Saturday, July 20, 2013

MAOMBI YA TOBA(kUMI LA KUSAMEHEWA)PART 3

Asalaam Aleiykum,

Napenda ufahamu vitendo vyote ulotenda vipo vimeandikwa na wala havifutiki mpaka viombewe msamaha ili upate kuepukana na adhabu ya siku ya Kiyama, Inabidi lazima ufunge safari ya kutubu ili upate kuepuka kuangamia siku hiyo ya hukumu, Sasa hii kutubu imeanzia wapi, kapewa nani? na je wewe pia unapewa maneno haya na muongozo huu, Kihudhurie kisa cha Nabii Adam a.s alipo kosa na kuletewa maneno ya kutubu.
"فَتَلَقَّىٰٓ ءَادَمُ مِن رَّبِّهِۦ كَلِمَـٰتٍ۬ فَتَابَ عَلَيۡهِ‌ۚ إِنَّهُ ۥ هُوَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ "
Akapokea Adam maneno(Ya Maombi)kwa Mollah wake(akaomba)na Mollah wake akapokea toba yake, hakika yeye ndiye mwingi wa kupokea toba, na mwingi wa kurehemu.
Ewe Ndugu yangu umo katika Mwezi wa Ramadhan, na katika aya hiyo yametajwa maneno mawili muhimu kutubu na rehema, ama kumi la mwanzo ni kumi la kurehemewa na hili kumi la pili ndilo la kusamehewa, na wewe unafanya nini? Mwenye enzi Mungu kakujaalia kila usiku unafanya kitu gani?, huu sio mwezi wa kukesha kwenye Tv, wala kwenye gumzo ila mwezi huu unatakiwa uwe unafanya nini? jawabu la kufanya utalipata sura ya Adh dhaariyat 17mpaka18"كَانُواْ قَلِيلاً۬ مِّنَ ٱلَّيۡلِ مَا يَہۡجَعُونَ  "Walikua wakilala kidogo(nyakati)za usiku" "وَبِٱلۡأَسۡحَارِ هُمۡ يَسۡتَغۡفِرُونَ"Na wakiomba Msamaha (Maghfira) Nyakati za kabla ya alfajiri" Na wewe si unahudhuria (Sala ya Taraweih) si Unasali (Qiyyam layla) basi umo katika hao, sasa midamu ushalipata kumi la rehma, basi na sasa pia una uwezo na wewe kupokea maneno ya Mollah wako ya kutubu, na sio lazima yaje kama alivopewa Nabii Adam a.s, lakini yanaweza kuja kwa njia nyingine na mifano mengine, kama ukumbusho huu ya kuwa leo ukumbuke dhanmbi zako zote za nyuma, na kuanzia leo uwe unalia kwenye msala na kujuta, na kudhamiria hutofanya tena, wewe unakiri umekosea  kwenda kushinda kwa waganga, kumdhulumu fulani, na kama yuhai nenda ukamlipe, kama yupo mbali mpigie simu, (hatopata kukupiga ngumi)umtake samahani,kama Umezini huu ndio wakati wa kutubu, kuna ulowatia maradhi kwa matendo yako, kuna ulowadhuru kwa maneno yako, kuna ulowahasidi kwa kuwasingizia mambo chungu nzima, sasa umepata nafasi katika kumi hili taka radhi za Mollah wako, Omba msamaha ili upate kusamehewa, na utakapomalizika mwezi huu endelea kutenda mema kwani kutenda mema kumetajwa katika sura ya Furqan aya ya 70.
"إِلَّا مَن تَابَ وَءَامَنَ وَعَمِلَ عَمَلاً۬ صَـٰلِحً۬ا فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ يُبَدِّلُ ٱللَّهُ سَيِّـَٔاتِهِمۡ حَسَنَـٰتٍ۬‌ۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورً۬ا رَّحِيمً۬ا"
Ila yule atakayetubia  na kuamini na kufanya vitendo vizuri, basi hao ndio Mwenye enzi Mungu atawabadilishia maovu yao kuwa mema, na Mwenye enzi Mungu ni mwingi wa kusamehe (na) mwingi wa kurehemu. yale yote ulofanya ya uovu yatabadilishwa kuwa mema ikiwa kweli utazidisha wema wako. Mwenye enzi Mungu anakupa hekima na muongozo na unakumbuka hili nifanyalo ni kosa, huu mwenendo si mzuri, hapo jijue unapewa (chance) ya kutubu, ili upate kuwacha na kurejea kwa Mollah wako, na unapopewa fikra hizo za kutambua hilo ni kosa basi chunguza nyuma ya fikra hizo kuna neno Msamaha, basi omba msamaha haraka, kwa yale ulotenda ujanani, miezi ilopita au ndani ya mwezi huu kwa kutizama yalo haramu na kula vya haramu, sasa uombe vipi ? hakuna atokufundisha maneno ya kusema ila yeye Mwenyewe Mollah wako, na kama hufahamu hayo maneno unayopewa Moyoni, basi angaku na ujitupe kwa Mollah wako kwa maneno haya ya Toba ili yakuanzishe safari yako ya Kutubu.
"Ewe Mollah wangu Mwenye kujua siri na dhahiri, Mimi nilikua najidanganya katika kukuasi wewe, na sasa niko katika enzi yako yenye kumiliki huu uhai, mimi nimegundua nilofanya hayastahiki kuniweka mimi karibu na wewe, lakini kwa ruhusa ya rehma yako ulonikatia mimi, nakuomba nianguke mbele ya Enzi ya uweza wako ulonijaalia mimi kuweza kukukmbuka, na nikiwa katika mwezi huu Mtukufu ulonitengea ili nifanye Taqwa kwa ajili yako, basi nakuomba kwa dhati ya moyo wangu, UNISAMEHE, natanguliza kwako ahadi ya kutofanya tena maovu nikiwa na Imani kwa hilo utanisaidia, Na nyenyekea katika Enzi yako ya kusubiri, ile ambayo ilikua  ikinisubiria  wakati wote nilokua nikikuasi, Nateremsha mimi hii akili na vilivyomo ndani ya mwili huu, pia naondosha jeuri na viburi vyote nilobeba kwenye mabega yangu, nakuja mimi nikiwa nimebeba mizigo ya Madhanmbi na kuangusha kichwa hichi kwa sijida nikitafuta radhi na msamaha utokao kwako Mollah wangu. Katika Ufalme wako Mollah wangu sina mimi jitihada wala ujuzi wa vipi kujua kama utanisamehe au hunisamehe, lakini nimebeba Imani yangu nikiamini mapenzi yako juu yangu ya huku kuniumba na mimi kukubali na kufanya Ibadah kwa ajili yako, hilo linanipa Imani ya kuamini Mollah wangu utanisamehe kwa Uweza wako."Ewe Mollah wangu hakika mimi nimezama katika kiza cheusi cha madhanmbi, nimekabiliwa mimi na shetani Ibilis katika kila nyanja ya maisha yangu, mpaka jambo la Sala Mollah wangu ananipoteza Shetani Muovu, basi Naomba kwa dhati ya uweza wako Nikinge mimi na Shetani ili nisirudie kukuasi tena katika maisha yangu, kwa Fadhila za Mwezi huu wa Ramadhan na mengine itofata, nakuomba Mollah wangu wasamehe Walo fariki na walo hai, wape uzima waja wako wote wenye maradhi, wape wepesi wale wote wenye dhiki ya maisha, waondolee matatizo kwa kila wenye kuwafika balaa, ututie sote Peponi kwa uwezo wako Yaa Subbhanna.Amin".

No comments:

Post a Comment