Sunday, September 9, 2012

HAKI YA KUMSALIA MAITI UKIWA MBALI (PART 1)

Asalaam-Aleiykum:
Mwanaadamu kapewa cheo mara mbili na Mollah wake, kwanza pale alipoumbwa mara ya mwanzo Nabii Adam a.s  wakaambiwa Malaika wamsujudie,  Sote tunakifahamu kisa hiki hakuna haja ya kukirejea, Ikisha akapewa darja yengine anapofariki(kufa)basi atapewa heshima ya kusaliwa au kuombewa(utakavo penda kuita).
Bwana Mtume s.a.w akatufanyia hisani ya kutufundisha vipi njia ya kufanya na taratibu zake na mipango yake na dalili zake zote wala hakuweka kizuizi katika hilo.Vipi? Mbali na zile sala za kuwasalia maiti waliokuwepo machoni mwake pia aliwasalia walokuwa mbali na hata walokwisha kuzikwa ili atufahamishe sisi kuwa yote ni sahihi na ndio mafundisho yake, na wala hakuna pahala aliposema hivi msifanye nafanya mimi tu, kwa kuwa hili wamepangiwa ni Sala ya (Mitume)hakuna jambo hilo, nini alifanya Bwana Mtume s.a.w "Anahadithia Sayyid Abbi Hurairah r.a "Alipata habari siku alokufa Najash,(King-Negus-wa-Ethopia)Akatoka na masahaba kwenye(kiwanja)akawapanga safu,ikisha akatoa Takbira na (Kumsalia)fundisho la kwanza,(Bukhari-na-Muslim-kitab-janaiz)halafu kisa chengine yule Bibi wa kimaskini alokua akifanya kazi za kufagia msikiti, Alipewa habari Bwana Mtume s.a.w kuhusiana na maradhi yake akaagiza ikiwa atakufa basi nambieni, Alipofariki ilivokua usiku Mtume s.a.w kashalala Masahaba zake wakaamua kumzika bila ya kumuarifu Bwana Mtume s.a.w, ilipofika asubuhi wakampa taarifa akawaambia sikukuamrisheni mnipe habari atakapokufa?wakasema tulikhofu tusije kukuangaisha usiku "Ewe mjumbe wa Mwenye-enzi-Mungu"Akatoka Mtume s.a.w na Masahaba mpaka kwenye lile kaburi akawapanga safu masahaba zake ikisha akatoa takbira (4)yaani kumsalia:Imetajwa pia na (bukhari na Muslim katika kitab cha salah ya kwenye kaburi).Naam hiyo ndio habari, hayo ndio mafundisho hayana pingamizi ila uwe unampinga Mtume s.a.w, hapa sisi waislamu tumepata mafundisho hata ukiwa mbali unaweza kumsalia na kumuombea maiti yako, na hata kama kazikwa unaweza kumsalia kama vitendo vya hadith vinavoelezea na hii ni faraja kwa wale pengine kwa sababu zisizoweza kuzuilika hawatoweza kuhudhuria hiyo (Fardh-kifaya)basi wanaweza kusali na inajuzu kumsalia Maiti wako au muislam mwenzio yoyote yule.
Sasa na tuingie kwa undani tutazame kwanini tunasali hii Sala ya Maiti? Napenda uelewe sala hii ina sehemu mbili, ama sehemu ya kwanza ni ile kuupa heshima ule mwili wa marehemu kwa wale walokaribu wanapata nafasi hii ya kusimama mbele ya maiti na kumsalia(Sio kutoa heshima za mwisho)unafanya hivo pengine alokufa Mkeo, au Baba yako au Mama yako au Mwanao, nimewataja hawa wa karibu kuonesha umuhimu wa jamaa kwa yule alotangulia mbele ya haki, yule wewe umeishi naye, umekua naye, kipenzi chako umesimama mbele yake unapata nafasi ya kumuaga kwa kumsalia na kumuombea kwa njia za Mwenye-enzi-Mungu yule kiumbe mlokua pamoja katika ulimwengu huu(Nasisitiza wale walokaribu wasikae nje ya misikiti na kuacha kusalia Maiti zao)isiwe basi ndio kafunikwa vitambaa ndio yale mahusiano yenu yote yamekwisha anakuhitaji hususan siku hii ya leo, nitaita sehemu hii ya mwanzo ni (Physical).
Na hii sehemu ya pili ambayo nitaiita (Sipiritual-cum-Mental)hii ni ile ya kiroho au (Communion) napenda nifafanue (communion)ni tendo la moyo kwa moyo au roho kwa roho au (Roho)na (Mollah)wake, usije ukababaishwa na (Communication)ni (head to head)maombi hayo hayafiki kokote,  sasa nini mfano wa hiyo (Communion)ni kitendo cha hisia(Mfano)kama vile kaja mtu mbele yako hajakwambia chochote kasimama mbele yako machozi yanamtoka pengine na wewe yatakutoka machozi au bila ya kujitambua, kilochotokea hapo ndio hiyo (communion)ni mawasiliano ya kiroho au kimoyo ita utakavyo na mifano iko mingi wewe ishakutokea, kama vile umeona (Accident)umekwenda kutizama mgonjwa kuna kitu kinatokezea ndani ya (Ufahamu)wako na hiyo ndio adhma yangu ya kuizungumzia hii (Sipiritual communion)ambayo haikatiki, ianayokatika ni communication. Na  sio sisi  Binaadamu peke yetu wenye hii (communion)hata wanyama wanayo, Wanasayansi walifanya uchunguzi wakachukua wale wanyama wanozaa, wakawapeleka mji mwengine kabisa, Halafu wakachukua vitoto vya wale wanyama vikachinjwa, Wanasema wachunguzi hao tuliona mfadhaiko na huzuni kwa Mama za wanyama hawa, sasa ikiwa vinyama hali hiyo nini hali yetu sisi Binaadamu unapofiwa na alio wako?
Kutokana na hii (communion)ndio Bwana Mtume s.a.w akasema "Wakipatikana watu mia wasomshirikisha Mollah wao na chochote ikisha wakamuombea maiti anakua Mollah ni mwenye kuipokea dua yao na hadith ziko nyingi na zengine zimetaja watu (40)nk.
Kwanini sasa nikasisitiza watu wa karibu ni uzuri kumuombea (Maiti)? sababu zinazopelekea hapa ni ile (Communion)niloitaja, Nimehudhuria misiba kadhaa nimekuta watu wa marehemu labda kwa kutokujua au kufahamiswa vyengine wanakua hawasali sala hii, wengine wananifahamisha jambo hili halifai, au watamsalia walio karibu naye huko nyumbani, walomwambia hivo wao wenyewe hawana ushaihidi wa jambo hili, au pengine ndani ya mioyo yao hakuna (Communion)hisia zimeondoka na jambo hili ni hatari kubwa, Watu wanakuwa hawasalii watoto zao au watoto hawasalii wazee wao na hii ina kunyima siku hii adhimu ya kumuombea mzee wako,  ana hali gani yule mzee au mtoto atakapo tizama nyuma na kuoneshwa hata alo wako leo hataki kukuombea au kukusalia anapiga (story)za mambo ya kipuuzi na wenzie, basi jikumbushe mwanaadamu una mambo mawili ambayo huna uwezo nayo,Mambo yepi hayo? Endelea sehemu ya pili.

1 comment: