Asalaam Aleiykum,
وَخُذۡ بِيَدِكَ ضِغۡثً۬ا فَٱضۡرِب بِّهِۦ وَلَا تَحۡنَثۡۗ إِنَّا وَجَدۡنَـٰهُ صَابِرً۬اۚ نِّعۡمَ ٱلۡعَبۡدُۖ إِنَّهُ ۥۤ أَوَّابٌ۬
"Na Chukua majani mkononi mwako, kisha mpige nayo(Mkeo kwa kiapo ulichoapa kuwa utampiga kwa mabaya alofanya)wala usivunje kiapo, Hakika tulimkuta ni mwenye subira, Mja mwema, kwa hakika alikua mnyenyekevu sana".
Ewe wa (Ayoub)chukua jani umchape mkeo, hapa walovamia tafsiri wakadhani wapigeni wanawake, vipi Mollah wako aagize wanawake waonewe, itakuaje habari hii kuwa watu wamepewa amri ndani ya Quraan wawapige wake zao, Wanashindwa kufahamu Ujumbe uliomo kwenye aya hiyo, Ujumbe unasemaje?
Kwanza kabisa zinavunjwa dasturi zenu za viapo, kwamba ukimwambia mkeo naapa ukenda kwenu ndio itakua (Talaka)yako, Maskini na yule Mke akitoka akenda kwao inakua Balaa, wewe bado unampenda na mke bado anakupenda, lakini katikati mnamkuta Sheikh kavaa (Juba)lake bila ya fikira yoyote anasema Talaka imesihi, Talaka itasihi vipi wakati katikati kuna (Kiapo)na kiapo kinavunjwa kwa kafara, na hiyo ni zawadi ya kuweza kuzitunza ndoa pengine watu wamezaa, au wanapenda kwa ajili ya Mollah wao, wewe unaingia kati na kuwaachisha, nani alokwambia (Talaka)imesihi, itasihi kama wakitaka, na itavunjika ikiwa watatoa kafara, hakuna ukenda harusini ndio Talaka yako, msifanye mchezo huo mnawatia watu matatizoni na kusababisha vizazi kusambaratika na watoto kukulia katika makaazi ya mama peke yake. Naam na la pili chukua Jani umpige nalo ili ukivunje hicho kiapo, kwani kiapo kina mashaka, kiapo kinakutia maradhi, kiapo kinatoka na (Energy)maalumu na ni lazima kivunjwe ili ipatikane salama, Basi "Ewe" Ayoub, chukua jani, kwanini majani, si mnajua majani ni dawa, na yapo ya aina nyingi, unaambiwa hii saga ujipake utapona, hii chemsha unywe utapona, na kwa kuwa Nabii Ayoub a.s anampenda Mke wake basi kwanini achishwe nae, kwa hiyo mpige kwa Jani, unajua kuna nini katika Jani lile, mbali ya kuvunja kiapo? kuna (Transformation)imepatikana kwenye Jani lile, Mke wa Ayoub kapigwa na Mapenzi ya (Nature), Kapigwa kwa Ishara ya kusamehewa, (Chemical)zimemuingia zikambadilisha akarudi kwa Mumewe kwa mapenzi makubwa, Na hayo hayo Majani ndio kitu cha mwanzo Nabii Adam a.s na Bibi Hawa walipogundua (Sehemu zao za Siri)waliyachukua na kujifunika, na hayo hayo majani mpaka hii leo ndio tunavaa nguo zetu.
Na wewe katafute majani yako umpige nayo mwenzako ili upate kumsamehe mpate kuanza tena kama Nabii Ayoub, Pata subira ya Nabii Ayoub, kuwa na wema kama alokua nao Nabii Ayoub, kuwa mnyenyekevu upate kuzidi kupendwa,(Natoa Tahadhari usende ukatafute Jani la Mirungi Utamkosa mwenzio)
Naam Unapata njia ya kusamehe ili uitunze ndoa yako, Na jambo la tatu ni hilo la kujiuliza kwanini visa vyote, na magonvi yote bado mko pamoja, Jawabu kuwa hiyo ndoa yenu imefungana moyoni, bado mnapendana, lakini Akili zenu zimetafautiana, nyoyoni nyote baridi, lakini kichwani kila mtu anamuua mwenzie kwenye ndoto, lakini moyoni kuna kitu kwako na kwake bado hakijatoka ndio maana mpaka leo mko pamoja, sasa mkikigundua hicho kitu mnakua hamna haja ya magonvi, ama kama hamjakigundua kikatoka chenyewe basi hamkai hata dakika moja pamoja, na hivyo ndio inatokea kila siku kwenye mdomo mnagombana kwenye moyo mnapendana, Na moyo ndio wenye nguvu kwa hiyo unaamua kustahamili labda atabadilika, vituko vinaendelea, adhabu zinazidi na hapo unakua unaishi kwenye msiba wa ndoa, na unasahau kama unaweza kustahamili visa vyote, na adhabu zote, kinakushinda nini kuondoka ukafanya majaribio kuona jee huyu atanimiss, jee atanitafuta, Na kama huyawezi yote basi nyanyuka Umshtakie Mungu , Useme nakuomba Mollah wangu uwezo wa kuondoka sina, na Kukaa sasa nishachoka Madhila haya , sasa na nyamaza kimya nijengee jumba langu peponi, na sasa nayabadilisha mapenzi haya kugeukia kwako Mollah wangu naomba nipokee, Na huyu Mume wangu akiingia basi nimuone kama kabati. Amin.
No comments:
Post a Comment