Asalaam Aleiykum,
Hakika palikuwepo Msichana wa kiyahudi, yeye alisilimu akaukubali Uislam kwa Ukamilifu na kuukamilisha Uislam wake, Baadae akafa katika Uislam, Alipokufa alikuja Baba yake na Mama yake kwa Bwana Mtume s.a.w wakamwambia Yaa Muhammad s.a.w sisi tunataka kufahamu nini hali ya mtoto wetu Akhera, hivyo kenda Peponi kwa ajili ya Uislam au Kenda Motoni.
Bwana Mtume s.a.w Akamuomba Mwenye enzi Mungu amteremshie (Ilham ya uthibitisho)Akawachuka wazee wale mpaka makaburini, wakasimama kwenye kaburi akaita Bwana Mtume s.a.w "Ewe Fulani Binti Fulani" Ikatoka sauti Kaburini, Naam Ewe Mjumbe wa Mwenye enzi Mungu, Akamuuliza Bwana Mtume s.a.w Ewe Msichana Wajibu wazee wako(Wanataka kujua hali yako)alisema nini wakati yeye yuko kwenye makaazi ya Salama ya (Barzaq)Akajibu yule Msichana Ewe Bwana Mtume s.a.w mimi simjibu Baba yangu wakati yeye bado Yahudi, Akasema Bwana Mtume s.a.w Kwanini? akajibu yule Msichana mimi nimemkuta Mollah wangu Bora kuliko baba yangu.
(Ewe Mollah wangu nilipogundua mimi katika Moyo wangu anakaa asiyekua wewe, basi nilifanya hima kuujaza uongofu wako, hata ikawa hakai asiyekua wewe) Nimemkuta Mollah wangu ana kheri zisomfano, Palepale wale wazee wakasema "Ewe Muhammad s.a.w Tunashuhudia Mwenye enzi Mungu ni mmoja na wewe ni mjumbe wake wa haki.
Naam nini hali yetu sisi tulosahau Dini yetu na wazee wetu wema walotangulia, inapaswa tuombe Dua hii "Ewe Mwenye kugeuza nyoyo, Zigeuze nyoyo zetu zisadikishe Dini yako"
Kasema Bwana Mtume s.a.w "Enyi watu Msiwahuzunishe Maiti zenu kwa matendo Mabaya" kwani Maiti ni wenye kutambua maasi ya walio hai. Ukenda kuzini au kudhulumu yeye anatetemeka huko aliko(Barzqh) mpaka Roho wenzie wanamuuliza vipi mbona hivyo, Anajibu alo wangu anakwenda kwenye maasi na akija kunyakuliwa Roho yake pale alipo kabla ya kutubu, mnajua kitamkuta nini?
(Al-Qariah-aya ya 10-11."وَمَآ أَدۡرَٮٰكَ مَا هِيَهۡ "
Ni nini kitakujulisha hiyo Haawiya,
"نَارٌ حَامِيَةُۢ"
"Ni Moto uwakao kwa ukali(Sana)" Ndio usiku unaota unasema "jana nimemuota Mama yuko pembeni mnyonge", asiwe mnyonge na kayaona Manyago yote, na yeye hana njia ya kukukataza ila anakujia kwa ishara ewe Mwanangu acha, basi tena umezama sana, Na ikiwa yeye ndiye mwenye matatizo atakujia na ishara chungu nzima za kukuonesha nitumie dua Mwanangu, niombee japo kidogo, na kama huzifahamu anaambiwa kiwapi, kama ulivo ishi wewe na yeye anaishi hivyo hivyo, basi wafanyieni Ihsani Maiti zenu kwa kuwakumbuka kwa dua japo mwaka mara moja, msiwatupe kabisa kabisa ikawa kama hawakupita katika Ulimwengu huu. Tizama mfano Mti wa Mbuyu au Nyumba ipo mwaka wa mia unaiona, vipi Maiti yako leo imekufa mwaka wa pili tu unaisahau. Wakumbukeni walo wenu na waso wenu kwa Dua, Na Mollah wenu atakukumbukeni kwa Rehma zake.
No comments:
Post a Comment