Sunday, December 15, 2013

TAFAUTI YA RAHA NA FURAHA PART 2

Asalaam Aleiykum,

Nini Raha?
Raha ni Maumbile yako yaloambatana na Roho, Roho ni kitu kisichopenda karaha wala mateso na mfano mkubwa jitizame au mtizame yoyote yule alofikwa na maradhi hali yake inakua vipi, yatizame macho yake uyaone yalivojaa huzuni. Neno Raha limehusiana na (Roho)na Raha ni hicho ulichonacho chenye kukufanya uishi kwenye Ulimwengu huu bila ya Bughudha yoyote, bila ya mateso yoyote, Raha kwa lugha ya kigeni ni hiyo (Blissful) Raha haina kikomo, maisha yako yote ni Raha, ila bado hujayajua, unazaliwa katika Raha ikisha wewe mwenyewe unapanda ngazi huyo unatoka moyoni kuelekea kwenye Akili, unalifata tunda halafu unalitafuna kwa hiyari yako tena kwa mbwembwe, na ukisha kula tunda hapo hapo Raha inakupotea, na si kama imeondoka laa bali unasahau.Raha ni (Nature)yako, kinachotakiwa ufanye kazi ya kuikumbuka tena.
Na sababu kubwa itakayokujulisha kuwa umetoka kwenye Raha na umekwenda kwenye furaha  bila ya kujijua ni pale (Mfano) umemuacha Mke au Mume umekwenda nje kwa (Kimada), ulikua nyumbani umo kwenye Raha mstarehe, unakwenda nje kutafuta furaha, zikisha furaha hizo unakua unazitaka tena,Sababu ni za muda na zishapita,  sasa ushakua (Confused)Furaha imekwisha na Raha huipati, unaanza kutaka kuijaza(Gap)sasa unakua mteja wa kuzitafuta Furaha, labda kwa huyu au kwa yule atakupa furaha, na hiyo ndio sababu kubwa mkaambiwa msikurubie hizo Furaha za nje, unatoka katika (Qadir)ya Mollah wako alokupangia ya Raha unakwenda kwenye uchaguzi wako wewe wa kutafuta Furaha, (Mfano)mwengine upo ofisini unapata Riziki yako kwa urahisi unaacha kazi yako na kuamua kuanza Biashara, Unatoka kwenye Raha unakwenda kwenye furaha, Wewe hayo maisha yako yalivo jione uko kwenye Raha, Unaamka na Afya yako, unakwenda kazini na kucheka na wenzako huna tatizo lolote kabisa mpaka unalala kiumbe wewe hakijakukuta chochote, hakuna Raha kama jambo hilo, unaupata usingizi bila ya vidonge, unakula bila ya matatizo, unahema pasi na maradhi yoyote, umekaa salama usalimini hizo ni Raha za pekee.(Angalia Mfano wa viumbe wenzio kama)Mkulima anavoishi kwenye Raha, hana haja ya TV wala Taa ameridhika na (Nature)yake, sasa jaribu kwenda wewe Shamba, ukiona vijidudu vinameremeta(Vinawaka waka taa)utaanza kupiga kelele (Mbu)wa Shamba wamebeba(Tochi). Mtizame Mchukuzi yoyote yule anafanya kazi yake karidhia uangalie usingizi wake, Tajiri na mapesa yake yote hawezi kuununua, Kila usiku Mkulima au Mchukuzi kwa jinsi anavopendwa na Mollah wake anapewa Mapumziko ya Raha, analala kama (Sultan kwenye Ufalme wa Mwenye Enzi Mungu na akitoka Usingizini anapewa nguvu mpya za siku ya Pili. Watizame watoto bado wako Moyoni hawana habari ya Furaha, ndio maana ukimkera analia akimaliza kasahau, wacha ukerwe wewe ionekane balaa yake, sababu uko kwenye furaha na huwezi kurudi kwenye Raha tena ndio unapanda hamaki, hutaki kusamehe, kumbe sio lile kosa bali ni tafrani zako za kuwa huishi kwenye Raha, Raha kuamka Mollah kakuchangania na Furaha,kwenye Nafsi una Raha, mfukoni una furaha, Kwenye Nafsi umebarikiwa utulivu, kwenye maumbile umepewa sehemu na mahala pa kupumzikia hizo ndio Raha, ikiwa umepewa japo chembe ya mapenzi basi jijue umepewa Raha, Na raha zikizidi ndio utakuta mpenzi (Anaandika barua sasa mimi mwenzio sili wala silali)na hilo ni kweli kabisa unajua kwanini hali wala halali, kwa sababu anaona Raha, keshafika kwenye Roho yake na Roho hailali wala kula,(Kwa hiyo ni kweli halali wala hali)usidhani ni muongo, huyo yuko kwenye Raha, hajali mali wala kufilisika na wewe ukiishi kwenye Raha utakua  mtu wa aina hiyo, utakua huna (Attachment)ya kitu chochote katika Ulimwengu huu, huna habari ya kulimbikiza mali wala kuwa na (Account)ilonona, hutaki majumba wala magari ya kifahari, na unajua jambo moja muhimu kabisa nalo ni (You Belong to no one, and no one Belong to you)ukiwa katika hali kama hiyo wewe unakua uko katika ile njia ya (Balance)Ulimwenguni hupo na Akhera hujafika, hapo ndipo inapoishi Raha, na ukiwepo pahala hapo unakua simwenye kutenda dhanmbi kabisa, unakua Mja wa Huruma, mpole na kazi zako ni za kheri tupu.
Na hapo unaambiwa kwenye sura ya Rumi aya ya 15
فَأَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ فَهُمۡ فِى رَوۡضَةٍ۬ يُحۡبَرُونَ
Wale waloamini na kutenda mema watafurahishwa katika Bustani.
Endelea part 3

No comments:

Post a Comment