بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
Asalaam-aleikum
الَّذِينَ يَذْكُرُونَ اللَّهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمْ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ رَبَّنَا مَا خَلَقْتَ هَٰذَا بَاطِلًا سُبْحَانَكَ فَقِنَا عَذَابَ النَّارِ
(Ambao wanamkumbuka Mollah wao wakiwa wamesimama,wamekaa, na wakiwa wamelala, na wakafikiri katika kuumbwa mbingu na ardhi;wakasema Mollah wetu hukuviumba hivi bure,basi subhannaka tuepushe na adhabu ya moto).
Watu hawa ni wepi?, Jee na wewe umo katika watu hawa? (Laaillah-Illah-ALLAH).
Shahada ni jambo la kuendelea katika umri wako wote, sio jambo la mchezo ikawa umeona ikisha basi, laa ndio maana unatakiwa mpaka siku ya kufa kwako uwe unarudi kwa Mollah wako na neno hili(lakini muradi wake)ni kuthibitisha,kukubali (surrender) umekua muislam kamili (laaillah-illah-allah) ndio maana ikasisitizwa neno hili likuingie kwenye fahamu zako na haliwezi kukuingia ndio maana ukapewa (nyenzo) ikiwa unaweza kutumia njia ya moja kwa moja basi wewe umefaulu, lakini kwa kuwa njia ya moja kwa moja ni ngumu, ndio maana umepewa (kalimat-tawhid)I weze kukumbusha, na kama unapinga jaribu japo kwa masaa(12) kutamka neno hili kama utaweza, na ikiwa huwezi ndio maana ikawa njia ya shahada moja kwa moja ni vigumu.
Naam sasa watu gani hawa wenye kumkumbuka Mollah wao, hao ni watu ambao wamepata hekima kutoka kwa Mollah wao, vipi wamepata hekima hiyo, kwa ajili ya kukumbuka kwao wamepindukia kutoka kwenye akili wameingia kwenye hekima, utaona aya ya mwanzo imewataja wenye akili, na hii ya pili imetaja wenye kufikiri, kwanini kwa sababu ukidumu na (laaillah-illah-allah) mawazo yanapotea na hapo inazaliwa fikira(hekima)na hiyo huipati ila kutokea kwa Mollah wako.
Mja anapofunguliwa hekima huanza kuiona dunia hii kwa mtizamo mpya kabisa lakini lazima lipatikane lile shuruti lake la (kumkumbuka Mollah)wako, ukiwa umesimama yaani kusudio lake katika matendo uyafanyayo, kama vile upo kazini au unatembea nk, au ukiwa umekaa pengine unacheza karata, au upo msikitini barazani watu wanazungumza siasa wewe unamkumbuka Mollah wako, au umelala umejinyoosha basi umo katika hali ya kumkumbuka Mollah wako, basi ujue hata ukikushika usingizi ndotoni utakua unamkumbuka Mollah wako, ndoto za kipuuzi zote zitaanza kupotea, hapo inajumuisha matendo yote utayofanya ukiwa katika hali hizo, uwe unamkumbuka Mollah wako, ukiwa umejizatiti sawa sawa basi jaribu kwa muda wa siku saba(24-7)kulizoea neno hili utaanza kuliona faida yake.fanya majaribio, utaona faida yake.
Hiyo ndio shahada tunayotakiwa waislamu tuwe nayo katika vifua vyetu, na wakati wa kutoka roho zetu. (pale inaposomwa ile aya inayosema) "nasisi tupo karibu nae zaidi-lakini hamtuoni" (84-85-surat-al-waaqiah) huku wewe unajibu (laaillah-illah-allah) mimi nimeshuhudia katika uhai wangu na sasa nashuhudia kurejea kwa Mollah wangu.
Katika maudhui ilopita niliitaja hadithi ya Sayyidna Bilal (r.a) alipokua anakaa na udhu, hiyo ni njia moja na nyengine ni hii ya kulikumbuka neno hili la (tawhid)linakupeleka kumkumbuka Mollah wako, tafauti yake hili la pili linakupeleka zaidi, unaipata shahada.(laaillah-illah-allah) kama nilivo eleza, huo ni upande wa kwanza wa shahada, ama upande wa pili Muhammad Rassullallah huo unafatia katika
(maana ya shahada part 3 na 4)
Mollah wangu anajua zaidi
Abdallah Baja
جزاك الله خيرا
ReplyDeleteجزاك الله خيرا
ReplyDelete