Saturday, July 27, 2013

WAJUE WALOFUNGA MWAKA HUU PART 4

Asalaam Aleiykum,
Ikiwa umo kwenye Swaum na umeipata kweli kweli basi moyo wako lazima uwe maridhia kwa hukumu na amri zote za Mwenye enzi Mungu, aliyefunga mwezi huu anajishughulisha sana na kusoma Quraan, Sasa wacha tukugeukie wewe tukutizame na hiyo Swaum yako, umefanya mangapi katika hayo, jee umewahi kuipata hata saa moja katika mwezi huu kuitumia kwa ajili ya kumfikiri Mollah wako na alivyoviumba, umeufanya mwezi huu ni kwa ajili ya kutafuta mapenzi ya Mollah wako, kumbuka yeye ndie aliyekuumba na hivi karibuni utakwenda kukutana nae, basi ikiwa hujafanya hivyo basi kumbuka umebakisha siku kumi za mwisho, acha kila kitu upate kuwahi ili na wewe uwemo katika walofunga, mkimbie mwenye kukuita kwenye karata, sasa ni kipindi cha kuacha kutuma msg kwenye wassup.acha katika kumi hili kusikiliza muziki na kutizama Tv, utumie muda huu kumkumbuka Mollah wako kwa wingi, ipate Itikaf uisikilize salamu zinazokuja kwenye moyo wako, punguza kuuza na kununua ili uzijue kheri za Ramadhan, kakae uzidishe ibada asaa yaweza kuwa mwaka wako wakuipata Lailatul Qadir, tegemea aya  ya 35 Fussilat inavosema

" وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ذُو حَظٍّ عَظِيمٍ۬ "
Lakini (Jambo hili)hawatapewa ila wanosubiri, (Na)wala hawatopewa ila wenye Bahati kubwa(hadhi mbele ya Mollah wao)
hii inaweza kuwa usiku wako, hakikisha haukupiti hata mmoja katika hayo masiku kumi, Mkumbuke Mollah wako usiku akukumbuke mchana, mkumbuke kwenye furaha atakukumbuka kwenye shida, mkumbuke kwenye Swaum ili akuingize kwenye Pepo ya Al-Rayyan, Zidisha Ibada zako daima uwe Furahani. Mollah zipokee Ibada zetu, utusamehe Dhanmbi zetu, turidhie matendo yetu yawe kwako yenye kukuridhisha. Tunakuomba Neema na kheri zako zitushukie katika mwezi huu.Amin.


No comments:

Post a Comment