Thursday, November 1, 2012

SHAIRI LA MCHA MUNGU-PART-2

Asalaam Aleiykum,

Uamsho huu wa ndani au wa aina ya pili unatokana na Mollah wako, na Mtu au watu wakisha amshwa na Mollah wao inakua tabu tena kuwalaza hata ukitumia nguvu ukali hawalali tena, sababu wanakua washajua na siri ya kujua inakaa moyoni, ndio maana Mcha Mungu akautaja Moyo, na hakitajwi kitu chenye uzito kama moyo kikawa kitu cha upuuzi, lazima kuna faida kubwa kwa watakao kujua. Kwa fahamu zetu za haraka haraka tunafahamishwa moyo ni (Pump)inayo sukuma damu, ikisha tunaishia hapo hatutaki kwenda zaidi tukajua jee Moyo una siri gani kwetu sisi wanaadamu?.
Yapo mambo mengi yano pitikana katika Moyo ambayo wengi wetu hatuna habari nayo, Mcha Mungu aliposema "nilipogundua katika Moyo wangu anaweza kukaa asiye kuwa wewe" Haya ni maneno yalobeba siri kubwa ndani yake, na siri hii ina anza wiki tatu tu unapoanza kuumbwa katika(Umbo la kuonekana)mimba ikingia baada ya wiki tatu mpaka tano mapigo ya chombo hichi tayari yameshaanza kusikika na ambayo yataendelea mpaka mwisho wa umri(maisha)yako.
Kwa mtazamo wa nje moyo ni (Pump)inayosukuma damu, lakini kwa mtazamo wa Mcha Mungu anajua kuwa Moyo una kazi nyengine lakini mpaka uzinduke au upate(Uamsho)ndio unakutana  na hiyo siri ya utendaji wa kazi nyengine, na ukigundua siri hiyo ndio unakua, umefanikiwa, ushavuka na daima unakua Mcha Mungu lakini lazima siri hii akufunulie pazia Mollah mwenyewe na hapo inakua tabu tena kwa wewe kurejea katika ulimwengu wa maasi, shida za kidunia. Inakuaje chombo hichi chenye kudumu na sisi mpaka mwisho wa uhai wetu na hizo kazi za siri? Na siri gani alogundua Mcha Mungu hata akautaja Moyo?Wanasema wanasayansi kitu cha mwanzo kufanya kazi katika huo Moyo kinaitwa(Sino-Node)au(Electric-Conduction-System)huo ndio Moyo kitaaluma tunaishia hapo (Pump)inafanya kazi.
Lakini Mcha Mungu kakataa kuishia hapo, kaamua kwenda mbele zaidi kidogo ndio (akagundua kwenye moyo kuna nafasi ikiwa hakua makini nafasi hiyo yaweza kukaliwa na asiye kuwa Mollah wake, kuna wengine watashangaa mbona sasa anazungumza mambo mapya, mbona haya mageni, vipi moyo ukawa na kazi nyengine, naam hiyo ni kawaida walishangaa wenye kushangaa pale walipoambiwa maji ni (Gas)mbili na (formula)yake ni (HO2)lakini mshangao unakuja hapa, Mbona gas hizi mbili zipo lakini hazigeuki maji, Siri yake lazima ipatikane kitu cha tatu nayo hiyo (Elecricity)ndio kifanye hayo maji, Mcha Mungu yeye kaita (Rehma)Quraan-Anbiya-"وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَىۡءٍ حَىٍّ‌ۖ أَفَلَا يُؤۡمِنُونَ "
"Tukajaalia maji (Kwa)kila kilicho hai(Tulichokiumba), Jee hawaamini".
Naam hiyo iliyomo kwenye Moyo na kwenye maji lazima ipatikane sasa mnaulizwa jee hamuamini?, Kuwa mstahamilivu tuko tunamfata Mcha Mungu na maneno yake, usije ukahadaika na maneno ya Mcha Mungu ukaja kukwama kwenye maneno, bali chukua ujumbe uliomo kwenye maneno haya,"Nilipogundua katika huu Moyo wangu kwamba anaweza kukaa asiye kuwa wewe"jee unataka kujua undani wa maneno haya basi endelea-part-3




1 comment:

  1. Alhamdullillah twafaidika kwa nasiha zako,Allah akupe taufiq upanue uwanja huu wafaidike wengi.

    ReplyDelete