Saturday, July 27, 2013

WAJUE WALOFUNGA MWAKA HUU PART 2

Asalaam Aleiykum,

Hali ya mwanzo jaalia hivi umepinda kichochoro, ukakutana na mti mzuri, angalia nini kinatokea ndani ya mwili wako(Nothing happen)katika hisia zako, halafu nenda mbele zaidi ukutane na mwanamke au mwanamme mzuri, sasa angalia tena hali gani unakua ndani ya kiwiliwili chako, Sasa kama utakua mwerevu basi ushazigundua (Switch)mbili basi itumie (switch)iloona mti, kwani hii inapatikana kirahisi mwezi huu wa Ramadhan, ndio maana ukaambiwa (kufunga)kunakata matamanio, itumie (switch) hii mwezi huu na miezi mengine ukiwacha kuangalia matamanio utawasha (Switch) ya Taqwa, ambayo ndio inayotakiwa katika mwezi huu ili upate kufanya shughuli za Taqwa kwa utulivu, inawezekana pia kutumika (Switch) hiyo  katika kusikia, kwani tayari unaitumia lakini hujui matumizi yake kwa njia ya ufundi muda huu. Sasa wacha nikufahamishe vipi inakua (Switch) ya kusikia na kazi zake, tuseme una sikiliza Quraan, unasikia jogoo linawika, gari inapita, ndege wanaimba, lakini yote hayo yanapita sikio hili na kutokea upande wa pili, na masikio yako yamelenga kwenye Quraan pekee unaisikiliza na kuifahamu, na yale mengine umeyasikia lakini hayaja kushughulisha kabisa, na hivo ndivyo inavotakiwa katika mwezi huu uwe mwenye kusikiliza mambo mema, umo katika mwezi huu tumepita katika macho na masikio ili turejee katika Taqwa ya Ramadhan, na sisi tuwemo katika walofunga, usikate tamaa, bado unao wakati wa kuiwahi gari ya mwisho isije ikakuacha, irekebishe Swaum yako uwemo katika kundi la walofunga. Nani alofunga? alofunga wakati wote anajijua yeye yumo ndani ya Swaum, inakua hajajizuia na kula na kunywa tu, bali alofunga  kazuia kauli zake hapiti akitukana ovyo na kutoa maneno machafu, hendi kila pahala na kusengenya watu, ndani ya kifua chake marfuku katika mwezi huu mzima kutoa kauli nzito nzito za kujeruhi wenzie na kuwashtumu kwa jambo hili na lile, umo kutaka kumjua alofunga basi mtizame yule asonyanyua mkono na kumdhuru mwenzie, wala kuchukua kisicho halali yake, mwiko kwake kumdhulumu mtu, na Wala hanyanyui miguu yake kwenda kokote anako asiwa mpenzi  Mollah wake, aliyeipata Swaum hajishughulishi na kauli chafu, hatoi ukali wala kugombana, hafanyi mambo ya kipuuzi wakati huu wa Taqwa, hamkejeli mtu na kujiona yeye bora, daima hukumbuka mimi nimefunga, kila akiona maovu hukumbuka mimi nimefunga, akiona mambo ya kipuuzi anakumbuka mimi nimefunga.
Alopata Swaum anakua kafunga masikio, kafunga macho, kafunga ulimi, kafunga mikono, kafunga miguu baada ya hayo yote kuyakamilisha, sasa anafungua mlango wa Taqwa. Ukoje Mlango huo endelea Part 3

No comments:

Post a Comment