoja tu naye ni (Mcha Mungu) mpenzi wa Mungu, na sisi Nabii Musa a.s katuona mapema kuwa wafanya Biashara, tushachuma Dhanmbi nyingi, hatuwezi kuwa wacha Mungu mpaka tujitolee (Muhanga) nayo ni hiyo (Painful Death)nayo ni Jihad, ndio neno la pili akatwambia nikujulisheni sasa Biashara, baada ya kuamini, na ukiamini tu uko tayari kwa lolote, ukiona unasita basi jijue Imani haijafika Moyoni, na kama imefika kweli jambo la mwanzo kupimwa kama kweli unautaka Ucha Mungu ni hiyo (Investment) ya Mali yako.
endelea part 3
No comments:
Post a Comment