Sunday, September 29, 2013

UZURI WA MAISHA PART 2

Asalaam Aleiykum,

Kutokana na hali hiyo sote tunajijua Wagonjwa na sasa tunahitaji dawa ili tupate nafuu ya maradhi haya, tupate japo kidogo katika umri wetu kuona uzuri wa maisha, Na (Dose) ipo huna haja ya kwenda hospital au pharmacy, huko wanakwenda walozidiwa wewe unaweza kutibiwa nyumbani bila ya matatizo, na dawa ya mwanzo kabisa utaipata ndani ya (Quraan) nitakupa hii sura ambayo kama utaifanyia kazi ina siri ndani yake, inaponesha maradhi ya fikra ulo nayo, inaponesha (Depression) inaondoa wasiwasi akilini, inakutuliza ama kwa kuisoma au kusomewa iwe kwa kuandikiwa au kutiliwa kwenye maji dawa (mjaarab) sana mimi mwenyewe binafsi nawapa watu na inawasaidia, Na hiyo ndio siri ya (Quraan)kama nilivoitaja katika Darsa yangu ya (Rehma na matibabu ya Quraan).
Katika sura hii ni sahihi kabisa kama ilivotajwa na (Masheikh wakubwa wakubwa kuwa imeteremshwa kwa ajili ya kumliwaza Bwana Mtume s.a.w)lakini kumbuka alichoteremshiwa Bwana Mtume s.a.w wameteremshiwa walimwengu wote, na kila Mwanaadamu inamgusa isipokua akiwa hataki mwenyewe, kabla ya kwenda kwenye sura yenyewe na kujua faida yake napenda kukujulisha dhumuni la nje la sura hii, kwa njia ya nje nayo ni (Rehma)inakutaka sura hii uwe Shahidi(Witness) na sio (Historian)kama ulivo sasa unaishi(in the past) inakutaka sura hii uwe na uwezo kama ulionao hivi sasa wa kuweza kusahau Mazuri basi na mabaya usiyakumbuke uwe mtu wa kati na kati( وَڪَانَ بَيۡنَ ذَٲلِكَ قَوَامً۬ا ) ukiiwacha tabia hiyo utapata nafasi ya kwenda  (Beyond Both) Utakua hukumbuki mazuri wala mabaya, fanya ((Balance and then you are)unakua ushawasili kwenye ushahidi, Nikamate mkono vizuri usafiri na mimi kwenye Ulimwengu huu nikutoe kwenye mashaka upate kuona Uzuri wa Maisha haya, fika pahala ambapo kama utazinduka basi kila jambo lako ukiwa maskini au tajiri, ukiwa na maradhi au afya utakua una furaha, na kila kitu chako utakiona kuwa ni kizuri, hapo ukishawasili kwa furaha za kuona uzuri wa maisha haya hata mtu akikupiga kibao shavu la kulia utamgeuzia na la kushoto akumalizie.
Na hiyo sehemu ya pili ya sura hii ambayo ndani yake kuna hizo (coded massage) za kutibu maradhi kama (Depression)na wasiwasi utaisoma pia ukiwa na donge la Roho ni kuandikiwa au kuyasomea maji mara 70 sura hii ya (Dhuhaa) inaondosha madhara ya Tafrani katika Akili yako, Na uteremkaji wa sura hii ulikuja pale Bwana Mtume s.a.w alipokaa muda mrefu ukawa (Wahyi)haukuteremka basi alikua katika hali ya huzuni kubwa ya maisha yake, na huku Watu wakimfanyia stihzai, vipi Mollah wako kakasirika nk, ndio ikateremka sura hii kumliwaza na kumpoza Bwana Mtume s.a.w, Na wewe pia inakupoza  sura hii kama ilivosemwa Quraan imeletwa kwa ajili ya (Mankind)basi na wewe umo, na Mollah wako anakupoza na ukiwa Shahidi utajua kweli na mimi nimepita katika hali hizo zote na hiyo ndio Quraan na maajabu yake, uongozi wake, matibabu yake pamoja na hizo Rehma. Sasa tutaipitia aya moja baada ya moja ili tugundue tufanye nini na sisi tufurahi kama alivofurahi Bwana Mtume s.a.w ilivoteremka sura hii, na hakuna furaha tutayoipata sisi kama kuona uzuri wa maisha haya, kumbe mambo hivi ndivo yalivyo. Endelea part 3

No comments:

Post a Comment