Sunday, December 15, 2013

TAFAUTI YA RAHA NA FURAHA PART 3

Asalaam Aleiykum,

Kuamini kuko moyoni, kuamini ni Raha katika mamlaka yake, ndio maana utaona mtu atachukua kila kilicho chako lakini hawezi kuchukua Imani yako, kuamini ni Raha, ndio utakuta mtu yuko tayari kufa kwa Imani yake, Raha ilioje anauliwa kakamata kamba ya Mwenye Enzi Mungu, ndio maana unamuona mwenye Imani ya kweli anakua ni mwenye kutenda mema, anakua mwenye huruma, anakua mpole, ana mapenzi matupu, ni mwenye kusaidia wenzie na anayafanya hayo yote kwa kuona Raha kwa ajili ya Mwenye enzi Mungu wake, basi hao kabla hata ya kufunga Macho wanafunguliwa pazia na kuwaonesha furaha zinazo wasubiri huko wendako, kwa sababu wao kuishi kwao kote katika Ulimwengu huu walikua wameitambua Raha kwa njia ya siri, wakaridhi (Qadara)ya Mollah wao, wakaamua kumtii Mollah wao na kuyafata aliyoamrisha, ikawa wao wakiumwa au wakiwa wazima wanamkumbuka Mollah wao, wakilala au wakiamka wako karibu na Mollah wao, na kuwa karibu ya Mollah wako ni kuzipata Raha zisizo mfano, na kuwa karibu ya Shetani unapata furaha yake lakini ni yenye madhila makubwa, yenye shida kubwa, basi ukitaka kugundua hilo wewe endelea na (Picnic)zako, ukiamka furaha imetoweka, piga mtindi ukiamka unaumwa, nenda (Shopping)ukirudi umenuna pesa zishakwisha, cheza ngoma ukiamka magoti yanachemka, Imba usiku kucha , ukiamka sauti haipo tena, jaribu kufanya utafiti uyajue yepi ya furaha za muda mfupi, na yepi yenye Raha za kudumu ili uyakamate, ukihangaisha Akili yako utayajua hayo moja baada ya jengine, kumbuka Furaha ni ya Muda Mfupi, na Raha ni yenye kudumu.Uchaguzi unao wewe.

No comments:

Post a Comment