Sunday, September 22, 2013

FURAHA YA MAPENZI PART 4

Asalaam Aleiykum,

Siri iliyopo hapo nikuwa Ukipenda wewe una (Disappear)Mkipendana nyote mna(Disappear) penzi pekee ndio linabakia, na (When love Disappear)Penzi likiondoka halendi kokote ila linarudi kwa mwenyewe alolileta, na likirudi hapo ndio sasa linabadilika na kuwa (Taqwa)." وَأَلۡقَيۡتُ عَلَيۡكَ مَحَبَّةً۬ مِّنِّى "
"Nimekutilia mapenzi yanayotokana kwangu" (Maneno hayo anaambiwa Nabii Musa a.s)(Taha 39 mpaka mwisho wa aya) Na wewe utayapata kama utajitupa kikweli kwa Mollah wako, hiyo ndio ngazi ya tatu ngazi ya Taqwa, ukifika  katika Taqwa mapenzi yako yanabadilika kuwa (Blissful) kuwa (Joy plus Celebration) hapo tena siwezi kuhadithia nini kinatokea, hadith hazina maana tena, kumbukumbu hazitakiwi hapo, huwezi kutoa hadidu rejea, hapo unatokea mripuko wa mapenzi, mfano wa FashFash au (Fire Work)hapo inabidi ufike mwenyewe, na pahala hapo ndio  watu wanatumia kila mbinu na maarifa kupafikia na pametajwa baadhi ya mbinu wanazotumia Makasisi au Mapadri walotajwa katika sura ya (Hadid aya ya 27)

ثُمَّ قَفَّيۡنَا عَلَىٰٓ ءَاثَـٰرِهِم بِرُسُلِنَا وَقَفَّيۡنَا بِعِيسَى ٱبۡنِ مَرۡيَمَ وَءَاتَيۡنَـٰهُ ٱلۡإِنجِيلَ وَجَعَلۡنَا فِى قُلُوبِ ٱلَّذِينَ ٱتَّبَعُوهُ رَأۡفَةً۬ وَرَحۡمَةً۬ وَرَهۡبَانِيَّةً ٱبۡتَدَعُوهَا مَا كَتَبۡنَـٰهَا عَلَيۡهِمۡ إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ رِضۡوَٲنِ ٱللَّهِ فَمَا رَعَوۡهَا حَقَّ رِعَايَتِهَا‌ۖ فَـَٔاتَيۡنَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنۡہُمۡ أَجۡرَهُمۡ‌ۖ وَكَثِيرٌ۬ مِّنۡہُمۡ فَـٰسِقُونَ
Ikisha tukawafatishia nyuma yao Mitume wetu, Na tukamfuatishia Isa bin Maryam, na tukampa Injili, Na tukaweka upole na Rehma katika nyoyo za wale waliomfata, na Uruhubani (Wakutooa au Kuolewa)wameubuni(wenyewe)Sisi hatukuwaandikia hayo,(Waliyafanya haya wenyewe)ili kutaka Radhi(Mapenzi) ya Mwenye enzi Mungu, lakini hawakuufata(Huo Utawa)kama inavotakiwa kuufata, basi tukawapa wale waloamini miongoni mwao ujira wao, na wengi wao ni (W)maasi.
Hiyo ndio (Power of Sex) ukijidai kuizuia itakuadhiri na ukiichezea sana itakukashifu(Hapo havuki mtu) ila mtu afate muongozo wa Mollah wetu kuitumia (Energy) hii kwa uangalifu baina ya (Mume na Mke)tena kwa Mapenzi, hakuna njia nyengine ila utaingia hasarani.
Wako waloweza kuufata huo (Utawa) kikamilifu ndio wakaambiwa watalipwa kutokana na jitihada yao hiyo, Lakini Mwenye enzi Mungu hakututakia mazito anajua tunapata taabu, ndio akatuletea njia zake za mapenzi tuishi kwa Raha na furaha, Maisha yanatakiwa baina ya (Positive na Negative) Baina ya (Mke na Mume) ndipo yanapopatikana Mapenzi Kamili.
Mwisho sina Budi kunukuu maneno ya (Rumi)
God has placed a ladder before our feet, we must climb it, step by step.

No comments:

Post a Comment