Asalaam Aleiykum
Mie mpenzi sana wa Lugha ya Kiswahili, Lugha ambayo imekusanya maneno kutoka lugha nyingi tafauti na kujiunda lugha moja ya Kiswahili, ndani yake kimo Kihindi, Kiengereza,Kireno,Kiarabu,Kiafrica na lugha nyengine kadhaa, Ndani ya Lugha hii kuna misemo mingi ilo jaa hekima, Mie leo nimechagua msemo ulokua unapendwa na wazee usemao,"Asofunzwa na Mamae hufunzwa na Ulimwengu".
Hapa yametumika maneno yenye thamani kubwa, Maneno ambayo yanaishinda almasi, ukiyazingatia maneno haya utagundua hayajatokea kwenye Akili, Wapi yametokea? hilo ndio dhumuni ya darsa yetu leo.
Nina Tabia niendapo likizo Nyumbani Africa hupendelea kujumuika na vijana kwenye vikao vya kahawa, siku moja wakati tumekaa alipita kijana mmoja maskin anacheka na kuzungumza peke yake, Vijana nilokaa nao wakanambia yakua kijana Mwenzao kapoteza saa, Mimi nikawajibu basi tumsaidie kutafuta, wale walokuwepo pale walicheka sana, Mimi nilifahamu yule kijana ni mgonjwa wa Akili, wao wakanifahamu mimi ni mjinga wa Lugha, na sifahamu chochote, lakini ndani ya Nafsi yangu nilikua nawaangalia jee wale waliopo pale wamefunzwa na Ulimwengu, nikagundua wamesema maneno makubwa lakini hawajui maana yake, kama vile kusema Kiarabu ukawa hujui tafsiri yake.
Sasa mimi leo Nakuchukua katika Safari hii ya "Miujiza Nje ya Akili" ili upate kufahamu kwa uzuri inakuaje ukipoteza saa. nje ya Akili inakuje,Watoto wa Nabii Adam a.s Habil na Kabil Mmoja wao alipomuua mwenzie akabakia kakamata saa hajui afanyeje, Ulimwengu ulimfunza vipi?
فَبَعَثَ ٱللَّهُ غُرَابً۬ا يَبۡحَثُ فِى ٱلۡأَرۡضِ لِيُرِيَهُ ۥ كَيۡفَ يُوَٲرِى سَوۡءَةَ أَخِيهِۚ قَالَ يَـٰوَيۡلَتَىٰٓ أَعَجَزۡتُ أَنۡ أَكُونَ مِثۡلَ هَـٰذَا ٱلۡغُرَابِ فَأُوَٲرِىَ سَوۡءَةَ أَخِىۖ فَأَصۡبَحَ مِنَ ٱلنَّـٰدِمِينَ (٣١)
Hapo Mwenye enzi Mungu akamleta kunguru anayefukua katika Ardhi ili amuonyeshe jinsi ya kuificha maiti ya ndugu yake, (Akasema yule Ndugu aliyeua) ole wangu nimeshindwa kuwa sawa na kunguru huyu na kuficha maiti ya ndugu yangu, basi akawa miongoni mwa wenye kujuta.
Kwanini akajuta?, kwa sababu Kunguru kaja na hekima, yeye akasoma kupitia kwa Kunguru, Basi kujuta kwake ni kule kumdhulumu ndugu yake na kushindwa kuuhifadhi Mwili wa ndugu yake.
Nimekupa aya hii moja ili iwe muongozo wa darsa yetu, yule ndugu aliyeua ilipomponyoka saa alishuhudia kitendo cha mshangao, Kutokana na amri ya Mwenye enzi Mungu kaletwa kunguru kwa njia ya Hekima ili amuoneshe vipi kuustiri maiti ya ndugu yake. Asofunzwa na Mamae hufunzwa na Ulimwengu.
Saa ilokusudiwa hapo ni hiyo Akili(Mind), Napenda uelewe mambo yote yanotokea katika Akili yanahitaji muda, ndio hiyo saa au ita (Time) ukijumlisha ndio unapata siku, pahala, jana na kesho, hiyo ndio (Time) au (Memory) ukiyapoteza au ukitoka katika (system) hiyo ndio huko kupoteza saa.
Na huko kupoteza saa kupo kwa aina mbili, aina ya kwanza ni ile ya kupoteza Fahamu, ugonjwa wa Akili, (Drugs) N.k, Na aina ya Pili ndio hio Miujiza una (Function)au unaingia kwenye (Eternity)au (Wisdom). (Mfano) ukilala unapoteza saa hujijui, lakini wakati wa kufa unapoteza saa unajijua.
Endelea part 2 uingie kwenye Ulimwengu wa Hekima.
endelea part 2
Friday, December 2, 2016
MIUJIZA NJE YA AKILI PART 2
Asalaam Aleiykum
Naam, Mtoto yumo kwenye hiyo (Hekima)(Wisdom)Lakini hajijui ndio maana hata Kwenye Quraan lilipotajwa jambo la (Hekima) Luqman alimuanza nani? isome Quraan uone vipi inakua kupoteza saa, vipi unajua tafauti ya saa na (Hekima). Anasemaje Mollah wako? Luqman aya ya 12 mpaka 13 na kuendelea. Zama kwenye maneno hayo ujue hekima inatokea wapi.
وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا لُقۡمَـٰنَ ٱلۡحِكۡمَةَ أَنِ ٱشۡكُرۡ لِلَّهِۚ وَمَن يَشۡڪُرۡ فَإِنَّمَا يَشۡكُرُ لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَنِىٌّ حَمِيدٌ۬
Kwa yakini tulimpa Luqman Hekima(Wisdom), Tukamwambia Mshukuru Mwenye Enzi Mungu, Na atakaeshukuru kwa yakini anashukuru kwa ajili ya Nafsi yake, Na atakae kufuru Mwenye enzi Mungu(Amejitosheleza)Mkwasi asifiwaye, (Si Mwenye kuhitaji shukurani zenu)
Nini (Wisdom)au Hekima? Ni hali au uwezo wa kumiliki Nafsi yako nje ya Akili, au kwa lugha nyengine ni mkusanyiko wa ufahamu mambo yalopita na yajayo ukawa unaishi nayo sasa hivi, hiyo ndio tafsiri ya Rahisi ya hilo jambo la (hekima)lakini hata halijafikia ukaribu wake na kusudio ya hiyo hali ya kuwa na (Hekima).
Anasemaje Luqman? Tulimpa Luqman Hekima, tukamwambia Mshukuru Mollah wako, kwanini ashukuru, kwa sababu kitu hicho ni kitu (Adhimu)ni (State of Knowing),Hiyo ndio Hekima, Binaadamu ukijijua basi unashukuru kwa kupewa neema na rehma hiyo, Mnyama ana lala na wewe unalala, halafu nyote mnaamka, lakini kuna mmoja anajijua kaamka, na huyo ni wewe, Shukuru kwa Neema hiyo ya kuumbwa Mwanaadamu na ukapewa cheo cha kujijua, Shukuru kwa Nafsi yako uko mzima, unavuta pumzi bila ya taabu, unatembea na kurudi bila ya shida, unapata riziki yako kama ilivopangwa, shukuru kwa ajili ya Nafsi yako, na kama hutaki hilo au kumshukuru Mollah wako, Yeye hana (haja na shukuruni yako), endelea kumkanusha, kumpinga na kumuasi na yeye atakunyima miujiza hii nje ya Akili.
Naam sasa toka kwenye saa uingie kwenye miujiza wa (Hekima) za (Luqman), Hekima inakuja kwa njia ya kusubiri, katika Ulimwengu wa sasa Binaadamu kasoma sana, lakini kwa kufanya hivyo kapoteza (Hekima), kwa sababu ya haraka za maisha, ndio maana (Luqman)akaona aanze kwa Kumtahadharisha Mwanawe, kwa sababu (Asiye funzwa na mamae hufunzwa na Ulimwengu).
وَإِذۡ قَالَ لُقۡمَـٰنُ لِٱبۡنِهِۦ وَهُوَ يَعِظُهُ ۥ يَـٰبُنَىَّ لَا تُشۡرِكۡ بِٱللَّهِۖ إِنَّ ٱلشِّرۡكَ لَظُلۡمٌ عَظِيمٌ۬
Na(Wakumbushe)Luqman alipomwambia Mwanawe na hali yakuwa anampa nasiha, Ewe Mwanangu usimshirikishe Mwenye Enzi Mungu, Maana kushirikisha ndiyo dhulma kubwa.
Hapo kuna tafauti kubwa baina ya Baba na mtoto, tafauti yenyewe mwenye hekima hawezi kukupa hekima yake, ila ikitoka kwake inakua nasiha. Nasiha ni tahadhari na hapa kuna maneno makubwa inatupasa kuyazingatia. Kasema Luqman usimshirikishe Mwenye enzi Mungu hakika shirki ni dhulma kubwa.
Katika kuifahamu au kujificha katika aya hii watu wengi wakadhani Shirki ni ile ya kuabudu kitu chengine pekee cha asiekuwa Mwenye enzi Mungu, lakini mengine yote hayapo kwenye Shirki, leo hii nakwambieni ukiapa kwa jina la Mwenye enzi Mungu kiapo cha uongo hiyo ni dhulma na umemshirikisha Mwenye enzi Mungu na ni dhulma kubwa,(Umelitumia jina lake kwenye Uharamia wako).
Ukimuomba asiyekua Yeye basi umemshirikisha, ukimtegemea asiyekua yeye basi umemshirikisha, ukitoa ushahidi wa uongo basi umemshirikisha,Ukenda kwa mganga kuroga umemshirikisha Mollah wako, Kwanini ikawa hivyo? Kwa sababu wewe unazo sifa zake mbili muhimu za (kuona na kusikia)Kheri hii alokupa ndio unaifanya nyenzo ya kuibia au kupata kisicho haki yako, Na hiyo ni dhulma kubwa kabisa. Ndio maana kwenye aya ya 15 Mwenye enzi Mungu wasia wake kwa wanaadamu akasema,Na kuanza na wazazi wako, iwapo wazazi wako wakikulazimisha kunishirikisha mimi basi usiwatii (Abadan).
Endelea Part 3
Naam, Mtoto yumo kwenye hiyo (Hekima)(Wisdom)Lakini hajijui ndio maana hata Kwenye Quraan lilipotajwa jambo la (Hekima) Luqman alimuanza nani? isome Quraan uone vipi inakua kupoteza saa, vipi unajua tafauti ya saa na (Hekima). Anasemaje Mollah wako? Luqman aya ya 12 mpaka 13 na kuendelea. Zama kwenye maneno hayo ujue hekima inatokea wapi.
وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا لُقۡمَـٰنَ ٱلۡحِكۡمَةَ أَنِ ٱشۡكُرۡ لِلَّهِۚ وَمَن يَشۡڪُرۡ فَإِنَّمَا يَشۡكُرُ لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَنِىٌّ حَمِيدٌ۬
Kwa yakini tulimpa Luqman Hekima(Wisdom), Tukamwambia Mshukuru Mwenye Enzi Mungu, Na atakaeshukuru kwa yakini anashukuru kwa ajili ya Nafsi yake, Na atakae kufuru Mwenye enzi Mungu(Amejitosheleza)Mkwasi asifiwaye, (Si Mwenye kuhitaji shukurani zenu)
Nini (Wisdom)au Hekima? Ni hali au uwezo wa kumiliki Nafsi yako nje ya Akili, au kwa lugha nyengine ni mkusanyiko wa ufahamu mambo yalopita na yajayo ukawa unaishi nayo sasa hivi, hiyo ndio tafsiri ya Rahisi ya hilo jambo la (hekima)lakini hata halijafikia ukaribu wake na kusudio ya hiyo hali ya kuwa na (Hekima).
Anasemaje Luqman? Tulimpa Luqman Hekima, tukamwambia Mshukuru Mollah wako, kwanini ashukuru, kwa sababu kitu hicho ni kitu (Adhimu)ni (State of Knowing),Hiyo ndio Hekima, Binaadamu ukijijua basi unashukuru kwa kupewa neema na rehma hiyo, Mnyama ana lala na wewe unalala, halafu nyote mnaamka, lakini kuna mmoja anajijua kaamka, na huyo ni wewe, Shukuru kwa Neema hiyo ya kuumbwa Mwanaadamu na ukapewa cheo cha kujijua, Shukuru kwa Nafsi yako uko mzima, unavuta pumzi bila ya taabu, unatembea na kurudi bila ya shida, unapata riziki yako kama ilivopangwa, shukuru kwa ajili ya Nafsi yako, na kama hutaki hilo au kumshukuru Mollah wako, Yeye hana (haja na shukuruni yako), endelea kumkanusha, kumpinga na kumuasi na yeye atakunyima miujiza hii nje ya Akili.
Naam sasa toka kwenye saa uingie kwenye miujiza wa (Hekima) za (Luqman), Hekima inakuja kwa njia ya kusubiri, katika Ulimwengu wa sasa Binaadamu kasoma sana, lakini kwa kufanya hivyo kapoteza (Hekima), kwa sababu ya haraka za maisha, ndio maana (Luqman)akaona aanze kwa Kumtahadharisha Mwanawe, kwa sababu (Asiye funzwa na mamae hufunzwa na Ulimwengu).
وَإِذۡ قَالَ لُقۡمَـٰنُ لِٱبۡنِهِۦ وَهُوَ يَعِظُهُ ۥ يَـٰبُنَىَّ لَا تُشۡرِكۡ بِٱللَّهِۖ إِنَّ ٱلشِّرۡكَ لَظُلۡمٌ عَظِيمٌ۬
Na(Wakumbushe)Luqman alipomwambia Mwanawe na hali yakuwa anampa nasiha, Ewe Mwanangu usimshirikishe Mwenye Enzi Mungu, Maana kushirikisha ndiyo dhulma kubwa.
Hapo kuna tafauti kubwa baina ya Baba na mtoto, tafauti yenyewe mwenye hekima hawezi kukupa hekima yake, ila ikitoka kwake inakua nasiha. Nasiha ni tahadhari na hapa kuna maneno makubwa inatupasa kuyazingatia. Kasema Luqman usimshirikishe Mwenye enzi Mungu hakika shirki ni dhulma kubwa.
Katika kuifahamu au kujificha katika aya hii watu wengi wakadhani Shirki ni ile ya kuabudu kitu chengine pekee cha asiekuwa Mwenye enzi Mungu, lakini mengine yote hayapo kwenye Shirki, leo hii nakwambieni ukiapa kwa jina la Mwenye enzi Mungu kiapo cha uongo hiyo ni dhulma na umemshirikisha Mwenye enzi Mungu na ni dhulma kubwa,(Umelitumia jina lake kwenye Uharamia wako).
Ukimuomba asiyekua Yeye basi umemshirikisha, ukimtegemea asiyekua yeye basi umemshirikisha, ukitoa ushahidi wa uongo basi umemshirikisha,Ukenda kwa mganga kuroga umemshirikisha Mollah wako, Kwanini ikawa hivyo? Kwa sababu wewe unazo sifa zake mbili muhimu za (kuona na kusikia)Kheri hii alokupa ndio unaifanya nyenzo ya kuibia au kupata kisicho haki yako, Na hiyo ni dhulma kubwa kabisa. Ndio maana kwenye aya ya 15 Mwenye enzi Mungu wasia wake kwa wanaadamu akasema,Na kuanza na wazazi wako, iwapo wazazi wako wakikulazimisha kunishirikisha mimi basi usiwatii (Abadan).
Endelea Part 3
MIUJIZA NJE YA AKILI PART 3
Asalaam Aleiykum
Tuko katika kutizama (Hekima) za Luqman, Na kwenye aya ya 18 anasema:
وَلَا تُصَعِّرۡ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمۡشِ فِى ٱلۡأَرۡضِ مَرَحًاۖ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخۡتَالٍ۬ فَخُورٍ۬
Wala usiwatizame (Watu kwa Jeuri)kwa upande mmoja wa uso(Dharau)wala usende katika nchi kwa maringo, Hakika Mwenye enzi Mungu Hampendi kila ajivunae, ajifahirishaye.
Ukiingia au kupewa Hekima unajua Mwenye Enzi Hapendi wala kuchukia kwa sababu Yeye hana mfano wa Binaadamu, lakini kwa ajili ya kuwasiliana na wewe ndio yakatumika maneno hayo, Lakini ndani ya maneno ya Luqman kwenye hekima yake anajua kuwa Wanaadamu wana (Energy)maalum inayotoka katika Roho zao, kutokana na nguvu za (Energy)hiyo Mwenye enzi Mungu anakuondoshea kinga yake kwa yale unayowafanyia wenzio, na maringo yako, ndio mara unaanguka kimaisha au kupata maradhi.
Nimemtumia Luqman kuonesha ukipewa Hekima unakua mtu wa aina gani. Mama akishirikiana na Ulimwengu anakulea taratibu, kama vile Mti unavokua, mboga zinavyochipua, matunda yanavo wiva, Ulimwengu hautaki haraka unakwenda na sheria ilivopangwa.
Sasa ukija na Ujana wako umebeba saa, unaishi ndani ya saa yako, ndio utajiona uko mbioni unahangaika na maisha, Ama Mtu mzima yeye ana (Option)kwa sababu kashapewa nasiha, Akitaka na kuridhiwa na Mollah wake ana uwezo wa kuingia kwenye Hekima, Na kama hakutaka basi atabakia na saa lake mpaka kufa kwake.
Sasa ukiingia au kupewa Hekima Miujiza gani inatokezea?.
Kwa Mara ya Mwanzo unapata utulivu wa Akili, unakua hupangi au kuamua mambo kwa kutumia Akili, huoni au kuangalia kwa kutumia Akili, Kwa Mara ya Mwanzo unapata mambo kwa uhakika, hapo tena unajijua rasmi kama utakufa, ukioneshwa rangi ya kijani unaiyona kwa uhalisia wake, hukioni chama au bendera unaona (Pure)green na kazi zake, Kwa mara ya mwanzo unapata kuwasiliana na Roho yako, Na Maswali na majibu yanatoka kwenye hiyo (Source), Hukurupuki na kujibu maswali ovyo ovyo kama ufanyavo hivi sasa, Naam hiyo ndio Hekima, na hayo kwako ndio yatakua miujiza ya kuipoteza hiyo saa ulonayo hivi sasa.
Sasa Pazia linaondoshwa ukiwa hai baina ya Akili na Roho yako, hiyo ndio Hekima. Madhanmbi unayaona kwenye asili yake na madhara yake, sasa hivi unajua dhanmbi lakini hujui dhara yake, omba au ingia kwenye Hekima uone dhara yake. Ingia kwenye Muujiza huu wa Hekima upate kuona mambo kwenye original yake, Hekima ni haki yako fanya jitihada upoteze saa ili uipate hekima, najua unashituka kuipoteza saa yako, lakini kumbuka saa umeinunua kutoka kwa wazee wako, walimu wako, marafiki zako, lakini Hekima ni (Original)yako, kumbuka ulivokua mtoto ukawa unashangaa hichi nini na kile nini, rejea tena kule kwa mara ya pili ukashuhudie Miujiza, kaipate (Truth), Ndio Maana Mwenye enzi mungu akasema sura ya (Baqarah aya ya 269)
يُؤۡتِى ٱلۡحِڪۡمَةَ مَن يَشَآءُۚ وَمَن يُؤۡتَ ٱلۡحِڪۡمَةَ فَقَدۡ أُوتِىَ خَيۡرً۬ا ڪَثِيرً۬اۗ وَمَا يَذَّڪَّرُ إِلَّآ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَـٰبِ
Mwenye enzi Mungu humpa hekima amtakaye, Na aliyepewa Hekima bila shaka amepewa kheri nyingi, Na hawakumbuki ila wenye Akili.
Kwa hiyo ni vizuri kuwa na hiyo saa ambayo itakufanya uikumbuke hiyo Hekima, na Akili imewekwa ni kama sehemu ya kuchupia uende kwenye hiyo Hekima, Muujiza uko hapo katika kukumbuka ukachupa.
Wacha niendelee kufafanua ili ufahamu vizuri, Elimu ni Mafunzo ya Nafsi, Sheikh kakwambia hivi, Mwalimu kakwambia vile, watu wanasema haya, na wewe unajua hili, ni mambo katika Ulimwengu huu yaloletwa na hiyo saa, Lakini hekima ni Mafundisho ya Kiroho ambayo yanatoka kwa Mwenyewe subhanna, kama vile ukitia mbegu kwenye Ardhi unatokeza kuwa Mti, Kwa hiyo Elimu ni jambo litokealo nje, Na hekima ni jambo unalolipata kutokea ndani, kumbuka la kwanza kutokea kwenye Akili na la pili ni lile litokalo kwenye Roho.
Unaweza Ukapewa Kitabu, umesoma na (PHD)lakini ukawa hukupewa Hekima, unakua na hasara kubwa, kile cha muhimu huna, umebakia na saa lako, ndio maana ukipewa Hekima unaambiwa Ushukuru kama alivo (Shukuru)Luqman.
Sasa Muujiza nje ya Akili ni upi, Ni ule uwezo wa kuishi katika (State)au hali Mbili, Ya kwanza ni ile ya Mnyama, unalala, unakula, Na ya pili ni ile ya Ubinaadamu ya kuelewa (There is something beyond)Unakumbuka na kusahau, unapita katika hali hizi mara umeponyoka umetenda dhanmbi, halafu unakumbuka unarudi tena na kutubu, ukiwa katika hali hiyo ya kukumbuka huo ndio muujiza wenyewe na ukipewa ukawa unakumbuka daima huo ndio ucha Mungu, na kuishi katika kukumbuka ndio huko kuipoteza saa, sababu saa inabadilika lakini kukumbuka kuko vile vile, Ukiingia kwenye sala, ukitoka wewe uko vile vile mpaka ukilala unajijua wewe nani, Na ukiamka unajijua wewe nani hubadiliki, kumbuka saa yako inabadilika lakini hekima yako iko vile vile. Ishi kwenye hekima upate Miujiza yake na hutotaka kutoka tena kwa Uwezo wa Mollah wako.
Tuko katika kutizama (Hekima) za Luqman, Na kwenye aya ya 18 anasema:
وَلَا تُصَعِّرۡ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمۡشِ فِى ٱلۡأَرۡضِ مَرَحًاۖ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخۡتَالٍ۬ فَخُورٍ۬
Wala usiwatizame (Watu kwa Jeuri)kwa upande mmoja wa uso(Dharau)wala usende katika nchi kwa maringo, Hakika Mwenye enzi Mungu Hampendi kila ajivunae, ajifahirishaye.
Ukiingia au kupewa Hekima unajua Mwenye Enzi Hapendi wala kuchukia kwa sababu Yeye hana mfano wa Binaadamu, lakini kwa ajili ya kuwasiliana na wewe ndio yakatumika maneno hayo, Lakini ndani ya maneno ya Luqman kwenye hekima yake anajua kuwa Wanaadamu wana (Energy)maalum inayotoka katika Roho zao, kutokana na nguvu za (Energy)hiyo Mwenye enzi Mungu anakuondoshea kinga yake kwa yale unayowafanyia wenzio, na maringo yako, ndio mara unaanguka kimaisha au kupata maradhi.
Nimemtumia Luqman kuonesha ukipewa Hekima unakua mtu wa aina gani. Mama akishirikiana na Ulimwengu anakulea taratibu, kama vile Mti unavokua, mboga zinavyochipua, matunda yanavo wiva, Ulimwengu hautaki haraka unakwenda na sheria ilivopangwa.
Sasa ukija na Ujana wako umebeba saa, unaishi ndani ya saa yako, ndio utajiona uko mbioni unahangaika na maisha, Ama Mtu mzima yeye ana (Option)kwa sababu kashapewa nasiha, Akitaka na kuridhiwa na Mollah wake ana uwezo wa kuingia kwenye Hekima, Na kama hakutaka basi atabakia na saa lake mpaka kufa kwake.
Sasa ukiingia au kupewa Hekima Miujiza gani inatokezea?.
Kwa Mara ya Mwanzo unapata utulivu wa Akili, unakua hupangi au kuamua mambo kwa kutumia Akili, huoni au kuangalia kwa kutumia Akili, Kwa Mara ya Mwanzo unapata mambo kwa uhakika, hapo tena unajijua rasmi kama utakufa, ukioneshwa rangi ya kijani unaiyona kwa uhalisia wake, hukioni chama au bendera unaona (Pure)green na kazi zake, Kwa mara ya mwanzo unapata kuwasiliana na Roho yako, Na Maswali na majibu yanatoka kwenye hiyo (Source), Hukurupuki na kujibu maswali ovyo ovyo kama ufanyavo hivi sasa, Naam hiyo ndio Hekima, na hayo kwako ndio yatakua miujiza ya kuipoteza hiyo saa ulonayo hivi sasa.
Sasa Pazia linaondoshwa ukiwa hai baina ya Akili na Roho yako, hiyo ndio Hekima. Madhanmbi unayaona kwenye asili yake na madhara yake, sasa hivi unajua dhanmbi lakini hujui dhara yake, omba au ingia kwenye Hekima uone dhara yake. Ingia kwenye Muujiza huu wa Hekima upate kuona mambo kwenye original yake, Hekima ni haki yako fanya jitihada upoteze saa ili uipate hekima, najua unashituka kuipoteza saa yako, lakini kumbuka saa umeinunua kutoka kwa wazee wako, walimu wako, marafiki zako, lakini Hekima ni (Original)yako, kumbuka ulivokua mtoto ukawa unashangaa hichi nini na kile nini, rejea tena kule kwa mara ya pili ukashuhudie Miujiza, kaipate (Truth), Ndio Maana Mwenye enzi mungu akasema sura ya (Baqarah aya ya 269)
يُؤۡتِى ٱلۡحِڪۡمَةَ مَن يَشَآءُۚ وَمَن يُؤۡتَ ٱلۡحِڪۡمَةَ فَقَدۡ أُوتِىَ خَيۡرً۬ا ڪَثِيرً۬اۗ وَمَا يَذَّڪَّرُ إِلَّآ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَـٰبِ
Mwenye enzi Mungu humpa hekima amtakaye, Na aliyepewa Hekima bila shaka amepewa kheri nyingi, Na hawakumbuki ila wenye Akili.
Kwa hiyo ni vizuri kuwa na hiyo saa ambayo itakufanya uikumbuke hiyo Hekima, na Akili imewekwa ni kama sehemu ya kuchupia uende kwenye hiyo Hekima, Muujiza uko hapo katika kukumbuka ukachupa.
Wacha niendelee kufafanua ili ufahamu vizuri, Elimu ni Mafunzo ya Nafsi, Sheikh kakwambia hivi, Mwalimu kakwambia vile, watu wanasema haya, na wewe unajua hili, ni mambo katika Ulimwengu huu yaloletwa na hiyo saa, Lakini hekima ni Mafundisho ya Kiroho ambayo yanatoka kwa Mwenyewe subhanna, kama vile ukitia mbegu kwenye Ardhi unatokeza kuwa Mti, Kwa hiyo Elimu ni jambo litokealo nje, Na hekima ni jambo unalolipata kutokea ndani, kumbuka la kwanza kutokea kwenye Akili na la pili ni lile litokalo kwenye Roho.
Unaweza Ukapewa Kitabu, umesoma na (PHD)lakini ukawa hukupewa Hekima, unakua na hasara kubwa, kile cha muhimu huna, umebakia na saa lako, ndio maana ukipewa Hekima unaambiwa Ushukuru kama alivo (Shukuru)Luqman.
Sasa Muujiza nje ya Akili ni upi, Ni ule uwezo wa kuishi katika (State)au hali Mbili, Ya kwanza ni ile ya Mnyama, unalala, unakula, Na ya pili ni ile ya Ubinaadamu ya kuelewa (There is something beyond)Unakumbuka na kusahau, unapita katika hali hizi mara umeponyoka umetenda dhanmbi, halafu unakumbuka unarudi tena na kutubu, ukiwa katika hali hiyo ya kukumbuka huo ndio muujiza wenyewe na ukipewa ukawa unakumbuka daima huo ndio ucha Mungu, na kuishi katika kukumbuka ndio huko kuipoteza saa, sababu saa inabadilika lakini kukumbuka kuko vile vile, Ukiingia kwenye sala, ukitoka wewe uko vile vile mpaka ukilala unajijua wewe nani, Na ukiamka unajijua wewe nani hubadiliki, kumbuka saa yako inabadilika lakini hekima yako iko vile vile. Ishi kwenye hekima upate Miujiza yake na hutotaka kutoka tena kwa Uwezo wa Mollah wako.
Thursday, November 3, 2016
TAA YA FAHAMU PART 1
Asalaam Aleiykum,
Kuna Msemo wa "Kiswahili Mzuri sana"unasema hivi"(Ukweli ukidhihiri uongo hujitenga) Hiyo ni kweli kabisa, hali kama hiyo Mwanaadamu unayo lakini bado hujaifanyia kazi, pengine dunia imekushughulisha, basi kutokana na makumbusho haya labda waweza kuanza kutafakari na kujiwezesha kuwacha kuishi kizani,utaanza kuishi kwa njia ya kutumia Taa ulonayo,Usikubali tena Umeme wa Nje Uzimwe na wa ndani kwenye Nafsi yako Uzimike.
Nini Taa?. Mpaka leo hakuna aliyeweza kutwambia au kuchambua , au kujua nini Taa, Si Wanasayansi wa Dunia wala wa Dini walofanikiwa kujua nini Taa, Wanasayansi wao wamechambua na kufikia kuieleza utendaji wake wa kazi, wakasema hakuna kitu kiendacho kwa kasi kama Taa(speed of light) na hivi karibuni wamegundua kuwa kila kitu mwishoe kinabadilika na kuwa hiyo Taa(Light), Lakini wakiulizwa Taa yenyewe ni kitu gani hawawezi kulijibu swali hilo.
Na Wanasayansi wa Kidini au niwaite(Wanazuoni)wao wamegundua kuwa kila ukenda ndani au kuzidisha Ibada unakutana na hii Taa(Light), Lakini pia hawajui nini uwezo wa hiyo Taa ya ndani, nini kazi yake?, ila wanaamini hii Taa ina uwezo wa kukuongoza kutoka kwenye giza kwenda kwenye Nuru, ziko dalili zinaonesha iwapo utapunguza Ibada au kutenda Dhanmbi inakua inapungua nuru ya taa hiyo.
Tukizungumza Taa inabidi tuieleze Taa ya aina gani, kwa sababu Taa ziko za aina nyingi japokua asili yake ni moja. Mfano Taa hii ya Jua ambayo ndani yake zinapatikana faida nyingi tu si za kuondosha usiku pekee mpaka (Vitamin D)imo kwenye Taa hiyo. Kwa hiyo taa ni nyingi na zina kazi tafauti, leo sisi tutaizungumzia Taa ya ndani, taa ya Nafsi yako, kabla ya kwenda mbali wacha tuutizame mfano mdogo ili utupe muelekeo wa Darsa yetu, na hapa tutaichukua Taa yetu ya kawaida(Umeme), Na wakati mzuri ni ule ambao Taa zimezimwa, Kiza kimetawala chumbani, nini kinatokezea?.
Inapokua kiza maana yake huoni kitu, lakini mara inapoletwa au kuwashwa Taa unaviona vitu vyote viliopo katika chumba hicho, na hivyo pia ndivyo Taa ya Fahamu inavofanya kazi yake, mfano ni uleule hakuna tafauti.
Sasa kwa Mwanaadamu Taa hii ina kazi mbili ama kazi ya kwanza nini kukutoa kwenye Ujinga na kukupeleka kwenye werevu au ita (Elimu)na kazi ya pili ni kukuonesha chumba chako cha Nafsi na Takataka, mavumbi, fanicha na vyote vilojificha kwenye Nafsi yako. Ndio maana tutatumia aya moja kutufahamisha kuwapo kwa Taa hii, na vipi "Ukweli Ukidhihiri uongo hujitenga", vipi inakua wakati ukiigundua taa hii, faida gani unaipata katika kuitumia Taa hii.
Sura ya Kiyama aya ya (14-15)
بَلِ ٱلۡإِنسَـٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٌ۬
Bali Mwanaadamu ni Shahidi(Mwenye kuona)Nafsi yake.
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُ
Ingawa anatoa Nyudhuru zake.
Naam ilipotajwa kuona au kuishuhudia Nafsi yako hapo inatakiwa ujiulize nini kimekusudiwa, Lazima ujiulize nini nafsi na nani Mwenye kuiona, na utafute maana halisi yakutambua kumbe kama najiona ina maana mimi ni tafauti na nafsi. Basi ikiwa tafauti kwanini naleta Nyudhuru, ukiweza kugundua mawili hayo hapo hapo utaelewa kumbe hii nyudhuru ndiko huko kuzima hiyo Taa.
Mwanaadamu unajiona matendo yako yote, na kuona huku ndio huo Muujiza, kwa sababu macho yanoona wewe una uwezo wa kuyaona, sasa hicho kinachoona nini?, kifanyie kazi upate kukijua, kama nilivosema wewe na Nafsi ni vitu viwili tafauti, ila unazidiwa na nafsi, Nafsi inakutawala nakuchukua madaraka yako, inatakiwa ufanye kazi kubwa sana kuishinda Nafsi, ndio Nabii Yusuf akathibitisha kwenye quraan sura ya Yussuf aya 53.
وَمَآ أُبَرِّئُ نَفۡسِىٓۚ إِنَّ ٱلنَّفۡسَ لَأَمَّارَةُۢ بِٱلسُّوٓءِ إِلَّا مَا رَحِمَ رَبِّىٓۚ إِنَّ رَبِّى غَفُورٌ۬ رَّحِيمٌ۬
Nami sijitakasi nafsi yangu , kwa hakika (Kila) Nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu, isipokua ile ambayo Mollah wangu ameirehemu, Hakika Mollah wangu ni Mwingi wa Kusamehe na Mwingi wa Kurehemu.
Naam hiyo ndio Akili ina Mwenendo upi?
Endelea Part 2
Kuna Msemo wa "Kiswahili Mzuri sana"unasema hivi"(Ukweli ukidhihiri uongo hujitenga) Hiyo ni kweli kabisa, hali kama hiyo Mwanaadamu unayo lakini bado hujaifanyia kazi, pengine dunia imekushughulisha, basi kutokana na makumbusho haya labda waweza kuanza kutafakari na kujiwezesha kuwacha kuishi kizani,utaanza kuishi kwa njia ya kutumia Taa ulonayo,Usikubali tena Umeme wa Nje Uzimwe na wa ndani kwenye Nafsi yako Uzimike.
Nini Taa?. Mpaka leo hakuna aliyeweza kutwambia au kuchambua , au kujua nini Taa, Si Wanasayansi wa Dunia wala wa Dini walofanikiwa kujua nini Taa, Wanasayansi wao wamechambua na kufikia kuieleza utendaji wake wa kazi, wakasema hakuna kitu kiendacho kwa kasi kama Taa(speed of light) na hivi karibuni wamegundua kuwa kila kitu mwishoe kinabadilika na kuwa hiyo Taa(Light), Lakini wakiulizwa Taa yenyewe ni kitu gani hawawezi kulijibu swali hilo.
Na Wanasayansi wa Kidini au niwaite(Wanazuoni)wao wamegundua kuwa kila ukenda ndani au kuzidisha Ibada unakutana na hii Taa(Light), Lakini pia hawajui nini uwezo wa hiyo Taa ya ndani, nini kazi yake?, ila wanaamini hii Taa ina uwezo wa kukuongoza kutoka kwenye giza kwenda kwenye Nuru, ziko dalili zinaonesha iwapo utapunguza Ibada au kutenda Dhanmbi inakua inapungua nuru ya taa hiyo.
Tukizungumza Taa inabidi tuieleze Taa ya aina gani, kwa sababu Taa ziko za aina nyingi japokua asili yake ni moja. Mfano Taa hii ya Jua ambayo ndani yake zinapatikana faida nyingi tu si za kuondosha usiku pekee mpaka (Vitamin D)imo kwenye Taa hiyo. Kwa hiyo taa ni nyingi na zina kazi tafauti, leo sisi tutaizungumzia Taa ya ndani, taa ya Nafsi yako, kabla ya kwenda mbali wacha tuutizame mfano mdogo ili utupe muelekeo wa Darsa yetu, na hapa tutaichukua Taa yetu ya kawaida(Umeme), Na wakati mzuri ni ule ambao Taa zimezimwa, Kiza kimetawala chumbani, nini kinatokezea?.
Inapokua kiza maana yake huoni kitu, lakini mara inapoletwa au kuwashwa Taa unaviona vitu vyote viliopo katika chumba hicho, na hivyo pia ndivyo Taa ya Fahamu inavofanya kazi yake, mfano ni uleule hakuna tafauti.
Sasa kwa Mwanaadamu Taa hii ina kazi mbili ama kazi ya kwanza nini kukutoa kwenye Ujinga na kukupeleka kwenye werevu au ita (Elimu)na kazi ya pili ni kukuonesha chumba chako cha Nafsi na Takataka, mavumbi, fanicha na vyote vilojificha kwenye Nafsi yako. Ndio maana tutatumia aya moja kutufahamisha kuwapo kwa Taa hii, na vipi "Ukweli Ukidhihiri uongo hujitenga", vipi inakua wakati ukiigundua taa hii, faida gani unaipata katika kuitumia Taa hii.
Sura ya Kiyama aya ya (14-15)
بَلِ ٱلۡإِنسَـٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٌ۬
Bali Mwanaadamu ni Shahidi(Mwenye kuona)Nafsi yake.
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُ
Ingawa anatoa Nyudhuru zake.
Naam ilipotajwa kuona au kuishuhudia Nafsi yako hapo inatakiwa ujiulize nini kimekusudiwa, Lazima ujiulize nini nafsi na nani Mwenye kuiona, na utafute maana halisi yakutambua kumbe kama najiona ina maana mimi ni tafauti na nafsi. Basi ikiwa tafauti kwanini naleta Nyudhuru, ukiweza kugundua mawili hayo hapo hapo utaelewa kumbe hii nyudhuru ndiko huko kuzima hiyo Taa.
Mwanaadamu unajiona matendo yako yote, na kuona huku ndio huo Muujiza, kwa sababu macho yanoona wewe una uwezo wa kuyaona, sasa hicho kinachoona nini?, kifanyie kazi upate kukijua, kama nilivosema wewe na Nafsi ni vitu viwili tafauti, ila unazidiwa na nafsi, Nafsi inakutawala nakuchukua madaraka yako, inatakiwa ufanye kazi kubwa sana kuishinda Nafsi, ndio Nabii Yusuf akathibitisha kwenye quraan sura ya Yussuf aya 53.
وَمَآ أُبَرِّئُ نَفۡسِىٓۚ إِنَّ ٱلنَّفۡسَ لَأَمَّارَةُۢ بِٱلسُّوٓءِ إِلَّا مَا رَحِمَ رَبِّىٓۚ إِنَّ رَبِّى غَفُورٌ۬ رَّحِيمٌ۬
Nami sijitakasi nafsi yangu , kwa hakika (Kila) Nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu, isipokua ile ambayo Mollah wangu ameirehemu, Hakika Mollah wangu ni Mwingi wa Kusamehe na Mwingi wa Kurehemu.
Naam hiyo ndio Akili ina Mwenendo upi?
Endelea Part 2
TAA YA FAHAMU PART 2
Asalaam Aleiykum
Akili ina mwenendo wa njia mbili, Njia ya kwanza kutupa kila kitu kwenye chumba chake, halafu inazima Taa, inajifanya haitazami tena, haina haja ya kuwasha Taa tena na kusafisha chumba, na njia ya Pili ambayo ya kusafisha hicho chumba au kuwasha Taa ukaona vitu vilivyomo huitumii kabisa, kumbuka kila kiingiacho chumbani kinahitaji kutolewa, na huwezi kuvitoa vitu hivyo mpaka uwashe Taa hii ya fahamu, Nikimaanisha jambo lolote linaloingia kwenye akili pia linashuka kwenye moyo, Sasa maradhi yote na matatizo yote yanakukuta sababu ndani ya chumba chako kuna takataka nyingi, vumbi limejaa, umebeba mizigo ambayo huna haja nayo katika safari yako.
Kwa hiyo unatakiwa ufanye jitihada kutupa yaliyomo ndani ili uishi kwenye Ulimwengu huu kwa Furaha, na kutokana na sababu hiyo ndio sasa nakutaka uwashe hiyo Taa ya fahamu ili upate kutoka kwenye kiza. Kumbuka Nabii Yusuf a.s anasema Nafsi ina amrisha maovu na kuna njia moja tu ya kuweza kuishinda nafsi ambayo yeye aliitumia na sasa ushafika wakati na wewe uitumie.
Aliendelea na kusema isipokua upate Rehma ya Mwenye enzi Mungu, vipi unaipata Rehma hiyo, kawaida yako wewe unafanya kazi ndani ya Rehma, maisha yako yote ni Rehma, na hakuna Rehma kubwa kama hii ya kuona. Sasa nini kinatokezea?kila jambo linatokezea unapeleka kwenye nafsi yako, Senema unaangalia wanawake au wanaume vimo humo, unafanya wizi na ufisadi, unasema uongo, unashuhudia maasi na kila machafu hayo yote kumbuka yanapita na kuingia kwenye chumba chako, ikisha unakwenda kulala wewe chumba kimejaa mambo, unazima taa huna wasiwasi, ukiamka unaanza tena na tena, sasa hata siku moja hujasafisha ndani ya chumba, unakata kucha, unapaka (Poda)unakoga unatia uturi, Nyumba nje Mashaallah inasafishwa kikweli, lakini nini habari ya ndani?, Nani basi wa kukusafishia isipokua Mwenyewe, na Chumbani kiza utasafisha vipi si lazima uwashe Taa.
Kumbuka yote uloyaona na kusikia yamo ndani na kusafisha kwenyewe lazima iwe (Reverse)kinyume chake. kumbuka Taa ikizimika Uharibifu wote ndio unatokea, kwa sababu umo gizani unajikwaa kwenye Furniture, unajikwaa kwenye kila Dhanmbi, unatibu watu wengine kumbe wewe Mwenyewe Mgonjwa, Watu wanakushangaa jamani huyu si Sheikh mbona anafanya mambo haya, kumbe hawajui wewe na wao nyote Taa zimezimwa.
Nabii Yusuf a.s aliposema sijitakasi Nafsi yangu alikua anajua hawezi kujichukulia dhamana na Nafsi pekee, nafsi ina vituko, imo kwenye kuamrisha ufisadi na maovu kutokana inaishi kwenye giza.
Sasa ufanye nini unatakiwa utoke gizani uelekee kwenye Nuru.
Endelea part 3
Akili ina mwenendo wa njia mbili, Njia ya kwanza kutupa kila kitu kwenye chumba chake, halafu inazima Taa, inajifanya haitazami tena, haina haja ya kuwasha Taa tena na kusafisha chumba, na njia ya Pili ambayo ya kusafisha hicho chumba au kuwasha Taa ukaona vitu vilivyomo huitumii kabisa, kumbuka kila kiingiacho chumbani kinahitaji kutolewa, na huwezi kuvitoa vitu hivyo mpaka uwashe Taa hii ya fahamu, Nikimaanisha jambo lolote linaloingia kwenye akili pia linashuka kwenye moyo, Sasa maradhi yote na matatizo yote yanakukuta sababu ndani ya chumba chako kuna takataka nyingi, vumbi limejaa, umebeba mizigo ambayo huna haja nayo katika safari yako.
Kwa hiyo unatakiwa ufanye jitihada kutupa yaliyomo ndani ili uishi kwenye Ulimwengu huu kwa Furaha, na kutokana na sababu hiyo ndio sasa nakutaka uwashe hiyo Taa ya fahamu ili upate kutoka kwenye kiza. Kumbuka Nabii Yusuf a.s anasema Nafsi ina amrisha maovu na kuna njia moja tu ya kuweza kuishinda nafsi ambayo yeye aliitumia na sasa ushafika wakati na wewe uitumie.
Aliendelea na kusema isipokua upate Rehma ya Mwenye enzi Mungu, vipi unaipata Rehma hiyo, kawaida yako wewe unafanya kazi ndani ya Rehma, maisha yako yote ni Rehma, na hakuna Rehma kubwa kama hii ya kuona. Sasa nini kinatokezea?kila jambo linatokezea unapeleka kwenye nafsi yako, Senema unaangalia wanawake au wanaume vimo humo, unafanya wizi na ufisadi, unasema uongo, unashuhudia maasi na kila machafu hayo yote kumbuka yanapita na kuingia kwenye chumba chako, ikisha unakwenda kulala wewe chumba kimejaa mambo, unazima taa huna wasiwasi, ukiamka unaanza tena na tena, sasa hata siku moja hujasafisha ndani ya chumba, unakata kucha, unapaka (Poda)unakoga unatia uturi, Nyumba nje Mashaallah inasafishwa kikweli, lakini nini habari ya ndani?, Nani basi wa kukusafishia isipokua Mwenyewe, na Chumbani kiza utasafisha vipi si lazima uwashe Taa.
Kumbuka yote uloyaona na kusikia yamo ndani na kusafisha kwenyewe lazima iwe (Reverse)kinyume chake. kumbuka Taa ikizimika Uharibifu wote ndio unatokea, kwa sababu umo gizani unajikwaa kwenye Furniture, unajikwaa kwenye kila Dhanmbi, unatibu watu wengine kumbe wewe Mwenyewe Mgonjwa, Watu wanakushangaa jamani huyu si Sheikh mbona anafanya mambo haya, kumbe hawajui wewe na wao nyote Taa zimezimwa.
Nabii Yusuf a.s aliposema sijitakasi Nafsi yangu alikua anajua hawezi kujichukulia dhamana na Nafsi pekee, nafsi ina vituko, imo kwenye kuamrisha ufisadi na maovu kutokana inaishi kwenye giza.
Sasa ufanye nini unatakiwa utoke gizani uelekee kwenye Nuru.
Endelea part 3
TAA YA FAHAMU PART 3
Asalaam Aleiykum,
Sasa nini ufanye Kiumbe wewe, Kumbuka Mwanaadamu una vitendea Kazi vitu viwili, Kimoja katika hivyo hakiguswi na chochote, hakuna jambo lolote linaloweza kufikia kitu hicho ambacho ndio hiyo Taa ya Fahamu(Pure Soul). Kama Mwanaadamu utakua unakitumia kifaa hiki au nikipe heshima kwa sababu ni kitu kitakatifu(Roho)kwa uerevu, basi daima utakua umo furahani, kwanini nikasema umo kwa sababu (Roho)(Nature)yake ni Furaha(Nisiseme hivi Mkasema kasema anaijua roho kitu hicho hakijulikani), lakini hasara yetu Wanaadamu Tunaishi au kutawaliwa na hicho chengine chenye kutupeleka kwenye kiza, kipi hicho?.
Akili(Hii ni sehemu ya Nafsi) ni nyenzo ambayo tunatakiwa kuitumia kwa uangalifu kwani ni (Very Powerful weapon)silaha kubwa sana, ukimilikiwa na Akili Binaadamu umekwisha, huna (Control) ya maisha yako kabisa.
Kwa sababu Akili inafanya kazi yake ya kukusanya, kupokea na kutupa kwenye hicho chumba, chumba hiki kiite (Memory or Subconscious)na kwa kuwa lolote lile lilopita kwenye taa yako ya Fahamu kumbuka liko humo chumbani umeliweka na wala halitoki, Sasa nini kinatokezea kuna baadhi ya nyakati Taa inawaka na kumurika yale mambo yaliyomo kwenye chumba iwe chuki, hasada, uzinifu, wizi, na ukimurika tu likija juu lazima ulitende kwa sababu hujalitupa ila umeliweka akiba, kwa hiyo tahadhari sana unapokwenda kwenye chumba chako, utakua unatenda mambo bila ya kukusudia, sasa kwa kuwa mambo yana kukera ndio unaamua kuzima Taa, na huku watu wanatumia ule msemo kajitoa fahamu.
Quraan imekuhurumia imesema unaleta nyudhuru yaani unazima Taa, ndio ikaendelea kukumbusha kuwa Mwanaadamu ni Mwenye kuiona Nafsi yake, ikimaanisha unao uwezo wa kuishinda Akili, tumepewa maarifa ya kukishinda kifaa hiki, kwanza kwa kujulishwa wewe na hicho kifaa ni tafauti, ndio maana ukaambiwa wewe unakiona kitu hicho, na una uwezo wa kukitumia usiache kikakutumia.
Sasa nini tumepewa ili ufike au urudi kwenye Taa yako ya fahamu, itabidi tuchukue mbinu hii ya Quraan ili tupate mafanikio ya kuitawala hii Akili badala ya Akili kututawala sisi, Napenda ufahamu ukitawaliwa na akili unakuwa mteja(addicted)na ukiitawala Akili unakua Mcha Mungu, hiyo ndio tafauti yake.Ndio maana tunajikuta huyu mteja wa mazungumzo, yule mteja wa wanawake, huyu mteja wa mali, mwengine yeye hafurahi mpaka agombane, mwengine mteja wa kuumwa tu haipiti siku bila ya kujipa maradhi, wengine wao wagonjwa wa (facebook)hiyo ndio Akili ilivyo ikikosa Balance, wengine wanataka wale tu akiona chakula hajiwezi, kuna maradhi ya kusema uongo, balaa zimetushukia wanaadamu na hatujui tufanye nini.
Sasa namalizia kwa kutoa dawa ifanye dawa hii na maajabu yake yatakua kama alivosema Nabii Yussuf a.s.. Ufanye nini?.
kitu kimoja anza zoezi hili la kuitizama Nafsi yako kwa kila ufanyacho, tabia zetu wanaadamu tunatizama yanotokea nje ya Nafsi zetu, sasa fanya kinyume chake tazama yanotokea ndani ya nafsi yako, utaanza kuona miujiza kidogo kidogo inatokezea, ukikitizama chakula wakati unakula basi hutokula mpaka tumbo livimbe utafikia pahala nafsi itakwambia nishatosheka, ukiitizima akili yako utaona Traffic ya mambo yanavopita, wewe tizama usjiunge na Traffic, Mwanamke au Mwanamme anapita wewe itizame akili yako na (Action)zake, kidogo kidogo utaona uteja unaanza kupungua, ukimaliza kutizama kwa njia hiyo sasa ukikaa kitandani umefunga macho tizama takataka za chumbani, anza kusafisha mavumbi, kidogo kidogo utaona unaanza kupunguza mambo yaliyomo kwenye chumba chako cha mawazo, kumbuka mambo yote yameingia kwa njia ya kutizama, na tumia njia hiyo ya kutizama ili uyatoe yote yalojaa kwenye Nafsi yako, mpaka ndoto za kipumbavu zinatoweka, taratibu utaona mwanga wa Taa yako ya Fahamu unaanza kuchomoza, na siku ambayo Taa itamurika chumba kizima siku hiyo ndio siku ya Rehma, ambapo akili inakukabidhi utawala wako unakua wewe ndio Mfalme wa nafsi yako, utakua kama mfano wa Nabii Yusuf a.s Mwanamke anakuja unakimbilia mlangoni na kanzu yako inachanwa kwa nyuma. ukifikia daraja hiyo elewa na Mollah wako anakusamehe madhanbi yako na hapo unaanza kuufahamu Ulimwengu huu vyengine kabisa, Akili ikaapo pembeni kila kitu unakiona kwa kutumia Nuru yako ya Fahamu, kama ulivokua utotoni ulipokua unaanza kupata Fahamu, kila kitu Miujiza, iwashe tena Taa hiyo na yote yalopita yatakua (History).
Kumbuka kutizama, kwanini nikasema kutizama na sio kuona, kwa sababu kutizama uko mbali na kuona uko karibu, na ukiwa karibu lazima ujiunge, "Waswahili wanasema utamu wa ngoma kucheza ukizunguka raha zimezidi" kwa hiyo na wewe usicheze utakuja kuzunguka, na ukizunguka hutoki kwenye duara, itakua unakera unafanya unatubu, unafanya tena unatubu, haina faida yoyote unateseka mpaka unaondoka kwenye Ulimwengu huu, utakuja kufufuliwa uteswe tena, hakuna atopata tabu isipokua wewe, unapewa njia itumie ili upate faida ya kurehemewa na Mollah wako. Hicho chumba nilichokitaja ni hiyo (Mind) ambayo uloijenga ukawa unaingia na kutoka, siku (Mind) itakaposita utabakiwa na (Brain) na Taa yako, hapo tena utakua Muhsin, Mja Mwema, kumbuka Mambo mema yanayafuta mabaya na huko ndio kusamehewa.
Sasa nini ufanye Kiumbe wewe, Kumbuka Mwanaadamu una vitendea Kazi vitu viwili, Kimoja katika hivyo hakiguswi na chochote, hakuna jambo lolote linaloweza kufikia kitu hicho ambacho ndio hiyo Taa ya Fahamu(Pure Soul). Kama Mwanaadamu utakua unakitumia kifaa hiki au nikipe heshima kwa sababu ni kitu kitakatifu(Roho)kwa uerevu, basi daima utakua umo furahani, kwanini nikasema umo kwa sababu (Roho)(Nature)yake ni Furaha(Nisiseme hivi Mkasema kasema anaijua roho kitu hicho hakijulikani), lakini hasara yetu Wanaadamu Tunaishi au kutawaliwa na hicho chengine chenye kutupeleka kwenye kiza, kipi hicho?.
Akili(Hii ni sehemu ya Nafsi) ni nyenzo ambayo tunatakiwa kuitumia kwa uangalifu kwani ni (Very Powerful weapon)silaha kubwa sana, ukimilikiwa na Akili Binaadamu umekwisha, huna (Control) ya maisha yako kabisa.
Kwa sababu Akili inafanya kazi yake ya kukusanya, kupokea na kutupa kwenye hicho chumba, chumba hiki kiite (Memory or Subconscious)na kwa kuwa lolote lile lilopita kwenye taa yako ya Fahamu kumbuka liko humo chumbani umeliweka na wala halitoki, Sasa nini kinatokezea kuna baadhi ya nyakati Taa inawaka na kumurika yale mambo yaliyomo kwenye chumba iwe chuki, hasada, uzinifu, wizi, na ukimurika tu likija juu lazima ulitende kwa sababu hujalitupa ila umeliweka akiba, kwa hiyo tahadhari sana unapokwenda kwenye chumba chako, utakua unatenda mambo bila ya kukusudia, sasa kwa kuwa mambo yana kukera ndio unaamua kuzima Taa, na huku watu wanatumia ule msemo kajitoa fahamu.
Quraan imekuhurumia imesema unaleta nyudhuru yaani unazima Taa, ndio ikaendelea kukumbusha kuwa Mwanaadamu ni Mwenye kuiona Nafsi yake, ikimaanisha unao uwezo wa kuishinda Akili, tumepewa maarifa ya kukishinda kifaa hiki, kwanza kwa kujulishwa wewe na hicho kifaa ni tafauti, ndio maana ukaambiwa wewe unakiona kitu hicho, na una uwezo wa kukitumia usiache kikakutumia.
Sasa nini tumepewa ili ufike au urudi kwenye Taa yako ya fahamu, itabidi tuchukue mbinu hii ya Quraan ili tupate mafanikio ya kuitawala hii Akili badala ya Akili kututawala sisi, Napenda ufahamu ukitawaliwa na akili unakuwa mteja(addicted)na ukiitawala Akili unakua Mcha Mungu, hiyo ndio tafauti yake.Ndio maana tunajikuta huyu mteja wa mazungumzo, yule mteja wa wanawake, huyu mteja wa mali, mwengine yeye hafurahi mpaka agombane, mwengine mteja wa kuumwa tu haipiti siku bila ya kujipa maradhi, wengine wao wagonjwa wa (facebook)hiyo ndio Akili ilivyo ikikosa Balance, wengine wanataka wale tu akiona chakula hajiwezi, kuna maradhi ya kusema uongo, balaa zimetushukia wanaadamu na hatujui tufanye nini.
Sasa namalizia kwa kutoa dawa ifanye dawa hii na maajabu yake yatakua kama alivosema Nabii Yussuf a.s.. Ufanye nini?.
kitu kimoja anza zoezi hili la kuitizama Nafsi yako kwa kila ufanyacho, tabia zetu wanaadamu tunatizama yanotokea nje ya Nafsi zetu, sasa fanya kinyume chake tazama yanotokea ndani ya nafsi yako, utaanza kuona miujiza kidogo kidogo inatokezea, ukikitizama chakula wakati unakula basi hutokula mpaka tumbo livimbe utafikia pahala nafsi itakwambia nishatosheka, ukiitizima akili yako utaona Traffic ya mambo yanavopita, wewe tizama usjiunge na Traffic, Mwanamke au Mwanamme anapita wewe itizame akili yako na (Action)zake, kidogo kidogo utaona uteja unaanza kupungua, ukimaliza kutizama kwa njia hiyo sasa ukikaa kitandani umefunga macho tizama takataka za chumbani, anza kusafisha mavumbi, kidogo kidogo utaona unaanza kupunguza mambo yaliyomo kwenye chumba chako cha mawazo, kumbuka mambo yote yameingia kwa njia ya kutizama, na tumia njia hiyo ya kutizama ili uyatoe yote yalojaa kwenye Nafsi yako, mpaka ndoto za kipumbavu zinatoweka, taratibu utaona mwanga wa Taa yako ya Fahamu unaanza kuchomoza, na siku ambayo Taa itamurika chumba kizima siku hiyo ndio siku ya Rehma, ambapo akili inakukabidhi utawala wako unakua wewe ndio Mfalme wa nafsi yako, utakua kama mfano wa Nabii Yusuf a.s Mwanamke anakuja unakimbilia mlangoni na kanzu yako inachanwa kwa nyuma. ukifikia daraja hiyo elewa na Mollah wako anakusamehe madhanbi yako na hapo unaanza kuufahamu Ulimwengu huu vyengine kabisa, Akili ikaapo pembeni kila kitu unakiona kwa kutumia Nuru yako ya Fahamu, kama ulivokua utotoni ulipokua unaanza kupata Fahamu, kila kitu Miujiza, iwashe tena Taa hiyo na yote yalopita yatakua (History).
Kumbuka kutizama, kwanini nikasema kutizama na sio kuona, kwa sababu kutizama uko mbali na kuona uko karibu, na ukiwa karibu lazima ujiunge, "Waswahili wanasema utamu wa ngoma kucheza ukizunguka raha zimezidi" kwa hiyo na wewe usicheze utakuja kuzunguka, na ukizunguka hutoki kwenye duara, itakua unakera unafanya unatubu, unafanya tena unatubu, haina faida yoyote unateseka mpaka unaondoka kwenye Ulimwengu huu, utakuja kufufuliwa uteswe tena, hakuna atopata tabu isipokua wewe, unapewa njia itumie ili upate faida ya kurehemewa na Mollah wako. Hicho chumba nilichokitaja ni hiyo (Mind) ambayo uloijenga ukawa unaingia na kutoka, siku (Mind) itakaposita utabakiwa na (Brain) na Taa yako, hapo tena utakua Muhsin, Mja Mwema, kumbuka Mambo mema yanayafuta mabaya na huko ndio kusamehewa.
Sunday, October 2, 2016
MWANZO MAPENZI MWISHO MAPENZI PART 1
Asalaam Aleiykum
Siku zote inasomwa aya hii inosema:
وَإِذَا قُرِئَ ٱلۡقُرۡءَانُ فَٱسۡتَمِعُواْ لَهُ ۥ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na isomwapo Quraan isikilizeni, Nyamazeni ili mpate kurehemewa.
Watu wengi wamepata tafsiri tafauti na kusudio ya aya hii, wengine wanadhani kurehemewa hapo ni kupewa mali, au kupewa utajiri, na hili limetokana na Akili zetu kuzihusisha sana na mambo ya kipato, au biashara, ukifanya hivi utalipwa vile, Mwanaadamu unakua hupo kabisa unaambiwa kitu chengine unafahamu kitu chengine, Unaambiwa lete (Kawa)unaleta kahawa, huko kabisa mawazo yapo kwengine, ndio maana mkaambiwa itakaposomwa isikilizeni, halafu nyamazeni, kwanini yakasemwa maneno hayo kwa sababu kusikiliza ni jambo jengine na kunyamaza pia ni jambo jengine, lazima uyaunganishe mawili haya ndio unaipata hiyo Rehma, unaipata hiyo Fahamu, lakini kama hujayaunganisha mawili haya matokeo ndio yanakua hayo ya (Kawa na Kahawa).
maana ya kusikiliza ni tendo ambalo huna (Miliki nalo)unasikia kila jambo, lakini maana ya kunyamaza ni kuwa unakua (empty) katika (Mind)yako, kimya unasikiliza kitu hususia, na hapo kitu chenyewe ni hayo maneno ya ndani ya Quraan, na Rehma yenyewe ni hiyo fahamu, lakini wale wenye kusikiliza bila ya kufahamu inakua Rehma haifiki, unaishia kupenda sauti, unaishia kupenda anavosoma, hasara ilioje kuikosa Rehma ya kitabu cha Mwenye enzi Mungu. Bwana Mtume s.a.w anaambiwa nini?(Muzzamil aya ya 5)"إِنَّا سَنُلۡقِى عَلَيۡكَ قَوۡلاً۬ ثَقِيلاً ".
"Hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito".
Sasa maneno yashateremka unaambiwa tulia uyasikilize ili urehemewe, kurehemewa kwenyewe kukoje, kuko hivi, katika kupewa Sheria na Muongozo, kupewa Dawa ndani ya maneno hayo, kujazwa Imani katika nyoyo yako, na mengi yalojificha makubwa makubwa ambayo huyajui, na ndio ukaambiwa tulia ufunguliwe mambo, poa upewe maana, wacha kelele upewe code za mambo zimo ndani ya Quraan, lakini wapi, nani anaye sikiliza, wangapi wenye kuipata maana ya ndani ya Kitabu hichi, hutowakuta ila wachache sana.
Sasa vipi utajua kuwa Rehma imekuteremkia?Pale itakaposomwa aya ima iwe kwenye Sala au venginevyo, Na wewe ukawa nje unasikiza ndani umetulia hakuna hadith za ajabu zinaingia mawazoni, hakuna biashara unafanya kwenye Akili, ndio pale itakaposomwa aya mfano wa hii sura ya (Rumi aya ya 21)
وَمِنۡ ءَايَـٰتِهِۦۤ أَنۡ خَلَقَ لَكُم مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ أَزۡوَٲجً۬ا لِّتَسۡكُنُوٓاْ إِلَيۡهَا وَجَعَلَ بَيۡنَڪُم مَّوَدَّةً۬ وَرَحۡمَةًۚ إِنَّ فِى ذَٲلِكَ لَأَيَـٰتٍ۬ لِّقَوۡمٍ۬ يَتَفَكَّرُونَ
"Na Katika Ishara zake(Za kuonesha Mapenzi yake juu yenu)ni kuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsi yenu ili mupate utulivu kwao, naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu, Bila shaka katika haya zimo ishara kwa watu wanaofikiri".
Mwanzo Mapenzi Mwisho Mapenzi.
endelea part 2
Siku zote inasomwa aya hii inosema:
وَإِذَا قُرِئَ ٱلۡقُرۡءَانُ فَٱسۡتَمِعُواْ لَهُ ۥ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na isomwapo Quraan isikilizeni, Nyamazeni ili mpate kurehemewa.
Watu wengi wamepata tafsiri tafauti na kusudio ya aya hii, wengine wanadhani kurehemewa hapo ni kupewa mali, au kupewa utajiri, na hili limetokana na Akili zetu kuzihusisha sana na mambo ya kipato, au biashara, ukifanya hivi utalipwa vile, Mwanaadamu unakua hupo kabisa unaambiwa kitu chengine unafahamu kitu chengine, Unaambiwa lete (Kawa)unaleta kahawa, huko kabisa mawazo yapo kwengine, ndio maana mkaambiwa itakaposomwa isikilizeni, halafu nyamazeni, kwanini yakasemwa maneno hayo kwa sababu kusikiliza ni jambo jengine na kunyamaza pia ni jambo jengine, lazima uyaunganishe mawili haya ndio unaipata hiyo Rehma, unaipata hiyo Fahamu, lakini kama hujayaunganisha mawili haya matokeo ndio yanakua hayo ya (Kawa na Kahawa).
maana ya kusikiliza ni tendo ambalo huna (Miliki nalo)unasikia kila jambo, lakini maana ya kunyamaza ni kuwa unakua (empty) katika (Mind)yako, kimya unasikiliza kitu hususia, na hapo kitu chenyewe ni hayo maneno ya ndani ya Quraan, na Rehma yenyewe ni hiyo fahamu, lakini wale wenye kusikiliza bila ya kufahamu inakua Rehma haifiki, unaishia kupenda sauti, unaishia kupenda anavosoma, hasara ilioje kuikosa Rehma ya kitabu cha Mwenye enzi Mungu. Bwana Mtume s.a.w anaambiwa nini?(Muzzamil aya ya 5)"إِنَّا سَنُلۡقِى عَلَيۡكَ قَوۡلاً۬ ثَقِيلاً ".
"Hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito".
Sasa maneno yashateremka unaambiwa tulia uyasikilize ili urehemewe, kurehemewa kwenyewe kukoje, kuko hivi, katika kupewa Sheria na Muongozo, kupewa Dawa ndani ya maneno hayo, kujazwa Imani katika nyoyo yako, na mengi yalojificha makubwa makubwa ambayo huyajui, na ndio ukaambiwa tulia ufunguliwe mambo, poa upewe maana, wacha kelele upewe code za mambo zimo ndani ya Quraan, lakini wapi, nani anaye sikiliza, wangapi wenye kuipata maana ya ndani ya Kitabu hichi, hutowakuta ila wachache sana.
Sasa vipi utajua kuwa Rehma imekuteremkia?Pale itakaposomwa aya ima iwe kwenye Sala au venginevyo, Na wewe ukawa nje unasikiza ndani umetulia hakuna hadith za ajabu zinaingia mawazoni, hakuna biashara unafanya kwenye Akili, ndio pale itakaposomwa aya mfano wa hii sura ya (Rumi aya ya 21)
وَمِنۡ ءَايَـٰتِهِۦۤ أَنۡ خَلَقَ لَكُم مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ أَزۡوَٲجً۬ا لِّتَسۡكُنُوٓاْ إِلَيۡهَا وَجَعَلَ بَيۡنَڪُم مَّوَدَّةً۬ وَرَحۡمَةًۚ إِنَّ فِى ذَٲلِكَ لَأَيَـٰتٍ۬ لِّقَوۡمٍ۬ يَتَفَكَّرُونَ
"Na Katika Ishara zake(Za kuonesha Mapenzi yake juu yenu)ni kuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsi yenu ili mupate utulivu kwao, naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu, Bila shaka katika haya zimo ishara kwa watu wanaofikiri".
Mwanzo Mapenzi Mwisho Mapenzi.
endelea part 2
MWANZO MAPENZI MWISHO MAPENZI PATR 2
Asalaam Aleiykum
Sasa swali la kujiuliza au kutafakari ni hili iwapo pamesemwa "Amejaalia mapenzi na huruma baina yenu" nini habari yetu sisi kuhusu haya maisha yote tunayoishi katika "Ulimwengu huu", ukenda (Deep)Ndani kabisa utagundua kule Kuumbwa kwenyewe kwetu sisi kumetokana na Mapenzi ya Mollah wetu, kwani hujasoma aya iliyomo kwenye sura ya (Insaan aya 1)
هَلۡ أَتَىٰ عَلَى ٱلۡإِنسَـٰنِ حِينٌ۬ مِّنَ ٱلدَّهۡرِ لَمۡ يَكُن شَيۡـًٔ۬ا مَّذۡكُورًا
Hakika ulimpitia Mwanaadamu wakati mrefu katika dahari, hakuwa katika kitu kinachotajwa.
Hali kama hiyo wewe inakuhusu, Jikumbushe pale wazee wako wawili walipofanya maridhiano ya kufunga ndoa Mapenzi yakawateremkia na kukutana katika godoro la mapenzi, nini kilitokezea, kilotokezea hapo ni hiyo (Rehma)ambayo ni wewe, na ndio hiyo(Product of Love).
إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٍ۬ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَـٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا
"Kwa Hakika tumemuumba Mwanaadamu (Mtu)kutokana na mbegu ya Uhai iliyochanganyika,(Ya Mwanaume na Mwanamke)Na Tukamfanya Mwenye kusikia na kuona."
Kwa hiyo Wewe ni matunda ya mapenzi, ndio maana wakati mwengine unajihisi mapenzi na wakati mwengine umejaa chuki, (You are Both)Kama utatafakari utaziona hali zote hizo mbili zikikutokezea, yaani una urithi wa jinsia zote mbili, unageuka wakati(mara mama yako, mara baba yako)Jiangalie.
Nini cha kuangalia zaidi kitachokupa Afya na Furaha ni ile hali ya kukumbuka kuwa wewe ni (Full of Love) hiyo ndio (Nature)yako, ukiona mambo ya chuki, ufisadi unakuzungukia toka haraka sana katika hali hiyo, na hiyo ndio itakua dawa yako.
Kwani wewe hukumbuki Umelelewa kwa mapenzi, umeshawahi kujiuliza chanzo cha mapenzi hayo kimetokea wapi?. Majibu yapo kwenye sura ya (Taha aya ya 39)"وَأَلۡقَيۡتُ عَلَيۡكَ مَحَبَّةً۬ مِّنِّى وَلِتُصۡنَعَ عَلَىٰ عَيۡنِىٓ "Na nimekutilia Mapenzi yanaotokana kwangu, na ili ulelewe machoni mwangu, (Maneno hayo anaambiwa Nabii Musa a.s lakini kila mmoja wetu alopita kwenye Ulimwengu huu yanamgusa." Na hivi ndio kila mmoja wetu anavolelewa kwa mapenzi makubwa, Analelewa mtu kwa bawa la huruma, wazazi hawalali usiku kucha, ukiumwa wanahangaika ili wakupe dawa upone, ikisha ukitimia umri wa kuweza kutembea na kujitegemea Mwenyewe hapo wanakuacha kwenye uangalizi wa miujiza utokao kwa Mollah wako.
إِن كُلُّ نَفۡسٍ۬ لَّمَّا عَلَيۡہَا حَافِظٌ۬
"Hakuna Nafsi yoyote ila inayo mchungaji juu yake".
Ulipofika Umri wa kuachiwa huru unapata ulinzi mwengine wa yule aliyeumba mapenzi na kukuletea mchungaji(Malaika)unaambiwa kwa njia usizofahamu hapa usende, kule usipite, gari hii usipande, unanusuriwa na kila mabaya na mabalaa pasi na wewe kuyajua, yote hayo yanafanyika ndani ya kivuli cha mapenzi, "ewe binaadamu upendwe vipi ujijue unapendwa".
Mwanzo Mapenzi Mwisho Mapenzi.
Endelea part 3
Sasa swali la kujiuliza au kutafakari ni hili iwapo pamesemwa "Amejaalia mapenzi na huruma baina yenu" nini habari yetu sisi kuhusu haya maisha yote tunayoishi katika "Ulimwengu huu", ukenda (Deep)Ndani kabisa utagundua kule Kuumbwa kwenyewe kwetu sisi kumetokana na Mapenzi ya Mollah wetu, kwani hujasoma aya iliyomo kwenye sura ya (Insaan aya 1)
هَلۡ أَتَىٰ عَلَى ٱلۡإِنسَـٰنِ حِينٌ۬ مِّنَ ٱلدَّهۡرِ لَمۡ يَكُن شَيۡـًٔ۬ا مَّذۡكُورًا
Hakika ulimpitia Mwanaadamu wakati mrefu katika dahari, hakuwa katika kitu kinachotajwa.
Hali kama hiyo wewe inakuhusu, Jikumbushe pale wazee wako wawili walipofanya maridhiano ya kufunga ndoa Mapenzi yakawateremkia na kukutana katika godoro la mapenzi, nini kilitokezea, kilotokezea hapo ni hiyo (Rehma)ambayo ni wewe, na ndio hiyo(Product of Love).
إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٍ۬ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَـٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا
"Kwa Hakika tumemuumba Mwanaadamu (Mtu)kutokana na mbegu ya Uhai iliyochanganyika,(Ya Mwanaume na Mwanamke)Na Tukamfanya Mwenye kusikia na kuona."
Kwa hiyo Wewe ni matunda ya mapenzi, ndio maana wakati mwengine unajihisi mapenzi na wakati mwengine umejaa chuki, (You are Both)Kama utatafakari utaziona hali zote hizo mbili zikikutokezea, yaani una urithi wa jinsia zote mbili, unageuka wakati(mara mama yako, mara baba yako)Jiangalie.
Nini cha kuangalia zaidi kitachokupa Afya na Furaha ni ile hali ya kukumbuka kuwa wewe ni (Full of Love) hiyo ndio (Nature)yako, ukiona mambo ya chuki, ufisadi unakuzungukia toka haraka sana katika hali hiyo, na hiyo ndio itakua dawa yako.
Kwani wewe hukumbuki Umelelewa kwa mapenzi, umeshawahi kujiuliza chanzo cha mapenzi hayo kimetokea wapi?. Majibu yapo kwenye sura ya (Taha aya ya 39)"وَأَلۡقَيۡتُ عَلَيۡكَ مَحَبَّةً۬ مِّنِّى وَلِتُصۡنَعَ عَلَىٰ عَيۡنِىٓ "Na nimekutilia Mapenzi yanaotokana kwangu, na ili ulelewe machoni mwangu, (Maneno hayo anaambiwa Nabii Musa a.s lakini kila mmoja wetu alopita kwenye Ulimwengu huu yanamgusa." Na hivi ndio kila mmoja wetu anavolelewa kwa mapenzi makubwa, Analelewa mtu kwa bawa la huruma, wazazi hawalali usiku kucha, ukiumwa wanahangaika ili wakupe dawa upone, ikisha ukitimia umri wa kuweza kutembea na kujitegemea Mwenyewe hapo wanakuacha kwenye uangalizi wa miujiza utokao kwa Mollah wako.
إِن كُلُّ نَفۡسٍ۬ لَّمَّا عَلَيۡہَا حَافِظٌ۬
"Hakuna Nafsi yoyote ila inayo mchungaji juu yake".
Ulipofika Umri wa kuachiwa huru unapata ulinzi mwengine wa yule aliyeumba mapenzi na kukuletea mchungaji(Malaika)unaambiwa kwa njia usizofahamu hapa usende, kule usipite, gari hii usipande, unanusuriwa na kila mabaya na mabalaa pasi na wewe kuyajua, yote hayo yanafanyika ndani ya kivuli cha mapenzi, "ewe binaadamu upendwe vipi ujijue unapendwa".
Mwanzo Mapenzi Mwisho Mapenzi.
Endelea part 3
MWANZO MAPENZI MWISHO MAPENZI PART 3
Asalaam Aleiykum
Unapofikia kubaleghe au ujanani sio kuwa mapenzi hayo yanasita bali yanaendelea japokua unapita katika dhoruba za uharibifu wa maasi, unafanya ya kufanya bado mapenzi yanaendelea kumiminika kutoka kwa wazazi wako na kwa Mollah wako.
Ukiumwa Mollah wako anakuponesha, Anakupa riziki na mengineyo, huku wazee nao wanataabika kwa mapenzi wakitaka ushike njia ilonyooka. Kwa mapenzi hayo ukapambiwa Ulimwengu huu kila jambo zuri, ukatiliwa furaha ambayo unaishi nayo, jiangalie wewe ukiwa mgonjwa unaweza kuwa na furaha, ndio maana ukaambiwa unapewa Uhuru wa kuchagua ama shukuru kwa mapenzi haya au kufuru.
Vipi kushukuru?, jee unamkumbuka aliyekupa na kukufanyia mapenzi haya, una (share)mapenzi haya na wenzio, kwa kile unachopewa unakitoa, unaonea huruma wenzio, ama ukenda kinyume na hayo ndio huko kukufuru. Na kukufuru ni hiyo njia ya mateso, njia ya chuki, kwa ajili ya mapenzi ya Mollah wetu anatusubiria na kutuacha tuishi katika enzi yake ya mapenzi, ama wale wenye (gratitude)waloridhika na mapenzi ya Mollah wao, wao hawana shaka, wameridhika kwa kuumbwa kwao na kila walichopewa, Na kila linalokuja wako tayari wakijua linafanyika kwa ajili ya mapenzi ya Mwenye enzi Mungu, hakika walokufuru ni wale wenye kuyakataa mapenzi haya, wale wasoridhika na (Qadara) ya Mollah wao.
Na kwanini hawaridhiki hali wanapewa kupumzika wakichoka(Usingizi), wakishapumzika wanaamshwa ili waendelee na harakati za maisha, wakishikwa na njaa wanapewa chakula na riziki zao nyengine, wakishikwa na Kiu wanapewa maji, wanapewa uwezo wa kuona na kusikia, wakiumwa Mollah wao anawaponesha, Na ukizidi kumuasi husema asaa hawa viumbe wangu huwenda pengine wakarudi, lau ingekua si mapenzi ya Mollah wetu basi tungeangamia. Chukua mfano unamuasi Mollah wako kwa kulewa, "Tena unaimba ningekua na Pajero ningelewa Tirarira"Unalewa tirarira"Unaendesha Pajero lako, unafika nyumbani kwako Mollah wako anakutoa kwenye Pajero kwa usalama bila hata kuchuna kioo, unakwenda kwenye kitanda unalala na kuamka salama, basi hujijui kiumbe wewe kwamba unaishi ndani ya (Being of Love)Mapenzi.Na kila ukipindukia ukawa huogopi, na umefika katika umuri wa Utu uzima bado upo kwenye vilabu vya pombe, hutoki kwenye vikao vya Taarab, unaendelea kufanya maasi, Mollah wako anakwita kwa njia ya mapenzi, vipi?
قُلۡ يَـٰعِبَادِىَ ٱلَّذِينَ أَسۡرَفُواْ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡ لَا تَقۡنَطُواْ مِن رَّحۡمَةِ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ يَغۡفِرُ ٱلذُّنُوبَ جَمِيعًاۚ إِنَّهُ ۥ هُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ
"Sema "Enyi waja wangu Mlojidhulumu nafsi zenu msikate tamaa na Rehma ya Mwenye enzi Mungu, bila shaka Mwenye enzi Mungu husamehe dhanmbi zote, hakika yeye ni Mwingi wa kusamehe(Na)Mwingi wa kurehemu."
Kusamehe pekee mapenzi, kurehemewa ndio huo upole(Kindness)kunusuriwa na adhabu, mpaka Mwisho wa maisha yenu mapenzi yanakufateni, rehema zinakufateni, unachotakiwa ni kugeuka kidogo ukajiunga na hiyo (Gratitude)ili uwe katika walofuzu, jiunge na mapenzi ya Ulimwengu huu ili nawe uwe Mcha Mungu.
Sasa ikiwa hapo juu umeambiwa usikate tamaa hapa chini inafatia aya nyengine zilizomo kwenye sura ya (Fajr 27 mpaka 30)"Zina kuita kwa jina jengine, kule uliitwa (Abdi)hapa kwenye sura hii unaitwa Ewe Nafsi"uliyetua, Nafsi iliyotua ni ile yenye matumaini, Nafsi ambayo imekiri makosa yake na kukubali mazuri yake, ikarejea kwa Mollah wake hali ya kujua ima imefeli mitihani yake au imepasi, Na kwa ajili hiyo haina nafsi uwezo wa kufanya lolote ila kumuachia Mwenye enzi Mungu mwenye mapenzi ya kiumbe chake kumsamehe na kumuingiza na kumuweka na waja wema peponi.
Nini Matumaini?Matumaini ni (State of Gurantee)Ni hali ya kujiridhisha kisaikolijia, Kwa sababu hakuna Mwenye (Gurantee) isipokua kutoka kwa Mollah wako uliyopewa kwenye kitabu, na ukifikia mpaka kulijua hilo ina maana na wewe umo, unatakiwa katika safari hiyo, ambayo hakuna ajuae unakwenda wapi? nini kinatokea ukishafukiwa kwenye dongo, hesabu zako zimefichwa, pepo imefichwa, Moto umefichwa, Lakini kwa Mapenzi ya Mollah wetu matumaini kayaweka wazi, basi usikubali mtu yoyote ayachukue, sababu Mwenyewe alokuumba anakwambia rejea kipenzi changu, kwa sababu kutokana na mapenzi yangu wewe nimekuumba, kutokana na mapenzi yangu leo nakuchukua urejee nyumbani ulikotokea ndio maana umeitwa kwa jina la Nafsi, (sio Abdulla au jina jengine wewe Nafsi)leo rudi umeishi pengine kwa raha au dhiki, umeishi na maradhi au furaha basi rejea nyumbani uje kupumzika kama unavopumzika (Ukilala). Tena ondoa khofu ukiwa peke yako utakua (Boring)wewe unapenda (chit chat)kuzungumza basi ingia ukakutane na waja wema, hakuna mazungumzo ya kipuuzi tena huku ujako. Mwanzo Mapenzi mwisho Mapenzi, na kama utataka kinyume cha hayo Mapenzi ndio hiyo Dhiki tupu, mara wasiwasi, mara maradhi, mara hasira mara chuki, mara umehamaki, mara umenuna, Binaadamu jihadhari sana na kujitia maradhini, jitahidi kuyalea mapenzi na ndio hiyo (Taqwa).
Sasa utayajuaje hayo mapenzi? Mapenzi yenyewe ni haya maisha, Maisha ni zawadi kubwa Mwanaadamu alopewa na Mollah wake, ambayo unatakiwa uithamini. Jitahidi sana wakati unaishi kwenye Ulimwengu huu ishi na watu kwa mapenzi, ona raha kuwa umeamka mpaka unalala hujamkera Mollah wako, hujakera viumbe wenzako, hujaua hata kinyama, umeabudu kwa utulivu, ukiimaliza siku kwa njia hiyo jijue umo kwenye mapenzi, na hayo ndio matumaini ambayo yanakupa (gurantee)Bila ya khofu. Omba sana msamaha kwa ili uwe Mapenzini.
Unapofikia kubaleghe au ujanani sio kuwa mapenzi hayo yanasita bali yanaendelea japokua unapita katika dhoruba za uharibifu wa maasi, unafanya ya kufanya bado mapenzi yanaendelea kumiminika kutoka kwa wazazi wako na kwa Mollah wako.
Ukiumwa Mollah wako anakuponesha, Anakupa riziki na mengineyo, huku wazee nao wanataabika kwa mapenzi wakitaka ushike njia ilonyooka. Kwa mapenzi hayo ukapambiwa Ulimwengu huu kila jambo zuri, ukatiliwa furaha ambayo unaishi nayo, jiangalie wewe ukiwa mgonjwa unaweza kuwa na furaha, ndio maana ukaambiwa unapewa Uhuru wa kuchagua ama shukuru kwa mapenzi haya au kufuru.
Vipi kushukuru?, jee unamkumbuka aliyekupa na kukufanyia mapenzi haya, una (share)mapenzi haya na wenzio, kwa kile unachopewa unakitoa, unaonea huruma wenzio, ama ukenda kinyume na hayo ndio huko kukufuru. Na kukufuru ni hiyo njia ya mateso, njia ya chuki, kwa ajili ya mapenzi ya Mollah wetu anatusubiria na kutuacha tuishi katika enzi yake ya mapenzi, ama wale wenye (gratitude)waloridhika na mapenzi ya Mollah wao, wao hawana shaka, wameridhika kwa kuumbwa kwao na kila walichopewa, Na kila linalokuja wako tayari wakijua linafanyika kwa ajili ya mapenzi ya Mwenye enzi Mungu, hakika walokufuru ni wale wenye kuyakataa mapenzi haya, wale wasoridhika na (Qadara) ya Mollah wao.
Na kwanini hawaridhiki hali wanapewa kupumzika wakichoka(Usingizi), wakishapumzika wanaamshwa ili waendelee na harakati za maisha, wakishikwa na njaa wanapewa chakula na riziki zao nyengine, wakishikwa na Kiu wanapewa maji, wanapewa uwezo wa kuona na kusikia, wakiumwa Mollah wao anawaponesha, Na ukizidi kumuasi husema asaa hawa viumbe wangu huwenda pengine wakarudi, lau ingekua si mapenzi ya Mollah wetu basi tungeangamia. Chukua mfano unamuasi Mollah wako kwa kulewa, "Tena unaimba ningekua na Pajero ningelewa Tirarira"Unalewa tirarira"Unaendesha Pajero lako, unafika nyumbani kwako Mollah wako anakutoa kwenye Pajero kwa usalama bila hata kuchuna kioo, unakwenda kwenye kitanda unalala na kuamka salama, basi hujijui kiumbe wewe kwamba unaishi ndani ya (Being of Love)Mapenzi.Na kila ukipindukia ukawa huogopi, na umefika katika umuri wa Utu uzima bado upo kwenye vilabu vya pombe, hutoki kwenye vikao vya Taarab, unaendelea kufanya maasi, Mollah wako anakwita kwa njia ya mapenzi, vipi?
قُلۡ يَـٰعِبَادِىَ ٱلَّذِينَ أَسۡرَفُواْ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡ لَا تَقۡنَطُواْ مِن رَّحۡمَةِ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ يَغۡفِرُ ٱلذُّنُوبَ جَمِيعًاۚ إِنَّهُ ۥ هُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ
"Sema "Enyi waja wangu Mlojidhulumu nafsi zenu msikate tamaa na Rehma ya Mwenye enzi Mungu, bila shaka Mwenye enzi Mungu husamehe dhanmbi zote, hakika yeye ni Mwingi wa kusamehe(Na)Mwingi wa kurehemu."
Kusamehe pekee mapenzi, kurehemewa ndio huo upole(Kindness)kunusuriwa na adhabu, mpaka Mwisho wa maisha yenu mapenzi yanakufateni, rehema zinakufateni, unachotakiwa ni kugeuka kidogo ukajiunga na hiyo (Gratitude)ili uwe katika walofuzu, jiunge na mapenzi ya Ulimwengu huu ili nawe uwe Mcha Mungu.
Sasa ikiwa hapo juu umeambiwa usikate tamaa hapa chini inafatia aya nyengine zilizomo kwenye sura ya (Fajr 27 mpaka 30)"Zina kuita kwa jina jengine, kule uliitwa (Abdi)hapa kwenye sura hii unaitwa Ewe Nafsi"uliyetua, Nafsi iliyotua ni ile yenye matumaini, Nafsi ambayo imekiri makosa yake na kukubali mazuri yake, ikarejea kwa Mollah wake hali ya kujua ima imefeli mitihani yake au imepasi, Na kwa ajili hiyo haina nafsi uwezo wa kufanya lolote ila kumuachia Mwenye enzi Mungu mwenye mapenzi ya kiumbe chake kumsamehe na kumuingiza na kumuweka na waja wema peponi.
Nini Matumaini?Matumaini ni (State of Gurantee)Ni hali ya kujiridhisha kisaikolijia, Kwa sababu hakuna Mwenye (Gurantee) isipokua kutoka kwa Mollah wako uliyopewa kwenye kitabu, na ukifikia mpaka kulijua hilo ina maana na wewe umo, unatakiwa katika safari hiyo, ambayo hakuna ajuae unakwenda wapi? nini kinatokea ukishafukiwa kwenye dongo, hesabu zako zimefichwa, pepo imefichwa, Moto umefichwa, Lakini kwa Mapenzi ya Mollah wetu matumaini kayaweka wazi, basi usikubali mtu yoyote ayachukue, sababu Mwenyewe alokuumba anakwambia rejea kipenzi changu, kwa sababu kutokana na mapenzi yangu wewe nimekuumba, kutokana na mapenzi yangu leo nakuchukua urejee nyumbani ulikotokea ndio maana umeitwa kwa jina la Nafsi, (sio Abdulla au jina jengine wewe Nafsi)leo rudi umeishi pengine kwa raha au dhiki, umeishi na maradhi au furaha basi rejea nyumbani uje kupumzika kama unavopumzika (Ukilala). Tena ondoa khofu ukiwa peke yako utakua (Boring)wewe unapenda (chit chat)kuzungumza basi ingia ukakutane na waja wema, hakuna mazungumzo ya kipuuzi tena huku ujako. Mwanzo Mapenzi mwisho Mapenzi, na kama utataka kinyume cha hayo Mapenzi ndio hiyo Dhiki tupu, mara wasiwasi, mara maradhi, mara hasira mara chuki, mara umehamaki, mara umenuna, Binaadamu jihadhari sana na kujitia maradhini, jitahidi kuyalea mapenzi na ndio hiyo (Taqwa).
Sasa utayajuaje hayo mapenzi? Mapenzi yenyewe ni haya maisha, Maisha ni zawadi kubwa Mwanaadamu alopewa na Mollah wake, ambayo unatakiwa uithamini. Jitahidi sana wakati unaishi kwenye Ulimwengu huu ishi na watu kwa mapenzi, ona raha kuwa umeamka mpaka unalala hujamkera Mollah wako, hujakera viumbe wenzako, hujaua hata kinyama, umeabudu kwa utulivu, ukiimaliza siku kwa njia hiyo jijue umo kwenye mapenzi, na hayo ndio matumaini ambayo yanakupa (gurantee)Bila ya khofu. Omba sana msamaha kwa ili uwe Mapenzini.
Saturday, September 10, 2016
MAJAALIWA YA KUONA NA KUSIKIA PART 1
Asalaam Aleiykum
Zimekujia Fahamu za vitendo viwili hivi vya kuona na kusikia,
Umepata angalau kujua kwanini unaona?, na uwezo huu unatokea wapi, unaijua fadhila ya kusikia na uzuri wa jambo hilo?, na nini habari yako wewe kama moja katika hilo litaondoshwa utakua katika hali gani, Uwe wewe (Tajiri wakupindukia) ichukuliwe tu (Jaala)hii ya kuona au kusikia ujitizame vipi unakua, ushawahi wewe kuumwa macho yakawa hayaoni au masikio yameziba ukawa husikii japo kwa siku moja unakuaje, vitu kama hivi tunavichukulia ni kama jambo jepesi sana, tunachukulia kama tuna vimiliki vitu hivi wala hatuna wasiwasi hata wakujua vinatokea wapi na kwanini tunapewa?.
Unakumbuka lini wewe umewahi kuamka bila ya kukumbushwa ukamshukuru Mollah wako?, Ukashukuru tu Alhamdullilah(ahsante)Mollah wangu kwa kunipa tena siku hii ya leo kuona na kusikia, Imeshakufikia habari ile siku mambo mawili haya yatakapoondoshwa ukawa huoni wala husikii yaliyomo kwenye Ulimwengu huu. Basi ikiwa msahaulivu au una (Kiburi) fulani isome darsa hii upate kufungua macho yako, kwani wakati huu ulo nao macho yako wazi lakini hayaoni.
Napenda kukumbusha uelewe jambo hili la kuona na kusikia imekua katika ihsan kubwa Mollah wako alizokufanyia za kukufanya ukaribie Ufalme wake wakati ukiwa hai katika ulimwengu huu. Amekupa wewe (Sifat Basiran) Na akakuongezea (Wasifat Samian) Akakupa zaidi na (Sifa ya Aliim)Mwenye kujua, na pia kukupa wewe kiumbe hizo nguvu (Sifa ya Qawwiy) Amekupa mambo mengi nimeyataja hayo kwa uchache ili ujue vipi Mapenzi ya Mwenye enzi Mungu juu yako wewe Kiumbe. Kiumbe wewe huna malipo ila kumsahau, huna jengine isipokua ufisadi, Basi kabla ya kuzama kwenye Bahari hii ya kuona na kusikia wacha kwanza tuangalie nini kinatokea kabla ya kulala na kuondoshewa huko kuona na kusikia.
Endelea part 2
Zimekujia Fahamu za vitendo viwili hivi vya kuona na kusikia,
Umepata angalau kujua kwanini unaona?, na uwezo huu unatokea wapi, unaijua fadhila ya kusikia na uzuri wa jambo hilo?, na nini habari yako wewe kama moja katika hilo litaondoshwa utakua katika hali gani, Uwe wewe (Tajiri wakupindukia) ichukuliwe tu (Jaala)hii ya kuona au kusikia ujitizame vipi unakua, ushawahi wewe kuumwa macho yakawa hayaoni au masikio yameziba ukawa husikii japo kwa siku moja unakuaje, vitu kama hivi tunavichukulia ni kama jambo jepesi sana, tunachukulia kama tuna vimiliki vitu hivi wala hatuna wasiwasi hata wakujua vinatokea wapi na kwanini tunapewa?.
Unakumbuka lini wewe umewahi kuamka bila ya kukumbushwa ukamshukuru Mollah wako?, Ukashukuru tu Alhamdullilah(ahsante)Mollah wangu kwa kunipa tena siku hii ya leo kuona na kusikia, Imeshakufikia habari ile siku mambo mawili haya yatakapoondoshwa ukawa huoni wala husikii yaliyomo kwenye Ulimwengu huu. Basi ikiwa msahaulivu au una (Kiburi) fulani isome darsa hii upate kufungua macho yako, kwani wakati huu ulo nao macho yako wazi lakini hayaoni.
Napenda kukumbusha uelewe jambo hili la kuona na kusikia imekua katika ihsan kubwa Mollah wako alizokufanyia za kukufanya ukaribie Ufalme wake wakati ukiwa hai katika ulimwengu huu. Amekupa wewe (Sifat Basiran) Na akakuongezea (Wasifat Samian) Akakupa zaidi na (Sifa ya Aliim)Mwenye kujua, na pia kukupa wewe kiumbe hizo nguvu (Sifa ya Qawwiy) Amekupa mambo mengi nimeyataja hayo kwa uchache ili ujue vipi Mapenzi ya Mwenye enzi Mungu juu yako wewe Kiumbe. Kiumbe wewe huna malipo ila kumsahau, huna jengine isipokua ufisadi, Basi kabla ya kuzama kwenye Bahari hii ya kuona na kusikia wacha kwanza tuangalie nini kinatokea kabla ya kulala na kuondoshewa huko kuona na kusikia.
Endelea part 2
MAJAALIWA YA KUONA NA KUSIKIA PART 2
Asalaam Aleiykum
Nini Kinatokea?
Katika maumbile yako ya kawaida mambo haya yanatokea ikiwa hujijui au huyajui, Kimaumbile Tabia uliyoizoea ni kama ile ya taa, kuwaka na kuzimika, ila unaona ukisema hivyo watu watakushangaa kwa hiyo umechagua jina la kudumu unaita kulala na kuamka.
Lakini kama utakua Mwanasayansi wa dini basi utakuja kugundua Kulala huko na kuamka kwako kuna (Process)kubwa lazima uipitie ndio uvipate viwili hivyo na vyengine, Maajabu yanotokea hapo ni makubwa, ni taabu kuyaeleza unaweza kuyaona lakini inataka ifanyike jitihada kubwa kuyashuhudia, Inatakikana upatikane ustahamilivu wa hali ya juu kuiona hali hiyo yenye kutisha, hali ambayo ikikutokea inaambatana na khofu ya umauti.
Kuishuhudia hali hiyo kunahitaji maandalizi makubwa yenye kuambatana na ushujaa, sisemi ni rahisi yaweza kukuchukua miaka au miezi, au pengine masiku kadhaa tu ukaliona tukio hilo kwa ukamilifu, Na zaidi yategemea Majaaliwa na Ridhaa kutoka kwa Mollah wako.
Usije ukaona mbona huyu anazungumza Mambo ya ajabu, au analeta mafunzo mepya, mambo yapo, yametajwa ndani ya (Quraan fussilat aya ya 53)
سَنُرِيهِمۡ ءَايَـٰتِنَا فِى ٱلۡأَفَاقِ وَفِىٓ أَنفُسِہِمۡ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَهُمۡ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّۗ أَوَلَمۡ يَكۡفِ بِرَبِّكَ أَنَّهُ ۥ عَلَىٰ كُلِّ شَىۡءٍ۬ شَہِيدٌ
"Tutawaonesha (Ukweli)wa Alama zetu katika Nchi(Mbingu)za Mbali na katika Nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli. Je haikutoshi kwa Mollah wako kuwa yeye ni mjuzi wa kila kitu".
Wanasayansi wamekwenda kwanza (Nje)Mbinguni kama ilivosema (Quraan)Na Wacha Mungu wao wamekwenda kwanza ndani kwenye Nafsi kuipata Yakini, Na wewe nenda usiogope, hee mpaka unakufa hutaki kujua chochote cha upande wa pili.
Naam hivyo ndio hali ya mambo ilivyo, Sasa turudi nyuma ili tuendelee na darsa yetu ya kuona na kusikia.
Endelea part 3
Nini Kinatokea?
Katika maumbile yako ya kawaida mambo haya yanatokea ikiwa hujijui au huyajui, Kimaumbile Tabia uliyoizoea ni kama ile ya taa, kuwaka na kuzimika, ila unaona ukisema hivyo watu watakushangaa kwa hiyo umechagua jina la kudumu unaita kulala na kuamka.
Lakini kama utakua Mwanasayansi wa dini basi utakuja kugundua Kulala huko na kuamka kwako kuna (Process)kubwa lazima uipitie ndio uvipate viwili hivyo na vyengine, Maajabu yanotokea hapo ni makubwa, ni taabu kuyaeleza unaweza kuyaona lakini inataka ifanyike jitihada kubwa kuyashuhudia, Inatakikana upatikane ustahamilivu wa hali ya juu kuiona hali hiyo yenye kutisha, hali ambayo ikikutokea inaambatana na khofu ya umauti.
Kuishuhudia hali hiyo kunahitaji maandalizi makubwa yenye kuambatana na ushujaa, sisemi ni rahisi yaweza kukuchukua miaka au miezi, au pengine masiku kadhaa tu ukaliona tukio hilo kwa ukamilifu, Na zaidi yategemea Majaaliwa na Ridhaa kutoka kwa Mollah wako.
Usije ukaona mbona huyu anazungumza Mambo ya ajabu, au analeta mafunzo mepya, mambo yapo, yametajwa ndani ya (Quraan fussilat aya ya 53)
سَنُرِيهِمۡ ءَايَـٰتِنَا فِى ٱلۡأَفَاقِ وَفِىٓ أَنفُسِہِمۡ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَهُمۡ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّۗ أَوَلَمۡ يَكۡفِ بِرَبِّكَ أَنَّهُ ۥ عَلَىٰ كُلِّ شَىۡءٍ۬ شَہِيدٌ
"Tutawaonesha (Ukweli)wa Alama zetu katika Nchi(Mbingu)za Mbali na katika Nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli. Je haikutoshi kwa Mollah wako kuwa yeye ni mjuzi wa kila kitu".
Wanasayansi wamekwenda kwanza (Nje)Mbinguni kama ilivosema (Quraan)Na Wacha Mungu wao wamekwenda kwanza ndani kwenye Nafsi kuipata Yakini, Na wewe nenda usiogope, hee mpaka unakufa hutaki kujua chochote cha upande wa pili.
Naam hivyo ndio hali ya mambo ilivyo, Sasa turudi nyuma ili tuendelee na darsa yetu ya kuona na kusikia.
Endelea part 3
MAJAALIWA YA KUONA NA KUSIKIA PART 3
Asalaam Aleiykum
Siku zote nasisistiza uielewe sifa ya Jaala ni yenye kuja na kuondoka, Na sifa hii inatosha kukuthibitishia kuwa Kiama kipo na kinakuja, ima utakua hai siku hiyo au utafufuliwa lakini siku hiyo ipo na inathibitishwa na sifa hii ya Jaala. Basi yachunguze wewe mambo makubwa makubwa kuhusishwa na sifa ya (Temporary).
sifa kama zipi?(1)sura ya Nabaa,
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَـٰدً۬ا
Je hatukuifanya ardhi kuwa (kama)Tandiko. Sasa kwanini likaitwa tandiko, kwa sababu wakati mwengine tandiko linaondoshwa au kuwekwa pembeni, na hayo yanafanyika katika ardhi ima kwa kudidimia au kwa mtetemeko wa ardhi.
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتً۬ا
Na tukaufanya usingizi wenu kama kufa. Na aya hii ndio inaigusa aya yetu moja kwa moja kwa kuondoshwa hayo majaaliwa ya kuona na kusikia.Ikisha unarejeshewa mambo hayo.
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسً۬ا
Na tukaufanya Usiku kama guo(Mnalofunikwa)kama utazingatia nyakati za kuzama jua utaona vipi kiza kinavo kuvaa na kukuondoshea nuru ya kuona.
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّہَارَ مَعَاشً۬ا
Na Tukaufanya mchana Kama kufufuka. Hayo yanataka mazingatio pale mwanzo unaporejeshewa kuona na kusikia ndio utajua vipi inakua huko kuona na kusikia.
وَجَعَلۡنَا سِرَاجً۬ا وَهَّاجً۬ا
Na Tukaifanya taa ingarayo na yenye joto kubwa.hilo ndio Jua lenye kutupa vitamin na nyenzo zengine za maisha, kama chakula na kadhalika. Hayo ni machache ambayo ni (Temporary)huja na kuondoka kutokana na anavopanga Mollah wako.
Ukichunguza maneno yangu utagundua siku zote nasisitiza kuwa sifa hii ya jaala ni yenye kuja na kuondoka, Na ikiwa umepewa Akili ya mazingatio basi pia litakuongezea nguvu za imani yako pale utakapoona kumbe sifa hii pia imo kwenye nafsi yangu, Ukajua kumbe yupo Mwenye kunipa sifa hii ya kuona na kusikia.
إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٍ۬ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَـٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا
Hakika tumemuumba Mwanaadamu kutokana na mbegu ya Uhai iliyochanganyika,( ya Mwanamme na Mwanamke)ili tumfanyie mtihani, kwa hiyo tukamfanya Mwenye kusikia na Mwenye kuona.
Sasa inakuaje majaaliwa haya, Nini kinatokezea?.
Wacha nikuchukue kwenye safari hii ambayo unaiogopa sana lakini huna budi ni lazima uende, si umeambiwa tukaujaalia huo usingizi wao kama kufa, Basi wacha na sisi tuanzie hapo kuhusu yale mambo niloyataja huko mwanzo ambayo yanaondoshwa taratibu(Slow motion)au labda uwe umechoka ndio unazimika ghafla. Lakini (Process)za kawaida ziko, wacha nikupe mfano ili uone jambo gani la mwanzo hilo lenye kuondoshwa taratibu?kwenye hiyo (Process).
Basi Jitizame katika kusinzia utaona nguvu zinakuishia, ndio maana utaona kama umekaa unataka kama kuanguka,(Balance)huna, nguvu zinachukuliwa taratibu, Na Jambo la pili kuondoshwa ni huo uwezo wa kuona kidogo kidogo huo unaondoshwa mpaka kupotea.
Na jambo la tatu uwezo wa kusikia nao unaondoshwa ndio maana utaona chakacha au disco inapigwa yeye kalala anakoroma, "Wewe unashangaa sauti hii huyu anakoroma" kumbe mwenzio pale kama maiti, (Tukaujaalia usingizi wao kama kufa)unaendelea kushangaa ngoma hizi na sauti hii na huyu kalala chini ya (speaker)bado hasikii kitu huyu.
Na Jambo la Mwisho kuondoshwa ni hiyo (Knowing) au ita (consciousness), hapo tena Mwanaadamu unakua kama maiti. Sasa kwa wale Wacha Mungu au wanasayansi wa ndani wao wanafanya maandalizi na kuomba ridhaa ya Mollah wao ili wapewe uwezo wa kushuhudia (Process) yote hii huku wamebakishiwa hiyo (Knowing) au (Consciousness)vile vitatu vinatoweka hichi kimoja kinabakia na hiyo ni Fadhila kubwa kutoka kwa Mollah wao.
Ukijaaliwa kuipata hali kama hiyo unakua umefuzu katika Ulimwengu na huko uendako kwa Mollah wako.
Sasa nini Habari yetu sisi viumbe wa kawaida ukipata bahati ya kushuhudia, kama utakua makini ni rahisi kwako kushuhudia kuamka kwako, (Process) ni ile ile, ila sasa inakuja kinyume chake, katika kuamka lile liloondoka mwisho ndio lenye kuja mwanzo, Yaani hiyo (Knowing) au (Consciousness)au (Fahamu) Napenda uelewe wewe upo ila viloondoshwa ni hivyo vitendea kazi vya kuona na kusikia, kwanini nikasema wewe upo, kwa sababu jiulize nani Mwenye kuona ndoto, ukipata jawabu endelea kusoma ili upate faida zaidi, niliposema hili la (Kufufuliwa) ni rahisi kulipata nimekusudia wakati mwengine inakutokezea lile jambo la mwanzo la kujua(Knowing)linapokuja unazinduka ukawa hujui uko wapi, wewe nani?, Halafu jambo la pili linafatia ni kusikia, unasikia watu wanazungumza kwa mbali, halafu hapo tena inakuja kuona ikifatiwa na nguvu, ukiyapata hayo kama mja Mwema unaamka na Alhamdullilah, Nakushukuru Mollah wangu kwa kunijaalia uhai baada ya Mauti yangu.Kuna mambo mengine yenye faida nitayazungumza nini ufanye wakati unapata Rehma hii ya kuamka, huko siku za mbele nikijaaliwa.
Siku zote nasisistiza uielewe sifa ya Jaala ni yenye kuja na kuondoka, Na sifa hii inatosha kukuthibitishia kuwa Kiama kipo na kinakuja, ima utakua hai siku hiyo au utafufuliwa lakini siku hiyo ipo na inathibitishwa na sifa hii ya Jaala. Basi yachunguze wewe mambo makubwa makubwa kuhusishwa na sifa ya (Temporary).
sifa kama zipi?(1)sura ya Nabaa,
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَـٰدً۬ا
Je hatukuifanya ardhi kuwa (kama)Tandiko. Sasa kwanini likaitwa tandiko, kwa sababu wakati mwengine tandiko linaondoshwa au kuwekwa pembeni, na hayo yanafanyika katika ardhi ima kwa kudidimia au kwa mtetemeko wa ardhi.
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتً۬ا
Na tukaufanya usingizi wenu kama kufa. Na aya hii ndio inaigusa aya yetu moja kwa moja kwa kuondoshwa hayo majaaliwa ya kuona na kusikia.Ikisha unarejeshewa mambo hayo.
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسً۬ا
Na tukaufanya Usiku kama guo(Mnalofunikwa)kama utazingatia nyakati za kuzama jua utaona vipi kiza kinavo kuvaa na kukuondoshea nuru ya kuona.
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّہَارَ مَعَاشً۬ا
Na Tukaufanya mchana Kama kufufuka. Hayo yanataka mazingatio pale mwanzo unaporejeshewa kuona na kusikia ndio utajua vipi inakua huko kuona na kusikia.
وَجَعَلۡنَا سِرَاجً۬ا وَهَّاجً۬ا
Na Tukaifanya taa ingarayo na yenye joto kubwa.hilo ndio Jua lenye kutupa vitamin na nyenzo zengine za maisha, kama chakula na kadhalika. Hayo ni machache ambayo ni (Temporary)huja na kuondoka kutokana na anavopanga Mollah wako.
Ukichunguza maneno yangu utagundua siku zote nasisitiza kuwa sifa hii ya jaala ni yenye kuja na kuondoka, Na ikiwa umepewa Akili ya mazingatio basi pia litakuongezea nguvu za imani yako pale utakapoona kumbe sifa hii pia imo kwenye nafsi yangu, Ukajua kumbe yupo Mwenye kunipa sifa hii ya kuona na kusikia.
إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٍ۬ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَـٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا
Hakika tumemuumba Mwanaadamu kutokana na mbegu ya Uhai iliyochanganyika,( ya Mwanamme na Mwanamke)ili tumfanyie mtihani, kwa hiyo tukamfanya Mwenye kusikia na Mwenye kuona.
Sasa inakuaje majaaliwa haya, Nini kinatokezea?.
Wacha nikuchukue kwenye safari hii ambayo unaiogopa sana lakini huna budi ni lazima uende, si umeambiwa tukaujaalia huo usingizi wao kama kufa, Basi wacha na sisi tuanzie hapo kuhusu yale mambo niloyataja huko mwanzo ambayo yanaondoshwa taratibu(Slow motion)au labda uwe umechoka ndio unazimika ghafla. Lakini (Process)za kawaida ziko, wacha nikupe mfano ili uone jambo gani la mwanzo hilo lenye kuondoshwa taratibu?kwenye hiyo (Process).
Basi Jitizame katika kusinzia utaona nguvu zinakuishia, ndio maana utaona kama umekaa unataka kama kuanguka,(Balance)huna, nguvu zinachukuliwa taratibu, Na Jambo la pili kuondoshwa ni huo uwezo wa kuona kidogo kidogo huo unaondoshwa mpaka kupotea.
Na jambo la tatu uwezo wa kusikia nao unaondoshwa ndio maana utaona chakacha au disco inapigwa yeye kalala anakoroma, "Wewe unashangaa sauti hii huyu anakoroma" kumbe mwenzio pale kama maiti, (Tukaujaalia usingizi wao kama kufa)unaendelea kushangaa ngoma hizi na sauti hii na huyu kalala chini ya (speaker)bado hasikii kitu huyu.
Na Jambo la Mwisho kuondoshwa ni hiyo (Knowing) au ita (consciousness), hapo tena Mwanaadamu unakua kama maiti. Sasa kwa wale Wacha Mungu au wanasayansi wa ndani wao wanafanya maandalizi na kuomba ridhaa ya Mollah wao ili wapewe uwezo wa kushuhudia (Process) yote hii huku wamebakishiwa hiyo (Knowing) au (Consciousness)vile vitatu vinatoweka hichi kimoja kinabakia na hiyo ni Fadhila kubwa kutoka kwa Mollah wao.
Ukijaaliwa kuipata hali kama hiyo unakua umefuzu katika Ulimwengu na huko uendako kwa Mollah wako.
Sasa nini Habari yetu sisi viumbe wa kawaida ukipata bahati ya kushuhudia, kama utakua makini ni rahisi kwako kushuhudia kuamka kwako, (Process) ni ile ile, ila sasa inakuja kinyume chake, katika kuamka lile liloondoka mwisho ndio lenye kuja mwanzo, Yaani hiyo (Knowing) au (Consciousness)au (Fahamu) Napenda uelewe wewe upo ila viloondoshwa ni hivyo vitendea kazi vya kuona na kusikia, kwanini nikasema wewe upo, kwa sababu jiulize nani Mwenye kuona ndoto, ukipata jawabu endelea kusoma ili upate faida zaidi, niliposema hili la (Kufufuliwa) ni rahisi kulipata nimekusudia wakati mwengine inakutokezea lile jambo la mwanzo la kujua(Knowing)linapokuja unazinduka ukawa hujui uko wapi, wewe nani?, Halafu jambo la pili linafatia ni kusikia, unasikia watu wanazungumza kwa mbali, halafu hapo tena inakuja kuona ikifatiwa na nguvu, ukiyapata hayo kama mja Mwema unaamka na Alhamdullilah, Nakushukuru Mollah wangu kwa kunijaalia uhai baada ya Mauti yangu.Kuna mambo mengine yenye faida nitayazungumza nini ufanye wakati unapata Rehma hii ya kuamka, huko siku za mbele nikijaaliwa.
Monday, August 1, 2016
MAPENZI NI SIRI YAKO PART 1
Asalaam Aleiykum
Umepata kujiuliza kwanini mapenzi yakawa siri?. Jee unajua sababu yake?.Basi jiulize swali hili kwa njia ya kutaka kujua na hapo utakua umepanda mbegu ambayo haina kikomo katika kukua kwake, Haina mwisho katika kutoa Miti na Matunda yake. Napenda Uelewe nikizungumza neno Mapenzi sikusudii chembe yako ya mapenzi ya matamanio, sizungumzii upya wowote wa mapenzi unayo yafahamu wewe, au kama natoa (style)upate kupendwa na wanawake au wanaume, au wengine wakadhani natoa mbinu za upatikanaji wa mapenzi ya matamanio, hilo sio kusudio langu, kusudio langu ni kukufahamisha kuwa yapo mapenzi ya aina nyengine na kama utayapata daima utakua furahani, dhiki zitakuondoka, kila siku kwako itakua siku ya (Eid).
Mapenzi ninayokufahamisha leo ni jambo la siri, Kwanini ikawa siri kwa sababu ukiizungumza tu(Ushaipoteza) ladha yake inapotea, utamu wake unakatika, uchu wake unaondoka, kwa wale wenye kujua siri ya Mapenzi haya hawasemi chochote kwani wanajua siri ikisemwa inakua sio siri tena. Basi na mimi leo sitakwambia kwa uwazi hayo mapenzi ila ntaashiria ukakutane nayo Mwenyewe.
Basi kwanza ntakujulisha mapenzi uloyazoea ya Mwanamme na Mwanamke, au mapenzi ya kupenda nyumba yako, mapenzi ya kupenda farasi, gari na vitu vidogo vidogo ambavyo vimetajwa kwenye Quraan aya ya (14) Al-Imran.
زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ ٱلشَّهَوَٲتِ مِنَ ٱلنِّسَآءِ وَٱلۡبَنِينَ وَٱلۡقَنَـٰطِيرِ ٱلۡمُقَنطَرَةِ مِنَ ٱلذَّهَبِ وَٱلۡفِضَّةِ وَٱلۡخَيۡلِ ٱلۡمُسَوَّمَةِ وَٱلۡأَنۡعَـٰمِ وَٱلۡحَرۡثِۗ ذَٲلِكَ مَتَـٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَٱللَّهُ عِندَهُ ۥ حُسۡنُ ٱلۡمَـَٔابِ
"Watu wametiwa huba(Mapenzi)ya kupenda wanawake na watoto na marundi ya dhahabu na fedha, Na Farasi wanaotunzwa vizuri, na wanyama na mashamba, Na hayo ni (kwa ajili ya)matumizi ya maisha katika dunia, Na kwa Mwenye enzi Mungu ndiko kwenye marejeo mazuri"
Mapenzi yako ya aina mbili, aina ya kwanza ndio hiyo ilotajwa hapo juu ulotiwa nayo, unayo tayari, huwezi kuikwepa ni muhimu kwa ajili ya maisha yako ya kidunia, bila ya hivyo maisha yako yatakua kama maiti, upo tu duniani unakera watu, kila kitu kwako kibaya, kutokana huna hata hayo mapenzi ambayo ni haki yako kuwa nayo, ambayo Mollah kampa kila mja wake, wewe hata hilo hukupata, ukifikia hali kama hiyo inafaa ujiulize kwanini?.
Na aina ya pili ya Mapenzi ndio hiyo siri yenyewe, sasa kabla ya kwenda mbele hebu tuirejee aya tutizame, ikisha tujiulize kwanini ikataja Wanaume na sio wanawake?. Ikiwa wewe unanifatilia vizuri utagundua ama kwa Wanawake wanayo tayari (Nature) ya (Love)Mapenzi, Mwanamke kwake rahisi ku(surrender)yuradhi kukiri na kumtii mpenzi wake, hiyo ndio hulka ya Mwanamke, anatuonesha vipi mapenzi yake yalivo katika kuwalea na kuwapenda watoto wake, Mwanamke kajaa Moyo wa mapenzi, Mwanamke hana shaka katika penzi lake, na hajui hata inakuaje ila yeye kajaa mapenzi, ndio maana kwa Mwanamke rahisi kwake kwenda kwenye hilo penzi la siri.
Kwanini ikawa hivyo?
Kwa sababu Mwanamke Mapenzi kazaliwa nayo, Mapenzi yako Moyoni, Na hiyo ni siri yake wala haisemi, anao uwezo na ujuzi wa kumpenda Mtu akanyamaza kimya, Na hiyo ndio tunapata ishara ya siri ya Mapenzi (alopewa mwanamke).
Ama kuhusu Mwanamme(Yeye alotiwa)Penzi, Penzi hilo lipo (Kichwani) na wala sio moyoni, Ndio maana "Mwanamme mara huku mara kule", Mara kapenda hichi mara kapenda kile, na hiyo ndio tafauti yao. Kwa hiyo kawaida hiyo inatujulisha Mwanamke yeye yuko tayari kuchupa kwenye Bahari ya Mapenzi ya siri, Ndio maana utaona wao hawendi vitani, (Wao sio Violence) kwa hiyo katika kwenda kwenye Penzi la siri Mwanamke yeye njia yake ni(One Way)(from the heart to the beyond). Lakini Mwanamme yeye ni (Two way)Lazima urudi chini, lazima utoke kwenye kichwa uende moyoni, lazima upate (Faminine Quality).
Ndio Maana utaona "Wacha Mungu"wapole, (Very Loving).
Kwa Mungu hakutakiwi Ujabali, Kwa Mungu hakutakiwi Kuua, Hakutakiwi(Violence)huko ni salama juu ya salama, hakutakiwi chuki, Hakutakiwi hamaki wala hasira.
Sasa leo wacha nikushike mkono labda utachupa na mimi kwenye hiyo bahari ya Mapenzi ya siri ili na wewe upate neema yake. Lakini ili usije ukaweka tamaa au kupanda kiburi kuwa utafanikiwa itabidi nikujulishe kuwa mapenzi haya wanayapata watu wa aina mbili kama ilivosema Quraan sura ya (Fussilat aya ya 34 na 35)
وَلَا تَسۡتَوِى ٱلۡحَسَنَةُ وَلَا ٱلسَّيِّئَةُۚ ٱدۡفَعۡ بِٱلَّتِى هِىَ أَحۡسَنُ فَإِذَا ٱلَّذِى بَيۡنَكَ وَبَيۡنَهُ ۥ عَدَٲوَةٌ۬ كَأَنَّهُ ۥ وَلِىٌّ حَمِيمٌ۬
Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa, ondosha (ubaya unaofanyiwa kwa mema)tahamaki yule ambaye baina yake kuna uadui atakua kama ni jamaa (Yako)mwenye kukufia uchungu.
وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ذُو حَظٍّ عَظِيمٍ۬
Lakini (Jambo hili)hawatapewa ila wale wanaosubiri, wala hawatapewa ila wenye hadhi (Bahati)kubwa (Kwa Mwenye enzi Mungu)
Ipate maana ya maneno haya katika part 2
Umepata kujiuliza kwanini mapenzi yakawa siri?. Jee unajua sababu yake?.Basi jiulize swali hili kwa njia ya kutaka kujua na hapo utakua umepanda mbegu ambayo haina kikomo katika kukua kwake, Haina mwisho katika kutoa Miti na Matunda yake. Napenda Uelewe nikizungumza neno Mapenzi sikusudii chembe yako ya mapenzi ya matamanio, sizungumzii upya wowote wa mapenzi unayo yafahamu wewe, au kama natoa (style)upate kupendwa na wanawake au wanaume, au wengine wakadhani natoa mbinu za upatikanaji wa mapenzi ya matamanio, hilo sio kusudio langu, kusudio langu ni kukufahamisha kuwa yapo mapenzi ya aina nyengine na kama utayapata daima utakua furahani, dhiki zitakuondoka, kila siku kwako itakua siku ya (Eid).
Mapenzi ninayokufahamisha leo ni jambo la siri, Kwanini ikawa siri kwa sababu ukiizungumza tu(Ushaipoteza) ladha yake inapotea, utamu wake unakatika, uchu wake unaondoka, kwa wale wenye kujua siri ya Mapenzi haya hawasemi chochote kwani wanajua siri ikisemwa inakua sio siri tena. Basi na mimi leo sitakwambia kwa uwazi hayo mapenzi ila ntaashiria ukakutane nayo Mwenyewe.
Basi kwanza ntakujulisha mapenzi uloyazoea ya Mwanamme na Mwanamke, au mapenzi ya kupenda nyumba yako, mapenzi ya kupenda farasi, gari na vitu vidogo vidogo ambavyo vimetajwa kwenye Quraan aya ya (14) Al-Imran.
زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ ٱلشَّهَوَٲتِ مِنَ ٱلنِّسَآءِ وَٱلۡبَنِينَ وَٱلۡقَنَـٰطِيرِ ٱلۡمُقَنطَرَةِ مِنَ ٱلذَّهَبِ وَٱلۡفِضَّةِ وَٱلۡخَيۡلِ ٱلۡمُسَوَّمَةِ وَٱلۡأَنۡعَـٰمِ وَٱلۡحَرۡثِۗ ذَٲلِكَ مَتَـٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَٱللَّهُ عِندَهُ ۥ حُسۡنُ ٱلۡمَـَٔابِ
"Watu wametiwa huba(Mapenzi)ya kupenda wanawake na watoto na marundi ya dhahabu na fedha, Na Farasi wanaotunzwa vizuri, na wanyama na mashamba, Na hayo ni (kwa ajili ya)matumizi ya maisha katika dunia, Na kwa Mwenye enzi Mungu ndiko kwenye marejeo mazuri"
Mapenzi yako ya aina mbili, aina ya kwanza ndio hiyo ilotajwa hapo juu ulotiwa nayo, unayo tayari, huwezi kuikwepa ni muhimu kwa ajili ya maisha yako ya kidunia, bila ya hivyo maisha yako yatakua kama maiti, upo tu duniani unakera watu, kila kitu kwako kibaya, kutokana huna hata hayo mapenzi ambayo ni haki yako kuwa nayo, ambayo Mollah kampa kila mja wake, wewe hata hilo hukupata, ukifikia hali kama hiyo inafaa ujiulize kwanini?.
Na aina ya pili ya Mapenzi ndio hiyo siri yenyewe, sasa kabla ya kwenda mbele hebu tuirejee aya tutizame, ikisha tujiulize kwanini ikataja Wanaume na sio wanawake?. Ikiwa wewe unanifatilia vizuri utagundua ama kwa Wanawake wanayo tayari (Nature) ya (Love)Mapenzi, Mwanamke kwake rahisi ku(surrender)yuradhi kukiri na kumtii mpenzi wake, hiyo ndio hulka ya Mwanamke, anatuonesha vipi mapenzi yake yalivo katika kuwalea na kuwapenda watoto wake, Mwanamke kajaa Moyo wa mapenzi, Mwanamke hana shaka katika penzi lake, na hajui hata inakuaje ila yeye kajaa mapenzi, ndio maana kwa Mwanamke rahisi kwake kwenda kwenye hilo penzi la siri.
Kwanini ikawa hivyo?
Kwa sababu Mwanamke Mapenzi kazaliwa nayo, Mapenzi yako Moyoni, Na hiyo ni siri yake wala haisemi, anao uwezo na ujuzi wa kumpenda Mtu akanyamaza kimya, Na hiyo ndio tunapata ishara ya siri ya Mapenzi (alopewa mwanamke).
Ama kuhusu Mwanamme(Yeye alotiwa)Penzi, Penzi hilo lipo (Kichwani) na wala sio moyoni, Ndio maana "Mwanamme mara huku mara kule", Mara kapenda hichi mara kapenda kile, na hiyo ndio tafauti yao. Kwa hiyo kawaida hiyo inatujulisha Mwanamke yeye yuko tayari kuchupa kwenye Bahari ya Mapenzi ya siri, Ndio maana utaona wao hawendi vitani, (Wao sio Violence) kwa hiyo katika kwenda kwenye Penzi la siri Mwanamke yeye njia yake ni(One Way)(from the heart to the beyond). Lakini Mwanamme yeye ni (Two way)Lazima urudi chini, lazima utoke kwenye kichwa uende moyoni, lazima upate (Faminine Quality).
Ndio Maana utaona "Wacha Mungu"wapole, (Very Loving).
Kwa Mungu hakutakiwi Ujabali, Kwa Mungu hakutakiwi Kuua, Hakutakiwi(Violence)huko ni salama juu ya salama, hakutakiwi chuki, Hakutakiwi hamaki wala hasira.
Sasa leo wacha nikushike mkono labda utachupa na mimi kwenye hiyo bahari ya Mapenzi ya siri ili na wewe upate neema yake. Lakini ili usije ukaweka tamaa au kupanda kiburi kuwa utafanikiwa itabidi nikujulishe kuwa mapenzi haya wanayapata watu wa aina mbili kama ilivosema Quraan sura ya (Fussilat aya ya 34 na 35)
وَلَا تَسۡتَوِى ٱلۡحَسَنَةُ وَلَا ٱلسَّيِّئَةُۚ ٱدۡفَعۡ بِٱلَّتِى هِىَ أَحۡسَنُ فَإِذَا ٱلَّذِى بَيۡنَكَ وَبَيۡنَهُ ۥ عَدَٲوَةٌ۬ كَأَنَّهُ ۥ وَلِىٌّ حَمِيمٌ۬
Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa, ondosha (ubaya unaofanyiwa kwa mema)tahamaki yule ambaye baina yake kuna uadui atakua kama ni jamaa (Yako)mwenye kukufia uchungu.
وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ذُو حَظٍّ عَظِيمٍ۬
Lakini (Jambo hili)hawatapewa ila wale wanaosubiri, wala hawatapewa ila wenye hadhi (Bahati)kubwa (Kwa Mwenye enzi Mungu)
Ipate maana ya maneno haya katika part 2
MAPENZI NI SIRI YAKO PART 2
Asalaam Aleiykum
Aya ya 34 inaanza hivi "Mambo mazuri na Mabaya hayawi sawa" Mambo mazuri ni nini?, ndio hayo Mapenzi ya siri, ondosha Ubaya unaofanyiwa kwa mwema, Tahamaki yule ambaye baina yake kuna uadui atakua kama ni jamaa yako mwenye kukufia uchungu.
Hiyo ndio (Power of Love) sio kuwa umempa mtu pesa au gari au nyumba. Na wewe ukigeuka panga la Mapenzi, basi yule adui yako machozi yatamiminika akikuona tu, atapigana kwa uchungu, yuko tayari kufa kwa ajili yako.
Aya ya 35 inaendelea kuwataja, "Lakini (Jambo hilo)hawatapewa ila wale wanaosubiri" (Na)Wala hawatapewa ila wenye hadhi(bahati)kubwa kwa Mwenye enzi Mungu. Sasa hawa wenye kusubiri ni wepi na wenye hadhi ni wepi, hapo ndio tunaingia katika sehemu yetu ya pili ya hilo (Penzi Lenyewe).
Nini Mapenzi?
Mpaka leo hajatokea awezaye kulijibu swali hilo, halijibiki kwa njia ya maneno, hakuna lugha inayoweza kutafsiri, ile ya Mwanzo tumepewa jawabu na Mollah wetu, lakini hili la pili ndio hiyo siri yenyewe inayokupa ladha na furaha, inakupa na utulivu, inakupa maisha, sasa shuka chini ya huo mti uoneshwe hili shina, huu mzizi, na hii ndio mbegu yenyewe, itabidi uichukue mbegu hiyo uipande mwenyewe.
Nini Mapenzi?
Mapenzi ni (Mystic Force) inayotokea kwa mollah wako na kukuvaa, ni hali unayoipata ya kukumiminia (Bliss)Raha juu ya Raha, hali ambayo haina kikomo, sasa unayapataje Mapenzi haya.
Hapo juu wametajwa watu wa aina mbili wenye kusubiri na wenye hadhi.
Ama tafauti ya wawili hawa wenye kusubiri ni wale wenye kufanya mambo kidogo kidogo, Na wale wenye hadhi ni wale wenye kuendea kheri hizo kwa haraka. Vipi inakua hali hiyo ya Mapenzi ya siri?.
Endelea part 3
Aya ya 34 inaanza hivi "Mambo mazuri na Mabaya hayawi sawa" Mambo mazuri ni nini?, ndio hayo Mapenzi ya siri, ondosha Ubaya unaofanyiwa kwa mwema, Tahamaki yule ambaye baina yake kuna uadui atakua kama ni jamaa yako mwenye kukufia uchungu.
Hiyo ndio (Power of Love) sio kuwa umempa mtu pesa au gari au nyumba. Na wewe ukigeuka panga la Mapenzi, basi yule adui yako machozi yatamiminika akikuona tu, atapigana kwa uchungu, yuko tayari kufa kwa ajili yako.
Aya ya 35 inaendelea kuwataja, "Lakini (Jambo hilo)hawatapewa ila wale wanaosubiri" (Na)Wala hawatapewa ila wenye hadhi(bahati)kubwa kwa Mwenye enzi Mungu. Sasa hawa wenye kusubiri ni wepi na wenye hadhi ni wepi, hapo ndio tunaingia katika sehemu yetu ya pili ya hilo (Penzi Lenyewe).
Nini Mapenzi?
Mpaka leo hajatokea awezaye kulijibu swali hilo, halijibiki kwa njia ya maneno, hakuna lugha inayoweza kutafsiri, ile ya Mwanzo tumepewa jawabu na Mollah wetu, lakini hili la pili ndio hiyo siri yenyewe inayokupa ladha na furaha, inakupa na utulivu, inakupa maisha, sasa shuka chini ya huo mti uoneshwe hili shina, huu mzizi, na hii ndio mbegu yenyewe, itabidi uichukue mbegu hiyo uipande mwenyewe.
Nini Mapenzi?
Mapenzi ni (Mystic Force) inayotokea kwa mollah wako na kukuvaa, ni hali unayoipata ya kukumiminia (Bliss)Raha juu ya Raha, hali ambayo haina kikomo, sasa unayapataje Mapenzi haya.
Hapo juu wametajwa watu wa aina mbili wenye kusubiri na wenye hadhi.
Ama tafauti ya wawili hawa wenye kusubiri ni wale wenye kufanya mambo kidogo kidogo, Na wale wenye hadhi ni wale wenye kuendea kheri hizo kwa haraka. Vipi inakua hali hiyo ya Mapenzi ya siri?.
Endelea part 3
MAPENZI NI SIRI YAKO PART 3
Asalaam Aleiykum
Mapenzi hayo ya siri yanapatikana kwa jitihada, kwa sababu yale ya aina ya kwanza umepewa na Mwenyewe, haya ya pili inatakiwa uyatafute Mwenyewe, Na hiyo ndio maana ya (Ibada)umepewa nusu na nusu uitafute, kwa sababu sasa hivi penzi lako ni (Fragment) vipande vipande, unatakiwa ufanye juhudi uliunganishe, kwanini ikawa vipande vipande, wacha nikujulishe ili upate kulijua penzi la siri likoje, na ukiliunganisha lina faida ipi. Ntakuonesha kwa mfano wa Quraan Al-Ahzab(35)
إِنَّ ٱلۡمُسۡلِمِينَ وَٱلۡمُسۡلِمَـٰتِ وَٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَـٰتِ وَٱلۡقَـٰنِتِينَ وَٱلۡقَـٰنِتَـٰتِ وَٱلصَّـٰدِقِينَ وَٱلصَّـٰدِقَـٰتِ وَٱلصَّـٰبِرِينَ وَٱلصَّـٰبِرَٲتِ وَٱلۡخَـٰشِعِينَ وَٱلۡخَـٰشِعَـٰتِ وَٱلۡمُتَصَدِّقِينَ وَٱلۡمُتَصَدِّقَـٰتِ وَٱلصَّـٰٓٮِٕمِينَ وَٱلصَّـٰٓٮِٕمَـٰتِ وَٱلۡحَـٰفِظِينَ فُرُوجَهُمۡ وَٱلۡحَـٰفِظَـٰتِ وَٱلذَّٲڪِرِينَ ٱللَّهَ كَثِيرً۬ا وَٱلذَّٲڪِرَٲتِ أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُم مَّغۡفِرَةً۬ وَأَجۡرًا عَظِيمً۬ا
Bila shaka Wanaume wenye kuufata (vizuri) Uislam, na wanawake wenye kuufata (vizuri) Uislam, Na Wanaume wanoamini (vizuri), Na Wanawake wanoamini(Vizuri), Na wanaume wanotii, Na wanawake wanotii, Na Wanaume wasemao kweli, Na wanawake wasemao kweli, Na wanaume wanosubiri, Na wanawake wanosubiri, Na wanaume wanonyenyekea, Na wanawake wanonyenyekea, Na wanaume wanotoa sadaka, Na wanawake wanotoa sadaka, Na wanaume wanofunga, Na Wanawake wanofunga, Na wanaume wanaojihifadhi tupu zao, Na wanawake wanaojihifadhi, Na wanaume wanomtaja Mungu kwa wingi, Na wanawake wanomtaja Mwenye enzi Mungu kwa wingi, Mwenye enzi Mungu amewaandalia Msamaha na ujira mkubwa.
Hapo utaona wametajwa wale wenye mapenzi lakini ya tafauti tafauti, huyu anatoa sadaka, huyu anatii, huyu anaamin, huyu anahifadhi tupu, wote hao wanafanya hayo kwa ajili ya mapenzi. Nini habari yako wewe kama utachanganya mambo hayo yote, siri yake ni kupata msamaha, na tunza yake ni kupata huo ujira mkubwa, ukisamehewa unaipata (Pepo), Na hapo ndio utakapo ipata (Mapenzi ni siri yako)jaribu kukusanya uone inakuaje, ipate hali kama hiyo ukutane na mambo ya ajabu.
Na hapo ndio unapata kujua kumbe Uislam ni Dini ya Mapenzi na amani, kwa vipi na imesemwa wapi.Siku zote si Mnasema (Love is Blind)kweli hamjakosea, lakini kwenye Uislam Mwenye enzi Mungu kayafanyia nini hayo mapenzi?.
Quraan (Baqarah aya ya 2 mpaka ya 3) Ipate siri hii ya Mapenzi ili na wewe ufanikiwe.
ذَٲلِكَ ٱلۡڪِتَـٰبُ لَا رَيۡبَۛ فِيهِۛ هُدً۬ى لِّلۡمُتَّقِينَ
"Hiki ni kitabu kisichokua na shaka ndani yake, ni uongozi kwa (wapenzi)wamchao Mwenye enzi Mungu".
Ukishampenda Mollah wako ni lazima upate uongozi ili usije ukapotea, usije ukajigonga na makuta, usije ukachaniwa majuba ndio unapewa hichi kitabu ili kikuongoze, Kwa sababu hayo wayafanyayo hao walotajwa hapo juu yote ni kwa ajili ya mapenzi.
Sasa wamefanyaje hata wakayapata mapenzi hayo.
ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَـٰهُمۡ يُنفِقُونَ
Ambao huyaamini ya (Siri)yasionekana Na husimamisha Sala na hutoa katika yale tuliyowapa.
Kuamini ni jambo rahisi sana, kuamini ni kazi mtu mwengine kakufanyia wewe unakubali, lakini tafsiri sahihi ni lazima uende (deep)ukatafute siri za huo upande wa pili, lazima ujishughulishe sana kutaka kujua kuna nini kwa Mollah wako, ufanye jitihada zako ukipata uthibitisho wa mambo yalofichwa huko japo chembe hapo utakua huzini tene, hudhulumu tena, hupiti kuua, unachorudi nacho kutoka upande wa pili ni kusimamisha Sala, kumbuka kuna kusali na kusimamisha sala, Kwanini ikawa hivyo?, kilosimamishwa lazima kwanza kilikua kimekaa au kulala, sasa wewe kwanini unakisimamisha? kwa sababu Wingi wa Wanaadamu siwenye kusimamisha sala, Maana ya kusimamisha Sala kujaa na mapenzi kwa ajili ya Mollah wako, huwezi kuiba ikisha ukenda kusali, huwezi kupokea rushwa halafu ukasali, huwezi kuzini ikisha ukasimamisha sala, haiwezekani ukaweka mapesa (Bank)huku unasimamisha sala. Utakua unamdanganya Mollah wako,(Bado Umelala) Mwenye kusimamisha sala amejaa mapenzi na akimaliza sala anatoa kile alichopewa na Mwenye enzi Mungu, Unaona Mollah wetu alivojaa mapenzi anatupa uhuru, anatupa uhai, anatupa mali na mengi mengineyo, kwa hiyo yoyote yule Mwenye mapenzi lazima awe na athari ya kutoa, tena athari hiyo haihitaji maonesho ni siri yake na kila akitoa anasikia furaha ya mapenzi kwa wale awapao. Na hiyo ndio siri ya mapenzi unasisitizwa uipate. hapo utaona vipi (Mapenzi yanavo miminika kutoka Mbinguni).
Mapenzi hayo ya siri yanapatikana kwa jitihada, kwa sababu yale ya aina ya kwanza umepewa na Mwenyewe, haya ya pili inatakiwa uyatafute Mwenyewe, Na hiyo ndio maana ya (Ibada)umepewa nusu na nusu uitafute, kwa sababu sasa hivi penzi lako ni (Fragment) vipande vipande, unatakiwa ufanye juhudi uliunganishe, kwanini ikawa vipande vipande, wacha nikujulishe ili upate kulijua penzi la siri likoje, na ukiliunganisha lina faida ipi. Ntakuonesha kwa mfano wa Quraan Al-Ahzab(35)
إِنَّ ٱلۡمُسۡلِمِينَ وَٱلۡمُسۡلِمَـٰتِ وَٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَـٰتِ وَٱلۡقَـٰنِتِينَ وَٱلۡقَـٰنِتَـٰتِ وَٱلصَّـٰدِقِينَ وَٱلصَّـٰدِقَـٰتِ وَٱلصَّـٰبِرِينَ وَٱلصَّـٰبِرَٲتِ وَٱلۡخَـٰشِعِينَ وَٱلۡخَـٰشِعَـٰتِ وَٱلۡمُتَصَدِّقِينَ وَٱلۡمُتَصَدِّقَـٰتِ وَٱلصَّـٰٓٮِٕمِينَ وَٱلصَّـٰٓٮِٕمَـٰتِ وَٱلۡحَـٰفِظِينَ فُرُوجَهُمۡ وَٱلۡحَـٰفِظَـٰتِ وَٱلذَّٲڪِرِينَ ٱللَّهَ كَثِيرً۬ا وَٱلذَّٲڪِرَٲتِ أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُم مَّغۡفِرَةً۬ وَأَجۡرًا عَظِيمً۬ا
Bila shaka Wanaume wenye kuufata (vizuri) Uislam, na wanawake wenye kuufata (vizuri) Uislam, Na Wanaume wanoamini (vizuri), Na Wanawake wanoamini(Vizuri), Na wanaume wanotii, Na wanawake wanotii, Na Wanaume wasemao kweli, Na wanawake wasemao kweli, Na wanaume wanosubiri, Na wanawake wanosubiri, Na wanaume wanonyenyekea, Na wanawake wanonyenyekea, Na wanaume wanotoa sadaka, Na wanawake wanotoa sadaka, Na wanaume wanofunga, Na Wanawake wanofunga, Na wanaume wanaojihifadhi tupu zao, Na wanawake wanaojihifadhi, Na wanaume wanomtaja Mungu kwa wingi, Na wanawake wanomtaja Mwenye enzi Mungu kwa wingi, Mwenye enzi Mungu amewaandalia Msamaha na ujira mkubwa.
Hapo utaona wametajwa wale wenye mapenzi lakini ya tafauti tafauti, huyu anatoa sadaka, huyu anatii, huyu anaamin, huyu anahifadhi tupu, wote hao wanafanya hayo kwa ajili ya mapenzi. Nini habari yako wewe kama utachanganya mambo hayo yote, siri yake ni kupata msamaha, na tunza yake ni kupata huo ujira mkubwa, ukisamehewa unaipata (Pepo), Na hapo ndio utakapo ipata (Mapenzi ni siri yako)jaribu kukusanya uone inakuaje, ipate hali kama hiyo ukutane na mambo ya ajabu.
Na hapo ndio unapata kujua kumbe Uislam ni Dini ya Mapenzi na amani, kwa vipi na imesemwa wapi.Siku zote si Mnasema (Love is Blind)kweli hamjakosea, lakini kwenye Uislam Mwenye enzi Mungu kayafanyia nini hayo mapenzi?.
Quraan (Baqarah aya ya 2 mpaka ya 3) Ipate siri hii ya Mapenzi ili na wewe ufanikiwe.
ذَٲلِكَ ٱلۡڪِتَـٰبُ لَا رَيۡبَۛ فِيهِۛ هُدً۬ى لِّلۡمُتَّقِينَ
"Hiki ni kitabu kisichokua na shaka ndani yake, ni uongozi kwa (wapenzi)wamchao Mwenye enzi Mungu".
Ukishampenda Mollah wako ni lazima upate uongozi ili usije ukapotea, usije ukajigonga na makuta, usije ukachaniwa majuba ndio unapewa hichi kitabu ili kikuongoze, Kwa sababu hayo wayafanyayo hao walotajwa hapo juu yote ni kwa ajili ya mapenzi.
Sasa wamefanyaje hata wakayapata mapenzi hayo.
ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَـٰهُمۡ يُنفِقُونَ
Ambao huyaamini ya (Siri)yasionekana Na husimamisha Sala na hutoa katika yale tuliyowapa.
Kuamini ni jambo rahisi sana, kuamini ni kazi mtu mwengine kakufanyia wewe unakubali, lakini tafsiri sahihi ni lazima uende (deep)ukatafute siri za huo upande wa pili, lazima ujishughulishe sana kutaka kujua kuna nini kwa Mollah wako, ufanye jitihada zako ukipata uthibitisho wa mambo yalofichwa huko japo chembe hapo utakua huzini tene, hudhulumu tena, hupiti kuua, unachorudi nacho kutoka upande wa pili ni kusimamisha Sala, kumbuka kuna kusali na kusimamisha sala, Kwanini ikawa hivyo?, kilosimamishwa lazima kwanza kilikua kimekaa au kulala, sasa wewe kwanini unakisimamisha? kwa sababu Wingi wa Wanaadamu siwenye kusimamisha sala, Maana ya kusimamisha Sala kujaa na mapenzi kwa ajili ya Mollah wako, huwezi kuiba ikisha ukenda kusali, huwezi kupokea rushwa halafu ukasali, huwezi kuzini ikisha ukasimamisha sala, haiwezekani ukaweka mapesa (Bank)huku unasimamisha sala. Utakua unamdanganya Mollah wako,(Bado Umelala) Mwenye kusimamisha sala amejaa mapenzi na akimaliza sala anatoa kile alichopewa na Mwenye enzi Mungu, Unaona Mollah wetu alivojaa mapenzi anatupa uhuru, anatupa uhai, anatupa mali na mengi mengineyo, kwa hiyo yoyote yule Mwenye mapenzi lazima awe na athari ya kutoa, tena athari hiyo haihitaji maonesho ni siri yake na kila akitoa anasikia furaha ya mapenzi kwa wale awapao. Na hiyo ndio siri ya mapenzi unasisitizwa uipate. hapo utaona vipi (Mapenzi yanavo miminika kutoka Mbinguni).
Tuesday, July 5, 2016
WAFALME WA PEPONI PART 1
Asalaam Aleiykum
Zipate darsa zenye kufungua maono yako ili usije kushangaa katika mambo usoyajua yakakuletea balaa za ubishi, Soma kwa uangalifu ili upate maelekezo yatoridhisha nafsi yako kuhusiana na huo upande wa pili unaokwenda kuishi. Pia napenda uelewe hayawafiki mafunzo haya Matajiri wala Wanasiasa kwa kuwa hawana haja nayo, Na pia ukiwa na uchu wa kutafuta mali inakua vigumu mafunzo kama haya kukufikia.
Kwanini ikawa hivyo?(Quran-145-Al-Imran)
وَمَا كَانَ لِنَفْسٍ أَنْ تَمُوتَ إِلاَّ بِإِذْنِ الله كِتَابًا مُّؤَجَّلاً وَمَن يُرِدْ ثَوَابَ الدُّنْيَا نُؤْتِهِ مِنْهَا وَمَن يُرِدْ ثَوَابَ الآخِرَةِ نُؤْتِهِ مِنْهَا وَسَنَجْزِي الشَّاكِرِينَ
"Na Nafsi yoyote haitoweza kufa ila kwa amri ya Mwenye enzi Mungu(na) kwa ajali iliyowekewa, Na Anayetaka malipo ya duniani tutampa hapa (hapa), Na anayetaka malipo ya Akhera tutampa huko (huko), Na kwa yakini tutawalipa wanaoshukuru".
Kwanini aya imeanza na kutajwa mauti? kwa sababu humkuti tajiri au mtu yoyote mwenye harakati nyingi za maisha akataka kujua habari hizi, akajiuliza kwanini kaumbwa, lini atakufa? upande wa pili ukoje, nini wajibu wake, ajabu gani za maisha, kwanini anaishi, na akimaliza maisha haya itakuaje, hataki kabisa maswali haya yamzonge katika shughuli zake za utafutaji wa mali.
Mtu kama huyu utakua naye Msikitini, kipindi cha Sala hakimpiti lakini hana akifanyacho ila mazoea ya mazoezi ya viungo, Sala haipatikani kabisa. Kutokana na hali hiyo Mtu huyo awe wewe au mimi anajiweka mbali na pepo.
Sasa wepi watakayoipata hiyo pepo, zama katika hii darsa angalau uchungulie mfano wa pepo au maana yake ikoje. Naam nani wanoingia? aya hapo juu imeanza vizuri sana imetaja "hakuna Nafsi itokufa ila kwa Idhini ya Mwenye enzi Mungu" Hapo ni kuoneshwa yupo Mfalme Mwenye kukumiliki na hufi hata ujitupe ghorofa mia ila atake yeye, na si hivyo tu bali umeshapangiwa kifo hicho na kimo ndani ya Kitabu kilichohifadhiwa.
Watakao ingia katika hiyo Pepo ni Maskini, Nisije kusema Maskini ukaanza kushangiria na kujiona namie nimo sababu sina nyumba, sina pesa, sipati chakula kwa kawaida, Maskini Mwenyewe sio wewe, kwa sababu wewe na Tajiri hamna tafauti, nyote mkenda kusali maombi yenu yaleyale, Mmoja anaomba apewe utajiri, na Mwengine anaomba azidishiwe utajiri, mali yake isipungue, Mwanawe apasi Mtihani, anaomba asitumbuliwe jipu, apandishwe cheo, Mkewe au Mumewe asichepuke, jirani anyimwe bahati, wewe itizame sala yako utadhani unakwenda kwa (Mganga wa Kienyeji) Kumbe umehudhuria kwa Yule alokupa uhai.
Sasa basi Masikini wepi walokusudiwa hapo, itabidi hapa tuvuke bahari twende ngambo ya pili tukaazime maneno yalotamkwa na Nabii Isa a.s au (Yesu)ndani ya (Injili) pale aliposema:
(Bless are the poor in spirit:for theirs is the kingdom of heaven-Matthew:5:3).
Wamebarikiwa wale masikini wa Kiroho:Kwao wao upo(Urithi) Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Nini maana ya maneno haya? na upi huo Ufalme wa Mwenye enzi Mungu?, Na kwanini Ufalme huo utakua wao?, Basi kwanza kabla ya kugusa mambo hayo itatubidi tuujue Ufalme wenyewe ulokusudiwa ni upi?, Umo katika darsa ya Wafalme wa Pepo nakutaka uilekeze Akili yako katika kitabu Kitukufu chenye ukweli ndani yake ili kikujulishe vipi utakua Ufalme huo.
Endelea part 2
Zipate darsa zenye kufungua maono yako ili usije kushangaa katika mambo usoyajua yakakuletea balaa za ubishi, Soma kwa uangalifu ili upate maelekezo yatoridhisha nafsi yako kuhusiana na huo upande wa pili unaokwenda kuishi. Pia napenda uelewe hayawafiki mafunzo haya Matajiri wala Wanasiasa kwa kuwa hawana haja nayo, Na pia ukiwa na uchu wa kutafuta mali inakua vigumu mafunzo kama haya kukufikia.
Kwanini ikawa hivyo?(Quran-145-Al-Imran)
وَمَا كَانَ لِنَفْسٍ أَنْ تَمُوتَ إِلاَّ بِإِذْنِ الله كِتَابًا مُّؤَجَّلاً وَمَن يُرِدْ ثَوَابَ الدُّنْيَا نُؤْتِهِ مِنْهَا وَمَن يُرِدْ ثَوَابَ الآخِرَةِ نُؤْتِهِ مِنْهَا وَسَنَجْزِي الشَّاكِرِينَ
"Na Nafsi yoyote haitoweza kufa ila kwa amri ya Mwenye enzi Mungu(na) kwa ajali iliyowekewa, Na Anayetaka malipo ya duniani tutampa hapa (hapa), Na anayetaka malipo ya Akhera tutampa huko (huko), Na kwa yakini tutawalipa wanaoshukuru".
Kwanini aya imeanza na kutajwa mauti? kwa sababu humkuti tajiri au mtu yoyote mwenye harakati nyingi za maisha akataka kujua habari hizi, akajiuliza kwanini kaumbwa, lini atakufa? upande wa pili ukoje, nini wajibu wake, ajabu gani za maisha, kwanini anaishi, na akimaliza maisha haya itakuaje, hataki kabisa maswali haya yamzonge katika shughuli zake za utafutaji wa mali.
Mtu kama huyu utakua naye Msikitini, kipindi cha Sala hakimpiti lakini hana akifanyacho ila mazoea ya mazoezi ya viungo, Sala haipatikani kabisa. Kutokana na hali hiyo Mtu huyo awe wewe au mimi anajiweka mbali na pepo.
Sasa wepi watakayoipata hiyo pepo, zama katika hii darsa angalau uchungulie mfano wa pepo au maana yake ikoje. Naam nani wanoingia? aya hapo juu imeanza vizuri sana imetaja "hakuna Nafsi itokufa ila kwa Idhini ya Mwenye enzi Mungu" Hapo ni kuoneshwa yupo Mfalme Mwenye kukumiliki na hufi hata ujitupe ghorofa mia ila atake yeye, na si hivyo tu bali umeshapangiwa kifo hicho na kimo ndani ya Kitabu kilichohifadhiwa.
Watakao ingia katika hiyo Pepo ni Maskini, Nisije kusema Maskini ukaanza kushangiria na kujiona namie nimo sababu sina nyumba, sina pesa, sipati chakula kwa kawaida, Maskini Mwenyewe sio wewe, kwa sababu wewe na Tajiri hamna tafauti, nyote mkenda kusali maombi yenu yaleyale, Mmoja anaomba apewe utajiri, na Mwengine anaomba azidishiwe utajiri, mali yake isipungue, Mwanawe apasi Mtihani, anaomba asitumbuliwe jipu, apandishwe cheo, Mkewe au Mumewe asichepuke, jirani anyimwe bahati, wewe itizame sala yako utadhani unakwenda kwa (Mganga wa Kienyeji) Kumbe umehudhuria kwa Yule alokupa uhai.
Sasa basi Masikini wepi walokusudiwa hapo, itabidi hapa tuvuke bahari twende ngambo ya pili tukaazime maneno yalotamkwa na Nabii Isa a.s au (Yesu)ndani ya (Injili) pale aliposema:
(Bless are the poor in spirit:for theirs is the kingdom of heaven-Matthew:5:3).
Wamebarikiwa wale masikini wa Kiroho:Kwao wao upo(Urithi) Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Nini maana ya maneno haya? na upi huo Ufalme wa Mwenye enzi Mungu?, Na kwanini Ufalme huo utakua wao?, Basi kwanza kabla ya kugusa mambo hayo itatubidi tuujue Ufalme wenyewe ulokusudiwa ni upi?, Umo katika darsa ya Wafalme wa Pepo nakutaka uilekeze Akili yako katika kitabu Kitukufu chenye ukweli ndani yake ili kikujulishe vipi utakua Ufalme huo.
Endelea part 2
WAFALME WA PEPONI PART 2
Asalaam Aleiykum
Sura ya Maryam aya (61,62,63).
"جَنَّـٰتِ عَدۡنٍ ٱلَّتِى وَعَدَ ٱلرَّحۡمَـٰنُ عِبَادَهُ ۥ بِٱلۡغَيۡبِۚ إِنَّهُ ۥ كَانَ وَعۡدُهُ ۥ مَأۡتِيًّ۬ا"
Pepo za milele ambazo (Mollah)Mwingi wa Rehma amewaahidi waja wake katika siri, Bila shaka ahadi yake ni yenye kuja.
"لَّا يَسۡمَعُونَ فِيہَا لَغۡوًا إِلَّا سَلَـٰمً۬اۖ وَلَهُمۡ رِزۡقُهُمۡ فِيہَا بُكۡرَةً۬ وَعَشِيًّ۬ا"
Hawatasikia humo upuuzi ila Salama, Na watapata humo riziki yao asubuhi na jioni.
"تِلۡكَ ٱلۡجَنَّةُ ٱلَّتِى نُورِثُ مِنۡ عِبَادِنَا مَن كَانَ تَقِيًّ۬ا "
Hiyo ndio pepo tutakayowarithisha katika waja wetu wale ambao (Walikua)ni Wanamcha Mungu.
Aya tatu lakini zina tafsiri kubwa kabisa inataka siku nzima kuichambua tafsiri hiyo, lakini kwa ufupi tukio hilo linaashiria kwenye aya ya mwanzo kuwepo kwa uendelevu wa maisha,Maisha ambayo wewe utakua ni "Bwana" Utakua ni Mfalme, Jee wewe huitaki ahadi hii ya siri ya Mollah wako, kama ninavosema, (nasema kila mara)uhai ni kitu cha kudumu, ila maisha ndio kitu cha (Mpito)au(Temporary). Kwa hiyo hichi kitu kinachoitwa Pepo ni ahadi ya siri, Lakini daima ahadi ya Mwenye enzi Mungu ni yenye kutimia, kwa hiyo kaa ukijua utakapomaliza muda wa kuishi hapa Ulimwenguni kuna maisha mengine.
Na Maisha ya huko hayana porojo za wanasiasa, hakuna uongo wa wafanya biashara, mambo ya kipuuzi yote yana katika katika dunia hii, huko unakutana na hali ya usalama(Peace)tupu, hakuna chuki wala uhasama, na humo wewe ni Mwenye kuhudumiwa kila kitu chako unaishi maisha ya Kifalme, Sasa hivi unaona kwenye TV tu lakini huko na wewe utayapata, utakua Mwenye kupata riziki yako asubuhi na jioni, hakuna tena shida ya kutafuta wala kuhangaika.
Hiyo ndio hiyo pepo watakayorithi wale walokua na Mapenzi na Mollah wao, wakakubali yupo na kumtii kwa ajili ya Ibada na kufata amri na sheria zake. Lakini uingiaji wake una shuruti lazima uwe Maskini, Sasa Umasikini huu ukoje? (Quraan imeashiria jambo kwenye sura ya Ash-Shuura aya ya 20) inasemaje?.
مَن كَانَ يُرِيدُ حَرۡثَ ٱلۡأَخِرَةِ نَزِدۡ لَهُ ۥ فِى حَرۡثِهِۦۖ وَمَن كَانَ يُرِيدُ حَرۡثَ ٱلدُّنۡيَا نُؤۡتِهِۦ مِنۡہَا وَمَا لَهُ ۥ فِى ٱلۡأَخِرَةِ مِن نَّصِيبٍ
"Mwenye kutaka jaza ya Akhera tutamzidishia katika Jaza yake hiyo, Na anayetaka Jaza ya Dunia tutampa, Lakini Akhera hatakuwa na sehemu yoyote ya kheri".
Sasa kwanini ikawa moja utazidishiwa, na nyengine utapewa, kuna mambo yamejificha wewe huyajui, maana ya kusemwa hivyo kuna kitu wewe unacho tayari lakini hukijui, na kitofanyika ni kuzidishiwa, unaweza kukipata hapa hapa na ndio haki yako ikiwa utamcha Mwenye enzi Mungu, lakini kupewa ni kwa muda unaweza ukapoteza, unaweza kunyanganywa au kukupotea. Kwa hiyo tabia ya Mwanaadamu ni vigumu sana kuvitaka vyote vilotajwa kwenye aya hiyo.
Ni watu wachache sana wanoweza kufanikiwa, Na sababu kubwa viumbe hatuna (Balance), Ndio maana tukapewa uhuru wetu kwa yule Mwenye kutaka Dunia anapewa, na Mwenye kuitaka Akhera pia anapewa. Sasa Maskini yupi Mwenye kurithi huo Ufalme?, Usikilize ukweli unapo dhihiri, Yasome Maneno ya Mwenye enzi Mungu kupitia katika vinywa vya Mitume wake wanasemaje.
Anasema Isa a.s "Wamebarikiwa Maskini kwani wao ndio watorithi Ufalme wa Mwenye enzi Mungu" Kwanini likatajwa neno kubarikiwa(Blessing)Kwa sababu hao wamechagua kitu kizuri sana, Wao wamechagua (Both) wako kwenye (Balance) (Irejee aya juu imetaja kuzidishiwa na kupewa) maana ya kuzidishiwa tayari unacho, na kupewa ndio hicho cha ziada, ukichagua (Both) unakuaje? na ukichagua kimoja unakuaje?.
Ukichagua Dunia na ndio wengi tunaichagua unakua unajishughulisha sana na kutafuta mali, mashamba, ufakhari, Na ukichagua Akhera pekee unakua Mwenye kutaka kufa, ushachoka na maisha, kila kitu haramu, muradi wako unakua (Neurotic) kwa sababu huna (Balance). Sasa uchague vipi? chagua kama ilivosema katika Quraan, imesemwa vipi?
Endelea part 3
Sura ya Maryam aya (61,62,63).
"جَنَّـٰتِ عَدۡنٍ ٱلَّتِى وَعَدَ ٱلرَّحۡمَـٰنُ عِبَادَهُ ۥ بِٱلۡغَيۡبِۚ إِنَّهُ ۥ كَانَ وَعۡدُهُ ۥ مَأۡتِيًّ۬ا"
Pepo za milele ambazo (Mollah)Mwingi wa Rehma amewaahidi waja wake katika siri, Bila shaka ahadi yake ni yenye kuja.
"لَّا يَسۡمَعُونَ فِيہَا لَغۡوًا إِلَّا سَلَـٰمً۬اۖ وَلَهُمۡ رِزۡقُهُمۡ فِيہَا بُكۡرَةً۬ وَعَشِيًّ۬ا"
Hawatasikia humo upuuzi ila Salama, Na watapata humo riziki yao asubuhi na jioni.
"تِلۡكَ ٱلۡجَنَّةُ ٱلَّتِى نُورِثُ مِنۡ عِبَادِنَا مَن كَانَ تَقِيًّ۬ا "
Hiyo ndio pepo tutakayowarithisha katika waja wetu wale ambao (Walikua)ni Wanamcha Mungu.
Aya tatu lakini zina tafsiri kubwa kabisa inataka siku nzima kuichambua tafsiri hiyo, lakini kwa ufupi tukio hilo linaashiria kwenye aya ya mwanzo kuwepo kwa uendelevu wa maisha,Maisha ambayo wewe utakua ni "Bwana" Utakua ni Mfalme, Jee wewe huitaki ahadi hii ya siri ya Mollah wako, kama ninavosema, (nasema kila mara)uhai ni kitu cha kudumu, ila maisha ndio kitu cha (Mpito)au(Temporary). Kwa hiyo hichi kitu kinachoitwa Pepo ni ahadi ya siri, Lakini daima ahadi ya Mwenye enzi Mungu ni yenye kutimia, kwa hiyo kaa ukijua utakapomaliza muda wa kuishi hapa Ulimwenguni kuna maisha mengine.
Na Maisha ya huko hayana porojo za wanasiasa, hakuna uongo wa wafanya biashara, mambo ya kipuuzi yote yana katika katika dunia hii, huko unakutana na hali ya usalama(Peace)tupu, hakuna chuki wala uhasama, na humo wewe ni Mwenye kuhudumiwa kila kitu chako unaishi maisha ya Kifalme, Sasa hivi unaona kwenye TV tu lakini huko na wewe utayapata, utakua Mwenye kupata riziki yako asubuhi na jioni, hakuna tena shida ya kutafuta wala kuhangaika.
Hiyo ndio hiyo pepo watakayorithi wale walokua na Mapenzi na Mollah wao, wakakubali yupo na kumtii kwa ajili ya Ibada na kufata amri na sheria zake. Lakini uingiaji wake una shuruti lazima uwe Maskini, Sasa Umasikini huu ukoje? (Quraan imeashiria jambo kwenye sura ya Ash-Shuura aya ya 20) inasemaje?.
مَن كَانَ يُرِيدُ حَرۡثَ ٱلۡأَخِرَةِ نَزِدۡ لَهُ ۥ فِى حَرۡثِهِۦۖ وَمَن كَانَ يُرِيدُ حَرۡثَ ٱلدُّنۡيَا نُؤۡتِهِۦ مِنۡہَا وَمَا لَهُ ۥ فِى ٱلۡأَخِرَةِ مِن نَّصِيبٍ
"Mwenye kutaka jaza ya Akhera tutamzidishia katika Jaza yake hiyo, Na anayetaka Jaza ya Dunia tutampa, Lakini Akhera hatakuwa na sehemu yoyote ya kheri".
Sasa kwanini ikawa moja utazidishiwa, na nyengine utapewa, kuna mambo yamejificha wewe huyajui, maana ya kusemwa hivyo kuna kitu wewe unacho tayari lakini hukijui, na kitofanyika ni kuzidishiwa, unaweza kukipata hapa hapa na ndio haki yako ikiwa utamcha Mwenye enzi Mungu, lakini kupewa ni kwa muda unaweza ukapoteza, unaweza kunyanganywa au kukupotea. Kwa hiyo tabia ya Mwanaadamu ni vigumu sana kuvitaka vyote vilotajwa kwenye aya hiyo.
Ni watu wachache sana wanoweza kufanikiwa, Na sababu kubwa viumbe hatuna (Balance), Ndio maana tukapewa uhuru wetu kwa yule Mwenye kutaka Dunia anapewa, na Mwenye kuitaka Akhera pia anapewa. Sasa Maskini yupi Mwenye kurithi huo Ufalme?, Usikilize ukweli unapo dhihiri, Yasome Maneno ya Mwenye enzi Mungu kupitia katika vinywa vya Mitume wake wanasemaje.
Anasema Isa a.s "Wamebarikiwa Maskini kwani wao ndio watorithi Ufalme wa Mwenye enzi Mungu" Kwanini likatajwa neno kubarikiwa(Blessing)Kwa sababu hao wamechagua kitu kizuri sana, Wao wamechagua (Both) wako kwenye (Balance) (Irejee aya juu imetaja kuzidishiwa na kupewa) maana ya kuzidishiwa tayari unacho, na kupewa ndio hicho cha ziada, ukichagua (Both) unakuaje? na ukichagua kimoja unakuaje?.
Ukichagua Dunia na ndio wengi tunaichagua unakua unajishughulisha sana na kutafuta mali, mashamba, ufakhari, Na ukichagua Akhera pekee unakua Mwenye kutaka kufa, ushachoka na maisha, kila kitu haramu, muradi wako unakua (Neurotic) kwa sababu huna (Balance). Sasa uchague vipi? chagua kama ilivosema katika Quraan, imesemwa vipi?
Endelea part 3
WAFALME WA PEPONI PART 3
Asalaam Aleiykum
(Quraan Baqarah aya ya 201)
وَمِنۡهُم مَّن يَقُولُ رَبَّنَآ ءَاتِنَا فِى ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةً۬ وَفِى ٱلۡأَخِرَةِ حَسَنَةً۬ وَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ
"Na Miongoni mwao wako wasemao Mollah wetu tupe mema duniani na (Tupe)Mema Akhera, Na utulinde na adhabu ya moto".
Kauli ni ile ile Mollah wangu nibariki kwa mambo mazuri hapa duniani(Blessing)na huko Akhera, Ikisha niepushe na adhabu ya moto, na unapoepushwa na adhabu ya moto kinachofatia ni kupewa au kuingizwa kwenye huo ufalme wa Mwenye enzi Mungu. Hao ndio watorithi Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Sasa tuwatizame warithi wenyewe ni Maskini wa aina gani?, (Usije ukadhani ni wale omba omba) Walotajwa ni wale Maskini wa Roho wenye kutafuta utajiri wa kumjua na kumpenda Mollah wao, Hao ni Maskini wa Ibada, Maskini wa kufanya mambo ya kheri, maskini wa Mapenzi, Maskini wa Huruma, Maskini wenye Uchu wa Kumkumbuka na kumtii Mollah wao, Maskini walokua hawana Kiburi, Maskini wenye hamu kubwa ya kumjua Mollah wao, Maskini ambao wakati wote wamo kwenye Dunia lakini mawazo na fikra zao zote wamejishughulisha kumkumbuka Mollah wao.
Hao ndio walochagua (Both) Dunia na Akhera, na ndivo inavotakiwa, ndivo ilivosema Quraan, ukiweza kufanya hivyo nini kinatokezea? (Quraan Ahqaf aya 13-14)
"إِنَّ ٱلَّذِينَ قَالُواْ رَبُّنَا ٱللَّهُ ثُمَّ ٱسۡتَقَـٰمُواْ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ "
Hakika wale waliosema Mollah wetu ni Mwenye enzi Mungu kisha wakatengenea(Kusimama kwenye kufanya yalo haki)hawatakua na hofu na wala hawatahuzunika.
"أُوْلَـٰٓٮِٕكَ أَصۡحَـٰبُ ٱلۡجَنَّةِ خَـٰلِدِينَ فِيہَا جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ "
Hao ndio watu wa Peponi, watakaa humo (daima)ni malipo ya yale waliyokuwa wakiyatenda.
Sasa hapa duniani unapata nini?
Unapewa na Mwenye enzi Mungu mambo mawili hapa hapa duniani iwe mfano wa mambo yatakavokua huko Akhera kwenye Ufalme wenyewe. Jambo la Mwanzo Unateremshiwa (Body Guard) Malaika wawe na wewe popote uendapo, unapata ulinzi(Ukitaka kuwaona niandikie pembeni ntakufundisha vipi uwaone?, Najua utashangaa ndio maana ya kukwambia, kumbuka unakoga katika bahari usishangae maji kugusa)Naam na Jambo la pili ndio huo mfano wa pepo unapewa kitu adhimu sana, kitu hichi ukikipata ukaweza kudumu nacho basi kiumbe unakua ushafuzu katika maisha yako ya Ulimwenguni na huko akhera, Kitu gani hichi cha pili?, hakuna chengine isipokua kupewa (Control) ya (Mind) Akili yako, hapa itabidi nieleze vizuri ili upate kujua maana ya atakua hana khofu wala huzuni ikoje?.
Hali hii anaipata kila mtu lakini inakujia mara chache sana, kwa mimi naita hali hiyo (To make contact with your being) unapata baadhi ya Nyakati pale unapokua (Total engaged)Mfano, kama wewe mcheza mpira au unatizama kipindi chako kwenye TV, au unapozungumza hapo Akili au (Mind)inapotea, hakuna mawazo, unakua hufikiri chochote, kwa sababu Akili haiwezi kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja, basi hapo unakua (full Being)huna huzuni, huna khofu na ukiwa katika hali hiyo unakuwa huwezi kutenda kosa.
Hivyo ndio wanavokua "Hao Maskini walotajwa" wenye kurithi huo Ufalme, Wanakua ni wenye kudumu katika hali hiyo, sio kwamba hawana Akili ila ana uwezo wa kuitumia wakati anaotaka Mwenyewe kwa hiyo muda wote ulobakia yuko kwenye (Being)yake na hapo ndio kwenye hiyo (Bliss), Kwa hiyo tafauti yako na yeye wewe unatumia nyakati maalumu za kucheza mpira, kutizama TV, kuzungumza na yeye anaendelea kuwa nayo (Being)yake wakati wote, kwa hiyo hapo mambo yanakua (Vice Versa), Wewe unatumia (Mind)Akili wakati wote na yeye anatumia(Being) wakati wote. Na kama utakua na ubishi kwenye Nafsi yako basi jiangalie mara chache sana unaipata hiyo (Being)lakini muda wote umetawaliwa na mafikra, mawazo juu ya mawazo(Stress)zimekujaa, dhana za kila aina, wanawake au wanaume wanaishi humo, madeni yanaishi humo, chuki zinaishi humo binaadamu huna mapumziko, huzuni juu ya huzuni, mashaka na khofu chungu nzima, Na hiyo ndio Akili uliyoibeba na ndio ilokufanya uchague dunia dhidi ya Akhera.
Sasa Wacha nikuchukue kwenye mfano wa Ufalme wa vinyama hususan ndege uone wanaishi vipi?.
Endelea Part 4
(Quraan Baqarah aya ya 201)
وَمِنۡهُم مَّن يَقُولُ رَبَّنَآ ءَاتِنَا فِى ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةً۬ وَفِى ٱلۡأَخِرَةِ حَسَنَةً۬ وَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ
"Na Miongoni mwao wako wasemao Mollah wetu tupe mema duniani na (Tupe)Mema Akhera, Na utulinde na adhabu ya moto".
Kauli ni ile ile Mollah wangu nibariki kwa mambo mazuri hapa duniani(Blessing)na huko Akhera, Ikisha niepushe na adhabu ya moto, na unapoepushwa na adhabu ya moto kinachofatia ni kupewa au kuingizwa kwenye huo ufalme wa Mwenye enzi Mungu. Hao ndio watorithi Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Sasa tuwatizame warithi wenyewe ni Maskini wa aina gani?, (Usije ukadhani ni wale omba omba) Walotajwa ni wale Maskini wa Roho wenye kutafuta utajiri wa kumjua na kumpenda Mollah wao, Hao ni Maskini wa Ibada, Maskini wa kufanya mambo ya kheri, maskini wa Mapenzi, Maskini wa Huruma, Maskini wenye Uchu wa Kumkumbuka na kumtii Mollah wao, Maskini walokua hawana Kiburi, Maskini wenye hamu kubwa ya kumjua Mollah wao, Maskini ambao wakati wote wamo kwenye Dunia lakini mawazo na fikra zao zote wamejishughulisha kumkumbuka Mollah wao.
Hao ndio walochagua (Both) Dunia na Akhera, na ndivo inavotakiwa, ndivo ilivosema Quraan, ukiweza kufanya hivyo nini kinatokezea? (Quraan Ahqaf aya 13-14)
"إِنَّ ٱلَّذِينَ قَالُواْ رَبُّنَا ٱللَّهُ ثُمَّ ٱسۡتَقَـٰمُواْ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ "
Hakika wale waliosema Mollah wetu ni Mwenye enzi Mungu kisha wakatengenea(Kusimama kwenye kufanya yalo haki)hawatakua na hofu na wala hawatahuzunika.
"أُوْلَـٰٓٮِٕكَ أَصۡحَـٰبُ ٱلۡجَنَّةِ خَـٰلِدِينَ فِيہَا جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ "
Hao ndio watu wa Peponi, watakaa humo (daima)ni malipo ya yale waliyokuwa wakiyatenda.
Sasa hapa duniani unapata nini?
Unapewa na Mwenye enzi Mungu mambo mawili hapa hapa duniani iwe mfano wa mambo yatakavokua huko Akhera kwenye Ufalme wenyewe. Jambo la Mwanzo Unateremshiwa (Body Guard) Malaika wawe na wewe popote uendapo, unapata ulinzi(Ukitaka kuwaona niandikie pembeni ntakufundisha vipi uwaone?, Najua utashangaa ndio maana ya kukwambia, kumbuka unakoga katika bahari usishangae maji kugusa)Naam na Jambo la pili ndio huo mfano wa pepo unapewa kitu adhimu sana, kitu hichi ukikipata ukaweza kudumu nacho basi kiumbe unakua ushafuzu katika maisha yako ya Ulimwenguni na huko akhera, Kitu gani hichi cha pili?, hakuna chengine isipokua kupewa (Control) ya (Mind) Akili yako, hapa itabidi nieleze vizuri ili upate kujua maana ya atakua hana khofu wala huzuni ikoje?.
Hali hii anaipata kila mtu lakini inakujia mara chache sana, kwa mimi naita hali hiyo (To make contact with your being) unapata baadhi ya Nyakati pale unapokua (Total engaged)Mfano, kama wewe mcheza mpira au unatizama kipindi chako kwenye TV, au unapozungumza hapo Akili au (Mind)inapotea, hakuna mawazo, unakua hufikiri chochote, kwa sababu Akili haiwezi kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja, basi hapo unakua (full Being)huna huzuni, huna khofu na ukiwa katika hali hiyo unakuwa huwezi kutenda kosa.
Hivyo ndio wanavokua "Hao Maskini walotajwa" wenye kurithi huo Ufalme, Wanakua ni wenye kudumu katika hali hiyo, sio kwamba hawana Akili ila ana uwezo wa kuitumia wakati anaotaka Mwenyewe kwa hiyo muda wote ulobakia yuko kwenye (Being)yake na hapo ndio kwenye hiyo (Bliss), Kwa hiyo tafauti yako na yeye wewe unatumia nyakati maalumu za kucheza mpira, kutizama TV, kuzungumza na yeye anaendelea kuwa nayo (Being)yake wakati wote, kwa hiyo hapo mambo yanakua (Vice Versa), Wewe unatumia (Mind)Akili wakati wote na yeye anatumia(Being) wakati wote. Na kama utakua na ubishi kwenye Nafsi yako basi jiangalie mara chache sana unaipata hiyo (Being)lakini muda wote umetawaliwa na mafikra, mawazo juu ya mawazo(Stress)zimekujaa, dhana za kila aina, wanawake au wanaume wanaishi humo, madeni yanaishi humo, chuki zinaishi humo binaadamu huna mapumziko, huzuni juu ya huzuni, mashaka na khofu chungu nzima, Na hiyo ndio Akili uliyoibeba na ndio ilokufanya uchague dunia dhidi ya Akhera.
Sasa Wacha nikuchukue kwenye mfano wa Ufalme wa vinyama hususan ndege uone wanaishi vipi?.
Endelea Part 4
WAFALME WA PEPONI PART 4
Asalaam Aleiykum
Ipate japo siku moja hata nusu saa, kuwa (Mad)kama (Shk Baja)kakae kwenye Bustani au kwenye(Garden) au nenda (Park)au hata shamba asubuhi na mapema, halafu kashuhudie vipi(Unconscious Being)wanavoishi, Wanaishi kama unavoishi, Wana Nyumba zao tena wamezijenga wenyewe, wana watoto wao na wake zao, wanatafuta chakula kama mfanyavo nyinyi, wanalala na kuamka, wanakwenda huku na kule kwenye bustani, mara kwenye mti huu mara kwenye mti ule, mara kwenye maji wanakunywa, mara kwenye mti wanapumzika, Na mara wanaimba kwa furaha na baraka alizowapa Mollah wao.
Wao katika Ufalme huo wanaishi kwa mapenzi kama utayafahamu, mara wanaruka mara wametulia wanatizama neema walizopewa na Mollah wao, Na wakishikwa na maradhi wao wako kwenye subra wanajua Mollah wao anawaponesha daima. Basi wao wapo kwenye (Mfano)wao wa pepo na ikifika wakati wanajifia na kurejea kwa Mollah wao(Blissful), Viungo vyao vinaanguka na kugeuka Mchanga kama wewe utakavogeuka wakati wa kifo chako.
Naam unapewa mifano hii ya pepo ili na wewe uchague vipi unataka. Na ukiwa utaridhia huo umasikini ukaipata hali hiyo niloitaja kwenye (Part 3)basi Ufalme gani utakaoupata wewe?
Quraan Waqiah aya ya 10.
"وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ"
Walioko mbele(Kwenye Ucha Mungu)nao ndio wlioko mbele
"أُوْلَـٰٓٮِٕكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ"
Hao ndio watakaokaribishwa(Kwenye Ufalme wa Mwenye enzi Mungu)
"فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ"
Katika Mabustani yenye Neema
" ثُلَّةٌ۬ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ"
Sehemu kubwa ni miongoni mwa (watu)wa mwanzo(Zamani)
Kwani ikawa zamani kwa sababu walikua wakiishi kwenye (Being)zao, wanaishi kwa (Feeling)kutumia moyo sio kwa njia za (Mind)Akili .
"وَقَلِيلٌ۬ مِّنَ ٱلۡأَخِرِينَ"
"Na sehemu ndogo ni miongoni mwa watu wa mwisho
Huu wakati tulonao ni mashaka makubwa ya kurithi au kuyapata au kupata kuwa karibu na Mollah wetu kutokana na ujanja tulonao, kila mtu kabeba mzigo wa mawazo machafu, mawazo mabaya, dhuluma, magonvi, hasada, chuki, viburi. Na maelezo yanaendelea mpaka aya ya 26 kuwaeleza hao watakaorithi huo Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Ama wale waloshindwa kuupata huo umasikini lakini wakafanya kheri, na walotubia makosa yao nao imetajwa sehemu watakayokua wao nayo inaanzia aya ya 27 mpaka aya ya 40. Kwa hiyo bidii yako ndio itakayokufanya ima uwe Mfalme au Mtu wa kawaida, zisome hizo aya halafu utafanya uamuzi unataka vipi. Na kama umeshindwa kabisa basi jitaarishe na kundi la tatu ambalo litakua makaazi yako Motoni, Na kumbuka hiyo ni ahadi ya Mwenye enzi Mungu.
Ipate japo siku moja hata nusu saa, kuwa (Mad)kama (Shk Baja)kakae kwenye Bustani au kwenye(Garden) au nenda (Park)au hata shamba asubuhi na mapema, halafu kashuhudie vipi(Unconscious Being)wanavoishi, Wanaishi kama unavoishi, Wana Nyumba zao tena wamezijenga wenyewe, wana watoto wao na wake zao, wanatafuta chakula kama mfanyavo nyinyi, wanalala na kuamka, wanakwenda huku na kule kwenye bustani, mara kwenye mti huu mara kwenye mti ule, mara kwenye maji wanakunywa, mara kwenye mti wanapumzika, Na mara wanaimba kwa furaha na baraka alizowapa Mollah wao.
Wao katika Ufalme huo wanaishi kwa mapenzi kama utayafahamu, mara wanaruka mara wametulia wanatizama neema walizopewa na Mollah wao, Na wakishikwa na maradhi wao wako kwenye subra wanajua Mollah wao anawaponesha daima. Basi wao wapo kwenye (Mfano)wao wa pepo na ikifika wakati wanajifia na kurejea kwa Mollah wao(Blissful), Viungo vyao vinaanguka na kugeuka Mchanga kama wewe utakavogeuka wakati wa kifo chako.
Naam unapewa mifano hii ya pepo ili na wewe uchague vipi unataka. Na ukiwa utaridhia huo umasikini ukaipata hali hiyo niloitaja kwenye (Part 3)basi Ufalme gani utakaoupata wewe?
Quraan Waqiah aya ya 10.
"وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ"
Walioko mbele(Kwenye Ucha Mungu)nao ndio wlioko mbele
"أُوْلَـٰٓٮِٕكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ"
Hao ndio watakaokaribishwa(Kwenye Ufalme wa Mwenye enzi Mungu)
"فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ"
Katika Mabustani yenye Neema
" ثُلَّةٌ۬ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ"
Sehemu kubwa ni miongoni mwa (watu)wa mwanzo(Zamani)
Kwani ikawa zamani kwa sababu walikua wakiishi kwenye (Being)zao, wanaishi kwa (Feeling)kutumia moyo sio kwa njia za (Mind)Akili .
"وَقَلِيلٌ۬ مِّنَ ٱلۡأَخِرِينَ"
"Na sehemu ndogo ni miongoni mwa watu wa mwisho
Huu wakati tulonao ni mashaka makubwa ya kurithi au kuyapata au kupata kuwa karibu na Mollah wetu kutokana na ujanja tulonao, kila mtu kabeba mzigo wa mawazo machafu, mawazo mabaya, dhuluma, magonvi, hasada, chuki, viburi. Na maelezo yanaendelea mpaka aya ya 26 kuwaeleza hao watakaorithi huo Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Ama wale waloshindwa kuupata huo umasikini lakini wakafanya kheri, na walotubia makosa yao nao imetajwa sehemu watakayokua wao nayo inaanzia aya ya 27 mpaka aya ya 40. Kwa hiyo bidii yako ndio itakayokufanya ima uwe Mfalme au Mtu wa kawaida, zisome hizo aya halafu utafanya uamuzi unataka vipi. Na kama umeshindwa kabisa basi jitaarishe na kundi la tatu ambalo litakua makaazi yako Motoni, Na kumbuka hiyo ni ahadi ya Mwenye enzi Mungu.
Wednesday, June 1, 2016
RAMADHAN NI VAZI LA UCHA MUNGU PART 1
Asalaam Aleiykum
Zimekufikia habari za Mwezi ambao ndani yake kuna Rehma, Kati yake kuna Maghfira(Msamaha), Na Mwisho wake kuna Dhamana.
Vipi basi yanapatikana matatu haya?, hili ndio shiko la darsa yetu ya leo, Ndio safari tutakayo kwenda mimi na wewe kama walivokwenda Nabii Musa a.s na Msaidizi wake, Nini kilitokea kwenye hiyo safari yao, na nini ilikua kusudio ya safari ile?. Quraan sura ya (Al-Kahf )kuanzia aya ya 60.
"وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِفَتَٮٰهُ لَآ أَبۡرَحُ حَتَّىٰٓ أَبۡلُغَ مَجۡمَعَ ٱلۡبَحۡرَيۡنِ أَوۡ أَمۡضِىَ حُقُبً۬ا "
Na (Kumbukeni) Musa alipomwambia kijana(Msaidizi)wake nitaendelea kwenda (hii safari)mpaka nifike katika maungano ya bahari mbili, au niendelee kwa karne(mpaka nikutane na huyo ninayetaka kukutana naye).
Na hivyo ndio inavotakiwa katika kutafuta elimu hakuna kuchoka wala kuzeeka, vipi ilitokea safari hii, Anahadithia Ubai ibn Kaab alimsikia Mtume s.a.w akisema, siku moja Nabii Musa a.s alikua akitoa mawaidha akaulizwa swali hili, Kiumbe gani Mwenye elimu kupita wote, akajibu ni mimi, Hapo Mwenye enzi Mungu akamwambia yuko aliyekuzidi "Ewe Musa" alijibiwa hivyo kwa sababu hajarejesha jawabu hilo kwa Mwenye enzi Mungu na kwa kutaka kufahamishwa akaambiwa nenda utakutana na Mtu huyo kwenye makutano ya Bahari mbili, Sehemu hiyo haijatajwa wapi lakini wanazuoni wamekisia ilikua labda ilikua (gulf of Suez and Gulf of Aqaba) kaskazini mwisho kwenye (Red Sea) na wengine wanasema yaweza kua baina ya (Bitter lake and Timsah lake) katika eneo la (Suez Canal) Kwa hiyo fundisho hapo usijitie kiburi ukasema wewe una Elimu kushinda wenzio, wewe ndio mwenye kujua zaidi.
Unaingia katika Mwezi wa Ramadhan usione uvivu kusoma na kujifunza mambo yenye faida kubwa na wewe, wacha yapasue moyo wako utapata faida kubwa kabisa ikiwa utazingatia unachokisoma, kumbuka darsa hii inatoka moyoni kwangu kuja moyoni kwako moja kwa moja ili tupate kufanikisha Ramadhan yetu kwa uadilifu na Imani ya hali ya juu kabisa.
" فَلَمَّا بَلَغَا مَجۡمَعَ بَيۡنِهِمَا نَسِيَا حُوتَهُمَا فَٱتَّخَذَ سَبِيلَهُ ۥ فِى ٱلۡبَحۡرِ سَرَبً۬ا "
Basi walipofika wote wawili (Sehemu)zinapoungana (hizo Bahari)walimsahau samaki wao, Naye akashika njia yake kwenda baharini, hali yakuwa inafanya alama.
Hapo yanatokea mambo ya ajabu(mystical) Na ajabu yoyote haitokei mpaka uchoke, ujanja umekwisha, ukaidi huna tena ndio unatulia kufahamu mambo kwa undani kabisa, hapo tena unakua huna msimamo huna chochote ndio ukweli unadhihiri, mambo ya ajabu yanatokea Samaki kishapikwa anashika njia kurudi baharini.
"فَلَمَّا جَاوَزَا قَالَ لِفَتَٮٰهُ ءَاتِنَا غَدَآءَنَا لَقَدۡ لَقِينَا مِن سَفَرِنَا هَـٰذَا نَصَبً۬ا "
Na Walipofika mbele (Nabii Musa)alimwambia (Msaidizi)kijana wake, Tupe chakula chetu cha asubuhi, maana tumepata uchofu katika safari yetu.
Mpaka jitihada zako zimalizike, mpaka uwe ushachoka ndio ukweli unajitokeza, hiyo kufahamishwa Elimu haiji ila kutoka kwa Mwenye enzi Mungu, na wewe inakutokezea wakati mwengine unafanya kitu hupati jawabu, au jina la mtu utalifikiri haliji Akilini, mara umekaa tu na shughuli nyengine linakujia jawabu, na hivyo ni kufahamishwa Elimu zote zinatoka kwake yeye Mjuzi wa kila jambo.
" قَالَ أَرَءَيۡتَ إِذۡ أَوَيۡنَآ إِلَى ٱلصَّخۡرَةِ فَإِنِّى نَسِيتُ ٱلۡحُوتَ وَمَآ أَنسَٮٰنِيهُ إِلَّا ٱلشَّيۡطَـٰنُ أَنۡ أَذۡكُرَهُ ۥۚ وَٱتَّخَذَ سَبِيلَهُ ۥ فِى ٱلۡبَحۡرِ عَجَبً۬ا "
Akasema unaona pale tulipopumzika katika Mlima(Jabali)basi hapo nimesahau(kukupa habari)ya yule Samaki, Na hakuna aliyenisahaulisha isipokua Shetani, nisikumbuke, Naye akashika njia yake baharini kwa namna ya Ajabu. Mambo ya (mystical) lazima yawe ya ajabu, huwezi ku(Explain) na hivyo ndio inavokua katika safari zote za ajabu na kutafuta Elimu, lazima vya zamani visahaulike ili vipya vipate kuingia, usije kushangaa mbona samaki anatembea, mbona hili sijawahi kusomeshwa na Sheikh wangu, utakuja kukosa jambo la muhimu nalo la kupata ujuzi zaidi katika safari hii.
Kwa hiyo napenda kukujulisha kwenye kisa hicho msaidizi wa Nabii Musa a.s na yule samaki wote wanapotea na kusahauliwa, na mimi na maandishi yangu tutapotea katika safari hii utabakia wewe na Faida za Ramadhan na siri yake, pamoja na vazi lake, ni kama Nabii Musa a.s alivobaki na mambo matatu ya hekima alofundishwa na (Mja Mwenye Elimu).
Popote pale inapotajwa siri napenda ufahamu ni kitu chenye kujificha au kufichwa, Kwa hiyo ukisoma kwa moyo ulotulia utapata faida kubwa ya siri hizo, Lakini ukisoma kwa akili mimi tayari najua utajikuta unakwenda safari ya tabu na siku hizi lazima uombe(Visa), utajikuta umebaki na maneno yangu lakini umekosa kile kilichomo ndani ya maneno hayo.
Kutaka kulijua vazi hili la Ucha Mungu endelea part 2
Zimekufikia habari za Mwezi ambao ndani yake kuna Rehma, Kati yake kuna Maghfira(Msamaha), Na Mwisho wake kuna Dhamana.
Vipi basi yanapatikana matatu haya?, hili ndio shiko la darsa yetu ya leo, Ndio safari tutakayo kwenda mimi na wewe kama walivokwenda Nabii Musa a.s na Msaidizi wake, Nini kilitokea kwenye hiyo safari yao, na nini ilikua kusudio ya safari ile?. Quraan sura ya (Al-Kahf )kuanzia aya ya 60.
"وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِفَتَٮٰهُ لَآ أَبۡرَحُ حَتَّىٰٓ أَبۡلُغَ مَجۡمَعَ ٱلۡبَحۡرَيۡنِ أَوۡ أَمۡضِىَ حُقُبً۬ا "
Na (Kumbukeni) Musa alipomwambia kijana(Msaidizi)wake nitaendelea kwenda (hii safari)mpaka nifike katika maungano ya bahari mbili, au niendelee kwa karne(mpaka nikutane na huyo ninayetaka kukutana naye).
Na hivyo ndio inavotakiwa katika kutafuta elimu hakuna kuchoka wala kuzeeka, vipi ilitokea safari hii, Anahadithia Ubai ibn Kaab alimsikia Mtume s.a.w akisema, siku moja Nabii Musa a.s alikua akitoa mawaidha akaulizwa swali hili, Kiumbe gani Mwenye elimu kupita wote, akajibu ni mimi, Hapo Mwenye enzi Mungu akamwambia yuko aliyekuzidi "Ewe Musa" alijibiwa hivyo kwa sababu hajarejesha jawabu hilo kwa Mwenye enzi Mungu na kwa kutaka kufahamishwa akaambiwa nenda utakutana na Mtu huyo kwenye makutano ya Bahari mbili, Sehemu hiyo haijatajwa wapi lakini wanazuoni wamekisia ilikua labda ilikua (gulf of Suez and Gulf of Aqaba) kaskazini mwisho kwenye (Red Sea) na wengine wanasema yaweza kua baina ya (Bitter lake and Timsah lake) katika eneo la (Suez Canal) Kwa hiyo fundisho hapo usijitie kiburi ukasema wewe una Elimu kushinda wenzio, wewe ndio mwenye kujua zaidi.
Unaingia katika Mwezi wa Ramadhan usione uvivu kusoma na kujifunza mambo yenye faida kubwa na wewe, wacha yapasue moyo wako utapata faida kubwa kabisa ikiwa utazingatia unachokisoma, kumbuka darsa hii inatoka moyoni kwangu kuja moyoni kwako moja kwa moja ili tupate kufanikisha Ramadhan yetu kwa uadilifu na Imani ya hali ya juu kabisa.
" فَلَمَّا بَلَغَا مَجۡمَعَ بَيۡنِهِمَا نَسِيَا حُوتَهُمَا فَٱتَّخَذَ سَبِيلَهُ ۥ فِى ٱلۡبَحۡرِ سَرَبً۬ا "
Basi walipofika wote wawili (Sehemu)zinapoungana (hizo Bahari)walimsahau samaki wao, Naye akashika njia yake kwenda baharini, hali yakuwa inafanya alama.
Hapo yanatokea mambo ya ajabu(mystical) Na ajabu yoyote haitokei mpaka uchoke, ujanja umekwisha, ukaidi huna tena ndio unatulia kufahamu mambo kwa undani kabisa, hapo tena unakua huna msimamo huna chochote ndio ukweli unadhihiri, mambo ya ajabu yanatokea Samaki kishapikwa anashika njia kurudi baharini.
"فَلَمَّا جَاوَزَا قَالَ لِفَتَٮٰهُ ءَاتِنَا غَدَآءَنَا لَقَدۡ لَقِينَا مِن سَفَرِنَا هَـٰذَا نَصَبً۬ا "
Na Walipofika mbele (Nabii Musa)alimwambia (Msaidizi)kijana wake, Tupe chakula chetu cha asubuhi, maana tumepata uchofu katika safari yetu.
Mpaka jitihada zako zimalizike, mpaka uwe ushachoka ndio ukweli unajitokeza, hiyo kufahamishwa Elimu haiji ila kutoka kwa Mwenye enzi Mungu, na wewe inakutokezea wakati mwengine unafanya kitu hupati jawabu, au jina la mtu utalifikiri haliji Akilini, mara umekaa tu na shughuli nyengine linakujia jawabu, na hivyo ni kufahamishwa Elimu zote zinatoka kwake yeye Mjuzi wa kila jambo.
" قَالَ أَرَءَيۡتَ إِذۡ أَوَيۡنَآ إِلَى ٱلصَّخۡرَةِ فَإِنِّى نَسِيتُ ٱلۡحُوتَ وَمَآ أَنسَٮٰنِيهُ إِلَّا ٱلشَّيۡطَـٰنُ أَنۡ أَذۡكُرَهُ ۥۚ وَٱتَّخَذَ سَبِيلَهُ ۥ فِى ٱلۡبَحۡرِ عَجَبً۬ا "
Akasema unaona pale tulipopumzika katika Mlima(Jabali)basi hapo nimesahau(kukupa habari)ya yule Samaki, Na hakuna aliyenisahaulisha isipokua Shetani, nisikumbuke, Naye akashika njia yake baharini kwa namna ya Ajabu. Mambo ya (mystical) lazima yawe ya ajabu, huwezi ku(Explain) na hivyo ndio inavokua katika safari zote za ajabu na kutafuta Elimu, lazima vya zamani visahaulike ili vipya vipate kuingia, usije kushangaa mbona samaki anatembea, mbona hili sijawahi kusomeshwa na Sheikh wangu, utakuja kukosa jambo la muhimu nalo la kupata ujuzi zaidi katika safari hii.
Kwa hiyo napenda kukujulisha kwenye kisa hicho msaidizi wa Nabii Musa a.s na yule samaki wote wanapotea na kusahauliwa, na mimi na maandishi yangu tutapotea katika safari hii utabakia wewe na Faida za Ramadhan na siri yake, pamoja na vazi lake, ni kama Nabii Musa a.s alivobaki na mambo matatu ya hekima alofundishwa na (Mja Mwenye Elimu).
Popote pale inapotajwa siri napenda ufahamu ni kitu chenye kujificha au kufichwa, Kwa hiyo ukisoma kwa moyo ulotulia utapata faida kubwa ya siri hizo, Lakini ukisoma kwa akili mimi tayari najua utajikuta unakwenda safari ya tabu na siku hizi lazima uombe(Visa), utajikuta umebaki na maneno yangu lakini umekosa kile kilichomo ndani ya maneno hayo.
Kutaka kulijua vazi hili la Ucha Mungu endelea part 2
RAMADHAN NI VAZI LA UCHA MUNGU PART 2
Asalaam Aleiykum
Tuanze na aya iliyomo kwenye sura ya (Aaraf)aya ya 26, tunalitafuta guo la Ucha Mungu aya hii itatufunganisha na darsa yetu ya leo ili tupate kuanza safari yetu ya uchambuzi, aya inasema nini kuhusu kadhia hii.
يَـٰبَنِىٓ ءَادَمَ قَدۡ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكُمۡ لِبَاسً۬ا يُوَٲرِى سَوۡءَٲتِكُمۡ وَرِيشً۬اۖ وَلِبَاسُ ٱلتَّقۡوَىٰ ذَٲلِكَ خَيۡرٌ۬ۚ ذَٲلِكَ مِنۡ ءَايَـٰتِ ٱللَّهِ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ
Enyi Wanaadamu hakika tumekuteremshieni nguo zifichazo tupu zenu na nguo za pambo, Na nguo za utawa(Ucha Mungu)ndizo bora, hayo ni katika ishara za Mwenye enzi Mungu ili wapate kukumbuka.
Nataka uyatizame maneno mawili yaliyomo katika aya hiyo yanosema (Ishara na Kukumbuka)hayo yatakua na faida kubwa na wewe katika kuifahamu darsa hii.
Naam:tumepewa aina mbili za nguo, ama ile ya kwanza sote tunaijua ni kwa ajili ya kuhifadhi tupu zetu na kadhalika kujipamba, unalikumbuka neno (Ishara) basi inaanzia hapa, kwanini ikatajwa tupu?, kwa sababu jambo la mwanzo Mwanaadamu au tumtaje Baba yetu Nabii Adam na Mama yetu Hawa, walolipata (Awareness)Fahamu Waligundua tupu zao. Vipi hilo linahusiana na (Saum) ya Mwezi wa Ramadhan?, endelea kusoma kwa uangalifu ili uzipate (ishara), maana ya Ishara ni kuashiria jambo.
"Ewe Adam Msiukaribie mti huu mkala tunda lake" Pasipo na uwerevu, na ushawishi wa (Shetani)wakapinga Amri ya Mwenye enzi Mungu wakala tunda kutoka kwenye ule mti na kutolewa Peponi, Yote haya yamehusiana na hiyo (Awareness)Fahamu waloipata, ndio sasa ikaonekana itakua shida kuishi katika Ulimwengu huu, vipi tutatizamana na vizazi vyetu, vipi tutawaangalia wazee wetu ndipo Mollah akatuteremshia vazi la kujistiri, Na hii imekwenda (Deep)hata yale Makabila (Primitive)yanafunika tupu zao, kwa sababu ingekua hatari ee tunafunika hali hii(sex)imo mawazoni nyakati zote, ukiona mtu kajipamba unawacha mpaka(tasbih).
Kilichokusudiwa kuhifadhiwa Rasmi sio hiyo tupu kumbuka kuna neno ishara ambalo linaashiria kuhifadhiwa na kutulizwa ni hiyo (Mind)yako(Akili), au ita (awareness), hilo ndilo kusudio ya guo la kwanza lilotajwa kwenye hiyo aya. Kumbuka umo katika Safari ya kulijua Vazi la Ucha Mungu katika Mwezi huu wa Ramadhan, Vipi tuifunge na vipi tuipate Taqwa inokuja na hayo mambo matatu yalotajwa mwanzoni mwa Darsa hii.
Sasa Wacha tulifungue Guo la pili ambalo ndio hilo vazi la Ucha Mungu.
Endelea Part 3
Tuanze na aya iliyomo kwenye sura ya (Aaraf)aya ya 26, tunalitafuta guo la Ucha Mungu aya hii itatufunganisha na darsa yetu ya leo ili tupate kuanza safari yetu ya uchambuzi, aya inasema nini kuhusu kadhia hii.
يَـٰبَنِىٓ ءَادَمَ قَدۡ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكُمۡ لِبَاسً۬ا يُوَٲرِى سَوۡءَٲتِكُمۡ وَرِيشً۬اۖ وَلِبَاسُ ٱلتَّقۡوَىٰ ذَٲلِكَ خَيۡرٌ۬ۚ ذَٲلِكَ مِنۡ ءَايَـٰتِ ٱللَّهِ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ
Enyi Wanaadamu hakika tumekuteremshieni nguo zifichazo tupu zenu na nguo za pambo, Na nguo za utawa(Ucha Mungu)ndizo bora, hayo ni katika ishara za Mwenye enzi Mungu ili wapate kukumbuka.
Nataka uyatizame maneno mawili yaliyomo katika aya hiyo yanosema (Ishara na Kukumbuka)hayo yatakua na faida kubwa na wewe katika kuifahamu darsa hii.
Naam:tumepewa aina mbili za nguo, ama ile ya kwanza sote tunaijua ni kwa ajili ya kuhifadhi tupu zetu na kadhalika kujipamba, unalikumbuka neno (Ishara) basi inaanzia hapa, kwanini ikatajwa tupu?, kwa sababu jambo la mwanzo Mwanaadamu au tumtaje Baba yetu Nabii Adam na Mama yetu Hawa, walolipata (Awareness)Fahamu Waligundua tupu zao. Vipi hilo linahusiana na (Saum) ya Mwezi wa Ramadhan?, endelea kusoma kwa uangalifu ili uzipate (ishara), maana ya Ishara ni kuashiria jambo.
"Ewe Adam Msiukaribie mti huu mkala tunda lake" Pasipo na uwerevu, na ushawishi wa (Shetani)wakapinga Amri ya Mwenye enzi Mungu wakala tunda kutoka kwenye ule mti na kutolewa Peponi, Yote haya yamehusiana na hiyo (Awareness)Fahamu waloipata, ndio sasa ikaonekana itakua shida kuishi katika Ulimwengu huu, vipi tutatizamana na vizazi vyetu, vipi tutawaangalia wazee wetu ndipo Mollah akatuteremshia vazi la kujistiri, Na hii imekwenda (Deep)hata yale Makabila (Primitive)yanafunika tupu zao, kwa sababu ingekua hatari ee tunafunika hali hii(sex)imo mawazoni nyakati zote, ukiona mtu kajipamba unawacha mpaka(tasbih).
Kilichokusudiwa kuhifadhiwa Rasmi sio hiyo tupu kumbuka kuna neno ishara ambalo linaashiria kuhifadhiwa na kutulizwa ni hiyo (Mind)yako(Akili), au ita (awareness), hilo ndilo kusudio ya guo la kwanza lilotajwa kwenye hiyo aya. Kumbuka umo katika Safari ya kulijua Vazi la Ucha Mungu katika Mwezi huu wa Ramadhan, Vipi tuifunge na vipi tuipate Taqwa inokuja na hayo mambo matatu yalotajwa mwanzoni mwa Darsa hii.
Sasa Wacha tulifungue Guo la pili ambalo ndio hilo vazi la Ucha Mungu.
Endelea Part 3
RAMADHAN NI VAZI LA UCHA MUNGU PART 3
Asalaam Aleiykum
Tumekwisha kuona au kusoma au kujua vipi (awareness)Fahamu zetu zinavokua zikikutana na jambo la (tupu), vipi akili ina haribika, uharibifu gani unatokea, na sasa tunajua nini kinatokea kama kitu hicho kitafunikwa. Sasa ni wakati wa kulihudhuria Vazi la pili la Ucha Mungu, lile la mwanzo ni Vazi la (Mind)Akili na Utupu, Na hili la Pili ni la (Roho)na Ibada.
Kazi yetu kubwa hapa ni kujua vipi tutalivaa, basi kama aya ilivosema vazi hilo ni bora kwenu na hizo ni (alama)kutoka kwa Mollah wetu ili tupate "kukumbuka". Naendelea kukuonesha tena neno "(kukumbuka)", nakutaka ukumbuke lile vazi la kwanza Nje ni Guo na ndani ni utulivu, Na hili la Pili Nje (Action) ndani Mapenzi, Nini Utulivu? Utulivu ni (Peace)Islam(Surrender), Nini Mapenzi? ni (Bliss).
Kutokana na hayo Mapenzi wewe ndio umeumbwa, kutokana na hayo mapenzi wewe ndio unaishi, kutokana na hayo mapenzi wewe Unaruzukiwa, kutokana na hayo mapenzi Ulimwengu huu unamsabahi Mwenye enzi Mungu, Sasa na wewe unakumbushwa jiunge na Mapenzi hayo ili upate Furaha, upate afya na uipate Pepo ya Mollah wako, Na sharti lenyewe la kujiunga ni lazima uvae hili vazi la Ucha Mungu, unatakiwa bila ya kulazimishwa Umpende Mollah wako, uwapende viumbe wenzako, na utende yalo mema.
Ikiwa utafanya hivo kwa uadilifu kwa upande wake Mwenye enzi Mungu atakupa hayo mambo matatu ambayo yamo katika hiyo Ramadhan, Rehma, Maghfira na Dhamana ya kutoingia motoni.
Vipi tutalivaa Guo hili la Taqwa?
Kumbuka bado tumo kwenye safari yetu ya kutafuta vazi la Taqwa na sasa tunachukua aya hususia iloamrisha kufunga Ramadhan(Baqara 183).
"يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡڪُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِڪُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ "
Enyi Mloamini Mmelazimishwa kufunga(saumu)kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu.
Kabla ya kuendelea mbele wacha turudi nyuma tukalihudhurie lile tukio maarufu la mwanzo waloambiwa wazee wetu Bwana Adam na Bibi Hawa walipokatazwa wasile tunda kwenye ule mti, Nini kiliwatokezea walipokwenda kinyume na Amri ya Mwenye enzi Mungu? walipata (Awareness)Fahamu.
Basi Napenda utambue na hivi sasa mnaamrishwa tena msile(Fungeni) Nini Kinapatikana?, Hapa itabidi mnipe nafasi nifafanue japo kwa ufupi ili mpate kunifahamu, Napenda kufahamisha kuwa kuna vitu vitatu vinatokea kwa Mollah wetu navyo ni hivi(From awareness to intelligence from intelligence to love) Na hayo Mapenzi ndio zawadi ya juu Mja kushushiwa kutoka kwa Mollah wako, Nisiseme Mapenzi watu (Wakaanza kuchemsha Supu za Pweza, wengine wakatafuta uji wa kungu manga, na wengine kumtafuta ndege kisiji)sio aina hiyo ya mapenzi, Mapenzi yalokusudiwa hapo yale yanokuja bila sababu, yale unatoa huhitaji malipo, yale ambayo uko radhi kulala na njaa mwenzio apate kula yeye, mapenzi ya mfano wa Mama hatarajii hata kama utampenda kama anavokupenda yeye, yeye anafanya (for the sake of Love)Sasa nini unapata kama utafunga kikweli kweli kwa Imani ya juu kabisa? hapa inabidi ukumbuke tena ulipokula tunda ulipata (Awareness)Fahamu, na sasa kitu cha mwanzo unapata nini?
Endelea part 4
Tumekwisha kuona au kusoma au kujua vipi (awareness)Fahamu zetu zinavokua zikikutana na jambo la (tupu), vipi akili ina haribika, uharibifu gani unatokea, na sasa tunajua nini kinatokea kama kitu hicho kitafunikwa. Sasa ni wakati wa kulihudhuria Vazi la pili la Ucha Mungu, lile la mwanzo ni Vazi la (Mind)Akili na Utupu, Na hili la Pili ni la (Roho)na Ibada.
Kazi yetu kubwa hapa ni kujua vipi tutalivaa, basi kama aya ilivosema vazi hilo ni bora kwenu na hizo ni (alama)kutoka kwa Mollah wetu ili tupate "kukumbuka". Naendelea kukuonesha tena neno "(kukumbuka)", nakutaka ukumbuke lile vazi la kwanza Nje ni Guo na ndani ni utulivu, Na hili la Pili Nje (Action) ndani Mapenzi, Nini Utulivu? Utulivu ni (Peace)Islam(Surrender), Nini Mapenzi? ni (Bliss).
Kutokana na hayo Mapenzi wewe ndio umeumbwa, kutokana na hayo mapenzi wewe ndio unaishi, kutokana na hayo mapenzi wewe Unaruzukiwa, kutokana na hayo mapenzi Ulimwengu huu unamsabahi Mwenye enzi Mungu, Sasa na wewe unakumbushwa jiunge na Mapenzi hayo ili upate Furaha, upate afya na uipate Pepo ya Mollah wako, Na sharti lenyewe la kujiunga ni lazima uvae hili vazi la Ucha Mungu, unatakiwa bila ya kulazimishwa Umpende Mollah wako, uwapende viumbe wenzako, na utende yalo mema.
Ikiwa utafanya hivo kwa uadilifu kwa upande wake Mwenye enzi Mungu atakupa hayo mambo matatu ambayo yamo katika hiyo Ramadhan, Rehma, Maghfira na Dhamana ya kutoingia motoni.
Vipi tutalivaa Guo hili la Taqwa?
Kumbuka bado tumo kwenye safari yetu ya kutafuta vazi la Taqwa na sasa tunachukua aya hususia iloamrisha kufunga Ramadhan(Baqara 183).
"يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡڪُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِڪُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ "
Enyi Mloamini Mmelazimishwa kufunga(saumu)kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu.
Kabla ya kuendelea mbele wacha turudi nyuma tukalihudhurie lile tukio maarufu la mwanzo waloambiwa wazee wetu Bwana Adam na Bibi Hawa walipokatazwa wasile tunda kwenye ule mti, Nini kiliwatokezea walipokwenda kinyume na Amri ya Mwenye enzi Mungu? walipata (Awareness)Fahamu.
Basi Napenda utambue na hivi sasa mnaamrishwa tena msile(Fungeni) Nini Kinapatikana?, Hapa itabidi mnipe nafasi nifafanue japo kwa ufupi ili mpate kunifahamu, Napenda kufahamisha kuwa kuna vitu vitatu vinatokea kwa Mollah wetu navyo ni hivi(From awareness to intelligence from intelligence to love) Na hayo Mapenzi ndio zawadi ya juu Mja kushushiwa kutoka kwa Mollah wako, Nisiseme Mapenzi watu (Wakaanza kuchemsha Supu za Pweza, wengine wakatafuta uji wa kungu manga, na wengine kumtafuta ndege kisiji)sio aina hiyo ya mapenzi, Mapenzi yalokusudiwa hapo yale yanokuja bila sababu, yale unatoa huhitaji malipo, yale ambayo uko radhi kulala na njaa mwenzio apate kula yeye, mapenzi ya mfano wa Mama hatarajii hata kama utampenda kama anavokupenda yeye, yeye anafanya (for the sake of Love)Sasa nini unapata kama utafunga kikweli kweli kwa Imani ya juu kabisa? hapa inabidi ukumbuke tena ulipokula tunda ulipata (Awareness)Fahamu, na sasa kitu cha mwanzo unapata nini?
Endelea part 4
RAMADHAN NI VAZI LA UCHA MUNGU PART 4
Asalaam Aleiykum
Kitu cha Mwanzo safari hii upatacho ni (awareness of Love) vipi inakua, pengine Mja siku zote mambo haya yanakutokezea huyajui, basi anza kuyajua mambo haya kwenye Ramadhan yako ya mwanzo ili usikose makusudio na faida ya Ramadhan. Kitu cha mwanzo kama utachunguza wakati unavaa guo hili la (Taqwa) ni njaa, wewe umezoea wakati wote unakula asubuhi, mchana na usiku, leo umefika ule wakati hujatia chakula, hapo mazoea yanaondoka inakuja(1) (Awareness of Body)Fahamu ya mwili wako, unahitaji chakula wakati wake ushafika na wewe huupi chakula, Na vyakula vyote vimo kwenye nyumba na Mahotelini na madukani vinauzwa, lakini wewe kwa Mapenzi tu ya kufata amri ya Mollah wako leo Umefunga hugusi chakula.
(2)(Mind)Akili inataka mambo yake ya kusema watu, kuzini, kudhulumu,wizi,rushwa,mazungumzo yasofaa, kutizama mambo machafu, wewe umekazana hutekelezi amri za akili, ukiweza kwenda (Beyond) vitu viwili hivyo ndipo unapojikuta wewe ni (Pure Soul)Roho safi, hapo ndipo yanapokaa ita(Mapenzi)(Dhikr)(Watch)(Witness)(Remember)(Kukumbuka)(Mindful)ita jina lolote lakini hapo ndipo kwenye kusudio la (Saumu)hapo ndipo kwenye hiyo(Itikaf)unakua huna fikra chafu ila kumkumbuka Mollah wako, una (Watch)kila kitu lakini hushiriki, njaa inakuja,watu wanaendelea na upuuzi wao wewe unabaki kuwa shahidi tu, unaishi katika hali ya kusikia na kuona mambo yote yanatokea lakini wewe hayakugusi, Unaishi kwenye (Roho)uko (Alert)wakati wote unakumbuka unamtaja Mollah wako ukiwa katika hali ya (Full Aware).
Napenda nikumbushe tena wakati ule wa mwanzo Mzee wetu Adam alivopata (Awareness) kapata katika hali ya kuasi kutokana na (kutokujua). Lakini safari hii wewe umo kwenye werevu(Awareness)Fahamu yenye kutii, umejaa mapenzi ya Mollah wako, umejifunga kutekeleza amri yake, umevijua kua Mwili una njaa, na Akili ina mshipa wa Maasi vyote hivyo umeweza kuvimudu na kuvishinda, sasa umefika wakati wa kusema Mollah wangu nimeyefanya haya kwa ajili yako Mollah wangu.(Quraan Al-Anaam-162)
"قُلۡ إِنَّ صَلَاتِى وَنُسُكِى وَمَحۡيَاىَ وَمَمَاتِى لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَـٰلَمِينَ "
Sema,Hakika Sala yangu, Na Ibada zangu, na Uzima wangu, Na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenye enzi Mungu Muumba wa walimwengu wote.
Kutokana na Uwezo huo mimi nasimama kutekeleza vitendo vya mapenzi Mollah wangu, kama vipi?
Endelea part 5
Kitu cha Mwanzo safari hii upatacho ni (awareness of Love) vipi inakua, pengine Mja siku zote mambo haya yanakutokezea huyajui, basi anza kuyajua mambo haya kwenye Ramadhan yako ya mwanzo ili usikose makusudio na faida ya Ramadhan. Kitu cha mwanzo kama utachunguza wakati unavaa guo hili la (Taqwa) ni njaa, wewe umezoea wakati wote unakula asubuhi, mchana na usiku, leo umefika ule wakati hujatia chakula, hapo mazoea yanaondoka inakuja(1) (Awareness of Body)Fahamu ya mwili wako, unahitaji chakula wakati wake ushafika na wewe huupi chakula, Na vyakula vyote vimo kwenye nyumba na Mahotelini na madukani vinauzwa, lakini wewe kwa Mapenzi tu ya kufata amri ya Mollah wako leo Umefunga hugusi chakula.
(2)(Mind)Akili inataka mambo yake ya kusema watu, kuzini, kudhulumu,wizi,rushwa,mazungumzo yasofaa, kutizama mambo machafu, wewe umekazana hutekelezi amri za akili, ukiweza kwenda (Beyond) vitu viwili hivyo ndipo unapojikuta wewe ni (Pure Soul)Roho safi, hapo ndipo yanapokaa ita(Mapenzi)(Dhikr)(Watch)(Witness)(Remember)(Kukumbuka)(Mindful)ita jina lolote lakini hapo ndipo kwenye kusudio la (Saumu)hapo ndipo kwenye hiyo(Itikaf)unakua huna fikra chafu ila kumkumbuka Mollah wako, una (Watch)kila kitu lakini hushiriki, njaa inakuja,watu wanaendelea na upuuzi wao wewe unabaki kuwa shahidi tu, unaishi katika hali ya kusikia na kuona mambo yote yanatokea lakini wewe hayakugusi, Unaishi kwenye (Roho)uko (Alert)wakati wote unakumbuka unamtaja Mollah wako ukiwa katika hali ya (Full Aware).
Napenda nikumbushe tena wakati ule wa mwanzo Mzee wetu Adam alivopata (Awareness) kapata katika hali ya kuasi kutokana na (kutokujua). Lakini safari hii wewe umo kwenye werevu(Awareness)Fahamu yenye kutii, umejaa mapenzi ya Mollah wako, umejifunga kutekeleza amri yake, umevijua kua Mwili una njaa, na Akili ina mshipa wa Maasi vyote hivyo umeweza kuvimudu na kuvishinda, sasa umefika wakati wa kusema Mollah wangu nimeyefanya haya kwa ajili yako Mollah wangu.(Quraan Al-Anaam-162)
"قُلۡ إِنَّ صَلَاتِى وَنُسُكِى وَمَحۡيَاىَ وَمَمَاتِى لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَـٰلَمِينَ "
Sema,Hakika Sala yangu, Na Ibada zangu, na Uzima wangu, Na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenye enzi Mungu Muumba wa walimwengu wote.
Kutokana na Uwezo huo mimi nasimama kutekeleza vitendo vya mapenzi Mollah wangu, kama vipi?
Endelea part 5
RAMADHAN NI VAZI LA UCHA MUNGU PART 5
Asalaam Aleiykum
Mapenzi hayajulikani, lakini vitendo vyake vinajulikana ndio watu wakasema fulani anapenda, Na kama wewe ni kweli mpenzi wa Mungu basi matendo yako yatakua kulisha maskini, Kuwaangalia mayatima, kuwapa haki ndugu jamaa na marafiki, kujishughulisha kuwasaidia hata wapita njia, na kuwatunza mpaka wanyama wenye kuishi katika Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Kujiepusha na kila jambo baya ambalo Mwenye enzi Mungu amelikataza, pia kujielewa miezi yote kumi na moja ulikua hujavaa guo la Ucha Mungu, ona haya Mollah wako anakuona, Malaika wanakuona kua huna cha kukusitiri, upo Mtupu, sasa umekujia Mwezi huu Mtukufu omba sana kwa Mollah wako akuvike guo hili la mapenzi, Sema nitie mapenzi niwe nakuabudu japo sikuoni, hakika mimi mapenzi siyajui, ila nasubiri kutoka katika enzi yako unipe mapenzi kama ulivonipa (awareness)Fahamu.
Basi nipe mapenzi ya kukupenda wewe niwe Rafiki yako wa (kimya), Nipe mapenzi nivipende viumbe vyako na kuwa karibu na wewe, Nitie matumaini ya kupata Rehma zako kwenye kumi hili la mwanzo, nipe mapenzi yako unisamehe kwenye kumi lako la pili, Nifanye niwe katika waja wako walio karibu na wewe, Ikisha nichukulie mimi dhamana ya kutoingia motoni.
Mollah wangu Najua Mwenye kulivaa guo lako la Ucha Mungu hapati tabu kwenye maisha, hana mahuzuniko wala shida katika Uhai wake, Na daima yumo Furahani kwa kupata Rehma, Kheri, Na Neema zako wewe Subhanna.
Basi na Mimi ntakapolivaa guo hili la Ucha Mungu nijaalie nidumu nalo kwa Rehma zako, isije ikawa ikisha Ramadhan nalivua tena kwa kulichana chana guo hili. Niepushe mimi na kuvaa nguo za chuki, dhulma na balaa za ujambazi wa Kiroho.
Mollah wangu wewe ni mwenye kuona na kusikia basi natuma maombi yangu nikitaraji utanikubalia. Ipate hali hiyo utakua umeipata Saumu, ipate hali hiyo utayapata mapenzi ya Mwenye enzi Mungu.
Mapenzi hayajulikani, lakini vitendo vyake vinajulikana ndio watu wakasema fulani anapenda, Na kama wewe ni kweli mpenzi wa Mungu basi matendo yako yatakua kulisha maskini, Kuwaangalia mayatima, kuwapa haki ndugu jamaa na marafiki, kujishughulisha kuwasaidia hata wapita njia, na kuwatunza mpaka wanyama wenye kuishi katika Ufalme wa Mwenye enzi Mungu.
Kujiepusha na kila jambo baya ambalo Mwenye enzi Mungu amelikataza, pia kujielewa miezi yote kumi na moja ulikua hujavaa guo la Ucha Mungu, ona haya Mollah wako anakuona, Malaika wanakuona kua huna cha kukusitiri, upo Mtupu, sasa umekujia Mwezi huu Mtukufu omba sana kwa Mollah wako akuvike guo hili la mapenzi, Sema nitie mapenzi niwe nakuabudu japo sikuoni, hakika mimi mapenzi siyajui, ila nasubiri kutoka katika enzi yako unipe mapenzi kama ulivonipa (awareness)Fahamu.
Basi nipe mapenzi ya kukupenda wewe niwe Rafiki yako wa (kimya), Nipe mapenzi nivipende viumbe vyako na kuwa karibu na wewe, Nitie matumaini ya kupata Rehma zako kwenye kumi hili la mwanzo, nipe mapenzi yako unisamehe kwenye kumi lako la pili, Nifanye niwe katika waja wako walio karibu na wewe, Ikisha nichukulie mimi dhamana ya kutoingia motoni.
Mollah wangu Najua Mwenye kulivaa guo lako la Ucha Mungu hapati tabu kwenye maisha, hana mahuzuniko wala shida katika Uhai wake, Na daima yumo Furahani kwa kupata Rehma, Kheri, Na Neema zako wewe Subhanna.
Basi na Mimi ntakapolivaa guo hili la Ucha Mungu nijaalie nidumu nalo kwa Rehma zako, isije ikawa ikisha Ramadhan nalivua tena kwa kulichana chana guo hili. Niepushe mimi na kuvaa nguo za chuki, dhulma na balaa za ujambazi wa Kiroho.
Mollah wangu wewe ni mwenye kuona na kusikia basi natuma maombi yangu nikitaraji utanikubalia. Ipate hali hiyo utakua umeipata Saumu, ipate hali hiyo utayapata mapenzi ya Mwenye enzi Mungu.
Sunday, May 1, 2016
MILANGO MINNE YA DHANMBI PART 1
Asalaam Aleiykum
Pata fursa nzuri ya kuijua Milango hii minne ya Dhanmbi inayotutesa sisi Walimwengu mpaka tukawa tunaishi bila ya Raha, tunaishi na Maradhi ya Dhanmbi, tunaishi kinyume na sheria za Ulimwengu huu, na sababu kubwa ni kupita kwetu kwenye Milango hii na kuingia kwenye hicho chumba chenye kuishi Dhanmbi.
Vipi tunaingia katika chumba hicho ndio chanzo cha darsa ya leo, Na dhumuni kubwa ni kukufanya usiwe unatumia milango hii kuingia kwenye hicho chumba.Labda tukikuonesha Alama na kukwambia (No Entry)pengine Mja unaweza kuepuka mateso na maangamizi yaletwayo na Dhanmbi.
Dhanmbi ilikujaje?, Ilikuja ili kutizamwa Mwanaadamu utamtii Mollah wako pale utakapo kula tunda la kujua, ndio maana kabla ya kula tunda hili unakua huna dhanmbi, na muda mchache baada ya kula unapata bahati ya kusamehewa, lakini matatizo yanakuja ukenda kuchuma tena au kuendelea kuishi kwenye bustani hii ya Dhanmbi.
Nini Dhanmbi?
Ili usije ukajichanganya kwenye ufafanuzi wacha nikupe tafsiri ya neno dhanmbi, Dhanmbi ni makatazo yote yaendayo kinyume na sheria za Mwenye enzi Mungu, Hapa nimetaja makatazo ili usibabaishwe na tafsiri ya neno Maamrisho, (Maamrisho na Makatazo)ni maneno mawili tafauti.
Naam hiyo ndio Dhanmbi, Sasa vipi unaingia?. ili kujua vipi unaingia itabidi kama ilivyo kawaida yetu tuombe muongozo au tusome aya ndani ya (Quraan) ili itujulishe kitu kilichomo ndani ya Bahari hii ya (Milango Minne ya Dhanmbi), na utakapo pata fahamu za kuelewa sababu zake hapo tena utachukua hatua za kujiepusha au kutumia milango hii ya dhanmbi.
Napenda kukumbusha tena jumba hili japokuwa lina milango minne lakini lina vyumba vingi, kuna vyumba vya Haram ambavyo ndio (Dhanmbi) na kadhalika kuna vyumba vya Halali ambavyo ni (Thawabu) na vyenginevyo. Hapa leo tunashughulika na vyumba hivi vya (Dhanmbi) na aya ya ukumbusho inasemaje kuhusiana na kadhia hii ya Milango.(An-Nisaa-17)
إِنَّمَا ٱلتَّوۡبَةُ عَلَى ٱللَّهِ لِلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسُّوٓءَ بِجَهَـٰلَةٍ۬ ثُمَّ يَتُوبُونَ مِن قَرِيبٍ۬ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ يَتُوبُ ٱللَّهُ عَلَيۡہِمۡۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَڪِيمً۬ا
"Toba Inayopokelewa na Mwenye Enzi Mungu ni ya Wale wanaofanya uovu(Dhanmbi)kwa Ujinga, ikisha wakatubia kwa upesi, hao ndio Mwenye Enzi Mungu huipokea Toba yao, Na Mwenye Enzi Mungu ni Mjuzi na Mwenye Hekima".
Kitu cha mwanzo kabisa napenda nikujulishe kuwa daima (Ujinga unambatana na Werevu) aya inayofatia ya (18)ikaendelea na kusema.
وَلَيۡسَتِ ٱلتَّوۡبَةُ لِلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِ حَتَّىٰٓ إِذَا حَضَرَ أَحَدَهُمُ ٱلۡمَوۡتُ قَالَ إِنِّى تُبۡتُ ٱلۡـَٔـٰنَ وَلَا ٱلَّذِينَ يَمُوتُونَ وَهُمۡ ڪُفَّارٌۚ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ أَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابًا أَلِيمً۬ا
"Hawana Toba wale ambao hufanya maovu mpaka mauti yamemhudhuria mmoja wao, Akasema, Hakika mimi sasa natubu, Na (Hawana Toba)wale ambao wanakufa katika hali ukafiri, hao tumewaandalia adhabu iumizayo."
Sasa nini kinatokezea kutokana na meneno yaliyomo kwenye aya mbili hizi, ili kupata faida zake endelea part 2
Pata fursa nzuri ya kuijua Milango hii minne ya Dhanmbi inayotutesa sisi Walimwengu mpaka tukawa tunaishi bila ya Raha, tunaishi na Maradhi ya Dhanmbi, tunaishi kinyume na sheria za Ulimwengu huu, na sababu kubwa ni kupita kwetu kwenye Milango hii na kuingia kwenye hicho chumba chenye kuishi Dhanmbi.
Vipi tunaingia katika chumba hicho ndio chanzo cha darsa ya leo, Na dhumuni kubwa ni kukufanya usiwe unatumia milango hii kuingia kwenye hicho chumba.Labda tukikuonesha Alama na kukwambia (No Entry)pengine Mja unaweza kuepuka mateso na maangamizi yaletwayo na Dhanmbi.
Dhanmbi ilikujaje?, Ilikuja ili kutizamwa Mwanaadamu utamtii Mollah wako pale utakapo kula tunda la kujua, ndio maana kabla ya kula tunda hili unakua huna dhanmbi, na muda mchache baada ya kula unapata bahati ya kusamehewa, lakini matatizo yanakuja ukenda kuchuma tena au kuendelea kuishi kwenye bustani hii ya Dhanmbi.
Nini Dhanmbi?
Ili usije ukajichanganya kwenye ufafanuzi wacha nikupe tafsiri ya neno dhanmbi, Dhanmbi ni makatazo yote yaendayo kinyume na sheria za Mwenye enzi Mungu, Hapa nimetaja makatazo ili usibabaishwe na tafsiri ya neno Maamrisho, (Maamrisho na Makatazo)ni maneno mawili tafauti.
Naam hiyo ndio Dhanmbi, Sasa vipi unaingia?. ili kujua vipi unaingia itabidi kama ilivyo kawaida yetu tuombe muongozo au tusome aya ndani ya (Quraan) ili itujulishe kitu kilichomo ndani ya Bahari hii ya (Milango Minne ya Dhanmbi), na utakapo pata fahamu za kuelewa sababu zake hapo tena utachukua hatua za kujiepusha au kutumia milango hii ya dhanmbi.
Napenda kukumbusha tena jumba hili japokuwa lina milango minne lakini lina vyumba vingi, kuna vyumba vya Haram ambavyo ndio (Dhanmbi) na kadhalika kuna vyumba vya Halali ambavyo ni (Thawabu) na vyenginevyo. Hapa leo tunashughulika na vyumba hivi vya (Dhanmbi) na aya ya ukumbusho inasemaje kuhusiana na kadhia hii ya Milango.(An-Nisaa-17)
إِنَّمَا ٱلتَّوۡبَةُ عَلَى ٱللَّهِ لِلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسُّوٓءَ بِجَهَـٰلَةٍ۬ ثُمَّ يَتُوبُونَ مِن قَرِيبٍ۬ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ يَتُوبُ ٱللَّهُ عَلَيۡہِمۡۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَڪِيمً۬ا
"Toba Inayopokelewa na Mwenye Enzi Mungu ni ya Wale wanaofanya uovu(Dhanmbi)kwa Ujinga, ikisha wakatubia kwa upesi, hao ndio Mwenye Enzi Mungu huipokea Toba yao, Na Mwenye Enzi Mungu ni Mjuzi na Mwenye Hekima".
Kitu cha mwanzo kabisa napenda nikujulishe kuwa daima (Ujinga unambatana na Werevu) aya inayofatia ya (18)ikaendelea na kusema.
وَلَيۡسَتِ ٱلتَّوۡبَةُ لِلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِ حَتَّىٰٓ إِذَا حَضَرَ أَحَدَهُمُ ٱلۡمَوۡتُ قَالَ إِنِّى تُبۡتُ ٱلۡـَٔـٰنَ وَلَا ٱلَّذِينَ يَمُوتُونَ وَهُمۡ ڪُفَّارٌۚ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ أَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابًا أَلِيمً۬ا
"Hawana Toba wale ambao hufanya maovu mpaka mauti yamemhudhuria mmoja wao, Akasema, Hakika mimi sasa natubu, Na (Hawana Toba)wale ambao wanakufa katika hali ukafiri, hao tumewaandalia adhabu iumizayo."
Sasa nini kinatokezea kutokana na meneno yaliyomo kwenye aya mbili hizi, ili kupata faida zake endelea part 2
Subscribe to:
Posts (Atom)