Tuesday, July 9, 2013

MALIPO YA TAQWA NI KUSAMEHEWA(QIYYAM LAYLA)PART 1

Asalaam Aleiykum,

Ingia katika Darsa yetu ya leo ili nipate kukujulisha kitu muhimu ambacho kama utakianza leo au kesho kwenye (Yaumu Shaka)basi chaweza kuwa muongozo wa kuupata msingi madhubuti wa hiyo(Taqwa)na ukapata nafasi ya kusamehewa (Dhanmbi)zako katika mwezi huu wa Ramadhan. Sina kipya ninachofundisha ila kukupa upeo mwengine wa kuweza kufahamu njia au mbinu nyengine za kuipata Taqwa.
Pata habari hii ya Ugunduzi wa zama za zamani ulofanywa na wana(Taaluma)wa Sayansi ya utesaji, wanasema hivi, kama utamuashia Taa Mwanaadamu akawa hapati usingizi kwa kipindi cha Mwezi au miezi miwili, basi ataanza kusema yote alotenda, aloyaona na kusikia, iwe  siri ya aina yoyote ama iwe Dhanmbi ilofichika miaka yote, basi atavizungumza vyote na kuvitoa ndani ya kifua chake, kwanza ataanza kimya kimya na siku zikizidi ataanza kutoa sauti kwa nguvu, Na hilo si jambo la kubisha kwani wewe mwenyewe unaweza kuwa kutwa nzima unasema peke yako kichwani mwako, pengine unarejea maneno hayo kwa hayo mara chungu nzima, hayo ndio maafa yanopatikana kwa mateso ya kunyimwa usingizi kwa lazima, na hiyo ni taa walowasha wanaadamu wenzio kwa kukulazimisha, Sasa hebu tupate habari kutoka kwa wanasayansi wa (Kidini)wao wanasemaje kuhusu jambo hili la kuwapo kwa taa, Katika Ulimwengu huu kila kitu kimeumbwa(In Pairs)Adh-Dhaariyat (49).

"وَمِن ڪُلِّ شَىۡءٍ خَلَقۡنَا زَوۡجَيۡنِ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ"
"Na katika kila kitu tumeumba dume na jike ili mpate kufahamu"
Wanasema Wanasayansi wa kidini (Mawalii na Wacha Mungu)Na sisi tumegundua hiyo Taa ya pili ambayo inawaka yenyewe ndani ya mwili wako ambayo sikama hii muanayo, hiyo ni (Nuru) na taa hii unaiwasha kwa hiyari yako mwenyewe kwa wingi wa Ibadah na Taqwa, "Kwani hamjasikia kuna kitu kinaitwa Nuru ya Moyo" Sasa nini ufanye mpaka uwashe hiyo (Nuru)?. Mwanzo tumeshaambiwa ukinyimwa usingizi siri na dhanmbi zote zinatoka nje, unatoa mwenyewe habari zote, nini kinafanyika inapowaka hii taa ya moyoni ambayo ni Nuru?.
Sababu tunaingia katika mwezi Mtukufu wa Ramadhan wacha tuchukue nafasi hii kupeana faida japo kwa uchache ili tupate kuifanya Taqwa kwa ajili ya Mollah wetu, ili na yeye kwa mapenzi yake apate kutusamehe Madhanmbi yetu.Wanasema (Mawalii na Wacha Mungu) kama wao wametumia Sayansi ya nje kuzipata siri zenu, sisi tunakupeni Sayansi ya ndani mpate kusamehewa Dhanmbi zenu. Nini Mfanye, Kasomeni maagizo ya Mollah wenu katika sura ya Muzzamil kuanzia aya ya "1 mpaka aya ya 8" itakutosheni kuiwasha hiyo Nuru. Mollah wenu anakuiteni kwa khiyari yenu mkae macho ili mfanye nini?
Anaambiwa Bwana Mtume s.a.w na sisi sote tunayo tabia hiyo,

"يَـٰٓأَيُّہَا ٱلۡمُزَّمِّلُ" "Ewe uliyejifunika maguo" nguo zinakupa joto joto, ushazizoea, bila ya kujifunika hupati usingizi, sasa unaambiwa ziondoshe, wakati ushafika kama una haja ya kuzungumza na Mollah wako, kama unataraji kuwa karibu na Mollah wako hususan katika mwezi huu wa Ramadhan na miezi mengine, itabidi ufanye jambo hili,"قُمِ ٱلَّيۡلَ إِلَّا قَلِيلاً۬" Simama usiku (Kucha ukifanya Ibada)ila muda kidogo" fanya jitihada ya kuiwasha hiyo (Nuru)kaa macho kwa ajili ya Mollah wako, Sali sana upate kufanikiwa uyapate mapenzi ya Mollah wako, na hayo mapenzi yakupate wewe,
 "Pia napenda uelewe  (Sharaf ya Muumin) ni (Qiyyam Layla) Utukufu wa Muumin ni kisimamo cha usiku," huna haja ya kulala masaa yote, futa madhanmbi yako kwa kuzungumza na Mollah wako sana, usije ukaiwacha nafasi hii ndani ya mwezi wa Ramadhan. Na kama huwezi ufanye nini?
Endelea Part 2.


No comments:

Post a Comment