Sunday, July 14, 2013

MTIHANI WA TAQWA PART 2

Asalaam Aleiykum,

Angalia vizuri sana ikiwa Una Madaraka sehemu yoyote, au wewe mfanya Biashara, au una maisha ya kawaida kama mimi na wewe pamoja na umaskini wetu, utaona aya hii imetukusanya sote kama hupo juu basi chini imekuhusu, na wajibu wa aya hii ni kutukumbusha nini Taqwa, Imekusanya aya hii chanzo cha Mapenzi ya Imani, Kwanini nikataja Imani na nisitaje Kuamini, Kwa sababu kuamini ni rahisi sana(Beliving) Tizama mtoto siku zote anavokuamini unapo mdanganya nikirudi nitakuletea(Sweets)na ukirudi huleti, au unakwenda senema mpaka unatoka unaamini (mkubwa wa Adui)kafa kweli, hivyo ndio kuamini. Lakini (Trust) au Imani ni kitu chengine kabisa, na hicho hakihusiani kabisa na kuamini, Sasa hiyo Imani ikoje?, Imani ilokusudiwa katika hiyo aya ni hiyo (Trust) kabla ya kuendelea mbele zaidi wacha nikujulishe mifano miwili mitatu ya hiyo Imani au (Trust) inakuaje.
Imani inaishi ndani ya Kifua chako na hujitokeza japo kwa uhafifu pale ambapo , tuseme unapanda Ndege, Jiangalie wewe unakua hali gani, Huku Wahudumu wanakuhimiza ufunge mkanda, wanakwambia kama hukufunga hatari tupu, mpaka simu zimeni isije ikatufika balaa, au likatokea la kutokea, tena unazidishiwa habari kwa kuambiwa kama itatokea dharura yoyote au mambo yakizidi pumzi za (Oxygen) tutakupeni sisi, baada ya vitisho vyote hivyo hakuna hata mtu mmoja anaeomba kushuka, unajua kwanini, Sababu (Deep inside of you) kuna Imani (Trust), hapo tena ndege hiyo inaruka na huku dua zinakuporomoka, kwa mara ya mwanzo pengine inakujia walotengeneza ndege hii wamepata ujuzi wao kutoka kwa Mnyama ndege, na kutokana na Mnyama huyo Mwenye enzi Mungu kasema katika sura ya Mulk aya ya 19,

"أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلطَّيۡرِ فَوۡقَهُمۡ صَـٰٓفَّـٰتٍ۬ وَيَقۡبِضۡنَ‌ۚ مَا يُمۡسِكُهُنَّ إِلَّا ٱلرَّحۡمَـٰنُ‌ۚ إِنَّهُ ۥ بِكُلِّ شَىۡءِۭ بَصِيرٌ"
Jee hawaoni Ndege walioko  juu (Angani) wanavo zinyoosha (Mbawa zao)na kuzikunja, Hakuna anayewazuia (wasianguke) ila (Mwenye enzi Mungu),Mwingi wa Rehma, hakika yeye anaona kila kitu. Na mimi sasa naweka Imani yangu yote kwa Mollah wangu ili anivue salama dege hili lisije likaporomoka.
Na kadhalika mkiwa Baharini vilevile Bahari imechafuka nyote mnarejea kwa Mollah wenu na Ahadi na madua makubwa makubwa, Au Mtu akiumwa anakua na Imani mpaka pale anakata Roho, au ukenda kulala unakua na Imani Asubuhi utaamka, basi hizo kwa uchache ni dalili za kuijua hiyo Imani, ili huko mbele katika safari yetu itakapotajwa Imani ujue tunazungumza nini, na tumekusudia kitu gani, Hiyo ndio Imani iliyo tafauti na kuamini.
Sasa Wacha nikupeleke chumba cha mtihani, Na Mtihani ukianza nakuomba kitu kimoja kifanye kwa ajili ya manufaa yako, Utakapoona alama ya Kuuliza (?)na neno funga macho basi jifanyie Ihsani ya kweli yafunge macho yako ili jawabu liwe lako mwenyewe na sio unikopie, hasara yake ukikopia utabakia daima hujui, daima huchunguzi, daima unaamini na unakua huna Imani.
Endelea part 3

No comments:

Post a Comment