Sunday, September 8, 2013

HEKIMA YA UZEE PART 1

Asalaam Aleiykum,

Hudhuria aya ya 269 ya sura ya Al-Baqara ukutane na maelezo ya Quraan yenye kuhusiana na mafunzo ya Hekima na ukumbusho wake, "

"يُؤۡتِى ٱلۡحِڪۡمَةَ مَن يَشَآءُ‌ۚ وَمَن يُؤۡتَ ٱلۡحِڪۡمَةَ فَقَدۡ أُوتِىَ خَيۡرً۬ا ڪَثِيرً۬ا‌ۗ وَمَا يَذَّڪَّرُ إِلَّآ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَـٰبِ
"(Mwenye enzi Mungu)"Humpa Hikima amtakaye, Na aliyepewa Hekima bila ya Shaka amepewa kheri nyingi(Kitu cha thamani)Na hawakumbuki ila wenye Akili.
Yametajwa maneno haya  mawili ili kuonesha nini hikima na ipi Akili, na imepatikana tafsiri ya wazi pale iliposemwa hawakumbuki isipokua wenye Akili.
Nini Hekima? Najua hutoshangaa nikikwambia Uzee ni kifo (A very slow death)Kifo hichi kimeambatana na Uhai, kila siku Unakufa na kila siku unaishi, na ndani ya huo Uhai ndimo inaishi hiyo Hekima, na katika hicho Kifo kinabakia hiyo Akili, Na Akili ina kazi mbili ima  kukumbuka ya Zamani (Death) au Kukumbuka mepya(Life)yenye kuishi wakati huu tulonao.
Leo hii imeniwajibikia juu yangu kukusaidia ili ukumbuke na upate kuzingatia japo kwa uchache hicho kifo cha Akili na kuzaliwa kwa Hekima ambayo inakusaidia kuona vipi unapita katika Mauti haya ya Aina Mbili. Watu wengi wameghafilika na kitendo hichi cha Umauti ambao uko wazi na sote ni wenye kushuhudia, lakini labda tumejitoa fahamu au kwa ukweli kabisa tumelala usingizi mzito na kutofahamu nini kinaendelea. Ama kifo cha Mwanzo chenye kutokea ni (Physical Death) Na hili limetajwa katika sura ya Yaasin 68 "وَمَن نُّعَمِّرۡهُ نُنَڪِّسۡهُ فِى ٱلۡخَلۡقِ‌ۖ أَفَلَا يَعۡقِلُونَ"
"Na tunayempa umri(Akawa mtu mzima)tunamrejesha nyuma katika Umbo(Uzee)Basi hawayatii Akilini(Kuyafikiri)"
Huko kurejeshwa nyuma ni kupita katika (Process)ya Kifo, kifo chenyewe kwanza ilikua (Foward) sasa imekua (Reverse) na vyote hivyo vinapita katika jambo hili moja la kudumu, jambo la milele nalo hilo (Life) au Maisha, na katika hayo maisha ndipo inatokea hiyo (Hikima) ambayo inashuhudia vifo vyote viwili cha mwanzo (Physical) na cha Pili (Mind), Kijue kifo cha mwanzo kinatokea vipi?
Kina mambo haya yafatayo:Ambayo yanakutokea unayajua, unayaona lakini bila  kutumia (Hekima)
(1)Kupungua kwa pumzi/kuchoka, (2)Kupungua kwa Nguvu(3)Kupungua kwa Usingizi(4)Masikio kutokusikia Uzuri(5)Macho kupungua Nuru yake(6)Kupunguza Kuongea(7)Kuwasili kwa Maradhi(8)Kukunjika kwa Ngozi(9)Mifupa kuwa Dhaifu(10)Kungoka na Meno(11)Na Kupotea kwa Sex(Matamanio)
Kinakutafuna kifo hichi mpaka ufikie Umri wa Miaka (7x6=42)au Umri wa Miaka 40 na 42 ndio unafikia hichi cha pili ambacho unashuhudia (Death of Mind)Kifo cha Akili, ambacho mambo yake ni haya:(1)Kuanza kuona Mabadiliko(2)Kupungua kwa (Social activity)(3)Marafiki wanatoweka(4)Ukenda Disco au Taarab unakua wewe wa mwanzo kuonekana(5)Vivazi vyako vinakua tafauti(6)Fikra zako zinakua za Woga(7)Akili yako inakua haina uwezo tena kuhimili mafunzo mepya(8)Kwa kuwa ushafikia kikomo unabaki kungangania Historia(9)Unakua Mkaidi(10)Hufurahi na chochote na hata kama kufurahi ni kujionesha tu(11)Hupendezewi na kufurahi na wenzio(12)Umechoshwa na maisha(13)Unatamani Maisha ya Vijana(14)Unafilisika Kifikra(Maarifa) Sasa kutaka kumjua Mwenye hekima ni kumgundua yule alopata ku(Jump) au (Chance) ya kuipata hiyo Hikima na yeye akaichukua na kuitumia ipasavyo, na kila mmoja anapewa nafasi hii, wako wanopewa mapema ambao ni wachache sana, na hupewa baina ya miaka 28 na 35, na ukipata Fadhila hii unakua umepewa Fadhila kubwa kabisa na Mollah wako, unageuka kuwa mtu mwengine kabisa, kwa sababu Hekima (Wisdom)sio (Knowledge),Elimu wanafundisha watu kama wewe, zimejaa kwenye vitabu, ni kama (copy). Lakini Hekima (Wisdom)Inatokea kwa Mollah wako, ni kitu ambacho (Beyond Education)Kwenye (Wisdom)kuna kitu kimetokezea na wewe kwa furaha una (Share) na wenzio.Sasa kutaka kuijua hiyo Hekima endelea Part 2

No comments:

Post a Comment