Asalaam Aleiykum,
"Ewe" Muumin umo katika kumi la mwanzo, kumi la Rehma, Ndani ya kumi hili inakupasa tukupe peni na karatasi ikisha tukuingize katika chumba cha mtihani, Na chumba chenyewe ni huo Msikiti au hata Chumbani kwako unapofanya Ibadah, halafu ufanye nini ukisha kuingia, kaa kimya au kaa Itikaf upate kuikamata karatasi ya maswali uanze kulijibu moja baada ya jengine hayo yaliyomo kwenye hiyo karatasi.Maswali yenyewe ya huu mtihani yanahusiana na Taqwa, mwisho wa mtihani huu utajua Mwenyewe jee unafanya Taqwa au unaiga kufanya Taqwa. Majibu utakayopata kwa uyakinifu yatakupa nafasi katika mwezi huu wa Ramadhani ya kujirekebisha, au kama utataka kuendelea kama ulivyo, pia huo ni uamuzi wako, na wala hakuna atokulazimisha ukichagua kuwa (Muflis) katika mambo ya Dini.
Unafanyiwa Mtihani huu kutokana na aya moja tu katika sura ya Baqarah aya ya 177,
"لَّيۡسَ ٱلۡبِرَّ أَن تُوَلُّواْ وُجُوهَكُمۡ قِبَلَ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَلَـٰكِنَّ ٱلۡبِرَّ مَنۡ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأَخِرِ وَٱلۡمَلَـٰٓٮِٕڪَةِ وَٱلۡكِتَـٰبِ وَٱلنَّبِيِّـۧنَ وَءَاتَى ٱلۡمَالَ عَلَىٰ حُبِّهِۦ ذَوِى ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَـٰمَىٰ وَٱلۡمَسَـٰكِينَ وَٱبۡنَ ٱلسَّبِيلِ وَٱلسَّآٮِٕلِينَ وَفِى ٱلرِّقَابِ وَأَقَامَ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَى ٱلزَّڪَوٰةَ وَٱلۡمُوفُونَ بِعَهۡدِهِمۡ إِذَا عَـٰهَدُواْۖ وَٱلصَّـٰبِرِينَ فِى ٱلۡبَأۡسَآءِ وَٱلضَّرَّآءِ وَحِينَ ٱلۡبَأۡسِۗ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ ٱلَّذِينَ صَدَقُواْۖ وَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ هُمُ ٱلۡمُتَّقُونَ"
Sio wema(Taqwa) kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa Mashariki na Magharib(Katika Kusali)Bali wema(Taqwa)ni (wale)wanomuamini Mwenye enzi Mungu na siku ya mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, Na wanawapa mali (Zile) wanozipenda, Jamaa (Wakaribu)na Mayatima na Maskini na Wasafiri(Waloharibikiwa njiani)na Waombao na katika (kuwakomboa) Watumwa, Na wakawa wanasimamisha Sala na Kutoa Zaka, Na watekelezao Ahadi zao wanazoahidi, na Wavumiliao katika shida na dhara wakati wa vita, hao ndio walosadikisha(Dini yao)Na hao ndio Wamchao Mungu(Wafanyao Taqwa).
Umo katika Ustaadh wa Kulea Roho wacha nikuchukue pole pole ili upate kujiangalia jee japo kwa uchache mimi ninayo japo matatu katika mambo hayo, Yanatakiwa matatu ili upate kufikiriwa labda unaipata hiyo Taqwa. basi kwa kuanza huo Mtihani endelea part 2.
No comments:
Post a Comment