Asalaam Aleiykum,
Hii Quraan Inatumia Sauti(Sound)na ukimya wa Sauti(Soundless)kufanya utibabu wake, Na hiyo Sauti nyenzo yake kubwa za kutendea kazi yake ni (Air)upepo na (Water) maji, kumbuka wewe mwenyewe 85% ya (Body)mwili wako umetawaliwa na maji, na upepo unahitajika(Oxygen) kwa (Supply)ya vilivyomo kwenye kifua chako.
Quraan inatibu kwa kutumia (Secret coded massage) zilizomo kwenye sura au aya kukutibu wewe maradhi mbali mbali ima iwe kwa kusomewa au kwa kuandikwa, yote hayo yanatoa huduma zake kwa yule mwenye kufanyiwa, Na kwanini isiwe hivyo, kwanini unabisha, wakati unafahamu kuwa sauti hiyo hiyo ukiambiwa mtu wako wa karibu amefariki(unatoka na machozi) na ukiiambiwa amepona maradhi(Unafurahi), nini kinatokea hapo, wewe uko mbali hujawa shahidi wa hayo yote mawili lakini sauti inakubadilisha, sasa ikiweza kufanya kazi hiyo kwanini isiweze kufanya kazi ya kukupa ponyo kwa yaliyomo kwenye kifua chako.
Kumbuka aloleta Mti shamba ukutibu ndio yule yule aloleta hii Quraan na Muujiza wake wa hayo Mambo 4 niliyoyataja, na ukichunguza utagundua hayo na utakutana na mshangao mkubwa nikikwambia kuna sura zikisomwa kwa sauti maalum kama mgonjwa taabani basi inafanyika safari yako ya (Umauti)kuwa nyepesi na ya haraka, elimu hiyo inaitwa (Burdai)na mpaka leo wako wachache walo nayo huko Zanzibar.
Hivyo ndio yanavopatikana masomo haya ya Quraan kwa yule mwenye kujua asome kitu gani kukutibu kitu hayo maradhi, na inayopatikana hapo ni hiyo (Combination of sound)na matamko ya aya yaliyomo kwenye hiyo aya, na pia inategemea mjuzi wa elimu hii na ufahamu wake wa kutumia elimu hii ya Kitabu hichi.Usije ukaondoka hapa na kutaka kusoma kimafamba, ndio yatakukuta ya yule alotaka pesa na kusoma (Surat-masad-Lahab).
Na huo Muongozo ambalo ni jambo la tatu ni ndio huo wa kukutoa kwenye giza na kukupeleka kwenye nuru, kukufahamisha mabaya ukayaepuka na mazuri ukayafata, kutujulisha kwamba kuna moto na pepo vinatusubiri, vipi tumuabudu Mollah na kuwatendea wema, wazee na watoto, maskini na mayatima, wajane na waloharibikiwa katika maisha nk, Muongozo wenyewe ni hii dira ya Uislam ambayo tunaifata, na kama utaifata ipasavyo hutoweza kupotea.
Na Rehma hii ya Quraan imetengewa (Special)kwa waloamini, Rehma ziko nyingi na viumbe wote ni wenye kuzipata, lakini hii ya Quraan inatokea kwa Muumin pekee, hii ni hususia kwa kuwa kuna kitu kinatokea, unapatikana mripuko fulani ndani ya nafsi yako na huo haupati kila mtu, na chunguza pale inaposomwa Quraan umekaa wewe na Muislam mwenzako lakini yeye ana Iman hafifu na dini yake, si mwenye kuitaka Quraan, wala hashughuliki nayo, inaposomwa wewe kinaingia kitu fulani moyoni, hiyo ndio Rehma, hicho kinacho kuingia inaweza kua ponyo(Dawa)au muongozo au Nasaha, na hiyo ndio (Rahman Rahiim) inaweza kuwa chochote, wewe sikiliza tulia wacha yende ndani ikapasue, haikuumizi ila ni Rehma tu, na yule mwenzio aliyekuwepo hapo hapati chochote anaona kitabu kama vilivyo vitabu vyengine.
Nakuomba uelewe kama wewe Muumin uzidishe juhudi sasa ushiajua siri yake hii Quraan, usikubali tena ikasomwa au kuisoma mwenyewe ukawa una mawazo mengine, tulia usikilize ili uzipate hizo Rehma, na kidogo kidogo ukifatilia utakuja kuyaamini maneno yangu, nazungumza katika uzoefu sio katika ukanda wa kusikia. Tulia usikize uyapate mambo hayo 4 pamoja utakua mwenye kufanikiwa, utakua umehifadhi kitu kikubwa ndani ya Moyo wako, Na daima utatembea na Rehma hizo za Quraan. Mollah atujaalie kusoma na kufahamu, atukirimu kusikiliza na kutulia ili tupate Rehma zake. Amin.
No comments:
Post a Comment