Sunday, August 3, 2014

ELIMU YA DUNIA NA AKHERA PART 1

Asalaam Aleiykum

Limekuja swali Muulizaji kauliza anataka kujua kama iko tafauti ya Elimu ya Dunia na Elimu ya Akhera, Na Jawabu lake nimelijibu hivi, Naam tafauti ipo japokua Elimu ni hiyo hiyo moja,  tafauti yake Elimu ya Dunia (Ni Past Education)Na Elimu ya Akhera(Ni Future Education). Basi kwanza kabla ya kwenda huko mbali tuijue nini Elimu?.
Elimu ni nyenzo au mjumbe anokutoa kwenye kiza na kukupeleka kwenye Taa, Na kwa Maana hiyo lazima wewe uko pahala umekaa, na hapo pahali wewe yaonekana huwezi kutumia macho yako ukaona ndio lazima upelekwe kwa daktari wa macho akuangalie, akuoneshe hii A, hii B, na hii C. Lakini ungekua unaona basi huna haja ya kupelekwa kwa Daktari, na wako wachache wanatoka wenyewe kwenye kiza na kwenda kwenye Nuru.
Na hivi sasa Wanasayansi wametengeneza Miwani unaona ukiwa kizani bila ya matatizo, Na hiyo ndio sawa na Elimu wewe mwenyewe unaishi ndani ya hiyo Elimu, Kila kitu kimezungukwa na Elimu,  tafauti hii ya Dunia ni ya (Copy) au kama nilivyo ita mwanzoni ya (Past) au niseme (Dead education) kwanini nikaita imekufa sababu imeandikwa kwenye mabuku, mwalimu wako kasoma ikisha kakusomesha wewe, au mtu kapata mafundisho ikisha kakufundisha wewe, kila kitu unachosoma wenzio washasoma kabla yako, sio kipya kabisa fani yoyote ile wewe sio wa mwanzo, hiyo ndio Elimu ya Dunia ambayo mifano yake imetajwa Mpaka kwenye Quraan, kama zilivotajwa kwenye sura ya Rahman kuhusiana na Bahari mbili zisizoingiliana na mengi mengineyo ya Elimu za Kidunia.
Halafu kuna Elimu ya Akhera , hii ni Elimu ya (Future) ijayo, hii haisomwi, ina njia moja tu nayo kuijua, lakini huko kujua unatakiwa uwe na jitihada kubwa kwa sababu kujua sio sawa na kusoma. Kusoma utakwenda kwa Mwalimu, utakwenda kwa Sheikh, wote watakusomesha, lakini kujua lazima ukae na anaejua upate kuona kajua vipi ili apate kukufundisha na wewe mbinu za kujua, lazima uwe karibu akupe ujuzi wa kuona gizani, mabuku hapo hayafai, haitakiwi (Tuition)hapo, sasa huyu unokaa nae kwani yeye ana nini?.
Yeye anakua kapata kitu cha kumuwezesha kuona pande zote mbili za Elimu ya Dunia na ile ya Akhera, kumbuka nyote mnaona lakini tafauti yake ni ya (Level) Ya muono wenyewe, kenda zaidi ya kuona na kabahatika kwenda (Beyond Education) Na ukenda (Beyond Education) unakua hujenda kokote ila umerejea kwenye hiyo (Source)ya (Education) Ambayo ndio hiyo (Inteligence).
Nini (Inteligince)? Ukiniuliza mimi nitakwambia (Inteligence) ni Rehma, Na Rehma hii ya (Inteligence)kila Mtu kabarikiwa kuwa nayo, isipokua ina (Level) mbili, ya kwanza inakua wazi haina kipingamizi chochote, kama ilivokuja ndivo inavotumika, Na ya pili inapata kizingiti cha Elimu yako ya Dunia una (Block Inteligence) haifanyi kazi tena kama ilivo sasa mpaka hesabu unafanyiwa na (Computer) huwezi hata kufanya hesabu ya kujumuisha.
Kwa hiyo utaona Baina ya hiyo (Inteligence) kuna hizo tafauti mbili za Elimu ya Dunia na ya Akhera, (Inteligence) ndio inokusaidia uzipate elimu mbili hizo. Na hiyo (Inteligence) yenyewe haina (Past) au (Future) ni huu wakati tulonao ndio wakati wa hiyo Rehma ya (Inteligence) ukirudi (School) utamiss na ukisubiri Akhera utakua umechelewa, unatakiwa Elimu hizo zote mbili uzipate sasa hivi ndio ziwe na manufaa na wewe,yepi ? hii ya dunia ikupatie mkate wako wa kila siku hapa Ulimwenguni, na hiyo ya Akhera ikakupatiea hayo uliyopewa ahadi kuwa utayapata. Na hapo ndio wacha nikuchukue kwenye safari ilojaa hiyo (Inteligence) au Rehma au Tuite Hekima ilotokeya kwa hao walokwenda na wewe utofatia kwenda katika safari yako yoyote ulokusudia.
Endelea part 2

No comments:

Post a Comment