Sunday, December 1, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(SHAKUR)PART 2

Asalaam Aleiykum,

فَٱذۡكُرُونِىٓ أَذۡكُرۡكُمۡ وَٱشۡڪُرُواْ لِى وَلَا تَكۡفُرُونِ 
"Basi nikumbukeni,(Namie)Nitakukumbukeni, Na Mnishukuru wala msinikufuru"
Ukianza kulitumia jina la (Shakur) au mengine yote unakua unafanya vitendo viwili kwa wakati mmoja kwanza unakumbuka halafu unatumia maana ya hilo neno, kwa hiyo nikumbukeni, nani umkumbuke Mollah wako, nini ukumbuke (Ya Shakur) uwe mwenye kutoa shukurani, Nini kitatokea na yeye atakukumbuka na hakuna fadhila ilo bora, raha isokwisha kama kukumbukwa na Mollah wako.
Yeye Mollah wetu ni mwenye kutukumbuka kwa mapenzi yake, basi anastahiki Shukurani zetu hususan tukikumbuka pale ndugu na jamaa wakishakukufikia ardhini wewe unabaki na nani? Mshukuru Mollah wako yeye ndiye (Shakur). Mshukuru Mollah wako aliyekupa uwezo wa kufikiri, kuona kusikia, na kuzungumza, yeye yuko pamoja na wewe kila wakati kwa hiyo wajibu wako kumshukuru.
Mshukuru yule ambaye bila ya kunyoosha mikono anakupa kila zawadi katika Ulimwengu huu, kuanzia chakula, afya, pumzi na kila kitu, huyo ndiye anayestahiki kushukuriwa na kila kiumbe, kaa kila wakati ukikumbuka fadhila zake kwako zisizokua na kipimo basi kila ukikaa kumbuka yuko alokuumba na anastahiki kushukuriwa.
Na ukitumia Jina hili la (Shakur) litakupeleka kumjua Mollah wako kwa undani zaidi, na furaha ilioje kumjua Mollah wako kupitia sifa hii ya Shukurani.

No comments:

Post a Comment