Sunday, December 29, 2013

DAWA YA DHIKI PART 2

Asalaam Aleiykum,

Kwenye hiyo aya imetajwa chochote ili usije kudhani labda vyengine havimo. Sasa Dhiki ina Pande mbili kama ilivo Shilingi, Upande wa kwanza una maandishi ya (kuhitaji)kuna kitu (Missing)lakini hukijui nini?, Na upande wa Pili kuna maandishi Dhiki ni Kapu la Dhanmbi, Dhiki haiji lazima kuna majanga unayatengeneza(Lazima unakwenda Shopping na kapu lako), na sasa matokeo yake kapu limejaa ndio maana unasikia (Dhiki).
Vipi unakua mpaka kufikia (Stage)hiyo, hapa nitaitaja mifano miwili mitatu na mengine utaongezea mwenyewe, na Mengine itakua (Surprise)lakini kwa kuwa ni sehemu ya Dhiki itabidi niitaje ili tupate faida yake. Vipi unaanza kuchuma Dhiki kwenye Nafsi yako? kumbuka huko nyuma umesoma kila kitu kinalipwa, sasa pengine unamtania mtu na yeye hapendi, hapo tayari ushachuma Dhiki, pia kumbuka Dhiki ni kitendo baina ya Nafsi kwa Nafsi, Ukiikera Nafsi na wewe malipo yake unapewa Dhiki, Unamsengenya mtu, mbali ya kuandikiwa Dhanmbi pia unapewa na Dhiki(Na mfano tizama kama ghafla atatokea huyo unomsengenya unakua vipi)hilo ndilo chumo la Dhiki, Unawatesa viumbe wenzio na wewe unapewa Dhiki, Unatamani Mke au Mume wa Mtu, huku kwa nyuma unapewa(Double dose)ya Dhiki na matatizo, Wewe Tajiri unaonea na kuwadhalilisha wafanyakazi wako, huku na wewe unapewa Dhiki huna Raha, Wewe kiongozi unaonea unaowaongoza huku unapewa Dhiki unakua huna Raha Kabisa, Hata ukimuona Nyoka maskini anakukimbia anaelekea shimoni kwake, ukaamua kumpiga akafa, basi na huku unapewa Dhiki kwani na yeye ana haki ya kuishi kama ulivo wewe.
Na Kubwa zaidi ni hili umeshakusanya Dhiki sasa zimekujaa (Tafrani)imekushika ghafla unaamua kumbe kuna kitu kinaitwa Sala, unaingia Dini kwa mikiki, sasa mahitajio yako yote ni (Pepo)ya (Express)tizama madhara ya Dhiki zako unavofanya katika Ibada zako, la kwanza inakua watu wote walosali miaka yote wanakua hawajui kusali, lazima uwafundishe tena, unakuja na hasira na jazba kubwa kabisa, unajua kwanin,i ni ile ile Dhiki inakutesa, kwanza ilikua katika Dunia sasa imehamia kwenye Akhera, ndio maana utaona matendo yako japokua mazuri lakini yamejaa chuki, mafundisho yako yanaweza kuwa yanafaa lakini kwa jinsi unavo yatoa yamejaa Dhiki, kwa hiyo inakua hasara juu ya hasara, Na unajua hayo yote ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu unataka upate(Attention)Kwanini? kwa Sababu pengine mwanzo watu walikua wanakujua kwa sifa fulani na sasa unataka ujulikane kwa sifa ya (Ucha Mungu)hiyo ndio kazi ya Dhiki kwa Jumla, na wewe fanya Uchunguzi utayajua vizuri sana, chunguza Dhiki zako zinatokana na nini, lazima kuna (Source)fulani inayokusababishia hiyo Dhiki.
Jitizame mie mbona hivi nakerwa kazini hamaki zangu namalizia Nyumbani, kwanini upo katika hali kama hiyo, Unakerwa na watu wazima unawakasirikia watoto inakuaje hali hiyo, Sasa jiulize nini kinachokufanya usiwe katika hali ya kawaida alokupangia Mwenye Enzi Mungu wako, Basi ikiwa Mja umo katika hali ya Dhiki elewa unahitaji Dawa, Na Dawa gani utatumia ili Dhiki zikutoke.Endelea Part 3

No comments:

Post a Comment