Friday, July 5, 2013

RAMADHAN:KUFUNGA (SWAUM)NI MAUMBILE PART 3

Asalaam Aleiykum,

Kuna wengine wanaitumia fahamu hii kwa kucheza karata, wengine wanatumia kwa kucheza bao au kutizama senema au na kujishughulisha na harakati zengine ili wapate kujizubaisha na hii (Awareness)kumbukumbu ilowashukia, wanasema poteza muda ili masaa yaende, kumbe hapo wanakosa kitu adhimu kabisa cha kuzungumza kwanza na Mwili wako, habari za siku nyingi, tulikua tumegandana hata ukanisahau, mimi naitwa kiwiliwili na sasa nina njaa, mwenzio taabani, hivi sasa nina hamu ya maji, ukipata fahamu kama hii ushaweza kujitenga na kiwiliwili, sasa unajua kumbe anosikia njaa ni kiwiliwili(Body) mimi ninayefahamu kuwa kiwiliwili kina njaa ni nani?, hapo inakua ushapata (Separation) na hiyo (Separation) ndio kusudio la (Funga) na hapo inakua (Taa) ishawaka unaanza safari ya kwenda huko kwenye (Taqwa). Hapo inatakiwa uigeuze (Fahamu) hiyo sio kwa mambo nilotaja hapo juu, badala ya kucheza karata elekeza mawazo yako katika kipindi hicho kusoma Quraan sana, Badala ya kucheza Bao Sali sana, badala ya kutizama Tv kaa umkumbuke Mollah wako akufungulie Fahamu zaidi, badala ya kujizubaisha Mkumbuke Mollah wako kwa kumsabihi na kumtaja kwa majina yake na ujitahidi uyajue na maana yake, fanya hima vitendo vyako vyote viwe vya kheri na hiyo ndio maana ya "Kama walopita kabla yenu ili Kumcha Mungu"
Na hapa ndio unapata Fahamu ya kujua kumbe katika mwezi huu wa Ramadhan kuna vitu viwili muhimu nimevijua na lazima nivipate, cha kwanza ni hiyo (Swaum) ita unavopenda, kuwaka kwa (Taa)ita (Awareness)ita(Fahamu)ama(Kukumbuka-Dhikr) lakini dhumuni lake ni hilo la (Muamsho). Napenda vilevile ufahamu tafauti yako wewe Muumin na Mcha Mungu ni hiyo (Taa)au(Hadhir)au(Awareness) Muumin yeye anazima na kuwasha, Mcha Mungu inakua imewaka wakati wote, Ndio kwenye mwezi huu wa Ramadhan mnaitwa sasa washeni moja kwa moja, na (Taa) ikiwaka kikweli Shetani haonekani, hapo utastaajabu kwanini Taa imewaka na Shetani haonekani, Sababu Shetani ni mwizi hakai kwenye nuru(Anafungwa)gizani.
Ndio maana utaona ukishawasha hiyo (Switch)(Energy)inatumika pahala pengine, unakua hutamani (Sex)na kila kitu kinakatika, na kikubwa mtu anageuza Fahamu yake yote katika chakula, kila kitu anaona hakitoshi, kashughulika mtu atakula nini (Magaharib)lau angepata kumkumbuka Mollah wake Badala ya chakula mja huyu daraja yake ingekua ya aina nyengine katika mwezi huu wa Ramadhan. Angejua Mawazo yote alokua nayo angeyageuza katika hiyo Taqwa, na asingekumbuka (Makalmati na vyakula vyengine) ila angekua Mwenye kufanya (Itiqaf)au(Sala)au(Kusoma Quraan) na kila ukizidisha vitatu hivyo katika mwezi huu na daraja yako inapanda, Na ukibahatika kufika kileleni ndio unaipata hiyo inayoitwa(Lailatul-Qadir) Umeshapanda kwa Mollah wako na ukiupata usiku huo ndio Malaika wakiteremka na Roho yako unakua ushabadilika, unakua kiumbe mwengine kabisa, na hiyo ndio Maana ya "Bora kuliko miezi elfu" au miaka yako yote 83 ikiwa utaishi, ukiupata usiku huu unatakasika na unakua(Pure) hiyo ndio faida ya (Taqwa)iliyotimia, lakini kumbuka ina vishindo kufikia hali hiyo, hautakiwi uzembe wala uvivu, unatakiwa uwe safi kuanzia Macho,Akili, mpaka chakula chako kinachokwenda ndani ya kiwiliwili. Ikisha ukumbuke " أَيَّامً۬ا مَّعۡدُودَٲتٍ۬‌ۚ" "Ni siku chache"(Kidogo) "Ewe" Mwanaadamu wewe umepewa uhai na ukapewa maisha haya ya dunia na vyote ulivonayo, basi Amri hii ya siku kidogo inakushinda, unaona dhiki kwa ajili ya kufunga, huoni fakhari wewe kutii amri ya Mollah wako, Mbona (Boss) wako kazini unamtii amri zake, Basi ikiwa umezinduka ifanye Ramadhan ya mwaka huu iwe umeitwa na Mollah wako na wewe unatii wito wake, kwa furaha na mapenzi na huo ndio mwanzo wa Taqwa.

" فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٍ۬ فَعِدَّةٌ۬ مِّنۡ أَيَّامٍ أُخَرَ‌ۚ وَعَلَى ٱلَّذِينَ يُطِيقُونَهُ ۥ فِدۡيَةٌ۬ طَعَامُ مِسۡكِينٍ۬‌ۖ فَمَن تَطَوَّعَ خَيۡرً۬ا فَهُوَ خَيۡرٌ۬ لَّهُ ۥ‌ۚ وَأَن تَصُومُواْ خَيۡرٌ۬ لَّڪُمۡ‌ۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ"
"Na atakayekuwa mgonjwa katika nyinyi au katika safari(Akala mchana)basi (atimize)hisabu katika siku nyengine, Na wale wasoweza watoe fidia kwa kumlisha maskini, na atakayefanya wema kwa radhi ya nafsi yake, basi ni bora kwake, Na kufunga ni bora kwenu, ikiwa mnajua".
Na hiyo Swaum ni kheri kwenu ikiwa mnatambua, Sasa zigundue kheri mbili za Swaum, ya kwanza ni (Cure)Matibabu inaponesha maradhi mengi katika kiwiliwili cha mwanaadamu, Na jambo la pili unapata hiyo (Pureness of the Soul) unapata (Taqwa) hizo ndizo kheri mbili zipatikanazo katika funga ya Ramadhan, kupona kwa maradhi na kutakasika kwa Roho nayo ni hiyo Taqwa.
Tunakuomba Mollah wetu zikubali nia zetu, uzikubali funga zetu, uturidhie tuupate Ucha Mungu, sio kwa mwezi huu wa Ramadhan tu bali hadi mwisho wa uhai wetu. Amin.


No comments:

Post a Comment