Asalaam Aleiykum,
Na Mwenye kupata hiyo hekima ndio anakua na uwezo wa kuvishuhudia kwa Ukamilifu vifo hivi viwili vinavyotokezea cha mwili na cha Akili, Mwenye Hekima anacheka, mwenye Hekima ana furaha, anaridhia kwa kujua kuna kitu chenye Thamani kushinda viwili hivi.
Sasa Unakuwaje ukiipata hiyo Hekima(Wisdom)?
Kitu cha kwanza kabisa unakua mwenye Furaha sababu hekima na (Happiness)vinaenda sambamba, sababu hata dhiki ikiwepo wewe unaiona kwa upeo mwengine, Na kubwa katika hilo unakua unaishi katika (Level)nyengine ya (Consciousness) sio ya (Mind) tena.
Kwa ajili ya kuishi kwako kwenye (Consciousness)unakua una uwezo wa kushiriki(Level)zote za jamii, ukiwa kwenye kundi la watoto wanakuona mwenziwao, ukiwa na vijana wala hawababaiki wanajua unawafahamu nyendo zao,Ukiwa na Wazee wanakuhisi wewe Mmoja katika wao, Kila anaye kuona anataka ushauri kutoka kwako kwa sababu wanavutika na Hekima zako, Kila anaekuheshimu na wewe unamuheshimu, Kila ukionekana upo kwenye furaha, Na hiyo ndio alama kubwa ya Hikima(Wisdom) ambayo inatokea inapotokea Afya,Furaha,Msiba na Kadhalika.
Mwenye Hekima Hawi Muongozaji bali anakua Muelekezaji,Mwenye Hekima anakua mwepesi kukiri kosa lake, hawi mshindani,wala si mwenye kutafuta ushindi, ila yeye anakua Mja wa subira.
Mwenye Hekima Maradhi na msiba vikija anaviangalia sababu kashatambua hivo vitu viko vinakuja wala hana uwezo wa kuvizuia, Maradhi yakifika haya muhuzunishi, Kifo kikikaribia anaelewa sasa wakati ushafika wa kuondoka kikamilifu kwenye huu Mwili(Body).
Marafiki wakipungua anajua sasa ni wakati wa kumtafuta yule Rafiki yake Mkubwa aliye hai Milele wala simwenye kumkimbia, na huyo ni Mollah wake Muumba.
Mwenye Hekima daima anakua na Fikra mpya, na wala haogopi mambo mepya, anakua sio mkaidi wa kupinga kila jambo, anafurahi akiona wenzie wanafurahi, Mwisho kabisa mwenye Hekima anao ujuzi wa kujua kwamba matamanio ya (Sex)yakitoweka basi (Energy)hiyo sasa inakua (Transformed to Love)inageuka mapenzi, anakua Mtu huyo mapenzi matupu, sasa hana Dhara kwa yoyote yule, akishauriwa mambo ya hatari anasema laa msifanye, pakitaka kutokea dhara anakua wa mwanzo kuiepusha.
Sasa soma Part 3 Umuhudhurie yule asokua na Hekima anakua hali gani?
No comments:
Post a Comment