Sunday, June 30, 2013

HASARA YA VUNJA JUNGU PART 1

Asalaam Aleiykum,

Unamjua anayepata hasara bila ya kujijua? yule Mwenye kujiita Muumin halafu unapokaribia Mwezi Mtukufu wa Ramadhan anaukaribisha kwa (Party na Picnic). Huyo anafanya Sherehe za kumuaga Rafiki yake (Shetani)na kumpa ahadi nisubiri Yaumu shaka tutakutana tena bila ya wasiwasi, Huku Mwenye enzi Mungu anawaita waja wake kwa Mapenzi akisema "Ewe kiumbe wangu wee" njoo ukiwa msafi, anza kujisafisha, njoo ukiwa (Tohara) ili uzifanye hizi siku chache ziwe za utiifu kwa ajili yangu, uje ufanye mambo ya (Taqwa), Wewe Unamjibu ngoja nijichafue zaidi, nipe muda nitie Najis katika Kiwiliwili changu, Niwache nije kwako huku nina kumbukumbu za Rafiki yangu Shetani, mimi katika huo mwezi wako Nakuja Shingo upande, ndio imenibidi tu sababu watu wote wananijua mimi Muislam, lakini kwa uhakika mapenzi yangu yote yapo kwa Shetani na hiyo miezi kumi na mmoja ilobaki, Najua Mollah wangu wewe umenipa Uhai, ikisha Wewe ndio Unanipa Riziki na kila kitu ninacho hitaji lakini mie niache sijiwezi kwa shughuli za (Vunja Jungu).
Enyi "Wanaadamu" hususan nyinyi Waumin hamjikumbushi wakati mtakapo ulizwa kwani hamkusoma Quraan sura ya Yaasin aya ya 60,

"أَلَمۡ أَعۡهَدۡ إِلَيۡكُمۡ يَـٰبَنِىٓ ءَادَمَ أَن لَّا تَعۡبُدُواْ ٱلشَّيۡطَـٰنَ‌ۖ إِنَّهُ ۥ لَكُمۡ عَدُوٌّ۬ مُّبِينٌ۬"
Jee sikukuagizeni Enyi Wanaadamu kuwa msimuabudu Shetani, Hakika yeye ni adui aliye dhahiri(Wazi)kwenu.
Na mmekua hamtaki kusikia ila lazima mvunje Jungu, lazima msondo upigwe, tena kuna watu ikikolea wanasema bila ya kulewa ntaichezaje, (Maskini)hawa hawajalewa wako hali hiyo, nini taarifa zetu tunazopokea yanofanyika katika hilo Vunja Jungu. Hakuna hadith za huko isipokua Maasi, halafu huku unasema unajiandaa kufanya (Taqwa) lakini kwa kupitia njia ya Maasi, Iwapi Ramadhan yako wewe mvunja Jungu, Hana Ramadhan yoyote yule mwenye kufanya maasi katika hili kumi la mwisho la Shaaban(sababu zake utakutana nazo huko mbele). Mfano wa kwanza kabisa kitizame chakula kinavofanya kazi kwenye (System)ya (Tumbo)lako kwanza kinakaa siku nzima kwenye (Utumbo) halafu kinachujwa na (Parcent)kubwa inakwenda kwenye Akili, na bado hujui kwenye Akili kinakaa muda gani, Sasa jiulize Pombe nayo inakaa muda gani, pia kumbuka kuna muda wa vitu kukaa katika hiyo (Body System)yako, kuna vya siku saba na vyengine kumi na nne, na vyengine mpaka siku arobaini havitoki katika kiwiliwili chako, vipi leo Mvunja Jungu useme unaipata Ramadhan.
Huna Ramadhan kwa kunywa Pombe kesho Ramadhan, Huna Ramadhan kwa kunuwiya kula haramu kwa kuwapandishia Waumin bei za Chakula, huna Ramadhan kwa kucheza viuno kwenye Taraab au kutembea Uchi nk, vipi wewe utaipata Ramadhan. Endelea Part 2

1 comment:

  1. Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.

    Mume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
    Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
    Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.

    Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
    Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na kufanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
    Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
    Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
    Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
    Nitaendelea kushukuru milele.
    Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi ili kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
    . Usaidizi wa kurejesha ndoa
    . Tamaduni za ujauzito ili kupata mimba
    . Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
    . Mwongozo na ulinzi wa kiroho
    . kutokuwa na uhakika wa ubaba au ubaba usio na sifa

    Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159

    dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete