Sunday, December 22, 2013

UJUMBE WA MAREHEMU PART 2

Asalaam Aleiykum,

Lazima Mtu atahadhari sana katika Ulimwengu huu, Aangalie vipi anaishi maisha yake, akumbuke kuna masiku mazito mbele yake wala si mchezo, Anaendelea Allamah wetu kutujuza yakwamba mawasiliano yapo ndio maana wakati mwengine mgonjwa akiwa taabani kazimia akija juu anasema nimewaona Bibi na Babu wamekuja nipokea, Anasema Allamah wetu"(Ukiona)au kuota Mtu alokufa anaingia kwenye nyumba basi jua ima maradhi yatakaa kwa muda mrefu au mgonjwa atakufa karibuni, Naam huo ndio Ujumbe wao kwa uchache wanaouleta ili kuwasiliana na wale walo hai.
Na yanaendelea Mawasiliano haya mpaka kwa vitendo vile vile ikiwa umewaachia watoto (Nyumba)za kuuzia ulevi wao wataendeleza, ikiwa umewaachia (Nyumba)za kuja watu (Beach)kustarehe wao wataziendeleza, ikiwa umewaachia mapesa ya Haramu na wao watayatumia kiharamu haramu kama inavotakiwa, lakini ikiwa ulikua Mja mwema utapata mfano huu katika Quraan (Kahf 82)
وَأَمَّا ٱلۡجِدَارُ فَكَانَ لِغُلَـٰمَيۡنِ يَتِيمَيۡنِ فِى ٱلۡمَدِينَةِ وَكَانَ تَحۡتَهُ ۥ كَنزٌ۬ لَّهُمَا وَكَانَ أَبُوهُمَا صَـٰلِحً۬ا فَأَرَادَ رَبُّكَ 
أَن يَبۡلُغَآ أَشُدَّهُمَا وَيَسۡتَخۡرِجَا كَنزَهُمَا رَحۡمَةً۬ مِّن رَّبِّكَ‌ۚ وَمَا فَعَلۡتُهُ ۥ عَنۡ أَمۡرِى‌ۚ
Na Ama (kuhusu)Ukuta, ulikua (kwa)ajili ya watoto wawili mayatima katika mji Ule, Na chini yake kulikuwa na Hazina yao, Na Baba yao alikuwa (Mja)Mwema, kwa hivyo, Mollah wako alitaka wafikie Baleghe yao na wajitolee hazina yao, hiyo ni Rehma inayotoka kwa Mollah wako, Na mie sikuyafanya haya kwa amri yangu.
Naam ukuta umejengwa na Mja mwema, chini ya Ukuta kawacha hazina ya Halali, Nani atakae hifadhi Mali yako ya halali hakuna ila Mollah wako Mlezi, hawezi kukutunzia Hotel zako za Maasi, hawezi kuinusuru Mali yako ya Haramu, hazipiti Rehma zake kabisa, sasa kwanini yakafanyika hayo, sababu huyo Baba(Mzee)alikua Mwema, yeye keshakufa lakini ujumbe wa Rehma ya Mollah wake unaendelea kufanya kazi yake(Shauri yenu na wale wanopita wakakwambieni haifai hata kuwataja)mnapata hasara kubwa, Na hayo hayakufanyika kwa Elimu ya yule Mja alofatana na Nabii Musa a.s bali ni kwa amri ya Mwenye Enzi Mungu, Na hapo ndio tunapoigusa Hadith ilosimuliwa Na Imam Nabhani katika kitabu chake kinachoitwa (Al-Anwar Muhammdiyah).Endelea part 3




No comments:

Post a Comment