Sunday, December 1, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(SHAKUR)PART 1

Asalaam Aleiykum,

Hakuna Jina lenye Ibada yenye kumridhisha na Mollah na kumfurahisha Kiumbe kama jina hili la (Shakur)
Mwenye Kushukuru, Ndio Maana hata kwenye ufunguzi wa Sala Unaanza kwa kushukuru(Alhamdulillah)Namshukuru Mollah wa viumbe vyote, Hapana apasae kuabudiwa na kushukuriwa isipokua Mwenye enzi Mungu wa haki. Kila kilichomo katika matendo yako kinastahiki shukran kwa ajili ya Mollah wako, Yeye ndiye aliyekupa Uhai kwa Mapenzi yake, Una nini wewe cha kumlipa isipokua hiyo shukurani ya dhati itokayo kwenye Moyo wako.
Wewe Shukuru kwa wema na Ihsani aliyokufanyia kakupa Afya na Mali, Kakupa Majumba na Magari ushakaa na kuyafikiri hayo halafu ukajaa furaha Moyoni yenye kutambua katika wengi wa viumbe vyake Mollah kanichagua mimi kunipa haya nilonayo, Usipewe hayo basi mengine ambayo unachukulia kwa mzaha kama vile umetoka usingizini mara ngapi unakumbuka umetoa Shukurani kwa kuamka kwako na ukasema(Alhamdulillah).
Jee labda umemaliza kuozesha Mwanao umekumbuka kutoa Shukurani kwa Mollah wako na kusema nakushukuru Mollah wangu kazi yangu ya ulezi ulonipa nimeimaliza salama, Jee siku ulopata hicho cheo umekimbilia Msala peke yako ukamshukuru Mollah wako, usiogope najua umemshukuru (Boss)wako mie nakukumbusha tu Jina la (Shakur).
Sasa una Afya nzuri maradhi yametoweka jee unakumbuka kila wakati kumshukuru Mollah wako, au unasubiri mpaka uanze kuumwa tena ndio uanze (Toba Yarabi), Umekaa peke yako ikakujia kushukuru kwa ajili ya kuumbwa tu kwenye Ulimwengu huu, Ishakujia fikra kuwa hata utakapo kufa basi Mollah wako atakufufua tena akupe Uhai kwa Mapenzi yake, ushawahi kushukuru kwa jambo hilo.
Ushawahi kushukuru kwa ajili ya kupewa Elimu na Akili ya kuyajua mazuri yaliyomo kwenye Ulimwengu huu ukayafurahia. Basi elewa hakuna mwenye kustahiki kushukuriwa kwa haki isipokua Mollah wako aliye Mkarim.Isiwe unasubiri mpaka upate kitu kizuri ndio Ushukuru lazima kila siku iwe siku ya Shukura kutoka kwako kwa ajili ya kupewa kwako maisha haya unayoishi. Mollah wako si mwenye kuhitaji shukurani yako, lakini kila ukishukuru moyo wako unazidi kuelekea kwake Muumba wako na hiyo ndio Ibada kama inavosema aya ya 66 sura ya Zumar,
بَلِ ٱللَّهَ فَٱعۡبُدۡ وَكُن مِّنَ ٱلشَّـٰكِرِينَ 
"Bali Muabudu Mwenye Enzi Mungu na uwe Miongoni mwa wenye kushukuru"
Na ukaendelea kukumbushwa kwenye sura ya Baqarah aya ya 152 inasema:endelea part 2

No comments:

Post a Comment