Asalaam Aleiykum,
Binaadamu yanatupata matatizo makubwa pale tunaposhindwa kutafautisha Baina ya Matatizo na Dhiki, Matatizo ni kitu cha nje, Matatizo ni majambo katika mambo ya Maisha, Lakini Dhiki ni yenye kuishi kwenye hiyo (Roho) yako, Na kaa ukijua mwenye Dhiki hana Raha ya Maisha, Ujaji wa Dhiki unakuja mfano uleule wa Matatizo, kama, yaweza kuwa Una Dhiki ya Mapenzi, au Dhiki ya utafutaji wako wa Riziki, mbona mambo hayendi, unaweza kuwa na Dhiki ya Moyo mambo yamekujaa na hujui utayatoa vipi, unaogopa kumhadithia mtu, kumbuka hayo yote yamo ndani ya (Nafsi) yako.
Sasa itabidi ujiulize ilikuaje hata ukafikia hali kama hiyo, huna haja ya Hadith wala kisa cha zamani eti ndio yakujulishe vipi umefika hapo, huna haja ya kwenda kwa Mmasai au kwa (Babu) ili upatiwe Dawa, kumbuka Dawa unayo mwenyewe, na kazi yangu mimi ni kukumbusha umeiweka wapi hiyo Dawa, ufanye nini utoke kwenye Dhiki, lakini utatokaje kabla ya kujua njia?
Ipi njia yenyewe, ni hiyo ya kuijua Dhiki ukaweza kuitafautisha na matatizo. Nini matatizo? Matatizo yanakuja kwa Kutamani, ikawa hichi unataka na kile unakitaka, unakua na (Ambitions) za kila aina, hivyo ndio kujitia kwenye matatizo. Nini Dhiki? Dhiki ni kuhitaji(Mahitaji)Unahitaji Raha, Unahitaji (Blissful life) Unahitaji Ku(Surrender)unahitaji utulivu, unahitaji (Normality)au tuite (Balance). kwanini sasa mambo yako yameharibika mpaka umefikia unaishi ndani ya Dhiki? sababu ziko na wewe mwenyewe ndiye muanzilishi, wewe ndie mtengenezaji wa hiyo Dhiki, na kabla hatujenda mbali wacha nikukumbushe kitu labda huwenda ukajua ama kweli Dhiki nimejitakia mwenyewe. Wacha nikujulishe Sheria ilopangwa na Mwenyewe aliyeumba Ulimwengu, Anasemaje kupitia Kwa Mja wake alompa Hekima Luqman a.s (Sura ya Luqman aya ya 16.
يَـٰبُنَىَّ إِنَّہَآ إِن تَكُ مِثۡقَالَ حَبَّةٍ۬ مِّنۡ خَرۡدَلٍ۬ فَتَكُن فِى صَخۡرَةٍ أَوۡ فِى ٱلسَّمَـٰوَٲتِ أَوۡ فِى ٱلۡأَرۡضِ يَأۡتِ بِہَا ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَطِيفٌ خَبِيرٌ۬
"Ewe Mwanangu Kwa hakika jambo lolote (Japo)liwe na uzito wa(Atom)chembe ya Hardali, likawa(Limetendeka au kufichwa)ndani ya Jabali au Mbinguni au Katika Ardhi, Mwenye Enzi Mungu atalileta (Na Kumlipa aliyelitenda),Hakika Mwenye Enzi Mungu ni Mwenye kujua (mambo) yalofichikana na (Mambo)yalodhahiri".
Kaanza kupewa Onyo mtoto sababu bado hajaingia kwenye Dhiki, Bado hajalimbikiza mali au mambo ya kidunia anaambiwa kaa ukijua chochote kile utendacho lazima ulipwe, na hiyo ndio sheria ya Mwenye Enzi Mungu lazima itekelezwe. Sasa vipi wewe umefikia katika hali hiyo ya Dhiki? Endelea part 2
No comments:
Post a Comment