Sunday, December 8, 2013

HAKUNA SHEIKH-A-KAMA WEWE PART 2

Asalaam Aleiykum,

Al-Hujurat (13) يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّاسُ إِنَّا خَلَقۡنَـٰكُم مِّن ذَكَرٍ۬ وَأُنثَىٰ وَجَعَلۡنَـٰكُمۡ شُعُوبً۬ا وَقَبَآٮِٕلَ لِتَعَارَفُوٓاْ‌ۚ إِنَّ أَڪۡرَمَكُمۡ عِندَ ٱللَّهِ أَتۡقَٮٰكُمۡ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ۬ 
"Enyi Watu hakika tumekuumbeni Wanaume na Wanawake na tumekufanyeni Mataifa na Makabila(Mbali mbali)ili (Mpate)mjuane(Tu)Hakika ahishimiwaye sana(Mwenye cheo na daraja)miongoni mwenu mbele ya Mwenye enzi Mungu ni yule amchaye Mungu zaidi katika nyinyi,(Mwenye mapenzi na Mollah wake) Hakika Mwenye enzi Mungu ni mjuzi, na Mwenye habari."
Huna haja ya kujifanya fanya wewe una msimamo au ndio uko katika usawa, Mollah wako anajua kila kitu anazo habari zote mpaka katika kifua chako kuna kitu gani, huna haja ya kudanganya, wala usimwachie mtu akakudanganya kukwambia wewe ndio pekee unafanya sawa wengine wote sio sawa, kazi hiyo mwachie Mollah wako ndie atakae ifanyia uamuzi, unachotakiwa wewe uombe Imani ikujae kwenye nafsi yako, na Imani ikikujaa unakua huyumbi, unakua ushaupata ukweli, Na ukiujua ukweli hutaki tena kushikiwa Dini yako, unakua hutaki Sheikh yoyote, au mjanja yoyote wa maneno akusogelee, Bali wewe mwenyewe unageuka kuwa huo ukweli, na kila unapokuwepo unauwakilisha huo ukweli, na ukweli wenyewe ni huo Uislam na matendo yake.
Basi Mwenye kuujua ukweli ndio anaambiwa "Enyi Watu" tumekuumbeni Wanaume na Wanawake katika tafauti ya Maumbile tu, lakini katika jumuiko la (Roho)nyote sawa,  Tafauti yenu katika maumbile ambayo yana dhumuni maalum, ama katika mambo ya Nje Mwanamme yeye ndie Mwenye dhamana, na kuhusu mambo ya ndani Mwanamke anachukua madaraka kamili, kama Mwanamme anapigana vita ya Mpakani, Mwanamke anapigana vita ya Moyoni ambayo ndio nzito zaidi kuliko ya mpakani, Mpakani ukipigwa risasi kazi yako imekwisha, lakini ya moyoni kifo chake ni taratibu, machungu yake ni ya muda mrefu, ndio maana utakuta Mwanamke mstahamilivu anabeba mimba na huku mtoto anaumbwa ndani ya tumbo lake kwa muda wa miezi tisa, yote hayo Wanaume tunayajua na ukipata kuyajua hayo basi utafahamu kuwa sisi sote ni viumbe na inapaswa kuheshimiana.
Tukakujaalieni Mataifa na Makabila na hilo kama Muumin unalifahamu ni kwa ajili ya kujuana tu. 
 Kujuana(Knowing) Ipo kwenye Akili, na Akili ni nyenzo ya kutumika kwa mahitaji ya kuishi siku hadi siku, Lakini kipo cha zaidi ambacho kitu hicho nyote mnakutana kwenye (Level)moja, hakuna huyu Mweupe huyu Mweusi, huyu kabila fulani yule kabila hili, huyu ana cheo hichi yule ana utajiri huu, katika (Level) hiyo Muumin wa kweli ambaye kaamini kwa dhati huondosha Kiburi chake, anafahamu pahala hapa niache jeuri zangu, pahala hapa mimi si chochote,pahala hapa niwache kuwadanganya wenzangu, pahala hapa mimi sina madaraka yoyote  ya kumjua nani mwema na nani mbaya, Nani kashika dini na yupi kaichia, Na pahala hapo ndio sote tunapokutana kwenye Mamlaka ya (Kiroho)Na Mfano midogo ipo (Angalia sote tunakula uwe tajiri au maskini, sote tunavuta pumzi, sote tunalala, sote tunaongea, sote tunacheka, sote tunatembea, sote tuna ndoto zetu, sote tunaona na kusikia, sote tuna majina na mengi mengineyo)basi haikujii fikira ewe Mwanaadamu kwamba kuna pahala tunakutana, na pahala hapo ndipo pekee penye Mamlaka ya kujua kwamba kiumbe anatenda kheri au shari, nani mwenye msimamo na yupi hana, Sala yake inakubaliwa au haikubaliwi, dua yake imefika au haijafika, kwa hiyo asizuke mtu akakupeni habari yeye ni mwenye kujua dua au anajua njia za kukupeleka peponi, au yeye yupo kwenye kabila fulani au kikundi fulani ambacho ndicho kinakubalika hakuna kitu kama hicho kabisa, ndio maana aya ikasema dhumuni lake la huo Utaifa na ukabila ni kujuana tu, na wala halina kazi nyengine.
Endelea part 3



No comments:

Post a Comment