Asalaam Aleiykum
Kuna kitu kila Mwanaadamu anakitafuta kwa kuwa kimempotea, Kitu hichi uwe Kiongozi au Jambazi, Uwe Mkarim au Uwe Katili Mwenye kuwatesa wenzio, Uwe Tajiri Mwenye kumiminika Mapesa kitu hichi sote kimetukaa moyoni na ndio lengo letu muhimu kufanikiwa kukipata.
Watu wengi wanakitafuta kitu hiki kwa njia nyingi tafauti, Na ndio maana utaona unatafuta Utajiri ukiupata mwisho wake unaona hauna faida yoyote na Bado kuna kitu (Missing), Ukitafuta Mke aliye mzuri au Mume aliye (Handsome) ukishampata unaona bado kuna kitu (Missing), Ukipata cheo ukawa Rais au Mbunge au Waziri ukishafanikiwa unaona bado kuna kitu (Missing) sasa sababu za kukitafuta kitu hichi ni tafauti lakini lengo lililojificha ndani ya nafsi ya kila mmoja wetu ni lile lile moja la kukipata hicho kitu, na hiyo ndio (Nature) yetu hata kama utaleta sababu nyenginee.
Fanya ufanyavyo lakini hamu yako na matarijio ni kitu hicho na hakuna chengine, ndio Maana upesi ukiwa Mzee au ukiwa Mgonjwa unakua na Huzuni unaona sasa Mauti yashakaribia na wewe huna hakika kama utakipata kitu hicho au litatokea tukio lengine usilotarajia, ndio maana watu wote wakati wa kufa wanakua wenye kukata tamaa kwa sababu hawajakipata kitu hichi, sababu kwenye Ulimwengu huu ulikua umeshughulika na mambo mengine chungu nzima.
Sasa kwanini ikawa sote tunataraji kitu hichi wakati hatukijui, Jawabu linafatia kitu hichi tunakijua lakini tumekisahau, hatukijui nini kitu hichi katika Ulimwengu huu wa Ardhini, Lakini ndani ya Nafsi zetu tunakikumbuka kitu hichi kipo ndio maana tunafanya jitihada ya kukipata tena. Kumbuka tumeumbwa kwa Nafsi moja iliyotokana na Baba yetu Adam a.s ambayo makaazi yake yalianzia Peponi, (Al-Baqarah 35)
وَقُلۡنَا يَـٰٓـَٔادَمُ ٱسۡكُنۡ أَنتَ وَزَوۡجُكَ ٱلۡجَنَّةَ وَكُلَا مِنۡهَا رَغَدًا حَيۡثُ شِئۡتُمَا وَلَا تَقۡرَبَا هَـٰذِهِ ٱلشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ
"Na tulisema (kumwambia) Ewe Adam kaa wewe na Mkeo katika Bustani hii (peponi), Na kuleni humo maridhawa popote mpendapo, lakini msiukaribie mti huu, msije kuwa miongoni mwa waliodhulumu"(nafsi zao kwa kuziacha Amri za Mwenye enzi Mungu).
Huko ndiko nafsi ilipoonja hicho kitu kinachoitwa (Bliss) au (Joy) ya Peponi na hilo pekee ndilo Walimwengu wote tunalotaraji tulipate lakini njia yake ni ngumu, na hakuna jambo la rahisi usijidanganye, masharti yake yana vishindo, sio kwa kusema tu ukadhani utaipata tunza hii, inatakiwa ufanye bidii kubwa na mapenzi ya kudumu utakapoigundua Njia hiyo ya Mcha Mungu.
Endelea Part 2
Sunday, December 14, 2014
NJIA YA MCHA MUNGU PART 2
Asalaam Aleiykum
Kwa hali tulo nayo sasa hivi sote tumo katika kiza, kila Mtu anapapasa vipi ataiona njia hii, Tunapigana vikumbo Misikitini lakini ni wachache wenye kuigundua njia hii, toa sadaka, jenga visima, jenga misikiti yote hayo ni bure unafanya (Business) ya kuipata njia hii kwa (Cheap)Elewa kitu hichi hakinunuliwi na pesa abadan, kinanunuliwa kwa nafsi yako na wala sivengine, kama huna Ucha Mungu wewe Muflis, na haipatikani ila mpaka uigundue njia hii ikisha Udumu nayo, Na wengi wanaigundua njia hii lakini kila mara inawapotea.
Kwanini Unapotea ? Kutaka kujua kwanini unapotea ndio Darsa yetu inatuchukua katika safari muhimu ili upate kujua (Drugs) au vile vishawishi vinavyo tupoteza na kama unaweza kuviacha basi basi hayo ni mafanikio yako, hata siku ya kufa kwako utakua ni mwenye furaha badala ya huzuni. Jambo hili ni vigumu sana na pia ni Rahisi sana, kati yake kunakaa maamuzi yako ya kuutaka Ucha Mungu.
Jee Unataka kubakia kwenye njia hiyo, Wewe unataka zawadi Maalumu ya Mollah wako ya (Bliss) idumu na wewe milele, basi ikiwa unalitaka hilo kwanza itabidi tujitizame sisi Binaadamu Umbile letu likoje?, Halafu tuanze na kazi ya Mataarisho ya kwenda kwenye njia ya Ucha Mungu.
Mwanaadamu umetokana na Ardhi, Na kila kitu chako ulichoumbiwa kinaitegemea hiyo hiyo Ardhi ili upate kuishi kwenye Ulimwengu huu, Na ukiangalia (System) yako yote Mwanaadamu ina mwenendo wa kula kama tutavyoona katika uchambuzi wetu, Unaona vipi ukila ukashiba hali yako inavokua namna gani, Unapumzika unataka kulala, na mambo mengine ya matamanio ya Kilimwengu, hicho ndio chakula cha kukuweka hai, halafu kuna chakula chengine chenye kukufanya kuishi.
Napenda Uwelewe kuwa Hai na Kuishi ni mambo mawili tafauti, (Mfano)Mgonjwa yuko kwenye (Coma) yuko Hai lakini Haishi, kwa hiyo kuishi kunategemea matendo, Na hayo matendo ndio hicho chakula cha Pili, Tahadhari sana katika hicho chakula cha pili unakula nini?(Banii Israel 36)
"وَلَا تَقۡفُ مَا لَيۡسَ لَكَ بِهِۦ عِلۡمٌۚ إِنَّ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡبَصَرَ وَٱلۡفُؤَادَ كُلُّ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ كَانَ عَنۡهُ مَسۡـُٔولاً۬ "
Wala usifate usiyo na Elimu nayo, Hakika Masikio na Macho na Moyo hivyo vyote vitaulizwa.
Sasa Jitizame unaifata wewe njia ya Ucha Mungu kwa matendo?, Au unafata yale usokua na Elimu nayo(Unapinga Amri za Mwenye Enzi Mungu) yepi hayo unayoyafata wewe?, Sasa unapata dawa kama hii usiitupe japo chungu imeze itakuponesha ni (Gurantee)n hakuna alomeza kidonge hiki akawa asipone.
Tafauti yako Wewe na Mcha Mungu ni ndogo sana, ni kama hivi yeye anajua, wewe hujui, Yeye anayo (Torch) Wewe huna unapita kujipiga na makuta huoni kitu, Yeye ana Elimu yenye manufaa wewe unafata Elimu isiyo na manufaa, Na ukifata Elimu isiyokua na manufaa inakupoteza ima iwe kwenye Dini au Dunia unakua (Split Mind) kama kwenye Dini unaamua kupiga marufuku vitu vyote unasema (Haram) na kama umezama kwenye Dunia vitu vyote unaona Halali unakua huna elimu ya kuvitenganisha, sababu elimu zote unofata ni za kusikia, labda umesikia fulani kasema hivi, au umehadithiwa, Sasa katika Njia hii ya Mwenye Enzi Mungu unatakiwa umfate kwa Makini Mcha Mungu yeye yuko mbele wewe uko nyuma ili upate kuweka Alama pale utakapobakia peke yako ujue wapi pakupita na wapi pakuepuka.
Endelea part 3
Kwa hali tulo nayo sasa hivi sote tumo katika kiza, kila Mtu anapapasa vipi ataiona njia hii, Tunapigana vikumbo Misikitini lakini ni wachache wenye kuigundua njia hii, toa sadaka, jenga visima, jenga misikiti yote hayo ni bure unafanya (Business) ya kuipata njia hii kwa (Cheap)Elewa kitu hichi hakinunuliwi na pesa abadan, kinanunuliwa kwa nafsi yako na wala sivengine, kama huna Ucha Mungu wewe Muflis, na haipatikani ila mpaka uigundue njia hii ikisha Udumu nayo, Na wengi wanaigundua njia hii lakini kila mara inawapotea.
Kwanini Unapotea ? Kutaka kujua kwanini unapotea ndio Darsa yetu inatuchukua katika safari muhimu ili upate kujua (Drugs) au vile vishawishi vinavyo tupoteza na kama unaweza kuviacha basi basi hayo ni mafanikio yako, hata siku ya kufa kwako utakua ni mwenye furaha badala ya huzuni. Jambo hili ni vigumu sana na pia ni Rahisi sana, kati yake kunakaa maamuzi yako ya kuutaka Ucha Mungu.
Jee Unataka kubakia kwenye njia hiyo, Wewe unataka zawadi Maalumu ya Mollah wako ya (Bliss) idumu na wewe milele, basi ikiwa unalitaka hilo kwanza itabidi tujitizame sisi Binaadamu Umbile letu likoje?, Halafu tuanze na kazi ya Mataarisho ya kwenda kwenye njia ya Ucha Mungu.
Mwanaadamu umetokana na Ardhi, Na kila kitu chako ulichoumbiwa kinaitegemea hiyo hiyo Ardhi ili upate kuishi kwenye Ulimwengu huu, Na ukiangalia (System) yako yote Mwanaadamu ina mwenendo wa kula kama tutavyoona katika uchambuzi wetu, Unaona vipi ukila ukashiba hali yako inavokua namna gani, Unapumzika unataka kulala, na mambo mengine ya matamanio ya Kilimwengu, hicho ndio chakula cha kukuweka hai, halafu kuna chakula chengine chenye kukufanya kuishi.
Napenda Uwelewe kuwa Hai na Kuishi ni mambo mawili tafauti, (Mfano)Mgonjwa yuko kwenye (Coma) yuko Hai lakini Haishi, kwa hiyo kuishi kunategemea matendo, Na hayo matendo ndio hicho chakula cha Pili, Tahadhari sana katika hicho chakula cha pili unakula nini?(Banii Israel 36)
"وَلَا تَقۡفُ مَا لَيۡسَ لَكَ بِهِۦ عِلۡمٌۚ إِنَّ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡبَصَرَ وَٱلۡفُؤَادَ كُلُّ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ كَانَ عَنۡهُ مَسۡـُٔولاً۬ "
Wala usifate usiyo na Elimu nayo, Hakika Masikio na Macho na Moyo hivyo vyote vitaulizwa.
Sasa Jitizame unaifata wewe njia ya Ucha Mungu kwa matendo?, Au unafata yale usokua na Elimu nayo(Unapinga Amri za Mwenye Enzi Mungu) yepi hayo unayoyafata wewe?, Sasa unapata dawa kama hii usiitupe japo chungu imeze itakuponesha ni (Gurantee)n hakuna alomeza kidonge hiki akawa asipone.
Tafauti yako Wewe na Mcha Mungu ni ndogo sana, ni kama hivi yeye anajua, wewe hujui, Yeye anayo (Torch) Wewe huna unapita kujipiga na makuta huoni kitu, Yeye ana Elimu yenye manufaa wewe unafata Elimu isiyo na manufaa, Na ukifata Elimu isiyokua na manufaa inakupoteza ima iwe kwenye Dini au Dunia unakua (Split Mind) kama kwenye Dini unaamua kupiga marufuku vitu vyote unasema (Haram) na kama umezama kwenye Dunia vitu vyote unaona Halali unakua huna elimu ya kuvitenganisha, sababu elimu zote unofata ni za kusikia, labda umesikia fulani kasema hivi, au umehadithiwa, Sasa katika Njia hii ya Mwenye Enzi Mungu unatakiwa umfate kwa Makini Mcha Mungu yeye yuko mbele wewe uko nyuma ili upate kuweka Alama pale utakapobakia peke yako ujue wapi pakupita na wapi pakuepuka.
Endelea part 3
NJIA YA MCHA MUNGU PART 3
Asalaam Aleiykum
Katika Njia hii Mcha Mungu katika kutufahamisha hatumii neno (haramu) ila anatumia neno(Haifai) halafu wewe mwenyewe ndio utaamua unautaka Ucha Mungu au huutaki, Kwa kuwa huo Ucha Mungu unakuja kwa njia ya Mapenzi, Na mapenzi hayalazimishwi ila inatakiwa hiyari.
Naam hichi chakula cha Pili ndio hicho kilotajwa katika hiyo aya kuwa Masikio, Macho, na Moyo vyote vitaulizwa, sasa jitizame unakula nini kupitia vitu hivyo?, hakuna mengine ila unakula wewe kwa kusikiliza Maasi yote kutwa nzima, Uongo na Matusi, nyimbo vyote vinakwenda kufanya makaazi kwenye Moyo wako, mpaka unakua vitu hivyo (Automatic) katika mazuungumzo yako, jitizame ukiulizwa japo saa, mtu anakuuliza saa ngapi basi ikiwa tano na dakika tatu, utamwambia na dakika saba, ukimgomba mtoto lazima tusi japo jepesi litakutoka, basi elewa mambo hayo yanaishi moyoni, Yanafanyiwa (Process) moyoni, hiyo ndio huduma ya kwanza kwa kile chakula unachokula, nini kinafanyika ? Matusi na Music kazi yake kubwa ikipita katika Moyo ni kwenda kusimamisha Mshipa wa Matamanio, Ndio maana (Music) au Nyimbo ikipigwa unatingishika sababu ishajenga jukwaa moyoni.
Kuna kitu ndani ya Nafsi yako kina nyanyuka kama Nyoka (Cobra) anavyonyanyuka akipigiwa firimbi, Lakini hili la (Music) wewe hulioni, tafauti yako na (Cobra) inakua hasikii lakini anaona, wewe huoni ila unasikia, Na (Energy) hii ikishanyanyuliwa si Rahisi kupanda juu tena inateremka bondeni ndio maana mawazo mabaya mabaya yanakujia, upo kwenye Sala umerukuu unasoma sura ya (Fatiha), hivyo ndio athari za kusikiliza (Music), Ndio maana utaona kwenye (Dance) watu wanakatika viuno kuashiria kuwa sasa Furaha ya matamanio ishashuka kiunoni, Nyimbo iko kichwani na matamanio yashateremka kiuononi sasa lete mdundo tukimaliza tukakate matamanio.
Na hapo kama wapo wenye kushuhudia, Macho yanakula mpaka kuvimbiwa, Balaa tupu, hii anacheza vile, duuh sauti ile inakuaje lazima nimfatilie, Balaa kubwa wakati ule, muda ukiwa huyaoni yale basi unaamua ukaangalie TV ili uendelee kula kila aina ya maasi, Macho yanakula kila Maasi, Watu wanatembea Utupu, na ghasia zote za (Advertisement) na ikisha ukenda kulala huna usingizi ila moyo unakaa kwenye shift, unaanza kuchambua kwa njia ya ndoto kipi nitapike, kiporo gani nikale kesho, ikisha huyo ukiamka asubuhi unaanza tena, na kama hutizami unakula japo kwa kugusa lakini mwenyewe hujitambui unapeana mikono na wanawake na hivi na vile huku unaendelea kula kwa njia ya matamanio.
Kwa njia hiyo ndivyo tunavyo shiba chakula cha Dhanmbi, Na kwa hilo tutakwenda kuulizwa kwanini hamjafata njia ya Ucha Mungu.
Ipi Njia Hiyo?
Njia yenyewe ni Rahisi sana na pia ni vigumu sana lakini ukiamua unaweza kufanikiwa, ufanye nini ? anza kidogo kidogo kupunguza kusikiliza maasi, nyimbo, matusi, uongo, punguza kutizama mambo ya maasi na kusoma mambo mambo ya habari za kipuuzi, kidogo kidogo ukifanikiwa kuyapunguza mambo hayo utaona Muangaza unaanza kutokea kwenye Moyo, (Torch) ya Ucha Mungu inaanza kukuonesha njia, ni kama chumba chenye kiza ukaleta (Kibatari) au (Taa) na huo muangaza ni kuacha hayo matendo niliyoyataja hapo juu, na siku utakapo pata Muangaza ukawa (Full) katika chumba chako cha moyo, hapo utakua tayari huna wasiwasi unaweza kutizama TV lakini Moyoni kuna (adhkari ya Mollah wako)unaweza kukaa na watu wanatukana lakini matusi yao hayaingii moyoni mwako, unaweza kusikiliza nyimbo lakini hazifiki moyoni mwako zinapita kama sauti nyengine tu, sasa hivi si unasikia ndege, treni, gari lakini yote hayo hayaingii moyoni mwako na siku utakayopata (Taa) ya Ucha Mungu utakua na hali kama hiyo, hapo tena utabadilika utakua hukai katika mambo hayo, hutizami mambo hayo, husikilizi mambo hayo, lakini huyaogopi kwa sababu hayakai moyoni mwako, hayana nafasi tena ya kukutawala, ila wewe umeyatawala, na huo ndio Ukhalifa, huo ndio Ucha Mungu. Tunamuomba Mollah atujaalie kutufiksha katika njia hiyo.
Katika Njia hii Mcha Mungu katika kutufahamisha hatumii neno (haramu) ila anatumia neno(Haifai) halafu wewe mwenyewe ndio utaamua unautaka Ucha Mungu au huutaki, Kwa kuwa huo Ucha Mungu unakuja kwa njia ya Mapenzi, Na mapenzi hayalazimishwi ila inatakiwa hiyari.
Naam hichi chakula cha Pili ndio hicho kilotajwa katika hiyo aya kuwa Masikio, Macho, na Moyo vyote vitaulizwa, sasa jitizame unakula nini kupitia vitu hivyo?, hakuna mengine ila unakula wewe kwa kusikiliza Maasi yote kutwa nzima, Uongo na Matusi, nyimbo vyote vinakwenda kufanya makaazi kwenye Moyo wako, mpaka unakua vitu hivyo (Automatic) katika mazuungumzo yako, jitizame ukiulizwa japo saa, mtu anakuuliza saa ngapi basi ikiwa tano na dakika tatu, utamwambia na dakika saba, ukimgomba mtoto lazima tusi japo jepesi litakutoka, basi elewa mambo hayo yanaishi moyoni, Yanafanyiwa (Process) moyoni, hiyo ndio huduma ya kwanza kwa kile chakula unachokula, nini kinafanyika ? Matusi na Music kazi yake kubwa ikipita katika Moyo ni kwenda kusimamisha Mshipa wa Matamanio, Ndio maana (Music) au Nyimbo ikipigwa unatingishika sababu ishajenga jukwaa moyoni.
Kuna kitu ndani ya Nafsi yako kina nyanyuka kama Nyoka (Cobra) anavyonyanyuka akipigiwa firimbi, Lakini hili la (Music) wewe hulioni, tafauti yako na (Cobra) inakua hasikii lakini anaona, wewe huoni ila unasikia, Na (Energy) hii ikishanyanyuliwa si Rahisi kupanda juu tena inateremka bondeni ndio maana mawazo mabaya mabaya yanakujia, upo kwenye Sala umerukuu unasoma sura ya (Fatiha), hivyo ndio athari za kusikiliza (Music), Ndio maana utaona kwenye (Dance) watu wanakatika viuno kuashiria kuwa sasa Furaha ya matamanio ishashuka kiunoni, Nyimbo iko kichwani na matamanio yashateremka kiuononi sasa lete mdundo tukimaliza tukakate matamanio.
Na hapo kama wapo wenye kushuhudia, Macho yanakula mpaka kuvimbiwa, Balaa tupu, hii anacheza vile, duuh sauti ile inakuaje lazima nimfatilie, Balaa kubwa wakati ule, muda ukiwa huyaoni yale basi unaamua ukaangalie TV ili uendelee kula kila aina ya maasi, Macho yanakula kila Maasi, Watu wanatembea Utupu, na ghasia zote za (Advertisement) na ikisha ukenda kulala huna usingizi ila moyo unakaa kwenye shift, unaanza kuchambua kwa njia ya ndoto kipi nitapike, kiporo gani nikale kesho, ikisha huyo ukiamka asubuhi unaanza tena, na kama hutizami unakula japo kwa kugusa lakini mwenyewe hujitambui unapeana mikono na wanawake na hivi na vile huku unaendelea kula kwa njia ya matamanio.
Kwa njia hiyo ndivyo tunavyo shiba chakula cha Dhanmbi, Na kwa hilo tutakwenda kuulizwa kwanini hamjafata njia ya Ucha Mungu.
Ipi Njia Hiyo?
Njia yenyewe ni Rahisi sana na pia ni vigumu sana lakini ukiamua unaweza kufanikiwa, ufanye nini ? anza kidogo kidogo kupunguza kusikiliza maasi, nyimbo, matusi, uongo, punguza kutizama mambo ya maasi na kusoma mambo mambo ya habari za kipuuzi, kidogo kidogo ukifanikiwa kuyapunguza mambo hayo utaona Muangaza unaanza kutokea kwenye Moyo, (Torch) ya Ucha Mungu inaanza kukuonesha njia, ni kama chumba chenye kiza ukaleta (Kibatari) au (Taa) na huo muangaza ni kuacha hayo matendo niliyoyataja hapo juu, na siku utakapo pata Muangaza ukawa (Full) katika chumba chako cha moyo, hapo utakua tayari huna wasiwasi unaweza kutizama TV lakini Moyoni kuna (adhkari ya Mollah wako)unaweza kukaa na watu wanatukana lakini matusi yao hayaingii moyoni mwako, unaweza kusikiliza nyimbo lakini hazifiki moyoni mwako zinapita kama sauti nyengine tu, sasa hivi si unasikia ndege, treni, gari lakini yote hayo hayaingii moyoni mwako na siku utakayopata (Taa) ya Ucha Mungu utakua na hali kama hiyo, hapo tena utabadilika utakua hukai katika mambo hayo, hutizami mambo hayo, husikilizi mambo hayo, lakini huyaogopi kwa sababu hayakai moyoni mwako, hayana nafasi tena ya kukutawala, ila wewe umeyatawala, na huo ndio Ukhalifa, huo ndio Ucha Mungu. Tunamuomba Mollah atujaalie kutufiksha katika njia hiyo.
Sunday, December 7, 2014
ELIMU ZA AJABU PART 4
Asalaam Aleiykum
Tunaendelea kutafuta kuifahamu japo kwa uchache elimu hii ya kuruka, na hakuna chengine kitotupa taarifa ya jambo hili ila tumuulize Mfalme wa (Mysticism) Nabii Suleiman a.s yeye alipewa nini? Quraan Sura ya (Saba aya ya 12)
وَلِسُلَيۡمَـٰنَ ٱلرِّيحَ غُدُوُّهَا شَہۡرٌ۬ وَرَوَاحُهَا شَہۡرٌ۬ۖ وَأَسَلۡنَا لَهُ ۥ عَيۡنَ ٱلۡقِطۡرِۖ وَمِنَ ٱلۡجِنِّ مَن يَعۡمَلُ بَيۡنَ يَدَيۡهِ بِإِذۡنِ رَبِّهِۖۦ وَمَن يَزِغۡ مِنۡہُمۡ عَنۡ أَمۡرِنَا نُذِقۡهُ مِنۡ عَذَابِ ٱلسَّعِيرِ
"Na Kwa Suleiman(Tulimpa amri ya elimu ya)Upepo(Uliokwenda)Safari yake ya asubuhi(Kasi yake ni mwendo)wa mwezi mmoja, Na Safari yake ya jioni(Kasi yake ni mwendo wa)mwezi mmoja, Na tukamyayushia chem chem ya Shaba, Na katika Majini(Kulikuwapo)waliofanya kazi mbele yake kwa idhini ya Mwenye Enzi Mungu wake, Na kila anyejitenga(Akataka kutoroka)na amri yetu miongoni mwao tunamuonjesha adhabu ya moto uwakao."
Hivi ndivo tunavyojulishwa na Quraan kuwa jambo hilo lipo na linawezekana na wapo mpaka leo wanopewa taaluma hiyo adhimu ya kuweza (Kupaa angani), Walipewa pia Baadhi ya majini na Binaadamu katika zama hizo elimu tafauti kama tutakavo soma tukiendelea kuzichambua elimu hizi za Ajabu.
Sasa wacha tuiangalie Elimu hii ya kuruka au kupaa kama ndege ikoje, kwanza itatubidi tujiulize kwanini ukatajwa upepo? jee habari hizi zinatujulisha ndege za zama hizo? jee (Technology)hiyo bado ipo, Jawabu naam elimu hii bado ipo japo walo nayo kwa zama hizi wachache sana.
Nini Upepo? Upepo ni (Transport system)ya Ardhi yetu hii, Upepo kwa njia ya Rehma za Mwenye enzi Mungu ndio wenye kusafirisha maji kwa njia ya mawingu yakatolewa sehemu moja kupelekwa sehemu nyengine(Mvua) Upepo unasafirisha Mimea, upepo ndio tegemeo la vyombo vyote vya usafiri wa nchi kavu, majini na angani, hivyo vyote vinategemea upepo kwa njia tafauti kuweza kutekeleza kazi zake.
Na hizi Pepo zipo tafauti zipo za Misimu ya (Local, National, na Inaternational)zipo zinazoletwa kwa ghafla na zipo zinazodumu katika njia zake daima, zipo pepo hii za masafa marefu na masafa mafupi, zipo za juu sana na katikati pia na chini kabisa ambazo vyombo vyetu vya usafiri kama Jahazi ndivyo vinautegemea baada ya kubeba Marobota ya katani, na vyuma na saruji ikisha wakafunga kipande cha kitambaa hao kuelekea Mombasa kwa kutegemea upepo ambao hawana Amri nao wala kuwa na ujuzi nao sasa nini habari yako wewe kama utapata Elimu hii ya upepo na nini cha kufanya?.
Endelea Part 5
Tunaendelea kutafuta kuifahamu japo kwa uchache elimu hii ya kuruka, na hakuna chengine kitotupa taarifa ya jambo hili ila tumuulize Mfalme wa (Mysticism) Nabii Suleiman a.s yeye alipewa nini? Quraan Sura ya (Saba aya ya 12)
وَلِسُلَيۡمَـٰنَ ٱلرِّيحَ غُدُوُّهَا شَہۡرٌ۬ وَرَوَاحُهَا شَہۡرٌ۬ۖ وَأَسَلۡنَا لَهُ ۥ عَيۡنَ ٱلۡقِطۡرِۖ وَمِنَ ٱلۡجِنِّ مَن يَعۡمَلُ بَيۡنَ يَدَيۡهِ بِإِذۡنِ رَبِّهِۖۦ وَمَن يَزِغۡ مِنۡہُمۡ عَنۡ أَمۡرِنَا نُذِقۡهُ مِنۡ عَذَابِ ٱلسَّعِيرِ
"Na Kwa Suleiman(Tulimpa amri ya elimu ya)Upepo(Uliokwenda)Safari yake ya asubuhi(Kasi yake ni mwendo)wa mwezi mmoja, Na Safari yake ya jioni(Kasi yake ni mwendo wa)mwezi mmoja, Na tukamyayushia chem chem ya Shaba, Na katika Majini(Kulikuwapo)waliofanya kazi mbele yake kwa idhini ya Mwenye Enzi Mungu wake, Na kila anyejitenga(Akataka kutoroka)na amri yetu miongoni mwao tunamuonjesha adhabu ya moto uwakao."
Hivi ndivo tunavyojulishwa na Quraan kuwa jambo hilo lipo na linawezekana na wapo mpaka leo wanopewa taaluma hiyo adhimu ya kuweza (Kupaa angani), Walipewa pia Baadhi ya majini na Binaadamu katika zama hizo elimu tafauti kama tutakavo soma tukiendelea kuzichambua elimu hizi za Ajabu.
Sasa wacha tuiangalie Elimu hii ya kuruka au kupaa kama ndege ikoje, kwanza itatubidi tujiulize kwanini ukatajwa upepo? jee habari hizi zinatujulisha ndege za zama hizo? jee (Technology)hiyo bado ipo, Jawabu naam elimu hii bado ipo japo walo nayo kwa zama hizi wachache sana.
Nini Upepo? Upepo ni (Transport system)ya Ardhi yetu hii, Upepo kwa njia ya Rehma za Mwenye enzi Mungu ndio wenye kusafirisha maji kwa njia ya mawingu yakatolewa sehemu moja kupelekwa sehemu nyengine(Mvua) Upepo unasafirisha Mimea, upepo ndio tegemeo la vyombo vyote vya usafiri wa nchi kavu, majini na angani, hivyo vyote vinategemea upepo kwa njia tafauti kuweza kutekeleza kazi zake.
Na hizi Pepo zipo tafauti zipo za Misimu ya (Local, National, na Inaternational)zipo zinazoletwa kwa ghafla na zipo zinazodumu katika njia zake daima, zipo pepo hii za masafa marefu na masafa mafupi, zipo za juu sana na katikati pia na chini kabisa ambazo vyombo vyetu vya usafiri kama Jahazi ndivyo vinautegemea baada ya kubeba Marobota ya katani, na vyuma na saruji ikisha wakafunga kipande cha kitambaa hao kuelekea Mombasa kwa kutegemea upepo ambao hawana Amri nao wala kuwa na ujuzi nao sasa nini habari yako wewe kama utapata Elimu hii ya upepo na nini cha kufanya?.
Endelea Part 5
ELIMU ZA AJABU PART 5
Asalaam Aleiykum
Halafu kuna upepo mwengine ambao mmeugundua karne hii tulonayo labda miaka 40 na ushei ambao upo takriban ya masafa ni kama (Mile) Saba kwa juu, mkauita (Jet Stream)ambao unaizunguka dunia ambapo hata hizi ndege zirukazo zinautegemea katika kuruka nk, Kwa hiyo wakati wa Nabii Suleiman a.s na yeye alipata Elimu ya kufahamishwa (Mystic Stream)na mpaka leo wapo wenye kuigundua Elimu hii ya Kuruka ama kwa kuitafuta au kwa bahati unakumbana nayo, kwa hiyo zile hadithi ulokua unasikia Walii fulani kaachwa Mangapwani au Bagamoyo mkamkuta kafika mjini mwanzo bila ya gari usije ukashangaa.
Nini Kinatokea huyo katumia Elimu yake ya siri ya kupaa hewani, na safari hii ni nzuri hata kupita hizi safari za ndege au hiyo gari unayopanda. Na kwanini isiwe hivyo wakati wale wanoishi nchi za Ulaya wanajua kuwa Mtu anatengeneza (Kishada) au (Kite) au (Hang Glider) akenda kwenye Kilima au kichuguu na kujifunga mgongoni au kwenye mabega na kujiachia akacheza angani kwa masaa huku akipunga mkono, Kwa hiyo Elimu ya Kuruka ipo inatakiwa utekeleze masharti yake ili uweze kuimiliki, na ntalisema hili sharti moja na kuyaacha mengine ili watu wasije wakadhurika, Sharti lenyewe kwanza lazima umiliki elimu ya (Levitation) katika Ulimwengu huu zipo Elimu mbili moja inayotuweka kwenye Ardhi ambayo ni (Gravitation) na hii ya pili ni hiyo (Levitation) ya kupaa ukiweza kunyanyuka ukaugundua Upepo wa (Mystic Jet stream) na wewe utakua unafanya safari zako bila ya wasiwasi, lakini kikwazo chenyewe huwezi kupata elimu ya (Levitation) mpaka uipate elimu ya kupotea, ndani ya elimu hiyo ndio wanaishi Majini kama inavotaja aya ya 27 sura ya (Al-Aaraf)mpaka inapoishia.
إِنَّهُ ۥ يَرَٮٰكُمۡ هُوَ وَقَبِيلُهُ ۥ مِنۡ حَيۡثُ لَا تَرَوۡنَہُمۡۗ
"Hakika yeye(Ibilis) pamoja na Kabila yake wanakuoneni, na hali ya kuwa(Nyinyi) hamuwaoni".
Hiyo ndio Elimu ya Ulimwengu wa majini wanaishi ndani yake kwa kutoonekana, hiyo ndio elimu ya kupotea, ipo kama vile mithili ya moto mwanzo unakua haupo na mara unauwasha unatokezea, ikisha ukiuzima unapotea sasa jiulize mwanzo ulikua wapi? na sasa umekwenda wapi?, ukijua jawabu lake basi utakua ushaanza kuipata elimu hii ya kupaa, ndio maana ukaambiwa Majini kwao Rahisi kuruka kwa kuwa wameumbwa kwa Moto Baridi, na wewe potea ukakutane na moto baridi ukoje? Potea ukakutane na elimu hii ya (Levitation), itakua Rahisi kuanza kusafiri kama wafanyavyo Mawalii (Mystic) na baadhi ya wengine wenye kutumia elimu hizi kwa ufisadi.
Endelea part 6
Halafu kuna upepo mwengine ambao mmeugundua karne hii tulonayo labda miaka 40 na ushei ambao upo takriban ya masafa ni kama (Mile) Saba kwa juu, mkauita (Jet Stream)ambao unaizunguka dunia ambapo hata hizi ndege zirukazo zinautegemea katika kuruka nk, Kwa hiyo wakati wa Nabii Suleiman a.s na yeye alipata Elimu ya kufahamishwa (Mystic Stream)na mpaka leo wapo wenye kuigundua Elimu hii ya Kuruka ama kwa kuitafuta au kwa bahati unakumbana nayo, kwa hiyo zile hadithi ulokua unasikia Walii fulani kaachwa Mangapwani au Bagamoyo mkamkuta kafika mjini mwanzo bila ya gari usije ukashangaa.
Nini Kinatokea huyo katumia Elimu yake ya siri ya kupaa hewani, na safari hii ni nzuri hata kupita hizi safari za ndege au hiyo gari unayopanda. Na kwanini isiwe hivyo wakati wale wanoishi nchi za Ulaya wanajua kuwa Mtu anatengeneza (Kishada) au (Kite) au (Hang Glider) akenda kwenye Kilima au kichuguu na kujifunga mgongoni au kwenye mabega na kujiachia akacheza angani kwa masaa huku akipunga mkono, Kwa hiyo Elimu ya Kuruka ipo inatakiwa utekeleze masharti yake ili uweze kuimiliki, na ntalisema hili sharti moja na kuyaacha mengine ili watu wasije wakadhurika, Sharti lenyewe kwanza lazima umiliki elimu ya (Levitation) katika Ulimwengu huu zipo Elimu mbili moja inayotuweka kwenye Ardhi ambayo ni (Gravitation) na hii ya pili ni hiyo (Levitation) ya kupaa ukiweza kunyanyuka ukaugundua Upepo wa (Mystic Jet stream) na wewe utakua unafanya safari zako bila ya wasiwasi, lakini kikwazo chenyewe huwezi kupata elimu ya (Levitation) mpaka uipate elimu ya kupotea, ndani ya elimu hiyo ndio wanaishi Majini kama inavotaja aya ya 27 sura ya (Al-Aaraf)mpaka inapoishia.
إِنَّهُ ۥ يَرَٮٰكُمۡ هُوَ وَقَبِيلُهُ ۥ مِنۡ حَيۡثُ لَا تَرَوۡنَہُمۡۗ
"Hakika yeye(Ibilis) pamoja na Kabila yake wanakuoneni, na hali ya kuwa(Nyinyi) hamuwaoni".
Hiyo ndio Elimu ya Ulimwengu wa majini wanaishi ndani yake kwa kutoonekana, hiyo ndio elimu ya kupotea, ipo kama vile mithili ya moto mwanzo unakua haupo na mara unauwasha unatokezea, ikisha ukiuzima unapotea sasa jiulize mwanzo ulikua wapi? na sasa umekwenda wapi?, ukijua jawabu lake basi utakua ushaanza kuipata elimu hii ya kupaa, ndio maana ukaambiwa Majini kwao Rahisi kuruka kwa kuwa wameumbwa kwa Moto Baridi, na wewe potea ukakutane na moto baridi ukoje? Potea ukakutane na elimu hii ya (Levitation), itakua Rahisi kuanza kusafiri kama wafanyavyo Mawalii (Mystic) na baadhi ya wengine wenye kutumia elimu hizi kwa ufisadi.
Endelea part 6
ELIMU ZA AJABU PART 6
Asalaam Aleiykum
Tunaendelea kupata habari hizi za elimu ya kuruka na napenda kukumbusha uelewe safari hii inafanyika nyakati za usiku, kwa kuwa ndio wakati muafaka wa kuingia katika (zone) ya (Levitation).
Ama kuhusu Elimu ya kupotea hii ni vigumu kufahamika kutokana na uhusiano wake wa karibu na Sayansi ya zama hizi, kama umeshawahi kusikia Sayansi ya (Time Travel)ambayo inazungumzwa na Wanasayansi wa kileo basi hiyo ndio elimu ya kupotea, ambayo wanasayansi wa kisasa wameigundua inawezekana lakini bado hawajajua inafanyika vipi, Na ndiyo ilotumika wakati wa Nabii Suleiman a.s kama ilivyotajwa katika Quraan sura ya (Naml) aya ya 38 mpaka 40,
قَالَ يَـٰٓأَيُّہَا ٱلۡمَلَؤُاْ أَيُّكُمۡ يَأۡتِينِى بِعَرۡشِہَا قَبۡلَ أَن يَأۡتُونِى مُسۡلِمِينَ
(Nabii Suleiman a.s akawakusanya wazee wa Baraza lake la Hekima)"akasema Enyi Wakuu ni nani atakayeniletea kiti chake cha enzi kabla hawajakuja kwangu, hali ya kuwa wamekwisha kusilimu.
قَالَ عِفۡرِيتٌ۬ مِّنَ ٱلۡجِنِّ أَنَا۟ ءَاتِيكَ بِهِۦ قَبۡلَ أَن تَقُومَ مِن مَّقَامِكَۖ وَإِنِّى عَلَيۡهِ لَقَوِىٌّ أَمِينٌ۬
Mjasiri(Ifrit) mmoja wa Majini akasema"Mimi nitakuletea kabla hujainuka mahali pako hapo(Ulipokaa) na mimi bila shaka ninazo nguvu za hayo (na) ni Muaminifu.
قَالَ ٱلَّذِى عِندَهُ ۥ عِلۡمٌ۬ مِّنَ ٱلۡكِتَـٰبِ أَنَا۟ ءَاتِيكَ بِهِۦ قَبۡلَ أَن يَرۡتَدَّ إِلَيۡكَ طَرۡفُكَۚ فَلَمَّا رَءَاهُ مُسۡتَقِرًّا عِندَهُ ۥ قَالَ هَـٰذَا مِن فَضۡلِ رَبِّى لِيَبۡلُوَنِىٓ ءَأَشۡكُرُ أَمۡ أَكۡفُرُۖ وَمَن شَكَرَ فَإِنَّمَا يَشۡكُرُ لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ رَبِّى غَنِىٌّ۬ كَرِيمٌ۬
Akasema Yule aliyekuwa na (Elimu) Ya kitabu, Mimi nitakuletea kabla ya kupepesa jicho lako(Kufumba na kufumbua) Basi alipokiona kimewekwa mbele yake alinena, Haya ni kwa fadhila za Mollah wangu, ili anijaribu nitashukuru au (nitakuwa mwizi wa Fadhila)Kukufuru, Na anaye shukuru, anashukuru kwa manufaa ya nafsi yake, na anayekufuru, kwa hakika Mollah wangu ni Mkwasi na Karimu.
Hiyo ndio Elimu ya Kitabu, elimu ya kuukunja (Wakati na Sehemu)(Appear and Dis-Appear) sio Mazingaombwe(Uchawi) Mnahadithiwa habari hizi za Mawalii(Mystic) mlokua mkisikia wanatiwa Gerezani lakini Usiku wanalala nyumbani, sala ya Alfajiri anasali msikitini halafu huyo anarejea (Mahabusu). Na Ukiipata Elimu hii ndio ushapata elimu ya kuonana na Majini na mambo mengine ya Ajabu, Unaweza sasa kuingia na kutoka Ughaibuni bila ya Mtu kujua, unaweza hata kumsoma Mtu Akili nini anawaza, Ametukuka Mwenye Enzi Mungu Mwenye kutukirimu elimu hizi za Ajabu.
Ama kuhusu Elimu ya kutibu wengine wanadhani huyo anataka kutibu Malaria akiwa mbali, kusudio langu ni kuzungumzia Elimu yenye kutibu tafrani hususan zenye kuhusiana na dhiki za Moyo na Akili, Na hili ni tendo ambalo wanaweza kufanya wale walopewa Hijaza na Mollah wao hata wakiwa mbali kwa kutumia sauti zao wakaponesha baadhi ya maradhi na kuondosha misukosuko ya dhiki za Moyo, ni jambo linalowezekana, kwanini lisiwezekane wakati unaweza kumsikia mtu kwenye simu aliyeko mbali bila ya waya kukamatana, na kama akikwambia nyumba yako imeungua unaanza kutokwa na machozi, na akikwambia nakulipa deni lako unajawa na furaha, nini kinatokezea? kinachotokezea hapo ndicho kile kile(Chenye kutokezea kwenye Dua), Na yule mwenye kujua kuponesha akajua kuitumia (Universal Mind)Ambayo hii tutaizungumza siku za mbele kwenye (Majaaliwa) basi anaweza kukutibu hata akiwa mbali, kwani maradhi ni yale yale anayotibu aliye karibu, au anayeomba aliyekaribu yote yanategemeana na mfumo wa (Dua) ndio maana wengine wanarekodiwa (CD) na kutibiwa, ni jambo linalowezekana na wala halina (Mushkeli wowote).
Ama kuhusu Elimu ya Kungara hii sitokwenda ndani sana kutokana vielelezo vyake ni virefu, lakini nitasema kwa kifupi Elimu hii inategemea vipi utaweza (kujikurubisha) au kuji(Tune) na mionzi ya Jua, na ukiweza kupata taaluma hii na wewe utakua unangara kama (Taa) na ukiwa mwanasiasa au Mtu wa kupenda vyeo hapo tena chaguzi zote unashinda wewe, na kila atokua karibu yako atakua mwenye kuvutiwa na wewe, lakini elimu hii ina kasoro zake na mbili katika kasoro hizo (Watu watakuwa wanavutiwa na wewe kimatamanio) Na kama huwezi kujizuia utakua na wapenzi hata elfu, na kasoro ya pili utakua katika hali ya umoto baridi (Mithili ya Majini), kwa hiyo utakua unaishi katika Ulimengu wa (Hasira) nyakati zote kwa kuwa sio (Nature yako).
Ama hii Elimu ya kutisha ni kama hiyo ya kungara ila hii imeambatana na (usiku) Giza, si unaona kila mtu anaogopa giza, ukiweza kuambatana ukaingia ndani ya (Dark matter)ukauingia usiku ukakuvaa, basi utakua unatisha mpaka watoto wako wakikuona watakukimbia, lakini ukifunikwa na mionzi ya giza tahadhari kwani utakumbwa na uvivu usiweze hata kunyanyuka kitandani, sababu kiza kinaletewa watu kupumzika na wewe unakitumia wakati wa mchana, kiza kishaondoka wewe umebaki na kivuli chake unatishia watu, hizo ni baadhi ya elimu za ajabu ambazo ziko nyingi, Na kama inavosema aya ikiwa utazitumia kwa manufaa ya uzuri basi ni fadhila kubwa kutoka kwa Mollah wako, lakini ukizitumia kwa ufisadi basi utakua umeangamia na kukufuru kukubwa, kwa sababu utakua unazitumia kinyume cha sheria.
Haya ni kwa ajili ya kukujulisheni uwapo wa Elimu hizi lakini cha muhimu zaidi ni kumuabudu Mollah wako na umuachie Mwenyewe ikiwa Kakupa Elimu hizi basi zitumie kwa manufaa na ukinyimwa basi shukuru wala usihangaike sababu utakua unanusuriwa na mengi. "Na wala hatukukupeni Elimu zetu isipoua kwa Uchache tu".
Tunaendelea kupata habari hizi za elimu ya kuruka na napenda kukumbusha uelewe safari hii inafanyika nyakati za usiku, kwa kuwa ndio wakati muafaka wa kuingia katika (zone) ya (Levitation).
Ama kuhusu Elimu ya kupotea hii ni vigumu kufahamika kutokana na uhusiano wake wa karibu na Sayansi ya zama hizi, kama umeshawahi kusikia Sayansi ya (Time Travel)ambayo inazungumzwa na Wanasayansi wa kileo basi hiyo ndio elimu ya kupotea, ambayo wanasayansi wa kisasa wameigundua inawezekana lakini bado hawajajua inafanyika vipi, Na ndiyo ilotumika wakati wa Nabii Suleiman a.s kama ilivyotajwa katika Quraan sura ya (Naml) aya ya 38 mpaka 40,
قَالَ يَـٰٓأَيُّہَا ٱلۡمَلَؤُاْ أَيُّكُمۡ يَأۡتِينِى بِعَرۡشِہَا قَبۡلَ أَن يَأۡتُونِى مُسۡلِمِينَ
(Nabii Suleiman a.s akawakusanya wazee wa Baraza lake la Hekima)"akasema Enyi Wakuu ni nani atakayeniletea kiti chake cha enzi kabla hawajakuja kwangu, hali ya kuwa wamekwisha kusilimu.
قَالَ عِفۡرِيتٌ۬ مِّنَ ٱلۡجِنِّ أَنَا۟ ءَاتِيكَ بِهِۦ قَبۡلَ أَن تَقُومَ مِن مَّقَامِكَۖ وَإِنِّى عَلَيۡهِ لَقَوِىٌّ أَمِينٌ۬
Mjasiri(Ifrit) mmoja wa Majini akasema"Mimi nitakuletea kabla hujainuka mahali pako hapo(Ulipokaa) na mimi bila shaka ninazo nguvu za hayo (na) ni Muaminifu.
قَالَ ٱلَّذِى عِندَهُ ۥ عِلۡمٌ۬ مِّنَ ٱلۡكِتَـٰبِ أَنَا۟ ءَاتِيكَ بِهِۦ قَبۡلَ أَن يَرۡتَدَّ إِلَيۡكَ طَرۡفُكَۚ فَلَمَّا رَءَاهُ مُسۡتَقِرًّا عِندَهُ ۥ قَالَ هَـٰذَا مِن فَضۡلِ رَبِّى لِيَبۡلُوَنِىٓ ءَأَشۡكُرُ أَمۡ أَكۡفُرُۖ وَمَن شَكَرَ فَإِنَّمَا يَشۡكُرُ لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ رَبِّى غَنِىٌّ۬ كَرِيمٌ۬
Akasema Yule aliyekuwa na (Elimu) Ya kitabu, Mimi nitakuletea kabla ya kupepesa jicho lako(Kufumba na kufumbua) Basi alipokiona kimewekwa mbele yake alinena, Haya ni kwa fadhila za Mollah wangu, ili anijaribu nitashukuru au (nitakuwa mwizi wa Fadhila)Kukufuru, Na anaye shukuru, anashukuru kwa manufaa ya nafsi yake, na anayekufuru, kwa hakika Mollah wangu ni Mkwasi na Karimu.
Hiyo ndio Elimu ya Kitabu, elimu ya kuukunja (Wakati na Sehemu)(Appear and Dis-Appear) sio Mazingaombwe(Uchawi) Mnahadithiwa habari hizi za Mawalii(Mystic) mlokua mkisikia wanatiwa Gerezani lakini Usiku wanalala nyumbani, sala ya Alfajiri anasali msikitini halafu huyo anarejea (Mahabusu). Na Ukiipata Elimu hii ndio ushapata elimu ya kuonana na Majini na mambo mengine ya Ajabu, Unaweza sasa kuingia na kutoka Ughaibuni bila ya Mtu kujua, unaweza hata kumsoma Mtu Akili nini anawaza, Ametukuka Mwenye Enzi Mungu Mwenye kutukirimu elimu hizi za Ajabu.
Ama kuhusu Elimu ya kutibu wengine wanadhani huyo anataka kutibu Malaria akiwa mbali, kusudio langu ni kuzungumzia Elimu yenye kutibu tafrani hususan zenye kuhusiana na dhiki za Moyo na Akili, Na hili ni tendo ambalo wanaweza kufanya wale walopewa Hijaza na Mollah wao hata wakiwa mbali kwa kutumia sauti zao wakaponesha baadhi ya maradhi na kuondosha misukosuko ya dhiki za Moyo, ni jambo linalowezekana, kwanini lisiwezekane wakati unaweza kumsikia mtu kwenye simu aliyeko mbali bila ya waya kukamatana, na kama akikwambia nyumba yako imeungua unaanza kutokwa na machozi, na akikwambia nakulipa deni lako unajawa na furaha, nini kinatokezea? kinachotokezea hapo ndicho kile kile(Chenye kutokezea kwenye Dua), Na yule mwenye kujua kuponesha akajua kuitumia (Universal Mind)Ambayo hii tutaizungumza siku za mbele kwenye (Majaaliwa) basi anaweza kukutibu hata akiwa mbali, kwani maradhi ni yale yale anayotibu aliye karibu, au anayeomba aliyekaribu yote yanategemeana na mfumo wa (Dua) ndio maana wengine wanarekodiwa (CD) na kutibiwa, ni jambo linalowezekana na wala halina (Mushkeli wowote).
Ama kuhusu Elimu ya Kungara hii sitokwenda ndani sana kutokana vielelezo vyake ni virefu, lakini nitasema kwa kifupi Elimu hii inategemea vipi utaweza (kujikurubisha) au kuji(Tune) na mionzi ya Jua, na ukiweza kupata taaluma hii na wewe utakua unangara kama (Taa) na ukiwa mwanasiasa au Mtu wa kupenda vyeo hapo tena chaguzi zote unashinda wewe, na kila atokua karibu yako atakua mwenye kuvutiwa na wewe, lakini elimu hii ina kasoro zake na mbili katika kasoro hizo (Watu watakuwa wanavutiwa na wewe kimatamanio) Na kama huwezi kujizuia utakua na wapenzi hata elfu, na kasoro ya pili utakua katika hali ya umoto baridi (Mithili ya Majini), kwa hiyo utakua unaishi katika Ulimengu wa (Hasira) nyakati zote kwa kuwa sio (Nature yako).
Ama hii Elimu ya kutisha ni kama hiyo ya kungara ila hii imeambatana na (usiku) Giza, si unaona kila mtu anaogopa giza, ukiweza kuambatana ukaingia ndani ya (Dark matter)ukauingia usiku ukakuvaa, basi utakua unatisha mpaka watoto wako wakikuona watakukimbia, lakini ukifunikwa na mionzi ya giza tahadhari kwani utakumbwa na uvivu usiweze hata kunyanyuka kitandani, sababu kiza kinaletewa watu kupumzika na wewe unakitumia wakati wa mchana, kiza kishaondoka wewe umebaki na kivuli chake unatishia watu, hizo ni baadhi ya elimu za ajabu ambazo ziko nyingi, Na kama inavosema aya ikiwa utazitumia kwa manufaa ya uzuri basi ni fadhila kubwa kutoka kwa Mollah wako, lakini ukizitumia kwa ufisadi basi utakua umeangamia na kukufuru kukubwa, kwa sababu utakua unazitumia kinyume cha sheria.
Haya ni kwa ajili ya kukujulisheni uwapo wa Elimu hizi lakini cha muhimu zaidi ni kumuabudu Mollah wako na umuachie Mwenyewe ikiwa Kakupa Elimu hizi basi zitumie kwa manufaa na ukinyimwa basi shukuru wala usihangaike sababu utakua unanusuriwa na mengi. "Na wala hatukukupeni Elimu zetu isipoua kwa Uchache tu".
Sunday, November 30, 2014
ELIMU ZA AJABU PART 1
Asalaam Aleiykum
Leo napenda kukuchukua kwenye Safari ya Elimu za Ajabu, Lakini Safari hii watakwenda wale wenye kupenda kuyajua mambo mepya, wale wasochoka na kupata habari zilofichika, na zaidi ni wale Dini yao haijaishia kwenye kutia (Udhu) peke yake, Roho daima ina uchu wa kutaka kujua mambo ndio maana wakati mwingi tunatumia katika viwanja vya kutafuta habari, Sasa ukija kwangu mimi daima utapata mambo mepya kwani naelewa Elimu za Mwenye Enzi Mungu hazina mwisho wala upeo, Bahari yake haina Kipimo kila ukizama unaendelea chini wala hufiki Mwisho kwa kuwa mwisho wake ndio mwanzo wake, Kwa hiyo sisi hatujui mwanzo wake, vipi leo tutajua mwisho wake.
Najua Wengine Darsa zangu zinawakera wanakimbia ikisha wanarudi tena kuchungulia safari hii kaleta nini, hiyo ni kazi yangu ninayoifanya kwa siri juu yako ili upate mabadiliko, na ukiona umerudi tena kuchungulia ina maana ushaanza kupata Muongozo fulani ambao unakufanya uchungulie tena, hiyo ni ishara nzuri endelea utapata mafanikio makubwa.
Sasa leo pata faida ya Safari wanayokwenda (Mystic). Nini (Mystic)?.
Nimekuja kufahamu kwamba (Mystic)ni Mwanasayansi wa Dini, Mnao wanasayansi wenu wa Dunia, Na sisi tuna hawa wetu wa Dini, Tafauti yao hawa wa Dunia wanachambua kwa njia ya nje mpaka mara inatokezea tu kwenye (Akili)zao wakapata hii ni (DNA)Nikisema inatokezea nina maana wanafunguliwa na Mwenye enzi Mungu hiyo elimu ya kujua.
Na Wanasayansi wa Dini wao Wanakwenda Ndani Wanataka kujua hiyo (DNA)imetokea wapi, Nani aloileta kwa hiyo kwa kutaka kuyajua hayo ndio lazima Mwanasayansi wa Dini achupe katika kiza kinene, kwani nje kuna muangaza lakini ndani kuna Giza zito lazima ulipite giza hilo ndio utokeze kwenye Muangaza wa Elimu za Ajabu, ndio maana kuwa Mwanasayansi wa Dunia ni rahisi lakini kuelekea Uwanasayansi wa Dini ni kazi nzito ambayo mashujaa peke wanoweza kuchupa, wengine wanafanikiwa na wengine wanadhurika wakawa waharibifu na hata kufikia kupoteza Akili kwa mambo makubwa wanayokutana nayo huko kwenye hii (Mystical Journey).
Ndani ya Safari hii ndio unakutana na hizo Elimu za Ajabu, Kama Elimu ya Kuruka(Ukapaa kama ndege)
Elimu ya Kupotea(Mara ukawa huonekani)
Elimu ya Kutibu ukiwa Mbali.
Elimu ya kuona Viumbe wengine.
Elimu ya Kutisha Viumbe wakakuogopa.
Elimu ya Kungara ukawa unapendwa na halaiki ya watu.
Na Elimu chungu nzima ambazo hazina idadi maalum ambazo katika safari hii kila ukigundua zinazidi kuongezeka na hapo ndio Kiumbe kwa papara za kutaka yote anarudi Safari hii pengine kaambulia kupata elimu moja tu katika maajabu hayo, Napenda uelewe Safari hiyo ni ndefu na inataka mataarisho makubwa, kuzidi kuyachambua haya mambo endelea part 2
Leo napenda kukuchukua kwenye Safari ya Elimu za Ajabu, Lakini Safari hii watakwenda wale wenye kupenda kuyajua mambo mepya, wale wasochoka na kupata habari zilofichika, na zaidi ni wale Dini yao haijaishia kwenye kutia (Udhu) peke yake, Roho daima ina uchu wa kutaka kujua mambo ndio maana wakati mwingi tunatumia katika viwanja vya kutafuta habari, Sasa ukija kwangu mimi daima utapata mambo mepya kwani naelewa Elimu za Mwenye Enzi Mungu hazina mwisho wala upeo, Bahari yake haina Kipimo kila ukizama unaendelea chini wala hufiki Mwisho kwa kuwa mwisho wake ndio mwanzo wake, Kwa hiyo sisi hatujui mwanzo wake, vipi leo tutajua mwisho wake.
Najua Wengine Darsa zangu zinawakera wanakimbia ikisha wanarudi tena kuchungulia safari hii kaleta nini, hiyo ni kazi yangu ninayoifanya kwa siri juu yako ili upate mabadiliko, na ukiona umerudi tena kuchungulia ina maana ushaanza kupata Muongozo fulani ambao unakufanya uchungulie tena, hiyo ni ishara nzuri endelea utapata mafanikio makubwa.
Sasa leo pata faida ya Safari wanayokwenda (Mystic). Nini (Mystic)?.
Nimekuja kufahamu kwamba (Mystic)ni Mwanasayansi wa Dini, Mnao wanasayansi wenu wa Dunia, Na sisi tuna hawa wetu wa Dini, Tafauti yao hawa wa Dunia wanachambua kwa njia ya nje mpaka mara inatokezea tu kwenye (Akili)zao wakapata hii ni (DNA)Nikisema inatokezea nina maana wanafunguliwa na Mwenye enzi Mungu hiyo elimu ya kujua.
Na Wanasayansi wa Dini wao Wanakwenda Ndani Wanataka kujua hiyo (DNA)imetokea wapi, Nani aloileta kwa hiyo kwa kutaka kuyajua hayo ndio lazima Mwanasayansi wa Dini achupe katika kiza kinene, kwani nje kuna muangaza lakini ndani kuna Giza zito lazima ulipite giza hilo ndio utokeze kwenye Muangaza wa Elimu za Ajabu, ndio maana kuwa Mwanasayansi wa Dunia ni rahisi lakini kuelekea Uwanasayansi wa Dini ni kazi nzito ambayo mashujaa peke wanoweza kuchupa, wengine wanafanikiwa na wengine wanadhurika wakawa waharibifu na hata kufikia kupoteza Akili kwa mambo makubwa wanayokutana nayo huko kwenye hii (Mystical Journey).
Ndani ya Safari hii ndio unakutana na hizo Elimu za Ajabu, Kama Elimu ya Kuruka(Ukapaa kama ndege)
Elimu ya Kupotea(Mara ukawa huonekani)
Elimu ya Kutibu ukiwa Mbali.
Elimu ya kuona Viumbe wengine.
Elimu ya Kutisha Viumbe wakakuogopa.
Elimu ya Kungara ukawa unapendwa na halaiki ya watu.
Na Elimu chungu nzima ambazo hazina idadi maalum ambazo katika safari hii kila ukigundua zinazidi kuongezeka na hapo ndio Kiumbe kwa papara za kutaka yote anarudi Safari hii pengine kaambulia kupata elimu moja tu katika maajabu hayo, Napenda uelewe Safari hiyo ni ndefu na inataka mataarisho makubwa, kuzidi kuyachambua haya mambo endelea part 2
ELIMU ZA AJABU PART 2
Asalaam Aleiykum
Anahadithia Sayyidna Abu Huraira r.a "Akisema" Bwana Mtume s.a.w kanifundisha Elimu mbili ya kwanza nimekupeni, lakini ningekupeni hii ya pili mngenikata kichwa. Hayo ni maneno ya Sahaba wa Bwana Mtume s.a.w ambaye yeye kaenda hiyo safari kubwa ya (Mystical Journey)inayoitwa Miraji.Sura ya Israa aya 1.
سُبۡحَـٰنَ ٱلَّذِىٓ أَسۡرَىٰ بِعَبۡدِهِۦ لَيۡلاً۬ مِّنَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ إِلَى ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡأَقۡصَا ٱلَّذِى بَـٰرَكۡنَا حَوۡلَهُ ۥ لِنُرِيَهُ ۥ مِنۡ ءَايَـٰتِنَآۚ إِنَّهُ ۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡبَصِيرُ
Utukufu ni wake yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku kutoka msikiti Mtukufu wa(Makka)mpaka Msikiti wa mbali wa Aqsa(Bayyitul Muqadas)ambao tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake, ili tumuoneshe baadhi ya Alama zetu, Hakika (Mwenye enzi Mungu)ni Mwenye kusikia (na) kuona.
Kweli angekatwa kichwa kwa sababu ee hivi leo kuna baadhi ya watu wamo ndani ya Uislam wanaipinga safari hiyo kwa malumbano, seuze hayo mambo yalioko huko, kwa hiyo kuwa na hakika elimu hizo zipo na ziliwahi hata kuandikwa baadhi yake kwenye vitabu lakini maskini vikachomwa moto vyote mwanzoni mwa miaka ya 70 na (Library zote kufungwa), na hiyo ndio ikawa hasara ya (Generation)hii kunyimwa elimu hizi za Ajabu.
Imebakia sasa hivi elimu zinazofahamika ni zile za wazi, kwa hiyo umefika wakati sasa japo kuashiria, angalau kukumbusha kwamba hizi elimu zilikuwepo, zipo na zitaendelea kuwepo na pengine (Generation) ijayo itaweza kufatilia kwa undani. Kwani kutokana na aya hii ya sura ya (Fussilat 53)
"سَنُرِيهِمۡ ءَايَـٰتِنَا فِى ٱلۡأَفَاقِ وَفِىٓ أَنفُسِہِمۡ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَهُمۡ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّۗ "
Tutawaonesha(Ukweli wa)Maneno yetu haya katika nchi za mbali na katika nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli.
Kutokana na maneno hayo inaonesha wazi mambo makubwa ya ajabu yasokwisha yapo, yanaendelea kuvumbuliwa kwa njia ya nje na ndani katika fani zote za maisha haya ya Ulimwenguni, Lakini kwa (Mystic) inakua tabu kuyaandika au kuhadithia kwa kuwa ni ya ajabu na hayana mfano, kwa hiyo (Mystic) anakaa kimya na kuashiria tu kuna hichi na kile, ili uende ukaone mwenyewe.
Sasa Baada ya kuizungumza Dhumuni la darsa yetu hii sasa wacha tuanze safari yetu hii ili tupate angalau chembe ya muangaza wa Elimu hizi za Ajabu. Basi tuanze na ajabu ya mwanzo iliyomo ndani ya kitabu hichi cha Quraan, Kumbuka kitu kimoja vitabu vyote unasoma unavimaliza lakini hichi cha Quraan hukimalizi, unaambiwa kisome daima, Jee huoni Ajabu kwa Jambo hilo, kwanini ukisome ikisha ukirejee tena na tena mpaka mwisho wa umri wako?, mbona vyengine ukimaliza inakua basi, kwanini hichi tu ndio uendelee?.
Utajibiwa Swali lako hilo na baadhi ya aya za Quraan ili upate muongozo na mimi nita (Share) ajabu hiyo na wewe ili upate kuijua kwa vizuri.
Endelea part 3
Anahadithia Sayyidna Abu Huraira r.a "Akisema" Bwana Mtume s.a.w kanifundisha Elimu mbili ya kwanza nimekupeni, lakini ningekupeni hii ya pili mngenikata kichwa. Hayo ni maneno ya Sahaba wa Bwana Mtume s.a.w ambaye yeye kaenda hiyo safari kubwa ya (Mystical Journey)inayoitwa Miraji.Sura ya Israa aya 1.
سُبۡحَـٰنَ ٱلَّذِىٓ أَسۡرَىٰ بِعَبۡدِهِۦ لَيۡلاً۬ مِّنَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ إِلَى ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡأَقۡصَا ٱلَّذِى بَـٰرَكۡنَا حَوۡلَهُ ۥ لِنُرِيَهُ ۥ مِنۡ ءَايَـٰتِنَآۚ إِنَّهُ ۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡبَصِيرُ
Utukufu ni wake yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku kutoka msikiti Mtukufu wa(Makka)mpaka Msikiti wa mbali wa Aqsa(Bayyitul Muqadas)ambao tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake, ili tumuoneshe baadhi ya Alama zetu, Hakika (Mwenye enzi Mungu)ni Mwenye kusikia (na) kuona.
Kweli angekatwa kichwa kwa sababu ee hivi leo kuna baadhi ya watu wamo ndani ya Uislam wanaipinga safari hiyo kwa malumbano, seuze hayo mambo yalioko huko, kwa hiyo kuwa na hakika elimu hizo zipo na ziliwahi hata kuandikwa baadhi yake kwenye vitabu lakini maskini vikachomwa moto vyote mwanzoni mwa miaka ya 70 na (Library zote kufungwa), na hiyo ndio ikawa hasara ya (Generation)hii kunyimwa elimu hizi za Ajabu.
Imebakia sasa hivi elimu zinazofahamika ni zile za wazi, kwa hiyo umefika wakati sasa japo kuashiria, angalau kukumbusha kwamba hizi elimu zilikuwepo, zipo na zitaendelea kuwepo na pengine (Generation) ijayo itaweza kufatilia kwa undani. Kwani kutokana na aya hii ya sura ya (Fussilat 53)
"سَنُرِيهِمۡ ءَايَـٰتِنَا فِى ٱلۡأَفَاقِ وَفِىٓ أَنفُسِہِمۡ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَهُمۡ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّۗ "
Tutawaonesha(Ukweli wa)Maneno yetu haya katika nchi za mbali na katika nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli.
Kutokana na maneno hayo inaonesha wazi mambo makubwa ya ajabu yasokwisha yapo, yanaendelea kuvumbuliwa kwa njia ya nje na ndani katika fani zote za maisha haya ya Ulimwenguni, Lakini kwa (Mystic) inakua tabu kuyaandika au kuhadithia kwa kuwa ni ya ajabu na hayana mfano, kwa hiyo (Mystic) anakaa kimya na kuashiria tu kuna hichi na kile, ili uende ukaone mwenyewe.
Sasa Baada ya kuizungumza Dhumuni la darsa yetu hii sasa wacha tuanze safari yetu hii ili tupate angalau chembe ya muangaza wa Elimu hizi za Ajabu. Basi tuanze na ajabu ya mwanzo iliyomo ndani ya kitabu hichi cha Quraan, Kumbuka kitu kimoja vitabu vyote unasoma unavimaliza lakini hichi cha Quraan hukimalizi, unaambiwa kisome daima, Jee huoni Ajabu kwa Jambo hilo, kwanini ukisome ikisha ukirejee tena na tena mpaka mwisho wa umri wako?, mbona vyengine ukimaliza inakua basi, kwanini hichi tu ndio uendelee?.
Utajibiwa Swali lako hilo na baadhi ya aya za Quraan ili upate muongozo na mimi nita (Share) ajabu hiyo na wewe ili upate kuijua kwa vizuri.
Endelea part 3
ELIMU ZA AJABU PART 3
Asalaam Aleiykum
Ajabu yenyewe inaanzia katika maneno haya ya aya ya 5 na 6 sura ya (Muzzamil)"إِنَّا سَنُلۡقِى عَلَيۡكَ قَوۡلاً۬ ثَقِيلاً ""hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito""إِنَّ نَاشِئَةَ ٱلَّيۡلِ هِىَ أَشَدُّ وَطۡـًٔ۬ا وَأَقۡوَمُ قِيلاً ""Hakika kuamka usiku(Na kufanya Ibada)kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno (yake) yanatua zaidi.
Hapo pametajwa jambo la ajabu, umetajwa moyo ikatajwa kutua kwa maneno, Maneno yanatokea wapi?, kwenye Akili, Moyoni yanakwenda kupewa tafsiri au maana, ndio maana ukaambiwa nyanyuka usiku, kwanini ikawa usiku? Kwa sababu umelala na Akili isha (Process) mambo yanotokea mchana wote, Unaamka ukiwa Mweupe, unasoma kitabu cha Mwenye Enzi Mungu kwa utulivu wa hali ya juu pasipo kuwa na mawazo mengine, hapo tena neno linaanguka moyoni na likianguka tu wakati umepata utulivu ndio unapata hicho kitu kinaitwa (Awakening) na ukipata hali hiyo japo kwa aya moja basi ushaonja tone la (Mysticism) na unabadilika daima, aya moja inakufanya utembee kwenye Bahari, aya moja itakufanya uwatibie wenzio Maradhi yao, pamoja na wewe mwenyewe.
Na kwanini isiwe hivyo na wakati imetajwa ndani ya Quraan kuwa huu ni muongozo na ponesho la maradhi yaliyomo kwenye vifua vyenu, na kifua kina mambo mengi, husda imo humo, kutokuamini kumo humo, Ini limo humo, Figo limo humo, lakini kuupata huo muongozo na ponesho lenyewe linahitaji huyo msomaji yupo kwenye daraja gani.Maskini leo wako wapi wale (Mystic) walokua wakiyasomea maji kama unaumwa tumbo linapoa, kama Mwanamke hazai anapata uja uzito, Ndio maana ukatajwa Usiku ndio wakati bora wa kutokea tukio hilo, "Hakika tutakuteremshia maneno mazito".
Sasa nini habari ya wale wasojua kusoma au wanajua lakini hawana nafasi ya kusoma, wao wanaambiwa Al-Araf (204)
وَإِذَا قُرِئَ ٱلۡقُرۡءَانُ فَٱسۡتَمِعُواْ لَهُ ۥ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na Itakaposomwa Quraan isikilizeni na nyamazeni ili mpate kurehemewa.
Kwanza isikilize halafu kaa kimya, yametajwa maneno mawili ya mfano mzuri sana, kwanini usikilize? kwa sababu wewe hufanyi yote mawili, pengine inasomwa wewe unasikiliza sauti ya msomaji badala ya Quraan, na huku Akili yako inatizama labda videvu vya Sheikh, au kakosea Nun au hajatia shada na huku maskini unakosa kitu adhimu kinakupita cha Rehma ya Mollah wako nilichokitaja hapo juu, kwa hiyo ndio unaambiwa sikiliza ikisha ukae kimya, yaani nje unasikiliza na ndani huna mawazo yanoendelea kwenye Akili yako hapo huenda likatokea hilo tukio la Ajabu.
Pengine aya huenda ikapita na kuupasua hilo jipo la fahamu ukabubujikwa na machozi bila ya kujielewa, Ndio maana mnaambiwa sikilizeni mawaidha asaa yanaweza kukubadilisha, Lakini inategemea msomaji na huyo msikilizaji. Ama kwa wale wanotaka kushuhudiwa wao waisome Alfajiri, (Angalia katika Darsa yangu ya kushuhudiwa na Quraan).
Basi Naam yasome maneno haya mazito yaloteremshwa na Mwenye Enzi Mungu ambayo Mwanaadamu hujui ndani yake kuna Ajabu gani, Soma upate kujua kwanini Jahazi ya Nabii Nuhu a.s ilikua ikenda na kusimama kutokana na maneno ya (Bismillahi Majriha wamursaha), hayo ndio baadhi ya maajabu machache niloyataja yaliyomo kwenye Quraan, yapo mengi lakini muda wetu hautoshi kuyazungumza yote kwa njia ya maandishi, na Mifano ya maajabu hayo ni kama vile kuzuia gari isiondoke, ukasoma mpaka ukafanya Treni ikusubiri, Ndege isiruke nk, najua mtashangaa ndio maana nikaita Elimu za Ajabu na hayo ndio mambo ya (Mysticsim).
Sasa tuingie katika Elimu ya (Kuruka au Kupaa) sisemi hivi mtu akaanza kuniuliza(Method) ya kufanya, mimi nazungumza kwa njia ya Elimu, wewe una hiyari yako kutafuta(Method) ukija kukwama kwenye Miti mimi sichukui dhamana, wapi imepatikana Elimu hii tutaendelea wiki ijayo kwenye Part 4.
Shukran.
Ajabu yenyewe inaanzia katika maneno haya ya aya ya 5 na 6 sura ya (Muzzamil)"إِنَّا سَنُلۡقِى عَلَيۡكَ قَوۡلاً۬ ثَقِيلاً ""hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito""إِنَّ نَاشِئَةَ ٱلَّيۡلِ هِىَ أَشَدُّ وَطۡـًٔ۬ا وَأَقۡوَمُ قِيلاً ""Hakika kuamka usiku(Na kufanya Ibada)kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno (yake) yanatua zaidi.
Hapo pametajwa jambo la ajabu, umetajwa moyo ikatajwa kutua kwa maneno, Maneno yanatokea wapi?, kwenye Akili, Moyoni yanakwenda kupewa tafsiri au maana, ndio maana ukaambiwa nyanyuka usiku, kwanini ikawa usiku? Kwa sababu umelala na Akili isha (Process) mambo yanotokea mchana wote, Unaamka ukiwa Mweupe, unasoma kitabu cha Mwenye Enzi Mungu kwa utulivu wa hali ya juu pasipo kuwa na mawazo mengine, hapo tena neno linaanguka moyoni na likianguka tu wakati umepata utulivu ndio unapata hicho kitu kinaitwa (Awakening) na ukipata hali hiyo japo kwa aya moja basi ushaonja tone la (Mysticism) na unabadilika daima, aya moja inakufanya utembee kwenye Bahari, aya moja itakufanya uwatibie wenzio Maradhi yao, pamoja na wewe mwenyewe.
Na kwanini isiwe hivyo na wakati imetajwa ndani ya Quraan kuwa huu ni muongozo na ponesho la maradhi yaliyomo kwenye vifua vyenu, na kifua kina mambo mengi, husda imo humo, kutokuamini kumo humo, Ini limo humo, Figo limo humo, lakini kuupata huo muongozo na ponesho lenyewe linahitaji huyo msomaji yupo kwenye daraja gani.Maskini leo wako wapi wale (Mystic) walokua wakiyasomea maji kama unaumwa tumbo linapoa, kama Mwanamke hazai anapata uja uzito, Ndio maana ukatajwa Usiku ndio wakati bora wa kutokea tukio hilo, "Hakika tutakuteremshia maneno mazito".
Sasa nini habari ya wale wasojua kusoma au wanajua lakini hawana nafasi ya kusoma, wao wanaambiwa Al-Araf (204)
وَإِذَا قُرِئَ ٱلۡقُرۡءَانُ فَٱسۡتَمِعُواْ لَهُ ۥ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na Itakaposomwa Quraan isikilizeni na nyamazeni ili mpate kurehemewa.
Kwanza isikilize halafu kaa kimya, yametajwa maneno mawili ya mfano mzuri sana, kwanini usikilize? kwa sababu wewe hufanyi yote mawili, pengine inasomwa wewe unasikiliza sauti ya msomaji badala ya Quraan, na huku Akili yako inatizama labda videvu vya Sheikh, au kakosea Nun au hajatia shada na huku maskini unakosa kitu adhimu kinakupita cha Rehma ya Mollah wako nilichokitaja hapo juu, kwa hiyo ndio unaambiwa sikiliza ikisha ukae kimya, yaani nje unasikiliza na ndani huna mawazo yanoendelea kwenye Akili yako hapo huenda likatokea hilo tukio la Ajabu.
Pengine aya huenda ikapita na kuupasua hilo jipo la fahamu ukabubujikwa na machozi bila ya kujielewa, Ndio maana mnaambiwa sikilizeni mawaidha asaa yanaweza kukubadilisha, Lakini inategemea msomaji na huyo msikilizaji. Ama kwa wale wanotaka kushuhudiwa wao waisome Alfajiri, (Angalia katika Darsa yangu ya kushuhudiwa na Quraan).
Basi Naam yasome maneno haya mazito yaloteremshwa na Mwenye Enzi Mungu ambayo Mwanaadamu hujui ndani yake kuna Ajabu gani, Soma upate kujua kwanini Jahazi ya Nabii Nuhu a.s ilikua ikenda na kusimama kutokana na maneno ya (Bismillahi Majriha wamursaha), hayo ndio baadhi ya maajabu machache niloyataja yaliyomo kwenye Quraan, yapo mengi lakini muda wetu hautoshi kuyazungumza yote kwa njia ya maandishi, na Mifano ya maajabu hayo ni kama vile kuzuia gari isiondoke, ukasoma mpaka ukafanya Treni ikusubiri, Ndege isiruke nk, najua mtashangaa ndio maana nikaita Elimu za Ajabu na hayo ndio mambo ya (Mysticsim).
Sasa tuingie katika Elimu ya (Kuruka au Kupaa) sisemi hivi mtu akaanza kuniuliza(Method) ya kufanya, mimi nazungumza kwa njia ya Elimu, wewe una hiyari yako kutafuta(Method) ukija kukwama kwenye Miti mimi sichukui dhamana, wapi imepatikana Elimu hii tutaendelea wiki ijayo kwenye Part 4.
Shukran.
Sunday, November 23, 2014
MAMBO MATATU YANOKOSESHA PEPO PART 1
Asalaam Aleiykum
Siku moja Mcha Mungu Hadad alisisitiza katika maombi yake kwa Mungu aoneshwe kwenye usingizi wake nani Mcha Mungu zaidi katika Mji wake, "Akajibiwa kwenye usingizi ni Jirani yako" akafurahi sana kujua kumbe Jirani yake ndio kamshinda kwa Ibada na mapenzi ya Allah, Akaomba tena sasa naomba nijulishwe yule Mtenda Dhanmbi kubwa kuliko wote ili nipate kumjua, "Akajibiwa tena ndani ya Usingizi wake ni Jirani yako" Mambo haya yalimshangaza sana Hadad akawa hajui la kufanya, kwa sababu Ucha Mungu anauona kwa yule Jirani, ana Duka lake, anasali kama kawaida, anatoa Sadaka, Lakini anashindwa kuona nini maasi yake.
Sote tumejificha kama huyo Jirani, kwa sababu Jirani alikua na udhaifu mkubwa, vita vya kujizuia na hili jambo la mwanzo vilimshinda, akichukua watoto wa watu mitaani kwa siri na kuzini nao, akichukua wake za watu na kufanya nao mapenzi, Jambo hili la (1)(Sex)lilimuhujumu kabisa ikawa kwa Binaadamu wenzie wasomjua wanamuona Mcha Mungu kwa kuwa hatoki katika Nyumba za Ibada na kutenda mambo mema,na ana simamisha Sala sana, lakini usiku ukiingia anageuka (Dracula). Na hivi ndivo wengi tunavoishi upande (Sinner) na tukigeuzwa upande wa pili (Saints).
Sex ni adui wetu mkubwa wa kutuzuilia kuipata (Pepo) ya Mwenye enzi Mungu, Ni tendo lenye kuichafua Roho, na kukaribisha maradhi ya Mwili na Akili yake ikiwa itatumika sivyo na maamrisho kama yalivyoteremka kwenye sura ya Muuminun aya ya 5 na 6. وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَـٰفِظُونَ.
"Na wale ambao wanalinda Tupu zao"
Vinatakiwa kulindwa Vipande vya nyama hizi kwa ulinzi wa hali ya juu kabisa, kwani ikiwa kitatumika kwa njia nyengine isiyokua ya kisheria kipande cha nyama hichi kitaleta madhara makubwa kwa muhusika na jamii nzima kwa jumla, kitapita njia zisizo amrishwa na kufanya uharibifu mkubwa kama vile wa kuacha kizazi kisichokua na familia ya upande mmoja, Muhusika atakua akisambaza maradhi kutoka huku kwenda kule, atakua akiacha maumivu makubwa kwa wale anowatekeleza, Ikiwa jambo hili halikuwekewa ulinzi linakufukuza kabisa katika enzi ya kumkumbuka Mollah wako, ndio maana likaambiwa jambo hili limeruhusiwa lakini ila kwa.
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٲجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَـٰنُہُمۡ فَإِنَّہُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ
"Isipokua kwa wake zao au kwa(Wanawake)wale iliyowamiliki mikono yao ya Kiume(Kulia)Basi hao ndio wasiolaumiwa.
Endelea part 2
Siku moja Mcha Mungu Hadad alisisitiza katika maombi yake kwa Mungu aoneshwe kwenye usingizi wake nani Mcha Mungu zaidi katika Mji wake, "Akajibiwa kwenye usingizi ni Jirani yako" akafurahi sana kujua kumbe Jirani yake ndio kamshinda kwa Ibada na mapenzi ya Allah, Akaomba tena sasa naomba nijulishwe yule Mtenda Dhanmbi kubwa kuliko wote ili nipate kumjua, "Akajibiwa tena ndani ya Usingizi wake ni Jirani yako" Mambo haya yalimshangaza sana Hadad akawa hajui la kufanya, kwa sababu Ucha Mungu anauona kwa yule Jirani, ana Duka lake, anasali kama kawaida, anatoa Sadaka, Lakini anashindwa kuona nini maasi yake.
Sote tumejificha kama huyo Jirani, kwa sababu Jirani alikua na udhaifu mkubwa, vita vya kujizuia na hili jambo la mwanzo vilimshinda, akichukua watoto wa watu mitaani kwa siri na kuzini nao, akichukua wake za watu na kufanya nao mapenzi, Jambo hili la (1)(Sex)lilimuhujumu kabisa ikawa kwa Binaadamu wenzie wasomjua wanamuona Mcha Mungu kwa kuwa hatoki katika Nyumba za Ibada na kutenda mambo mema,na ana simamisha Sala sana, lakini usiku ukiingia anageuka (Dracula). Na hivi ndivo wengi tunavoishi upande (Sinner) na tukigeuzwa upande wa pili (Saints).
Sex ni adui wetu mkubwa wa kutuzuilia kuipata (Pepo) ya Mwenye enzi Mungu, Ni tendo lenye kuichafua Roho, na kukaribisha maradhi ya Mwili na Akili yake ikiwa itatumika sivyo na maamrisho kama yalivyoteremka kwenye sura ya Muuminun aya ya 5 na 6. وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَـٰفِظُونَ.
"Na wale ambao wanalinda Tupu zao"
Vinatakiwa kulindwa Vipande vya nyama hizi kwa ulinzi wa hali ya juu kabisa, kwani ikiwa kitatumika kwa njia nyengine isiyokua ya kisheria kipande cha nyama hichi kitaleta madhara makubwa kwa muhusika na jamii nzima kwa jumla, kitapita njia zisizo amrishwa na kufanya uharibifu mkubwa kama vile wa kuacha kizazi kisichokua na familia ya upande mmoja, Muhusika atakua akisambaza maradhi kutoka huku kwenda kule, atakua akiacha maumivu makubwa kwa wale anowatekeleza, Ikiwa jambo hili halikuwekewa ulinzi linakufukuza kabisa katika enzi ya kumkumbuka Mollah wako, ndio maana likaambiwa jambo hili limeruhusiwa lakini ila kwa.
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٲجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَـٰنُہُمۡ فَإِنَّہُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ
"Isipokua kwa wake zao au kwa(Wanawake)wale iliyowamiliki mikono yao ya Kiume(Kulia)Basi hao ndio wasiolaumiwa.
Endelea part 2
MAMBO MATATU YANOKOSESHA PEPO PART 2
Asalaam Aleiykum
Lakini utapojaribu njia nyengine yoyote ya kuiba zabibu za watu basi ujue utalaumiwa, Kwa sababu njia uliyoifata ni chafu na ina mambo ya kila aina, na ni Mwenendo mbaya kabisa ambao maradhi yake ni magumu kupona, Na pia yana tabia ya kujirejea kwa kuwa yanaishi Akilini na wewe huna uhodari wa kuishinda Akili pamoja na (Ibilis).
Ndio maana ukianza uzinifu ni vigumu kuepuka, inatakiwa ifanyike kazi kubwa sana mpaka utolewe katika mzunguko huu wa mapenzi ya zinaa, Sasa sababu gani ikakupelekea mpaka ukaikosa pepo, sababu zipo nyingi lakini mie nitazitaja hizi mbili ili tupate kuzizingatia, Sababu ya kwanza(Sex)inakushughulisha humkumbuki kabisa Mollah wako, kwa sababu mambo mawili hayo hayakai pamoja moja linalaza na moja linakuamsha, (na mfano unao mwenyewe ukiwa na huyo wa halali wako mke au mume mkitaka kufanya tendo la ndoa ukiambiwa tutie udhu tusali Rakaa mbili basi hamu yote hapo hapo inaondoka)Kwa sababu unakua ushaamshwa, ushatolewa katika hali yakua mnyama umerejeshwa kwenye ubinaadamu, sasa jitizame huko uendako usikoambiwa tia udhu unakuaje, Wewe na mnyama hamna tafauti.
Unalala ukikoroma ndio maana hutaki mambo ya dini, huwezi hata kusali, kutokana na tendo unalo jishughulisha nalo ni la kukatazwa, na chochote kile unachokatazwa kina kushughulisha sana, wewe chunguza pahala uambiwe usichungulie uone utakavo hangaika kutaka kujua kuna nini hata nisichungulie?.Kwa hivyo tulivyoambiwa Zinaa ni haramu tumeumia, inafikia ukisikia muazini una hamaki, yana kushughulisha mambo haya mpaka kufikia Utu uzima bado mambo yamekuganda Akilini, Tahadhari sana huku mwili ushachoka, maradhi yashawasili na wewe umeshakua Muflis huna tamaa tena ya pepo.
Na Jambo la pili ni ule uharibifu unopita kuufanya, unaumiza Roho za Binaadamu wenzio, Unawacha kizazi kisichokua na Familia, basi kama wanavoteseka hao binaadamu wenzio jua na wewe maandalizi ya Adhabu yanakusubiri bila ya shaka yoyote na hilo pekee linakutosha kukukosesha pepo.
Lakini utapojaribu njia nyengine yoyote ya kuiba zabibu za watu basi ujue utalaumiwa, Kwa sababu njia uliyoifata ni chafu na ina mambo ya kila aina, na ni Mwenendo mbaya kabisa ambao maradhi yake ni magumu kupona, Na pia yana tabia ya kujirejea kwa kuwa yanaishi Akilini na wewe huna uhodari wa kuishinda Akili pamoja na (Ibilis).
Ndio maana ukianza uzinifu ni vigumu kuepuka, inatakiwa ifanyike kazi kubwa sana mpaka utolewe katika mzunguko huu wa mapenzi ya zinaa, Sasa sababu gani ikakupelekea mpaka ukaikosa pepo, sababu zipo nyingi lakini mie nitazitaja hizi mbili ili tupate kuzizingatia, Sababu ya kwanza(Sex)inakushughulisha humkumbuki kabisa Mollah wako, kwa sababu mambo mawili hayo hayakai pamoja moja linalaza na moja linakuamsha, (na mfano unao mwenyewe ukiwa na huyo wa halali wako mke au mume mkitaka kufanya tendo la ndoa ukiambiwa tutie udhu tusali Rakaa mbili basi hamu yote hapo hapo inaondoka)Kwa sababu unakua ushaamshwa, ushatolewa katika hali yakua mnyama umerejeshwa kwenye ubinaadamu, sasa jitizame huko uendako usikoambiwa tia udhu unakuaje, Wewe na mnyama hamna tafauti.
Unalala ukikoroma ndio maana hutaki mambo ya dini, huwezi hata kusali, kutokana na tendo unalo jishughulisha nalo ni la kukatazwa, na chochote kile unachokatazwa kina kushughulisha sana, wewe chunguza pahala uambiwe usichungulie uone utakavo hangaika kutaka kujua kuna nini hata nisichungulie?.Kwa hivyo tulivyoambiwa Zinaa ni haramu tumeumia, inafikia ukisikia muazini una hamaki, yana kushughulisha mambo haya mpaka kufikia Utu uzima bado mambo yamekuganda Akilini, Tahadhari sana huku mwili ushachoka, maradhi yashawasili na wewe umeshakua Muflis huna tamaa tena ya pepo.
Na Jambo la pili ni ule uharibifu unopita kuufanya, unaumiza Roho za Binaadamu wenzio, Unawacha kizazi kisichokua na Familia, basi kama wanavoteseka hao binaadamu wenzio jua na wewe maandalizi ya Adhabu yanakusubiri bila ya shaka yoyote na hilo pekee linakutosha kukukosesha pepo.
MAMBO MATATU YANOKOSESHA PEPO PART 3
Asalaam Aleiykum
Jambo la pili nii hizi Hamaki tulonazo.
Sasa tunaingia kwenye Sumu ya maangamizi ambayo kama utakunywa sumu hii basi wewe kwa hiyari yako umejiharamishia Pepo. Hamaki ni madhara makubwa kama utaitizama kwa undani, magonvi yote yanaletwa na hamaki, chuki zote zinatokana na hamaki, Hebu tuliangalie tendo hili la hamaki mwanzo wake wapi.
Hamaki ni tendo linalotokea ndani ya mwili wako ambalo ni (Energy)maalum inayoripuka kutokana na kitendo cha nje kilichofanywa na Mtu mwengine, Nini kafanya? kajeruhi (Chemical) za (Kiburi) katika Akili yako, Na Ufalme wako wa (Kiburi)ukiguswa kidogo tu hata na mtoto mdogo jiangalie unakuaje, ukikataliwa na mwanamke jiangalie unakuaje, ukinyimwa cheo tizama unafanyaje, ukigombana kitu kidogo angalia huzungumzi milele pengine na ndugu zako.
Sasa nini kimetokezea umeikera ile (Energy) yenye kukupa huruma na upole na kuipeleka kwenye Akili kwa njia ya kasi ambapo ndio inazaa Hamaki, unafanya mambo ukiwa umelala usingizi, inakwenda kukaa (Energy) hiyo kwenye Akili yako na kila mara huwa inakukumbusha ulivyofanyiwa, hapo tena unaondoka na visasi, unaondoka na chuki za uharibifu hupumziki na wewe mpaka ulipize japo kwa siri kwa lile tendo alofanya fulani siku ile, utakwenda kutafuta ushirikina, utatuma watu ili wamdhuru, utapigana vita, utapoteza maisha ya watu kwa kitu kimoja, au utaanza kutapakaza habari zisizo za kweli ambazo zinaleta madhara kwa muhusika, hayo yote unayafanya kutokana na Hamaki zako,na ukienda safari hiyo unasahau kabisa kuwa kuna Mollah wako, unafanya hasira za kudumu hali yakua ungesubiri kidogo au uka kaa chini ile (Energy)irudi sehemu yake badala ya kukupeleka kwenye uharibifu ingekupeleka Peponi, kutokana na (Energy) hiyo hiyo zinazaliwa huruma za mapenzi na upole, lakini ukiifata wakati imekwenda kichwani hiyo ndio inakua sababu ya uharibifu na kukukosesha Pepo.
Jambo la Tatu Kupenda Mali.
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
"Na Mnapenda Mali Mapenzi mengi"(Makubwa)
Mnapenda majumba, Mnapenda magari, Mnapenda anasa za dunia, Mnapenda viumbe wenzenu Na Mali zenu hususan Pesa, zinakushughulisha kwa mapenzi makubwa, unasahau kabisa kama umeumbwa, unasahau kabisa kama unatakiwa ufanye Ibada, unatakiwa ufanye wema na Ihsan, unasahau kama mauti yanakunyanganya kila kitu na kukuacha mweupe, nini unafanya, unahesabu mali na kushughulika na watoto, unanyanganya huku na kule, uko tayari wende motoni ili wengine wastarehe na kufurahi kwa chumo lako, jiulize wewe unapata faida gani kwa shughuli hizo.
Angalia vipi mipango ya kazi na shopping ilivokuzonga, Fulani atavaa nini, leo tutakula nini, nani kenda nani karudi, harusi ya fulani iko lini, pesa ngapi zimetumika, kesho nani anacheza mechi ya mpira, kipindi changu cha Tv kinaanza saa ngapi, (Wassup)mbona sijapata (Msg) hivi ndivo tabia zetu za kila siku zenye kutusahaulisha mambo ambayo Mollah wetu katuamrisha ambayo ni ya kumkumbuka yeye na kufanya Ibada. Ukiangalia Mambo hayo yote Matatu ni yanokupelekea nje mja wewe, Maskini umekaa dirishani unashughulika na mambo ya Nje wakati huku ndani ya kifua chako, wamejificha (Hurulain)ndani kifuani kwako imejificha (Furaha ya Imani na Huruma na mapenzi) na humo ndani ya kifua chako kumejificha (Hazina) kubwa lakini wapi,, unashughulika na mambo ya nje kupita kiasi mpaka yanakua sababu ya adhabu yako, yanakutesa hapa duniani na unashindwa kujiuliza vipi itakua hali yako huko Akhera uendako. Basi Mja Unatakiwa Ujiulize hivyo uko tayari hapa Ulimwenguni uteseke na huko Uendako pia ukateseke, uamuzi unao mwenyewe, na kama umefahamu anza sasa ili usiikose Pepo ya Mollah wako,na kumbuka hayo yote unayafanya upate raha na furaha, Na Mollah wako kakwambia ukifanya Ibada, utayapata hayo yote na zaidi katika Ufalme wake wa Milele.
Jambo la pili nii hizi Hamaki tulonazo.
Sasa tunaingia kwenye Sumu ya maangamizi ambayo kama utakunywa sumu hii basi wewe kwa hiyari yako umejiharamishia Pepo. Hamaki ni madhara makubwa kama utaitizama kwa undani, magonvi yote yanaletwa na hamaki, chuki zote zinatokana na hamaki, Hebu tuliangalie tendo hili la hamaki mwanzo wake wapi.
Hamaki ni tendo linalotokea ndani ya mwili wako ambalo ni (Energy)maalum inayoripuka kutokana na kitendo cha nje kilichofanywa na Mtu mwengine, Nini kafanya? kajeruhi (Chemical) za (Kiburi) katika Akili yako, Na Ufalme wako wa (Kiburi)ukiguswa kidogo tu hata na mtoto mdogo jiangalie unakuaje, ukikataliwa na mwanamke jiangalie unakuaje, ukinyimwa cheo tizama unafanyaje, ukigombana kitu kidogo angalia huzungumzi milele pengine na ndugu zako.
Sasa nini kimetokezea umeikera ile (Energy) yenye kukupa huruma na upole na kuipeleka kwenye Akili kwa njia ya kasi ambapo ndio inazaa Hamaki, unafanya mambo ukiwa umelala usingizi, inakwenda kukaa (Energy) hiyo kwenye Akili yako na kila mara huwa inakukumbusha ulivyofanyiwa, hapo tena unaondoka na visasi, unaondoka na chuki za uharibifu hupumziki na wewe mpaka ulipize japo kwa siri kwa lile tendo alofanya fulani siku ile, utakwenda kutafuta ushirikina, utatuma watu ili wamdhuru, utapigana vita, utapoteza maisha ya watu kwa kitu kimoja, au utaanza kutapakaza habari zisizo za kweli ambazo zinaleta madhara kwa muhusika, hayo yote unayafanya kutokana na Hamaki zako,na ukienda safari hiyo unasahau kabisa kuwa kuna Mollah wako, unafanya hasira za kudumu hali yakua ungesubiri kidogo au uka kaa chini ile (Energy)irudi sehemu yake badala ya kukupeleka kwenye uharibifu ingekupeleka Peponi, kutokana na (Energy) hiyo hiyo zinazaliwa huruma za mapenzi na upole, lakini ukiifata wakati imekwenda kichwani hiyo ndio inakua sababu ya uharibifu na kukukosesha Pepo.
Jambo la Tatu Kupenda Mali.
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
"Na Mnapenda Mali Mapenzi mengi"(Makubwa)
Mnapenda majumba, Mnapenda magari, Mnapenda anasa za dunia, Mnapenda viumbe wenzenu Na Mali zenu hususan Pesa, zinakushughulisha kwa mapenzi makubwa, unasahau kabisa kama umeumbwa, unasahau kabisa kama unatakiwa ufanye Ibada, unatakiwa ufanye wema na Ihsan, unasahau kama mauti yanakunyanganya kila kitu na kukuacha mweupe, nini unafanya, unahesabu mali na kushughulika na watoto, unanyanganya huku na kule, uko tayari wende motoni ili wengine wastarehe na kufurahi kwa chumo lako, jiulize wewe unapata faida gani kwa shughuli hizo.
Angalia vipi mipango ya kazi na shopping ilivokuzonga, Fulani atavaa nini, leo tutakula nini, nani kenda nani karudi, harusi ya fulani iko lini, pesa ngapi zimetumika, kesho nani anacheza mechi ya mpira, kipindi changu cha Tv kinaanza saa ngapi, (Wassup)mbona sijapata (Msg) hivi ndivo tabia zetu za kila siku zenye kutusahaulisha mambo ambayo Mollah wetu katuamrisha ambayo ni ya kumkumbuka yeye na kufanya Ibada. Ukiangalia Mambo hayo yote Matatu ni yanokupelekea nje mja wewe, Maskini umekaa dirishani unashughulika na mambo ya Nje wakati huku ndani ya kifua chako, wamejificha (Hurulain)ndani kifuani kwako imejificha (Furaha ya Imani na Huruma na mapenzi) na humo ndani ya kifua chako kumejificha (Hazina) kubwa lakini wapi,, unashughulika na mambo ya nje kupita kiasi mpaka yanakua sababu ya adhabu yako, yanakutesa hapa duniani na unashindwa kujiuliza vipi itakua hali yako huko Akhera uendako. Basi Mja Unatakiwa Ujiulize hivyo uko tayari hapa Ulimwenguni uteseke na huko Uendako pia ukateseke, uamuzi unao mwenyewe, na kama umefahamu anza sasa ili usiikose Pepo ya Mollah wako,na kumbuka hayo yote unayafanya upate raha na furaha, Na Mollah wako kakwambia ukifanya Ibada, utayapata hayo yote na zaidi katika Ufalme wake wa Milele.
Sunday, November 16, 2014
URADI WA DHIKR YA (KUMTAJA MOLLAH) PART 1
Asalaam Aleiykum
Kukumbuka kuko kwa aina mbili, aina ya kwanza ya kukumbuka ni kwa njia ya kuona, na aina ya pili ni huko kusikia au kutaja ambacho ni kitendo kimoja kisichokua na tafauti na kuzungumza, kwani njia utaratibu ni uleule wa kusikia sauti ndio maana hata huyo mzungumzaji lazima atoe au apate (Gap) ya kuweza kulisikia analo zungumza au sivyo itakua tayari anasumbuliwa na matatizo kwenye Akili yake, (Ndio maana Mabingwa wa maradhi ya Akili wanatwambia tahadhari ukimuona mtu anazungumza sana bila ya kituo, jua huyo ana tatizo fulani na ukilichunguza utalijua).
Japokua kukumbuka ni jambo moja lakini hili la kutaja lina kazi maalum ambayo ndio msingi mzima wa darsa yetu ya leo ya (Kumtaja Allah).
Kabla ya kuanza na ufafanuzi huo napenda nikumbushe kitu kwa wale ambao kwa njia ya kusikia tu wanayapinga mambo bila ya kupata ithbati ya jambo hilo, bila ya kusoma au kufanya uchunguzi unasimama na kuharamisha kitu ambacho hufahamu undani wake, midamu umesikia Fulani kasema jambo hilo halifai na wewe unasimama kidete kulipinga, usifanye hivyo na wewe kwanza lipatie yakini ya kuto kufaa kwake, usisimame ukapinga na kukanusha kitu usichokua na uhakika nacho.
Kuna kisa kimoja itabidi mnipe nafasi nikieleze ili uwe mfano kwa watozingatia, Kuna kipindi katika Kisiwa cha (Zanzibar) walikuja (Wajapan) kwa ajili ya kujenga Barabara na wakatangaza wanataka wafanyakazi, wakenda vijana wenzangu na walipofika wakaambiwa kila mmoja aandike jina lake, walipokwisha andika yule (Mjapan) akaanza kuita yale majina akaita kama watu kumi yakabakia majina mawili "Na watu wawili tu ndio walobakia""Akaita (Sidilia Adalasi)kimya, akaita tena nani (Sidilia Adalasi)kimya akaendelea kuita lile jina lengine akabaki kijana mmoja kamuuliza wewe jina yako nani, yule kijana akajibu mimi naitwa (Said Bin Abdullah)akampa peni hebu andika jina lako, yule kijana akaandika (Sidilia Adalasi)"Maskini ikawa peke yake (Said Bin Abdullah) ndio alokosa kazi, Basi na wewe (Please)usianze kusimama ukawa unapinga mambo au kukataa Uradi, ukawa unawacheka wale wenye kudumisha utajo huu tukikupa kalamu uandike kumbe na wewe (Sidilia Adalasi) kasome nenda (Deep) jifunze ukisha kujua na kufahamu ndio njoo utuambie sasa nimegundua Uradi haufai.
Pia nataka uelewe kufahamu na kujua ni vitu viwili tafauti, kujua kunatokana na (Experience) na kufahamu kunatokana na hekima(Wisdom)ambayo anakupa Mollah wako, sasa kitizame kisa hichi kilichotokea kwenye kijiji fulani kwenye zama hizo za zamani, "Kwa Bahati katika kijiji kile alikuwepo Mtu mmoja tu ambaye kafundishwa kusoma, ikawa Barua za kijiji kizima anasoma yeye" yatizame mabega yake yakoje yalivyo beba kiburi ya kujiona kumbe peke yake ndie anayejua kusoma""Ikatokea siku moja Mama mmoja akamfata anataka aandikiwe Barua, Akamjibu Mguu unauma, yule Bibi akenda akarudi siku ya pili na kujibiwa tena mguu unauma, akasema yule Bibi leo siondoki mpaka unambie Mguu umehusiana nini na kuandika, akamjibu unajua kile kijiji iendako barua hii hakuna anoweza kusoma (Herufi)zangu mpaka nende mwenyewe" na siri kubwa kumbe alikua hajui kuandika, kwa hiyo kazi yake kuhifadhi yale maneno halafu ndio aende kijiji cha pili na kumwambia huyo alokusudiwa hiyo barua, na kijiji kikiwa mbali ndio lazima mguu utakuuma(umefahamu).
Endelea part 2
Kukumbuka kuko kwa aina mbili, aina ya kwanza ya kukumbuka ni kwa njia ya kuona, na aina ya pili ni huko kusikia au kutaja ambacho ni kitendo kimoja kisichokua na tafauti na kuzungumza, kwani njia utaratibu ni uleule wa kusikia sauti ndio maana hata huyo mzungumzaji lazima atoe au apate (Gap) ya kuweza kulisikia analo zungumza au sivyo itakua tayari anasumbuliwa na matatizo kwenye Akili yake, (Ndio maana Mabingwa wa maradhi ya Akili wanatwambia tahadhari ukimuona mtu anazungumza sana bila ya kituo, jua huyo ana tatizo fulani na ukilichunguza utalijua).
Japokua kukumbuka ni jambo moja lakini hili la kutaja lina kazi maalum ambayo ndio msingi mzima wa darsa yetu ya leo ya (Kumtaja Allah).
Kabla ya kuanza na ufafanuzi huo napenda nikumbushe kitu kwa wale ambao kwa njia ya kusikia tu wanayapinga mambo bila ya kupata ithbati ya jambo hilo, bila ya kusoma au kufanya uchunguzi unasimama na kuharamisha kitu ambacho hufahamu undani wake, midamu umesikia Fulani kasema jambo hilo halifai na wewe unasimama kidete kulipinga, usifanye hivyo na wewe kwanza lipatie yakini ya kuto kufaa kwake, usisimame ukapinga na kukanusha kitu usichokua na uhakika nacho.
Kuna kisa kimoja itabidi mnipe nafasi nikieleze ili uwe mfano kwa watozingatia, Kuna kipindi katika Kisiwa cha (Zanzibar) walikuja (Wajapan) kwa ajili ya kujenga Barabara na wakatangaza wanataka wafanyakazi, wakenda vijana wenzangu na walipofika wakaambiwa kila mmoja aandike jina lake, walipokwisha andika yule (Mjapan) akaanza kuita yale majina akaita kama watu kumi yakabakia majina mawili "Na watu wawili tu ndio walobakia""Akaita (Sidilia Adalasi)kimya, akaita tena nani (Sidilia Adalasi)kimya akaendelea kuita lile jina lengine akabaki kijana mmoja kamuuliza wewe jina yako nani, yule kijana akajibu mimi naitwa (Said Bin Abdullah)akampa peni hebu andika jina lako, yule kijana akaandika (Sidilia Adalasi)"Maskini ikawa peke yake (Said Bin Abdullah) ndio alokosa kazi, Basi na wewe (Please)usianze kusimama ukawa unapinga mambo au kukataa Uradi, ukawa unawacheka wale wenye kudumisha utajo huu tukikupa kalamu uandike kumbe na wewe (Sidilia Adalasi) kasome nenda (Deep) jifunze ukisha kujua na kufahamu ndio njoo utuambie sasa nimegundua Uradi haufai.
Pia nataka uelewe kufahamu na kujua ni vitu viwili tafauti, kujua kunatokana na (Experience) na kufahamu kunatokana na hekima(Wisdom)ambayo anakupa Mollah wako, sasa kitizame kisa hichi kilichotokea kwenye kijiji fulani kwenye zama hizo za zamani, "Kwa Bahati katika kijiji kile alikuwepo Mtu mmoja tu ambaye kafundishwa kusoma, ikawa Barua za kijiji kizima anasoma yeye" yatizame mabega yake yakoje yalivyo beba kiburi ya kujiona kumbe peke yake ndie anayejua kusoma""Ikatokea siku moja Mama mmoja akamfata anataka aandikiwe Barua, Akamjibu Mguu unauma, yule Bibi akenda akarudi siku ya pili na kujibiwa tena mguu unauma, akasema yule Bibi leo siondoki mpaka unambie Mguu umehusiana nini na kuandika, akamjibu unajua kile kijiji iendako barua hii hakuna anoweza kusoma (Herufi)zangu mpaka nende mwenyewe" na siri kubwa kumbe alikua hajui kuandika, kwa hiyo kazi yake kuhifadhi yale maneno halafu ndio aende kijiji cha pili na kumwambia huyo alokusudiwa hiyo barua, na kijiji kikiwa mbali ndio lazima mguu utakuuma(umefahamu).
Endelea part 2
URADI WA DHIKR YA (KUMTAJA MOLLAH) PART 2
Asalaam Aleiykum
Siri yenyewe yule Bwana alikua hajui kuandika ila yeye anajua kusoma, basi na wewe nenda kajifundishe elimu zote, elimu ni bahari ambazo kwenye Ulimwengu huu zipo tano,(Indian ocean, Pacific, Nk)kwa hiyo koga zote ili tukija kukuuliza usitwambie Mguu unakuuma, Na mwisho Usije kumlaumu(Doctor) wa Miwani kwa kuwa kakwambia ukipima miwani utaweza kusoma na kuandika, jilaumu mwenyewe kwanini hukujifunza kusoma na kuandika, ukimaliza hapo na wewe utakua na Mamlaka ya kusema (Dhikiri Haifai).
Sasa Tunaanza Darsa yetu kwa kujiuliza nini (Dhikiri)?ya kumtaja Mollah.
Wacha nikupe Dawa hii ambayo yaweza kukuponesha maradhi mengi na kukufanya Mja mwenye Afya nzuri kabisa, Kama nilivyosema mwanzoni Dhikiri zipo za aina mbili zenye kuashiria kitu kimoja, ile ya aina ya kwanza wewe imekushinda, ile ya kumkumbuka Mollah wako kwa kuona Nyota na Mwezi, kwa kuangalia Jua na Mbingu, kwa Kutizama Miti na Wanyama hayo yote haya kukumbushi Mollah wako, Na unaijua Sababu kubwa mpaka yakajiri hayo?. Sababu Kichwa kimejaa(Gossip)Kichwa kimejaa Siasa na Biashara, kichwa kina mambo mengi (Cinema)zimo humo, Utajiri umo humo, Umaskini umo humo, hasira na magonvi yote yamejaa kwenye kichwa hicho, wanawake na wanaume wote umewarekodi wewe, kila kitu Mja wewe unakihifadhi katika kichwa hicho, vipi leo unaweza kuwa na nafasi ya kumkumbuka Mollah wako.
Ukijiangalia Mja wewe kila baada ya sekunde chache Fikra za kila aina zinakujia kichwani humo, mara mipira mara madeni, mara nyimbo na mikasa ya kila aina, na kwa hali hiyo hakuna kabisa nafasi ya kumkumbuka Mollah wako.
Sasa nini Kifanyike?
Ndio Wale walotangulia wenye Hekima wakatafuta njia nyengine ya kumkumbuka Mollah wao kwa kuhama kutoka Juu kwenye Akili na kushuka chini kwenye Moyo. Na kwenye Moyo hakuna lugha nyengine inayofahamika isipokua utajo wa Mollah wako, huo ndio (Uradi), hiyo ndio dawa pekee ambayo ntakupa utumie kutwa mara zote. Sio ule Uradi wenu mnosoma wiki mara moja ile ni dua Uradi ni huu wa kudumisha kwa njia ya kurejea utajo wa Mollah wako, chukua dawa hii ya kumsabahi Mollah wako kwa majina yake yote 99.
Mimi nimekuchagulia hili la (Laa illah illah Allah)lidumishe ndani yake kuna siri kubwa, kuna mambo makubwa. Endelea part 3
Siri yenyewe yule Bwana alikua hajui kuandika ila yeye anajua kusoma, basi na wewe nenda kajifundishe elimu zote, elimu ni bahari ambazo kwenye Ulimwengu huu zipo tano,(Indian ocean, Pacific, Nk)kwa hiyo koga zote ili tukija kukuuliza usitwambie Mguu unakuuma, Na mwisho Usije kumlaumu(Doctor) wa Miwani kwa kuwa kakwambia ukipima miwani utaweza kusoma na kuandika, jilaumu mwenyewe kwanini hukujifunza kusoma na kuandika, ukimaliza hapo na wewe utakua na Mamlaka ya kusema (Dhikiri Haifai).
Sasa Tunaanza Darsa yetu kwa kujiuliza nini (Dhikiri)?ya kumtaja Mollah.
Wacha nikupe Dawa hii ambayo yaweza kukuponesha maradhi mengi na kukufanya Mja mwenye Afya nzuri kabisa, Kama nilivyosema mwanzoni Dhikiri zipo za aina mbili zenye kuashiria kitu kimoja, ile ya aina ya kwanza wewe imekushinda, ile ya kumkumbuka Mollah wako kwa kuona Nyota na Mwezi, kwa kuangalia Jua na Mbingu, kwa Kutizama Miti na Wanyama hayo yote haya kukumbushi Mollah wako, Na unaijua Sababu kubwa mpaka yakajiri hayo?. Sababu Kichwa kimejaa(Gossip)Kichwa kimejaa Siasa na Biashara, kichwa kina mambo mengi (Cinema)zimo humo, Utajiri umo humo, Umaskini umo humo, hasira na magonvi yote yamejaa kwenye kichwa hicho, wanawake na wanaume wote umewarekodi wewe, kila kitu Mja wewe unakihifadhi katika kichwa hicho, vipi leo unaweza kuwa na nafasi ya kumkumbuka Mollah wako.
Ukijiangalia Mja wewe kila baada ya sekunde chache Fikra za kila aina zinakujia kichwani humo, mara mipira mara madeni, mara nyimbo na mikasa ya kila aina, na kwa hali hiyo hakuna kabisa nafasi ya kumkumbuka Mollah wako.
Sasa nini Kifanyike?
Ndio Wale walotangulia wenye Hekima wakatafuta njia nyengine ya kumkumbuka Mollah wao kwa kuhama kutoka Juu kwenye Akili na kushuka chini kwenye Moyo. Na kwenye Moyo hakuna lugha nyengine inayofahamika isipokua utajo wa Mollah wako, huo ndio (Uradi), hiyo ndio dawa pekee ambayo ntakupa utumie kutwa mara zote. Sio ule Uradi wenu mnosoma wiki mara moja ile ni dua Uradi ni huu wa kudumisha kwa njia ya kurejea utajo wa Mollah wako, chukua dawa hii ya kumsabahi Mollah wako kwa majina yake yote 99.
Mimi nimekuchagulia hili la (Laa illah illah Allah)lidumishe ndani yake kuna siri kubwa, kuna mambo makubwa. Endelea part 3
URADI WA DHIKR YA (KUMTAJA MOLLAH) PART 3
Asalaam Aleiykum
Nini Uradi?
Uradi ni nyenzo au (Method) ya kuinyanganya (Mind)Akili uwezo wake wa kukutawala kama ifanyavyo hivi sasa, Ndio walo wema walotangulia wakafanya njia hii ya kuidunda(Kuipiga)Akili kwa Majina ya Mwenye enzi Mungu, wakafanya hivyo kwa kutumia mambo matatu (Body, Mind, and Soul)kwa hiyo msipite mkawakejeli(Kuwafanyia mzaha) wazee kwa kushika (Tasbih mikononi)Tasbih maana yake ni (Body) inakumbuka na (Mind)kazi yake inahesabu na (Soul)Roho inataja na hakuna maana nyengine isipokua ndio hiyo ya Uradi.
Na yakijumuika na kukusanyika pamoja mambo hayo matatu katika huo Uradi wa Kumtaja Mollah kwa njia ya marejeo (Repitition)utaanza kuona zile fikra za Maimuna au Muumin, au za mpira na nyimbo zinaanza kutoweka kidogo kidogo mpaka unafikia wakati hakuna tena mawazo au fikra za kipuuzi katika (Mind)Akili yako ila linabaki jina la Mollah wako.
Na ukifikia hatua hiyo inakua wewe sasa uko tayari kwenda (Beyond name to the Nameless)Utakuwa wewe tayari ushafika kwa wale wenye kutajwa katika sura ya (Al-Imran aya ya 191)
"ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَـٰمً۬ا وَقُعُودً۬ا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَڪَّرُونَ فِى خَلۡقِ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَـٰذَا بَـٰطِلاً۬ سُبۡحَـٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ"
Ambao humkumbuka Mwenye enzi Mungu wakiwa wima(Wamesimama)na wakikaa na wakilala, na hufikiri Umbo la Mbingu na Ardhi(wakasema)Mollah wetu hukuviumba hivi bure, Utukufu ni wako, Basi tuepushe na adhabu ya Moto.
Na wewe sasa utakua unamtaja Mollah wako mpaka ukiwa usingizini, akiwa kuna Mtu analala na wewe basi anaweza kusikia kukoroma kwako kunataja (Laa illah Ilah Allah).
Na hizo ndizo faida za Uradi umeshindwa kwenye akili sasa shuka moyoni uwe kama hao walotajwa katika hiyo aya, na utaanza kuona kwa mara ya mwanzo moyo unashukiwa na mapenzi, wakati wote utakua furahani ukiwa sokoni au barazani wewe utakua unamtaja Mollah wako, jaribu japo wiki uone faida yake, na ukijaa mapenzi ya Mollah wako ndio unapanda kwenye daraja nyengine ya Imani unaingia katika kundi la wale walotajwa katika sura ya (Israa aya ya 107)
"قُلۡ ءَامِنُواْ بِهِۦۤ أَوۡ لَا تُؤۡمِنُوٓاْۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ مِن قَبۡلِهِۦۤ إِذَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡہِمۡ يَخِرُّونَ لِلۡأَذۡقَانِ سُجَّدً۬ا "
Sema Iamini au Msiamini(Hiyo Quraan) Hakika wale walopewa Elimu (Zamani)kabla hii(ya Quraan)wanaposomewa(aya zetu)huanguka kifudi fudi wanasujdu.
Huo ndio Uradi , hivyo ndio ukishiba Jina la Mwenye enzi Mungu utakavyokua, japo kwa sasa utaona haya kwa kudhani watu watasemaje lakini utasujudu mayoni kama vile afanyavyo mgonjwa, Huo ndio Uradi udumishe ukupele (Beyond) hiyo ndio itakua dawa yako ya kuondokewa na Dhiki moyoni mwako na pia katika maisha yako. Ukitaka soma kwa sauti au kimya kimya kwenye moyo wako yote ni sawa. Sio Haramu wala hukosei.
Nini Uradi?
Uradi ni nyenzo au (Method) ya kuinyanganya (Mind)Akili uwezo wake wa kukutawala kama ifanyavyo hivi sasa, Ndio walo wema walotangulia wakafanya njia hii ya kuidunda(Kuipiga)Akili kwa Majina ya Mwenye enzi Mungu, wakafanya hivyo kwa kutumia mambo matatu (Body, Mind, and Soul)kwa hiyo msipite mkawakejeli(Kuwafanyia mzaha) wazee kwa kushika (Tasbih mikononi)Tasbih maana yake ni (Body) inakumbuka na (Mind)kazi yake inahesabu na (Soul)Roho inataja na hakuna maana nyengine isipokua ndio hiyo ya Uradi.
Na yakijumuika na kukusanyika pamoja mambo hayo matatu katika huo Uradi wa Kumtaja Mollah kwa njia ya marejeo (Repitition)utaanza kuona zile fikra za Maimuna au Muumin, au za mpira na nyimbo zinaanza kutoweka kidogo kidogo mpaka unafikia wakati hakuna tena mawazo au fikra za kipuuzi katika (Mind)Akili yako ila linabaki jina la Mollah wako.
Na ukifikia hatua hiyo inakua wewe sasa uko tayari kwenda (Beyond name to the Nameless)Utakuwa wewe tayari ushafika kwa wale wenye kutajwa katika sura ya (Al-Imran aya ya 191)
"ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَـٰمً۬ا وَقُعُودً۬ا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَڪَّرُونَ فِى خَلۡقِ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَـٰذَا بَـٰطِلاً۬ سُبۡحَـٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ"
Ambao humkumbuka Mwenye enzi Mungu wakiwa wima(Wamesimama)na wakikaa na wakilala, na hufikiri Umbo la Mbingu na Ardhi(wakasema)Mollah wetu hukuviumba hivi bure, Utukufu ni wako, Basi tuepushe na adhabu ya Moto.
Na wewe sasa utakua unamtaja Mollah wako mpaka ukiwa usingizini, akiwa kuna Mtu analala na wewe basi anaweza kusikia kukoroma kwako kunataja (Laa illah Ilah Allah).
Na hizo ndizo faida za Uradi umeshindwa kwenye akili sasa shuka moyoni uwe kama hao walotajwa katika hiyo aya, na utaanza kuona kwa mara ya mwanzo moyo unashukiwa na mapenzi, wakati wote utakua furahani ukiwa sokoni au barazani wewe utakua unamtaja Mollah wako, jaribu japo wiki uone faida yake, na ukijaa mapenzi ya Mollah wako ndio unapanda kwenye daraja nyengine ya Imani unaingia katika kundi la wale walotajwa katika sura ya (Israa aya ya 107)
"قُلۡ ءَامِنُواْ بِهِۦۤ أَوۡ لَا تُؤۡمِنُوٓاْۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ مِن قَبۡلِهِۦۤ إِذَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡہِمۡ يَخِرُّونَ لِلۡأَذۡقَانِ سُجَّدً۬ا "
Sema Iamini au Msiamini(Hiyo Quraan) Hakika wale walopewa Elimu (Zamani)kabla hii(ya Quraan)wanaposomewa(aya zetu)huanguka kifudi fudi wanasujdu.
Huo ndio Uradi , hivyo ndio ukishiba Jina la Mwenye enzi Mungu utakavyokua, japo kwa sasa utaona haya kwa kudhani watu watasemaje lakini utasujudu mayoni kama vile afanyavyo mgonjwa, Huo ndio Uradi udumishe ukupele (Beyond) hiyo ndio itakua dawa yako ya kuondokewa na Dhiki moyoni mwako na pia katika maisha yako. Ukitaka soma kwa sauti au kimya kimya kwenye moyo wako yote ni sawa. Sio Haramu wala hukosei.
Sunday, November 9, 2014
MUANGAZA WA ROHO PART 1
Asalaam Aleiykum
Leo nakuomba safiri na mimi ili tuishi katika aya ya 85 ya sura ya (Israa) tupate kuhisi Muangaza wa (Roho)tujue ikoje taa yake.
وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلرُّوحِۖ قُلِ ٱلرُّوحُ مِنۡ أَمۡرِ رَبِّى وَمَآ أُوتِيتُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِ إِلَّا قَلِيلاً۬
Na Wanakuuliza habari ya Roho, Sema Roho ni Jambo lilohusika na (Amri)ya Mollah wangu. Na nyinyi hamkupewa katika elimu isipokua kidogo (Hivi).
Kumbuka kila mmoja wetu anauliza swali hili, ikiwa haulizi kwa mtu anajiuliza yeye mwenyewe, nini hasa hii Roho? kwanini likaja swali hili, lazima (Deep) katika nafsi zetu kuna Kiu(Thirsty) ya kutaka kujua nini hii Roho? kweli inaishi maisha, na kila mtu anauliza swali hili kutaka kujitosheleza kwa kuamini hakuna mwisho ila kuna uwepo wa kudumu milele, hamu kubwa na shauku Mwanaadamu imemkamata kulijua hili, Na kila mara japo ukilisukuma swali hili lisirudi ndio kwanza linazidi kukuandama.
Sasa ufanye nini? ndio kila mara mtu inabidi aende kuchungulia katika kisima hichi cha fikra ili apate kuona kama kuna maji apate kukata kiu yake ya kuijua Roho. Lakini kawaida ya kisima inataka ufanye kazi kupata kuyaona hayo maji kama yapo, sababu kisima ni kikubwa sana, hata ukipata huo Muangaza ukayaona maji inabidi ufanye jitihada ya kuyachota maji hayo.
"Wanakuuliza nini Habari ya Roho"
Napenda utambue waulizaji wa habari hizi si watoto au vijana ni mara chache sana wenye umri wa rika hilo kuulizia habari kama hizi,Waulizaji wakubwa wa habari hizi ni wale walofikia Umuri wa makamo au rika ya uzee. Pia napenda kukufahamisha waulizaji wako wengi lakini wafatiliaji ni wachache sana, Na sababu kubwa safari hii ya uchunguzi wa kujua nini Roho inatisha, ni safari mja unatakiwa uende peke yako, huna mshirika, na hivi sasa wakati ndio umefika, pengine watoto wameshakua na kuondoka nyumbani, Majumba umeshajenga yamemalizika, Mapesa (Bank)yamefurika, huna tena la kufanya, hakuna la zaidi, sasa swali hili ndio linakuja kila mara nini Roho?.
Na ukiona swali hili linakujia mara kwa mara basi elewa bila shaka limegusana na Mauti(Sio kwamba unakufa lakini ni njia moja ya Ulimwengu huu kukupa habari za hiyo siku ya siku). kwa hiyo ukiwa katika wale walo wengi ambao wanaogopa swali hili hapo tena utaanza kutafuta vitu vya kukusahaulisha, utaanza kukimbilia senema(Cinema)mara kwenye ma(Disco)hukosekani, kwenye Taarab wewe unakua wa mwanzo kuingia na wa mwisho kutoka, na kila sehemu inayokufanya wewe usahau habari hii wewe ndio unakua (Kinara wake)ili upate nafasi ya kusahau kuijua kadhia hii ya Roho.
Endelea part 2
Leo nakuomba safiri na mimi ili tuishi katika aya ya 85 ya sura ya (Israa) tupate kuhisi Muangaza wa (Roho)tujue ikoje taa yake.
وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلرُّوحِۖ قُلِ ٱلرُّوحُ مِنۡ أَمۡرِ رَبِّى وَمَآ أُوتِيتُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِ إِلَّا قَلِيلاً۬
Na Wanakuuliza habari ya Roho, Sema Roho ni Jambo lilohusika na (Amri)ya Mollah wangu. Na nyinyi hamkupewa katika elimu isipokua kidogo (Hivi).
Kumbuka kila mmoja wetu anauliza swali hili, ikiwa haulizi kwa mtu anajiuliza yeye mwenyewe, nini hasa hii Roho? kwanini likaja swali hili, lazima (Deep) katika nafsi zetu kuna Kiu(Thirsty) ya kutaka kujua nini hii Roho? kweli inaishi maisha, na kila mtu anauliza swali hili kutaka kujitosheleza kwa kuamini hakuna mwisho ila kuna uwepo wa kudumu milele, hamu kubwa na shauku Mwanaadamu imemkamata kulijua hili, Na kila mara japo ukilisukuma swali hili lisirudi ndio kwanza linazidi kukuandama.
Sasa ufanye nini? ndio kila mara mtu inabidi aende kuchungulia katika kisima hichi cha fikra ili apate kuona kama kuna maji apate kukata kiu yake ya kuijua Roho. Lakini kawaida ya kisima inataka ufanye kazi kupata kuyaona hayo maji kama yapo, sababu kisima ni kikubwa sana, hata ukipata huo Muangaza ukayaona maji inabidi ufanye jitihada ya kuyachota maji hayo.
"Wanakuuliza nini Habari ya Roho"
Napenda utambue waulizaji wa habari hizi si watoto au vijana ni mara chache sana wenye umri wa rika hilo kuulizia habari kama hizi,Waulizaji wakubwa wa habari hizi ni wale walofikia Umuri wa makamo au rika ya uzee. Pia napenda kukufahamisha waulizaji wako wengi lakini wafatiliaji ni wachache sana, Na sababu kubwa safari hii ya uchunguzi wa kujua nini Roho inatisha, ni safari mja unatakiwa uende peke yako, huna mshirika, na hivi sasa wakati ndio umefika, pengine watoto wameshakua na kuondoka nyumbani, Majumba umeshajenga yamemalizika, Mapesa (Bank)yamefurika, huna tena la kufanya, hakuna la zaidi, sasa swali hili ndio linakuja kila mara nini Roho?.
Na ukiona swali hili linakujia mara kwa mara basi elewa bila shaka limegusana na Mauti(Sio kwamba unakufa lakini ni njia moja ya Ulimwengu huu kukupa habari za hiyo siku ya siku). kwa hiyo ukiwa katika wale walo wengi ambao wanaogopa swali hili hapo tena utaanza kutafuta vitu vya kukusahaulisha, utaanza kukimbilia senema(Cinema)mara kwenye ma(Disco)hukosekani, kwenye Taarab wewe unakua wa mwanzo kuingia na wa mwisho kutoka, na kila sehemu inayokufanya wewe usahau habari hii wewe ndio unakua (Kinara wake)ili upate nafasi ya kusahau kuijua kadhia hii ya Roho.
Endelea part 2
MUANGAZA WA ROHO PART 2
Asalaam Aleiykum
Lakini ukiwa katika wale wachache ambao kwa Ushujaa wanalikabili swali hili la nini Roho?, Basi wewe ndio katika wale wanoanza ile Safari ndefu yenye kutisha, yenye miujiza na mambo ya ajabu, Safari yenyewe ni ngumu lakini inaendeka. Kinachotakiwa katika safari yako hii ni yakini katika moyo wako kuwa sasa nachupa nimeamua kutumbukia kisimani kitachonikuta sawa lakini lazima nijijue mimi nani.
Na mwanzo kabisa ukiamua kuchupa kuanza safari hii na kuuliza nini Roho?ina maana ushafanya (Tafauti)baina yako na huo Mwili(Body)zishakujia fikra kuwa wewe sio huu Mwili, kuna kitu chengine ambacho unataka ukijue, hapo tena ndio unaanza hiyo(Sipiritual journey)ambayo imeitwa safari ndefu.
"Wanakuuliza habari ya Roho sema(Waambie)" wala hakuna makosa mtu kutaka kujua nini Roho, cha muhimu kwanza kabisa uelewe kuwa hata hiyo (Body) Mwili wako si mali yako, ni zawadi uliyopewa nusu kutoka kwa Baba yako na nusu nyengine kutoka kwa Mama yako, halafu tena ndio unaendelezwa Mwili wako huo kwa njia ya chakula, sasa ukiwa huu mwili ni hicho chakula mimi nilobakia nisokua chakula mimi ni nani?, Nimetokea wapi, na wapi ninapo kwenda. Nini habari yangu mimi siku ile nitakapozimika,nini kinatokezea?.
"Wanakuuliza nini habari ya Roho Sema" uwaambie hakika ya hiyo Roho ni (Amri)ya Mollah wangu, ndio maana utaona mambo yote yenye kuhusiana na Roho unayakabili peke yako, umeshapata kujiuliza nani huyu Mke wangu au Mume wangu, nani hawa watoto wangu, wote hawa wametokea wapi, mbona naona sote sisi kama wageni tulokutana katika Ulimwengu huu, Jee hii ndio ile maana ya watoto zenu na mali zenu ni adui kwenu? unainza safari hii kwa unyenyekevu mkubwa kabisa, huku ukijua kumbe katika mambo ya Kiroho niko peke yangu, na kila kitu nitakikabili peke yangu, hayatonifaa mali wala watoto ila lazima nirudi kwa Mollah wangu nikiwa safi, sasa Nani huyu anaye Rudi?
"Wanakuuliza nini habari ya Roho Sema" Waambie hiyo Roho ni kwa ajili ya (Amri) ya Mwenye enzi Mungu, Neno Amri inafaa tulizingatie sana tafsiri ya neno hili, Watu wengi wanadhani au wanashindwa kutafautisha baina ya Amri na maagizo, Amri ni tendo lisilopingika wala kubadilika isipokua mpaka atake huyo Mwenye kutoa Amri Mwenye Enzi Mungu mwenye Ufalme wa Milele.
Hizi zenu mnazotoa nyinyi si Amri sababu amri haipingiki, hayo yenu ni maagizo ndio maana kuna wakati mtu anakwenda kinyume na kiongozi au bosi wake, kwa kuwa hayo ni maagizo hawana hakika nayo ndio sababu pakawekwa washauri kuwasaidia kupitisha hayo maagizo. Ukilizingatia vizuri hili neno Amri litakusaidia pakubwa katika safari yako hii ya kutafuta Muangaza wa Roho.
Waambie habari hii wala usiwafiche kuwa imehusiana na Mwenye enzi Mungu na yoyote yule Mwenye kutaka kuijua habari hii anarudi kwa Mollah wake, Na kurudi huku ndiko kunakujulisha ukajua kila kitu katika Ulimwengu huu kinatii hiyo Amri ya Mwenye enzi Mungu, Mpaka huo Mwili wako (Body)unatii Amri hiyo, Moyo unapiga kwa kutii amri hiyo, Ini linasafisha damu kwa amri hiyo, damu inasambazwa kwenye Mwili kutokana na amri hiyo ikitimizwa na hewa itokayo nje unayovuta bila ya tabu wala kuitaka au kuikataa, ni katika mazingira ya kuitii Amri itokayo kwa Mollah wako, Mwili unahisi njaa unakula chakula, ikisha kinasagwa kwa kutii Amri hiyo, ikisha mwili ukichoka unalala hayo yote sio wewe, sasa wewe ni kitu gani?
Endelea part 3
Lakini ukiwa katika wale wachache ambao kwa Ushujaa wanalikabili swali hili la nini Roho?, Basi wewe ndio katika wale wanoanza ile Safari ndefu yenye kutisha, yenye miujiza na mambo ya ajabu, Safari yenyewe ni ngumu lakini inaendeka. Kinachotakiwa katika safari yako hii ni yakini katika moyo wako kuwa sasa nachupa nimeamua kutumbukia kisimani kitachonikuta sawa lakini lazima nijijue mimi nani.
Na mwanzo kabisa ukiamua kuchupa kuanza safari hii na kuuliza nini Roho?ina maana ushafanya (Tafauti)baina yako na huo Mwili(Body)zishakujia fikra kuwa wewe sio huu Mwili, kuna kitu chengine ambacho unataka ukijue, hapo tena ndio unaanza hiyo(Sipiritual journey)ambayo imeitwa safari ndefu.
"Wanakuuliza habari ya Roho sema(Waambie)" wala hakuna makosa mtu kutaka kujua nini Roho, cha muhimu kwanza kabisa uelewe kuwa hata hiyo (Body) Mwili wako si mali yako, ni zawadi uliyopewa nusu kutoka kwa Baba yako na nusu nyengine kutoka kwa Mama yako, halafu tena ndio unaendelezwa Mwili wako huo kwa njia ya chakula, sasa ukiwa huu mwili ni hicho chakula mimi nilobakia nisokua chakula mimi ni nani?, Nimetokea wapi, na wapi ninapo kwenda. Nini habari yangu mimi siku ile nitakapozimika,nini kinatokezea?.
"Wanakuuliza nini habari ya Roho Sema" uwaambie hakika ya hiyo Roho ni (Amri)ya Mollah wangu, ndio maana utaona mambo yote yenye kuhusiana na Roho unayakabili peke yako, umeshapata kujiuliza nani huyu Mke wangu au Mume wangu, nani hawa watoto wangu, wote hawa wametokea wapi, mbona naona sote sisi kama wageni tulokutana katika Ulimwengu huu, Jee hii ndio ile maana ya watoto zenu na mali zenu ni adui kwenu? unainza safari hii kwa unyenyekevu mkubwa kabisa, huku ukijua kumbe katika mambo ya Kiroho niko peke yangu, na kila kitu nitakikabili peke yangu, hayatonifaa mali wala watoto ila lazima nirudi kwa Mollah wangu nikiwa safi, sasa Nani huyu anaye Rudi?
"Wanakuuliza nini habari ya Roho Sema" Waambie hiyo Roho ni kwa ajili ya (Amri) ya Mwenye enzi Mungu, Neno Amri inafaa tulizingatie sana tafsiri ya neno hili, Watu wengi wanadhani au wanashindwa kutafautisha baina ya Amri na maagizo, Amri ni tendo lisilopingika wala kubadilika isipokua mpaka atake huyo Mwenye kutoa Amri Mwenye Enzi Mungu mwenye Ufalme wa Milele.
Hizi zenu mnazotoa nyinyi si Amri sababu amri haipingiki, hayo yenu ni maagizo ndio maana kuna wakati mtu anakwenda kinyume na kiongozi au bosi wake, kwa kuwa hayo ni maagizo hawana hakika nayo ndio sababu pakawekwa washauri kuwasaidia kupitisha hayo maagizo. Ukilizingatia vizuri hili neno Amri litakusaidia pakubwa katika safari yako hii ya kutafuta Muangaza wa Roho.
Waambie habari hii wala usiwafiche kuwa imehusiana na Mwenye enzi Mungu na yoyote yule Mwenye kutaka kuijua habari hii anarudi kwa Mollah wake, Na kurudi huku ndiko kunakujulisha ukajua kila kitu katika Ulimwengu huu kinatii hiyo Amri ya Mwenye enzi Mungu, Mpaka huo Mwili wako (Body)unatii Amri hiyo, Moyo unapiga kwa kutii amri hiyo, Ini linasafisha damu kwa amri hiyo, damu inasambazwa kwenye Mwili kutokana na amri hiyo ikitimizwa na hewa itokayo nje unayovuta bila ya tabu wala kuitaka au kuikataa, ni katika mazingira ya kuitii Amri itokayo kwa Mollah wako, Mwili unahisi njaa unakula chakula, ikisha kinasagwa kwa kutii Amri hiyo, ikisha mwili ukichoka unalala hayo yote sio wewe, sasa wewe ni kitu gani?
Endelea part 3
MUANGAZA WA ROHO PART 3
Asalaam Aleiykum
Kuna kitu ambacho ni muhimu sana kukijua ndio maana unahimizwa kukumbuka mauti, kwanini ikawa Mauti kwa sababu Mauti yanachukua kila kitu isipokua kitu hicho ambayo ndio hiyo Roho,ndio hiyo wewe ambaye sasa hivi unaisoma habari hii, Na siri ya kukumbuka Mauti nikuwa kila ukikumbuka Mauti unapunguza dhanmbi, na dhanmbi zikipungua inakua rahisi kuijua Roho yako(قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّٮٰهَا)"Bila shaka Amefuzu aliyeitakasa(Roho yake) .
"Wanakuuliza habari ya Roho Sema"
Tutizame sasa hili neno Amri linatokea wapi, Neno Amri ni tafsiri ile ile ya Majaala, na tutizame hili neno la kujaaliwa ni Amri hii inayopitishwa na Mwenyewe Mwenye enzi Mungu kama alivyosema kwenye aya nyingi mimi nitazitumia mbili ili zipate kutufungua macho tuweze kuona Muangaza wa Roho.
وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَىۡءٍ حَىٍّۖ
"Na tukajaalia(Kufanya)kwa maji kila kitu kilicho Hai"
Kitu chochote kilicho hai kimefanywa kwa Maji, hapo itakuonesha vipi vyengine ambavyo vikiwa havipo hai vinavyokua, mtizame Maiti wa Binaadamu au Mnyama akisha kufa anakuaje dalili ya mwanzo anaanza kuoza na (source)ya maji inakatika katika mwili huo ndio maana tunamwita Maiti na ukimfufua utaona keshakauka,maji yamemalizika, kwa hiyo katika Ulimwengu huu tumeoneshwa vilivyo hai na vilivyokufa, kimoja kinategemea maji na chengine maji yashatoweka, chochote kile kisichotegemea maji kinakua Maiti, ile amri ya maji kuwepo kwenye kitu hicho imeshakatika, kumbuka vyote vinaishi ila kimoja katika uhai na chengine katika umauti, Na hiyo Roho yako inaishi katika sehemu hizo zote mbili,kwa hiyo kama huamini kufufuliwa zingatia sana habari hii nilokupa halafu uifanyie kazi. Katika daraja hilo la maisha ndipo ilipo Roho yako kwa amri ya Mwenye enzi Mungu.
"Wanakuuliza nini habari ya Roho sema" Na waambie kwa Amri hiyo hiyo ya kujaaliwa na nyinyi mnapewa vitu muhimu sana navyo ni sura ya As-Sajda aya ya 9.
ثُمَّ سَوَّٮٰهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِۦۖ وَجَعَلَ لَكُمُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَـٰرَ وَٱلۡأَفۡـِٔدَةَۚ قَلِيلاً۬ مَّا تَشۡڪُرُونَ
Kisha akamtengeneza(Kumuumba) na Akampulizia Roho yake, na akakupeni masikio na macho na nyoyo, ni kidogo tu shukurani yenu.
Baada ya kwisha kuumbwa ukapuliziwa Roho itokayo na yeye Mwenyewe Mwenye enzi Mungu, ndio maana nikasema safari ya kutaka kuijua Roho ni kurejea kwa Mollah wako, ndio maana nikasema ni safari ya miujiza na yenye kutisha, ikapulizwa hiyo Roho katika hiyo (Body)yako, kwa hiyo Roho inaishi katika mwili wako lakini haikamatani na mwili wako, ndio maana ukaona mwili unafanya kazi zake pasi kuingiliwa na Roho,Lakini Roho ndio yenye ku (Control)huo mwili kwa kuwa wewe ni Khalifa wa huo mwili na hii Ardhi, halafu ukapewa hii amri au Jaala ya kuona na kusikia, Ifikiri sana habari hii ya kuona na kusikia, ina mazingatio makubwa katika muangaza wa Roho, huu ni uwezo wa kutoka kwa Mollah wako ndio maana utaona wakati wa usingizi wako amri hii unaondoshewa kwenye (Deep sleep)ukirejea kwa Mollah wako kikamilifu, na wakati Mwengine unakua nayo amri hii ndio unaona hizo ndoto na kusikia sauti, Ni lazima upewe viwili hivi adhimu ili upate uhai kwa ukamilifu na kama huna viwili hivi bado Roho yako iko hai lakini imenyimwa amri hii(Jaala)ya Muumba wako, ukapewa na huo Moyo ili uweze kujua, kumbuka macho ni kuona, masikio ni kusikia, halafu ukapewa na huu Moyo ili uwe na uwezo wa kujua, kupenda, kufahamu na hekima ya kuweza kuijua Roho yako. Kwa sasa hivi huwezi kujua moyo ulokusudiwa hapa mpaka ukifika mbali katika hiyo safari yako ya (Sipiritual Journey) ndio utajua alaa kumbe moyo una kazi mbili, na hii ya pili ndio ilokusudiwa katika Muangaza wa Roho.
Wanakuuliza nini habari ya Roho sema, ni jambo lilohusiana na (Amri) ya Mollah wangu, Na wala hamkupewa elimu isipokua kidogo.
Hakukataa Mwenye enzi Mungu wala hakuzuia mtu kutaka kujua nini hiyo Roho,ili kasema Elimu mliyopewa ni chache(Kidogo) basi mtu na aitafute asaa anaweza kupewa elimu ya Roho akaijua na ukiijua Roho yako, utapata ufahamu vipi ukawa wewe Khalifa katika Ardhi hii, usisubiri mpaka siku ya kufa ndio ukaijua Roho yako, anza sasa hivi kwa kujitakasa na kuusafisha moyo wako utaipata elimu hiyo, kumbukuka imetolewa kidogo lakini haikuzuiliwa kutolewa, Elimu zinazidi kutolewa, tunaendelea kuvumbua mambo,, na sote siku ya kufa tunakutana na roho zetu kwa hiyo hakuna jambo la kuogopa ima usubiri siku ya kufa au anza sasa hivi, na ukianza sasa hivi basi unakwenda (Beyond death),hiyo ndio maana "Ya Ewe Mja wangu mwema Rejea kwangu ukiwa umeridhi na kuridhiwa"(Operation ya Mauti inaendelea wewe unaangalia, unajijua sina cha kuhofia, mimi Roho narejea kwa yule alonileta, na wala sina khofu tena ya Operation hii), lakini kwanza lazima usafishe machafu yako, omba maghfira kwa wingi ili uitakase Roho yako,ikiwa safi hapo utaona Muangaza wake, utaona Muujiza wake, fanya safari hii muhimu ya Muangaza wa Roho na ukipata Muangaza huu wewe ushafanikiwa, hukai tena ukalinda mali ya Ulimwengu huu, hakuna chochote kitakacho kudhuru na utakua karibu sana na Mollah wako na hiyo ndio maana ya, nasi tukaribu naye zaidi kuliko huo mshipa wake wa shingo
وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنۡ حَبۡلِ ٱلۡوَرِيدِ.
Kuna kitu ambacho ni muhimu sana kukijua ndio maana unahimizwa kukumbuka mauti, kwanini ikawa Mauti kwa sababu Mauti yanachukua kila kitu isipokua kitu hicho ambayo ndio hiyo Roho,ndio hiyo wewe ambaye sasa hivi unaisoma habari hii, Na siri ya kukumbuka Mauti nikuwa kila ukikumbuka Mauti unapunguza dhanmbi, na dhanmbi zikipungua inakua rahisi kuijua Roho yako(قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّٮٰهَا)"Bila shaka Amefuzu aliyeitakasa(Roho yake) .
"Wanakuuliza habari ya Roho Sema"
Tutizame sasa hili neno Amri linatokea wapi, Neno Amri ni tafsiri ile ile ya Majaala, na tutizame hili neno la kujaaliwa ni Amri hii inayopitishwa na Mwenyewe Mwenye enzi Mungu kama alivyosema kwenye aya nyingi mimi nitazitumia mbili ili zipate kutufungua macho tuweze kuona Muangaza wa Roho.
وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَىۡءٍ حَىٍّۖ
"Na tukajaalia(Kufanya)kwa maji kila kitu kilicho Hai"
Kitu chochote kilicho hai kimefanywa kwa Maji, hapo itakuonesha vipi vyengine ambavyo vikiwa havipo hai vinavyokua, mtizame Maiti wa Binaadamu au Mnyama akisha kufa anakuaje dalili ya mwanzo anaanza kuoza na (source)ya maji inakatika katika mwili huo ndio maana tunamwita Maiti na ukimfufua utaona keshakauka,maji yamemalizika, kwa hiyo katika Ulimwengu huu tumeoneshwa vilivyo hai na vilivyokufa, kimoja kinategemea maji na chengine maji yashatoweka, chochote kile kisichotegemea maji kinakua Maiti, ile amri ya maji kuwepo kwenye kitu hicho imeshakatika, kumbuka vyote vinaishi ila kimoja katika uhai na chengine katika umauti, Na hiyo Roho yako inaishi katika sehemu hizo zote mbili,kwa hiyo kama huamini kufufuliwa zingatia sana habari hii nilokupa halafu uifanyie kazi. Katika daraja hilo la maisha ndipo ilipo Roho yako kwa amri ya Mwenye enzi Mungu.
"Wanakuuliza nini habari ya Roho sema" Na waambie kwa Amri hiyo hiyo ya kujaaliwa na nyinyi mnapewa vitu muhimu sana navyo ni sura ya As-Sajda aya ya 9.
ثُمَّ سَوَّٮٰهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِۦۖ وَجَعَلَ لَكُمُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَـٰرَ وَٱلۡأَفۡـِٔدَةَۚ قَلِيلاً۬ مَّا تَشۡڪُرُونَ
Kisha akamtengeneza(Kumuumba) na Akampulizia Roho yake, na akakupeni masikio na macho na nyoyo, ni kidogo tu shukurani yenu.
Baada ya kwisha kuumbwa ukapuliziwa Roho itokayo na yeye Mwenyewe Mwenye enzi Mungu, ndio maana nikasema safari ya kutaka kuijua Roho ni kurejea kwa Mollah wako, ndio maana nikasema ni safari ya miujiza na yenye kutisha, ikapulizwa hiyo Roho katika hiyo (Body)yako, kwa hiyo Roho inaishi katika mwili wako lakini haikamatani na mwili wako, ndio maana ukaona mwili unafanya kazi zake pasi kuingiliwa na Roho,Lakini Roho ndio yenye ku (Control)huo mwili kwa kuwa wewe ni Khalifa wa huo mwili na hii Ardhi, halafu ukapewa hii amri au Jaala ya kuona na kusikia, Ifikiri sana habari hii ya kuona na kusikia, ina mazingatio makubwa katika muangaza wa Roho, huu ni uwezo wa kutoka kwa Mollah wako ndio maana utaona wakati wa usingizi wako amri hii unaondoshewa kwenye (Deep sleep)ukirejea kwa Mollah wako kikamilifu, na wakati Mwengine unakua nayo amri hii ndio unaona hizo ndoto na kusikia sauti, Ni lazima upewe viwili hivi adhimu ili upate uhai kwa ukamilifu na kama huna viwili hivi bado Roho yako iko hai lakini imenyimwa amri hii(Jaala)ya Muumba wako, ukapewa na huo Moyo ili uweze kujua, kumbuka macho ni kuona, masikio ni kusikia, halafu ukapewa na huu Moyo ili uwe na uwezo wa kujua, kupenda, kufahamu na hekima ya kuweza kuijua Roho yako. Kwa sasa hivi huwezi kujua moyo ulokusudiwa hapa mpaka ukifika mbali katika hiyo safari yako ya (Sipiritual Journey) ndio utajua alaa kumbe moyo una kazi mbili, na hii ya pili ndio ilokusudiwa katika Muangaza wa Roho.
Wanakuuliza nini habari ya Roho sema, ni jambo lilohusiana na (Amri) ya Mollah wangu, Na wala hamkupewa elimu isipokua kidogo.
Hakukataa Mwenye enzi Mungu wala hakuzuia mtu kutaka kujua nini hiyo Roho,ili kasema Elimu mliyopewa ni chache(Kidogo) basi mtu na aitafute asaa anaweza kupewa elimu ya Roho akaijua na ukiijua Roho yako, utapata ufahamu vipi ukawa wewe Khalifa katika Ardhi hii, usisubiri mpaka siku ya kufa ndio ukaijua Roho yako, anza sasa hivi kwa kujitakasa na kuusafisha moyo wako utaipata elimu hiyo, kumbukuka imetolewa kidogo lakini haikuzuiliwa kutolewa, Elimu zinazidi kutolewa, tunaendelea kuvumbua mambo,, na sote siku ya kufa tunakutana na roho zetu kwa hiyo hakuna jambo la kuogopa ima usubiri siku ya kufa au anza sasa hivi, na ukianza sasa hivi basi unakwenda (Beyond death),hiyo ndio maana "Ya Ewe Mja wangu mwema Rejea kwangu ukiwa umeridhi na kuridhiwa"(Operation ya Mauti inaendelea wewe unaangalia, unajijua sina cha kuhofia, mimi Roho narejea kwa yule alonileta, na wala sina khofu tena ya Operation hii), lakini kwanza lazima usafishe machafu yako, omba maghfira kwa wingi ili uitakase Roho yako,ikiwa safi hapo utaona Muangaza wake, utaona Muujiza wake, fanya safari hii muhimu ya Muangaza wa Roho na ukipata Muangaza huu wewe ushafanikiwa, hukai tena ukalinda mali ya Ulimwengu huu, hakuna chochote kitakacho kudhuru na utakua karibu sana na Mollah wako na hiyo ndio maana ya, nasi tukaribu naye zaidi kuliko huo mshipa wake wa shingo
وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنۡ حَبۡلِ ٱلۡوَرِيدِ.
Tuesday, October 28, 2014
KUMKUMBUKA ALLAH(DHIKR)PART 1
Asalaam Aleiykum
Wanasema Wanasayansi Mwanaadamu Bingwa wa Maarifa(Genious)hodari wa kupita mfano anaitumia Akili kwa uchache wa Asilimia 15 tu, Na hiyo katika jambo pengine hususia la uvumbuzi wa kitu fulani na huku akiacha mambo mengine chungu nzima yakimpita. Sasa ikiwa hali kama hiyo inatokezea kwa Bingwa kama huyo, nini habari yetu ya mimi na wewe tunatumia kiwango gani cha Akili zetu katika kujishughulisha na mambo yote yalotuzunguka?.
Inapaswa Mwanaadamu ajiulize asilimia ngapi anatumia, na katika kuzipata asilimia hizo ujitizame pia kiasi gani unatumia katika kumkumbuka Mollah wako, kama hutaki mahangaiko hayo basi nipe nafasi nikuonee mimi huruma ili nikupe kiwango chako unachotumia kwa ukamilifu kumkumbuka Mollah wako kwa masaa 24, Wallahi huzidi ila dakika 10 na nitakuonesha vipi kama angalau unazipata hizo dakika 10, Anzia wewe mwanzo unapomkumbuka Mollah wako labda tuseme kwenye Adhana unapoisikia au kipindi cha Sala kinapoingia basi muda wote huo mpaka kusali kwako labda ni dakika mbili tu ambazo pengine ndizo unazo bakia na Mollah wako, lakini mawazo yako safarini kuanzia kwenye Udhu mpaka Sala nzima, hukai hata sekunde saba katika kumkumbuka huko Mollah wako, kutwa unaendelea ku (Process)mawazo haya na yale, na ukiingia katika hiyo Sala basi unaweza hata kutukana au bure linakutoka (Fonyo)kwa ajili ya fulani alivyo kukera, hutulii kwenye Sala Abadan, unakaribia kukufuru mambo chungu nzima yanakuja katika hiyo Sala, na hapo ndio sehemu moja pekee ambayo labda unatakiwa umkumbuke Mollah wako kwa ukamilifu, lakini wapi viuno vinakuja hapo, michezo ya Tv unamalizia hapo, madeni unayalipa hapo, imekua Sala yote ni kitendo cha kupanga mambo yako na vipi utayatekeleza, ndio maana nikakupa angalau dakika mbili labda unamkumbuka uso umeumbwa na haya katika masaa 24 basi usipate hata hizo dakika 10, usishangae kuna wengine hawapati kabisa, hawajaanza safari hii ya kukumbuka hata hatua moja. Sasa wewe ulopata nafasi ukayajua haya nakuomba Jiulize hivo yule alokuumba akakupa Uhai anastahiki dakika 10 au zaidi ya dakika hizo, katika darsa hii nakufungua macho ili upate kujua vipi utamkumbuka Mollah wako, nini ufanye mpaka upate ladha ya kuwa karibu na Mollah wako.
Endelea part 2
Wanasema Wanasayansi Mwanaadamu Bingwa wa Maarifa(Genious)hodari wa kupita mfano anaitumia Akili kwa uchache wa Asilimia 15 tu, Na hiyo katika jambo pengine hususia la uvumbuzi wa kitu fulani na huku akiacha mambo mengine chungu nzima yakimpita. Sasa ikiwa hali kama hiyo inatokezea kwa Bingwa kama huyo, nini habari yetu ya mimi na wewe tunatumia kiwango gani cha Akili zetu katika kujishughulisha na mambo yote yalotuzunguka?.
Inapaswa Mwanaadamu ajiulize asilimia ngapi anatumia, na katika kuzipata asilimia hizo ujitizame pia kiasi gani unatumia katika kumkumbuka Mollah wako, kama hutaki mahangaiko hayo basi nipe nafasi nikuonee mimi huruma ili nikupe kiwango chako unachotumia kwa ukamilifu kumkumbuka Mollah wako kwa masaa 24, Wallahi huzidi ila dakika 10 na nitakuonesha vipi kama angalau unazipata hizo dakika 10, Anzia wewe mwanzo unapomkumbuka Mollah wako labda tuseme kwenye Adhana unapoisikia au kipindi cha Sala kinapoingia basi muda wote huo mpaka kusali kwako labda ni dakika mbili tu ambazo pengine ndizo unazo bakia na Mollah wako, lakini mawazo yako safarini kuanzia kwenye Udhu mpaka Sala nzima, hukai hata sekunde saba katika kumkumbuka huko Mollah wako, kutwa unaendelea ku (Process)mawazo haya na yale, na ukiingia katika hiyo Sala basi unaweza hata kutukana au bure linakutoka (Fonyo)kwa ajili ya fulani alivyo kukera, hutulii kwenye Sala Abadan, unakaribia kukufuru mambo chungu nzima yanakuja katika hiyo Sala, na hapo ndio sehemu moja pekee ambayo labda unatakiwa umkumbuke Mollah wako kwa ukamilifu, lakini wapi viuno vinakuja hapo, michezo ya Tv unamalizia hapo, madeni unayalipa hapo, imekua Sala yote ni kitendo cha kupanga mambo yako na vipi utayatekeleza, ndio maana nikakupa angalau dakika mbili labda unamkumbuka uso umeumbwa na haya katika masaa 24 basi usipate hata hizo dakika 10, usishangae kuna wengine hawapati kabisa, hawajaanza safari hii ya kukumbuka hata hatua moja. Sasa wewe ulopata nafasi ukayajua haya nakuomba Jiulize hivo yule alokuumba akakupa Uhai anastahiki dakika 10 au zaidi ya dakika hizo, katika darsa hii nakufungua macho ili upate kujua vipi utamkumbuka Mollah wako, nini ufanye mpaka upate ladha ya kuwa karibu na Mollah wako.
Endelea part 2
KUMKUMBUKA ALLAH(DHIKR)PART 2
Asalaam Aleiykum
Sasa kama umeamua kwa Bidii kutaka kumkumbuka Mollah wako na uzidishe hizo dakika, basi soma maudhui hii kwa kituo ili ipate kukuonesha njia za kumkurubia Mollah wako na kumsabahi na kumkumbuka wakati bado una nguvu zako, usisubiri mpaka kuumwa au umefanya dhanmbi ndio ukakurupuka kukumbuka kuomba msamaha, au huna nguvu tena una wasiwasi karibu utakufa ndio ukaanza kazi hii, unatakiwa uianze mapema ikujae Moyoni na utapata manufaa yake makubwa baadae.
Nataka kukufahamisha kuwa ukitegemea kukumbuka ina maana wewe unaitegemea Akili, sawa, nzuri lakini inatakiwa uende (Beyond)Akili, kwa sababu Akili ina tabia ya kusahau ndio maana ukaambiwa ufikiri, lakini kuna kitu ambacho hakisahau ambacho ni huo moyo, na mifano nitakutolea hiyo sura ya (Fatiha)unaona unavyoisoma hutaki hata kuikumbuka sababu iko moyoni unaitoa (Direct)lakini zengine mpaka uzifikiri na mara unakwama, sasa nini kinachokusadia kukumbuka, kile ambacho hakikumbuki ila kinataja, moyo hausahau lakini unataka mazoea, lazima ujizoeshe ndio moyo unaweza kushika jambo, Na Mollah wako katumia mifano mingi kukupa mazoea hayo kwa kukujulisha kuwepo kwake, na kila mara anakukumbusha lakini wewe umo kuyasahau, sasa mambo hayo yepi ambayo unaishi nayo lakini hukumbuki chochote, kabla ya kuyataja mambo hayo wacha nikujulishe kitu kimoja kuhusiana na kile unachoambiwa kuona kwa moyo na kutaja kwake, moyo una uwezo wa kuona mara mbili ya mwanzo ni kuhisi(Feeling) na ya pili ni kuona kwa (Pureness)kuondokewa na pazia na unakua (Knower)unajua bila ya kuona huku kwa macho wala kufundishwa, kwa hiyo ukitia sauti ndani ya kujua huko ndio inakua sasa umetaja, na ukinyamaza kimya vilevile bado unaendelea kujua katika njia za ukimya, na yote hayo yamo katika kukumbuka, na kukumbuka huku kuna kua kila wakati na sio mara moja kama ilivyo sasa.
Sasa Ujumbe gani Mollah anatuletea ili tumkumbuke, endelea part 3.
Sasa kama umeamua kwa Bidii kutaka kumkumbuka Mollah wako na uzidishe hizo dakika, basi soma maudhui hii kwa kituo ili ipate kukuonesha njia za kumkurubia Mollah wako na kumsabahi na kumkumbuka wakati bado una nguvu zako, usisubiri mpaka kuumwa au umefanya dhanmbi ndio ukakurupuka kukumbuka kuomba msamaha, au huna nguvu tena una wasiwasi karibu utakufa ndio ukaanza kazi hii, unatakiwa uianze mapema ikujae Moyoni na utapata manufaa yake makubwa baadae.
Nataka kukufahamisha kuwa ukitegemea kukumbuka ina maana wewe unaitegemea Akili, sawa, nzuri lakini inatakiwa uende (Beyond)Akili, kwa sababu Akili ina tabia ya kusahau ndio maana ukaambiwa ufikiri, lakini kuna kitu ambacho hakisahau ambacho ni huo moyo, na mifano nitakutolea hiyo sura ya (Fatiha)unaona unavyoisoma hutaki hata kuikumbuka sababu iko moyoni unaitoa (Direct)lakini zengine mpaka uzifikiri na mara unakwama, sasa nini kinachokusadia kukumbuka, kile ambacho hakikumbuki ila kinataja, moyo hausahau lakini unataka mazoea, lazima ujizoeshe ndio moyo unaweza kushika jambo, Na Mollah wako katumia mifano mingi kukupa mazoea hayo kwa kukujulisha kuwepo kwake, na kila mara anakukumbusha lakini wewe umo kuyasahau, sasa mambo hayo yepi ambayo unaishi nayo lakini hukumbuki chochote, kabla ya kuyataja mambo hayo wacha nikujulishe kitu kimoja kuhusiana na kile unachoambiwa kuona kwa moyo na kutaja kwake, moyo una uwezo wa kuona mara mbili ya mwanzo ni kuhisi(Feeling) na ya pili ni kuona kwa (Pureness)kuondokewa na pazia na unakua (Knower)unajua bila ya kuona huku kwa macho wala kufundishwa, kwa hiyo ukitia sauti ndani ya kujua huko ndio inakua sasa umetaja, na ukinyamaza kimya vilevile bado unaendelea kujua katika njia za ukimya, na yote hayo yamo katika kukumbuka, na kukumbuka huku kuna kua kila wakati na sio mara moja kama ilivyo sasa.
Sasa Ujumbe gani Mollah anatuletea ili tumkumbuke, endelea part 3.
KUMKUMBUKA ALLAH(DHIKR)PART 3
Asalaam Aleiykum
Tuanze na sura ya Mulk aya ya 19 ina siri ndani yake aya hii nataka tuingie ili tuitizame kwa uangalifu wa hali ya juu labda itatupa muamko fulani wa kutuwezesha kupata kitu cha kuweza kutukumbusha Ufalme wa Mollah wetu, aya inasemaje?
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلطَّيۡرِ فَوۡقَهُمۡ صَـٰٓفَّـٰتٍ۬ وَيَقۡبِضۡنَۚ مَا يُمۡسِكُهُنَّ إِلَّا ٱلرَّحۡمَـٰنُۚ إِنَّهُ ۥ بِكُلِّ شَىۡءِۭ بَصِيرٌ
Jee hawawaoni ndege walioko juu yao namna wanavyozinyoosha na kuzikunja(Mbawa zao kwa kuruka)hakuna anayewazuia(Wasianguke)ila (Mwenye enzi Mungu)Mwingi wa Rehma, Hakika yeye anaona kila kitu.
Maneno yalotajwa hapo ni makubwa sana ukiyazingatia, aya imeanza kwa sifa ya kuona aliyopewa Mwanaadamu na sifa hii ya kuona maana yake uzingatie, kama huzingatii kuona kwako hakuna maana yoyote, huna faida ya kuona, yamekua kama macho ya mnyama yanaona lakini hayajui chochote, ndio maana mkaambiwa nyinyi Wanaadamu kwa kuwa nyinyi ni (Special)wateule wa Mwenye enzi Mungu isipokua wewe Mwenyewe uamue kubakia katika unyama hilo shauri lako, lakini kama unataka upande darja katika maisha yako unaulizwa jee huwaoni hao ndege?.
Na huko kuona sio ubakie hapo hapo katika kutizama mbawa zinafunguka na kufungika lazima ujiulize imekuaje hali hii, lazima uyatizame maisha haya ya ndege,ishi japo kwa nusu saa uone ndege vipi anaishi, angalia anaishi kama wewe ila yeye ana njia mbili za kwenda angani na ardhini, yeye ana nyumba kama yako wewe yake inaitwa Mti, ndege huyu anatoka asubuhi kwenda kutafuta Riziki kama utokavyo wewe na kurudi nyumbani kwake kuviletea vitoto vyake chakula, ndege huyu ana mke kama ulivyo wewe na familia yako, anaimba na kuishi na kulala kila uingiapo usiku tafauti yake yeye hendi (Disco)hamuasi Mollah wake, na wakati mwengine hicho chakula unachotupa wewe kwa dharau yeye hushuka kutoka angani akaja kukila hicho hicho, basi jiulize nani mwenye kuwapa uwezo huo wote isipokua yeye Rahmani inatosha ukimuona ndege wakati wote akawa anakukumbusha Mollah wako, na ujumbe wa Mollah wako hauji kutoka kwa Ndege peke yake, ukiona mvua ni ujumbe wake, ukiona Jua ni ukumbusho wake, ukiona Miti ni ukumbusho wake, ukiona Mwezi ni yeye Mwenye kukumbusha kuwepo kwake, ukiona vinyama anakuonesha ufalme wake, ukiona Bahari anakujulisha kuwepo kwake,ukihisi upepo ujue huo ni Ufalme wake, ukiamka una siha nzuri huo ni katika uweza wake,ukikiona chakula mbele yako tambua mpaka unakitia mdomoni ni yeye alokuletea Riziki hiyo, ukiamka unaumwa elewa katika matakwa yake, ukisikia watu wanacheka na kufurahi elewa ni katika uwezo wake, ukisikia sauti za ngurumo za radi au umeme kutokea Mbinguni jua ni katika Mambo ya Uwezo wake, ukiamka na furaha jua Mollah wako kakutakia Furaha hiyo, ukipatwa na msiba jua hili limeandikwa na sasa wakati wake umefika na mimi sina jinsi ila kuridhia, ukenda kusali elewa Mollah wako kakufanyia hisani ya kukuongoza umkumbuke yeye, Ukimuona Mtu kapotea basi Muombe Mollah wako amuongoze, ukiona wagonjwa wanasikitikia maradhi yao jua wao wameshughulishwa na maradhi na kumsahau yule aliyeyaleta basi waombee kwa Mollah wako, ukenda kulala kumbuka yeye Mollah wako ndio Mwenye kukuletea huo usingizi basi Muage kwa kumwambia Mollah wangu narudi katika Ufalme wako nikirimu mapenzi yako, Ukiamka sema Nashukuru kwa kunipa siku nyengine nikukumbuke wewe na Ufalme wako, basi nakuomba Mollah wangu nikukumbuke kwa kusali kutwa nzima huku nikikutaja wewe moyoni mwangu wakati naendelea na shughuli zangu, wakati naendelea na masomo yangu, kwani kila kilichomo katika Ulimwengu huu ni chako na kinanitosha mimi kukumbuka wewe, nikiona watoto Mollah wangu nakukumbuka wewe, nikiona wazee pia nakukumbuka wewe Mwenye uwezo wa kuona kila kitu, pia nashukuru ukanijaalia kunikirimu kuona huko na mimi Mja wako, basi nakuomba kila nikionacho na kusikia kinikumbushe wewe Mollah wangu uliyeumba kila kitu, nikukumbuke saa na dakika zote katika uhai huu, najua kwa sasa nimefunikwa na mambo ya dunia lakini kwa uwezo wako taratibu naanza kuyatoa na kuujaza ukumbusho wako, basi nakuomba nipe muda wa mimi kuishi mpaka nitakapo yatoa mambo yote ya dunia na ukabaki wewe Mollah wangu moyoni mwangu.
Kwa hili najua nivigumu kulitimiza lakini kwa uwezo wako Mollah wangu hakuna kisichowezekana, Mollah wangu nakuomba nipe ukumbusho wako kwa kila ninachokiona nikukumbuke wewe na nisahau vile nivionavyo, na hiyo ndio Dhikr na ukiipata ikatulia kwenye Moyo wako basi mpaka siku ya kufa kwako wewe utakua Furahani na bila ya msukosuko wowote.Rabbi tujaalie hali hiyo Aamin.
Tuanze na sura ya Mulk aya ya 19 ina siri ndani yake aya hii nataka tuingie ili tuitizame kwa uangalifu wa hali ya juu labda itatupa muamko fulani wa kutuwezesha kupata kitu cha kuweza kutukumbusha Ufalme wa Mollah wetu, aya inasemaje?
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلطَّيۡرِ فَوۡقَهُمۡ صَـٰٓفَّـٰتٍ۬ وَيَقۡبِضۡنَۚ مَا يُمۡسِكُهُنَّ إِلَّا ٱلرَّحۡمَـٰنُۚ إِنَّهُ ۥ بِكُلِّ شَىۡءِۭ بَصِيرٌ
Jee hawawaoni ndege walioko juu yao namna wanavyozinyoosha na kuzikunja(Mbawa zao kwa kuruka)hakuna anayewazuia(Wasianguke)ila (Mwenye enzi Mungu)Mwingi wa Rehma, Hakika yeye anaona kila kitu.
Maneno yalotajwa hapo ni makubwa sana ukiyazingatia, aya imeanza kwa sifa ya kuona aliyopewa Mwanaadamu na sifa hii ya kuona maana yake uzingatie, kama huzingatii kuona kwako hakuna maana yoyote, huna faida ya kuona, yamekua kama macho ya mnyama yanaona lakini hayajui chochote, ndio maana mkaambiwa nyinyi Wanaadamu kwa kuwa nyinyi ni (Special)wateule wa Mwenye enzi Mungu isipokua wewe Mwenyewe uamue kubakia katika unyama hilo shauri lako, lakini kama unataka upande darja katika maisha yako unaulizwa jee huwaoni hao ndege?.
Na huko kuona sio ubakie hapo hapo katika kutizama mbawa zinafunguka na kufungika lazima ujiulize imekuaje hali hii, lazima uyatizame maisha haya ya ndege,ishi japo kwa nusu saa uone ndege vipi anaishi, angalia anaishi kama wewe ila yeye ana njia mbili za kwenda angani na ardhini, yeye ana nyumba kama yako wewe yake inaitwa Mti, ndege huyu anatoka asubuhi kwenda kutafuta Riziki kama utokavyo wewe na kurudi nyumbani kwake kuviletea vitoto vyake chakula, ndege huyu ana mke kama ulivyo wewe na familia yako, anaimba na kuishi na kulala kila uingiapo usiku tafauti yake yeye hendi (Disco)hamuasi Mollah wake, na wakati mwengine hicho chakula unachotupa wewe kwa dharau yeye hushuka kutoka angani akaja kukila hicho hicho, basi jiulize nani mwenye kuwapa uwezo huo wote isipokua yeye Rahmani inatosha ukimuona ndege wakati wote akawa anakukumbusha Mollah wako, na ujumbe wa Mollah wako hauji kutoka kwa Ndege peke yake, ukiona mvua ni ujumbe wake, ukiona Jua ni ukumbusho wake, ukiona Miti ni ukumbusho wake, ukiona Mwezi ni yeye Mwenye kukumbusha kuwepo kwake, ukiona vinyama anakuonesha ufalme wake, ukiona Bahari anakujulisha kuwepo kwake,ukihisi upepo ujue huo ni Ufalme wake, ukiamka una siha nzuri huo ni katika uweza wake,ukikiona chakula mbele yako tambua mpaka unakitia mdomoni ni yeye alokuletea Riziki hiyo, ukiamka unaumwa elewa katika matakwa yake, ukisikia watu wanacheka na kufurahi elewa ni katika uwezo wake, ukisikia sauti za ngurumo za radi au umeme kutokea Mbinguni jua ni katika Mambo ya Uwezo wake, ukiamka na furaha jua Mollah wako kakutakia Furaha hiyo, ukipatwa na msiba jua hili limeandikwa na sasa wakati wake umefika na mimi sina jinsi ila kuridhia, ukenda kusali elewa Mollah wako kakufanyia hisani ya kukuongoza umkumbuke yeye, Ukimuona Mtu kapotea basi Muombe Mollah wako amuongoze, ukiona wagonjwa wanasikitikia maradhi yao jua wao wameshughulishwa na maradhi na kumsahau yule aliyeyaleta basi waombee kwa Mollah wako, ukenda kulala kumbuka yeye Mollah wako ndio Mwenye kukuletea huo usingizi basi Muage kwa kumwambia Mollah wangu narudi katika Ufalme wako nikirimu mapenzi yako, Ukiamka sema Nashukuru kwa kunipa siku nyengine nikukumbuke wewe na Ufalme wako, basi nakuomba Mollah wangu nikukumbuke kwa kusali kutwa nzima huku nikikutaja wewe moyoni mwangu wakati naendelea na shughuli zangu, wakati naendelea na masomo yangu, kwani kila kilichomo katika Ulimwengu huu ni chako na kinanitosha mimi kukumbuka wewe, nikiona watoto Mollah wangu nakukumbuka wewe, nikiona wazee pia nakukumbuka wewe Mwenye uwezo wa kuona kila kitu, pia nashukuru ukanijaalia kunikirimu kuona huko na mimi Mja wako, basi nakuomba kila nikionacho na kusikia kinikumbushe wewe Mollah wangu uliyeumba kila kitu, nikukumbuke saa na dakika zote katika uhai huu, najua kwa sasa nimefunikwa na mambo ya dunia lakini kwa uwezo wako taratibu naanza kuyatoa na kuujaza ukumbusho wako, basi nakuomba nipe muda wa mimi kuishi mpaka nitakapo yatoa mambo yote ya dunia na ukabaki wewe Mollah wangu moyoni mwangu.
Kwa hili najua nivigumu kulitimiza lakini kwa uwezo wako Mollah wangu hakuna kisichowezekana, Mollah wangu nakuomba nipe ukumbusho wako kwa kila ninachokiona nikukumbuke wewe na nisahau vile nivionavyo, na hiyo ndio Dhikr na ukiipata ikatulia kwenye Moyo wako basi mpaka siku ya kufa kwako wewe utakua Furahani na bila ya msukosuko wowote.Rabbi tujaalie hali hiyo Aamin.
Sunday, October 19, 2014
UFALME WA SHETANI (IBILIS)PART 1
Asalaam Aleiykum
Nakuletea zawadi nzuri ya maneno yalojaa hekima kama utayatafakari kwa makini na kuyapa uhuru maneno hayo kushuka moyoni mwako basi yatakua ndio mwanzo wa mageuzi yako ya kukufanya kuwa mtu wa Mungu, Ufahamu wako wa mambo ya maisha haya unayoishi utageuka kuwa mwengine kabisa, utakutana na ukweli uso na macho, hiyari itakua yako kuukubali ukweli au kuukataa,hapo utajijua katika falme hizi mbili wewe unaishi wapi, ukishagundua (Kukumbuka) wapi uliko itakua rahisi kwako kupata mafanikio ambayo yatafatia yenyewe baadae.
Kumbuka huwezi kugundua siri ilofichikana mpaka hayo maneno yaende (Deep)kwenye moyo wako neno baada ya neno, kwanza napenda ufahamu nilivyotaja falme mbili nilikua naelekeza Akili yako kwenye jambo fulani, Lakini haiwezekani kabisa katika Ulimwengu huu kuwepo Falme Mbili, Ufalme ni mmoja na ni wake pekee(Subbhanna Allah)Mollah wetu mlezi, ili upate kunifahamu nimekutajia huu Ufalme mwengine ambao ni (Fake) wa Uongo na ndio wengi wetu tumechagua kuishi katika kasiri hii ya (Mwinyi Ibilis).
Sasa tuingie kwenye chanzo cha Darsa yetu hii ya Ufalme wa Shetani kwa kuichukua aya iliyomo kwenye sura ya Al-Aaraf aya ya 16 mpaka 18.
قَالَ فَبِمَآ أَغۡوَيۡتَنِى لَأَقۡعُدَنَّ لَهُمۡ صِرَٲطَكَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ
"Akasema Kwa kuwa umenihukumu upotofu(Kupotea kwa jeuri yangu)Basi nitawakalia(Waja Wako)Katika njia ilonyooka(Ili nipate kuwapoteza)"
Isije kutajwa njia ukaona labda kuna njia reefu ikisha pana ya kupita, Njia ilonyooka ni ile kanuni ya haki yenye kubainisha Uhalali wa kila jambo katika Dunia hii, Yeye kachukua Ahadi ya kukaa kwenye hiyo halali ambayo nyinyi mnaitaraji ikuvueni kwa usalama katika maisha haya yeye ndio anakwenda kukaa hapo, nini anafanya? kazi ni moja kukusahaulisha na kukufitini na Mollah wako ndani ya hiyo Halali, na rahisi sana kughilibiwa ndani ya huo Uhalali kuliko kwenye hiyo haramu kama tutavoona huko mbele.Kwa sababu ndani ya Halali ni vigumu kugundua kwamba unafanya makosa, ni vigumu kuona kwamba umetoka kwenye Uhalali na unaishi katika Haramu, unatenda yalo ya haramu, umezama kwenye haramu na ufisadi lakini kupitia ndani ya halali, Vipi Mfalme Ibilis Kakaa kwenye njia ilonyooka?
Endelea part 2
Nakuletea zawadi nzuri ya maneno yalojaa hekima kama utayatafakari kwa makini na kuyapa uhuru maneno hayo kushuka moyoni mwako basi yatakua ndio mwanzo wa mageuzi yako ya kukufanya kuwa mtu wa Mungu, Ufahamu wako wa mambo ya maisha haya unayoishi utageuka kuwa mwengine kabisa, utakutana na ukweli uso na macho, hiyari itakua yako kuukubali ukweli au kuukataa,hapo utajijua katika falme hizi mbili wewe unaishi wapi, ukishagundua (Kukumbuka) wapi uliko itakua rahisi kwako kupata mafanikio ambayo yatafatia yenyewe baadae.
Kumbuka huwezi kugundua siri ilofichikana mpaka hayo maneno yaende (Deep)kwenye moyo wako neno baada ya neno, kwanza napenda ufahamu nilivyotaja falme mbili nilikua naelekeza Akili yako kwenye jambo fulani, Lakini haiwezekani kabisa katika Ulimwengu huu kuwepo Falme Mbili, Ufalme ni mmoja na ni wake pekee(Subbhanna Allah)Mollah wetu mlezi, ili upate kunifahamu nimekutajia huu Ufalme mwengine ambao ni (Fake) wa Uongo na ndio wengi wetu tumechagua kuishi katika kasiri hii ya (Mwinyi Ibilis).
Sasa tuingie kwenye chanzo cha Darsa yetu hii ya Ufalme wa Shetani kwa kuichukua aya iliyomo kwenye sura ya Al-Aaraf aya ya 16 mpaka 18.
قَالَ فَبِمَآ أَغۡوَيۡتَنِى لَأَقۡعُدَنَّ لَهُمۡ صِرَٲطَكَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ
"Akasema Kwa kuwa umenihukumu upotofu(Kupotea kwa jeuri yangu)Basi nitawakalia(Waja Wako)Katika njia ilonyooka(Ili nipate kuwapoteza)"
Isije kutajwa njia ukaona labda kuna njia reefu ikisha pana ya kupita, Njia ilonyooka ni ile kanuni ya haki yenye kubainisha Uhalali wa kila jambo katika Dunia hii, Yeye kachukua Ahadi ya kukaa kwenye hiyo halali ambayo nyinyi mnaitaraji ikuvueni kwa usalama katika maisha haya yeye ndio anakwenda kukaa hapo, nini anafanya? kazi ni moja kukusahaulisha na kukufitini na Mollah wako ndani ya hiyo Halali, na rahisi sana kughilibiwa ndani ya huo Uhalali kuliko kwenye hiyo haramu kama tutavoona huko mbele.Kwa sababu ndani ya Halali ni vigumu kugundua kwamba unafanya makosa, ni vigumu kuona kwamba umetoka kwenye Uhalali na unaishi katika Haramu, unatenda yalo ya haramu, umezama kwenye haramu na ufisadi lakini kupitia ndani ya halali, Vipi Mfalme Ibilis Kakaa kwenye njia ilonyooka?
Endelea part 2
UFALME WA SHETANI (IBILIS)PART 2
Asalaam Aleiykum
Anakaa Ibilis kwenye maisha yetu na kutuzunguka katika kila nyanja ya maisha yetu kuanzia kuamka kwetu mpaka kulala kwetu, kama alivyosema.
ثُمَّ لَأَتِيَنَّهُم مِّنۢ بَيۡنِ أَيۡدِيہِمۡ وَمِنۡ خَلۡفِهِمۡ وَعَنۡ أَيۡمَـٰنِہِمۡ وَعَن شَمَآٮِٕلِهِمۡۖ وَلَا تَجِدُ أَكۡثَرَهُمۡ شَـٰكِرِينَ
"Kisha nitawafikia kwa mbele yao na nyuma yao na kuumeni(Kulia)kwao na kushotoni kwao, wengi katika wao hutawakuta(Hutowaona)ni wenye kukushukuru(Kukumbuka)"
Wapi ntaanzia ili nipate kuwasahulisha kama wewe umewaumba na unataka kushukuriwa kwa hilo na kukumbukwa, Nimesema anaingia Shetani katika njia za halali, wala si haramu akijua yakini atakushughulisha mpaka umsahau Mollah wako,(1) kwanza anaingia katika ugonjwa wako wa kutafuta mali, huwezi kumkumbuka tena wakati duka umefungua na wateja wanamiminika hivyo kweli unadhani utaikumbuka (Subhanna)migodi ya dhahabu inapasuka unyenyembe huko utakumbuka Mollah kasema nini, Biashara zinatoka unanunua na kuuza utakumbuka kumtaja Mollah wako,uko kwenye mkutano wa siasa unaweza wewe kumsabahi Mollah wako, ofisini unafunga mahesabu unaweza kumkumbuka Mollah wako, haya umekaa barazani hufanyi chochote unaweza kumkumbuka Mollah wako,(Ibilis kazunguka kila pahala, ukiweza kumkumbuka wakati wote ambao umenasa kwenye biashara, maongezi, mikutano ya siasa,ofisini au umekaa barazani au unatizama senema basi wewe moja kwa moja ni mtu wa peponi, ndio maana vitabu vya dini zote vikahimiza kumkumbuka Mollah, vigumu sana kuupata Ufalme wa Mwenye enzi Mungu kwa kuwa Shetani anajua japokua hili ni halali lakini nitatumia njia hii kama silaha ya kuwasahaulisha Mollah wao.
(2)Pili ntawaingia hawa kwenye kadhia ya Mwanamke, kwanza ntamshughulisha huyu Mwanamke awe hana jengine isipokua kuushughulikia mwili wake kwa ajili ya kuutengeneza kwa kujipamba kwa hichi na kile mpaka atakua hamkumbuki Mollah wake kwa lolote isipokua kutaka kuwaridhisha walimwengu wamuone mzuri hususan hawa wanaume, atakua anajipamba huyu usiku na mchana, nitamtia wazimu wa (Shopping)nifisidi kipato chake awe hatoi hata ndururu ya sadaka, na kila akiangalia (TV)yangu hichi kioo ntakua na mwambia bado hujapendeza,Nguo haijabana vizuri, watasemaje kama hutingishiki, itampata shughuli atakua hana muda hata wa sekunde wa kumkumbuka Mollah wake, ikisha nahitimisha kwa Muziki ili nipate kuingia nao kwa urahisi, ndio maana utaona mwanamke akiingia katikati ya ngoma anakatika viuno basi anapata dharau kubwa, sababu hao wenye kushuhudia wanajua huyo tayari kashafukuzwa kwenye Ufalme wa Mwenye enzi Mungu. Na hawa wanaume japokua ni nyendo za halali nitawashughulisha wawe wanamsahau Mollah wao kwa ajili ya kushughulika zaidi na urembo wa mwanamke, kuangalia vifua vyao,kuangalia viuno vyao na kushughulika kuwatafuta mpaka wakawa hawana hamu tena ya kumkumbuka Mollah wao ila wanakumbuka mwanamke(Hiyvo kweli usikie mwanamke anakwita unaweza kumkumbuka Mollah wako), wanamfanyia kazi mwanamke, wanachuma kwa ajili ya mwanamke kutokana na matamanio waliyo nayo, katika viwili hivi ndio yatakua makaazi yangu makuu, nitawasahaulisha hawa hata wakenda kusali basi watakua wanakumbuka mambo yao kuliko kumkumbuka Mwenye enzi Mungu waliyekwenda kumuabudu. halafu nikisha wasahaulisha Mollah wao nitafanya nini?.
Nguvu zikimalizika kabisa, Familia zao walizokua wanazishughulikia na kuzikumbuka wakati wana afya wakifikia uzeeni kila mmoja anamkimbia hakuna anomsikiliza, wanamuacha peke yake na hakuna hata mmoja mwenye kumthamini hiyo ndio bei tunayolipia hapa hapa Ulimwenguni kwa ajili yakumsahau Mollah wetu, Familia, ndugu, wao ndio wanakuwa wa mwanzo ukiwa unaumwa kupanga mipango yako ya mazishi, Roho hata haijatoka uzuri unaona mtu anapita na sanda, mara karafuu maiti imemdondoka, na wewe upo kitandani wamekusahau kabisa kama ndio ulochuma mali, ndio ulojenga hiyo nyumba, ndio ulokua waziri, ukawa kiongozi wajuu na mtoa hukumu wenzio wateswe,leo Shetani kakumbia kakuacha uwazi wewe na wale ulokua ukiwapa kiupa umbele na kumsahau Mollah wako, leo hawana haja na wewe, yote yale yaliyokua yanakushughulisha yametoweka umebaki wewe na Mollah wako, mpaka Shetani keshakimbia, haji tena kwani huna maana kwake, unarudi kwenye Ufalme wa kweli wa Mollah wako ukiwa Muflis, huna kitu, mali zimerithiwa, mwanamke au mwanamme kaolewa au kaoa hivi ndio sote tunavoishi katika Ufalme wa Shetani Ibilis Ufalme wa udanganyifu. Sasa ukitaka uokoke, uepuke na janga hili la kupotezwa na Ibilis ufanye nini?
Endelea Part 3
Wapi ntaanzia ili nipate kuwasahulisha kama wewe umewaumba na unataka kushukuriwa kwa hilo na kukumbukwa, Nimesema anaingia Shetani katika njia za halali, wala si haramu akijua yakini atakushughulisha mpaka umsahau Mollah wako,(1) kwanza anaingia katika ugonjwa wako wa kutafuta mali, huwezi kumkumbuka tena wakati duka umefungua na wateja wanamiminika hivyo kweli unadhani utaikumbuka (Subhanna)migodi ya dhahabu inapasuka unyenyembe huko utakumbuka Mollah kasema nini, Biashara zinatoka unanunua na kuuza utakumbuka kumtaja Mollah wako,uko kwenye mkutano wa siasa unaweza wewe kumsabahi Mollah wako, ofisini unafunga mahesabu unaweza kumkumbuka Mollah wako, haya umekaa barazani hufanyi chochote unaweza kumkumbuka Mollah wako,(Ibilis kazunguka kila pahala, ukiweza kumkumbuka wakati wote ambao umenasa kwenye biashara, maongezi, mikutano ya siasa,ofisini au umekaa barazani au unatizama senema basi wewe moja kwa moja ni mtu wa peponi, ndio maana vitabu vya dini zote vikahimiza kumkumbuka Mollah, vigumu sana kuupata Ufalme wa Mwenye enzi Mungu kwa kuwa Shetani anajua japokua hili ni halali lakini nitatumia njia hii kama silaha ya kuwasahaulisha Mollah wao.
(2)Pili ntawaingia hawa kwenye kadhia ya Mwanamke, kwanza ntamshughulisha huyu Mwanamke awe hana jengine isipokua kuushughulikia mwili wake kwa ajili ya kuutengeneza kwa kujipamba kwa hichi na kile mpaka atakua hamkumbuki Mollah wake kwa lolote isipokua kutaka kuwaridhisha walimwengu wamuone mzuri hususan hawa wanaume, atakua anajipamba huyu usiku na mchana, nitamtia wazimu wa (Shopping)nifisidi kipato chake awe hatoi hata ndururu ya sadaka, na kila akiangalia (TV)yangu hichi kioo ntakua na mwambia bado hujapendeza,Nguo haijabana vizuri, watasemaje kama hutingishiki, itampata shughuli atakua hana muda hata wa sekunde wa kumkumbuka Mollah wake, ikisha nahitimisha kwa Muziki ili nipate kuingia nao kwa urahisi, ndio maana utaona mwanamke akiingia katikati ya ngoma anakatika viuno basi anapata dharau kubwa, sababu hao wenye kushuhudia wanajua huyo tayari kashafukuzwa kwenye Ufalme wa Mwenye enzi Mungu. Na hawa wanaume japokua ni nyendo za halali nitawashughulisha wawe wanamsahau Mollah wao kwa ajili ya kushughulika zaidi na urembo wa mwanamke, kuangalia vifua vyao,kuangalia viuno vyao na kushughulika kuwatafuta mpaka wakawa hawana hamu tena ya kumkumbuka Mollah wao ila wanakumbuka mwanamke(Hiyvo kweli usikie mwanamke anakwita unaweza kumkumbuka Mollah wako), wanamfanyia kazi mwanamke, wanachuma kwa ajili ya mwanamke kutokana na matamanio waliyo nayo, katika viwili hivi ndio yatakua makaazi yangu makuu, nitawasahaulisha hawa hata wakenda kusali basi watakua wanakumbuka mambo yao kuliko kumkumbuka Mwenye enzi Mungu waliyekwenda kumuabudu. halafu nikisha wasahaulisha Mollah wao nitafanya nini?.
Nguvu zikimalizika kabisa, Familia zao walizokua wanazishughulikia na kuzikumbuka wakati wana afya wakifikia uzeeni kila mmoja anamkimbia hakuna anomsikiliza, wanamuacha peke yake na hakuna hata mmoja mwenye kumthamini hiyo ndio bei tunayolipia hapa hapa Ulimwenguni kwa ajili yakumsahau Mollah wetu, Familia, ndugu, wao ndio wanakuwa wa mwanzo ukiwa unaumwa kupanga mipango yako ya mazishi, Roho hata haijatoka uzuri unaona mtu anapita na sanda, mara karafuu maiti imemdondoka, na wewe upo kitandani wamekusahau kabisa kama ndio ulochuma mali, ndio ulojenga hiyo nyumba, ndio ulokua waziri, ukawa kiongozi wajuu na mtoa hukumu wenzio wateswe,leo Shetani kakumbia kakuacha uwazi wewe na wale ulokua ukiwapa kiupa umbele na kumsahau Mollah wako, leo hawana haja na wewe, yote yale yaliyokua yanakushughulisha yametoweka umebaki wewe na Mollah wako, mpaka Shetani keshakimbia, haji tena kwani huna maana kwake, unarudi kwenye Ufalme wa kweli wa Mollah wako ukiwa Muflis, huna kitu, mali zimerithiwa, mwanamke au mwanamme kaolewa au kaoa hivi ndio sote tunavoishi katika Ufalme wa Shetani Ibilis Ufalme wa udanganyifu. Sasa ukitaka uokoke, uepuke na janga hili la kupotezwa na Ibilis ufanye nini?
Endelea Part 3
UFALME WA SHETANI (IBILIS)PART 3
Asalaam Aleiykum
قَالَ ٱخۡرُجۡ مِنۡہَا مَذۡءُومً۬ا مَّدۡحُورً۬اۖ لَّمَن تَبِعَكَ مِنۡہُمۡ لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكُمۡ أَجۡمَعِينَ
"Akasema (Mwenye enzi Mungu)Toka humo(Peponi-Mbinguni)hali ya kuwa ni mwenye kudharauliwa na mwenye kufukuzwa, atakayekufata miongoni mwao(Nitamtia motoni) niijaze jahannamu kwa nyinyi nyote"
Limetumika Neno kuijaza Jahannam kwa sababu kama nilvyo sema vigumu kumshinda shetani Ibilis isipokua kama utaweza kuyafanya mambo haya, ili kuweza kumshinda Ibilis na mbinu zake za kukupoteza kwanza inabidi utumie busara yako ya muamko ambao kama utauzingatia utatambua tafauti yako ya siku za utotoni na ujanani, na huu wakati ulo nao pengine wa uzeeni ambao busara zake zinakuonesha mambo wazi wazi pasipo na kizuizi, mfano hakika upo ukijitizama pale ulivopita utotoni bila ya fahamu zozote, umepita ukiwa huna maarifa na Akili imelala kabisa, na sasa umeamka ukawa unaelewa mambo kwa upeo wa mazingatio yakua hili baya na hili zuri,umegundua kumbe mali na vyote nilivyochuma havina maana kwangu, ukagundua siku zangu zinakaribia na huko niendako sichukui chochote, ukagundua mbona moyo wangu una mazito,Na vipi nitaufanya mwepesi tena, mwanzoni ulikua huwezi kupambanua lakini sasa hivi unaweza kutenganisha baya na zuri, haramu na halali na ukitaka kuyafanya unayafanya kwa hiyari yako ilojaa kusudi, kwa hiyo ukiamua kumsahau na kutomuabudu Mollah wako sasa hivi ni kusudi si usingizi tena, ukiamua kushughulikia mali hilo ni tendo la kusudi, ukijifunga na kushughulika na maumbile ya wanawake hilo pia ni kusudio ambalo huambiwi pole na utayapata mateso ya Mwenye enzi Mungu kama alivyosema mwenyewe kuwa ataijaza Jahannam kwa yoyote yule atakayemfata Ibilis, pia na wewe unafukuzwa na kudharauliwa kama nilivosema wa mwanzo kabisa kufanya hivyo Familia yako.
Sasa cha kufanya nini?Al-shuaraa-89 إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٍ۬ سَلِيمٍ۬
"Isipokua mwenye kuja kwa Mwenye enzi Mungu na moyo safi"
kupata ukumbusho wa Mwenye enzi Mungu Fanya Biashara, wapende wanawake, lakini fanya bila ya matamanio ya kudumu katika nafsi yako, Fanya Biashara ukiwa huna tamaa ya kupata utajiri, mpende mwanamke lakini usianze kumuabudu ikawa huli hulali,Elewa vitu hivi ni vya muda, halafu ielekeze daima nafasi ilobakia umkumbuke Mollah wako, hapo utakua katika njia ya kati yenye furaha na jaza njema kutoka kwa Mollah wako, hapo utakua Duniani upo na Akhera pia upo, hugandi katika kitu kimoja, ushagundua hakuna kitu cha kudumu, kama Uraisi, ubunge,uwaziri,ubalozi vyote vinapita na kuna siku vyote vitakukimbia na kimoja tu ndicho kitabaki na wewe nacho ni huyo Mollah wako, siku hiyo ikifika utakua na furaha ya kusema Mollah wangu japo nilikua kwenye Biashara, japo nilikua na Mke au Mume wangu lakini wewe ulikua hunitoki moyoni mwangu nikiamini siku hii itafika ya mimi kukutana na wewe kama vile ulivyoniumba mwanzoni, kwa hilo Mollah wangu nakuomba Nisamehe unikaribishe kwenye Ufalme wako wa Kudumu. Mollah wangu leo niko katika Ufalme wako nikiwa kimya mimi na Malaika wako, wakati Mpaka walo wangu wanaogopa hata kulala na mimi chumba kimoja kwa kuwa nimeshakufa, basi mimi sina mwenginewe isipokua wewe Mfalme wa Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo, na kwa hilo Mollah wangu nipokee kwenye utukufu wako hali ya kuwa nimesamehewa na nimeridhiwa kwa kuweza kumshinda Shetani Ibilis mwenye kuwapoteza waja wako.
Mollah wetu tujaalie mazingatio haya yadumu nyoyoni mwetu na tuwe wenye kufanikiwa na kupendwa na wewe Mlezi wetu. Amin
قَالَ ٱخۡرُجۡ مِنۡہَا مَذۡءُومً۬ا مَّدۡحُورً۬اۖ لَّمَن تَبِعَكَ مِنۡہُمۡ لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكُمۡ أَجۡمَعِينَ
"Akasema (Mwenye enzi Mungu)Toka humo(Peponi-Mbinguni)hali ya kuwa ni mwenye kudharauliwa na mwenye kufukuzwa, atakayekufata miongoni mwao(Nitamtia motoni) niijaze jahannamu kwa nyinyi nyote"
Limetumika Neno kuijaza Jahannam kwa sababu kama nilvyo sema vigumu kumshinda shetani Ibilis isipokua kama utaweza kuyafanya mambo haya, ili kuweza kumshinda Ibilis na mbinu zake za kukupoteza kwanza inabidi utumie busara yako ya muamko ambao kama utauzingatia utatambua tafauti yako ya siku za utotoni na ujanani, na huu wakati ulo nao pengine wa uzeeni ambao busara zake zinakuonesha mambo wazi wazi pasipo na kizuizi, mfano hakika upo ukijitizama pale ulivopita utotoni bila ya fahamu zozote, umepita ukiwa huna maarifa na Akili imelala kabisa, na sasa umeamka ukawa unaelewa mambo kwa upeo wa mazingatio yakua hili baya na hili zuri,umegundua kumbe mali na vyote nilivyochuma havina maana kwangu, ukagundua siku zangu zinakaribia na huko niendako sichukui chochote, ukagundua mbona moyo wangu una mazito,Na vipi nitaufanya mwepesi tena, mwanzoni ulikua huwezi kupambanua lakini sasa hivi unaweza kutenganisha baya na zuri, haramu na halali na ukitaka kuyafanya unayafanya kwa hiyari yako ilojaa kusudi, kwa hiyo ukiamua kumsahau na kutomuabudu Mollah wako sasa hivi ni kusudi si usingizi tena, ukiamua kushughulikia mali hilo ni tendo la kusudi, ukijifunga na kushughulika na maumbile ya wanawake hilo pia ni kusudio ambalo huambiwi pole na utayapata mateso ya Mwenye enzi Mungu kama alivyosema mwenyewe kuwa ataijaza Jahannam kwa yoyote yule atakayemfata Ibilis, pia na wewe unafukuzwa na kudharauliwa kama nilivosema wa mwanzo kabisa kufanya hivyo Familia yako.
Sasa cha kufanya nini?Al-shuaraa-89 إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٍ۬ سَلِيمٍ۬
"Isipokua mwenye kuja kwa Mwenye enzi Mungu na moyo safi"
kupata ukumbusho wa Mwenye enzi Mungu Fanya Biashara, wapende wanawake, lakini fanya bila ya matamanio ya kudumu katika nafsi yako, Fanya Biashara ukiwa huna tamaa ya kupata utajiri, mpende mwanamke lakini usianze kumuabudu ikawa huli hulali,Elewa vitu hivi ni vya muda, halafu ielekeze daima nafasi ilobakia umkumbuke Mollah wako, hapo utakua katika njia ya kati yenye furaha na jaza njema kutoka kwa Mollah wako, hapo utakua Duniani upo na Akhera pia upo, hugandi katika kitu kimoja, ushagundua hakuna kitu cha kudumu, kama Uraisi, ubunge,uwaziri,ubalozi vyote vinapita na kuna siku vyote vitakukimbia na kimoja tu ndicho kitabaki na wewe nacho ni huyo Mollah wako, siku hiyo ikifika utakua na furaha ya kusema Mollah wangu japo nilikua kwenye Biashara, japo nilikua na Mke au Mume wangu lakini wewe ulikua hunitoki moyoni mwangu nikiamini siku hii itafika ya mimi kukutana na wewe kama vile ulivyoniumba mwanzoni, kwa hilo Mollah wangu nakuomba Nisamehe unikaribishe kwenye Ufalme wako wa Kudumu. Mollah wangu leo niko katika Ufalme wako nikiwa kimya mimi na Malaika wako, wakati Mpaka walo wangu wanaogopa hata kulala na mimi chumba kimoja kwa kuwa nimeshakufa, basi mimi sina mwenginewe isipokua wewe Mfalme wa Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo, na kwa hilo Mollah wangu nipokee kwenye utukufu wako hali ya kuwa nimesamehewa na nimeridhiwa kwa kuweza kumshinda Shetani Ibilis mwenye kuwapoteza waja wako.
Mollah wetu tujaalie mazingatio haya yadumu nyoyoni mwetu na tuwe wenye kufanikiwa na kupendwa na wewe Mlezi wetu. Amin
Sunday, October 12, 2014
NINI MAPENZI ?TAQWA PART 1
Asalaam Aleiykum
Nimetakiwa nitoe ufafanuzi kuhusu darsa zilizopita niliposema (Taqwa) ni Mapenzi nilikua nina maana gani? kuihusisha (Taqwa)na Mapenzi, Ingekua rahisi kwangu kumjibu muulizaji kwa ufupi swali lake hili, lakini kanifunga aliponambia nilete ufafanuzi, sasa pakitakiwa ufafanuzi inakua pengine muulizaji pamoja na wale wengine wasouliza labda hawajui nini Mapenzi?, ndio maana ukatakiwa ufafanuzi ili wajue yana mahusiano gani na (Taqwa).
Sasa nakuchukua katika safari hii ili upate muangaza japo kidogo ikitokea siku nyengine unamwambia mtu neno la kupenda angalau uwe karibu japokua kwa neno, sababu sasa hivi unalitamka hujui hata maana yake, hujui hata kusudio, Nini Mapenzi?.
Mapenzi hayana Tafsiri ila yana ufafanuzi, na ufafanuzi wake ni kama hivi, Mapenzi ni Muujiza unaotoka(Mbinguni)unakuja na (Quality of your Being) au niseme mwenendo wa nafsi yako, na kila kiumbe anayo haki hii ya mapenzi, anaishi katika mapenzi na kinachotizamwa hapo ni hiyo (Quality)ya Mapenzi yake kayaelekezea wapi, tukijua yalipoelemea ndipo tutapata kufahamu ni mahusiano yepi yaliyopo baina ya Mapenzi na (Taqwa).
Mapenzi yanatokana na Mwenyewe Mwenye enzi Mungu, sisi hatuna uamuzi katika jambo hilo, tunachoweza sisi kufanya ni kulikataa hilo penzi kwa njia tunazochagua sisi wenyewe, Nini Mapenzi? Mapenzi ni (Sharing of your Being)ni nafsi ilojitolea kwa njia ya (jihad)ukiniuliza mimi nitakwambia soma sura ya (Baqarah aya 2 na 3)
ذَٲلِكَ ٱلۡڪِتَـٰبُ لَا رَيۡبَۛ فِيهِۛ هُدً۬ى لِّلۡمُتَّقِينَ
"Hicho ni Kitabu kisicho na shaka na Muongozo kwa wamchao Mungu"(Wenye Mapenzi)
Kitabu hichi wameletewa wale wenye mapenzi ili uwe muongozo wao wa kuepuka maovu(Mabaya)watu hawa kwani wana mapenzi ya aina gani?
ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَـٰهُمۡ يُنفِقُونَ
"Ambao huamini yasoonekana na husimamisha Sala na kutoa katika yale tuliyowapa"
Hiyo ndio (Quality of your Being) imejaa mapenzi ya kile kisichoonekana, Nafsi yako iko kwa ukamilifu wa kile unachoamini kipo na ndicho chenye kukuongoza katika maisha haya na hayo ya baadae,ndio maana Walimwengu wakasema(Love is Blind)kisichoonekana(Usilaumu macho kwa kuwa hakioni jambo hili ulaumu Moyo kwanini mpaka leo haujapenda hichi kisichoonekana, Juta sana kukosa kitu adhimu kama hicho, Ndio maana ukiangalia kwa yule aliyekuwemo kwenye mapenzi kikweli anakua haoni kitu, mnayeona nyinyi watazamaji, mbona anafanya hivi, mbona kaacha kila kitu, hivyo hajui kama anapoteza mali yake, hizo zinakua shida zenu nyinyi lakini yeye kwa wakati ule ana(Enjoy)mapenzi yake(Love is from Beyond)linachukua Mamlaka yote ya kiumbe akawa hana uwezo wowote wa maamuzi, Na ukipata mapenzi ya kumpenda Mollah wako ukapenda dini yako wewe ndio umepata (Taqwa), baada ya kulijua hilo basi wewe huna linalo kushughulisha isipokua kusimamisha Sala, kuwasiliana na Mollah wako asiyeonekana, Na Mollah wako kama utampa mapenzi yako kwa ukamilifu basi atakuonesha Ufalme wake bado ukiwa Hai, Na watu hao kwa kuwa wamejaa Mapenzi basi wao hawana haja tena ya kuvizuia vile wanavopewa na Mollah wao, wana (Share)na yoyote yule iwe mali au nafsi zao kwa kujitolea, hilo ndio penzi (First class)Namba moja, halafu kuna penzi namba mbili(Second Class) Endelea part 2
Nimetakiwa nitoe ufafanuzi kuhusu darsa zilizopita niliposema (Taqwa) ni Mapenzi nilikua nina maana gani? kuihusisha (Taqwa)na Mapenzi, Ingekua rahisi kwangu kumjibu muulizaji kwa ufupi swali lake hili, lakini kanifunga aliponambia nilete ufafanuzi, sasa pakitakiwa ufafanuzi inakua pengine muulizaji pamoja na wale wengine wasouliza labda hawajui nini Mapenzi?, ndio maana ukatakiwa ufafanuzi ili wajue yana mahusiano gani na (Taqwa).
Sasa nakuchukua katika safari hii ili upate muangaza japo kidogo ikitokea siku nyengine unamwambia mtu neno la kupenda angalau uwe karibu japokua kwa neno, sababu sasa hivi unalitamka hujui hata maana yake, hujui hata kusudio, Nini Mapenzi?.
Mapenzi hayana Tafsiri ila yana ufafanuzi, na ufafanuzi wake ni kama hivi, Mapenzi ni Muujiza unaotoka(Mbinguni)unakuja na (Quality of your Being) au niseme mwenendo wa nafsi yako, na kila kiumbe anayo haki hii ya mapenzi, anaishi katika mapenzi na kinachotizamwa hapo ni hiyo (Quality)ya Mapenzi yake kayaelekezea wapi, tukijua yalipoelemea ndipo tutapata kufahamu ni mahusiano yepi yaliyopo baina ya Mapenzi na (Taqwa).
Mapenzi yanatokana na Mwenyewe Mwenye enzi Mungu, sisi hatuna uamuzi katika jambo hilo, tunachoweza sisi kufanya ni kulikataa hilo penzi kwa njia tunazochagua sisi wenyewe, Nini Mapenzi? Mapenzi ni (Sharing of your Being)ni nafsi ilojitolea kwa njia ya (jihad)ukiniuliza mimi nitakwambia soma sura ya (Baqarah aya 2 na 3)
ذَٲلِكَ ٱلۡڪِتَـٰبُ لَا رَيۡبَۛ فِيهِۛ هُدً۬ى لِّلۡمُتَّقِينَ
"Hicho ni Kitabu kisicho na shaka na Muongozo kwa wamchao Mungu"(Wenye Mapenzi)
Kitabu hichi wameletewa wale wenye mapenzi ili uwe muongozo wao wa kuepuka maovu(Mabaya)watu hawa kwani wana mapenzi ya aina gani?
ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَـٰهُمۡ يُنفِقُونَ
"Ambao huamini yasoonekana na husimamisha Sala na kutoa katika yale tuliyowapa"
Hiyo ndio (Quality of your Being) imejaa mapenzi ya kile kisichoonekana, Nafsi yako iko kwa ukamilifu wa kile unachoamini kipo na ndicho chenye kukuongoza katika maisha haya na hayo ya baadae,ndio maana Walimwengu wakasema(Love is Blind)kisichoonekana(Usilaumu macho kwa kuwa hakioni jambo hili ulaumu Moyo kwanini mpaka leo haujapenda hichi kisichoonekana, Juta sana kukosa kitu adhimu kama hicho, Ndio maana ukiangalia kwa yule aliyekuwemo kwenye mapenzi kikweli anakua haoni kitu, mnayeona nyinyi watazamaji, mbona anafanya hivi, mbona kaacha kila kitu, hivyo hajui kama anapoteza mali yake, hizo zinakua shida zenu nyinyi lakini yeye kwa wakati ule ana(Enjoy)mapenzi yake(Love is from Beyond)linachukua Mamlaka yote ya kiumbe akawa hana uwezo wowote wa maamuzi, Na ukipata mapenzi ya kumpenda Mollah wako ukapenda dini yako wewe ndio umepata (Taqwa), baada ya kulijua hilo basi wewe huna linalo kushughulisha isipokua kusimamisha Sala, kuwasiliana na Mollah wako asiyeonekana, Na Mollah wako kama utampa mapenzi yako kwa ukamilifu basi atakuonesha Ufalme wake bado ukiwa Hai, Na watu hao kwa kuwa wamejaa Mapenzi basi wao hawana haja tena ya kuvizuia vile wanavopewa na Mollah wao, wana (Share)na yoyote yule iwe mali au nafsi zao kwa kujitolea, hilo ndio penzi (First class)Namba moja, halafu kuna penzi namba mbili(Second Class) Endelea part 2
NINI MAPENZI ?TAQWA PART 2
Asalaam Aleiykum
Al Imran 14
زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ ٱلشَّهَوَٲتِ مِنَ ٱلنِّسَآءِ وَٱلۡبَنِينَ وَٱلۡقَنَـٰطِيرِ ٱلۡمُقَنطَرَةِ مِنَ ٱلذَّهَبِ وَٱلۡفِضَّةِ وَٱلۡخَيۡلِ ٱلۡمُسَوَّمَةِ وَٱلۡأَنۡعَـٰمِ وَٱلۡحَرۡثِۗ ذَٲلِكَ مَتَـٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَٱللَّهُ عِندَهُ ۥ حُسۡنُ ٱلۡمَـَٔابِ
"Watu wametiwa Huba(Mapenzi)ya kupenda wanawake na watoto na mirundi(wingi)wa dhahabu na Fedha, na Farasi wanaotunzwa vizuri, na wanyama na mashamba, na hayo ni matumizi ya maisha katika dunia, na kwa Mwenye enzi Mungu ndiko kwenye marejeo mazuri".
Niliposema tumezungukwa na mapenzi nilikua namaanisha zilivyofanywa Nafsi zetu ni kuishi katika hayo mapenzi, hakuna kosa kabisa, ukiwa hupendi wewe utakua na matatizo, ukiwa hutaki wenzio wapende wewe ndio kabisa unaumwa, hayo mambo yamewekwa na Mwenye enzi Mungu mwenyewe ili mpate kufurahi katika Dunia hii, na ikisha mnapewa taarifa kuwa yapo mazuri zaidi huko Akhera mnaporejea.
Sasa ukiyatizama mapenzi hayo ni (Vipande vipande)umependa hiki au kile, umpenda gari, umependa nyumba, umependa chakula, huko ni kugawika kwa mapenzi, na mapenzi ukiyagawa ndipo yanapatikana matatizo makubwa, mara unampenda huyu mara akipita yule ushampenda huyu umemsahau, kwa hiyo unakwenda na tabia hiyo mpaka mapenzi ulopewa na Mwenye enzi Mungu yanageuka kuwa (Desire) unakua mwenye kutaka kitu kufa kupona, na jambo hilo linakusahaulisha kila kitu, na hapo unakua mwenye kuharibikiwa kabisa, kwa hiyo hilo (Penzi)la (Second Class)huwezi kuliita (Taqwa) kwa sababu lishakuondoa katika kumpenda Mollah wako, unamshirikisha na vitu vyengine, unapenda kila unachokiona, na (Quality)yako inakua (Fragment).
(Taqwa) ni (Unity of Love)ukimpenda Mollah wako vyote vinafatia bila kipingamizi, unakua unapenda kila kitu kwa pamoja, lakini kwa sasa hivi wewe ulivyo unachagua, na kuchagua ndio matatizo yanokufanya usiipate (Taqwa)sasa kama huipati Taqwa, hupati kuyakamilisha mapenzi yako unaamua kufanya nini mpaka kufa kwako? Endelea part 3.
Al Imran 14
زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ ٱلشَّهَوَٲتِ مِنَ ٱلنِّسَآءِ وَٱلۡبَنِينَ وَٱلۡقَنَـٰطِيرِ ٱلۡمُقَنطَرَةِ مِنَ ٱلذَّهَبِ وَٱلۡفِضَّةِ وَٱلۡخَيۡلِ ٱلۡمُسَوَّمَةِ وَٱلۡأَنۡعَـٰمِ وَٱلۡحَرۡثِۗ ذَٲلِكَ مَتَـٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَٱللَّهُ عِندَهُ ۥ حُسۡنُ ٱلۡمَـَٔابِ
"Watu wametiwa Huba(Mapenzi)ya kupenda wanawake na watoto na mirundi(wingi)wa dhahabu na Fedha, na Farasi wanaotunzwa vizuri, na wanyama na mashamba, na hayo ni matumizi ya maisha katika dunia, na kwa Mwenye enzi Mungu ndiko kwenye marejeo mazuri".
Niliposema tumezungukwa na mapenzi nilikua namaanisha zilivyofanywa Nafsi zetu ni kuishi katika hayo mapenzi, hakuna kosa kabisa, ukiwa hupendi wewe utakua na matatizo, ukiwa hutaki wenzio wapende wewe ndio kabisa unaumwa, hayo mambo yamewekwa na Mwenye enzi Mungu mwenyewe ili mpate kufurahi katika Dunia hii, na ikisha mnapewa taarifa kuwa yapo mazuri zaidi huko Akhera mnaporejea.
Sasa ukiyatizama mapenzi hayo ni (Vipande vipande)umependa hiki au kile, umpenda gari, umependa nyumba, umependa chakula, huko ni kugawika kwa mapenzi, na mapenzi ukiyagawa ndipo yanapatikana matatizo makubwa, mara unampenda huyu mara akipita yule ushampenda huyu umemsahau, kwa hiyo unakwenda na tabia hiyo mpaka mapenzi ulopewa na Mwenye enzi Mungu yanageuka kuwa (Desire) unakua mwenye kutaka kitu kufa kupona, na jambo hilo linakusahaulisha kila kitu, na hapo unakua mwenye kuharibikiwa kabisa, kwa hiyo hilo (Penzi)la (Second Class)huwezi kuliita (Taqwa) kwa sababu lishakuondoa katika kumpenda Mollah wako, unamshirikisha na vitu vyengine, unapenda kila unachokiona, na (Quality)yako inakua (Fragment).
(Taqwa) ni (Unity of Love)ukimpenda Mollah wako vyote vinafatia bila kipingamizi, unakua unapenda kila kitu kwa pamoja, lakini kwa sasa hivi wewe ulivyo unachagua, na kuchagua ndio matatizo yanokufanya usiipate (Taqwa)sasa kama huipati Taqwa, hupati kuyakamilisha mapenzi yako unaamua kufanya nini mpaka kufa kwako? Endelea part 3.
NINI MAPENZI ? TAQWA PART 3
Asalaam Aleiykum
Al-Fajr aya ya 20
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
Na Mnapenda Mali Pendo la kupita kiasi.
Kitizame kinyanganyiro kinacho kukumba, Mollah anakwita kwenye mapenzi yake, jitizame vipi unavo mjibu, bila kutoa sauti unamuonesha kwa ishara, mimi bado niko kwenye siasa, mimi bado nashughulika kutafuta mali,mimi niko nafanya maarifa vipi nitayamaliza mambo ya watu, mimi najenga majumba, mimi natafutia wake zangu na wanangu Mali, niko mbioni kusimamia mashamba, nakwenda kazini asubuhi mpaka jioni vipi nitakukumbka Mollah wangu, Fulani anaumwa mimi namshughulikia sipati wakati wa kuabudu, nasimamia jengo sina nafasi.
Mapenzi yakuchuma Mali yamekushughulisha huwezi kuyawacha ndio maana ukaambiwa bora "Ngamia ataweza kupita kwenye tundu ya shindano"kuliko wewe afadhali ngamia atakua anafafanya jitihada za kujikunja ili apite, lakini wewe kwanza utatafuta uzi uko wapi uuze kwanza ikisha ndio upite kwenye tundu ya shindano, Mali imekushughulisha sana, hujui tena hata maana ya kupenda, hata penzi likiwa mbele yako unauliza hichi nini?. Kila mmoja wetu kashughulika na utafutitaji wa Mali ikisha ikisha nini? unaziacha Ulimwenguni huendi hata na karatasi ya kusema mimi nilikua na Mali, Mimi nilikua na Majumba na magari, mimi nilikua na viwanja na mashamba, yale yote uliyokua unayashughulikia unayawacha unakwenda mikono mitupu, huja starehe kabisa sababu siku zote ulikua unatafuta na kuilinda mali yako, huku mapenzi yapo pembezoni mwako yanakwambia geuka unipende wewe upate furaha, acha na mambo ya kidunia hayana maana, ukiandikiwa uyapate utayapata, na kama hujaandikiwa basi utahangaika bure, na hayo ndio mapenzi ya hali ya chini kabisa, mapenzi ya mateso, na mifano ipo tazameni matajiri wenu hawana furaha kabisa, sikatai wana (Security)lakini furaha haipo, hawajui kupenda wala kupendwa, na wakipendwa wanadhani huyoo anataka mali yangu, hayo ndio mateso kila mmoja wetu anashindwa kuyaepuka.
Sasa jiulize wewe Mwenyewe ukoje katika kadhia hii ya mapenzi unapenda nini? Unampenda Mollah, au Mpira, Unawapenda watu au kikundi, unapenda Nyumba zako au Mashamba yanakusumbua na faida zake, au una maradhi ya pesa uzione tu ukishajigundua wewe mapenzi yako yamehimili wapi basi anza taratibu kuya(Mix)na kumpenda Mollah wako ili upate hiyo (Unity)ya mapenzi nayo ndio hiyo (Taqwa) na ukipata hiyo ndio umefanikiwa kukubwa na Raha na Furaha zilizopo hapo unatakiwa lazima wewe Mwenyewe upate (Exeperience)hiyo, hutoelewa mtu akikuhadithia, hayo ndio mapenzi katika kipimo chake cha juu kabisa.
Al-Fajr aya ya 20
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
Na Mnapenda Mali Pendo la kupita kiasi.
Kitizame kinyanganyiro kinacho kukumba, Mollah anakwita kwenye mapenzi yake, jitizame vipi unavo mjibu, bila kutoa sauti unamuonesha kwa ishara, mimi bado niko kwenye siasa, mimi bado nashughulika kutafuta mali,mimi niko nafanya maarifa vipi nitayamaliza mambo ya watu, mimi najenga majumba, mimi natafutia wake zangu na wanangu Mali, niko mbioni kusimamia mashamba, nakwenda kazini asubuhi mpaka jioni vipi nitakukumbka Mollah wangu, Fulani anaumwa mimi namshughulikia sipati wakati wa kuabudu, nasimamia jengo sina nafasi.
Mapenzi yakuchuma Mali yamekushughulisha huwezi kuyawacha ndio maana ukaambiwa bora "Ngamia ataweza kupita kwenye tundu ya shindano"kuliko wewe afadhali ngamia atakua anafafanya jitihada za kujikunja ili apite, lakini wewe kwanza utatafuta uzi uko wapi uuze kwanza ikisha ndio upite kwenye tundu ya shindano, Mali imekushughulisha sana, hujui tena hata maana ya kupenda, hata penzi likiwa mbele yako unauliza hichi nini?. Kila mmoja wetu kashughulika na utafutitaji wa Mali ikisha ikisha nini? unaziacha Ulimwenguni huendi hata na karatasi ya kusema mimi nilikua na Mali, Mimi nilikua na Majumba na magari, mimi nilikua na viwanja na mashamba, yale yote uliyokua unayashughulikia unayawacha unakwenda mikono mitupu, huja starehe kabisa sababu siku zote ulikua unatafuta na kuilinda mali yako, huku mapenzi yapo pembezoni mwako yanakwambia geuka unipende wewe upate furaha, acha na mambo ya kidunia hayana maana, ukiandikiwa uyapate utayapata, na kama hujaandikiwa basi utahangaika bure, na hayo ndio mapenzi ya hali ya chini kabisa, mapenzi ya mateso, na mifano ipo tazameni matajiri wenu hawana furaha kabisa, sikatai wana (Security)lakini furaha haipo, hawajui kupenda wala kupendwa, na wakipendwa wanadhani huyoo anataka mali yangu, hayo ndio mateso kila mmoja wetu anashindwa kuyaepuka.
Sasa jiulize wewe Mwenyewe ukoje katika kadhia hii ya mapenzi unapenda nini? Unampenda Mollah, au Mpira, Unawapenda watu au kikundi, unapenda Nyumba zako au Mashamba yanakusumbua na faida zake, au una maradhi ya pesa uzione tu ukishajigundua wewe mapenzi yako yamehimili wapi basi anza taratibu kuya(Mix)na kumpenda Mollah wako ili upate hiyo (Unity)ya mapenzi nayo ndio hiyo (Taqwa) na ukipata hiyo ndio umefanikiwa kukubwa na Raha na Furaha zilizopo hapo unatakiwa lazima wewe Mwenyewe upate (Exeperience)hiyo, hutoelewa mtu akikuhadithia, hayo ndio mapenzi katika kipimo chake cha juu kabisa.
Sunday, September 28, 2014
SALA YA TOBA PART 1
Asalaam Aleiykum
Ushapata kujiuliza kwanini ikawa umepewa nafasi Usali Sala hii ya Toba,? Kwani si ingetosha kuomba kwa kusema ikawa mambo yamekwisha, kuna tukio gani limejificha katika Sala hii ya toba, tumo katika maudhui ya Sala hii ya Toba ili tupate faida mbili tatu zipate kutusaidia kwa kuipata Rehma ya Mollah wetu ya kusamehewa, sasa ilikuaje mpaka tukafika katika tendo hilo la Toba, wacha nikujulishe kitu kiwe msaada katika safari yako hii ya Kusali Sala ya Toba.
Woga au (Hofu) ni (Absence) ya Utiifu, najua utashangaa lakini ndio hali ilivyo kila kitu kipya kinashangaza, Unamuogopa Nyoka sababu umempitia karibu na ushasikia ana sumu kali lakini hajawahi kukutafuna, hapo woga ushakuvaa, Unamuogopa Baba kakutisha atakupiga, Unamuogopa Mama kakwambia atakutia adabu hakupi chakula,Unaogopa Utawala sababu utakuadhibu, Unaogopa kiza hujui kitatokea nini ndani ya kiza hicho, unaogopa kufa sababu hujui kama kuna uhai mwengine kaburini au Akhera, na zaidi unaogopa kama upo uhai mwengine basi vipi utazikabili adhabu za huko, huo ni upande mmoja wa woga.
Upande wa pili wa Shilingi hii ya woga kuna Ushujaa, Ushujaa ni kama vile ulivyo woga, ila tafauti yake shujaa ni (Rebel)anaupinga huo utiifu, anaamua kuukabili, anaamua kuukabili utiifu na kupambana nao japo anajua kuna madhara, yeye anapinga kila kitu kwa kuvaliwa na jambo katika mambo mawili yaloujenga huu woga na ushujaa, na hakuna jengine ila hili la (Dark)na(Light) kusahau na kukumbuka, ukitizama kwa undani utajua anayeogopa ni Mwenye kukumbuka, na Shujaa ni Mwenye kusahau, Wawili hawa hawa wote wanapita kwenye (Usiku) na (Mchana) wa (Maasi) na (Kujuta), Mwoga akikumbuka anajuta ikisha (Anatubia)halafu anasahau, Shujaa anakumbuka lakini hajuti ikisha anaendelea kusahau, na wote wanayo ile (Nature) ya kuogopa ambayo inathibitisha kuwapo kwa adhabu za aina fulani, bila ya hivyo kuogopa kusingekuwepo.
Endelea part 2
Ushapata kujiuliza kwanini ikawa umepewa nafasi Usali Sala hii ya Toba,? Kwani si ingetosha kuomba kwa kusema ikawa mambo yamekwisha, kuna tukio gani limejificha katika Sala hii ya toba, tumo katika maudhui ya Sala hii ya Toba ili tupate faida mbili tatu zipate kutusaidia kwa kuipata Rehma ya Mollah wetu ya kusamehewa, sasa ilikuaje mpaka tukafika katika tendo hilo la Toba, wacha nikujulishe kitu kiwe msaada katika safari yako hii ya Kusali Sala ya Toba.
Woga au (Hofu) ni (Absence) ya Utiifu, najua utashangaa lakini ndio hali ilivyo kila kitu kipya kinashangaza, Unamuogopa Nyoka sababu umempitia karibu na ushasikia ana sumu kali lakini hajawahi kukutafuna, hapo woga ushakuvaa, Unamuogopa Baba kakutisha atakupiga, Unamuogopa Mama kakwambia atakutia adabu hakupi chakula,Unaogopa Utawala sababu utakuadhibu, Unaogopa kiza hujui kitatokea nini ndani ya kiza hicho, unaogopa kufa sababu hujui kama kuna uhai mwengine kaburini au Akhera, na zaidi unaogopa kama upo uhai mwengine basi vipi utazikabili adhabu za huko, huo ni upande mmoja wa woga.
Upande wa pili wa Shilingi hii ya woga kuna Ushujaa, Ushujaa ni kama vile ulivyo woga, ila tafauti yake shujaa ni (Rebel)anaupinga huo utiifu, anaamua kuukabili, anaamua kuukabili utiifu na kupambana nao japo anajua kuna madhara, yeye anapinga kila kitu kwa kuvaliwa na jambo katika mambo mawili yaloujenga huu woga na ushujaa, na hakuna jengine ila hili la (Dark)na(Light) kusahau na kukumbuka, ukitizama kwa undani utajua anayeogopa ni Mwenye kukumbuka, na Shujaa ni Mwenye kusahau, Wawili hawa hawa wote wanapita kwenye (Usiku) na (Mchana) wa (Maasi) na (Kujuta), Mwoga akikumbuka anajuta ikisha (Anatubia)halafu anasahau, Shujaa anakumbuka lakini hajuti ikisha anaendelea kusahau, na wote wanayo ile (Nature) ya kuogopa ambayo inathibitisha kuwapo kwa adhabu za aina fulani, bila ya hivyo kuogopa kusingekuwepo.
Endelea part 2
SALA YA TOBA PART 2
Asalaam Aleiykum
Kutokana na hali hiyo ya usahaulivu Mwanaadamu anapita katika hali ya makosa kila wakati wa saa na dakika zake, hakuna anayevuka katika hilo isipokua yule ambaye amekwenda (Beyond) ya Woga na Ushujaa, ambaye sasa kwa mara ya mwanzo anaishi katika Utiifu, na ukiishi katika Utiifu Woga na Ushujaa vyote vinapotea, unakua Mja wa Mwenye enzi Mungu kama ilivyotajwa kwenye sura ya (Yunus aya ya 62-64)
أَلَآ إِنَّ أَوۡلِيَآءَ ٱللَّهِ لَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
"Wale vipenzi(Waja)wa Mwenye enzi Mungu hawatakua na Khofu wala hawatahuzunika"
Kwa sababu hawana woga wala ushujaa wao wanaishi kwenye Utiifu, na woga na ushujaa ni kwa wale ambao hawajafikia daraja ya kuwa vipenzi vya Mollah wao ili wapate kuondoshewa viwili hivi, sasa hawa ni watu gani?
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَڪَانُواْ يَتَّقُونَ
"Nao ni wale Waloamini na wakawa wanamtii(Kumcha)Mwenye enzi Mungu(Wakawa wanajiepusha na maovu)"
Ukiwa unatii huna wasiwasi maisha yako yanakua (Simple)huna haja ya kutetemeka, unaridhika na kila kitu.
لَهُمُ ٱلۡبُشۡرَىٰ فِى ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَفِى ٱلۡأَخِرَةِۚ لَا تَبۡدِيلَ لِڪَلِمَـٰتِ ٱللَّهِۚ ذَٲلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
"Wao wana mema katika maisha ya dunia na katika maisha ya Akhera, hakuna mabadiliko katika maneno ya Mwenye enzi Mungu, huku ndiko kufuzu kukubwa"
Na ukisharidhika unakua ushafanikiwa kupata Mema kutoka kwa Mollah wako, maisha yako yanakua ya aina nyengine kabisa hata kuyaeleza hakuna mfano wake mpaka uishi ndio utajua yakoje maisha haya ya (Bliss)unayapata hapa Ulimwenguni na huko Akhera, Na Mwenye enzi Mungu anasema huko ni kufuzu kukubwa, lakini kufuzu huku kunatakiwa ujitolee huo (Muhanga) wa Utiifu, sasa kama huko tayari ndio unapewa nafasi ufanye japo kidogo kidogo kwa njia ya Toba.
Endelea part 3
Kutokana na hali hiyo ya usahaulivu Mwanaadamu anapita katika hali ya makosa kila wakati wa saa na dakika zake, hakuna anayevuka katika hilo isipokua yule ambaye amekwenda (Beyond) ya Woga na Ushujaa, ambaye sasa kwa mara ya mwanzo anaishi katika Utiifu, na ukiishi katika Utiifu Woga na Ushujaa vyote vinapotea, unakua Mja wa Mwenye enzi Mungu kama ilivyotajwa kwenye sura ya (Yunus aya ya 62-64)
أَلَآ إِنَّ أَوۡلِيَآءَ ٱللَّهِ لَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
"Wale vipenzi(Waja)wa Mwenye enzi Mungu hawatakua na Khofu wala hawatahuzunika"
Kwa sababu hawana woga wala ushujaa wao wanaishi kwenye Utiifu, na woga na ushujaa ni kwa wale ambao hawajafikia daraja ya kuwa vipenzi vya Mollah wao ili wapate kuondoshewa viwili hivi, sasa hawa ni watu gani?
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَڪَانُواْ يَتَّقُونَ
"Nao ni wale Waloamini na wakawa wanamtii(Kumcha)Mwenye enzi Mungu(Wakawa wanajiepusha na maovu)"
Ukiwa unatii huna wasiwasi maisha yako yanakua (Simple)huna haja ya kutetemeka, unaridhika na kila kitu.
لَهُمُ ٱلۡبُشۡرَىٰ فِى ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَفِى ٱلۡأَخِرَةِۚ لَا تَبۡدِيلَ لِڪَلِمَـٰتِ ٱللَّهِۚ ذَٲلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
"Wao wana mema katika maisha ya dunia na katika maisha ya Akhera, hakuna mabadiliko katika maneno ya Mwenye enzi Mungu, huku ndiko kufuzu kukubwa"
Na ukisharidhika unakua ushafanikiwa kupata Mema kutoka kwa Mollah wako, maisha yako yanakua ya aina nyengine kabisa hata kuyaeleza hakuna mfano wake mpaka uishi ndio utajua yakoje maisha haya ya (Bliss)unayapata hapa Ulimwenguni na huko Akhera, Na Mwenye enzi Mungu anasema huko ni kufuzu kukubwa, lakini kufuzu huku kunatakiwa ujitolee huo (Muhanga) wa Utiifu, sasa kama huko tayari ndio unapewa nafasi ufanye japo kidogo kidogo kwa njia ya Toba.
Endelea part 3
Subscribe to:
Posts (Atom)