Sunday, December 22, 2013

UJUMBE WA MAREHEMU PART 1

Asalaam Aleiykum,

Nani Marehemu?
Yoyote yule alotangulia mbele ya haki ndiye Marehemu, Na yule Alobaki katika Ulimwengu huu mimi na wewe tunoishi kwa hivi sasa sisi sote ni (Rahima) wenye Rehma. Na wale walotangulia ni wenye Kurehemewa, na hilo ndio lililotufanya sisi kumwita alotangulia Akhera ni Marehemu.
Mwanaadamu yaweza kuwa una Baba au Mama katangulia kwa Mollah wake, Iwe Dada au kaka yako, awe Mwanao au ndugu yako, na iwe Rafiki ili kuipima Dini yako wakati huu ulonao, kujua kama unazo fikra za Akhera basi inapasa kujiuliza mara ngapi  kwa siku au miezi  unawakumbuka walo wako, Jiulize jee wanatakiwa kukumbukwa? Nafahamu uzuri unajitahidi kusoma magazeti hayakupiti, vitabu vya historia umevihifadhi wewe, unakumbuka mambo ya zamani, Mababa wa Taifa unawakumbuka wewe, unakumbuka waanzilishi wa chama chako, unamkumbuka mwanasayansi fulani, lakini ni mwiko kwako kuwakumbuka walio karibu na wewe kwa dua ya maombezi, jua hao kuna  mahusiano ya mazazi juu yako.
Vipi wewe huwakumbuki wale wenye ukuruba wa kidamu juu yako, kumbuka mara ya mwisho lini umempelekea Rehma za Dua, kwa sababu huko kuzungumza kwako ni Rehma, na ukipeleka maombi basi unakua umepeleka Rehma(Mfano)wa(Recycle). Usije kubisha unajua umekata mawasiliano miaka mingi ilopita, Imekusahaulisha nafsi yako na kuamini yule mtu keshaoza kaburini, Na wala hahitaji kukumbukwa, kitu kimoja nakukumbusha kilicho kufa na kuzikwa ni kiwiliwili chake tu, lakini Roho yake iko hai kwenye Ufalme wa Mwenye enzi Mungu, Na hufurahi Roho hiyo ikiwa utaikumbuka kwa kuitakia (Msamaha au kuiombea Makaazi mema). Na zile Roho ziloishi na kupita kwenye Ulimwengu huu kwa kujisalimisha kwa Mollah wao basi nazo hupewa Radhi za Mollah wao na kupata fursa ya kuwasiliana na walio karibu nao katika mahusiano ya Kiroho.
Na wale ambao wamepita katika Ulimwengu huu wakafanya Shari za kupindukia na wao pia hupewa nafasi za kuwaonesha walo wao mambo yanayo wakuta huko walipo ili wawakumbushe jamani wee huku kumoto, tutupieni Dua japo siku kati ya masiku. Sasa vipi mawasiliano haya yanafanyika, Vipi wanatuma ujumbe huo ili ikufike wewe msomaji, kwa kutaka tujue kama kweli (Communication)inafanyika wacha tumuulize Allamah Muhammad bin Sireen R.A atueleze kuhusu kadhia hii "Anasema yapo mawasiliano baina ya waliyo hai na walio kufa""Na chochote kile anacho kufahamisha maiti kwenye (Ndoto)basi ujue ni cha ukweli, sababu wao wako mbele ya haki na hawasemi uongo.
Kwa hiyo Ukimuona Maiti yako anakwambia "Ewe Mwanangu au Rafiki yangu huku mwenzio makwaju ya fimbo za moto yamenizidi au minyororo ya shaba za moto zinaniumiza, au chumba hichi cha moshi mzito sikiwezi kinaniadhibu sana basi jua maiti yako hiyo inahitaji dua zako, ndio maana ya kukuhadithia mambo hayo, sio kama anakutisha, fanya haraka umpelekee dua zako, muombee kwa Mollah wako asaa huwenda akapata shufaa, usisubiri mtu akakwambia inafaa au haifai, wewe peleka usiweke wakili baina yako na Mollah wako, alipokuumba hakuwepo yoyote kwanini sasa hivi azuke mtu kukufundisha wakati gani wa kuwasiliana na Mollah wako, Pengine huyo Maiti kaomba nipeni nafasi labda fulani, huwenda mwanangu fulani yeye kashika Ibada huwenda nikaipata shufaa, asaa Mollah wangu aweza kukubali maombi yake, nipeni nafasi, kule anapewa nafasi wewe huku unashangilia pengine mpira au harusi mambo hayo sasa. Endelea part 2

No comments:

Post a Comment