Asalaam Aleiykum,
Kwanza nenda kafanye Hijja kwenye Moyo wako, hilo ni jambo la mwanzo linalotakiwa, sio kuonesha watu na wewe umekwenda Makka, hudhuria kwenye Moyo uondoshe Chuki, uondoshe Tamaa, Ondosha fitna moyoni, Sahau majeraha yalokupata, Rudisha mali uliyodhulumu, Wasemehe waliokukosea na pia omba usamehewe, Nenda (Deep) kwenye kisima cha Moyo wako anza kupenda walokaribu yako, watakie mema, waonee huruma, anza kujipenda mwenyewe kuwa umefanyiwa ukarim wakuweza hata kufikiria kwenda kuhudhuria nyumba ya Mwenye enzi Mungu, Wapende Maskini, Upende Ulimwengu na vilivyomo ikisha fungua Moyo ushukuru ya kwamba uko hai na unajitaarisha kwa safari hii Tukufu ya kwenda kwenye nyumba ya Mwenye enzi Mungu, Omba mapenzi ya Ucha Mungu yakushukie, fanya hima kwa kipindi hicho cha kusubiri uone nini kinatokea katika Moyo wako, jitizame mwenyewe kwa siri jee nabadilika, niko tayari mimi sasa kwenda Hajj, na kama muangalifu utayashuhudia mabadiliko yanatokea taratibu na utauona moyo wako unasafika, hamaki zinapungua, unakua mwenye huruma, husda inakatika, unaona mambo kwa mtizamo mwengine kabisa, unakua mpole, Imani na ukimya unakutawala, unapenda kusaidia wenzio, ukiona dalili hizo zimekushukia sasa wewe tayari ushakamilisha Hijja ya Moyoni na wakati wowote sasa moyo unaweza kushukiwa Miujiza kutoka Mbinguni, sababu umeshakua msafi, na sasa uko tayari kwenda kwenye hiyo Hijja ya nje, Hijja ya Kuhudhuria Nyumba ya Mollah wako Duniani, Pahali walipoishi viumbe watukufu katika (Historia) ya Ulimwengu huu, wakaacha mifano na (Special-Energy)zao mpaka leo zina (Viberate) Sasa funga Safari ya kwenda kwenye Mji huo, huku unamuendea Mollah wako na Moyo ulosalimika.
Endelea Part 3
No comments:
Post a Comment