Asalaam Aleiykum
Tumeingia ndani ya mwezi wa (December), ama kwa sisi wenye kuishi nchi za ulaya tunafahamu vipi kiza kinavo utawala mchana wetu, Sio kuwa mchana unakua mfupi tu, Bali hata Akili zetu zinafunikwa na huzuni ya kuikosa Taa hii ya jua ambayo ndio tegemezi ya mchangamko wa furaha. Madhara ya kukosa jua yanajulikana na yako mengi lakini leo hapa sio uwanja wake wa kuyazungumza, leo ni siku ya Taa, tunataka tujue siri zake taa ili tupate faida mbili tatu za hichi kitu kiitwacho (Taa au Nuru).
Nini Taa?
Kulijibu swali hili itabidi tutafute baadhi ya mashiko yenye kuhusiana na Taa, Taa au Nuru Hakuna Mwenye kuijua, wala aliyeiona, au atakae iona, huo ndio Muujiza katika miujiza mingi ya Taa. Hakuna sehemu nzuri ilipozungumzwa Taa kama katika sura ya (Noor aya ya 35)
"ٱللَّهُ نُورُ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ مَثَلُ نُورِهِۦ كَمِشۡكَوٰةٍ۬ فِيہَا مِصۡبَاحٌۖ ٱلۡمِصۡبَاحُ فِى زُجَاجَةٍۖ ٱلزُّجَاجَةُ كَأَنَّہَا كَوۡكَبٌ۬ دُرِّىٌّ۬ يُوقَدُ مِن شَجَرَةٍ۬ مُّبَـٰرَڪَةٍ۬ زَيۡتُونَةٍ۬ لَّا شَرۡقِيَّةٍ۬ وَلَا غَرۡبِيَّةٍ۬ يَكَادُ زَيۡتُہَا يُضِىٓءُ وَلَوۡ لَمۡ تَمۡسَسۡهُ نَارٌ۬ۚ نُّورٌ عَلَىٰ نُورٍ۬ۗ يَہۡدِى ٱللَّهُ لِنُورِهِۦ مَن يَشَآءُۚ وَيَضۡرِبُ ٱللَّهُ ٱلۡأَمۡثَـٰلَ لِلنَّاسِۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَىۡءٍ عَلِيمٌ۬"
"Mwenye enzi Mungu ni Nuru Ya Mbingu na Ardhi, Mfano wa Nuru yake ni kama Shubaka ndani yake (inakaa) Taa, Taa (ile imo)katika tungi(mfano Chemni)Tungi(Lile ni)ni kama nyota ingarayo, inayowashwa (Taa hiyo kwa mafuta yanayotoka)Katika Mti ulobarikiwa wa mzeituni, usio (Upande) wa Mashariki wala wa Magharibi, Yanakaribia mafuta yake kungara (Wenyewe) ingawa moto haujayagusa, Nuru juu ya nuru Mwenye enzi Mungu humuongoza katika Nuru yake amtakaye, Na Mwenye enzi Mungu hupiga mifano kwa watu, Na Mwenye enzi Mungu ni mjuzi wa kila kitu".
Naam tunaingia katika sayansi ya Quraan lazima uwe makini kukijua kinaelezwa nini ili upate kuifahamu darsa hii kwa ufanisi wa hali ya juu dhamira na makusudio yake ili upate kuijua faida ya Taa.
Aya inasema Mwenye enzi Mungu ni Nuru ya Mbingu na Ardhi, Kuna baadhi ya watu wakadhani hiyo Nuru ndio ufalme wenyewe kashajitaja.(Kumbuka Mollah wako hana alicho fanana nacho vipi fikra zako zikupeleke kwenye Nuru).Kumbuka kuna vitu viwili vimeumbwa kimoja tumeoneshwa chengine tumefichiwa na Muujiza wenyewe vyote hatuvijui mpaka leo, Cha mwanzo ni hiyo (Dark Matter)(Dhulumati)tunajua ipo (Kiza) lakini hatuwezi kukishika, Na hii (Light) hatujui ni kitu gani, tunachojua sisi kama Taa haipo kinatawala kiza, Taa ikiletwa kiza kinatoweka tunaona vilivyokua vimefunikwa wakati taa ilipoondokaa, Kwa hiyo Tunachojua sisi ni vile vinovyo murikwa na taa lakini hatuifahamu taa yenyewe.
Nini (Light)Taa.?
Endelea part 2
Saturday, December 2, 2017
MIUJIZA YA TAA PART 2
Asalaam Aleiykum
Sasa tuingie katika uchambuzi wa Nuru yenyewe ilivyo. katika utendaji wake kazi Mollah wetu akataja "Mfano wa Nuru yake ni kama shubaka" itabidi twende taratibu upate kunifahamu, ambayo imewekwa hiyo taa, taa hiyo imo kwenye tungi,(Kama chemni au hizi zenu za kisasa).
(1)Wanasayansi Wa Ulimwengu huu wanatwambia nini kuhusu Taa, Walipoifanyia Uchunguzi Taa wakasema cha kwanza kabisa Taa inasafiri kwa (Speed) kubwa kabisa ambayo hakuna kitu chengine chochote chenye kusafiri kuishinda taa, (Speed) yake ni (186,000).
(2)Taa ni kitu pekee kinacho safiri bila ya kutumia au kutegemea (Chombo)chengine kwa ajili ya kupatiwa nguvu, kwa Wale walosomea (Photon) wanajua nimekusudia nini, Kwa sababu kila kitu katika Ulimwengu huu kinategemea (Energy) isipokua Taa, Taa ni (Self-Energy)haitegemei msaada wowote, Wewe Unaishi lakini unategemea msaada kutokea kwengine ili uweze kuishi lakini taa haina mahitaji hayo, ndio ikasemwa katika hiyo aya "yanakaribia Mafuta yake kungara" ingawa moto haujayagusa.
Kumbuka Wakati tunaendelea na darsa hii, hiyo aya ni mfano ulopigwa kuzungumzia hiyo (Nuru)Taa, lakini kadhia ya Taa inaenda (Deep) haikuishia hapo.
Lengine la muujiza kitu chengine chochote chenye kwenda (speed)hiyo ya Taa kinageuka kuwa Taa. Kwa hiyo hapo utaona ndio kwa mfano huo likaingia neno "Mwenye Enzi Mungu ni Nuru ya Mbingu na Ardhi" Ikiwa hatuijui, hatujapata kuiona, na wala hakuna atoiona sio kwamba tufahamu hiyo Nuru ni Mwenye enzi Mungu, bali ni mfano ulopigiwa huu Ulimwengu, Umeumbwa Ulimwengu huu kutokana na mambo hayo ya Muujiza niloyataja katika Darsa hii ikiwemo hiyo Nuru.Kwa maana hiyo kila kitu ni (Energy) Na (Energy)ndio hiyo(Light) Na wala sio (Matter). Kwa hiyo tunaweza kusema (Matter) ni kitu kilichoambatanishwa au ufupisho wa (Light condense), ndio maana kikifikia (Speed)ya Taa kinarejea kwenye (Original)yake.
Na hiyo ndio maana ya Nuru juu ya Nuru, kila kitu ni (Light),Halafu muujiza mwengine kuwa (Light) haina haja ya kutegemea kuishi, Kama kila kitu kinavotegemea Maji kuishi, kama alivosema Mwenye Enzi Mungu "Tukajaalia kila chenye kuishi maji ndio kuwa chanzo chake"(sura ya Al-Anbiyaa aya ya 30)
وَلَمۡ يَرَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَنَّ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضَ ڪَانَتَا رَتۡقً۬ا فَفَتَقۡنَـٰهُمَاۖ وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَىۡءٍ حَىٍّۖ أَفَلَا يُؤۡمِنُونَ
"Jee Hawakuona wale waliokufuru ya kwamba mbingu na ardhi vilikuwa vimeambatana, kisha tukaviambua(Big bang). Na tukafanya kwa maji kila kitu kilicho hai, basi jee hawaamini".
Kila chenye Uhai kimefanywa na Maji ila Taa, Kwa hiyo utaona Maji yanaitegemea Taa, lakini Taa haitegemei maji, Nayo hiyo Taa inakwenda (Beyond)Uhai. Kwa hiyo hapo utaelewa Taa inaishi bila ya Uhai(Self Existence). Kila kitu kinaweza kuyayuka isipokua Taa haiwezi kuguswa na chochote kile, Isipokua Taa ikizimika basi kila kitu kitakufa katika Ulimwengu huu ikiwemo hayo maji.
Endelea part 3
Sasa tuingie katika uchambuzi wa Nuru yenyewe ilivyo. katika utendaji wake kazi Mollah wetu akataja "Mfano wa Nuru yake ni kama shubaka" itabidi twende taratibu upate kunifahamu, ambayo imewekwa hiyo taa, taa hiyo imo kwenye tungi,(Kama chemni au hizi zenu za kisasa).
(1)Wanasayansi Wa Ulimwengu huu wanatwambia nini kuhusu Taa, Walipoifanyia Uchunguzi Taa wakasema cha kwanza kabisa Taa inasafiri kwa (Speed) kubwa kabisa ambayo hakuna kitu chengine chochote chenye kusafiri kuishinda taa, (Speed) yake ni (186,000).
(2)Taa ni kitu pekee kinacho safiri bila ya kutumia au kutegemea (Chombo)chengine kwa ajili ya kupatiwa nguvu, kwa Wale walosomea (Photon) wanajua nimekusudia nini, Kwa sababu kila kitu katika Ulimwengu huu kinategemea (Energy) isipokua Taa, Taa ni (Self-Energy)haitegemei msaada wowote, Wewe Unaishi lakini unategemea msaada kutokea kwengine ili uweze kuishi lakini taa haina mahitaji hayo, ndio ikasemwa katika hiyo aya "yanakaribia Mafuta yake kungara" ingawa moto haujayagusa.
Kumbuka Wakati tunaendelea na darsa hii, hiyo aya ni mfano ulopigwa kuzungumzia hiyo (Nuru)Taa, lakini kadhia ya Taa inaenda (Deep) haikuishia hapo.
Lengine la muujiza kitu chengine chochote chenye kwenda (speed)hiyo ya Taa kinageuka kuwa Taa. Kwa hiyo hapo utaona ndio kwa mfano huo likaingia neno "Mwenye Enzi Mungu ni Nuru ya Mbingu na Ardhi" Ikiwa hatuijui, hatujapata kuiona, na wala hakuna atoiona sio kwamba tufahamu hiyo Nuru ni Mwenye enzi Mungu, bali ni mfano ulopigiwa huu Ulimwengu, Umeumbwa Ulimwengu huu kutokana na mambo hayo ya Muujiza niloyataja katika Darsa hii ikiwemo hiyo Nuru.Kwa maana hiyo kila kitu ni (Energy) Na (Energy)ndio hiyo(Light) Na wala sio (Matter). Kwa hiyo tunaweza kusema (Matter) ni kitu kilichoambatanishwa au ufupisho wa (Light condense), ndio maana kikifikia (Speed)ya Taa kinarejea kwenye (Original)yake.
Na hiyo ndio maana ya Nuru juu ya Nuru, kila kitu ni (Light),Halafu muujiza mwengine kuwa (Light) haina haja ya kutegemea kuishi, Kama kila kitu kinavotegemea Maji kuishi, kama alivosema Mwenye Enzi Mungu "Tukajaalia kila chenye kuishi maji ndio kuwa chanzo chake"(sura ya Al-Anbiyaa aya ya 30)
وَلَمۡ يَرَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَنَّ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضَ ڪَانَتَا رَتۡقً۬ا فَفَتَقۡنَـٰهُمَاۖ وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَىۡءٍ حَىٍّۖ أَفَلَا يُؤۡمِنُونَ
"Jee Hawakuona wale waliokufuru ya kwamba mbingu na ardhi vilikuwa vimeambatana, kisha tukaviambua(Big bang). Na tukafanya kwa maji kila kitu kilicho hai, basi jee hawaamini".
Kila chenye Uhai kimefanywa na Maji ila Taa, Kwa hiyo utaona Maji yanaitegemea Taa, lakini Taa haitegemei maji, Nayo hiyo Taa inakwenda (Beyond)Uhai. Kwa hiyo hapo utaelewa Taa inaishi bila ya Uhai(Self Existence). Kila kitu kinaweza kuyayuka isipokua Taa haiwezi kuguswa na chochote kile, Isipokua Taa ikizimika basi kila kitu kitakufa katika Ulimwengu huu ikiwemo hayo maji.
Endelea part 3
MIUJIZA YA TAA PART 3
Asalaam Aleiykum
Aya ikaendelea na maneno haya:
"Nuru juu ya nuru Mwenye enzi Mungu humuongoza katika Nuru yake amtakaye, Na Mwenye enzi Mungu hupiga mifano kwa watu, Na Mwenye enzi Mungu ni mjuzi wa kila kitu".
Aliposema anapiga mifano kwa watu ili kutueleza sisi Wanaadamu uwezo wa elimu yake na miujiza iliyopo katika hiyo Taa aliyoumba,
(Let There Be Light)
Inaendelea Miujiza hii kutufata kwanza imeanzia Kwenye Mbingu na Ardhi na sasa imetufata katika Nafsi, Anasema Mollah Humuongoza Katika Nuru yake amtakaye, Ipi nuru ilokusudiwa hapo?, Ama zile za kuifata Nyota tunazijua, Napenda kukumbusha kuwa sisi hatuoni Nuru(Light)ila tunaona vinavomurikwa na Nuru, Humuongoza katika Nuru yake amtakaye, Nuru katika nafsi inagawika katika aina mbili ile aina ya kwanza ni (Inner light) wacha niitolee mfano, kwa sababu hujapata kuiona hiyo (Inner Light)lakini unaijua, vipi utaijua hii (light). Jichukue Mwenyewe uende sehemu ya kiza kikubwa uwe huoni chochote, Katika kiza hicho kuna kitu kimoja utakua na hakika nacho kipo, Na hakuna kitu chengine isipokua wewe Mwenyewe, Kwa mfano huo ni lazima iwepo (Light) Ya kukufahamisha kuwa wewe upo, kumbuka kwenye kiza hakionekani kitu chochote, sasa vipi wewe unajiona kama upo?, Lazima una (Inner Light) ndio ukaweza kujiona, Wewe Mwenyewe (Light)tupu kuanzia kuumbwa kwako, Ikiwa Ulimwengu Umeumbwa kwa (Light), Na Ardhi hii ndio umeumbwa nayo wewe(What is You)Jiulize Mwenyewe, Ukifanya Uchunguzi ukenda (Deep)ndani ya Maumbile yako utakutana nayo hiyo Taa pasina shaka, Jitizame juu juu tu utaona Jambo la Mwanzo unaanza na (Spina cord, nerve,heart)vyote hivyo ni (Form of Light), Akili yako inafanya kazi kutumia hiyo (Light), hiyo ndio (Inner light) ya Nafsi yako, lakini bado (light) hiyo haina (Movement)yoyote imekaa ndani ya Mwili wako mpaka ipate (Guidance) Hapo ndio yanaingia yale maneno ya "Humuongoza amtakaye kwenye (Nuru)Taa yake.(Baqarah-257)
ٱللَّهُ وَلِىُّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يُخۡرِجُهُم مِّنَ ٱلظُّلُمَـٰتِ إِلَى ٱلنُّورِۖ وَٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَوۡلِيَآؤُهُمُ ٱلطَّـٰغُوتُ يُخۡرِجُونَهُم مِّنَ ٱلنُّورِ إِلَى ٱلظُّلُمَـٰتِۗ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ أَصۡحَـٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيہَا خَـٰلِدُونَ
"Mwenye Enzi Mungu ni Mlinzi wa wale Walioamini", Huwatoa katika giza na kuwaingiza katika Mwangaza, Lakini waliokufuru, walinzi wao ni Mashetani, huwatoa katika Mwangaza na kuwaingiza katika giza, hao ndio watu wa Motoni humo watakaa motoni".
Mwangaza ni (Outer light) ni (Nature) Ya Ulimwengu huu hakuna makosa kila kitu kiko kwenye (Parfection)Yake, sasa kwa kuwa wewe Mwanaadamu unafahamishwa hizo elimu zote ili upate kuijua (Light) Na kama wewe Muumin unaoneshwa fanya hivi, vile usifanye, hii itakudhuru, ile ina madhara, unamurikiwa mambo yote kwa ukamilifu, ukishayaona ukatulia katika Mwangaza wa (Consciouness)yako hapo ndio unapata (Affect)ya hiyo Nuru, Na hiyo ndio Ibada, huo ndio muongozo , yaani lazima uzame katika hiyo Taa, Lazima zikutane taa hizi mbili ya ndani na ya nje, ukiingia katika (Full Light) huo ndio Ucha Mungu, hapo ndio unasafishika na kila giza katika maisha yako.
"Lakini Mashetani kazi yao wao kukutoa kwenye hii Taa na kukupeleka kwenye giza, Na hilo giza kwa kuwa huoni basi utatumbukia motoni milele.
Na Dalili za giza unaziona hapa hapa Ulimwenguni, huna furaha, maisha tafran, mambo hayendi,kutwa unawaza magonjwa, huyaoni mazuri ya dunia hii kabisa, hata ufanyiwe nini huna raha kabisa, na hiyo ni dalili yakuwa taa yako ina sinzia, karibu itazimika, Iwashe kwa Ibada upate kuona mazuri ya Ulimwengu huu na Akiba yako ya Akhera. Zama Kwenye Miujiza Ya Taa, nayo itakuonesha mambo mengi yalofichika katika giza la Ulimwengu huu, Na ukipata hilo ndio umepata hicho kitu kiitwacho (Bliss)Na wewe sasa umegeuka kuwa Taa.
Aya ikaendelea na maneno haya:
"Nuru juu ya nuru Mwenye enzi Mungu humuongoza katika Nuru yake amtakaye, Na Mwenye enzi Mungu hupiga mifano kwa watu, Na Mwenye enzi Mungu ni mjuzi wa kila kitu".
Aliposema anapiga mifano kwa watu ili kutueleza sisi Wanaadamu uwezo wa elimu yake na miujiza iliyopo katika hiyo Taa aliyoumba,
(Let There Be Light)
Inaendelea Miujiza hii kutufata kwanza imeanzia Kwenye Mbingu na Ardhi na sasa imetufata katika Nafsi, Anasema Mollah Humuongoza Katika Nuru yake amtakaye, Ipi nuru ilokusudiwa hapo?, Ama zile za kuifata Nyota tunazijua, Napenda kukumbusha kuwa sisi hatuoni Nuru(Light)ila tunaona vinavomurikwa na Nuru, Humuongoza katika Nuru yake amtakaye, Nuru katika nafsi inagawika katika aina mbili ile aina ya kwanza ni (Inner light) wacha niitolee mfano, kwa sababu hujapata kuiona hiyo (Inner Light)lakini unaijua, vipi utaijua hii (light). Jichukue Mwenyewe uende sehemu ya kiza kikubwa uwe huoni chochote, Katika kiza hicho kuna kitu kimoja utakua na hakika nacho kipo, Na hakuna kitu chengine isipokua wewe Mwenyewe, Kwa mfano huo ni lazima iwepo (Light) Ya kukufahamisha kuwa wewe upo, kumbuka kwenye kiza hakionekani kitu chochote, sasa vipi wewe unajiona kama upo?, Lazima una (Inner Light) ndio ukaweza kujiona, Wewe Mwenyewe (Light)tupu kuanzia kuumbwa kwako, Ikiwa Ulimwengu Umeumbwa kwa (Light), Na Ardhi hii ndio umeumbwa nayo wewe(What is You)Jiulize Mwenyewe, Ukifanya Uchunguzi ukenda (Deep)ndani ya Maumbile yako utakutana nayo hiyo Taa pasina shaka, Jitizame juu juu tu utaona Jambo la Mwanzo unaanza na (Spina cord, nerve,heart)vyote hivyo ni (Form of Light), Akili yako inafanya kazi kutumia hiyo (Light), hiyo ndio (Inner light) ya Nafsi yako, lakini bado (light) hiyo haina (Movement)yoyote imekaa ndani ya Mwili wako mpaka ipate (Guidance) Hapo ndio yanaingia yale maneno ya "Humuongoza amtakaye kwenye (Nuru)Taa yake.(Baqarah-257)
ٱللَّهُ وَلِىُّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يُخۡرِجُهُم مِّنَ ٱلظُّلُمَـٰتِ إِلَى ٱلنُّورِۖ وَٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَوۡلِيَآؤُهُمُ ٱلطَّـٰغُوتُ يُخۡرِجُونَهُم مِّنَ ٱلنُّورِ إِلَى ٱلظُّلُمَـٰتِۗ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ أَصۡحَـٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيہَا خَـٰلِدُونَ
"Mwenye Enzi Mungu ni Mlinzi wa wale Walioamini", Huwatoa katika giza na kuwaingiza katika Mwangaza, Lakini waliokufuru, walinzi wao ni Mashetani, huwatoa katika Mwangaza na kuwaingiza katika giza, hao ndio watu wa Motoni humo watakaa motoni".
Mwangaza ni (Outer light) ni (Nature) Ya Ulimwengu huu hakuna makosa kila kitu kiko kwenye (Parfection)Yake, sasa kwa kuwa wewe Mwanaadamu unafahamishwa hizo elimu zote ili upate kuijua (Light) Na kama wewe Muumin unaoneshwa fanya hivi, vile usifanye, hii itakudhuru, ile ina madhara, unamurikiwa mambo yote kwa ukamilifu, ukishayaona ukatulia katika Mwangaza wa (Consciouness)yako hapo ndio unapata (Affect)ya hiyo Nuru, Na hiyo ndio Ibada, huo ndio muongozo , yaani lazima uzame katika hiyo Taa, Lazima zikutane taa hizi mbili ya ndani na ya nje, ukiingia katika (Full Light) huo ndio Ucha Mungu, hapo ndio unasafishika na kila giza katika maisha yako.
"Lakini Mashetani kazi yao wao kukutoa kwenye hii Taa na kukupeleka kwenye giza, Na hilo giza kwa kuwa huoni basi utatumbukia motoni milele.
Na Dalili za giza unaziona hapa hapa Ulimwenguni, huna furaha, maisha tafran, mambo hayendi,kutwa unawaza magonjwa, huyaoni mazuri ya dunia hii kabisa, hata ufanyiwe nini huna raha kabisa, na hiyo ni dalili yakuwa taa yako ina sinzia, karibu itazimika, Iwashe kwa Ibada upate kuona mazuri ya Ulimwengu huu na Akiba yako ya Akhera. Zama Kwenye Miujiza Ya Taa, nayo itakuonesha mambo mengi yalofichika katika giza la Ulimwengu huu, Na ukipata hilo ndio umepata hicho kitu kiitwacho (Bliss)Na wewe sasa umegeuka kuwa Taa.
Wednesday, November 1, 2017
NJIA YA KUMKUMBUKA ALLAH PART 1
Asalaam Aleiykum
Mnaniuliza vipi kumkumbuka Allah mbona sisi inatushinda inakuaje hali hiyo, Mbona hatuwezi wakati tunajitahidi?, Anapouliza Mja swali kama hili ajijue kashafika mlangoni, huyu anataka afunguliwe, sasa anagonga katokea mbali, kapanda milima na kupita kwenye majangwa mpaka kuwasili kutaka kujua kitu Adhimu kama hicho.
Siku zote wanasikia aya ya (191)sura ya (Al-Imran)inosema:
"ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَـٰمً۬ا وَقُعُودً۬ا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَڪَّرُونَ فِى خَلۡقِ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَـٰذَا بَـٰطِلاً۬ سُبۡحَـٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ"
"Ambao humkumbuka Mwenye Enzi Mungu Wakiwa Wima na Wakikaa na Wakilala, Na Hufikiri Umbo la Mbingu na Ardhi, (Wakasema)Mollah wetu huku viumba hivi bure, Utukufu ni wako, basi tuepushe na adhabu ya Moto".
Kwanza kabisa nataka kufundisha vipi utazama kwenye neno, ukitaka kuzama kwenye neno lazima ujiulize kwanini likawepo hapo, nikisema kuwepo hapo sina maana nyengine ila kutizama mashiko yake, mashiko yanayo onekana hapo ni kutajwa vitu viwili ambavyo wewe huvioni, ndio maana nikasema zama kwenye maneno, ndio maana Masheikh wazamani walikua wakichambua aya moja kwa siku nzima.
Sasa midamu umegonga Mlango na mimi ntakufungulia uchungulie ndani kidogo uone raha ya kufahamu, katika hiyo aya kumetajwa maneno mawili ambayo ndio tutozama nayo katika darsa hii yatuoneshe hiyo njia ya kumkumbuka Allah, Sasa itizame uzuri hiyo aya inasema neno la kwanza (kumkumbuka)halafu neno la pili(Kufikiri).
Naam Kumkumbuka ni lazima, Kukumbuka ndio (Nature)yako, Unalala unaamka, unasimama, unakaa yote hayo yanatokana na Amri ya Mwenye Enzi Mungu katika Rehma zake, huna haja ya kukumbuka mie niko hai, halafu tena unapewa nafasi ya kuchagua, Ukichagua Kumkumbuka Mollah alokufanyia hayo, hiyo ndio Pepo yako, Na ukichagua Mengine hayo ndio yanokupeleka kwenye moto wako, Sote tuko kwenye Ufalme wa Mwenye Enzi Mungu, ila katupa Uhuru, Uhuru wenyewe ndio huo uwezo wa (Kufikiri)Ambao linaingia neno la Pili.
Fikira ni tendo linohusiana na Akili au (Mind)yako, Akili ina desturi ya kuzunguka au niseme ina athari za (Rebellious), ndio maana utaona ukitaka kusali tu, inaanza kukuletea visa, unapanga biashara, unakumbuka mambo yote ulosahau, kwa sababu ya Athari zilezile za maasi, kwa hiyo ikiona unataka kutenda mema inakurejesha kule kule kwenye mabaya, ukitoka kusali inakukumbusha mpira, wanawake au wanaume, dhuluma, siasa fujo tupu hilo ndio linakufanya huwezi Kumkumbuka Mollah wako ukiwa unasali, umesimama au umekaa hata wakati umelala. Sasa hao walotajwa kwenye hiyo aya wamefanya nini hata wakapata mawili hayo?.
Endelea part 2
Mnaniuliza vipi kumkumbuka Allah mbona sisi inatushinda inakuaje hali hiyo, Mbona hatuwezi wakati tunajitahidi?, Anapouliza Mja swali kama hili ajijue kashafika mlangoni, huyu anataka afunguliwe, sasa anagonga katokea mbali, kapanda milima na kupita kwenye majangwa mpaka kuwasili kutaka kujua kitu Adhimu kama hicho.
Siku zote wanasikia aya ya (191)sura ya (Al-Imran)inosema:
"ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَـٰمً۬ا وَقُعُودً۬ا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَڪَّرُونَ فِى خَلۡقِ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَـٰذَا بَـٰطِلاً۬ سُبۡحَـٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ"
"Ambao humkumbuka Mwenye Enzi Mungu Wakiwa Wima na Wakikaa na Wakilala, Na Hufikiri Umbo la Mbingu na Ardhi, (Wakasema)Mollah wetu huku viumba hivi bure, Utukufu ni wako, basi tuepushe na adhabu ya Moto".
Kwanza kabisa nataka kufundisha vipi utazama kwenye neno, ukitaka kuzama kwenye neno lazima ujiulize kwanini likawepo hapo, nikisema kuwepo hapo sina maana nyengine ila kutizama mashiko yake, mashiko yanayo onekana hapo ni kutajwa vitu viwili ambavyo wewe huvioni, ndio maana nikasema zama kwenye maneno, ndio maana Masheikh wazamani walikua wakichambua aya moja kwa siku nzima.
Sasa midamu umegonga Mlango na mimi ntakufungulia uchungulie ndani kidogo uone raha ya kufahamu, katika hiyo aya kumetajwa maneno mawili ambayo ndio tutozama nayo katika darsa hii yatuoneshe hiyo njia ya kumkumbuka Allah, Sasa itizame uzuri hiyo aya inasema neno la kwanza (kumkumbuka)halafu neno la pili(Kufikiri).
Naam Kumkumbuka ni lazima, Kukumbuka ndio (Nature)yako, Unalala unaamka, unasimama, unakaa yote hayo yanatokana na Amri ya Mwenye Enzi Mungu katika Rehma zake, huna haja ya kukumbuka mie niko hai, halafu tena unapewa nafasi ya kuchagua, Ukichagua Kumkumbuka Mollah alokufanyia hayo, hiyo ndio Pepo yako, Na ukichagua Mengine hayo ndio yanokupeleka kwenye moto wako, Sote tuko kwenye Ufalme wa Mwenye Enzi Mungu, ila katupa Uhuru, Uhuru wenyewe ndio huo uwezo wa (Kufikiri)Ambao linaingia neno la Pili.
Fikira ni tendo linohusiana na Akili au (Mind)yako, Akili ina desturi ya kuzunguka au niseme ina athari za (Rebellious), ndio maana utaona ukitaka kusali tu, inaanza kukuletea visa, unapanga biashara, unakumbuka mambo yote ulosahau, kwa sababu ya Athari zilezile za maasi, kwa hiyo ikiona unataka kutenda mema inakurejesha kule kule kwenye mabaya, ukitoka kusali inakukumbusha mpira, wanawake au wanaume, dhuluma, siasa fujo tupu hilo ndio linakufanya huwezi Kumkumbuka Mollah wako ukiwa unasali, umesimama au umekaa hata wakati umelala. Sasa hao walotajwa kwenye hiyo aya wamefanya nini hata wakapata mawili hayo?.
Endelea part 2
NJIA YA KUMKUMBUKA ALLAH PART 2
Asalaam Aleiykum
Katika Dunia hii kila kitu kimeumbwa na mwenzake kuifahamu njia ya kumkumbuka Allah kwanza lazima uijue sheria ya (Foward)na (Reverse Affect)katika Akili yako. Tizama wewe inakuaje ukikatazwa kitu unavokua, au umwambie mtu jambo asiseme uone anavohangaika kulitangaza, na hivyo hivyo Ukijifanya, na sema Ukijifanya unataka kuwa Mcha Mungu jiangalie vipi ukatili, au ubaya unavyo kuzunguka katika Roho yako, Watizame hao wanojifanya watu wa dini wanavokua, nini hali zao, sisemi kitu angalia mwenyewe halafu utapata jawabu, usitizame makanzu yao angalia huyu hana (Reverse affect)kama hana basi huyo Mcha Mungu.
Yote hayo yanatokana na hiyo sheria niloitaja hapo juu, Kwa hiyo ukitaka Kumkumbuka Allah lazima uende (Beyond) ya Sheria hiyo, vipi utafanya?. Jambo la kwanza unatakiwa kuishughulisha Akili yako wakati wote iwe katika Kumfikiri Mollah wako katika mambo ya Uhai na Umauti, Na katika Ulimwengu huu sidhani kama utavimaliza vitu vyote katika kuitizama Neema na Rehma ya Mwenye Enzi Mungu alojaza katika Umbaji wake, iwe kila ukionacho basi kinakukumbusha Mollah wako, ukifanikiwa kufanya hivyo ndio utajiunga na walotajwa katika hiyo aya niloitaja hapo mwanzo, utakua na wewe unamkumbuka na kumfikiri kwa wakati mmoja, sio ukiona mbuzi unamkumbuka Mollah wako na ukiona Mbwa unakamata jiwe, hapo itakua kumbukumbuka ishakupotea, na utakua ni mwenye kupotea njia.
Ukifanikiwa kudumu kwa kila unachokiona kina kukumbusha uwezo wa Mwenye enzi Mungu hapo utakua umeiweza Akili, Na ukiiweza Akili unabaki kwenye kukumbuka na wewe unajiunga katika Waja walotajwa katika sura ya Furqan aya ya (63-64)
"وَعِبَادُ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلَّذِينَ يَمۡشُونَ عَلَى ٱلۡأَرۡضِ هَوۡنً۬ا وَإِذَا خَاطَبَهُمُ ٱلۡجَـٰهِلُونَ قَالُواْ سَلَـٰمً۬ا"
Na Waja wa Mwenye Enzi Mungu ni wale wanaokwenda Ulimwenguni kwa Unyenyekevu, Na Wajinga wakisema nao huwajibu Salama.
"وَٱلَّذِينَ يَبِيتُونَ لِرَبِّهِمۡ سُجَّدً۬ا وَقِيَـٰمً۬ا"
Na Wale wanaopitisha baadhi ya (Nyakati)saa za usiku kwa ajili ya Mollah wao kwa kusujudu na Kusimama.
Kwanini wakaitwa Waja wa Mwenye enzi Mungu kwa sababu saa zote wako na Mollah wao, hakiingi chengine kati yao, washafunguliwa siri za mambo, wanageuka kuwa wanyenyekevu, wanajua sisi hatuna cha kumlipa Mollah wetu, tumeletwa katika dunia hii kuhakikisha tunamkumbuka Mollah wetu wakati wote, Na ndio wakikutana na wasojua(Wajinga)wanawapa ishara ya huku kwetu Salama tupu, Na nyinyi chagueni kumkumbuka Allah mtaipata salama hiyo(Hawagombani nao)hawana mabishano neno lao ni usalama, na hiyo ndio sifa ya (Muumin)(Peace)Upande wa Mungu hakuna dhuluma, hakuna kutaka pesa, hakuna mabishano wala chuki, ukiona unayo mambo hayo basi jijue bado uko upande wa (Shetani) na endelea kumkumbuka shetani wako.
Na Mollah wako akijaa katika Akili yako huwezi kulala mpaka asubuhi bila ya kusujudu na kusimama kwa ajili yake, yeye ndie mwenye kukupa usingizi, Na mchana kutwa ulikua umeshughulika na maisha, kwa hiyo sasa usiku umeingia ni wakati mzuri wa kusimama kusema na Mollah wako na Ku(Surrender)kuanguka kwa ajili ya Sujjud.
Endelea Part 3
Katika Dunia hii kila kitu kimeumbwa na mwenzake kuifahamu njia ya kumkumbuka Allah kwanza lazima uijue sheria ya (Foward)na (Reverse Affect)katika Akili yako. Tizama wewe inakuaje ukikatazwa kitu unavokua, au umwambie mtu jambo asiseme uone anavohangaika kulitangaza, na hivyo hivyo Ukijifanya, na sema Ukijifanya unataka kuwa Mcha Mungu jiangalie vipi ukatili, au ubaya unavyo kuzunguka katika Roho yako, Watizame hao wanojifanya watu wa dini wanavokua, nini hali zao, sisemi kitu angalia mwenyewe halafu utapata jawabu, usitizame makanzu yao angalia huyu hana (Reverse affect)kama hana basi huyo Mcha Mungu.
Yote hayo yanatokana na hiyo sheria niloitaja hapo juu, Kwa hiyo ukitaka Kumkumbuka Allah lazima uende (Beyond) ya Sheria hiyo, vipi utafanya?. Jambo la kwanza unatakiwa kuishughulisha Akili yako wakati wote iwe katika Kumfikiri Mollah wako katika mambo ya Uhai na Umauti, Na katika Ulimwengu huu sidhani kama utavimaliza vitu vyote katika kuitizama Neema na Rehma ya Mwenye Enzi Mungu alojaza katika Umbaji wake, iwe kila ukionacho basi kinakukumbusha Mollah wako, ukifanikiwa kufanya hivyo ndio utajiunga na walotajwa katika hiyo aya niloitaja hapo mwanzo, utakua na wewe unamkumbuka na kumfikiri kwa wakati mmoja, sio ukiona mbuzi unamkumbuka Mollah wako na ukiona Mbwa unakamata jiwe, hapo itakua kumbukumbuka ishakupotea, na utakua ni mwenye kupotea njia.
Ukifanikiwa kudumu kwa kila unachokiona kina kukumbusha uwezo wa Mwenye enzi Mungu hapo utakua umeiweza Akili, Na ukiiweza Akili unabaki kwenye kukumbuka na wewe unajiunga katika Waja walotajwa katika sura ya Furqan aya ya (63-64)
"وَعِبَادُ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلَّذِينَ يَمۡشُونَ عَلَى ٱلۡأَرۡضِ هَوۡنً۬ا وَإِذَا خَاطَبَهُمُ ٱلۡجَـٰهِلُونَ قَالُواْ سَلَـٰمً۬ا"
Na Waja wa Mwenye Enzi Mungu ni wale wanaokwenda Ulimwenguni kwa Unyenyekevu, Na Wajinga wakisema nao huwajibu Salama.
"وَٱلَّذِينَ يَبِيتُونَ لِرَبِّهِمۡ سُجَّدً۬ا وَقِيَـٰمً۬ا"
Na Wale wanaopitisha baadhi ya (Nyakati)saa za usiku kwa ajili ya Mollah wao kwa kusujudu na Kusimama.
Kwanini wakaitwa Waja wa Mwenye enzi Mungu kwa sababu saa zote wako na Mollah wao, hakiingi chengine kati yao, washafunguliwa siri za mambo, wanageuka kuwa wanyenyekevu, wanajua sisi hatuna cha kumlipa Mollah wetu, tumeletwa katika dunia hii kuhakikisha tunamkumbuka Mollah wetu wakati wote, Na ndio wakikutana na wasojua(Wajinga)wanawapa ishara ya huku kwetu Salama tupu, Na nyinyi chagueni kumkumbuka Allah mtaipata salama hiyo(Hawagombani nao)hawana mabishano neno lao ni usalama, na hiyo ndio sifa ya (Muumin)(Peace)Upande wa Mungu hakuna dhuluma, hakuna kutaka pesa, hakuna mabishano wala chuki, ukiona unayo mambo hayo basi jijue bado uko upande wa (Shetani) na endelea kumkumbuka shetani wako.
Na Mollah wako akijaa katika Akili yako huwezi kulala mpaka asubuhi bila ya kusujudu na kusimama kwa ajili yake, yeye ndie mwenye kukupa usingizi, Na mchana kutwa ulikua umeshughulika na maisha, kwa hiyo sasa usiku umeingia ni wakati mzuri wa kusimama kusema na Mollah wako na Ku(Surrender)kuanguka kwa ajili ya Sujjud.
Endelea Part 3
NJIA YA KUMKUMBUKA ALLAH PART 3
Asalaam Aleiykum
Amesema Mwenye Enzi Mungu katika sura ya (Adh-Dhariyat-56)"وَمَا خَلَقۡتُ ٱلۡجِنَّ وَٱلۡإِنسَ إِلَّا لِيَعۡبُدُونِ"
"Sikuwaumba Majini na Watu ila wapate kuniabudu"
Sikuwaumba kwa ajili yoyote, ila nimewapa (Choice)wakitaka waniabudu watakua wamechagua Pepo wenyewe, Na wasipotaka na kukataa watakua wamechagua njia yao itakayo wapeleka kwenye mateso, kwani kwenda kinyume cha Maumbile(Nature)ya Ulimwengu huu utakua umechagua kinyume na atakavyo alokuumba.
Sasa kuipata hiyo Ibada yenyewe lazima uviunganishe vitu viwili nilivyovitaja vya Fikra na Kukumbuka yaani (Roho Na Akili) Vikiungana hivyo ndio unapata huo Unyenyekevu, Akili haiyumbi tena, Vipi Akili itayumba wakati daima uko mbele ya Mollah wako, Na Mbele ya Mollah lazima upate na Unyenyekevu, Na huku Duniani wakikuona wanahisi kuna kitu (kimetokezea)ndio wakikuuliza kitu mbona imekua hivi, au wakibishana na wewe huna la kusema ila unawaambia Salaam(Peace).
Kwa habari hii nilokupeni na ikiwa umeipokea sawa sawa na sasa na wewe unataka kuanza kuipata hali kama hiyo, Basi chukua moja katika majina 99 ya Mwenye Enzi Mungu halafu litaje (Non Stop) kwa miezi mitatu ikisha (Stop) baada ya hapo ndio utafunguliwa hiyo (Nameless) ya kukumbuka daima, Nje utakua Binaadamu wa kawaida lakini ndani kiumbe mwengine kabisa, kila kitu kinafunguliwa kwako, na ukiipata hali kama hiyo utakua ushaipata hiyo njia, Na njia hiyo ndio hiyo inotajwa (Mustaqim)ambayo inakupeleka kwa Mollah wako ukiwa safi umesafishika na dhanmbi zote ulizozifanya huko nyuma. Na Mollah ndie ajuae zaidi.
Amesema Mwenye Enzi Mungu katika sura ya (Adh-Dhariyat-56)"وَمَا خَلَقۡتُ ٱلۡجِنَّ وَٱلۡإِنسَ إِلَّا لِيَعۡبُدُونِ"
"Sikuwaumba Majini na Watu ila wapate kuniabudu"
Sikuwaumba kwa ajili yoyote, ila nimewapa (Choice)wakitaka waniabudu watakua wamechagua Pepo wenyewe, Na wasipotaka na kukataa watakua wamechagua njia yao itakayo wapeleka kwenye mateso, kwani kwenda kinyume cha Maumbile(Nature)ya Ulimwengu huu utakua umechagua kinyume na atakavyo alokuumba.
Sasa kuipata hiyo Ibada yenyewe lazima uviunganishe vitu viwili nilivyovitaja vya Fikra na Kukumbuka yaani (Roho Na Akili) Vikiungana hivyo ndio unapata huo Unyenyekevu, Akili haiyumbi tena, Vipi Akili itayumba wakati daima uko mbele ya Mollah wako, Na Mbele ya Mollah lazima upate na Unyenyekevu, Na huku Duniani wakikuona wanahisi kuna kitu (kimetokezea)ndio wakikuuliza kitu mbona imekua hivi, au wakibishana na wewe huna la kusema ila unawaambia Salaam(Peace).
Kwa habari hii nilokupeni na ikiwa umeipokea sawa sawa na sasa na wewe unataka kuanza kuipata hali kama hiyo, Basi chukua moja katika majina 99 ya Mwenye Enzi Mungu halafu litaje (Non Stop) kwa miezi mitatu ikisha (Stop) baada ya hapo ndio utafunguliwa hiyo (Nameless) ya kukumbuka daima, Nje utakua Binaadamu wa kawaida lakini ndani kiumbe mwengine kabisa, kila kitu kinafunguliwa kwako, na ukiipata hali kama hiyo utakua ushaipata hiyo njia, Na njia hiyo ndio hiyo inotajwa (Mustaqim)ambayo inakupeleka kwa Mollah wako ukiwa safi umesafishika na dhanmbi zote ulizozifanya huko nyuma. Na Mollah ndie ajuae zaidi.
Sunday, October 15, 2017
MWISHO WA UHAI PART 1
Asalaam Aleiykum
Zimekujia taarifa kama hivi karibuni utanyanganywa zawadi yako ulopewa, Hakuna zawadi njema ulopewa kama hii ya Uhai, ila ina masharti kuwa ni lazima baada ya muda ichukuliwe, Na kabla ya kuchukuliwa zawadi hii unaletewa dalili ili upate kujiandaa kuishi bila ya zawadi hiyo.
Umeshawahi kukaa na kuzichunguza dalili hizo ili upate kujua nini cha kufanya. Basi ikiwa bado hujafanya, nakupa nafasi usafiri na mimi ili kuzishuhudia dalili hizo na kuweza kuzifanyia kazi kwa dhumuni la kupewa tena zawadi hiyo ya uhai kwa mara ya pili.
Uhai utakaopewa kwa mara ya pili una mambo mawili Ima Furaha na Raha isokatika, Au Shida na Tabu za milele za kuendelea. Bado unayo nafasi ya Kubadilika, kwanini nikasema kubadilika nisiseme kugeuka, kugeuka ndio kawaida yako kama kinyonga, Mfano na wewe Mwenyewe jitizame unavo geuka Ukiwa na Mkeo Umehamaki, mara akiingia Rafiki unacheka, Mara umekua Sheikh mara unaasi, Mara hichi haramu, mara kile halali, wakati wowote unageuka, lakini mfano mmoja tu wa kubadilika utakutosha nao ni Kama vile (Butterflies)anavobadilik kutoka kwenye (Caterpiller)na kuwa Kipepeo.
Dalili gani zitakufanya ugeuke kabla ya mwisho wa uhai wako?. Mwenye Enzi Mungu simwenye kumdhulumu Mja wake katoa nafasi mpaka dakika za karibu ya Mwisho nafasi hiyo ipo, Lakini kwa Mwenye kutaka kuitumia, ziko dalili hizi kwenye Quraan lakini kwa Mwenye kusoma kwa Njia ya (Fahamu) ikiwa umesoma (Siri ya Fahamu)utajua nimekusudia nini.
Kwenye Quraan yamesemwa maneno yaloficha Hekima ndani yake, wakati ule ulipokua kijana na jeuri zako, mbishi husikilizi mtu uliambiwa maneno haya yaliyomo kwenye sura ya Tariq aya ya (5-6-7)."فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَـٰنُ مِمَّ خُلِقَ"
"Hebu ajitizame mtu, ameumbwa kwa kitu gani" Binaadamu umeumbwa kwa mali ghafi ya maji ya uhai, maji haya ni (Very Powerful)ulipoambiwa yatizame ili ujue uwezo wa maji hayo ambayo ukiyatoa yanaweza kutengeneza kiumbe kama wewe.
"خُلِقَ مِن مَّآءٍ۬ دَافِقٍ۬ "
"Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa" Kutokana na Dalili hiyo kinochupa chochote kinatoka juu na kwenda kutua chini, na hiyo ndio (Sex)lau ungekua unaweza kuzuia yasichupe maji hayo basi Miujiza mikubwa ingetokea juu yako, ndio maana (Watawa na Makasisi wanajificha) ili kuzuia (Gravitation)hii isitokee, kwa sababu kama haitokei (Gravitation)lazima Sheria ya maumbile ya mrengo wa pili wa (Levitation)ichukue nafasi yake, na hapo ndio yanatokea hayo (Mabadiliko)Rehma, Miujiza ita utakavyo.
Lakini maji haya (Nature)yake lazima yachupe yakitokea.
"يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآٮِٕبِ"
"Yatokayo katikati ya mifupa ya mgongo na Kifua"
Wewe hujapata au hujui kuyasikiza inakuaje yakitokea huko hali yake au Raha zake zinakua vipi, kwa sababu ya kushughulika kwako na akili ziko kwengine unashituka sekunde za mwisho, maskini hasara yako, mpaka unaondoka kwenye Ulimwengu huu hujapata kujua inakuaje ladha ya maji haya yakianza kuondoka kifuani au mgongoni hali inakuaje.(Hapa siko kwenye darsa ya mambo hayo ila nagusia na kupita njia tu). Nafahamisha kuwa zipo raha zaidi ukiwa una weledi wa mambo.
Wacha kutoa macho endelea part 2.
Zimekujia taarifa kama hivi karibuni utanyanganywa zawadi yako ulopewa, Hakuna zawadi njema ulopewa kama hii ya Uhai, ila ina masharti kuwa ni lazima baada ya muda ichukuliwe, Na kabla ya kuchukuliwa zawadi hii unaletewa dalili ili upate kujiandaa kuishi bila ya zawadi hiyo.
Umeshawahi kukaa na kuzichunguza dalili hizo ili upate kujua nini cha kufanya. Basi ikiwa bado hujafanya, nakupa nafasi usafiri na mimi ili kuzishuhudia dalili hizo na kuweza kuzifanyia kazi kwa dhumuni la kupewa tena zawadi hiyo ya uhai kwa mara ya pili.
Uhai utakaopewa kwa mara ya pili una mambo mawili Ima Furaha na Raha isokatika, Au Shida na Tabu za milele za kuendelea. Bado unayo nafasi ya Kubadilika, kwanini nikasema kubadilika nisiseme kugeuka, kugeuka ndio kawaida yako kama kinyonga, Mfano na wewe Mwenyewe jitizame unavo geuka Ukiwa na Mkeo Umehamaki, mara akiingia Rafiki unacheka, Mara umekua Sheikh mara unaasi, Mara hichi haramu, mara kile halali, wakati wowote unageuka, lakini mfano mmoja tu wa kubadilika utakutosha nao ni Kama vile (Butterflies)anavobadilik kutoka kwenye (Caterpiller)na kuwa Kipepeo.
Dalili gani zitakufanya ugeuke kabla ya mwisho wa uhai wako?. Mwenye Enzi Mungu simwenye kumdhulumu Mja wake katoa nafasi mpaka dakika za karibu ya Mwisho nafasi hiyo ipo, Lakini kwa Mwenye kutaka kuitumia, ziko dalili hizi kwenye Quraan lakini kwa Mwenye kusoma kwa Njia ya (Fahamu) ikiwa umesoma (Siri ya Fahamu)utajua nimekusudia nini.
Kwenye Quraan yamesemwa maneno yaloficha Hekima ndani yake, wakati ule ulipokua kijana na jeuri zako, mbishi husikilizi mtu uliambiwa maneno haya yaliyomo kwenye sura ya Tariq aya ya (5-6-7)."فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَـٰنُ مِمَّ خُلِقَ"
"Hebu ajitizame mtu, ameumbwa kwa kitu gani" Binaadamu umeumbwa kwa mali ghafi ya maji ya uhai, maji haya ni (Very Powerful)ulipoambiwa yatizame ili ujue uwezo wa maji hayo ambayo ukiyatoa yanaweza kutengeneza kiumbe kama wewe.
"خُلِقَ مِن مَّآءٍ۬ دَافِقٍ۬ "
"Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa" Kutokana na Dalili hiyo kinochupa chochote kinatoka juu na kwenda kutua chini, na hiyo ndio (Sex)lau ungekua unaweza kuzuia yasichupe maji hayo basi Miujiza mikubwa ingetokea juu yako, ndio maana (Watawa na Makasisi wanajificha) ili kuzuia (Gravitation)hii isitokee, kwa sababu kama haitokei (Gravitation)lazima Sheria ya maumbile ya mrengo wa pili wa (Levitation)ichukue nafasi yake, na hapo ndio yanatokea hayo (Mabadiliko)Rehma, Miujiza ita utakavyo.
Lakini maji haya (Nature)yake lazima yachupe yakitokea.
"يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآٮِٕبِ"
"Yatokayo katikati ya mifupa ya mgongo na Kifua"
Wewe hujapata au hujui kuyasikiza inakuaje yakitokea huko hali yake au Raha zake zinakua vipi, kwa sababu ya kushughulika kwako na akili ziko kwengine unashituka sekunde za mwisho, maskini hasara yako, mpaka unaondoka kwenye Ulimwengu huu hujapata kujua inakuaje ladha ya maji haya yakianza kuondoka kifuani au mgongoni hali inakuaje.(Hapa siko kwenye darsa ya mambo hayo ila nagusia na kupita njia tu). Nafahamisha kuwa zipo raha zaidi ukiwa una weledi wa mambo.
Wacha kutoa macho endelea part 2.
MWISHO WA UHAI PART 2
Asalaam Aleiykum
Siri ya hayo maji tuliyoitaja kwenye part 1 inatokezea hata wakati wa kulala au wa kufa kwako, nyakati nyengine lazima maji hayo yamiminike au yashuke ndio upate usingizi. Hiyo ni sehemu ya kwanza ya dalili za uhai ambazo zinakufanya huwezi kujizuia, maji lazima yatoke, fujo tupu mtaani watu wanachunga watoto wakiume na kike, ile isitokee fujo mitaani, mwanamke kafungiwa na wanaume wanaranda kama simba anatafuta swala, watu wanakwiba, wanadhulumu ,wanagombana yote sababu ya maji haya yanochupa kwa kasi.
Hiyo ni dalili ya kwanza ya Uhai, ikisha kuna dalili ya pili ya mwisho wa uhai. Soma taratibu kwa uangalifu mkubwa ili upate kufahamu kusudio ya darsa hii ili upate kubadilika, kumbuka sio kugeuka. Aya gani inayo tukumbusha Mwisho wa Uhai?
Sura ya Yaasin aya ya (68)
"وَمَن نُّعَمِّرۡهُ نُنَڪِّسۡهُ فِى ٱلۡخَلۡقِۖ أَفَلَا يَعۡقِلُونَ"
"Na tunayempa Umri tunamrejesha nyuma katika umbo(Lake)(Anakuwa kama mtoto)basi jee, hawayatii Akilini(Mafunzo haya).
Hapo kuna siri nzito ya kujiandaa na mwisho wa Uhai, katika aya hiyo kumetajwa umbo na Akili, Umbo linaondoshewa nguvu lina rudi kama ulivokua mtoto, Baba akiweza kukupiga, ulipokua mkubwa una nyanyua vyuma huoni kaacha kukupiga, na sasa hivi wewe kizee, kijana wakati wowote anaweza kukunasa vibao, Umbo linarejeshwa kama mtoto, unaona mwenyewe magoti hayafanyi kazi uzuri, miguu huwezi kukimbia, moyo unakunyima pumzi, macho na masikio haviwezi kutenda kazi kama zamani, meno yashapungua, sasa ushaanza kukaa ndani kipindi kirefu, habari za kutamani zimeshatangulia na wakati, mambo huyawezi tena, sasa kama huzijui dalili hizi ndio unaanza kukimbilia madawa ya kila aina ujirejeshe ujanani, ndio mnaambiwa hamyatii Akilini?.Kuyatia Akilini maana yake rudi kwenye (Siri ya Fahamu).
Lakini ilipotajwa akili ni kwa Tafsiri yetu ya kiswahili, ama tafsiri ilo karibu zaidi ni ile ya kizungu inayosema (Sense), lakini Tafsiri ilotimia ni kurudi kwenye Fahamu. Vipi kurudi kwenye Fahamu ni wewe kujitenga na (Body)ukajua sasa mwili umekwisha kazi yake, na sasa nimepewa nafasi niangalie upande wa pili huu ulonileta hapa ulimwenguni,(Kumbuka wewe ni Body na spirit) Kumbuka uliletwa kipindi cha mwanzo ulikua mtoto na sasa hivi unarejeshwa kwenye udhaifu uleule wa mtoto lakini ukiwa na kitu adhimu kabisa cha kujijua kuwa ulipita katika njia tatu hizi, ile ya kwanza ulikua hujijui, ukapita ya ujanani ukawa na desturi ya kutokujali au kusahau kwa njia ya ulevi wa kila aina, mara (gossip)mpira,tv, mambo chungu nzima, na sasa umeingia kwenye uzee ukiwa na fahamu yako nzuri umeshapata kujiuliza jee maji haya sasa yanakwenda wapi?.
Endelea part 3
Siri ya hayo maji tuliyoitaja kwenye part 1 inatokezea hata wakati wa kulala au wa kufa kwako, nyakati nyengine lazima maji hayo yamiminike au yashuke ndio upate usingizi. Hiyo ni sehemu ya kwanza ya dalili za uhai ambazo zinakufanya huwezi kujizuia, maji lazima yatoke, fujo tupu mtaani watu wanachunga watoto wakiume na kike, ile isitokee fujo mitaani, mwanamke kafungiwa na wanaume wanaranda kama simba anatafuta swala, watu wanakwiba, wanadhulumu ,wanagombana yote sababu ya maji haya yanochupa kwa kasi.
Hiyo ni dalili ya kwanza ya Uhai, ikisha kuna dalili ya pili ya mwisho wa uhai. Soma taratibu kwa uangalifu mkubwa ili upate kufahamu kusudio ya darsa hii ili upate kubadilika, kumbuka sio kugeuka. Aya gani inayo tukumbusha Mwisho wa Uhai?
Sura ya Yaasin aya ya (68)
"وَمَن نُّعَمِّرۡهُ نُنَڪِّسۡهُ فِى ٱلۡخَلۡقِۖ أَفَلَا يَعۡقِلُونَ"
"Na tunayempa Umri tunamrejesha nyuma katika umbo(Lake)(Anakuwa kama mtoto)basi jee, hawayatii Akilini(Mafunzo haya).
Hapo kuna siri nzito ya kujiandaa na mwisho wa Uhai, katika aya hiyo kumetajwa umbo na Akili, Umbo linaondoshewa nguvu lina rudi kama ulivokua mtoto, Baba akiweza kukupiga, ulipokua mkubwa una nyanyua vyuma huoni kaacha kukupiga, na sasa hivi wewe kizee, kijana wakati wowote anaweza kukunasa vibao, Umbo linarejeshwa kama mtoto, unaona mwenyewe magoti hayafanyi kazi uzuri, miguu huwezi kukimbia, moyo unakunyima pumzi, macho na masikio haviwezi kutenda kazi kama zamani, meno yashapungua, sasa ushaanza kukaa ndani kipindi kirefu, habari za kutamani zimeshatangulia na wakati, mambo huyawezi tena, sasa kama huzijui dalili hizi ndio unaanza kukimbilia madawa ya kila aina ujirejeshe ujanani, ndio mnaambiwa hamyatii Akilini?.Kuyatia Akilini maana yake rudi kwenye (Siri ya Fahamu).
Lakini ilipotajwa akili ni kwa Tafsiri yetu ya kiswahili, ama tafsiri ilo karibu zaidi ni ile ya kizungu inayosema (Sense), lakini Tafsiri ilotimia ni kurudi kwenye Fahamu. Vipi kurudi kwenye Fahamu ni wewe kujitenga na (Body)ukajua sasa mwili umekwisha kazi yake, na sasa nimepewa nafasi niangalie upande wa pili huu ulonileta hapa ulimwenguni,(Kumbuka wewe ni Body na spirit) Kumbuka uliletwa kipindi cha mwanzo ulikua mtoto na sasa hivi unarejeshwa kwenye udhaifu uleule wa mtoto lakini ukiwa na kitu adhimu kabisa cha kujijua kuwa ulipita katika njia tatu hizi, ile ya kwanza ulikua hujijui, ukapita ya ujanani ukawa na desturi ya kutokujali au kusahau kwa njia ya ulevi wa kila aina, mara (gossip)mpira,tv, mambo chungu nzima, na sasa umeingia kwenye uzee ukiwa na fahamu yako nzuri umeshapata kujiuliza jee maji haya sasa yanakwenda wapi?.
Endelea part 3
MWISHO WA UHAI PART 3
Asalaam aleiykum
Ukitaka kujua yanakwenda wapi itabidi ujitose kwenye sheria mbili za Ulimengu huu ya kwanza ile ya (Gravitation) na ya pili ile ya (Levitation),Mwanzo ilikua maji hayo yanashuka chini kwa kasi, na sasa yamesita lazima uchunguze nini kimetokea, jee yaweza kuwa ndio (Levitation) kupanda juu kumeanza kufanya kazi, na sio kila mtu anapata zawadi hiyo ya (Levitation)wengine maji yanabakia hapo hapo kiunoni kwenye chem chem mpaka yana haribika,lakini kama umeipata hiyo hali ya (Levitation) utaijua pale inapozaliwa hekima juu yako, ukagundua sasa matamanio yamekatika na mimi nimepewa nafasi ya kugeuka.
Itumie nafasi hii ya (Levitation)kwa kutafuta (Favour) kutoka kwa Mollah wako kuupata Ucha Mungu, utastarehe katika kipindi hichi kilichobaki cha Mwisho wa uhai wako, jikubalishe kuwa mtoto tena, ipate tena ile (Innocent) yako ya Utotoni, ukifanikiwa utaanza kusafisha dhanmbi zako, sio kwenda kwa waganga na (Doctor)Wamasai kutafuta nguvu, hayo yanakuharibu na kukupeleka kaburini kabla hujatumia nafasi ya mwisho wa uhai wako.
Kumbuka sasa hivi maji yametulia, inofanya zogo ni akili yako kwa ajili ya mambo ya zamani, ukiweza kuipuuza basi ile (System) ya pili ya (Levitation) inaanza kufanya kazi yake kama inavofanya (Brain)yako kwa kula 90% ya (Vitamin) kwenye chakula unacho kula.
Hapo ndio Maji hayo yanaanza kufata (System)mpya ya (Levitation)yanaanza kupanda juu, hayakai palepale na hapo ndio inaanza kuzaliwa au kufunguliwa hiyo (Hekima)kumbuka ulivokua mdogo miaka (14)ilifunguliwa na kwenda chini, Na hivi sasa imefungwa na ina kwenda Juu. Hapo tena Utulivu unarejea mwanzo ulikua ukitafuta mambo ya dunia, sasa unarejea kutafuta mambo ya Akhera, unaanza kupata khofu hii akhera ipo? nikenda itakuaje, Vipi ntakutana na aliyeniumba, hiyo ndio (Quest)ya Utu uzima, hapo tena unaanza kuhamia Msikitini, na ukilitizama hilo utaliona Wazee wamejaa misikitini na vijana wapo na dunia yao kwenye (Madisco).
Linatokea hilo kwa sisi Vizee kwa sababu tunajua (Mwisho wa Uhai)umekaribia, Ikifika hali kama hiyo sasa unatakiwa uwe na tahadhari kubwa, kwa sababu kuna jambo lengine jipya linakushughulisha ambalo linakujia wakati huu nalo ni la watoto na mali, Unaanza kuilinda mali ili isimalizike, na watoto wanaanza kukutesa huyu hivi yule vile, inapofika hali kama hii Mwenye Enzi Mungu anakukumbusha tena ili uwe makini kwa kukwambia maneno yaliyomo kwenye sura ya (Munafiqoon aya ya 9-11).
"يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تُلۡهِكُمۡ أَمۡوَٲلُكُمۡ وَلَآ أَوۡلَـٰدُڪُمۡ عَن ذِڪۡرِ ٱللَّهِۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٲلِكَ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ هُمُ ٱلۡخَـٰسِرُونَ"
"Enyi Mlioamini yasiku sahaulisheni mali yenu wala watoto wenu(Katika) kumkumbuka Mwenye enzi Mungu, Na wafanyao hayo, hao ndio wenye kuhasirika".
Onyo hili wanapewa wale wenye imani, Mwanzo ilikua starehe ya dunia na sasa imemalizika kuna chengine kinazuka ile Mali ulochuma na watoto wako ndio inakuja kukufisidi mwisho huu wa uhai, Unataka kulinda mali usifilisike, unaendelea kufunga mahesabu, unataka cheo chako kisiteremke, na kufanya hivyo kunakupelekea kumsahau Mollah wako kabisa, Na watoto wanakushughulisha kwa mahitaji yao na tabia zao inakua kwenye moyo wako wewe Mungu hakai kabisa, mambo ya Akhera huyataki kabisa na hiyo ndio hasara yenyewe.
"وَأَنفِقُواْ مِن مَّا رَزَقۡنَـٰكُم مِّن قَبۡلِ أَن يَأۡتِىَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوۡلَآ أَخَّرۡتَنِىٓ إِلَىٰٓ أَجَلٍ۬ قَرِيبٍ۬ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ "
"Na toeni katika yale tuliyokupeni kabla mmoja wenu hayajamfikia mauti, kisha akasema, Mollah wangu hunighairishii muda kidogo,(Ili)Nikatoa sadaka na nikawa miongoni mwa watendao mema".
Ama tendo la kutoa lina cheo kikubwa sana mbele ya Mwenye enzi Mungu, kwanini ikawa hivyo kwa sababu kutoa ni sifa ya Mwenye enzi Mungu, "Amekupa uhai, afya, mapenzi, Akili, Mali,watoto na mengi kadhalika unayoyajua na usiyoyajua"sasa katika mtihani wake alokupa mdogo tu, ni katika hiyo mali yako anakujaribu na kukutizama, kama unamuamini, Wewe Muislam wa kweli, Kipindi cha sala hakikupiti, unataka pepo yake, jee unaweza kutoa, ukiweza kufanya hilo basi pepo haina wasiwasi wako juu yako, lakini shuruti lake utoe uko hai una nguvu zako, sio uko kwenye kitanda unawaambia watoto watoe, Toa sasa hivi una nguvu zako, toa usijali wakakushughulisha watoto watarithi nini, hiyo sio tatizo lako, ila usiwaache wakapata shida, lakini kuwa mstari wa mbele katika kutoa.
Kwani usiwache tena ushakua mgonjwa taabani ndio una wasiwasi wa kufa ukaanza kujitia ucha Mungu unatarajia Mollah wako akupe muda ili upate kuwa katika waja wema.
"وَلَن يُؤَخِّرَ ٱللَّهُ نَفۡسًا إِذَا جَآءَ أَجَلُهَاۚ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ"
"Lakini Mwenye enzi Mungu Hatakhairisha nafsi yoyote inapokuja ajali yake, Na Mwenye enzi mungu anazo habari za Mnayoyatenda".
Usitake kudanganya unapigana kutokana na kuwa na khofu, hutaki kufa, sasa unataka na huko unakokwenda ukapate Raha, ndio moyoni unajisemesha nikhairishie kufa kwangu nikafanye mema, lakini inapofika mwisho wa uhai hakuna, msamaha kila mmoja wetu anakwenda, na Mwenye enzi mungu anajua yote mnayoyatenda. Kwa hiyo kabla Uhai haujamalizika zitoe mali zako, katake msamaha kwa makosa yako,zidisha kumkumbuka Mollah wako, tena mapenzi ya Mollah wako yatakushukia katika huu Mwisho wa uhai wako.
Ukitaka kujua yanakwenda wapi itabidi ujitose kwenye sheria mbili za Ulimengu huu ya kwanza ile ya (Gravitation) na ya pili ile ya (Levitation),Mwanzo ilikua maji hayo yanashuka chini kwa kasi, na sasa yamesita lazima uchunguze nini kimetokea, jee yaweza kuwa ndio (Levitation) kupanda juu kumeanza kufanya kazi, na sio kila mtu anapata zawadi hiyo ya (Levitation)wengine maji yanabakia hapo hapo kiunoni kwenye chem chem mpaka yana haribika,lakini kama umeipata hiyo hali ya (Levitation) utaijua pale inapozaliwa hekima juu yako, ukagundua sasa matamanio yamekatika na mimi nimepewa nafasi ya kugeuka.
Itumie nafasi hii ya (Levitation)kwa kutafuta (Favour) kutoka kwa Mollah wako kuupata Ucha Mungu, utastarehe katika kipindi hichi kilichobaki cha Mwisho wa uhai wako, jikubalishe kuwa mtoto tena, ipate tena ile (Innocent) yako ya Utotoni, ukifanikiwa utaanza kusafisha dhanmbi zako, sio kwenda kwa waganga na (Doctor)Wamasai kutafuta nguvu, hayo yanakuharibu na kukupeleka kaburini kabla hujatumia nafasi ya mwisho wa uhai wako.
Kumbuka sasa hivi maji yametulia, inofanya zogo ni akili yako kwa ajili ya mambo ya zamani, ukiweza kuipuuza basi ile (System) ya pili ya (Levitation) inaanza kufanya kazi yake kama inavofanya (Brain)yako kwa kula 90% ya (Vitamin) kwenye chakula unacho kula.
Hapo ndio Maji hayo yanaanza kufata (System)mpya ya (Levitation)yanaanza kupanda juu, hayakai palepale na hapo ndio inaanza kuzaliwa au kufunguliwa hiyo (Hekima)kumbuka ulivokua mdogo miaka (14)ilifunguliwa na kwenda chini, Na hivi sasa imefungwa na ina kwenda Juu. Hapo tena Utulivu unarejea mwanzo ulikua ukitafuta mambo ya dunia, sasa unarejea kutafuta mambo ya Akhera, unaanza kupata khofu hii akhera ipo? nikenda itakuaje, Vipi ntakutana na aliyeniumba, hiyo ndio (Quest)ya Utu uzima, hapo tena unaanza kuhamia Msikitini, na ukilitizama hilo utaliona Wazee wamejaa misikitini na vijana wapo na dunia yao kwenye (Madisco).
Linatokea hilo kwa sisi Vizee kwa sababu tunajua (Mwisho wa Uhai)umekaribia, Ikifika hali kama hiyo sasa unatakiwa uwe na tahadhari kubwa, kwa sababu kuna jambo lengine jipya linakushughulisha ambalo linakujia wakati huu nalo ni la watoto na mali, Unaanza kuilinda mali ili isimalizike, na watoto wanaanza kukutesa huyu hivi yule vile, inapofika hali kama hii Mwenye Enzi Mungu anakukumbusha tena ili uwe makini kwa kukwambia maneno yaliyomo kwenye sura ya (Munafiqoon aya ya 9-11).
"يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تُلۡهِكُمۡ أَمۡوَٲلُكُمۡ وَلَآ أَوۡلَـٰدُڪُمۡ عَن ذِڪۡرِ ٱللَّهِۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٲلِكَ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ هُمُ ٱلۡخَـٰسِرُونَ"
"Enyi Mlioamini yasiku sahaulisheni mali yenu wala watoto wenu(Katika) kumkumbuka Mwenye enzi Mungu, Na wafanyao hayo, hao ndio wenye kuhasirika".
Onyo hili wanapewa wale wenye imani, Mwanzo ilikua starehe ya dunia na sasa imemalizika kuna chengine kinazuka ile Mali ulochuma na watoto wako ndio inakuja kukufisidi mwisho huu wa uhai, Unataka kulinda mali usifilisike, unaendelea kufunga mahesabu, unataka cheo chako kisiteremke, na kufanya hivyo kunakupelekea kumsahau Mollah wako kabisa, Na watoto wanakushughulisha kwa mahitaji yao na tabia zao inakua kwenye moyo wako wewe Mungu hakai kabisa, mambo ya Akhera huyataki kabisa na hiyo ndio hasara yenyewe.
"وَأَنفِقُواْ مِن مَّا رَزَقۡنَـٰكُم مِّن قَبۡلِ أَن يَأۡتِىَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوۡلَآ أَخَّرۡتَنِىٓ إِلَىٰٓ أَجَلٍ۬ قَرِيبٍ۬ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ "
"Na toeni katika yale tuliyokupeni kabla mmoja wenu hayajamfikia mauti, kisha akasema, Mollah wangu hunighairishii muda kidogo,(Ili)Nikatoa sadaka na nikawa miongoni mwa watendao mema".
Ama tendo la kutoa lina cheo kikubwa sana mbele ya Mwenye enzi Mungu, kwanini ikawa hivyo kwa sababu kutoa ni sifa ya Mwenye enzi Mungu, "Amekupa uhai, afya, mapenzi, Akili, Mali,watoto na mengi kadhalika unayoyajua na usiyoyajua"sasa katika mtihani wake alokupa mdogo tu, ni katika hiyo mali yako anakujaribu na kukutizama, kama unamuamini, Wewe Muislam wa kweli, Kipindi cha sala hakikupiti, unataka pepo yake, jee unaweza kutoa, ukiweza kufanya hilo basi pepo haina wasiwasi wako juu yako, lakini shuruti lake utoe uko hai una nguvu zako, sio uko kwenye kitanda unawaambia watoto watoe, Toa sasa hivi una nguvu zako, toa usijali wakakushughulisha watoto watarithi nini, hiyo sio tatizo lako, ila usiwaache wakapata shida, lakini kuwa mstari wa mbele katika kutoa.
Kwani usiwache tena ushakua mgonjwa taabani ndio una wasiwasi wa kufa ukaanza kujitia ucha Mungu unatarajia Mollah wako akupe muda ili upate kuwa katika waja wema.
"وَلَن يُؤَخِّرَ ٱللَّهُ نَفۡسًا إِذَا جَآءَ أَجَلُهَاۚ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ"
"Lakini Mwenye enzi Mungu Hatakhairisha nafsi yoyote inapokuja ajali yake, Na Mwenye enzi mungu anazo habari za Mnayoyatenda".
Usitake kudanganya unapigana kutokana na kuwa na khofu, hutaki kufa, sasa unataka na huko unakokwenda ukapate Raha, ndio moyoni unajisemesha nikhairishie kufa kwangu nikafanye mema, lakini inapofika mwisho wa uhai hakuna, msamaha kila mmoja wetu anakwenda, na Mwenye enzi mungu anajua yote mnayoyatenda. Kwa hiyo kabla Uhai haujamalizika zitoe mali zako, katake msamaha kwa makosa yako,zidisha kumkumbuka Mollah wako, tena mapenzi ya Mollah wako yatakushukia katika huu Mwisho wa uhai wako.
Sunday, September 24, 2017
SIRI YA FAHAMU PART 1
Asalaam Aleiykum
Nakupeleka kwenye Safari ya kuondosha matatizo yako, Safari ambayo kama utajitahidi ukaienda mpaka ukafika basi utakua umezaliwa tena (Born again), faida yake ni kubwa sana kwako, Safari itakayo kufanya uondokane na kiza cha tegemezi ya jamii, waganga, madaktari, maprofesa, Masheikh na kila Mwenye (Control) ya Maisha yako, wote hao utawaweka kando utakapo fika safari yako katika mji wako wa Fahamu.
Huwezi kwenda kwenye mji huu wa fahamu lazima upitie kwenye Moyo, nikisema moyo watu wengine wanafahamu labda ufanyiwe operesheni, Kutokana na ile fahamu ya moyo ni kipande cha nyama, ndio ni kipande cha nyama lakini kina siri nyengine kimeificha ya (sipiritual)tunajua (Biological)ni (Pump)ya kusukuma damu, na vile vile tunaelewa kuwa damu ndio ina (Supply) kile chombo muhimu cha uhai wetu (Oxygen) lakini hatufahamu siri yake ya upande wa pili kuna nini, kulijua hilo ndio tunaingia katika darsa yetu ya leo (Siri ya Fahamu) ili upate kujua japo kwa uchache nini kinatokezea ukirudi kwenye fahamu.
Kumbuka hujawahi kurudi kwenye fahamu toka ulipotoka, na hilo ndio tatizo letu wengi, nakupa wasia jitahidi sana kabla ya kuondoka Ulimwengu huu urudi kwenye Fahamu yako, nikisema Fahamu nakusudia (Your real self). Ulipokua Mtoto ulikua na Fahamu lakini hukuwa na Akili, ulipokua mtu mzima umejaa Akili lakini umesahau Fahamu. Nimesema umesahau kwa sababu unayo ndio (original) yako, itafute urudi kama mwanzo, itafute urudi (pure) Vipi utaitafuta .
Endelea part 2
Nakupeleka kwenye Safari ya kuondosha matatizo yako, Safari ambayo kama utajitahidi ukaienda mpaka ukafika basi utakua umezaliwa tena (Born again), faida yake ni kubwa sana kwako, Safari itakayo kufanya uondokane na kiza cha tegemezi ya jamii, waganga, madaktari, maprofesa, Masheikh na kila Mwenye (Control) ya Maisha yako, wote hao utawaweka kando utakapo fika safari yako katika mji wako wa Fahamu.
Huwezi kwenda kwenye mji huu wa fahamu lazima upitie kwenye Moyo, nikisema moyo watu wengine wanafahamu labda ufanyiwe operesheni, Kutokana na ile fahamu ya moyo ni kipande cha nyama, ndio ni kipande cha nyama lakini kina siri nyengine kimeificha ya (sipiritual)tunajua (Biological)ni (Pump)ya kusukuma damu, na vile vile tunaelewa kuwa damu ndio ina (Supply) kile chombo muhimu cha uhai wetu (Oxygen) lakini hatufahamu siri yake ya upande wa pili kuna nini, kulijua hilo ndio tunaingia katika darsa yetu ya leo (Siri ya Fahamu) ili upate kujua japo kwa uchache nini kinatokezea ukirudi kwenye fahamu.
Kumbuka hujawahi kurudi kwenye fahamu toka ulipotoka, na hilo ndio tatizo letu wengi, nakupa wasia jitahidi sana kabla ya kuondoka Ulimwengu huu urudi kwenye Fahamu yako, nikisema Fahamu nakusudia (Your real self). Ulipokua Mtoto ulikua na Fahamu lakini hukuwa na Akili, ulipokua mtu mzima umejaa Akili lakini umesahau Fahamu. Nimesema umesahau kwa sababu unayo ndio (original) yako, itafute urudi kama mwanzo, itafute urudi (pure) Vipi utaitafuta .
Endelea part 2
SIRI YA FAHAMU PART 2
Asalaam Aleiykum
Hilo ndio kusudio la darsa yetu ya leo ili kukufanya kwa mara ya mwanzo uipate (Control)ya maisha yako, Kwa sababu muda huu wote (Control)Yote iko katika Maandiko(Akili). Akili imekutia uvivu, hutaki kujijua weye nani na hapa Ulimwenguni unafanya nini, Umri wote huu unaishi kwa kuitegemea Akili na imekuweka kwenye (Automatic Mode). Umefika wakati ukabidhiwe (Gear) uwe wewe Mwenyewe una (Control)Maisha yako.
Mwenye Enzi Mungu hakutunyima Elimu, Katwambia katika sura ya (Qalam)kwa kuapia Akili na kusema Naiapia Akili na kwa yaandikayo Akili hiyo, Na Wala haikua Neema hiyo kuwa wendaazimu, Akili yako kila siku inaandika na kwa kuwa unaituma sana sasa imejaa na ishachoka kwa hiyo imeweka desturi ya ku(Repeat)inarejea mambo hayo kwa hayo, mara chache unatumia nyenzo yako nyengine ulonayo ambayo ni hiyo Fahamu, au ita Roho, au ita (Consciousness)upendavyo wewe, ila ninacho kujulisha kuwa nyenzo hii unaitumia mara chache sana ima inapotokea mshituko au unapojifundisha jambo, na inawezekana umeitumia mara ya mwisho ulivokua mdogo, Nakuuliza jee umeshawahi kurudi tena pahala hapo kwenye (Centre)yako, najua unarudi mara kwa mara lakini hujijui.
Kabla ya kuendelea mbele wacha nifahamishe vizuri kusudio la neno (Fahamu) au (concsiousness). Mwenye Enzi Mungu Kaumba Mauti na Maisha katikati ya viwili hivi kuna hicho chenye kuishi enzi ya milele kiitwacho (Roho)au (Life)ambayo inaishi hiyo Fahamu.
Ndio maana utaona Fahamu ina (Capacity)yake, nisiseme hivi ukadhani Fahamu ndio hiyo Roho, Kwa sababu kumbuka unatokwa na Fahamu lakini roho unayo, Na hiyo Fahamu inaishi ndani ya Roho, kwa hiyo ndani ya hiyo fahamu kuna Muujiza wake wa aina mbili, unaweza kuipata Fahamu ndani ya Maisha au kwenye Mauti, ukawa huku unakufa na unajiona unavomalizika, Sasa ikiwa si mvivu unaweza hapa hapa ulimwenguni ukaishi katika hiyo fahamu ambayo itakufungulia mambo mengi, nisiseme fahamu ukaanza kudhani ni Akili, Fahamu ni (Sipritual Phenomenon) na Akili ni (Biological Process) Sasa vipi utaipata siri hii ili uwache kuishi kwenye Akili.
Endelea part 3
Hilo ndio kusudio la darsa yetu ya leo ili kukufanya kwa mara ya mwanzo uipate (Control)ya maisha yako, Kwa sababu muda huu wote (Control)Yote iko katika Maandiko(Akili). Akili imekutia uvivu, hutaki kujijua weye nani na hapa Ulimwenguni unafanya nini, Umri wote huu unaishi kwa kuitegemea Akili na imekuweka kwenye (Automatic Mode). Umefika wakati ukabidhiwe (Gear) uwe wewe Mwenyewe una (Control)Maisha yako.
Mwenye Enzi Mungu hakutunyima Elimu, Katwambia katika sura ya (Qalam)kwa kuapia Akili na kusema Naiapia Akili na kwa yaandikayo Akili hiyo, Na Wala haikua Neema hiyo kuwa wendaazimu, Akili yako kila siku inaandika na kwa kuwa unaituma sana sasa imejaa na ishachoka kwa hiyo imeweka desturi ya ku(Repeat)inarejea mambo hayo kwa hayo, mara chache unatumia nyenzo yako nyengine ulonayo ambayo ni hiyo Fahamu, au ita Roho, au ita (Consciousness)upendavyo wewe, ila ninacho kujulisha kuwa nyenzo hii unaitumia mara chache sana ima inapotokea mshituko au unapojifundisha jambo, na inawezekana umeitumia mara ya mwisho ulivokua mdogo, Nakuuliza jee umeshawahi kurudi tena pahala hapo kwenye (Centre)yako, najua unarudi mara kwa mara lakini hujijui.
Kabla ya kuendelea mbele wacha nifahamishe vizuri kusudio la neno (Fahamu) au (concsiousness). Mwenye Enzi Mungu Kaumba Mauti na Maisha katikati ya viwili hivi kuna hicho chenye kuishi enzi ya milele kiitwacho (Roho)au (Life)ambayo inaishi hiyo Fahamu.
Ndio maana utaona Fahamu ina (Capacity)yake, nisiseme hivi ukadhani Fahamu ndio hiyo Roho, Kwa sababu kumbuka unatokwa na Fahamu lakini roho unayo, Na hiyo Fahamu inaishi ndani ya Roho, kwa hiyo ndani ya hiyo fahamu kuna Muujiza wake wa aina mbili, unaweza kuipata Fahamu ndani ya Maisha au kwenye Mauti, ukawa huku unakufa na unajiona unavomalizika, Sasa ikiwa si mvivu unaweza hapa hapa ulimwenguni ukaishi katika hiyo fahamu ambayo itakufungulia mambo mengi, nisiseme fahamu ukaanza kudhani ni Akili, Fahamu ni (Sipritual Phenomenon) na Akili ni (Biological Process) Sasa vipi utaipata siri hii ili uwache kuishi kwenye Akili.
Endelea part 3
SIRI YA FAHAMU PART 3
Asalaam Aleiykum
Kuipata Siri hii ya Fahamu inatakiwa jambo la kwanza Urudi kwenye Moyo, vipi utarudi kwenye moyo, ukirudi kwenye moyo kwa kutumia akili utakutana na damu tupu, (Pump)inasukuma damu mambo yamekwisha, sasa vipi utarejea kwenye Moyo?.
Hakuna njia nyengine isipokua ukahudhurie aya ya (28)sura ya Rad ikupe habari ni vipi inakua.
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَطۡمَٮِٕنُّ قُلُوبُهُم بِذِكۡرِ ٱللَّهِۗ أَلَا بِذِڪۡرِ ٱللَّهِ تَطۡمَٮِٕنُّ ٱلۡقُلُوبُ
(Na) wale waloamini na zikatulia nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenye enzi mungu.Sikilizeni Kwa Kumkumbuka Mwenye enzi Mungu nyoyo hutulia.
Aya hiyo ni kama mbegu ukiipanda katika moyo wako basi ina faida kubwa kabisa, Mwanzo aya inataja kuamini, kwanini kuamini, kwa sababu Imani inatokana na kuambiwa, na kuambiwa ni kama kuoneshwa njia, usibaki njiani sasa unatakiwa uende, uende wapi, nenda moyoni kwa kufanya nini? kumkumbuka Mollah wako, "Hapa itabidi nifafanue"kuhusu kumkumbuka, sio kufanya ile dhikr ya kutoa sauti (Allahua Allahua)Kumkumbuka ni kuchagua katika vile alivyoumba Mwenye enzi Mungu halafu ukaanza kuzingatia uwezo wa Mwenye enzi Mungu bila ya kutumia Akili, Ni kazi lakini inawezekana, kwa sababu ukiangalia mpira unaweza unakuwepo katika (Centre)yako, ukiwepo senema hutumii Akili, Ukizungumza pia hutumii Akili, unatoa (Direct)unakuwepo kwenye Fahamu kwa hiyo hicho ndio kinachotakiwa kifanyike kila wakati, na wakati mwengine unapotizama jambo uwepo kwenye fahamu, Akili isiingie kati, ukitizama mti akili isiingie, ukiangalia Ua akili isiingie, kidogo kidogo ukiweza kufanya hivyo una (Polish your Heart)Mpaka ukisafika Moyo unatulia, kutulia kwake tena inakua huna (SplitMind)nani anakwenda motoni, nani haingii peponi, sala yako inakubalika haikubaliki hushughuliki kabisa na mambo ambayo hayako kwenye uwezo wako, hapo tena unakua umetulia unaanza kupata (Siri ya Fahamu)mambo mengi yanafunguliwa kwako, ita upendavyo (Hekima) au Makarama, Khofu zote zinaondoka, Sala zako zinakua tafauti, mazungumzo yako yanakua ya aina nyengine kutokana na kuishi kwako kwenye Fahamu.
Watu watakushangaa wakikukuta wanaona kuna kitu kimekutokezea lakini hawajui kitu gani, maisha yako yanakua na furaha tupu, ushaondoka kwenye Akili unaishi moyoni, Mtu akikusema, akikutukana unacheka tu, kwa sababu huna tena ile desturi ya Akili ya kureje rejea mambo, na ghadhabu, hamaki, Moyo umetulia unaishi kwenye siri ya mambo, lakini shuruti lake lazima (Uache kutumia Akili)uwe unaishi kwenye Fahamu ambayo ina (Control)akili, kumbuka jambo lolote unalotaka kulifanya ukiwa umetulia mwanzo linatokea kwenye Fahamu, halafu ndio linatumwa kwenye Akili, lakini kwa kuwa Akili imekutawala kwako wewe linaanza Akilini na kupeleka Amri kwenye Fahamu, ndio maana toba hazikwishi, Akili inailaza Fahamu, ndio utasikia anajitoa Fahamu kwa mazungumzo, kwa Ulevi na vyengine mnavyo vifahamu, zote hizo ni mbinu za kuilaza fahamu, lakini ukitumia njia za kufatilia kwa uwezo wake Muumba basi utafikia pahala utakua wewe ndio (Master)wa Akili yako.
Kumbuka Udogoni kwanini ulikua na Furaha? kwa sababu ulikua hujajaza (Book)lako la Akili ndio maana ulikua uki(Enjoy), basi uwezo wa kurejea tena unao, ndio maana utaona tuna uwezo wa kukumbuka raha za utotoni, pale tunakua tumerudi kwenye Fahamu, ndio kila mtu utoto wake anaeleza furaha alokua nayo, umemsikia mtu mzima akakwambia ana furaha(Stress) tupu kwa sababu ya Maisha ya Akili, utaona tuna uwezo wa kukumbuka mpaka umri wa miaka minne baadhi ya mambo, lakini ukipata fahamu yako unaweza kurudi nyuma ukakumbuka mpaka mtoto wa mwaka nini kilitokea, kwa sababu Roho yako sio Mtoto wala mtu mzima ni yenye kuishi milele na yenye kujua yote yenye kutokea katika maisha yako ya Uhai na mauti, itafute siri ya Fahamu uone uzuri wa maisha.
Kuipata Siri hii ya Fahamu inatakiwa jambo la kwanza Urudi kwenye Moyo, vipi utarudi kwenye moyo, ukirudi kwenye moyo kwa kutumia akili utakutana na damu tupu, (Pump)inasukuma damu mambo yamekwisha, sasa vipi utarejea kwenye Moyo?.
Hakuna njia nyengine isipokua ukahudhurie aya ya (28)sura ya Rad ikupe habari ni vipi inakua.
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَطۡمَٮِٕنُّ قُلُوبُهُم بِذِكۡرِ ٱللَّهِۗ أَلَا بِذِڪۡرِ ٱللَّهِ تَطۡمَٮِٕنُّ ٱلۡقُلُوبُ
(Na) wale waloamini na zikatulia nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenye enzi mungu.Sikilizeni Kwa Kumkumbuka Mwenye enzi Mungu nyoyo hutulia.
Aya hiyo ni kama mbegu ukiipanda katika moyo wako basi ina faida kubwa kabisa, Mwanzo aya inataja kuamini, kwanini kuamini, kwa sababu Imani inatokana na kuambiwa, na kuambiwa ni kama kuoneshwa njia, usibaki njiani sasa unatakiwa uende, uende wapi, nenda moyoni kwa kufanya nini? kumkumbuka Mollah wako, "Hapa itabidi nifafanue"kuhusu kumkumbuka, sio kufanya ile dhikr ya kutoa sauti (Allahua Allahua)Kumkumbuka ni kuchagua katika vile alivyoumba Mwenye enzi Mungu halafu ukaanza kuzingatia uwezo wa Mwenye enzi Mungu bila ya kutumia Akili, Ni kazi lakini inawezekana, kwa sababu ukiangalia mpira unaweza unakuwepo katika (Centre)yako, ukiwepo senema hutumii Akili, Ukizungumza pia hutumii Akili, unatoa (Direct)unakuwepo kwenye Fahamu kwa hiyo hicho ndio kinachotakiwa kifanyike kila wakati, na wakati mwengine unapotizama jambo uwepo kwenye fahamu, Akili isiingie kati, ukitizama mti akili isiingie, ukiangalia Ua akili isiingie, kidogo kidogo ukiweza kufanya hivyo una (Polish your Heart)Mpaka ukisafika Moyo unatulia, kutulia kwake tena inakua huna (SplitMind)nani anakwenda motoni, nani haingii peponi, sala yako inakubalika haikubaliki hushughuliki kabisa na mambo ambayo hayako kwenye uwezo wako, hapo tena unakua umetulia unaanza kupata (Siri ya Fahamu)mambo mengi yanafunguliwa kwako, ita upendavyo (Hekima) au Makarama, Khofu zote zinaondoka, Sala zako zinakua tafauti, mazungumzo yako yanakua ya aina nyengine kutokana na kuishi kwako kwenye Fahamu.
Watu watakushangaa wakikukuta wanaona kuna kitu kimekutokezea lakini hawajui kitu gani, maisha yako yanakua na furaha tupu, ushaondoka kwenye Akili unaishi moyoni, Mtu akikusema, akikutukana unacheka tu, kwa sababu huna tena ile desturi ya Akili ya kureje rejea mambo, na ghadhabu, hamaki, Moyo umetulia unaishi kwenye siri ya mambo, lakini shuruti lake lazima (Uache kutumia Akili)uwe unaishi kwenye Fahamu ambayo ina (Control)akili, kumbuka jambo lolote unalotaka kulifanya ukiwa umetulia mwanzo linatokea kwenye Fahamu, halafu ndio linatumwa kwenye Akili, lakini kwa kuwa Akili imekutawala kwako wewe linaanza Akilini na kupeleka Amri kwenye Fahamu, ndio maana toba hazikwishi, Akili inailaza Fahamu, ndio utasikia anajitoa Fahamu kwa mazungumzo, kwa Ulevi na vyengine mnavyo vifahamu, zote hizo ni mbinu za kuilaza fahamu, lakini ukitumia njia za kufatilia kwa uwezo wake Muumba basi utafikia pahala utakua wewe ndio (Master)wa Akili yako.
Kumbuka Udogoni kwanini ulikua na Furaha? kwa sababu ulikua hujajaza (Book)lako la Akili ndio maana ulikua uki(Enjoy), basi uwezo wa kurejea tena unao, ndio maana utaona tuna uwezo wa kukumbuka raha za utotoni, pale tunakua tumerudi kwenye Fahamu, ndio kila mtu utoto wake anaeleza furaha alokua nayo, umemsikia mtu mzima akakwambia ana furaha(Stress) tupu kwa sababu ya Maisha ya Akili, utaona tuna uwezo wa kukumbuka mpaka umri wa miaka minne baadhi ya mambo, lakini ukipata fahamu yako unaweza kurudi nyuma ukakumbuka mpaka mtoto wa mwaka nini kilitokea, kwa sababu Roho yako sio Mtoto wala mtu mzima ni yenye kuishi milele na yenye kujua yote yenye kutokea katika maisha yako ya Uhai na mauti, itafute siri ya Fahamu uone uzuri wa maisha.
Monday, August 21, 2017
TANGAZO LA KIFO PART 1
Asalaam Aleiykum
Kifo kimetangazwa chako wewe na mimi, sote kuna siku tutakufa japo kwa njia au maradhi tafauti, Kifo hichi kimetangazwa tokea siku ile ulipozaliwa kutoka katika Tumbo la mzee wako, ila nashangaa ndio kimekua adui wetu mkubwa, na ukimwambia Mtu kuwa Kifo ni rafiki yako anasema (Sheikh Baja)huyoo sasa lazima akachinjiwe kinda la Kunguru, pengine Akili zinampungua.
Napenda uelewe sote tutakufa itakapofika wakati wetu, Na wakati wenyewe haupo mbali unatunyemelea kidogo kidogo.
Sasa vipi Kifo hichi kinatangazwa?.
Kwanza kabisa unatakiwa ukumbuke vitu viwili hivi kuzaliwa na kufa ni Mtu na ndugu yake, kila kitu kimezungukwa na umauti, Mwenye enzi Mungu kasema kwenye Quraan tumeujaalia usingizi kama kufa, sasa jitizame wewe jee hujalala, vipi utajiangalia kama umelala jaribu kukumbuka jina lako japo kwa dakika moja ukiweza kukumbuka basi wewe umacho, lakini ukisahau tu unakua ushakwenda kwenye ndoto kama vile ulo lala usingizi wa kitandani, tafauti yake usingizi huu unaota uko macho,Unaamka siku ya kufa, hapo tena hakuna usingizi, hakuna kusahau, kila kitu kinakua (Original), unashuhudia Maisha upande wa kushoto yanakutoka, Unasikia watu kwa mbali wanapanga mazishi yako, vipi wataufukia mwili wako, wanasema huyu haji juu tena, Upande wako wa kulia Mauti yanatokea (Live) unaona (energy)hiyo inaondoka kwa (Speed)mbona si hisi miguu yangu, mbona moyo unapiga taratibu, macho mbona yanapoteza nuru na hivi na vile, kumbuka wewe unaendelea kuwa (Hai) Roho ulonayo haifi, ukiligundua hilo ndio utaona kumbe nimezungukwa na mauti kila saa na dakika, na hiyo ndio maana ya uhai na mauti mtu na ndugu yake, unaona vipi vinyama miti vidudu vinavopita na kufa katika ulimwengu huu, Na wewe ukizaliwa unapita wakati wa kukua mpaka kipindi maalum ambacho kukua huko kuna (Stop), Hapo tena unapita katika kipindi kifupi cha subira ambapo hamna chochote chenye kutokezea isipokua (Unachapa raha za Ujana)wakati huo wote (Kifo) kinatokea lakini kidogo kidogo pasi na wewe kujua. Halafu unafika wakati wa kulisikia tangazo wengine wanasema Tangazo hili linaanza unapogonga miaka 40 na wengine wanasema 50, Lakini kwa ujumla tangazo hili lina sauti ya ukimya, hii pale ulipokua mzima hujui kumbe unakufa ndani kwa ndani, na sauti ya wazi pale maradhi yanapowasili na kukupa taarifa sasa jiandae, karibu utaondoka, dongo lishachoka linataka likafukiwe, haliwezi kukubeba tena, sasa ukiamua kusikia au kutokusia hilo ni shauri yako.
Unapofika Umri huo nilotaja Rafiki huyu tunaye mtaja kwa jina la kifo anaanza kujitokeza wazi wazi kwa njia ya Maradhi, hapo ndio sote tunajijua kumbe tutakufa iwe kwa ugonjwa wa Sukari au Cancer, iwe Ugonjwa wa Moyo au Ukimwi, Iwe Malaria au Homa ya Maini na Maradhi mengi tunayoyajua na tusoyajua, Na kifo hichi kinatokea Mpaka kwenye Akili zetu kitu ambacho ndio kwanza tunapata nafasi ya kugundua, kwa ufupi Kifo kimetuzunguka kila upande, huwezi kuepuka, Kifo ni Rafiki yetu na sote tumeshaanza kufa toka zamani, Napenda uelewe kufa ni fadhila kubwa kutoka kwa Mollah wako, kwa sababu hebu jiangalie unakuaje ukiumwa bila ya kupata nafuu hiyo inakua (Quality)gani ya maisha, kwa hiyo ukifikia Umri wa kuondoka usinganganie hebu nenda kwa salama nyumbani kama ulivoambiwa. "Ewe Nafsi Mwenye Matumaini Rejea ukiwa umeridhika na Mollah wako karidhika na Wewe".
Sasa nini kino tufanya tusahau ni hizi akili zetu, na hilo ni jambo zuri kwani ingekua tunamkumbuka rafiki huyu hakuna yoyote angeweza kuishi. Sasa kwanini tunaogopa (Death)Kifo. Tunaogopa Kifo kwa sababu hatujui nini kitatokea baada ya kufa kwetu, na hilo ni jambo linalo chezea akili zetu (What Happen)?.Iman zetu zote zina simama hapo, Tunaishi kwa Ahadi lakini hata hiyo Ahadi tunaitilia shaka, Kwanini inakua hivyo? itabidi ujiulize swali hili siku zote unaumwa maradhi unayo, wakati wowote unaweza kufa, wenzako wengi washatangulia sasa kinachokupa khofu khassa ni kitu gani. Ntakufanyia wepesi wa jawabu kwa kukwambia khofu yote ipo kwenye kutolewa roho, kwenye huko kurejea, kwa sababu unajijua au ushaona huu Mwili wako ni (Body) ilotokana na Udongo, hilo huna shaka nalo, lakini matatizo makubwa hujijui wewe nani, Na Ukifa unakwenda wapi, na Mwanzo ulitokea wapi?.
Endelea part 2.
Kifo kimetangazwa chako wewe na mimi, sote kuna siku tutakufa japo kwa njia au maradhi tafauti, Kifo hichi kimetangazwa tokea siku ile ulipozaliwa kutoka katika Tumbo la mzee wako, ila nashangaa ndio kimekua adui wetu mkubwa, na ukimwambia Mtu kuwa Kifo ni rafiki yako anasema (Sheikh Baja)huyoo sasa lazima akachinjiwe kinda la Kunguru, pengine Akili zinampungua.
Napenda uelewe sote tutakufa itakapofika wakati wetu, Na wakati wenyewe haupo mbali unatunyemelea kidogo kidogo.
Sasa vipi Kifo hichi kinatangazwa?.
Kwanza kabisa unatakiwa ukumbuke vitu viwili hivi kuzaliwa na kufa ni Mtu na ndugu yake, kila kitu kimezungukwa na umauti, Mwenye enzi Mungu kasema kwenye Quraan tumeujaalia usingizi kama kufa, sasa jitizame wewe jee hujalala, vipi utajiangalia kama umelala jaribu kukumbuka jina lako japo kwa dakika moja ukiweza kukumbuka basi wewe umacho, lakini ukisahau tu unakua ushakwenda kwenye ndoto kama vile ulo lala usingizi wa kitandani, tafauti yake usingizi huu unaota uko macho,Unaamka siku ya kufa, hapo tena hakuna usingizi, hakuna kusahau, kila kitu kinakua (Original), unashuhudia Maisha upande wa kushoto yanakutoka, Unasikia watu kwa mbali wanapanga mazishi yako, vipi wataufukia mwili wako, wanasema huyu haji juu tena, Upande wako wa kulia Mauti yanatokea (Live) unaona (energy)hiyo inaondoka kwa (Speed)mbona si hisi miguu yangu, mbona moyo unapiga taratibu, macho mbona yanapoteza nuru na hivi na vile, kumbuka wewe unaendelea kuwa (Hai) Roho ulonayo haifi, ukiligundua hilo ndio utaona kumbe nimezungukwa na mauti kila saa na dakika, na hiyo ndio maana ya uhai na mauti mtu na ndugu yake, unaona vipi vinyama miti vidudu vinavopita na kufa katika ulimwengu huu, Na wewe ukizaliwa unapita wakati wa kukua mpaka kipindi maalum ambacho kukua huko kuna (Stop), Hapo tena unapita katika kipindi kifupi cha subira ambapo hamna chochote chenye kutokezea isipokua (Unachapa raha za Ujana)wakati huo wote (Kifo) kinatokea lakini kidogo kidogo pasi na wewe kujua. Halafu unafika wakati wa kulisikia tangazo wengine wanasema Tangazo hili linaanza unapogonga miaka 40 na wengine wanasema 50, Lakini kwa ujumla tangazo hili lina sauti ya ukimya, hii pale ulipokua mzima hujui kumbe unakufa ndani kwa ndani, na sauti ya wazi pale maradhi yanapowasili na kukupa taarifa sasa jiandae, karibu utaondoka, dongo lishachoka linataka likafukiwe, haliwezi kukubeba tena, sasa ukiamua kusikia au kutokusia hilo ni shauri yako.
Unapofika Umri huo nilotaja Rafiki huyu tunaye mtaja kwa jina la kifo anaanza kujitokeza wazi wazi kwa njia ya Maradhi, hapo ndio sote tunajijua kumbe tutakufa iwe kwa ugonjwa wa Sukari au Cancer, iwe Ugonjwa wa Moyo au Ukimwi, Iwe Malaria au Homa ya Maini na Maradhi mengi tunayoyajua na tusoyajua, Na kifo hichi kinatokea Mpaka kwenye Akili zetu kitu ambacho ndio kwanza tunapata nafasi ya kugundua, kwa ufupi Kifo kimetuzunguka kila upande, huwezi kuepuka, Kifo ni Rafiki yetu na sote tumeshaanza kufa toka zamani, Napenda uelewe kufa ni fadhila kubwa kutoka kwa Mollah wako, kwa sababu hebu jiangalie unakuaje ukiumwa bila ya kupata nafuu hiyo inakua (Quality)gani ya maisha, kwa hiyo ukifikia Umri wa kuondoka usinganganie hebu nenda kwa salama nyumbani kama ulivoambiwa. "Ewe Nafsi Mwenye Matumaini Rejea ukiwa umeridhika na Mollah wako karidhika na Wewe".
Sasa nini kino tufanya tusahau ni hizi akili zetu, na hilo ni jambo zuri kwani ingekua tunamkumbuka rafiki huyu hakuna yoyote angeweza kuishi. Sasa kwanini tunaogopa (Death)Kifo. Tunaogopa Kifo kwa sababu hatujui nini kitatokea baada ya kufa kwetu, na hilo ni jambo linalo chezea akili zetu (What Happen)?.Iman zetu zote zina simama hapo, Tunaishi kwa Ahadi lakini hata hiyo Ahadi tunaitilia shaka, Kwanini inakua hivyo? itabidi ujiulize swali hili siku zote unaumwa maradhi unayo, wakati wowote unaweza kufa, wenzako wengi washatangulia sasa kinachokupa khofu khassa ni kitu gani. Ntakufanyia wepesi wa jawabu kwa kukwambia khofu yote ipo kwenye kutolewa roho, kwenye huko kurejea, kwa sababu unajijua au ushaona huu Mwili wako ni (Body) ilotokana na Udongo, hilo huna shaka nalo, lakini matatizo makubwa hujijui wewe nani, Na Ukifa unakwenda wapi, na Mwanzo ulitokea wapi?.
Endelea part 2.
TANGAZO LA KIFO PART 2
Asalaam Aleiykum
Sasa kwa kuwa hatujijui wewe ni nani?, ina tushinda pia kuelewa lini unaondoka, Lini utavua guo la udongo na ubaki wewe (Pure Soul), siku gani hiyo utakayo kaa pembeni ukashuhudia watu wanakosha Mwili wako ikisha hao wanauchukua kuupeleka makaburini, halafu wanautupa bila hata ya dua.
Ukiishi Maisha ya Kiroho siku hiyo ni Rahisi kwako kuijua, au kusikia hilo tangazo kabla ya miezi sita kufika, leo hapa nitakupa dalili mbili za (Mystic)Mawalii wengi ambao wanajua kama karibu kuondoka, ndio maana wengine wanaandika, wengine wanasema, wengine wanataarisha sanda zao kwa kujua safari ishawadia, wewe unaogopa kuzijua kwa sababu ya mali yako, kwa sababu ya majumba yako, sababu mkeo au mumeo hutaki aolewe au kuoa mtu mwengine, au pengine hutaki kuondoka kwa sababu ya watoto wako, ndio maana inakua shida hata kutolewa hiyo roho, umengangania hutaki kuondoka, unabururwa mpaka chini ya vitanda.
Lakini ukiridhia laa hakuna mashaka taratibu unavua guo lako la udongo halafu baada ya siku tatu huyoo unapaa kwenda Barzak bila ya matatizo, lakini wapi ukingangania (Riyal au Pound au Shilingi)zako inakua Mtihani, hata ukipewa dawa za usingizi hazifanyi kazi kwa sababu mbishi, hutaki kuondoka, lakini ukiwa Maridhia umetulia watu wanafanya kazi yao kwa urahisi bila ya vishindo. Sasa leo ntakupeni dalili mbili za upande wa Mawalii ili mzijue ukianza kuziona hizo jitaarishe, halafu nitaelekeza wasemavyo wanasayansi ili tupate kuchungulia inakuaje wakati wakutoka Roho.
Endelea Part 3
Sasa kwa kuwa hatujijui wewe ni nani?, ina tushinda pia kuelewa lini unaondoka, Lini utavua guo la udongo na ubaki wewe (Pure Soul), siku gani hiyo utakayo kaa pembeni ukashuhudia watu wanakosha Mwili wako ikisha hao wanauchukua kuupeleka makaburini, halafu wanautupa bila hata ya dua.
Ukiishi Maisha ya Kiroho siku hiyo ni Rahisi kwako kuijua, au kusikia hilo tangazo kabla ya miezi sita kufika, leo hapa nitakupa dalili mbili za (Mystic)Mawalii wengi ambao wanajua kama karibu kuondoka, ndio maana wengine wanaandika, wengine wanasema, wengine wanataarisha sanda zao kwa kujua safari ishawadia, wewe unaogopa kuzijua kwa sababu ya mali yako, kwa sababu ya majumba yako, sababu mkeo au mumeo hutaki aolewe au kuoa mtu mwengine, au pengine hutaki kuondoka kwa sababu ya watoto wako, ndio maana inakua shida hata kutolewa hiyo roho, umengangania hutaki kuondoka, unabururwa mpaka chini ya vitanda.
Lakini ukiridhia laa hakuna mashaka taratibu unavua guo lako la udongo halafu baada ya siku tatu huyoo unapaa kwenda Barzak bila ya matatizo, lakini wapi ukingangania (Riyal au Pound au Shilingi)zako inakua Mtihani, hata ukipewa dawa za usingizi hazifanyi kazi kwa sababu mbishi, hutaki kuondoka, lakini ukiwa Maridhia umetulia watu wanafanya kazi yao kwa urahisi bila ya vishindo. Sasa leo ntakupeni dalili mbili za upande wa Mawalii ili mzijue ukianza kuziona hizo jitaarishe, halafu nitaelekeza wasemavyo wanasayansi ili tupate kuchungulia inakuaje wakati wakutoka Roho.
Endelea Part 3
TANGAZO LA KIFO PART 3
Asalaam Aleiykum
Dalili mbili za (Mystic) ni Rahisi kuzijua kama wewe mfatiliaji, kwa lugha ya kawaida miezi sita kabla ya Kufa kwako inapatikana harufu kama vile ya mtoto anavoingia kwenye Baleghe yake, hiyo kwa lugha yako ya kawaida, Ama kwa lugha ya Kiwalii hua unaonekana Rangi au kama (Energy) Fulani inaanza kupanda juu mithili ya moshi au nuru isiyokua na taa inatoka katika Mwili wako.
Na dalili ya pili, nisije nikaisema mkaanza maradhi ya kujitizama, ndio maana tunaogopa kusema mengi ili tusikutieni ugonjwa wa wasiwasi. Dalili ya pili ni ile unaposhindwa kutizama ncha ya pua yako, ukiona unaumwa na huwezi kuangalia ncha ya pua yako basi jua safari tayari, furahi anza kujitaarisha, au ukiwa una mgonjwa mwambie atizame pua yake akiwa hawezi basi elewa safari haiko mbali, macho yanaangalia juu, yashakaa kwenye (Position)ya Umauti ndio maana utaona watu wote wakisha kufa mboni za macho zinabiruka na kuangalia Mbinguni. Nakufahamisheni mambo kama haya ili mpate kujiandaa, ndio maana hata mtu akilala ukifumbua mboni zake za macho utazikuta zinaangalia juu.
Japokua Dalili zinaweza kutafautiana baina ya mtu na mtu lakini wanasayansi wamegundua ule wakati wa mwisho wa masaa yalobaki sote tunapita katika njia moja ya kutoka Roho, Wengine wana bahatika kutokupata dalili zozote za umauti, lakini wengi wetu tunapata kujua harakati za vipi Roho inavotoka kama jicho la (Doctor)linavo hadithia Binaadamu anavokufa.
Tembelea link hiyo hapo chini ukasome mambo yanavokua wewe Mwenyewe.
https://mobile.nytimes.com/2017/06/20/well/live/the-symptoms-of-dying.amp.html
Nakutakia usomaji wa kufahamu.
Dalili mbili za (Mystic) ni Rahisi kuzijua kama wewe mfatiliaji, kwa lugha ya kawaida miezi sita kabla ya Kufa kwako inapatikana harufu kama vile ya mtoto anavoingia kwenye Baleghe yake, hiyo kwa lugha yako ya kawaida, Ama kwa lugha ya Kiwalii hua unaonekana Rangi au kama (Energy) Fulani inaanza kupanda juu mithili ya moshi au nuru isiyokua na taa inatoka katika Mwili wako.
Na dalili ya pili, nisije nikaisema mkaanza maradhi ya kujitizama, ndio maana tunaogopa kusema mengi ili tusikutieni ugonjwa wa wasiwasi. Dalili ya pili ni ile unaposhindwa kutizama ncha ya pua yako, ukiona unaumwa na huwezi kuangalia ncha ya pua yako basi jua safari tayari, furahi anza kujitaarisha, au ukiwa una mgonjwa mwambie atizame pua yake akiwa hawezi basi elewa safari haiko mbali, macho yanaangalia juu, yashakaa kwenye (Position)ya Umauti ndio maana utaona watu wote wakisha kufa mboni za macho zinabiruka na kuangalia Mbinguni. Nakufahamisheni mambo kama haya ili mpate kujiandaa, ndio maana hata mtu akilala ukifumbua mboni zake za macho utazikuta zinaangalia juu.
Japokua Dalili zinaweza kutafautiana baina ya mtu na mtu lakini wanasayansi wamegundua ule wakati wa mwisho wa masaa yalobaki sote tunapita katika njia moja ya kutoka Roho, Wengine wana bahatika kutokupata dalili zozote za umauti, lakini wengi wetu tunapata kujua harakati za vipi Roho inavotoka kama jicho la (Doctor)linavo hadithia Binaadamu anavokufa.
Tembelea link hiyo hapo chini ukasome mambo yanavokua wewe Mwenyewe.
https://mobile.nytimes.com/2017/06/20/well/live/the-symptoms-of-dying.amp.html
Nakutakia usomaji wa kufahamu.
Friday, July 14, 2017
BARAKA ZA UGANGA PART 1
Asalaam aleiykum
Moja kwa moja naanza na maswali yenu mengi kuhusu mimi kama mnavo niuliza jee wewe Mganga?.
Jawabu ndio Mimi mganga tena mkubwa ila tatizo langu sitibu mtu, najiganga mwenyewe, na watu wachache wale ninao waona kweli wanahitaji utibabu, tena nafanya bure kwa kuwa mie nimejua bure, lakini ukija na shida zako za mahitaji mimi ni ghali sana sio kunilipa tu bali hata kunipata nikakufanyia huo uganga.
Sasa tuingie kwenye darsa yetu ya baraka za uganga.
Kwanza kabisa kabla ya kukoga kwenye bahari hii ya Uganga nataka nikufahamishe ili upate kujua kuwa Mganga mkubwa wa nafsi na Roho yako ni Mwenyewe aliyoiumba Rabbil-Allahu(Mwenye enzi Mungu). Ukiweza kuwasiliana naye utakua huna haja ya Waganga wadogo wadogo wa Kidunia.
Sasa Mtu wa mwanzo kutujulisha siri hii ya Mganga Mkubwa ni Rafiki wa Mwenye enzi Mungu Nabii Ibrahim a.s aliposema kwenye Quraan sura ya Shuaraa aya ya 80 "وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ "
"Na ninapoumwa Yeye ndiye anayeniponesha".
mmetaka tuzungumze mambo ya Uganga Uganga sasa wacha tuweke wazi baadhi ya siri za Kiganga ambazo mlikua hamzijui, kwa hiyo kuanzia leo kumbuka ukenda Hospital au ukija kwangu sie sio tunayekuponesha, sisi sote tunataka Idhini ya Mganga Mkuu ambaye ni Mollah wetu.
Na lakushangaza zaidi ambalo watu wengi hawalifahamu au kujiuliza kwanini wakati mwingi inasisitizwa Mgonjwa lazima alale au anapewa dawa ya usingizi au anakua kalala?, hapo kuna siri kubwa inafaa uzamie ili kupata kuijua. Leo tumo ndani ya darsa ya uganga wacha tuendelee na mambo ya kiganga na hakuna Mganga aliyetuonesha fani ya utibabu wa hali ya juu kama Nabii Isa a.s (Jesus).(Quraan Al-Imran- 49)
وَرَسُولاً إِلَىٰ بَنِىٓ إِسۡرَٲٓءِيلَ أَنِّى قَدۡ جِئۡتُكُم بِـَٔايَةٍ۬ مِّن رَّبِّڪُمۡۖ أَنِّىٓ أَخۡلُقُ لَڪُم مِّنَ ٱلطِّينِ كَهَيۡـٴَـةِِ ٱلطَّيۡرِ فَأَنفُخُ فِيهِ فَيَكُونُ طَيۡرَۢا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُبۡرِئُ ٱلۡأَڪۡمَهَ وَٱلۡأَبۡرَصَ وَأُحۡىِ ٱلۡمَوۡتَىٰ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُنَبِّئُكُم بِمَا تَأۡكُلُونَ وَمَا تَدَّخِرُونَ فِى بُيُوتِڪُمۡۚ إِنَّ فِى ذَٲلِكَ لَأَيَةً۬ لَّكُمۡ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ
"Na (Atamfanya) Mtume kwa wana wa Israili(Na kuwaambia) Nimekujieni na hoja (Muujiza) kutoka kwa Mollah wenu, ya kwamba nakuumbieni katika udongo(Natengeneza mfano)kama sura ya ndege kisha nampuliza mara anakua ndege, kwa Idhini ya Mwenye enzi Mungu, Na ninawaponesha Vipofu na Wenye Mabalanga(Ukoma)Na Ninawafufua (baadhi ya )walokufa, kwa Idhini ya Mwenye enzi Mungu, Na Ntakwambieni mtakavyovila na mtakavyoweka akiba katika nyumba zenu, Bila shaka katika hayo imo hoja kwenu ikiwa nyinyi ni watu wa kuamini.
Naam Mambo makubwa usidhani huo ni uchawi, tungetaka mambo ya kichawi tungemtafuta nabii Musa a.s lakini tupo tunachambua mambo ya Kiganga na tuna hadithiwa habari hii na yule Mganga aloletwa na Mollah wetu ili kuja kutupa taarifa na maalumati hayo, basi kwa uchambuzi zaidi endelea part 2.
Moja kwa moja naanza na maswali yenu mengi kuhusu mimi kama mnavo niuliza jee wewe Mganga?.
Jawabu ndio Mimi mganga tena mkubwa ila tatizo langu sitibu mtu, najiganga mwenyewe, na watu wachache wale ninao waona kweli wanahitaji utibabu, tena nafanya bure kwa kuwa mie nimejua bure, lakini ukija na shida zako za mahitaji mimi ni ghali sana sio kunilipa tu bali hata kunipata nikakufanyia huo uganga.
Sasa tuingie kwenye darsa yetu ya baraka za uganga.
Kwanza kabisa kabla ya kukoga kwenye bahari hii ya Uganga nataka nikufahamishe ili upate kujua kuwa Mganga mkubwa wa nafsi na Roho yako ni Mwenyewe aliyoiumba Rabbil-Allahu(Mwenye enzi Mungu). Ukiweza kuwasiliana naye utakua huna haja ya Waganga wadogo wadogo wa Kidunia.
Sasa Mtu wa mwanzo kutujulisha siri hii ya Mganga Mkubwa ni Rafiki wa Mwenye enzi Mungu Nabii Ibrahim a.s aliposema kwenye Quraan sura ya Shuaraa aya ya 80 "وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ "
"Na ninapoumwa Yeye ndiye anayeniponesha".
mmetaka tuzungumze mambo ya Uganga Uganga sasa wacha tuweke wazi baadhi ya siri za Kiganga ambazo mlikua hamzijui, kwa hiyo kuanzia leo kumbuka ukenda Hospital au ukija kwangu sie sio tunayekuponesha, sisi sote tunataka Idhini ya Mganga Mkuu ambaye ni Mollah wetu.
Na lakushangaza zaidi ambalo watu wengi hawalifahamu au kujiuliza kwanini wakati mwingi inasisitizwa Mgonjwa lazima alale au anapewa dawa ya usingizi au anakua kalala?, hapo kuna siri kubwa inafaa uzamie ili kupata kuijua. Leo tumo ndani ya darsa ya uganga wacha tuendelee na mambo ya kiganga na hakuna Mganga aliyetuonesha fani ya utibabu wa hali ya juu kama Nabii Isa a.s (Jesus).(Quraan Al-Imran- 49)
وَرَسُولاً إِلَىٰ بَنِىٓ إِسۡرَٲٓءِيلَ أَنِّى قَدۡ جِئۡتُكُم بِـَٔايَةٍ۬ مِّن رَّبِّڪُمۡۖ أَنِّىٓ أَخۡلُقُ لَڪُم مِّنَ ٱلطِّينِ كَهَيۡـٴَـةِِ ٱلطَّيۡرِ فَأَنفُخُ فِيهِ فَيَكُونُ طَيۡرَۢا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُبۡرِئُ ٱلۡأَڪۡمَهَ وَٱلۡأَبۡرَصَ وَأُحۡىِ ٱلۡمَوۡتَىٰ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُنَبِّئُكُم بِمَا تَأۡكُلُونَ وَمَا تَدَّخِرُونَ فِى بُيُوتِڪُمۡۚ إِنَّ فِى ذَٲلِكَ لَأَيَةً۬ لَّكُمۡ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ
"Na (Atamfanya) Mtume kwa wana wa Israili(Na kuwaambia) Nimekujieni na hoja (Muujiza) kutoka kwa Mollah wenu, ya kwamba nakuumbieni katika udongo(Natengeneza mfano)kama sura ya ndege kisha nampuliza mara anakua ndege, kwa Idhini ya Mwenye enzi Mungu, Na ninawaponesha Vipofu na Wenye Mabalanga(Ukoma)Na Ninawafufua (baadhi ya )walokufa, kwa Idhini ya Mwenye enzi Mungu, Na Ntakwambieni mtakavyovila na mtakavyoweka akiba katika nyumba zenu, Bila shaka katika hayo imo hoja kwenu ikiwa nyinyi ni watu wa kuamini.
Naam Mambo makubwa usidhani huo ni uchawi, tungetaka mambo ya kichawi tungemtafuta nabii Musa a.s lakini tupo tunachambua mambo ya Kiganga na tuna hadithiwa habari hii na yule Mganga aloletwa na Mollah wetu ili kuja kutupa taarifa na maalumati hayo, basi kwa uchambuzi zaidi endelea part 2.
BARAKA ZA UGANGA PART 2
Asalaam Aleiykum
Nabii Isa a.s kaja na mambo manne(4) Jambo la kwanza(1) kumtengeneza ndege kwa udongo ikisha akampuliza ndege huyo akaruka, kumbuka huo si uchawi kama vile (Magician)wanavo kutolea njiwa kwenye kofia. Halafu jambo la pili(2)Anaponesha Vipofu na wenye Ukoma. Jambo la tatu (3) Akawafufua baadhi ya walokufa. Na hilo la Nne (4)Ntakwambieni mtakavyokula na mtakavyo weka Akiba.
Hapo kuna mambo yanafaa kuzingatiwa wakati ukiendelea na darsa hii, katika hayo mambo manne tumefanikiwa kuyapata mawili tu nayo ni namba (2) na Namba (4), Nitayataja haya mawili tukiwa tunaendelea na darsa hii. Napenda Uelewe Uganga umegawika mapande mawili yenye sehemu mbili, Kama alivotuonesha Nabii Isa a.s hapo juu kuwa Uganga una sehemu ya (Body)yaani(Physical) hii unatibu kwa kutumia dawa za kienyeji na za kisasa na Una sehemu ya Roho nayo ni hiyo (Spiritual) hiyo tiba yake ni ya maombi na mambo mengine ya (Mystical), Wenzetu wa (Western)wamefanya jitihada kwenye utafiti wa (Physical)mpaka wamefanikiwa kuponesha maradhi mengi yakiwemo hayo ya ukoma na mpaka sasa wanajitahidi katika fani ya macho ili kuponesha upofu.
Na upande wa pili wa (Eastern)hapo zamani walikua wako (advance)katika mambo ya utibabu wa Kiroho na Kimwili lakini yalotokezea katika (History)ndio yalofanya mpaka leo hatujaendelea katika fani zote mbili isipokua kwa watu wachache sana walo bahatika au kubarikiwa.
Sasa nini Uganga?.
Kwa Mfano wa kwanza Uganga ni Baraka (Blessing)za Mollah wako unazopewa kuwatibu viumbe wenzio kama alivopewa Nabii Isa a.s, lakini Nabii Isa yeye alikua Mtume, na Uganga ni kama wakala, Ima uwe wa kusomea au wa kushushiwa na Mollah wako. Wakala huyo au Mganga ukenda kwake na shida zako au dhiki yako, au Maradhi yanayokusumbua basi atafanya elimu aliyojaaliwa na wewe kupona au kufanikiwa, au dhiki kukuondoka kwa njia usizozijua.
vipi anafanya endelea part 3.
Nabii Isa a.s kaja na mambo manne(4) Jambo la kwanza(1) kumtengeneza ndege kwa udongo ikisha akampuliza ndege huyo akaruka, kumbuka huo si uchawi kama vile (Magician)wanavo kutolea njiwa kwenye kofia. Halafu jambo la pili(2)Anaponesha Vipofu na wenye Ukoma. Jambo la tatu (3) Akawafufua baadhi ya walokufa. Na hilo la Nne (4)Ntakwambieni mtakavyokula na mtakavyo weka Akiba.
Hapo kuna mambo yanafaa kuzingatiwa wakati ukiendelea na darsa hii, katika hayo mambo manne tumefanikiwa kuyapata mawili tu nayo ni namba (2) na Namba (4), Nitayataja haya mawili tukiwa tunaendelea na darsa hii. Napenda Uelewe Uganga umegawika mapande mawili yenye sehemu mbili, Kama alivotuonesha Nabii Isa a.s hapo juu kuwa Uganga una sehemu ya (Body)yaani(Physical) hii unatibu kwa kutumia dawa za kienyeji na za kisasa na Una sehemu ya Roho nayo ni hiyo (Spiritual) hiyo tiba yake ni ya maombi na mambo mengine ya (Mystical), Wenzetu wa (Western)wamefanya jitihada kwenye utafiti wa (Physical)mpaka wamefanikiwa kuponesha maradhi mengi yakiwemo hayo ya ukoma na mpaka sasa wanajitahidi katika fani ya macho ili kuponesha upofu.
Na upande wa pili wa (Eastern)hapo zamani walikua wako (advance)katika mambo ya utibabu wa Kiroho na Kimwili lakini yalotokezea katika (History)ndio yalofanya mpaka leo hatujaendelea katika fani zote mbili isipokua kwa watu wachache sana walo bahatika au kubarikiwa.
Sasa nini Uganga?.
Kwa Mfano wa kwanza Uganga ni Baraka (Blessing)za Mollah wako unazopewa kuwatibu viumbe wenzio kama alivopewa Nabii Isa a.s, lakini Nabii Isa yeye alikua Mtume, na Uganga ni kama wakala, Ima uwe wa kusomea au wa kushushiwa na Mollah wako. Wakala huyo au Mganga ukenda kwake na shida zako au dhiki yako, au Maradhi yanayokusumbua basi atafanya elimu aliyojaaliwa na wewe kupona au kufanikiwa, au dhiki kukuondoka kwa njia usizozijua.
vipi anafanya endelea part 3.
BARAKA ZA UGANGA PART 3
Asalaam Aleiykum
Kabla ya kumjua vipi anafanya kwanza lazima uzijue sifa zake za kuwa huyu kweli ni mganga. Ama wale wa kidunia wao wanaweka matangazo na vyeti vyao, na wapi wamesoma na wamesomea nini, sasa huyu wa mambo ya kiroho utamgundua vipi na yeye hana cheti.
Vipi utamjua kama yeye ni Wakala wa Mwenye enzi Mungu, anazo Baraka kutoka kwa Mollah wake?. Jambo la kwanza kukujulisha ni Ucha Mungu wake, jambo la pili si mwenye kutaka sifa, jambo la tatu hana tamaa, hachukui pesa abadan, hata ukimpa hiyo ni hiyari yako, ukimpa kingi ni mafanikio yako ya haraka, na ukimpa kidogo na wewe mahitajio yako yatapatikana kidogo kidogo, huyo ndio mganga wa aina ya kwanza huyu yeye akinyanyua mikono dua yake hairudi, huyo ndio alopewa Baraka zitokazo kwa Mollah wake.
Ama Mganga wa aina ya pili ni yule mwenye kuijua au ku (Penetrate Third Eye) Nini kitakujulisha hiyo (Third Eye) hiyo ni (Sipiritual Eye) iliyopo Baina ya Macho yako mawili kati kati ya kipaji cha uso wako, kama uko Tanzania watizame Wagogo wanapo chanja, wao wanachanja hawajui maana yake wanasema inatibu maradhi, lakini kwa kujua zaidi watizame Mabaniani pale wanapotia alama zao kwenye paji la uso, hapo ndani yake ndio kuna hiyo (Third eye).
Hiyo (Third eye) ni jicho la Roho ambalo linakufanya uone mambo yalofichika katika Ulimwengu huu, lakini huwezi kuona hayo mambo mpaka ufunguliwe hilo jicho na Mtu anaefahamu elimu hizo, au lifunguke kwa Baraka za Mollah wako. Nini kinatokea Jicho likifunguka?, kwanza napenda uelewe vishindo vyake vikubwa, unaweza kudhani unapata wazimu, au kichwa kinangoka, au mfano kama vile unatumbukia kwenye shimo lisilokuwa na mwisho. Likifunguka jicho hilo unaona mambo ya ajabu, huoni tena kwa kawaida, miti unaona vyengine, kila kitu hutokiona kama mwanzo unavo viona, hapo tena kwa uwezo wa kuona mambo utaweza kuwa mtabiri, mtu akija na maradhi yake unaona kama (X-ray). Ndio maana ukenda kwa watu wengine wanakwambia wewe una jinsi kadhaa wa kadhaa, jua huyo anaona mambo (Live).
Hapo ndio unapata hiyo (Power) ya Uganga, unapata nguvu za kufanya mambo, unaweza kutumia kwa njia ya kheri ama ya shari, shauri linakua lako mwenyewe, unapata kuzijua dawa za ajabu, na unaweza kufanya mambo ya ajabu, ukazuia meli isiondoke, ukaharibu gari isiendeshwe,unaweza kudhuru watu, unaweza kuona viumbe vya ajabu ambavyo watu wengine hawavioni, unaweza kubadilisha matukio kutokana na huu uwezo wa (Third eye).huyo ndio Mganga wa aina ya pili.,
Halafu kuna Waganga wa aina ya Tatu, ambao wao wana uganga wa uongo, uganga wa kubahatisha, uganga wa nujum, uganga wa uramali, uganga wa Ramli, uganga wa (Numerology),uganga wa kutizama na kuisoma mikono ya watu. Mambo yao yote ya kubahatisha bahatisha, wakichangaya na miti shamba wanakwambia wao waganga, lakini hawana lolote isipokua mambo ya Uongo. Kwa hiyo namalizia kwa kusisitiza wanoweza kukusaidieni ni huyo wa kwanza na wapili kwa njia za halali na wala hakuna tatizo lolote, na hizo ndio Baraka za uganga mnazo niuliza kutaka kuzijua.
Kabla ya kumjua vipi anafanya kwanza lazima uzijue sifa zake za kuwa huyu kweli ni mganga. Ama wale wa kidunia wao wanaweka matangazo na vyeti vyao, na wapi wamesoma na wamesomea nini, sasa huyu wa mambo ya kiroho utamgundua vipi na yeye hana cheti.
Vipi utamjua kama yeye ni Wakala wa Mwenye enzi Mungu, anazo Baraka kutoka kwa Mollah wake?. Jambo la kwanza kukujulisha ni Ucha Mungu wake, jambo la pili si mwenye kutaka sifa, jambo la tatu hana tamaa, hachukui pesa abadan, hata ukimpa hiyo ni hiyari yako, ukimpa kingi ni mafanikio yako ya haraka, na ukimpa kidogo na wewe mahitajio yako yatapatikana kidogo kidogo, huyo ndio mganga wa aina ya kwanza huyu yeye akinyanyua mikono dua yake hairudi, huyo ndio alopewa Baraka zitokazo kwa Mollah wake.
Ama Mganga wa aina ya pili ni yule mwenye kuijua au ku (Penetrate Third Eye) Nini kitakujulisha hiyo (Third Eye) hiyo ni (Sipiritual Eye) iliyopo Baina ya Macho yako mawili kati kati ya kipaji cha uso wako, kama uko Tanzania watizame Wagogo wanapo chanja, wao wanachanja hawajui maana yake wanasema inatibu maradhi, lakini kwa kujua zaidi watizame Mabaniani pale wanapotia alama zao kwenye paji la uso, hapo ndani yake ndio kuna hiyo (Third eye).
Hiyo (Third eye) ni jicho la Roho ambalo linakufanya uone mambo yalofichika katika Ulimwengu huu, lakini huwezi kuona hayo mambo mpaka ufunguliwe hilo jicho na Mtu anaefahamu elimu hizo, au lifunguke kwa Baraka za Mollah wako. Nini kinatokea Jicho likifunguka?, kwanza napenda uelewe vishindo vyake vikubwa, unaweza kudhani unapata wazimu, au kichwa kinangoka, au mfano kama vile unatumbukia kwenye shimo lisilokuwa na mwisho. Likifunguka jicho hilo unaona mambo ya ajabu, huoni tena kwa kawaida, miti unaona vyengine, kila kitu hutokiona kama mwanzo unavo viona, hapo tena kwa uwezo wa kuona mambo utaweza kuwa mtabiri, mtu akija na maradhi yake unaona kama (X-ray). Ndio maana ukenda kwa watu wengine wanakwambia wewe una jinsi kadhaa wa kadhaa, jua huyo anaona mambo (Live).
Hapo ndio unapata hiyo (Power) ya Uganga, unapata nguvu za kufanya mambo, unaweza kutumia kwa njia ya kheri ama ya shari, shauri linakua lako mwenyewe, unapata kuzijua dawa za ajabu, na unaweza kufanya mambo ya ajabu, ukazuia meli isiondoke, ukaharibu gari isiendeshwe,unaweza kudhuru watu, unaweza kuona viumbe vya ajabu ambavyo watu wengine hawavioni, unaweza kubadilisha matukio kutokana na huu uwezo wa (Third eye).huyo ndio Mganga wa aina ya pili.,
Halafu kuna Waganga wa aina ya Tatu, ambao wao wana uganga wa uongo, uganga wa kubahatisha, uganga wa nujum, uganga wa uramali, uganga wa Ramli, uganga wa (Numerology),uganga wa kutizama na kuisoma mikono ya watu. Mambo yao yote ya kubahatisha bahatisha, wakichangaya na miti shamba wanakwambia wao waganga, lakini hawana lolote isipokua mambo ya Uongo. Kwa hiyo namalizia kwa kusisitiza wanoweza kukusaidieni ni huyo wa kwanza na wapili kwa njia za halali na wala hakuna tatizo lolote, na hizo ndio Baraka za uganga mnazo niuliza kutaka kuzijua.
Monday, May 22, 2017
MAFUNDISHO YA TAQWA PART 1
Asalaam Aleiykum
Nianze kwa kusema kwa anayejua atacheka sana akisikia eti (Taqwa)ina mafundisho, Lakini inabidi tuseme hivyo kwa ajili ya wale wasoijua, Kwa wale wenye kujua wanaelewa Taqwa haina haja ya mafundisho, Kwa sababu hakuna yoyote Mwenye kufundishwa Mapenzi. Lakini huruma ziwafikie wale ambao hawajawahi kupenda, au kufikia daraja hiyo ya Mapenzi ya Taqwa, hawa wanahitaji muongozo, wanataka kujua wakifika kwenye hilo daraja wafanye nini?. wana wasiwasi labda itakuaje, huwezi kuwalaumu kutokana na wasiwasi huo kwa sababu katika hali ya kawaida wanaogopa kupenda, Nini habari yetu sisi wakiingia kwenye Mapenzi ya Mwenye Enzi mungu itakuaje, wengine wanaamua kujiua, wengine wanaihama dunia, wengine wanapoteza akili kwenye mapenzi haya.
Utaona kuna siri kubwa ya kuyakwepa Mapenzi haya kwa njia za kutafuta ulevi wowote ule, wengine wanasema hakuna chochote, lakini ndani ya nafsi kuna shaka inabakia ya kiu cha kutaka kujua Mapenzi haya ya aina gani?, jee haya maisha yana mwisho au yanaendelea?, Napenda ukumbuke (Kiu)Ulonayo na dhiki ya maisha haviondoki mpaka uyapate Mapenzi ya Mwenye enzi Mungu. Nataka pia uelewe sio hujayapata, unayo lakini bado huyajui.
Najua tunajiuliza siku zote haya mapenzi yanatokea wapi?. Jawabu itabidi ujitizame Mwenyewe, pale unapokua huna dhiki, huna magonjwa, uko safi utagundua kwamba wewe una vipande vipande vya mapenzi, mara unapenda Mwanamke au Mwanamme, mara unapenda gari, halafu huyo unapenda shamba lako, na mara unapenda watoto wako, Jee ushawahi kujiuliza yanatokea wapi mapenzi haya?, Umeshawahi kwanini unachukia kufa?, Jee huijui kama hiyo ndio (Nature) yako, Quraan inasemaje kuhusu jambo hili la mapenzi. (Aya ya 14 Al-Imran).
زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ ٱلشَّهَوَٲتِ مِنَ ٱلنِّسَآءِ وَٱلۡبَنِينَ وَٱلۡقَنَـٰطِيرِ ٱلۡمُقَنطَرَةِ مِنَ ٱلذَّهَبِ وَٱلۡفِضَّةِ وَٱلۡخَيۡلِ ٱلۡمُسَوَّمَةِ وَٱلۡأَنۡعَـٰمِ وَٱلۡحَرۡثِۗ ذَٲلِكَ مَتَـٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَٱللَّهُ عِندَهُ ۥ حُسۡنُ ٱلۡمَـَٔابِ
Watu wametiwa huba ya kupenda Wanawake na watoto na (wingi)mirundi ya dhahabu na fedha, na farasi wanotunzwa vizuri, na wanyama na mashamba, Na hayo ni matumizi ya maisha katika dunia, Na Kwa Mwenye enzi Mungu ndiko kwenye marejeo mazuri.
Sasa ukisha kulijua hilo nakurejesha kwenye aya ya (183)iliyomo ndani ya sura ya (Bakarah) inayosema Melazimishwa kufunga ili mpate kumcha Mungu, Hapo nakuomba uitizame aya kwa undani, usipite juu juu utakua huipati maana yake, na hapo ndipo wengi wetu tunashindwa kufafanua tafauti na kusudio la aya hii. Sasa pata nafasi ya kuijua maana yake halisi, ijue siri iliyopo hapo upate kuitumia kama utakavo ifahamu.
Nakukumbusha kwamba aya imesema ili upate kumcha Mollah wako, au kwa lugha nyengine yapate mapenzi kwa ukamilifu (Higher love)unakumbuka kule ulikua na vipande vipande huku kama utafunga kwa Imani na ukawa (Total)ume (Surrender) ndio unaipata hiyo Taqwa au (Mapenzi ya Mwenye enzi Mungu).
Napenda ukumbuke aya haikutaja ulishe mayatima, wala kutoa sadaka, hukuambiwa ufanye hisan kwa yoyote yule ila umeambiwa upate kumcha Mollah wako(seek the love of your god). Jee unaijua maana ya Kumcha Mungu?, Basi kama huijui tuliza fikra zako ili upate kuijua maana ya kumcha Mungu. Halina maana nyengine neno hili ila kulipa hadhi ya mapenzi, lakini kwa kuwa katika hali ya kawaida hatuyajui mapenzi ni nini, ni bora tuliache pembeni neno hili ili twende kuitafuta maana ndani ya mwezi huu wa Ramadhan.
Tunafundishwa maana halisi ya Mwezi huu wa Ramadhan ni kuufanya ni (Special)kwa ajili ya Mollah wetu, Ni kwa ajili ya kutafuta mapenzi ya Mollah wetu, kugundua utukufu wa yule alotuumba, kuzitafuta Radhi zake, Kuelekeza Fikra, mawazo, maswali yote kwa ajili ya kumjua Mollah wako, kuna msemo unasema (Gonga utafunguliwa), kumuomba atuwezeshe kuyapata mambo manne muhimu yaliyomo ndani ya hiyo Taqwa katika Mwezi huu wa Ramadhan, Mambo yenyewe yepi yaliyomo ndani ya mwezi huu?.
Endelea part 2
Nianze kwa kusema kwa anayejua atacheka sana akisikia eti (Taqwa)ina mafundisho, Lakini inabidi tuseme hivyo kwa ajili ya wale wasoijua, Kwa wale wenye kujua wanaelewa Taqwa haina haja ya mafundisho, Kwa sababu hakuna yoyote Mwenye kufundishwa Mapenzi. Lakini huruma ziwafikie wale ambao hawajawahi kupenda, au kufikia daraja hiyo ya Mapenzi ya Taqwa, hawa wanahitaji muongozo, wanataka kujua wakifika kwenye hilo daraja wafanye nini?. wana wasiwasi labda itakuaje, huwezi kuwalaumu kutokana na wasiwasi huo kwa sababu katika hali ya kawaida wanaogopa kupenda, Nini habari yetu sisi wakiingia kwenye Mapenzi ya Mwenye Enzi mungu itakuaje, wengine wanaamua kujiua, wengine wanaihama dunia, wengine wanapoteza akili kwenye mapenzi haya.
Utaona kuna siri kubwa ya kuyakwepa Mapenzi haya kwa njia za kutafuta ulevi wowote ule, wengine wanasema hakuna chochote, lakini ndani ya nafsi kuna shaka inabakia ya kiu cha kutaka kujua Mapenzi haya ya aina gani?, jee haya maisha yana mwisho au yanaendelea?, Napenda ukumbuke (Kiu)Ulonayo na dhiki ya maisha haviondoki mpaka uyapate Mapenzi ya Mwenye enzi Mungu. Nataka pia uelewe sio hujayapata, unayo lakini bado huyajui.
Najua tunajiuliza siku zote haya mapenzi yanatokea wapi?. Jawabu itabidi ujitizame Mwenyewe, pale unapokua huna dhiki, huna magonjwa, uko safi utagundua kwamba wewe una vipande vipande vya mapenzi, mara unapenda Mwanamke au Mwanamme, mara unapenda gari, halafu huyo unapenda shamba lako, na mara unapenda watoto wako, Jee ushawahi kujiuliza yanatokea wapi mapenzi haya?, Umeshawahi kwanini unachukia kufa?, Jee huijui kama hiyo ndio (Nature) yako, Quraan inasemaje kuhusu jambo hili la mapenzi. (Aya ya 14 Al-Imran).
زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ ٱلشَّهَوَٲتِ مِنَ ٱلنِّسَآءِ وَٱلۡبَنِينَ وَٱلۡقَنَـٰطِيرِ ٱلۡمُقَنطَرَةِ مِنَ ٱلذَّهَبِ وَٱلۡفِضَّةِ وَٱلۡخَيۡلِ ٱلۡمُسَوَّمَةِ وَٱلۡأَنۡعَـٰمِ وَٱلۡحَرۡثِۗ ذَٲلِكَ مَتَـٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَٱللَّهُ عِندَهُ ۥ حُسۡنُ ٱلۡمَـَٔابِ
Watu wametiwa huba ya kupenda Wanawake na watoto na (wingi)mirundi ya dhahabu na fedha, na farasi wanotunzwa vizuri, na wanyama na mashamba, Na hayo ni matumizi ya maisha katika dunia, Na Kwa Mwenye enzi Mungu ndiko kwenye marejeo mazuri.
Sasa ukisha kulijua hilo nakurejesha kwenye aya ya (183)iliyomo ndani ya sura ya (Bakarah) inayosema Melazimishwa kufunga ili mpate kumcha Mungu, Hapo nakuomba uitizame aya kwa undani, usipite juu juu utakua huipati maana yake, na hapo ndipo wengi wetu tunashindwa kufafanua tafauti na kusudio la aya hii. Sasa pata nafasi ya kuijua maana yake halisi, ijue siri iliyopo hapo upate kuitumia kama utakavo ifahamu.
Nakukumbusha kwamba aya imesema ili upate kumcha Mollah wako, au kwa lugha nyengine yapate mapenzi kwa ukamilifu (Higher love)unakumbuka kule ulikua na vipande vipande huku kama utafunga kwa Imani na ukawa (Total)ume (Surrender) ndio unaipata hiyo Taqwa au (Mapenzi ya Mwenye enzi Mungu).
Napenda ukumbuke aya haikutaja ulishe mayatima, wala kutoa sadaka, hukuambiwa ufanye hisan kwa yoyote yule ila umeambiwa upate kumcha Mollah wako(seek the love of your god). Jee unaijua maana ya Kumcha Mungu?, Basi kama huijui tuliza fikra zako ili upate kuijua maana ya kumcha Mungu. Halina maana nyengine neno hili ila kulipa hadhi ya mapenzi, lakini kwa kuwa katika hali ya kawaida hatuyajui mapenzi ni nini, ni bora tuliache pembeni neno hili ili twende kuitafuta maana ndani ya mwezi huu wa Ramadhan.
Tunafundishwa maana halisi ya Mwezi huu wa Ramadhan ni kuufanya ni (Special)kwa ajili ya Mollah wetu, Ni kwa ajili ya kutafuta mapenzi ya Mollah wetu, kugundua utukufu wa yule alotuumba, kuzitafuta Radhi zake, Kuelekeza Fikra, mawazo, maswali yote kwa ajili ya kumjua Mollah wako, kuna msemo unasema (Gonga utafunguliwa), kumuomba atuwezeshe kuyapata mambo manne muhimu yaliyomo ndani ya hiyo Taqwa katika Mwezi huu wa Ramadhan, Mambo yenyewe yepi yaliyomo ndani ya mwezi huu?.
Endelea part 2
MAFUNDISHO YA TAQWA PART 2
Asalaam Aleiykum
Mambo hayo Manne yaliyomo ndani ya hiyo Taqwa ndio yatakusaidia kuyapata mapenzi ya Mwenye enzi Mungu, Na ukipata Mapenzi ya Allah hakika wewe umefanikiwa katika mafanikio yasio na mfano. Umo ndani ya ustaadh wa kulea Roho, jambo la mwanzo(1) kabisa ambalo ndio muhimu lenye kukutia au kukuletea hayo mapenzi ni hiyo "Shahada yako" Ya kumshuhudia Mollah wako ni Mmoja wala hana mshirika, Shahada hii daima unaitamka mdomoni(Lip sevice) inakua si lolote si chochote juu yako.
Sasa umo ndani ya Ustaadh wa kulea Roho na wewe unayataka mapenzi ya Mollah wako inabidi uende (Deep)ndio maana ya Ramadhan. Utakapoulizwa una shuhudia nini? ujue cha kujibu, usiwe unatoa macho huna cha kusema, sasa twende mimi na wewe tukatafute jawabu, vipi utalijibu swali hili ni lazima lihusiane na Roho yako na sio ulimi, vipi utaipata Shahada anza japo na Miti, anza kutafakari(Kwani maneno haya si yamesemwa ndani ya sura ya Ghashiyah 17-20)"Hawatazami jinsi ngamia walivoumbwa""Na Mbingu jinsi zilivyo inuliwa""Na Milima ilivyo thubutishwa""Na Ardhi Jinsi ilivyotandazwa", basi kama hivyo vitakua mbali ndio nimeanza na miti, tafakari kwa kujua kumbe hii miti inavuta pumzi kama ninavo vuta mimi, mimi natoa (Carbon dioxide) miti inaivuta ndani na kunitolea mimi (Oxygen)na mimi huyo navuta pumzi.
Pata kujua kwanini ukiona Rangi za kijani unajisikia (Fresh), jishughulishe uelewe kwanini kila ukenda Baharini unajisikia furaha, pata fahamu Jua lina mahusiano gani na mimi, Angalia wanyama mbona wana (System)kama mimi?, wanalala, wanakula, na ukifika muda wao wanakufa.
Fikiria pia kilichomo kwenye majani, na kwenye ardhi, na katika nyota pia kimo katika nafsi yangu, ukikaa ukafikiria japo muandamo wa mwezi na siku zake 28 basi kuna kitu ndani ya moyo wako kitakujulisha nini maana ya Mungu mmoja, au nini maana ya Shahada na wapi mapenzi yanapotokea, Na itakapotokea hali kama hiyo wewe Mwenyewe utagundua kumbe hii ndio taqwa, na hii ndio hiyo Rehma ninayo ambiwa, hapo ndio utapata nafasi ya kuliendea jambo la pili (2).
Nini hilo jambo la Pili ?.
Baada ya kuujuwa Uwezo wa Mwenye enzi Mungu na Ufalme wake, hapo tena kwa mapenzi ya hali ya juu unaanza kuomba (Mghfira)ita upendavyo(Kumi la pili)au Msamaha, unaomba msamaha huo kwa mara zisizo na idadi, usije ukadhani samahani yenye kutoka katika hali ya Taqwa ni kama ile yako ya kawaida ilojaa kiburi, unajiona ushaacha madhanbi na uko msikitini, au unafanya mema, Msamaha wa Taqwa ni ule wa (Realization)Msamaha wa kujua kwa yakini kumbe mimi nilokua na mkosea yupo, naye ndiye aliyeniumba akanipa uhai huu, Namuasi yule ambaye katika Ufalme wake kakidhibiti kila kitu pasi kuwa na mshirika, Huyu ndie Mollah wangu anayeniruzuku kila siku hata wakati ule nafanya maasi, Yeye ndie Mwenye kunipa Furaha kila niipatapo dhiki, Ananipa usingizi na Kuniamsha kila siku ya uhai wangu. Basi Mimi Mollah wangu sina cha kuomba mbele yako, na wala sistahiki chengine chochote isipokua Faraja ya Msamaha wako, na hakuna Msamaha utakao nipa mimi ila niyapate mapenzi yako ndani ya Mwezi huu wa na daima katika uhai wangu.
endelea part 3.
Mambo hayo Manne yaliyomo ndani ya hiyo Taqwa ndio yatakusaidia kuyapata mapenzi ya Mwenye enzi Mungu, Na ukipata Mapenzi ya Allah hakika wewe umefanikiwa katika mafanikio yasio na mfano. Umo ndani ya ustaadh wa kulea Roho, jambo la mwanzo(1) kabisa ambalo ndio muhimu lenye kukutia au kukuletea hayo mapenzi ni hiyo "Shahada yako" Ya kumshuhudia Mollah wako ni Mmoja wala hana mshirika, Shahada hii daima unaitamka mdomoni(Lip sevice) inakua si lolote si chochote juu yako.
Sasa umo ndani ya Ustaadh wa kulea Roho na wewe unayataka mapenzi ya Mollah wako inabidi uende (Deep)ndio maana ya Ramadhan. Utakapoulizwa una shuhudia nini? ujue cha kujibu, usiwe unatoa macho huna cha kusema, sasa twende mimi na wewe tukatafute jawabu, vipi utalijibu swali hili ni lazima lihusiane na Roho yako na sio ulimi, vipi utaipata Shahada anza japo na Miti, anza kutafakari(Kwani maneno haya si yamesemwa ndani ya sura ya Ghashiyah 17-20)"Hawatazami jinsi ngamia walivoumbwa""Na Mbingu jinsi zilivyo inuliwa""Na Milima ilivyo thubutishwa""Na Ardhi Jinsi ilivyotandazwa", basi kama hivyo vitakua mbali ndio nimeanza na miti, tafakari kwa kujua kumbe hii miti inavuta pumzi kama ninavo vuta mimi, mimi natoa (Carbon dioxide) miti inaivuta ndani na kunitolea mimi (Oxygen)na mimi huyo navuta pumzi.
Pata kujua kwanini ukiona Rangi za kijani unajisikia (Fresh), jishughulishe uelewe kwanini kila ukenda Baharini unajisikia furaha, pata fahamu Jua lina mahusiano gani na mimi, Angalia wanyama mbona wana (System)kama mimi?, wanalala, wanakula, na ukifika muda wao wanakufa.
Fikiria pia kilichomo kwenye majani, na kwenye ardhi, na katika nyota pia kimo katika nafsi yangu, ukikaa ukafikiria japo muandamo wa mwezi na siku zake 28 basi kuna kitu ndani ya moyo wako kitakujulisha nini maana ya Mungu mmoja, au nini maana ya Shahada na wapi mapenzi yanapotokea, Na itakapotokea hali kama hiyo wewe Mwenyewe utagundua kumbe hii ndio taqwa, na hii ndio hiyo Rehma ninayo ambiwa, hapo ndio utapata nafasi ya kuliendea jambo la pili (2).
Nini hilo jambo la Pili ?.
Baada ya kuujuwa Uwezo wa Mwenye enzi Mungu na Ufalme wake, hapo tena kwa mapenzi ya hali ya juu unaanza kuomba (Mghfira)ita upendavyo(Kumi la pili)au Msamaha, unaomba msamaha huo kwa mara zisizo na idadi, usije ukadhani samahani yenye kutoka katika hali ya Taqwa ni kama ile yako ya kawaida ilojaa kiburi, unajiona ushaacha madhanbi na uko msikitini, au unafanya mema, Msamaha wa Taqwa ni ule wa (Realization)Msamaha wa kujua kwa yakini kumbe mimi nilokua na mkosea yupo, naye ndiye aliyeniumba akanipa uhai huu, Namuasi yule ambaye katika Ufalme wake kakidhibiti kila kitu pasi kuwa na mshirika, Huyu ndie Mollah wangu anayeniruzuku kila siku hata wakati ule nafanya maasi, Yeye ndie Mwenye kunipa Furaha kila niipatapo dhiki, Ananipa usingizi na Kuniamsha kila siku ya uhai wangu. Basi Mimi Mollah wangu sina cha kuomba mbele yako, na wala sistahiki chengine chochote isipokua Faraja ya Msamaha wako, na hakuna Msamaha utakao nipa mimi ila niyapate mapenzi yako ndani ya Mwezi huu wa na daima katika uhai wangu.
endelea part 3.
MAFUNDISHO YA TAQWA PART 3
Asalaam Aleiykum
Hapo utakua tayari kuliingia jambo la tatu(3) ambalo ni kumuomba Mollah wako (Pepo yake). Unapotajiwa pepo akili yako mbio inakimbilia kwenye jumba la ghorofa na mto(River)inapita mbele, basi umemaliza. Lakini Jambo unalo ahidiwa na Mwenye enzi Mungu elewa halina mfano, ikiwa haya maisha ya dunia katika huu (Uhai)ulopewa unaupenda hali hii, ukiambiwa sasa wakati wako ushafika wa kurudi Akhera unakua na huzuni kubwa, hutaki kwenda, unapigana kwa kila hali, mara dawa hii mara ile, iteni (doctor)huyu au yule, Sasa hebu fikiria nini habari yetu sisi hiyo Pepo, (Jicho halijawahi kuona, sikio halijapatapo kusikia) ina hali gani Pepo ya Mollah wetu.
Nyinyi Mmeonewa huruma ndio maana hesabu zenu zikazidishwa, kwa sababu wengine wana Maringo wanadhani vijithawabu vyao katika miezi ya kawaida vinaweza kununu pepo. Basi thamani ya hiyo Pepo imetajwa kama unataka kuinunua itazame fadhila iliyomo ndani ya mwezi huu, umeambiwa nini?.
Ukifanya au ukitujia na jambo moja la kheri katika mwezi huu wa Ramadhan malipo yake ni sawa sawa na mambo sabini (70)ya Fardh, Pia unaambiwa "Ewe Mcha Mungu" huu ni mwezi wa subira, Na kwa ajili hiyo ya kujizuia kwako na mambo yote, basi imekua zawadi ya subira yako ni hiyo Pepo.
Nini (Sabr)? Subira ni (Eternity) ni sehemu ambayo haina mwisho, subira haina saa wala dakika, haina usiku wala mchana, haina miezi wala miaka, ndio maana ukiingia ndani ya tendo la subira mara moja linatoweka, yatizame mambo yote mazuri yanakwisha haraka sana, kwa sababu umeonja subira, umeonja mapenzi, umeonja Taqwa, lakini zitizame dhiki unavoziona zinadumu milele, ndio maana ukilala hujui masaa mangapi mpaka uamke, lakini ukiwa macho (Unasema Mwenyewe Funga ya leo kali haimaliziki).
Basi kwa ajili ya Mollah wako umefanya subira na kukubali amri yake, kwa hiyo malipo yako ndio hiyo Pepo.
Hiyo ndio maana ya ukitujia na jema moja tunakulipa mara sabini, kwa sababu hilo moja lako limo ndani ya hiyo (sabr)Subira, Jee unaijua Sabini ya Mwenye enzi Mungu ikoje?. (Wallahi)ungeijua ilivyo basi ungeifata kwa Magoti na unyenyekevu ukawalisha watu japo kokwa ya tende, ukawafutarisha watu japo maji, ukawapa japo maziwa, Nini habari yako Mja wewe ulokushika Ucha Mungu Mwaka huu Ukaamua Kuwafutarisha Masikini Mwezi Mzima malipo yake yatakuaje?.
Enyi Mliopo Arabuni na Ulaya na Kwengineko zikimbilieni Thawabu hizi zitakuja kukusaidieni siku ya kufunga macho ya dunia, siku ambayo utashangaa unatolewa Roho yako na huku mbele unaoneshwa malipo yako kwa ajili tu ya kumfutarisha mwenzio alofunga. Fanyeni bidii kuipata hiyo Taqwa kwa kuwalisha watu futari, Hayo ndio mapenzi ya Mwenye enzi Mungu juu yenu. Anataka na nyie muyapate ndio maana anakuhimizeni na kukuulizeni vile tulokupeni mmevitoa, Angalia kawaida ya Mwanaadamu jee anayo Tabia ya kutoa, hutokuta ila wachache sana, na hiyo ndio dalili ya mapenzi, ukiona huwezi kutoa basi na mapenzi au hiyo Taqwa itakua ngumu sana kuipata.
Mwenye enzi Mungu kakupa uhai hapa duniani na kesho Akhera, Ukiijua Rehma hiyo ndani ya Mwezi huu wa Ramadhan basi utafanya bidii kubwa kuyaendea mapenzi ya Mwenye enzi Mungu.
Utabadilika kuwa Mtu wa aina nyengine, hutomuasi Mollah wako, hutopindukia mipaka uliyowekewa, Ndani ya Mwezi huu Mollah wako kakukumbusha kuwa wewe ni (Special)Kakupa (Gurantee)ya Msamaha kwa ajili ya hiyo (Taqwa)yako, kwa kuwa huu ni Mwezi wake (Special) kakupa hilo jambo la (4) la kukunusuru na adhabu ya Moto wa Jahannam. Hiyo ndio (Taqwa) ndani ya mwezi huu wa Ramadhan.
Hapo utakua tayari kuliingia jambo la tatu(3) ambalo ni kumuomba Mollah wako (Pepo yake). Unapotajiwa pepo akili yako mbio inakimbilia kwenye jumba la ghorofa na mto(River)inapita mbele, basi umemaliza. Lakini Jambo unalo ahidiwa na Mwenye enzi Mungu elewa halina mfano, ikiwa haya maisha ya dunia katika huu (Uhai)ulopewa unaupenda hali hii, ukiambiwa sasa wakati wako ushafika wa kurudi Akhera unakua na huzuni kubwa, hutaki kwenda, unapigana kwa kila hali, mara dawa hii mara ile, iteni (doctor)huyu au yule, Sasa hebu fikiria nini habari yetu sisi hiyo Pepo, (Jicho halijawahi kuona, sikio halijapatapo kusikia) ina hali gani Pepo ya Mollah wetu.
Nyinyi Mmeonewa huruma ndio maana hesabu zenu zikazidishwa, kwa sababu wengine wana Maringo wanadhani vijithawabu vyao katika miezi ya kawaida vinaweza kununu pepo. Basi thamani ya hiyo Pepo imetajwa kama unataka kuinunua itazame fadhila iliyomo ndani ya mwezi huu, umeambiwa nini?.
Ukifanya au ukitujia na jambo moja la kheri katika mwezi huu wa Ramadhan malipo yake ni sawa sawa na mambo sabini (70)ya Fardh, Pia unaambiwa "Ewe Mcha Mungu" huu ni mwezi wa subira, Na kwa ajili hiyo ya kujizuia kwako na mambo yote, basi imekua zawadi ya subira yako ni hiyo Pepo.
Nini (Sabr)? Subira ni (Eternity) ni sehemu ambayo haina mwisho, subira haina saa wala dakika, haina usiku wala mchana, haina miezi wala miaka, ndio maana ukiingia ndani ya tendo la subira mara moja linatoweka, yatizame mambo yote mazuri yanakwisha haraka sana, kwa sababu umeonja subira, umeonja mapenzi, umeonja Taqwa, lakini zitizame dhiki unavoziona zinadumu milele, ndio maana ukilala hujui masaa mangapi mpaka uamke, lakini ukiwa macho (Unasema Mwenyewe Funga ya leo kali haimaliziki).
Basi kwa ajili ya Mollah wako umefanya subira na kukubali amri yake, kwa hiyo malipo yako ndio hiyo Pepo.
Hiyo ndio maana ya ukitujia na jema moja tunakulipa mara sabini, kwa sababu hilo moja lako limo ndani ya hiyo (sabr)Subira, Jee unaijua Sabini ya Mwenye enzi Mungu ikoje?. (Wallahi)ungeijua ilivyo basi ungeifata kwa Magoti na unyenyekevu ukawalisha watu japo kokwa ya tende, ukawafutarisha watu japo maji, ukawapa japo maziwa, Nini habari yako Mja wewe ulokushika Ucha Mungu Mwaka huu Ukaamua Kuwafutarisha Masikini Mwezi Mzima malipo yake yatakuaje?.
Enyi Mliopo Arabuni na Ulaya na Kwengineko zikimbilieni Thawabu hizi zitakuja kukusaidieni siku ya kufunga macho ya dunia, siku ambayo utashangaa unatolewa Roho yako na huku mbele unaoneshwa malipo yako kwa ajili tu ya kumfutarisha mwenzio alofunga. Fanyeni bidii kuipata hiyo Taqwa kwa kuwalisha watu futari, Hayo ndio mapenzi ya Mwenye enzi Mungu juu yenu. Anataka na nyie muyapate ndio maana anakuhimizeni na kukuulizeni vile tulokupeni mmevitoa, Angalia kawaida ya Mwanaadamu jee anayo Tabia ya kutoa, hutokuta ila wachache sana, na hiyo ndio dalili ya mapenzi, ukiona huwezi kutoa basi na mapenzi au hiyo Taqwa itakua ngumu sana kuipata.
Mwenye enzi Mungu kakupa uhai hapa duniani na kesho Akhera, Ukiijua Rehma hiyo ndani ya Mwezi huu wa Ramadhan basi utafanya bidii kubwa kuyaendea mapenzi ya Mwenye enzi Mungu.
Utabadilika kuwa Mtu wa aina nyengine, hutomuasi Mollah wako, hutopindukia mipaka uliyowekewa, Ndani ya Mwezi huu Mollah wako kakukumbusha kuwa wewe ni (Special)Kakupa (Gurantee)ya Msamaha kwa ajili ya hiyo (Taqwa)yako, kwa kuwa huu ni Mwezi wake (Special) kakupa hilo jambo la (4) la kukunusuru na adhabu ya Moto wa Jahannam. Hiyo ndio (Taqwa) ndani ya mwezi huu wa Ramadhan.
Monday, May 1, 2017
IJUWE RAMADHAN PART 1
Asalaam Aleiykum
Mwanzo napenda kufahamisha ili unielewe kwanini darsa hii ikaanza na sentensi (Ijuwe Ramadhan), kumbuka kuna tafauti nyingi ambazo zinatokea katika maisha na wewe bado huzifahamu, mfano kama (Kusikia na Kusikiliza)vitu viwili hivi tafauti lakini kuvifahamu lazima upate muongozo. Kawaida ya kusikia ni ile ya uhuru wa masikio kusikia kila kitu, Lakini kusikiliza inatakiwa umuhimu wa (Roho)yako ihudhurie pasi na kushughulishwa na chochote ili kukipa nafasi ya pekee hicho ambacho (Unaambiwa au kukisikia), kusikiliza unatakiwa usiingize chochote kati yake,kwa maana hiyo hata Akili yako isiingie kati katika hilo tendo la kusikiliza, Isiwe Mtu anakwambia kitu, wewe ndani ya Akili yako unatafisiri vyengine kabisa.
Hali kadhalika juhudi hiyo pia unatakiwa uifanye wakati wa kujifunza jambo, au ukiwa katika harakati za kujua. Kwa wale ambao bado hawajanifahamu wacha nifupishe misemo na kuwatolea mfano rahisi wa kujua, ni kama vile unafundishwa kuogelea ukaambiwa sasa jiregeze, usigombane na maji, peleka mkono huu taratibu mbele, mara huyo ukajiona umeelea, uko juu ya maji hapo inakua ushajua kuogelea na hiyo inaitwa (Experience),na hiyo ndio maana ya kujua.
Sasa vipi imehusiana na kuijua Ramadhan, Kwa sababu siku zote ""(Unasikia)"wanasema Masheikh Funga mwezi umefika, Na wewe huyo unaamua kukaa na njaa,Kwanini nikasema kukaa na njaa?, kwa sababu huipati Taqwa, pengine miaka yote hali kama hiyo inakukuta, sio makosa kwa sababu pengine ulikua hujui, lakini ukishamaliza kuisoma darsa hii ukaendelea kama ulivokua unafunga mwanzo, hapo utakua unatenda makosa kwa sababu umeshajua ila wewe sasa hutaki.
Nakuchukua katika (Deep sea) ili funga yako mwaka huu iwe vyengine kabisa, ili upate kujua kusudio la Mwezi huu na wewe ufunge kama mawalii, ufunge kama (Mystic). Siku zote nasema kama utaona mafunzo yangu (batil)huyafahamu, sio kama alivosema (Sheikh wako)basi niachie mwenyewe, mie ndio dhamana wa hili somo, na wewe baki na mwenendo wako, huna haja yakuchuma dhanmbi au kunitupia maneno yasofaa.
Kumbuka darsa zangu naziandaa ili nikufanyie (Shock)hakuna kitu kipya ila yale yale yalosemwa nyuma ila mimi nayaleta kwa njia nyengine tu. Kwa hiyo wakati mwengine utaona mbona mambo mepya haya, na hilo ndio kusudio langu, usibakie na mambo ya zamani, pata kujua mambo mepya, Ulimwengu huu una mambo mepya kila siku yanavumbuliwa, Kwanini unaogopa upya?. Naamsha moyo wako , Masheikh wanapiga kigoma cha daku kila mwaka na wewe bado umelala, sasa mimi nakuja na Tarumbeta(Saxphone)ili nipate kukushitua.
Nini Ramadhani?
Ramadhan ni kama ilivyo (Hajj)ila tafauti yake (Hijja)ni mara moja tena kwa mwenye uwezo, lakini Ramadhan ni kila mwaka unatakiwa ukahijji wapi?. Tuliza Akili upate kunifahamu vizuri na hii itakufanya uione Ramadhan kwa muonekano mpya kabisa, na kama darsa hii itafika moyoni mwako itakubadilisha milele kama ilivo nibadilisha mimi.
enedelea part 2
Mwanzo napenda kufahamisha ili unielewe kwanini darsa hii ikaanza na sentensi (Ijuwe Ramadhan), kumbuka kuna tafauti nyingi ambazo zinatokea katika maisha na wewe bado huzifahamu, mfano kama (Kusikia na Kusikiliza)vitu viwili hivi tafauti lakini kuvifahamu lazima upate muongozo. Kawaida ya kusikia ni ile ya uhuru wa masikio kusikia kila kitu, Lakini kusikiliza inatakiwa umuhimu wa (Roho)yako ihudhurie pasi na kushughulishwa na chochote ili kukipa nafasi ya pekee hicho ambacho (Unaambiwa au kukisikia), kusikiliza unatakiwa usiingize chochote kati yake,kwa maana hiyo hata Akili yako isiingie kati katika hilo tendo la kusikiliza, Isiwe Mtu anakwambia kitu, wewe ndani ya Akili yako unatafisiri vyengine kabisa.
Hali kadhalika juhudi hiyo pia unatakiwa uifanye wakati wa kujifunza jambo, au ukiwa katika harakati za kujua. Kwa wale ambao bado hawajanifahamu wacha nifupishe misemo na kuwatolea mfano rahisi wa kujua, ni kama vile unafundishwa kuogelea ukaambiwa sasa jiregeze, usigombane na maji, peleka mkono huu taratibu mbele, mara huyo ukajiona umeelea, uko juu ya maji hapo inakua ushajua kuogelea na hiyo inaitwa (Experience),na hiyo ndio maana ya kujua.
Sasa vipi imehusiana na kuijua Ramadhan, Kwa sababu siku zote ""(Unasikia)"wanasema Masheikh Funga mwezi umefika, Na wewe huyo unaamua kukaa na njaa,Kwanini nikasema kukaa na njaa?, kwa sababu huipati Taqwa, pengine miaka yote hali kama hiyo inakukuta, sio makosa kwa sababu pengine ulikua hujui, lakini ukishamaliza kuisoma darsa hii ukaendelea kama ulivokua unafunga mwanzo, hapo utakua unatenda makosa kwa sababu umeshajua ila wewe sasa hutaki.
Nakuchukua katika (Deep sea) ili funga yako mwaka huu iwe vyengine kabisa, ili upate kujua kusudio la Mwezi huu na wewe ufunge kama mawalii, ufunge kama (Mystic). Siku zote nasema kama utaona mafunzo yangu (batil)huyafahamu, sio kama alivosema (Sheikh wako)basi niachie mwenyewe, mie ndio dhamana wa hili somo, na wewe baki na mwenendo wako, huna haja yakuchuma dhanmbi au kunitupia maneno yasofaa.
Kumbuka darsa zangu naziandaa ili nikufanyie (Shock)hakuna kitu kipya ila yale yale yalosemwa nyuma ila mimi nayaleta kwa njia nyengine tu. Kwa hiyo wakati mwengine utaona mbona mambo mepya haya, na hilo ndio kusudio langu, usibakie na mambo ya zamani, pata kujua mambo mepya, Ulimwengu huu una mambo mepya kila siku yanavumbuliwa, Kwanini unaogopa upya?. Naamsha moyo wako , Masheikh wanapiga kigoma cha daku kila mwaka na wewe bado umelala, sasa mimi nakuja na Tarumbeta(Saxphone)ili nipate kukushitua.
Nini Ramadhani?
Ramadhan ni kama ilivyo (Hajj)ila tafauti yake (Hijja)ni mara moja tena kwa mwenye uwezo, lakini Ramadhan ni kila mwaka unatakiwa ukahijji wapi?. Tuliza Akili upate kunifahamu vizuri na hii itakufanya uione Ramadhan kwa muonekano mpya kabisa, na kama darsa hii itafika moyoni mwako itakubadilisha milele kama ilivo nibadilisha mimi.
enedelea part 2
IJUWE RAMADHAN PART 2
Asalaam Aleiykum
Kwanini Nikasema kama (Hajj)?.
Kumbuka haya ni maneno yangu, au ufahamu wangu, na nitakuonesha kwa mifano ipi hata nikaita Ramadhan ni kama (Hijja)ya kila mwaka kwa Muumin, Yamekua Mapenzi ya Allah makubwa juu yetu kwa kutuletea Mwezi huu Mtukufu wenye Baraka kila mwaka.
Ili upate kunifahamu vizuri itabidi nikujulishe mambo mawili ambayo ndio msingi wa darsa yetu, Ama jambo la kwanza ni ile desturi ya "Bwana Mtume s.a.w alipokua kila akilizungumza jambo la Taqwa akionesha kifuani kuashiria ndani""Alikua akiashiria kitu kilichomo ndani akisema Taqwa imo ndani, Taqwa imo Ndani", Wengi hawalijui na wanadhani alikua akionesha kifua chake, au kuashiria moyo, lakini kusudio lake ilikua kutufahamisha kuna kitu ndani ya mwili wetu, hicho ndio chenye uwezo wa kutenda Taqwa, mkiweza kukijua, mkifanikiwa kukigundua, basi moja kwa moja unakua Mcha Mungu, na usidhani Ucha Mungu unapatikana bila ya kitu hicho, unaweza kujidanganya, nje ukawa Mcha Mungu, lakini ndani kutwa ukawa unazini, unadhulumu,unafisidi hapo bado hujawa Mcha Mungu, Ucha Mungu lazima uwe na (Control)ya ndani na nje, lakini ukiona bado ndani unateseka basi fanya jitihada, zidisha safari ya (Umrah) ya ndani mpaka ukijue hicho kinachoweza kutenda (Taqwa).
Ama Jambo la Pili nalopenda kukufahamisha ni zile (Ngazi)tatu za kukufanya wewe ufikie huo Ucha Mungu au kuwa Muislam kamili, Wengi katika sisi tumepata baraka(Blessing)za kuzaliwa ndani ya Uislam, tumeinukia kwenye Uislam, kwa hilo tunapaswa kumshukuru Mollah kwa hisan hiyo, kwanini nikasema hisan, kwa sababu wewe hukuchagua uzaliwe na wazazi wa dini gani, kakuchagulia Mollah wako ndio na wewe ukajikuta Muislam, pengine ungezaliwa na wazee wenye dini nyengine usingekua Muislam, ndio maana nikaita (Ihsan).
Sasa jambo la mwanzo katika hizo (step 3)kuwa wengine Uislam kwao unakuja (Automatic)kama kwa kuzaliwa, na wengine wanaingia kwa kupewa (dawa)au mawaidha wakubali kuwa waislam. Sasa Uislam ni ngazi ya kwanza, ni kama kitambulisho, ndio maana unakua Muislam lakini unatenda mambo yote yenye kukatazwa na Mollah wako, huna tafauti na asiyekua Muislam, halafu jambo la pili katika hayo matatu niliyo yataja ni lile la wewe kuwa Muumin, Nini Muumin?.
Ni yule aliyeanza kuzitii Amri, akaanza kuzifata kidogo kidogo, mara anateleza anaanguka, ikisha anainuka na kuendelea na safari ya kujitahidi kuwa Muumin, Halafu jambo la tatu kukutana na (Truth)kufungukiwa na fahamu, kukutana (Face to Face)na yakini ya mambo yalofichwa kwa uwazi.kupata uhakika kwa njia ya (Ilham)Na ukipata au kujua uhakika hapo unakua Mbarikiwa, na wala si kwa njia ya kusoma sana ukakusanya (Information), Ni njia ya ku (Experience)kwenye moyo wako, hapo ndio inatokea hiyo (Surrender),unakua (Total)umewasili kwenye kisiwa cha (Taqwa)sasa wewe unaweza kuvaa taji la (Ucha Mungu).
Hapo ulipo visa vyote vinapotea, huna haja ya chochote, umeshagundua utajiri wa Mwenye enzi Mungu, humtegemei tena Binaadamu mwenzako, unakaa kimya kuangalia Ulimwengu, Raha za hali kama hiyo sio tena za Ulimwengu huu (Full of bliss). Hapo huna tamaa, huna chuki, huna ufisadi, huna hamaki, hutaki maasi, vyote vinatoweka katika nafsi yako, Na hiyo ndio funga ya Ramadhan ambayo na wewe unatakiwa uionje kila mwaka, pengine ukiigusa au kuionja hali kama hiyo unaweza kuamua kudumu nayo, ndio maana nikaita kama (Hijja),nenda kahudhurie uipate kila mwaka. Na hayo ndio mashiko yenye kutufungulia darsa yetu ya leo.
Endelea part 3
Kwanini Nikasema kama (Hajj)?.
Kumbuka haya ni maneno yangu, au ufahamu wangu, na nitakuonesha kwa mifano ipi hata nikaita Ramadhan ni kama (Hijja)ya kila mwaka kwa Muumin, Yamekua Mapenzi ya Allah makubwa juu yetu kwa kutuletea Mwezi huu Mtukufu wenye Baraka kila mwaka.
Ili upate kunifahamu vizuri itabidi nikujulishe mambo mawili ambayo ndio msingi wa darsa yetu, Ama jambo la kwanza ni ile desturi ya "Bwana Mtume s.a.w alipokua kila akilizungumza jambo la Taqwa akionesha kifuani kuashiria ndani""Alikua akiashiria kitu kilichomo ndani akisema Taqwa imo ndani, Taqwa imo Ndani", Wengi hawalijui na wanadhani alikua akionesha kifua chake, au kuashiria moyo, lakini kusudio lake ilikua kutufahamisha kuna kitu ndani ya mwili wetu, hicho ndio chenye uwezo wa kutenda Taqwa, mkiweza kukijua, mkifanikiwa kukigundua, basi moja kwa moja unakua Mcha Mungu, na usidhani Ucha Mungu unapatikana bila ya kitu hicho, unaweza kujidanganya, nje ukawa Mcha Mungu, lakini ndani kutwa ukawa unazini, unadhulumu,unafisidi hapo bado hujawa Mcha Mungu, Ucha Mungu lazima uwe na (Control)ya ndani na nje, lakini ukiona bado ndani unateseka basi fanya jitihada, zidisha safari ya (Umrah) ya ndani mpaka ukijue hicho kinachoweza kutenda (Taqwa).
Ama Jambo la Pili nalopenda kukufahamisha ni zile (Ngazi)tatu za kukufanya wewe ufikie huo Ucha Mungu au kuwa Muislam kamili, Wengi katika sisi tumepata baraka(Blessing)za kuzaliwa ndani ya Uislam, tumeinukia kwenye Uislam, kwa hilo tunapaswa kumshukuru Mollah kwa hisan hiyo, kwanini nikasema hisan, kwa sababu wewe hukuchagua uzaliwe na wazazi wa dini gani, kakuchagulia Mollah wako ndio na wewe ukajikuta Muislam, pengine ungezaliwa na wazee wenye dini nyengine usingekua Muislam, ndio maana nikaita (Ihsan).
Sasa jambo la mwanzo katika hizo (step 3)kuwa wengine Uislam kwao unakuja (Automatic)kama kwa kuzaliwa, na wengine wanaingia kwa kupewa (dawa)au mawaidha wakubali kuwa waislam. Sasa Uislam ni ngazi ya kwanza, ni kama kitambulisho, ndio maana unakua Muislam lakini unatenda mambo yote yenye kukatazwa na Mollah wako, huna tafauti na asiyekua Muislam, halafu jambo la pili katika hayo matatu niliyo yataja ni lile la wewe kuwa Muumin, Nini Muumin?.
Ni yule aliyeanza kuzitii Amri, akaanza kuzifata kidogo kidogo, mara anateleza anaanguka, ikisha anainuka na kuendelea na safari ya kujitahidi kuwa Muumin, Halafu jambo la tatu kukutana na (Truth)kufungukiwa na fahamu, kukutana (Face to Face)na yakini ya mambo yalofichwa kwa uwazi.kupata uhakika kwa njia ya (Ilham)Na ukipata au kujua uhakika hapo unakua Mbarikiwa, na wala si kwa njia ya kusoma sana ukakusanya (Information), Ni njia ya ku (Experience)kwenye moyo wako, hapo ndio inatokea hiyo (Surrender),unakua (Total)umewasili kwenye kisiwa cha (Taqwa)sasa wewe unaweza kuvaa taji la (Ucha Mungu).
Hapo ulipo visa vyote vinapotea, huna haja ya chochote, umeshagundua utajiri wa Mwenye enzi Mungu, humtegemei tena Binaadamu mwenzako, unakaa kimya kuangalia Ulimwengu, Raha za hali kama hiyo sio tena za Ulimwengu huu (Full of bliss). Hapo huna tamaa, huna chuki, huna ufisadi, huna hamaki, hutaki maasi, vyote vinatoweka katika nafsi yako, Na hiyo ndio funga ya Ramadhan ambayo na wewe unatakiwa uionje kila mwaka, pengine ukiigusa au kuionja hali kama hiyo unaweza kuamua kudumu nayo, ndio maana nikaita kama (Hijja),nenda kahudhurie uipate kila mwaka. Na hayo ndio mashiko yenye kutufungulia darsa yetu ya leo.
Endelea part 3
IJUWE RAMADHAN PART 3
Asalaam Aleiykum
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡڪُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِڪُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
(Bakarah 183)
"Enyi Mloamini Mmelazimishwa kufunga(Saumu)kama walivyolazimishwa waliokua kabla yenu ili mpate kumcha Mungu"
Kwanini aya ikaanza na enyi Mloamini melazimishwa, kwa sababu mngeambiwa mmeamrishwa bado mngebakia kama waislam wengine wanaendelea kutenda dhanmbi, wanabakia na kitambulisho tu cha majina, lakini kumbuka hiyo lazima ya hapo ni lazima ya mapenzi, sio lazima ya mtutu wa bunduki kama hufanyi utakufa, ila Mollah wako anataka uonje ladha ya kumtii yeye inakuaje, hali inayo kutokezea ukiwa karibu naye, anakutaka japo mara moja kwa mwaka uka (Hijj)ndani ya nafsi yako ujijue (How bless are you).
Sasa kwanza tuitizame funga yenyewe ina siri gani?, sitaki kwenda kwenye faida zake katika darsa hii nikawa kama nafanya biashara, kwani wengine wanasubiri wasikie funga inaponesha maradhi, ndio wanafunga ili wapate kupona, inafanya hivyo sikatai, lakini ukifunga kwa ajili hiyo utakua umeikosa Taqwa, unatakiwa ufunge kwa ajili ya mapenzi ya Mollah wako ili ukutane na hicho chenye kutenda taqwa.
Nini funga inafanya juu yako, na kwanini nikasema (Hijja)ya kila mwaka, siku zote unafunga hujui mambo haya, sasa kuanzia leo nataka funga yako iwe ya aina nyengine isiwe kama za miaka ya nyuma, ndio maana nikakwambia kwanza (Ijue Ramadhan)halafu ndio utaifunga kwa vizuri, ikisha ndio utaipata hiyo Taqwa.
Kitu cha mwanzo kabisa nataka ukumbuke tu, ndipo utaipata hiyo (Hijja)ya kuhudhuria (Body)Mwili wako, ili upate kujua vipi inakua, vipi unakumbuka, Jambo la kwanza kabisa au saumu yako ya mwanzo unapata jambo la kuwa (Alert)(Awareness) au Dhahir, unapata fahamu kuwa hujala, sasa itabidi ujiulize huyu nani mwenye kujijua sijala, na kuwa nimefunga, ukishagundua hilo litaanza kukupeleka kwenye mambo mengine moja baada ya jengine katika nafsi yako na hiyo ndio (Hijja)yenyewe nilokusudia.
Utaona vipi Akili inavo hangaika na kuhaha kutaka chakula, kwa kuwa (Body)yako yote ni (Intelligence)tupu inatambua kuwa (Boss)leo kagoma kuleta chakula, hakuna huduma kutoka nje, kwa hiyo inaanza kwenda ndani kwenye (Store) na kutoa akiba hapo (Body)inajilisha yenyewe(Cannibal)unajila mwenyewe, na hapo unapata hiyo (separation)baina ya Mwili wako na hicho chenye kutenda Taqwa ukiweza kulijua hilo unakua wewe ni Mwenye kufuzu.
Mara unaona njaa hiyo imepotea , kumbuka huyu mwenye kuona ni nani?, Ikipotea njaa mara unakuja usingizi, na usingizi upo wa aina mbili uko ule wa kulala umezidiwa au ule wa kujizubaisha ambapo Akili sasa imehamaki inakwambia rudi kwenye desturi yetu ya Miezi 11, ya nini unataka kugundua au kufanya jambo la Taqwa, wewe shika simu, au angalia TV, au twende tukajiliwaze senema, hee basi safari hii hata barazani hupiti, Akili inakuvuta kwenye mazoea yako ya kumuasi Mollah wako, inakurudisha katika yale mambo yote unayofanya miezi 11 ilopita, mimi nakwambia safari hii pigana na akili, Yaache mambo yote ya Mwezi wa kula mchana, nenda kinyume na maamrisho yake, vipi utafanya? usije ukashindana na akili, huwezi kushinda, ila nakupa (Trick)mawazo yote yakija (Just watch inside you)ukiweza kuangalia Akili yako mara baada ya sekunde chache wazo la karata, barazani,sokoni, kutizama wanawake au wanaume litatoweka, kidogo kidogo utaanza kuishinda Akili.
Kawaida unakuwa ni mwenye kushinda vita ya ndani, Njaa pale inapokuja unaipuuza, usingizi unapokuja unaushinda, lakini Ramadhan zote vita vya nje vinakushinda na hilo ndilo lenye kukukosesha hiyo Taqwa, Basi kama ulivoamrishwa na Mollah wako kumbuka Taqwa haitakiwi iwe nusu, inatakiwa (Total)Taqwa ni ncha mbili ndani na nje ndio uweze kuifikia, uweze kuigundua, uweze kuifanya, Kumbuka ndani unaishinda njaa, sex,usingizi, lakini nje mambo yote yanaendelea kama kawaida, haitakiwi hivyo, kuipata Taqwa unatakiwa hiyo (Surrender total)Itakubidi mwaka huu ubadilike, funga yako iwe ya aina nyengine, jiandae na mambo ya nje yote uyaache, kumbuka ni siku chache tu lakini manufaa yake ni ya kudumu, ikiwa unaweza kujizuia Bia na sigara na mirungi, maji, chakula na vyengine vyote unaweza kuviepuka, basi mwaka huu ongeza mambo ya nje, kimbia mambo ya kipuuzi, iepuke simu, achana na facebook, acha kukimbilia mazungumzo ya kipuuzi,gomea mipira,ichukie Tv,usitizame machafu,usende karibu na mambo machafu, acha kudhulumu, usiseme seme sana, acha uongo, jiepushe na matamanio, acha kuwa muandishi wa habari kuwa kila kitu ushuhudie, acha kukaa kuanza kufikiria mafutari, ukiweza kubakia (Empty) au kufanikiwa kuyashinda mengi katika hayo japo kwa siku tatu za mwanzo, hapo utaanza kupata (Glimpse)ya hiyo Taqwa, utaanza kui (Experience) wewe mwenyewe, nitakua sina haja ya kukuhadithia.
Taqwa itaanza kuzaliwa kwenye Roho yako, Utakua Mwenye(Bliss)umewasili nyumbani, (You are Blessed) Taqwa itakuchukua pale ambapo wanafika Mawalii, wanapofika (Mystic)utafika hapo kwenye kujibiwa duwa, utafika hapo kwenye (Makarama)yote wanapofika wacha Mungu, hutotaka tena Mtu akuombee dua, Hapo ndipo iliposemwa kumi la Mwanzo ni (Rehma)hiyo ndio taqwa ambayo ukiipata wewe ndio utakua shahid wa hilo, kumbuka darsa hii ni kuijua na darsa ijayo ukishakua katika hali ya hiyo Taqwa nini kinatokezea?kwanini nikasema kinatokezea kwa sababu hiyo ndio (Nature)ya Taqwa, na kama haitokezei basi unakaa na njaa, na wakati wa kukaa na njaa sasa ushakwisha unatakiwa ufunge huku umeshiba, na hiyo ndio Taqwa, na kumbuka ukishiba chakula lazima ukigawe, na hilo tutalikuta katika mada ya (Mafundisho ya Taqwa)Tukijaaliwa na Mollah wetu kabla ya kuingia katika mfungo wa Ramadhan.
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡڪُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِڪُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
(Bakarah 183)
"Enyi Mloamini Mmelazimishwa kufunga(Saumu)kama walivyolazimishwa waliokua kabla yenu ili mpate kumcha Mungu"
Kwanini aya ikaanza na enyi Mloamini melazimishwa, kwa sababu mngeambiwa mmeamrishwa bado mngebakia kama waislam wengine wanaendelea kutenda dhanmbi, wanabakia na kitambulisho tu cha majina, lakini kumbuka hiyo lazima ya hapo ni lazima ya mapenzi, sio lazima ya mtutu wa bunduki kama hufanyi utakufa, ila Mollah wako anataka uonje ladha ya kumtii yeye inakuaje, hali inayo kutokezea ukiwa karibu naye, anakutaka japo mara moja kwa mwaka uka (Hijj)ndani ya nafsi yako ujijue (How bless are you).
Sasa kwanza tuitizame funga yenyewe ina siri gani?, sitaki kwenda kwenye faida zake katika darsa hii nikawa kama nafanya biashara, kwani wengine wanasubiri wasikie funga inaponesha maradhi, ndio wanafunga ili wapate kupona, inafanya hivyo sikatai, lakini ukifunga kwa ajili hiyo utakua umeikosa Taqwa, unatakiwa ufunge kwa ajili ya mapenzi ya Mollah wako ili ukutane na hicho chenye kutenda taqwa.
Nini funga inafanya juu yako, na kwanini nikasema (Hijja)ya kila mwaka, siku zote unafunga hujui mambo haya, sasa kuanzia leo nataka funga yako iwe ya aina nyengine isiwe kama za miaka ya nyuma, ndio maana nikakwambia kwanza (Ijue Ramadhan)halafu ndio utaifunga kwa vizuri, ikisha ndio utaipata hiyo Taqwa.
Kitu cha mwanzo kabisa nataka ukumbuke tu, ndipo utaipata hiyo (Hijja)ya kuhudhuria (Body)Mwili wako, ili upate kujua vipi inakua, vipi unakumbuka, Jambo la kwanza kabisa au saumu yako ya mwanzo unapata jambo la kuwa (Alert)(Awareness) au Dhahir, unapata fahamu kuwa hujala, sasa itabidi ujiulize huyu nani mwenye kujijua sijala, na kuwa nimefunga, ukishagundua hilo litaanza kukupeleka kwenye mambo mengine moja baada ya jengine katika nafsi yako na hiyo ndio (Hijja)yenyewe nilokusudia.
Utaona vipi Akili inavo hangaika na kuhaha kutaka chakula, kwa kuwa (Body)yako yote ni (Intelligence)tupu inatambua kuwa (Boss)leo kagoma kuleta chakula, hakuna huduma kutoka nje, kwa hiyo inaanza kwenda ndani kwenye (Store) na kutoa akiba hapo (Body)inajilisha yenyewe(Cannibal)unajila mwenyewe, na hapo unapata hiyo (separation)baina ya Mwili wako na hicho chenye kutenda Taqwa ukiweza kulijua hilo unakua wewe ni Mwenye kufuzu.
Mara unaona njaa hiyo imepotea , kumbuka huyu mwenye kuona ni nani?, Ikipotea njaa mara unakuja usingizi, na usingizi upo wa aina mbili uko ule wa kulala umezidiwa au ule wa kujizubaisha ambapo Akili sasa imehamaki inakwambia rudi kwenye desturi yetu ya Miezi 11, ya nini unataka kugundua au kufanya jambo la Taqwa, wewe shika simu, au angalia TV, au twende tukajiliwaze senema, hee basi safari hii hata barazani hupiti, Akili inakuvuta kwenye mazoea yako ya kumuasi Mollah wako, inakurudisha katika yale mambo yote unayofanya miezi 11 ilopita, mimi nakwambia safari hii pigana na akili, Yaache mambo yote ya Mwezi wa kula mchana, nenda kinyume na maamrisho yake, vipi utafanya? usije ukashindana na akili, huwezi kushinda, ila nakupa (Trick)mawazo yote yakija (Just watch inside you)ukiweza kuangalia Akili yako mara baada ya sekunde chache wazo la karata, barazani,sokoni, kutizama wanawake au wanaume litatoweka, kidogo kidogo utaanza kuishinda Akili.
Kawaida unakuwa ni mwenye kushinda vita ya ndani, Njaa pale inapokuja unaipuuza, usingizi unapokuja unaushinda, lakini Ramadhan zote vita vya nje vinakushinda na hilo ndilo lenye kukukosesha hiyo Taqwa, Basi kama ulivoamrishwa na Mollah wako kumbuka Taqwa haitakiwi iwe nusu, inatakiwa (Total)Taqwa ni ncha mbili ndani na nje ndio uweze kuifikia, uweze kuigundua, uweze kuifanya, Kumbuka ndani unaishinda njaa, sex,usingizi, lakini nje mambo yote yanaendelea kama kawaida, haitakiwi hivyo, kuipata Taqwa unatakiwa hiyo (Surrender total)Itakubidi mwaka huu ubadilike, funga yako iwe ya aina nyengine, jiandae na mambo ya nje yote uyaache, kumbuka ni siku chache tu lakini manufaa yake ni ya kudumu, ikiwa unaweza kujizuia Bia na sigara na mirungi, maji, chakula na vyengine vyote unaweza kuviepuka, basi mwaka huu ongeza mambo ya nje, kimbia mambo ya kipuuzi, iepuke simu, achana na facebook, acha kukimbilia mazungumzo ya kipuuzi,gomea mipira,ichukie Tv,usitizame machafu,usende karibu na mambo machafu, acha kudhulumu, usiseme seme sana, acha uongo, jiepushe na matamanio, acha kuwa muandishi wa habari kuwa kila kitu ushuhudie, acha kukaa kuanza kufikiria mafutari, ukiweza kubakia (Empty) au kufanikiwa kuyashinda mengi katika hayo japo kwa siku tatu za mwanzo, hapo utaanza kupata (Glimpse)ya hiyo Taqwa, utaanza kui (Experience) wewe mwenyewe, nitakua sina haja ya kukuhadithia.
Taqwa itaanza kuzaliwa kwenye Roho yako, Utakua Mwenye(Bliss)umewasili nyumbani, (You are Blessed) Taqwa itakuchukua pale ambapo wanafika Mawalii, wanapofika (Mystic)utafika hapo kwenye kujibiwa duwa, utafika hapo kwenye (Makarama)yote wanapofika wacha Mungu, hutotaka tena Mtu akuombee dua, Hapo ndipo iliposemwa kumi la Mwanzo ni (Rehma)hiyo ndio taqwa ambayo ukiipata wewe ndio utakua shahid wa hilo, kumbuka darsa hii ni kuijua na darsa ijayo ukishakua katika hali ya hiyo Taqwa nini kinatokezea?kwanini nikasema kinatokezea kwa sababu hiyo ndio (Nature)ya Taqwa, na kama haitokezei basi unakaa na njaa, na wakati wa kukaa na njaa sasa ushakwisha unatakiwa ufunge huku umeshiba, na hiyo ndio Taqwa, na kumbuka ukishiba chakula lazima ukigawe, na hilo tutalikuta katika mada ya (Mafundisho ya Taqwa)Tukijaaliwa na Mollah wetu kabla ya kuingia katika mfungo wa Ramadhan.
Sunday, April 2, 2017
USINGIZI WA ROHO PART 1
Asalaam Aleiykum
Kuna Mambo Mwanaadamu yanatokezea unashindwa kujiuliza kwanini inakua hivi, mfano kwanini unapopigiwa honi kwa ghafla, au ukishtuliwa usingizini una hamaki?, umeshapata kujiuliza swali hili, au ndio umeshikiwa Dini yako na watu wengine hata mambo yako Mwenyewe lazima yasimamiwe na watu wengine.
Mimi kazi yangu kukuamsha usingizini unipende, au usinipende hilo sio tatizo langu, na kila ukinichukia najua kweli sasa unaanza kuamka, maradhi haya ya usingizi mzito yanaanza kupona.
Naijua sababu kubwa Mtu anakukera, Wewe unataka ubembelezwe yeye anakuja na kigoma cha daku,"Amka Amka" toka usingizini wewe, Kifo Kimekaribia, umeshakula chunvi nyingi, sasa hebu japo kidogo onja na sukari.
Najua unajiuliza kasema nimekula chunvi nyingi kakusudia nini kusema hivi?. Kwa Mimi Chunvi ni yale Matatizo yako, Mateso, Ghadhabu, Visasi, Chuki,Maudhi,Dhiki,Matamanio, Fikra Mbovu, Viburi na mengi ambayo unayajua, Ama kukuamsha kwangu ni kukwambia upo upande wa pili huku kuna sukari, ili kuipata unatakiwa uamke tu.Ukiamka utajua hazina ya Sukari isokwisha ni yale mazuri yaliyopo upande huo ambayo mara chache unayaonja lakini hujui kuwa hii ni sukari, kuwa nikenda mbele kidogo naweza kupata na (Asali), Lakini umekua Mteja wa Usingizi, una enjoy madhila na tabu za maisha haya na wala hutaki kuamka.
Sasa nimekuja kukuamsha basi kulala tena, inatosha ulivolala wacha kukoroma. Kulala kuko kwa aina mbili, aina ya kwanza ni ile ya (Nature)yako ilotajwa kwenye Quraan aya ya (9 sura ya Naba)
"وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتً۬ا "
Na tukaufanya usingizi wenu kama kufa.
Usingizi huu ni lazima kila kiumbe aupate, bila ya kulala siku saba tu utaanza kubadilika akili yako, na zikiendelea zaidi utapoteza akili na kupata madhara makubwa, kwa hiyo usingizi huu wa (Nature)ndio unaokufanya urejee Nyumbani,Na huwezi kurejea Nyumbani lazima upitie njia ya Mauti, ndio maana ukaambiwa(Tukaujaalia usingizi wao kama mauti). Sasa nini faida unayoipata ukenda huko nyumbani,(Ndio maana unasisitizwa uwe na tabia ya kulala mapema)huko unapata afya, unapata nguvu mpya,huko unapata (Vitality and Nourishment)huko ndiko kwenye mapumziko mazuri, huko ndiko unakotibiwa maradhi yako yote(Ndio Maana madaktari wanasisitiza mgonjwa mwacheni alale)mwacheni apumzike, na wao pia wanaomba kwenye nguvu za Miujiza na Rehma za Mollah wako zifanye kazi yake, huo ndio usingizi ambao pale ukiamka unasema najisikia vizuri,niko (Fresh) huo ni usingizi wa aina ya kwanza. Upi usingizi wa aina ya pili?.
endelea part 2
Kuna Mambo Mwanaadamu yanatokezea unashindwa kujiuliza kwanini inakua hivi, mfano kwanini unapopigiwa honi kwa ghafla, au ukishtuliwa usingizini una hamaki?, umeshapata kujiuliza swali hili, au ndio umeshikiwa Dini yako na watu wengine hata mambo yako Mwenyewe lazima yasimamiwe na watu wengine.
Mimi kazi yangu kukuamsha usingizini unipende, au usinipende hilo sio tatizo langu, na kila ukinichukia najua kweli sasa unaanza kuamka, maradhi haya ya usingizi mzito yanaanza kupona.
Naijua sababu kubwa Mtu anakukera, Wewe unataka ubembelezwe yeye anakuja na kigoma cha daku,"Amka Amka" toka usingizini wewe, Kifo Kimekaribia, umeshakula chunvi nyingi, sasa hebu japo kidogo onja na sukari.
Najua unajiuliza kasema nimekula chunvi nyingi kakusudia nini kusema hivi?. Kwa Mimi Chunvi ni yale Matatizo yako, Mateso, Ghadhabu, Visasi, Chuki,Maudhi,Dhiki,Matamanio, Fikra Mbovu, Viburi na mengi ambayo unayajua, Ama kukuamsha kwangu ni kukwambia upo upande wa pili huku kuna sukari, ili kuipata unatakiwa uamke tu.Ukiamka utajua hazina ya Sukari isokwisha ni yale mazuri yaliyopo upande huo ambayo mara chache unayaonja lakini hujui kuwa hii ni sukari, kuwa nikenda mbele kidogo naweza kupata na (Asali), Lakini umekua Mteja wa Usingizi, una enjoy madhila na tabu za maisha haya na wala hutaki kuamka.
Sasa nimekuja kukuamsha basi kulala tena, inatosha ulivolala wacha kukoroma. Kulala kuko kwa aina mbili, aina ya kwanza ni ile ya (Nature)yako ilotajwa kwenye Quraan aya ya (9 sura ya Naba)
"وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتً۬ا "
Na tukaufanya usingizi wenu kama kufa.
Usingizi huu ni lazima kila kiumbe aupate, bila ya kulala siku saba tu utaanza kubadilika akili yako, na zikiendelea zaidi utapoteza akili na kupata madhara makubwa, kwa hiyo usingizi huu wa (Nature)ndio unaokufanya urejee Nyumbani,Na huwezi kurejea Nyumbani lazima upitie njia ya Mauti, ndio maana ukaambiwa(Tukaujaalia usingizi wao kama mauti). Sasa nini faida unayoipata ukenda huko nyumbani,(Ndio maana unasisitizwa uwe na tabia ya kulala mapema)huko unapata afya, unapata nguvu mpya,huko unapata (Vitality and Nourishment)huko ndiko kwenye mapumziko mazuri, huko ndiko unakotibiwa maradhi yako yote(Ndio Maana madaktari wanasisitiza mgonjwa mwacheni alale)mwacheni apumzike, na wao pia wanaomba kwenye nguvu za Miujiza na Rehma za Mollah wako zifanye kazi yake, huo ndio usingizi ambao pale ukiamka unasema najisikia vizuri,niko (Fresh) huo ni usingizi wa aina ya kwanza. Upi usingizi wa aina ya pili?.
endelea part 2
USINGIZI WA ROHO PART 2
Asalaam Aleiykum
Ama ule wa aina ya pili, Ni ule unaporejea Ulimwenguni baada ya kulala ule wa mwanzo, unaona hautoshi bora uendelee kulala, na hivi ndivo ufanyavo umri wako wote. Vipi unalala, kumbuka kazi yangu ni kukuamsha, wala sikupigii vinada, nataka uamke uangalie ulimwengu kwa njia mpya kabisa, na hii leo ndio itakua uchambuzi wa darsa yetu.
Kwanza kabisa lazima ikumbukwe Kwenye (Quraan kwenye aya ya 9)imetajwa tukaujaalia usingizi kama kufa,Na kwenye hii aya ya (10)ikaendelea kusema "وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسً۬ا "Tukaujaalia Usiku kuwa ni Guo"(Nguo), Usiku huo huwafunika walale uzuri, wapate faida ya usingizi, sasa kama wewe usiku utakukuta umo kwenye vilabu vya starehe, au unacheza bao mpaka saa tisa za alfajiri, au unatizama senema, au uko kwenye taarab, hiyo ni hiyari yako, usiku huo hauji tena. unakua ushapita.Kuanzia leo kumbuka unakosa kitu muhimu sana katika wingi wa zawadi zitokazo kwa Mollah wako.
Ikaendelea aya ya (11)na kusema "وَجَعَلۡنَا ٱلنَّہَارَ مَعَاشً۬ا "Tukaujaalia Mchana(Muangaza)kama kufufuka".Tendo hili pekee linaweza kukuridhisha kuwa Kiama kipo na kweli utafufuliwa.
Unapokaribia huu Muangaza ndio wakati wako wa kurejea kwenye hiyo (Body) Sasa swali la kujiuliza kwani wewe Nani?.Kujijua wewe nani itabidi uhudhurie sura ya (Sajdah mwanzoni mwa aya ya 9)Inasemaje, "ثُمَّ سَوَّٮٰهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِ" Kisha akamtengeneza na Akampulizia Roho (Inayotokana na) yeye.(Mpaka inapomalizikia aya).
Napenda uijue thamani yako, Napenda kukufahamisha hazina ulo nayo, Napenda ujijue kuwa wewe ndio hiyo (Mysterious Being)ambayo bado hujijui, wewe sio hiyo (Skeleton)Mifupa ilobeba Nyama, wewe ni (Special, Unique Being)ukichanganywa na hiyo nyama na mifupa ndio unaitwa (Human Being)Wewe ni hiyo Roho ilotokana na Mwenye enzi Mungu, kwa sasa hufanyi jitihada za kujijua kwa kuwa unaendelea na usingizi, na wala hufanyi jitihada ukakutana na hiyo (Laiylatul Qadir)umeshughulika na Dunia wakati upande wa Pili kuna hazina yako isokwisha, huko kuna kila kitu ikiwemo kusafishwa na Kusamehewa dhanmbi zako, Utapata Rehma kubwa kubwa, Ukifanya jitihada na bidii na wewe wakati wowote unaweza kuwa walii, unaweza kuwa (Mystic).
Sasa nini kinacho kufanya uendelee kulala na hutaki kuamka, na ukiamka utapata nini?.
Endelea Part 3
Ama ule wa aina ya pili, Ni ule unaporejea Ulimwenguni baada ya kulala ule wa mwanzo, unaona hautoshi bora uendelee kulala, na hivi ndivo ufanyavo umri wako wote. Vipi unalala, kumbuka kazi yangu ni kukuamsha, wala sikupigii vinada, nataka uamke uangalie ulimwengu kwa njia mpya kabisa, na hii leo ndio itakua uchambuzi wa darsa yetu.
Kwanza kabisa lazima ikumbukwe Kwenye (Quraan kwenye aya ya 9)imetajwa tukaujaalia usingizi kama kufa,Na kwenye hii aya ya (10)ikaendelea kusema "وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسً۬ا "Tukaujaalia Usiku kuwa ni Guo"(Nguo), Usiku huo huwafunika walale uzuri, wapate faida ya usingizi, sasa kama wewe usiku utakukuta umo kwenye vilabu vya starehe, au unacheza bao mpaka saa tisa za alfajiri, au unatizama senema, au uko kwenye taarab, hiyo ni hiyari yako, usiku huo hauji tena. unakua ushapita.Kuanzia leo kumbuka unakosa kitu muhimu sana katika wingi wa zawadi zitokazo kwa Mollah wako.
Ikaendelea aya ya (11)na kusema "وَجَعَلۡنَا ٱلنَّہَارَ مَعَاشً۬ا "Tukaujaalia Mchana(Muangaza)kama kufufuka".Tendo hili pekee linaweza kukuridhisha kuwa Kiama kipo na kweli utafufuliwa.
Unapokaribia huu Muangaza ndio wakati wako wa kurejea kwenye hiyo (Body) Sasa swali la kujiuliza kwani wewe Nani?.Kujijua wewe nani itabidi uhudhurie sura ya (Sajdah mwanzoni mwa aya ya 9)Inasemaje, "ثُمَّ سَوَّٮٰهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِ" Kisha akamtengeneza na Akampulizia Roho (Inayotokana na) yeye.(Mpaka inapomalizikia aya).
Napenda uijue thamani yako, Napenda kukufahamisha hazina ulo nayo, Napenda ujijue kuwa wewe ndio hiyo (Mysterious Being)ambayo bado hujijui, wewe sio hiyo (Skeleton)Mifupa ilobeba Nyama, wewe ni (Special, Unique Being)ukichanganywa na hiyo nyama na mifupa ndio unaitwa (Human Being)Wewe ni hiyo Roho ilotokana na Mwenye enzi Mungu, kwa sasa hufanyi jitihada za kujijua kwa kuwa unaendelea na usingizi, na wala hufanyi jitihada ukakutana na hiyo (Laiylatul Qadir)umeshughulika na Dunia wakati upande wa Pili kuna hazina yako isokwisha, huko kuna kila kitu ikiwemo kusafishwa na Kusamehewa dhanmbi zako, Utapata Rehma kubwa kubwa, Ukifanya jitihada na bidii na wewe wakati wowote unaweza kuwa walii, unaweza kuwa (Mystic).
Sasa nini kinacho kufanya uendelee kulala na hutaki kuamka, na ukiamka utapata nini?.
Endelea Part 3
USINGIZI WA ROHO PART 3
Asalaam Aleiykum
Naam sasa turudi nyuma tujue nini kinacho kufanya uendelee kulala wakati ushaamka, na hilo ndio lenye kuchangia matatizo yako yote, ukiweza kulijua hilo na kulimiliki basi utakua Mwenye kufuzu. Sasa Wacha nikurudishe mwanzo pale unapoamka, kitu cha mwanzo kabisa kinatokea wakati ule ni kwanza unakua hujijui, baada ya (seconds)kadhaa unapata fahamu ya kujijua(Jitizame wewe kila ukiamka utaijua siri hii)hapo ndipo inapatikana (Separation)angalia kwa makini, kuwa mtulivu utaiona hali hiyo ambayo mimi naita(Presence)Hali ya uwepo, ni (Gap)ambayo bado huja(Connect)na(Mind)Yako.
Na kama utakua Mtu Mwenye Utulivu wa (Mind)basi unaweza kuona kumbe mimi na (Body)yangu ni vitu viwili tafauti, Na huo ni Muujiza mkubwa, siku utakayoona Mwili wako na wewe upo pembeni unautizama ndio siku utakayo badilika (Forever), wala usishtuke bado hujafa, hiyo ni (Gap)inapatikana kwa (seconds)chache lakini hasara yako huzioni kwa sababu unaruka na kujiunga na Akili moja kwa moja, Na Mollah ameitaja Akili kwa kusema katika sura ya (Qalam aya ya mwanzo)"نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ"
"Nuun"(Naapa kwa )Kalamu na yale waandikayo (Kwa kalamu hizo).
Kalamu yenyewe ndio hiyo Akili yako, sasa hebu ichunguze kalamu yako inaandika nini kwa siku, hiyo (Bio computer) yako inakusanya mambo mangapi kwa siku, kumbuka wewe umo ndani unaletewa taarifa huku umelala, (Mind)au Akili yako ndio yenye kufanya kazi, sasa kila ukiamka unavuta (Mafile)ya jana unaendelea nayo, huku ukitaarisha (Mafile)ya kesho, na hivi ndivo unavoendelea kuuchapa usingizi, (leo Mimi nipo najaribu kushare na wewe ujuzi huu)ili upate kuamka kiroho, huna haja ya kuiachia Akili ikufanyie kazi zote, Pata (direct communication ), ndio maana sasa hivi Sala zako, unakwenda hupo kabisa, unasali sikatai lakini inayokuongoza katika hiyo Sala ni akili, Roho imelala, ndio utajikuta mpaka unatukana ndani ya sala, unafonya, unauza na kununua humo humo kwenye Sala, umefunga sala umesimama unaonesha kidole cha shahada, bado hujijui kama umelala?, Jitizame wewe hata ukila mawazo yako kwengine hata raha ya chakula huoni, uko na mke au mume mekaa pamoja lakini wapi huyu yuko mpirani yule yuko kwenye taarab, halafu unageuka hanipendi, (inasikitisha sana ninapoona wana ndoa wanateseka kwa jambo la kipuuzi)Wengine wamo mpaka Misikitini, Wengine Maimamu lakini bado wamelala, wanadanganya wenzao, viburi vimewashika wanajiona wao ndio wenye kufanya mema, basi hebu amka uchungulie buku lako japo kidogo uone kama kweli unakwenda Peponi?.
Sasa nini kinatokea?, pale unapoamka(Awaken)kila siku unapewa nafasi hii ya kuamka lakini huitaki, wewe unafanya nini? jiangalie pale mwanzo usingizi unapokwisha, baada ya kuhudhuria muujiza uliopo hapo, wewe unarejea tena kulala, unajaribu kufunga macho, unageuka huku na kule, hiyo yote ni ile mbinu ya kujiunga tena na akili na kuendelea na mambo uloyaacha jana. Na Akili ikiona Mzee Kumbe Mvivu,(Watchman)hatizami nyumba yake, Hapo ndipo mfanyakazi anakamata madaraka, anachukua dhamana zote, na huyo mfanyakazi ndio hiyo Akili au (Mind)ambayo inakusanya yote mabaya na mazuri, lakini tabia ya mfanyakazi huyu haipendi mazuri, kwa sababu mazuri yote yanamilikiwa na (Roho), ndio maana utaona mambo mema rahisi kusahauliwa, na yale maovu yanakumbukwa kila mara kwa sababu ya hiyo Akili.
Sasa ufanye nini Mja wewe, kinatakiwa kitu kimoja uzijue mbinu za kumzuia mfanyakazi (Mind)isikutawale(stop the Mind then you are awake). na ukiamka ndio Uwalii, ukiamka ndio ucha Mungu, na nikisema ukiamka usidhani ulilala (Roho)hailali kinacho lala ni kiwiliwili chako(Ndio maana kwenye baadhi ya dua unasema mimi nimedhulumu nafsi dhulma kubwa kabisa)basi ukishaamka hufanyi dhulma tena, tabia zako zitabadilika, sio kwa kulazimisha na kujifanya Mcha Mungu, laa unakua Mcha Mungu (automatic)sio Ucha Mungu wa (wazimu) bali wa haki na mapenzi kwa ajili ya Mollah wako, na hapo kila kitu kinafunguliwa kwako, Riziki zako zitakuja kwa njia isojulikana, Dua zako zitakubaliwa kwa njia ya Maajabu, Sala zako zitakua hazina khitilafu kabisa, Maisha yako yatageuka yatakua ya (Blissful)na kila ataesogea karibu na wewe atakua anapata mambo ya kiajabu, atasikia furaha, mara atacheka, mara atataka kulia hajui nini kimetokea, akiwa karibu na wewe anahisi mambo ya kiajabu yanatokea lakini hajui chanzo chake, na Ulimwengu huu utauona kwa njia nyengine kabisa, kuna mambo yaso mwisho yatafunguliwa kwako, kinachotakiwa (Just)Amka(Then Blessing)(Then Benediction)(Then You are Awaken the rest is History).lakini kumbuka kitu kimoja isimamishe hiyo kalamu kuandika usoyataka. Mie sio mtoa Mawaidha ila ntakukumbusha baadhi ya mambo unayoambiwa yakusaidie kusimamisha kalamu yako, kama dondosha macho yako usitizame vya haramu, funga masikio yako usisikilize haramu, kwa maana nyengi jilinde na mambo ya kipuuzi, kidogo kidogo utaanza kuisimamisha Akili kuandika usoyataka.Na Akili ikisimama (Roho)inaamka, huna haja mpaka upigiwe honi, au uamshwe usingizini, utakua huna haja ya kuambiwa Sala bora kuliko usingizi, utakua unajua Mwenyewe, na huko ndiko kuamka, sio mpaka akwambie mtu, nenda peponi kwa mguu wako mwenyewe.
Na wapi utaanzia mazoezi haya ya kuisimamimsha hiyo Akili, hakuna kwengine isipokua kulifunua guo la usiku, ukanyanyuka nyakati za usiku na kufanya Ibada, kwani wakati huo umetajwa ndani ya (Quraan Muzzamil aya ya 6)
"إِنَّ نَاشِئَةَ ٱلَّيۡلِ هِىَ أَشَدُّ وَطۡـًٔ۬ا وَأَقۡوَمُ قِيلاً "
Hakika kuamka usiku(na kufanya Ibada)kunawafikiana zaidi na moyo, Na maneno (Yake)yanatuwa zaidi.
Msiseme haya ni maneno yangu, aya inathibitisha hapo juu kuhusu kuisimamisha Akili, Angalia vizuri tafsiri ya aya, halafu utizame ukimya wa maneno unasemaje?. Kwanza kwanini uamke?, Kwa sababu unatakiwa ukalale mapema, ukisha kulala mapema hiyo kalamu yako (Akili)inachambua Ma(File)yako yote ya Mchana kutwa, Ikisha unapoamka Akili ina(Stop). Sasa jiulize kwa sababu gani Maneno yanatuwa zaidi, kwa sababu Akili ishaanza kupunguza kazi za uchambuzi, kwa hiyo maneno utakayo yasoma moja kwa moja yanateremka kwenye moyo, na hapo inakua kama ulojifundisha (Baskeli)husahau tena, Mawasiliano ni baina ya (Roho) ilo macho na Nafsi yenye kupokea, ukiigundua hali kama hiyo ukawa unaishi nayo Mchana kutwa, basi wewe utakua (Msalihina, Muttakina,Musabihinna,Mudhakirinna)kila kitu utakua wewe. Pata kuamka Uipate zawadi ya kudumu.
Naam sasa turudi nyuma tujue nini kinacho kufanya uendelee kulala wakati ushaamka, na hilo ndio lenye kuchangia matatizo yako yote, ukiweza kulijua hilo na kulimiliki basi utakua Mwenye kufuzu. Sasa Wacha nikurudishe mwanzo pale unapoamka, kitu cha mwanzo kabisa kinatokea wakati ule ni kwanza unakua hujijui, baada ya (seconds)kadhaa unapata fahamu ya kujijua(Jitizame wewe kila ukiamka utaijua siri hii)hapo ndipo inapatikana (Separation)angalia kwa makini, kuwa mtulivu utaiona hali hiyo ambayo mimi naita(Presence)Hali ya uwepo, ni (Gap)ambayo bado huja(Connect)na(Mind)Yako.
Na kama utakua Mtu Mwenye Utulivu wa (Mind)basi unaweza kuona kumbe mimi na (Body)yangu ni vitu viwili tafauti, Na huo ni Muujiza mkubwa, siku utakayoona Mwili wako na wewe upo pembeni unautizama ndio siku utakayo badilika (Forever), wala usishtuke bado hujafa, hiyo ni (Gap)inapatikana kwa (seconds)chache lakini hasara yako huzioni kwa sababu unaruka na kujiunga na Akili moja kwa moja, Na Mollah ameitaja Akili kwa kusema katika sura ya (Qalam aya ya mwanzo)"نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ"
"Nuun"(Naapa kwa )Kalamu na yale waandikayo (Kwa kalamu hizo).
Kalamu yenyewe ndio hiyo Akili yako, sasa hebu ichunguze kalamu yako inaandika nini kwa siku, hiyo (Bio computer) yako inakusanya mambo mangapi kwa siku, kumbuka wewe umo ndani unaletewa taarifa huku umelala, (Mind)au Akili yako ndio yenye kufanya kazi, sasa kila ukiamka unavuta (Mafile)ya jana unaendelea nayo, huku ukitaarisha (Mafile)ya kesho, na hivi ndivo unavoendelea kuuchapa usingizi, (leo Mimi nipo najaribu kushare na wewe ujuzi huu)ili upate kuamka kiroho, huna haja ya kuiachia Akili ikufanyie kazi zote, Pata (direct communication ), ndio maana sasa hivi Sala zako, unakwenda hupo kabisa, unasali sikatai lakini inayokuongoza katika hiyo Sala ni akili, Roho imelala, ndio utajikuta mpaka unatukana ndani ya sala, unafonya, unauza na kununua humo humo kwenye Sala, umefunga sala umesimama unaonesha kidole cha shahada, bado hujijui kama umelala?, Jitizame wewe hata ukila mawazo yako kwengine hata raha ya chakula huoni, uko na mke au mume mekaa pamoja lakini wapi huyu yuko mpirani yule yuko kwenye taarab, halafu unageuka hanipendi, (inasikitisha sana ninapoona wana ndoa wanateseka kwa jambo la kipuuzi)Wengine wamo mpaka Misikitini, Wengine Maimamu lakini bado wamelala, wanadanganya wenzao, viburi vimewashika wanajiona wao ndio wenye kufanya mema, basi hebu amka uchungulie buku lako japo kidogo uone kama kweli unakwenda Peponi?.
Sasa nini kinatokea?, pale unapoamka(Awaken)kila siku unapewa nafasi hii ya kuamka lakini huitaki, wewe unafanya nini? jiangalie pale mwanzo usingizi unapokwisha, baada ya kuhudhuria muujiza uliopo hapo, wewe unarejea tena kulala, unajaribu kufunga macho, unageuka huku na kule, hiyo yote ni ile mbinu ya kujiunga tena na akili na kuendelea na mambo uloyaacha jana. Na Akili ikiona Mzee Kumbe Mvivu,(Watchman)hatizami nyumba yake, Hapo ndipo mfanyakazi anakamata madaraka, anachukua dhamana zote, na huyo mfanyakazi ndio hiyo Akili au (Mind)ambayo inakusanya yote mabaya na mazuri, lakini tabia ya mfanyakazi huyu haipendi mazuri, kwa sababu mazuri yote yanamilikiwa na (Roho), ndio maana utaona mambo mema rahisi kusahauliwa, na yale maovu yanakumbukwa kila mara kwa sababu ya hiyo Akili.
Sasa ufanye nini Mja wewe, kinatakiwa kitu kimoja uzijue mbinu za kumzuia mfanyakazi (Mind)isikutawale(stop the Mind then you are awake). na ukiamka ndio Uwalii, ukiamka ndio ucha Mungu, na nikisema ukiamka usidhani ulilala (Roho)hailali kinacho lala ni kiwiliwili chako(Ndio maana kwenye baadhi ya dua unasema mimi nimedhulumu nafsi dhulma kubwa kabisa)basi ukishaamka hufanyi dhulma tena, tabia zako zitabadilika, sio kwa kulazimisha na kujifanya Mcha Mungu, laa unakua Mcha Mungu (automatic)sio Ucha Mungu wa (wazimu) bali wa haki na mapenzi kwa ajili ya Mollah wako, na hapo kila kitu kinafunguliwa kwako, Riziki zako zitakuja kwa njia isojulikana, Dua zako zitakubaliwa kwa njia ya Maajabu, Sala zako zitakua hazina khitilafu kabisa, Maisha yako yatageuka yatakua ya (Blissful)na kila ataesogea karibu na wewe atakua anapata mambo ya kiajabu, atasikia furaha, mara atacheka, mara atataka kulia hajui nini kimetokea, akiwa karibu na wewe anahisi mambo ya kiajabu yanatokea lakini hajui chanzo chake, na Ulimwengu huu utauona kwa njia nyengine kabisa, kuna mambo yaso mwisho yatafunguliwa kwako, kinachotakiwa (Just)Amka(Then Blessing)(Then Benediction)(Then You are Awaken the rest is History).lakini kumbuka kitu kimoja isimamishe hiyo kalamu kuandika usoyataka. Mie sio mtoa Mawaidha ila ntakukumbusha baadhi ya mambo unayoambiwa yakusaidie kusimamisha kalamu yako, kama dondosha macho yako usitizame vya haramu, funga masikio yako usisikilize haramu, kwa maana nyengi jilinde na mambo ya kipuuzi, kidogo kidogo utaanza kuisimamisha Akili kuandika usoyataka.Na Akili ikisimama (Roho)inaamka, huna haja mpaka upigiwe honi, au uamshwe usingizini, utakua huna haja ya kuambiwa Sala bora kuliko usingizi, utakua unajua Mwenyewe, na huko ndiko kuamka, sio mpaka akwambie mtu, nenda peponi kwa mguu wako mwenyewe.
Na wapi utaanzia mazoezi haya ya kuisimamimsha hiyo Akili, hakuna kwengine isipokua kulifunua guo la usiku, ukanyanyuka nyakati za usiku na kufanya Ibada, kwani wakati huo umetajwa ndani ya (Quraan Muzzamil aya ya 6)
"إِنَّ نَاشِئَةَ ٱلَّيۡلِ هِىَ أَشَدُّ وَطۡـًٔ۬ا وَأَقۡوَمُ قِيلاً "
Hakika kuamka usiku(na kufanya Ibada)kunawafikiana zaidi na moyo, Na maneno (Yake)yanatuwa zaidi.
Msiseme haya ni maneno yangu, aya inathibitisha hapo juu kuhusu kuisimamisha Akili, Angalia vizuri tafsiri ya aya, halafu utizame ukimya wa maneno unasemaje?. Kwanza kwanini uamke?, Kwa sababu unatakiwa ukalale mapema, ukisha kulala mapema hiyo kalamu yako (Akili)inachambua Ma(File)yako yote ya Mchana kutwa, Ikisha unapoamka Akili ina(Stop). Sasa jiulize kwa sababu gani Maneno yanatuwa zaidi, kwa sababu Akili ishaanza kupunguza kazi za uchambuzi, kwa hiyo maneno utakayo yasoma moja kwa moja yanateremka kwenye moyo, na hapo inakua kama ulojifundisha (Baskeli)husahau tena, Mawasiliano ni baina ya (Roho) ilo macho na Nafsi yenye kupokea, ukiigundua hali kama hiyo ukawa unaishi nayo Mchana kutwa, basi wewe utakua (Msalihina, Muttakina,Musabihinna,Mudhakirinna)kila kitu utakua wewe. Pata kuamka Uipate zawadi ya kudumu.
Friday, March 3, 2017
KIDOLE KINAONESHA MBINGUNI PART 1
Asalaam Aleiykum
Katika Ulimwengu huu kuna vitu Binaadamu lazima uvijue kabla ya Mauti yako, Na kama hufanyi jitihada za kuvijua basi utaondoka kwenye Ulimwengu huu kama ulivokuja, itakua kama alivokufa kuku na wewe hakuna tafauti. Kwanini nikasema hivyo kwa sababu Mwenye enzi Mungu katupa sisi Fahamu za kujijua(Awareness)au Tuite kwa Lugha unayofahamu wewe (Roho), Kwanini nikasema kwa lugha, kwa sababu hujui bado nini hiyo (Roho)Japokua unayo Mwenyewe, Unajua kwa kutumia lugha lakini sio kitendo cha kufahamu.
Sasa nakuchukua kidogo kidogo katika darsa zangu asaa unaweza kuacha kushangaa (Ferry au Forodhani) Na ukaelekeza Mshangao wako kwenye Mbingu, Tembea na mimi kwenye Bustani hii ya kujua mambo ya Sayansi mbili ile ya ndani na nje katika Ulimwengu huu. Mwenye enzi Mungu katutaka sana katika kitabu chake kwa kutuonesha Tufikiri, Tutafakari, tutumie Nyenzo ya Akili ili apate kutufungulia mambo. Na ukiwa na Sayansi hii ya ndani basi mambo mengi unayajua (In-Advance)Kuna vitu vimeumbwa kama Usingizi, Njaa, Uzima, Kuamka, Usiku, Pumzi na mengi katika Ulimwengu huu ya sayansi ya ndani lakini hakuna hata mmoja mwenye kutaka kuingia katika darsa hizo na kujua vipi nalala au vipi naamka, vipi njaa inakuja wakati gani, vipi navuta pumzi, kwani ukiweza kuvijua vitu hivyo ndipo utaweza kujijua kama wewe ni Roho, lakini najua woga uko pale utakapo kutana na ukweli wa Mauti, utakapojua siku zako zimekaribia, ndio maana wengi tunajificha kwenye muziki, tunajificha kwenye mipira, siasa, ulevi, yote hayo ni mambo ya kujishaulisha hii sayansi ya ndani, basi ikiwa hiyo hatuiwezi, kwanini hatuongezi nguvu za Imani kwa kuijua sayansi ya Nje japokua tumefanyiwa na wenzetu ili tupate kuamini.
Miaka Elfu moja na Mia Nne Mwenye enzi Mungu alitutumia kitabu kupitia kwa Mtume wake s.a.w, ndani ya kitabu hicho alisema maneno haya yaliyomo kwenye aya ya 12 sura ya (Talaq).
ٱللَّهُ ٱلَّذِى خَلَقَ سَبۡعَ سَمَـٰوَٲتٍ۬ وَمِنَ ٱلۡأَرۡضِ مِثۡلَهُنَّ يَتَنَزَّلُ ٱلۡأَمۡرُ بَيۡنَہُنَّ لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَىۡءٍ۬ قَدِيرٌ۬ وَأَنَّ ٱللَّهَ قَدۡ أَحَاطَ بِكُلِّ شَىۡءٍ عِلۡمَۢا (١٢
Mwenye Enzi Mungu Ni Yule ambaye ameziumba Mbingu saba, Na Ardhi kuwa mfano wa hizo, Amri (zake) zinashuka baina yao, ili mjue kwamba Mwenye enzi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kila kitu, Na kwamba Mwenye enzi Mungu amekizunguka kila kitu kwa Elimu(Ujuzi)wake.
Katika aya hiyo hapo kuna neno itabidi ulizamie kusudio lake kwa ajili ya kuendelea uzuri na darsa yetu hii, tupia macho sentensi moja pekee isemayo,(Ili Mjue kwamba Mwenye enzi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kila kitu)kulikua na watu wanakitilia shaka kitabu cha Quraan na kukifananisha na (Bible)pale ilipotolewa makosa na (Galileo)aliposema Dunia sio (Centre of Everthings)haiko kati dunia, ila dunia inalizunguka jua, Walikuja juu viongozi baada ya kuona maneno hayo yamekwenda kinyume na kitabu, Wakamwambia abadilishe kauli yake.Kwa miaka mingi watu wakawa wanatafuta kuikosoa Quraan na hayo maneno yaliyomo kwenye hiyo aya ya kusema kuna Ardhi saba. Alosema maneno haya alikua Mwana sayansi wa (Inner science)akiishi Jangwani katika Bara la Arab, hakua na vifaa vyovyote vya kuchungulia huko Mbinguni, hivi majuzi Wanasayansi wa (Outer science) wamekuja na ugunduzi wao na kusema kweli tumeziona Ardhi saba zenye kufatana kwa Tabaka kama zilivo tajwa kwenye Quraan, Yafatilie maelezo hayo ya ugunduzi huo kupitia (NASA) na tafuta uvumbuzi huo wa hivi karibuni wa ardhi saba unaoitwa (Trappist-1planet discovery). tunapewa habari hizi ili kuzidisha Imani zetu, ili kupewa uthibitsho wa haki kuwa yupo Muumbaji, tumeoneshwa mfano wa Ardhi saba na bado hatujui ziko hizo tu au ziko zengine ambazo zimetapakaa kwenye Ulimwengu huu. Sasa Kwanini zikatajwa?.
Endelea part 2
Katika Ulimwengu huu kuna vitu Binaadamu lazima uvijue kabla ya Mauti yako, Na kama hufanyi jitihada za kuvijua basi utaondoka kwenye Ulimwengu huu kama ulivokuja, itakua kama alivokufa kuku na wewe hakuna tafauti. Kwanini nikasema hivyo kwa sababu Mwenye enzi Mungu katupa sisi Fahamu za kujijua(Awareness)au Tuite kwa Lugha unayofahamu wewe (Roho), Kwanini nikasema kwa lugha, kwa sababu hujui bado nini hiyo (Roho)Japokua unayo Mwenyewe, Unajua kwa kutumia lugha lakini sio kitendo cha kufahamu.
Sasa nakuchukua kidogo kidogo katika darsa zangu asaa unaweza kuacha kushangaa (Ferry au Forodhani) Na ukaelekeza Mshangao wako kwenye Mbingu, Tembea na mimi kwenye Bustani hii ya kujua mambo ya Sayansi mbili ile ya ndani na nje katika Ulimwengu huu. Mwenye enzi Mungu katutaka sana katika kitabu chake kwa kutuonesha Tufikiri, Tutafakari, tutumie Nyenzo ya Akili ili apate kutufungulia mambo. Na ukiwa na Sayansi hii ya ndani basi mambo mengi unayajua (In-Advance)Kuna vitu vimeumbwa kama Usingizi, Njaa, Uzima, Kuamka, Usiku, Pumzi na mengi katika Ulimwengu huu ya sayansi ya ndani lakini hakuna hata mmoja mwenye kutaka kuingia katika darsa hizo na kujua vipi nalala au vipi naamka, vipi njaa inakuja wakati gani, vipi navuta pumzi, kwani ukiweza kuvijua vitu hivyo ndipo utaweza kujijua kama wewe ni Roho, lakini najua woga uko pale utakapo kutana na ukweli wa Mauti, utakapojua siku zako zimekaribia, ndio maana wengi tunajificha kwenye muziki, tunajificha kwenye mipira, siasa, ulevi, yote hayo ni mambo ya kujishaulisha hii sayansi ya ndani, basi ikiwa hiyo hatuiwezi, kwanini hatuongezi nguvu za Imani kwa kuijua sayansi ya Nje japokua tumefanyiwa na wenzetu ili tupate kuamini.
Miaka Elfu moja na Mia Nne Mwenye enzi Mungu alitutumia kitabu kupitia kwa Mtume wake s.a.w, ndani ya kitabu hicho alisema maneno haya yaliyomo kwenye aya ya 12 sura ya (Talaq).
ٱللَّهُ ٱلَّذِى خَلَقَ سَبۡعَ سَمَـٰوَٲتٍ۬ وَمِنَ ٱلۡأَرۡضِ مِثۡلَهُنَّ يَتَنَزَّلُ ٱلۡأَمۡرُ بَيۡنَہُنَّ لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَىۡءٍ۬ قَدِيرٌ۬ وَأَنَّ ٱللَّهَ قَدۡ أَحَاطَ بِكُلِّ شَىۡءٍ عِلۡمَۢا (١٢
Mwenye Enzi Mungu Ni Yule ambaye ameziumba Mbingu saba, Na Ardhi kuwa mfano wa hizo, Amri (zake) zinashuka baina yao, ili mjue kwamba Mwenye enzi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kila kitu, Na kwamba Mwenye enzi Mungu amekizunguka kila kitu kwa Elimu(Ujuzi)wake.
Katika aya hiyo hapo kuna neno itabidi ulizamie kusudio lake kwa ajili ya kuendelea uzuri na darsa yetu hii, tupia macho sentensi moja pekee isemayo,(Ili Mjue kwamba Mwenye enzi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kila kitu)kulikua na watu wanakitilia shaka kitabu cha Quraan na kukifananisha na (Bible)pale ilipotolewa makosa na (Galileo)aliposema Dunia sio (Centre of Everthings)haiko kati dunia, ila dunia inalizunguka jua, Walikuja juu viongozi baada ya kuona maneno hayo yamekwenda kinyume na kitabu, Wakamwambia abadilishe kauli yake.Kwa miaka mingi watu wakawa wanatafuta kuikosoa Quraan na hayo maneno yaliyomo kwenye hiyo aya ya kusema kuna Ardhi saba. Alosema maneno haya alikua Mwana sayansi wa (Inner science)akiishi Jangwani katika Bara la Arab, hakua na vifaa vyovyote vya kuchungulia huko Mbinguni, hivi majuzi Wanasayansi wa (Outer science) wamekuja na ugunduzi wao na kusema kweli tumeziona Ardhi saba zenye kufatana kwa Tabaka kama zilivo tajwa kwenye Quraan, Yafatilie maelezo hayo ya ugunduzi huo kupitia (NASA) na tafuta uvumbuzi huo wa hivi karibuni wa ardhi saba unaoitwa (Trappist-1planet discovery). tunapewa habari hizi ili kuzidisha Imani zetu, ili kupewa uthibitsho wa haki kuwa yupo Muumbaji, tumeoneshwa mfano wa Ardhi saba na bado hatujui ziko hizo tu au ziko zengine ambazo zimetapakaa kwenye Ulimwengu huu. Sasa Kwanini zikatajwa?.
Endelea part 2
Subscribe to:
Posts (Atom)