Sunday, December 29, 2013

DAWA YA DHIKI PART 1

Asalaam Aleiykum,

Binaadamu yanatupata matatizo makubwa pale tunaposhindwa kutafautisha Baina ya Matatizo na Dhiki, Matatizo ni kitu cha nje, Matatizo ni majambo katika mambo ya Maisha, Lakini Dhiki ni yenye kuishi kwenye hiyo (Roho) yako, Na kaa ukijua mwenye Dhiki hana Raha ya Maisha, Ujaji wa Dhiki unakuja mfano uleule wa Matatizo, kama, yaweza kuwa Una Dhiki ya Mapenzi, au Dhiki ya utafutaji wako wa Riziki, mbona mambo hayendi, unaweza kuwa na Dhiki ya Moyo mambo yamekujaa na hujui utayatoa vipi, unaogopa kumhadithia mtu, kumbuka hayo yote yamo ndani ya (Nafsi) yako.
Sasa itabidi ujiulize ilikuaje hata ukafikia hali kama hiyo, huna haja ya Hadith wala kisa cha zamani eti ndio yakujulishe vipi umefika hapo, huna haja ya kwenda kwa Mmasai au kwa (Babu) ili upatiwe Dawa, kumbuka Dawa unayo mwenyewe, na kazi yangu mimi ni kukumbusha umeiweka wapi hiyo Dawa, ufanye nini utoke kwenye Dhiki, lakini utatokaje kabla ya kujua njia?
Ipi njia yenyewe, ni hiyo ya kuijua Dhiki ukaweza kuitafautisha na matatizo. Nini matatizo? Matatizo yanakuja kwa Kutamani, ikawa hichi unataka na kile unakitaka, unakua na (Ambitions) za kila aina, hivyo ndio kujitia kwenye matatizo. Nini Dhiki? Dhiki ni kuhitaji(Mahitaji)Unahitaji Raha, Unahitaji (Blissful life) Unahitaji Ku(Surrender)unahitaji utulivu, unahitaji (Normality)au tuite (Balance). kwanini sasa mambo yako yameharibika mpaka umefikia unaishi ndani ya Dhiki? sababu ziko na wewe mwenyewe ndiye muanzilishi, wewe ndie mtengenezaji wa hiyo Dhiki, na kabla hatujenda mbali wacha nikukumbushe kitu labda huwenda ukajua ama kweli Dhiki nimejitakia mwenyewe. Wacha nikujulishe Sheria ilopangwa na Mwenyewe aliyeumba Ulimwengu, Anasemaje kupitia Kwa Mja wake alompa Hekima Luqman a.s (Sura ya Luqman aya ya 16.
 يَـٰبُنَىَّ إِنَّہَآ إِن تَكُ مِثۡقَالَ حَبَّةٍ۬ مِّنۡ خَرۡدَلٍ۬ فَتَكُن فِى صَخۡرَةٍ أَوۡ فِى ٱلسَّمَـٰوَٲتِ أَوۡ فِى ٱلۡأَرۡضِ يَأۡتِ بِہَا ٱللَّهُ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَطِيفٌ خَبِيرٌ۬
"Ewe Mwanangu Kwa hakika jambo lolote (Japo)liwe na uzito wa(Atom)chembe ya Hardali, likawa(Limetendeka au kufichwa)ndani ya Jabali au Mbinguni au Katika Ardhi, Mwenye Enzi Mungu atalileta (Na Kumlipa aliyelitenda),Hakika Mwenye Enzi Mungu ni Mwenye kujua (mambo) yalofichikana na (Mambo)yalodhahiri".
Kaanza kupewa Onyo mtoto sababu bado hajaingia kwenye Dhiki, Bado hajalimbikiza mali au mambo ya kidunia anaambiwa kaa ukijua chochote kile utendacho lazima ulipwe, na hiyo ndio sheria ya Mwenye Enzi Mungu lazima itekelezwe. Sasa vipi wewe umefikia katika hali hiyo ya Dhiki? Endelea part 2

DAWA YA DHIKI PART 2

Asalaam Aleiykum,

Kwenye hiyo aya imetajwa chochote ili usije kudhani labda vyengine havimo. Sasa Dhiki ina Pande mbili kama ilivo Shilingi, Upande wa kwanza una maandishi ya (kuhitaji)kuna kitu (Missing)lakini hukijui nini?, Na upande wa Pili kuna maandishi Dhiki ni Kapu la Dhanmbi, Dhiki haiji lazima kuna majanga unayatengeneza(Lazima unakwenda Shopping na kapu lako), na sasa matokeo yake kapu limejaa ndio maana unasikia (Dhiki).
Vipi unakua mpaka kufikia (Stage)hiyo, hapa nitaitaja mifano miwili mitatu na mengine utaongezea mwenyewe, na Mengine itakua (Surprise)lakini kwa kuwa ni sehemu ya Dhiki itabidi niitaje ili tupate faida yake. Vipi unaanza kuchuma Dhiki kwenye Nafsi yako? kumbuka huko nyuma umesoma kila kitu kinalipwa, sasa pengine unamtania mtu na yeye hapendi, hapo tayari ushachuma Dhiki, pia kumbuka Dhiki ni kitendo baina ya Nafsi kwa Nafsi, Ukiikera Nafsi na wewe malipo yake unapewa Dhiki, Unamsengenya mtu, mbali ya kuandikiwa Dhanmbi pia unapewa na Dhiki(Na mfano tizama kama ghafla atatokea huyo unomsengenya unakua vipi)hilo ndilo chumo la Dhiki, Unawatesa viumbe wenzio na wewe unapewa Dhiki, Unatamani Mke au Mume wa Mtu, huku kwa nyuma unapewa(Double dose)ya Dhiki na matatizo, Wewe Tajiri unaonea na kuwadhalilisha wafanyakazi wako, huku na wewe unapewa Dhiki huna Raha, Wewe kiongozi unaonea unaowaongoza huku unapewa Dhiki unakua huna Raha Kabisa, Hata ukimuona Nyoka maskini anakukimbia anaelekea shimoni kwake, ukaamua kumpiga akafa, basi na huku unapewa Dhiki kwani na yeye ana haki ya kuishi kama ulivo wewe.
Na Kubwa zaidi ni hili umeshakusanya Dhiki sasa zimekujaa (Tafrani)imekushika ghafla unaamua kumbe kuna kitu kinaitwa Sala, unaingia Dini kwa mikiki, sasa mahitajio yako yote ni (Pepo)ya (Express)tizama madhara ya Dhiki zako unavofanya katika Ibada zako, la kwanza inakua watu wote walosali miaka yote wanakua hawajui kusali, lazima uwafundishe tena, unakuja na hasira na jazba kubwa kabisa, unajua kwanin,i ni ile ile Dhiki inakutesa, kwanza ilikua katika Dunia sasa imehamia kwenye Akhera, ndio maana utaona matendo yako japokua mazuri lakini yamejaa chuki, mafundisho yako yanaweza kuwa yanafaa lakini kwa jinsi unavo yatoa yamejaa Dhiki, kwa hiyo inakua hasara juu ya hasara, Na unajua hayo yote ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu unataka upate(Attention)Kwanini? kwa Sababu pengine mwanzo watu walikua wanakujua kwa sifa fulani na sasa unataka ujulikane kwa sifa ya (Ucha Mungu)hiyo ndio kazi ya Dhiki kwa Jumla, na wewe fanya Uchunguzi utayajua vizuri sana, chunguza Dhiki zako zinatokana na nini, lazima kuna (Source)fulani inayokusababishia hiyo Dhiki.
Jitizame mie mbona hivi nakerwa kazini hamaki zangu namalizia Nyumbani, kwanini upo katika hali kama hiyo, Unakerwa na watu wazima unawakasirikia watoto inakuaje hali hiyo, Sasa jiulize nini kinachokufanya usiwe katika hali ya kawaida alokupangia Mwenye Enzi Mungu wako, Basi ikiwa Mja umo katika hali ya Dhiki elewa unahitaji Dawa, Na Dawa gani utatumia ili Dhiki zikutoke.Endelea Part 3

DAWA YA DHIKI PART 3

Asalaam Aleiykum,

Nini cha kufanya mpaka urejee katika hali ya kawaida, Unatakiwa uwe tayari na ujitaarishe kumeza kidonge ambacho ukikimeza tu, kinaanza kazi yake ya kukuponesha, na unakipata kidonge hicho kwenye Quraan sura ya Hashir aya ya 18 na 19.
يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلۡتَنظُرۡ نَفۡسٌ۬ مَّا قَدَّمَتۡ لِغَدٍ۬‌ۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ 
"Enyi Mloamini Mcheni Mwenye Enzi Mungu, Na kila Mtu aangalie, (Atizame)(Be Witness)anayoyatanguliza kwa ajili ya kesho, Na Mcheni Mwenye Enzi Mungu, Hakika (Yeye)anazo habari za mnayoyatenda"
Imetajwa kumcha Mungu kwenye aya hiyo mara mbili, Mara ya kwanza ni kuzinduliwa kuwa umeze kidonge cha Ucha Mungu, halafu uwe Shahidi kwa matendo yako, moja baada ya moja, kwa ajili ya kesho(Akhera)na kesho hapa hapa duniani utizame (Chain of Reaction)ukifanya sasa hivi tizama baadae itatokea nini(Be Witness)utajua kinatokea nini, Na ukianza kutizama matendo yako kidogo kidogo Dhiki inapotea kwani hiyo Dhiki imeingia moyoni kwako baada ya kugundua upo (Empty)nafasi iwazi.
Na kutajwa mara ya pili kuwa ukianza Kumcha Mollah wako ukawa shahidi wa vitendo vyako, Dhiki inapotea kwa ajili hutendi maovu, na kila wakati unakua kwenye kuelewa Mollah wako ni mwenye kukuona na hiyo ndio (Taqwa), na hicho ndio kitu kinachopungua katika maumbile yako, na kikipungua tu, unakaribisha Dhiki ikutawale ndio maana ukaambiwa kwenye aya inayofatia.

وَلَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ نَسُواْ ٱللَّهَ فَأَنسَٮٰهُمۡ أَنفُسَہُمۡ‌ۚ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ هُمُ ٱلۡفَـٰسِقُونَ
"Wala msiwe kama wale walomsahau Mwenye Enzi Mungu, Na (Mwenye Enzi Mungu)Akawasahaulisha Nafsi zao, Hao ndio waasi wakubwa"
Kumsahau Mwenye Enzi Mungu ndio huko kukaribisha matendo ya Dhiki, Na ukimsahau Mwenye Enzi Mungu na yeye anakusahaulisha kuwa yeye yupo na dawa yako ya hiyo Dhiki ni Ucha Mungu, Nafsi inasahau kabisa ndio unaendelea kuteseka na unazama katika Bonde la maasi, usijione mbona mimi nasali na Dhiki bado ninazo,(No)Mwenye Enzi Mungu kakupa (Challenge)jitizame wewe Una Sali au unafanya mazoea(Hata kasuku akizoea Ata sali)itizame Sala yako kweli unaipeleka ipasavyo.
Basi hichi kidonge cha kwanza utakunywa kutwa Mara 5 nacho hicho cha (Taqwa), ukiitia moyoni mwako ukaitenda kwa (Ikhlasi)basi utakua ushaanza kupata ponesho la Dhiki, kwa Sababu penye Taqwa Dhiki haikai. Sasa kwanini inakaa? Sababu hitajio lako kubwa ni Taqwa, na wewe hilo umelitupa hulitaki, unalichukia au kama unafanya kwa ajili umemsikia Sheikh fulani kautaja Moto, na wewe unauogopa ndio unaanza kusali, lakini hupeleki Sala yako kwa ajili ya mapenzi ya Mollah wako, nakupa mfano huo ulotajwa utazame matendo yako hapo juu, jitizame ukitoa sadaka au kumsaidia mtu wewe unafanya kwa ajili  gani, la kwanza utagundua hufanyi kwa ajili ya Mollah wako sababu kwenye moyo wako hakuna linalotokezea, la Pili utaelewa unafanya kwa ajili ya kitu fulani, na la Tatu hakuna Hisia unafanya (Empty Heart)Na ukiona hivyo elewa Dhiki imejificha kwenye moyo wako, ndio maana Bwana Mtume s.a.w akaashiria mara tatu kwenye kifua chake na kusema (Taqwa)ipo humu, Nenda Moyoni ukagundue kinatokezea nini ili upate jawabu lako.
Na ukiipata Taqwa hapo unapewa kidonge cha Pili cha siri bila mwenyewe kujua unaona Dhiki imetoweka umekua mja wa furaha, ukiona Ndege anaimba wewe unacheka na dawa yenyewe ni hii (Alam-Nashrah aya ya 5)

فَإِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرًا
"Basi Hakika baada ya Dhiki Faraji"
Faraji ndio maumbile yako, usikubali kabisa kuishi kwenye Dhiki, hama utoke kwenye Dhiki uende kwenye Taqwa, ukutane na faraj, faraji ndio afya, faraj ndio mapenzi, faraj ndio (Nature) yetu, usikubali kinyume cha hayo, Na Mollah wetu atatusaidia kuipata Faraj.


Sunday, December 22, 2013

UJUMBE WA MAREHEMU PART 1

Asalaam Aleiykum,

Nani Marehemu?
Yoyote yule alotangulia mbele ya haki ndiye Marehemu, Na yule Alobaki katika Ulimwengu huu mimi na wewe tunoishi kwa hivi sasa sisi sote ni (Rahima) wenye Rehma. Na wale walotangulia ni wenye Kurehemewa, na hilo ndio lililotufanya sisi kumwita alotangulia Akhera ni Marehemu.
Mwanaadamu yaweza kuwa una Baba au Mama katangulia kwa Mollah wake, Iwe Dada au kaka yako, awe Mwanao au ndugu yako, na iwe Rafiki ili kuipima Dini yako wakati huu ulonao, kujua kama unazo fikra za Akhera basi inapasa kujiuliza mara ngapi  kwa siku au miezi  unawakumbuka walo wako, Jiulize jee wanatakiwa kukumbukwa? Nafahamu uzuri unajitahidi kusoma magazeti hayakupiti, vitabu vya historia umevihifadhi wewe, unakumbuka mambo ya zamani, Mababa wa Taifa unawakumbuka wewe, unakumbuka waanzilishi wa chama chako, unamkumbuka mwanasayansi fulani, lakini ni mwiko kwako kuwakumbuka walio karibu na wewe kwa dua ya maombezi, jua hao kuna  mahusiano ya mazazi juu yako.
Vipi wewe huwakumbuki wale wenye ukuruba wa kidamu juu yako, kumbuka mara ya mwisho lini umempelekea Rehma za Dua, kwa sababu huko kuzungumza kwako ni Rehma, na ukipeleka maombi basi unakua umepeleka Rehma(Mfano)wa(Recycle). Usije kubisha unajua umekata mawasiliano miaka mingi ilopita, Imekusahaulisha nafsi yako na kuamini yule mtu keshaoza kaburini, Na wala hahitaji kukumbukwa, kitu kimoja nakukumbusha kilicho kufa na kuzikwa ni kiwiliwili chake tu, lakini Roho yake iko hai kwenye Ufalme wa Mwenye enzi Mungu, Na hufurahi Roho hiyo ikiwa utaikumbuka kwa kuitakia (Msamaha au kuiombea Makaazi mema). Na zile Roho ziloishi na kupita kwenye Ulimwengu huu kwa kujisalimisha kwa Mollah wao basi nazo hupewa Radhi za Mollah wao na kupata fursa ya kuwasiliana na walio karibu nao katika mahusiano ya Kiroho.
Na wale ambao wamepita katika Ulimwengu huu wakafanya Shari za kupindukia na wao pia hupewa nafasi za kuwaonesha walo wao mambo yanayo wakuta huko walipo ili wawakumbushe jamani wee huku kumoto, tutupieni Dua japo siku kati ya masiku. Sasa vipi mawasiliano haya yanafanyika, Vipi wanatuma ujumbe huo ili ikufike wewe msomaji, kwa kutaka tujue kama kweli (Communication)inafanyika wacha tumuulize Allamah Muhammad bin Sireen R.A atueleze kuhusu kadhia hii "Anasema yapo mawasiliano baina ya waliyo hai na walio kufa""Na chochote kile anacho kufahamisha maiti kwenye (Ndoto)basi ujue ni cha ukweli, sababu wao wako mbele ya haki na hawasemi uongo.
Kwa hiyo Ukimuona Maiti yako anakwambia "Ewe Mwanangu au Rafiki yangu huku mwenzio makwaju ya fimbo za moto yamenizidi au minyororo ya shaba za moto zinaniumiza, au chumba hichi cha moshi mzito sikiwezi kinaniadhibu sana basi jua maiti yako hiyo inahitaji dua zako, ndio maana ya kukuhadithia mambo hayo, sio kama anakutisha, fanya haraka umpelekee dua zako, muombee kwa Mollah wako asaa huwenda akapata shufaa, usisubiri mtu akakwambia inafaa au haifai, wewe peleka usiweke wakili baina yako na Mollah wako, alipokuumba hakuwepo yoyote kwanini sasa hivi azuke mtu kukufundisha wakati gani wa kuwasiliana na Mollah wako, Pengine huyo Maiti kaomba nipeni nafasi labda fulani, huwenda mwanangu fulani yeye kashika Ibada huwenda nikaipata shufaa, asaa Mollah wangu aweza kukubali maombi yake, nipeni nafasi, kule anapewa nafasi wewe huku unashangilia pengine mpira au harusi mambo hayo sasa. Endelea part 2

UJUMBE WA MAREHEMU PART 2

Asalaam Aleiykum,

Lazima Mtu atahadhari sana katika Ulimwengu huu, Aangalie vipi anaishi maisha yake, akumbuke kuna masiku mazito mbele yake wala si mchezo, Anaendelea Allamah wetu kutujuza yakwamba mawasiliano yapo ndio maana wakati mwengine mgonjwa akiwa taabani kazimia akija juu anasema nimewaona Bibi na Babu wamekuja nipokea, Anasema Allamah wetu"(Ukiona)au kuota Mtu alokufa anaingia kwenye nyumba basi jua ima maradhi yatakaa kwa muda mrefu au mgonjwa atakufa karibuni, Naam huo ndio Ujumbe wao kwa uchache wanaouleta ili kuwasiliana na wale walo hai.
Na yanaendelea Mawasiliano haya mpaka kwa vitendo vile vile ikiwa umewaachia watoto (Nyumba)za kuuzia ulevi wao wataendeleza, ikiwa umewaachia (Nyumba)za kuja watu (Beach)kustarehe wao wataziendeleza, ikiwa umewaachia mapesa ya Haramu na wao watayatumia kiharamu haramu kama inavotakiwa, lakini ikiwa ulikua Mja mwema utapata mfano huu katika Quraan (Kahf 82)
وَأَمَّا ٱلۡجِدَارُ فَكَانَ لِغُلَـٰمَيۡنِ يَتِيمَيۡنِ فِى ٱلۡمَدِينَةِ وَكَانَ تَحۡتَهُ ۥ كَنزٌ۬ لَّهُمَا وَكَانَ أَبُوهُمَا صَـٰلِحً۬ا فَأَرَادَ رَبُّكَ 
أَن يَبۡلُغَآ أَشُدَّهُمَا وَيَسۡتَخۡرِجَا كَنزَهُمَا رَحۡمَةً۬ مِّن رَّبِّكَ‌ۚ وَمَا فَعَلۡتُهُ ۥ عَنۡ أَمۡرِى‌ۚ
Na Ama (kuhusu)Ukuta, ulikua (kwa)ajili ya watoto wawili mayatima katika mji Ule, Na chini yake kulikuwa na Hazina yao, Na Baba yao alikuwa (Mja)Mwema, kwa hivyo, Mollah wako alitaka wafikie Baleghe yao na wajitolee hazina yao, hiyo ni Rehma inayotoka kwa Mollah wako, Na mie sikuyafanya haya kwa amri yangu.
Naam ukuta umejengwa na Mja mwema, chini ya Ukuta kawacha hazina ya Halali, Nani atakae hifadhi Mali yako ya halali hakuna ila Mollah wako Mlezi, hawezi kukutunzia Hotel zako za Maasi, hawezi kuinusuru Mali yako ya Haramu, hazipiti Rehma zake kabisa, sasa kwanini yakafanyika hayo, sababu huyo Baba(Mzee)alikua Mwema, yeye keshakufa lakini ujumbe wa Rehma ya Mollah wake unaendelea kufanya kazi yake(Shauri yenu na wale wanopita wakakwambieni haifai hata kuwataja)mnapata hasara kubwa, Na hayo hayakufanyika kwa Elimu ya yule Mja alofatana na Nabii Musa a.s bali ni kwa amri ya Mwenye Enzi Mungu, Na hapo ndio tunapoigusa Hadith ilosimuliwa Na Imam Nabhani katika kitabu chake kinachoitwa (Al-Anwar Muhammdiyah).Endelea part 3




UJUMBE WA MAREHEMU PART 3

Asalaam Aleiykum,

Hakika palikuwepo Msichana wa kiyahudi, yeye alisilimu akaukubali Uislam kwa Ukamilifu na kuukamilisha Uislam wake, Baadae akafa katika Uislam, Alipokufa alikuja Baba yake na Mama yake kwa Bwana Mtume s.a.w wakamwambia Yaa Muhammad s.a.w sisi tunataka kufahamu nini hali ya mtoto wetu Akhera, hivyo kenda Peponi kwa ajili ya Uislam au Kenda Motoni.
Bwana Mtume s.a.w Akamuomba Mwenye enzi Mungu amteremshie (Ilham ya uthibitisho)Akawachuka wazee wale mpaka makaburini, wakasimama kwenye kaburi akaita Bwana Mtume s.a.w "Ewe Fulani Binti Fulani" Ikatoka sauti Kaburini, Naam Ewe Mjumbe wa Mwenye enzi Mungu, Akamuuliza Bwana Mtume s.a.w Ewe Msichana Wajibu wazee wako(Wanataka kujua hali yako)alisema nini wakati yeye yuko kwenye makaazi ya Salama ya (Barzaq)Akajibu yule Msichana Ewe Bwana Mtume s.a.w mimi simjibu Baba yangu wakati yeye bado Yahudi, Akasema Bwana Mtume s.a.w Kwanini? akajibu yule Msichana mimi nimemkuta Mollah wangu Bora kuliko baba yangu.
(Ewe Mollah wangu nilipogundua mimi katika Moyo wangu anakaa asiyekua wewe, basi nilifanya hima kuujaza uongofu wako, hata ikawa hakai asiyekua wewe) Nimemkuta Mollah wangu ana kheri zisomfano, Palepale wale wazee wakasema "Ewe Muhammad s.a.w Tunashuhudia Mwenye enzi Mungu ni mmoja na wewe ni mjumbe wake wa haki.
Naam nini hali yetu sisi tulosahau Dini yetu na wazee wetu wema walotangulia, inapaswa tuombe Dua hii "Ewe Mwenye kugeuza nyoyo, Zigeuze nyoyo zetu zisadikishe Dini yako"
Kasema Bwana Mtume s.a.w "Enyi watu Msiwahuzunishe Maiti zenu kwa matendo Mabaya" kwani Maiti ni wenye kutambua maasi ya walio hai. Ukenda kuzini au kudhulumu yeye anatetemeka huko aliko(Barzqh) mpaka Roho wenzie wanamuuliza vipi mbona hivyo, Anajibu alo wangu anakwenda kwenye maasi na akija kunyakuliwa Roho yake pale alipo kabla ya kutubu, mnajua kitamkuta nini?
(Al-Qariah-aya ya 10-11."وَمَآ أَدۡرَٮٰكَ مَا هِيَهۡ "
Ni nini kitakujulisha hiyo Haawiya,
"نَارٌ حَامِيَةُۢ"
"Ni Moto uwakao kwa ukali(Sana)" Ndio usiku unaota unasema "jana nimemuota Mama yuko pembeni mnyonge", asiwe mnyonge na kayaona Manyago yote, na yeye hana njia ya kukukataza ila anakujia kwa ishara ewe Mwanangu acha, basi tena umezama sana, Na ikiwa yeye ndiye mwenye matatizo atakujia na ishara chungu nzima za kukuonesha nitumie dua Mwanangu, niombee japo kidogo, na kama huzifahamu anaambiwa kiwapi, kama ulivo ishi wewe na yeye anaishi hivyo hivyo, basi wafanyieni Ihsani Maiti zenu kwa kuwakumbuka kwa dua japo mwaka mara moja, msiwatupe kabisa kabisa ikawa kama hawakupita katika Ulimwengu huu. Tizama mfano Mti wa Mbuyu au Nyumba ipo mwaka wa mia unaiona, vipi Maiti yako leo imekufa mwaka wa pili tu unaisahau. Wakumbukeni walo wenu na waso wenu kwa Dua, Na Mollah wenu atakukumbukeni kwa Rehma zake.

Sunday, December 15, 2013

TAFAUTI YA RAHA NA FURAHA PART 1

Asalaam Aleiykum,

Unaijua tafauti baina ya Furaha na Raha, vishawahi kukuta viwili hivi kwa wakati mmoja? Na kama huijui basi zinduka usingizini uelewe kuwa viwili hivi umbali wake kama Shamba na mjini, upeo wake mkubwa na inatakiwa kazi (Ya Ndovu na Mwanae)kuvikutanisha viwili hivi, Ikiwa Mja mwenye kutaka kufahamu na kutaka kujua ili unufaike kwa kuvipata vitu hivi viwili kwa wakati mmoja basi tuliza fahamu yako ili unufaike na darsa hii ya kukujulisha tafauti baina ya Raha na Furaha.
Kwanza kabisa napenda kukujulisha kwa hali ulokua nayo sasa hivi  ni vigumu kabisa kutafautisha nini Raha na nini Furaha, kwa hali ulonayo, inapokaa Raha furaha haionekani, vigumu Furaha kukufikia, na Inapokuwepo Furaha unakuwa ushaisahau Raha ndio maana Furaha ikimalizika unateseka sababu ni vigumu kwako kurejea katika hali ya Raha. Ukitaka kuyaelewa kwa uzuri mambo haya kwanza wacha nikuchukue katika Mji wa Furaha nikuoneshe mambo yake halafu nikupeleke kwenye mji wa Raha pia Ukashuhudie kukoje, halafu utaamua mwenyewe unataka kuishi katika Mji gani.
Hivi karibuni katika ziara zangu za nyumbani katika mji wa Mrima vijana waliniuliza swali niwape tafauti ya Raha na Furaha, Nikaanza kuwajibu kwamba Furaha ni kitu cha (Temproray)chenye kupita au kina kuja mara moja na kutoweka, hakidumu, na wewe ukichunguza utayagundua hayo, Furaha ni yenye kukaa kwenye Akili kwa muda, kwani si ushawahi kufanya harusi na ukiamka furaha zimekwisha, ukinunua kitu ukawa nacho muda mdogo tu furaha imekwisha, ukimuona rafiki yako wa siku nyingi unafurahi baada ya muda furaha imekwisha, iko mifano mingi furaha inavopita katika akili zetu kwa muda mchache, na zikitoweka furaha hizo tunakuwa wateja wakuzitafuta tena na tena mpaka 
tunasahau kuwa sisi tuna kitu muhimu tunacho ishi nacho nayo ni hiyo Raha ambayo mtu anatakiwa kwenda (Beyond)ili kuigundua tena hiyo Raha.
Kutaka kwenda kuigundua hiyo Raha itakubidi uteremke Bondeni, utoke juu Akilini uteremke taratibu moyoni kwenye raha za kudumu.
Endelea part 2 ujue nini Raha

TAFAUTI YA RAHA NA FURAHA PART 2

Asalaam Aleiykum,

Nini Raha?
Raha ni Maumbile yako yaloambatana na Roho, Roho ni kitu kisichopenda karaha wala mateso na mfano mkubwa jitizame au mtizame yoyote yule alofikwa na maradhi hali yake inakua vipi, yatizame macho yake uyaone yalivojaa huzuni. Neno Raha limehusiana na (Roho)na Raha ni hicho ulichonacho chenye kukufanya uishi kwenye Ulimwengu huu bila ya Bughudha yoyote, bila ya mateso yoyote, Raha kwa lugha ya kigeni ni hiyo (Blissful) Raha haina kikomo, maisha yako yote ni Raha, ila bado hujayajua, unazaliwa katika Raha ikisha wewe mwenyewe unapanda ngazi huyo unatoka moyoni kuelekea kwenye Akili, unalifata tunda halafu unalitafuna kwa hiyari yako tena kwa mbwembwe, na ukisha kula tunda hapo hapo Raha inakupotea, na si kama imeondoka laa bali unasahau.Raha ni (Nature)yako, kinachotakiwa ufanye kazi ya kuikumbuka tena.
Na sababu kubwa itakayokujulisha kuwa umetoka kwenye Raha na umekwenda kwenye furaha  bila ya kujijua ni pale (Mfano) umemuacha Mke au Mume umekwenda nje kwa (Kimada), ulikua nyumbani umo kwenye Raha mstarehe, unakwenda nje kutafuta furaha, zikisha furaha hizo unakua unazitaka tena,Sababu ni za muda na zishapita,  sasa ushakua (Confused)Furaha imekwisha na Raha huipati, unaanza kutaka kuijaza(Gap)sasa unakua mteja wa kuzitafuta Furaha, labda kwa huyu au kwa yule atakupa furaha, na hiyo ndio sababu kubwa mkaambiwa msikurubie hizo Furaha za nje, unatoka katika (Qadir)ya Mollah wako alokupangia ya Raha unakwenda kwenye uchaguzi wako wewe wa kutafuta Furaha, (Mfano)mwengine upo ofisini unapata Riziki yako kwa urahisi unaacha kazi yako na kuamua kuanza Biashara, Unatoka kwenye Raha unakwenda kwenye furaha, Wewe hayo maisha yako yalivo jione uko kwenye Raha, Unaamka na Afya yako, unakwenda kazini na kucheka na wenzako huna tatizo lolote kabisa mpaka unalala kiumbe wewe hakijakukuta chochote, hakuna Raha kama jambo hilo, unaupata usingizi bila ya vidonge, unakula bila ya matatizo, unahema pasi na maradhi yoyote, umekaa salama usalimini hizo ni Raha za pekee.(Angalia Mfano wa viumbe wenzio kama)Mkulima anavoishi kwenye Raha, hana haja ya TV wala Taa ameridhika na (Nature)yake, sasa jaribu kwenda wewe Shamba, ukiona vijidudu vinameremeta(Vinawaka waka taa)utaanza kupiga kelele (Mbu)wa Shamba wamebeba(Tochi). Mtizame Mchukuzi yoyote yule anafanya kazi yake karidhia uangalie usingizi wake, Tajiri na mapesa yake yote hawezi kuununua, Kila usiku Mkulima au Mchukuzi kwa jinsi anavopendwa na Mollah wake anapewa Mapumziko ya Raha, analala kama (Sultan kwenye Ufalme wa Mwenye Enzi Mungu na akitoka Usingizini anapewa nguvu mpya za siku ya Pili. Watizame watoto bado wako Moyoni hawana habari ya Furaha, ndio maana ukimkera analia akimaliza kasahau, wacha ukerwe wewe ionekane balaa yake, sababu uko kwenye furaha na huwezi kurudi kwenye Raha tena ndio unapanda hamaki, hutaki kusamehe, kumbe sio lile kosa bali ni tafrani zako za kuwa huishi kwenye Raha, Raha kuamka Mollah kakuchangania na Furaha,kwenye Nafsi una Raha, mfukoni una furaha, Kwenye Nafsi umebarikiwa utulivu, kwenye maumbile umepewa sehemu na mahala pa kupumzikia hizo ndio Raha, ikiwa umepewa japo chembe ya mapenzi basi jijue umepewa Raha, Na raha zikizidi ndio utakuta mpenzi (Anaandika barua sasa mimi mwenzio sili wala silali)na hilo ni kweli kabisa unajua kwanini hali wala halali, kwa sababu anaona Raha, keshafika kwenye Roho yake na Roho hailali wala kula,(Kwa hiyo ni kweli halali wala hali)usidhani ni muongo, huyo yuko kwenye Raha, hajali mali wala kufilisika na wewe ukiishi kwenye Raha utakua  mtu wa aina hiyo, utakua huna (Attachment)ya kitu chochote katika Ulimwengu huu, huna habari ya kulimbikiza mali wala kuwa na (Account)ilonona, hutaki majumba wala magari ya kifahari, na unajua jambo moja muhimu kabisa nalo ni (You Belong to no one, and no one Belong to you)ukiwa katika hali kama hiyo wewe unakua uko katika ile njia ya (Balance)Ulimwenguni hupo na Akhera hujafika, hapo ndipo inapoishi Raha, na ukiwepo pahala hapo unakua simwenye kutenda dhanmbi kabisa, unakua Mja wa Huruma, mpole na kazi zako ni za kheri tupu.
Na hapo unaambiwa kwenye sura ya Rumi aya ya 15
فَأَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ فَهُمۡ فِى رَوۡضَةٍ۬ يُحۡبَرُونَ
Wale waloamini na kutenda mema watafurahishwa katika Bustani.
Endelea part 3

TAFAUTI YA RAHA NA FURAHA PART 3

Asalaam Aleiykum,

Kuamini kuko moyoni, kuamini ni Raha katika mamlaka yake, ndio maana utaona mtu atachukua kila kilicho chako lakini hawezi kuchukua Imani yako, kuamini ni Raha, ndio utakuta mtu yuko tayari kufa kwa Imani yake, Raha ilioje anauliwa kakamata kamba ya Mwenye Enzi Mungu, ndio maana unamuona mwenye Imani ya kweli anakua ni mwenye kutenda mema, anakua mwenye huruma, anakua mpole, ana mapenzi matupu, ni mwenye kusaidia wenzie na anayafanya hayo yote kwa kuona Raha kwa ajili ya Mwenye enzi Mungu wake, basi hao kabla hata ya kufunga Macho wanafunguliwa pazia na kuwaonesha furaha zinazo wasubiri huko wendako, kwa sababu wao kuishi kwao kote katika Ulimwengu huu walikua wameitambua Raha kwa njia ya siri, wakaridhi (Qadara)ya Mollah wao, wakaamua kumtii Mollah wao na kuyafata aliyoamrisha, ikawa wao wakiumwa au wakiwa wazima wanamkumbuka Mollah wao, wakilala au wakiamka wako karibu na Mollah wao, na kuwa karibu ya Mollah wako ni kuzipata Raha zisizo mfano, na kuwa karibu ya Shetani unapata furaha yake lakini ni yenye madhila makubwa, yenye shida kubwa, basi ukitaka kugundua hilo wewe endelea na (Picnic)zako, ukiamka furaha imetoweka, piga mtindi ukiamka unaumwa, nenda (Shopping)ukirudi umenuna pesa zishakwisha, cheza ngoma ukiamka magoti yanachemka, Imba usiku kucha , ukiamka sauti haipo tena, jaribu kufanya utafiti uyajue yepi ya furaha za muda mfupi, na yepi yenye Raha za kudumu ili uyakamate, ukihangaisha Akili yako utayajua hayo moja baada ya jengine, kumbuka Furaha ni ya Muda Mfupi, na Raha ni yenye kudumu.Uchaguzi unao wewe.

Sunday, December 8, 2013

HAKUNA SHEIKH-A-KAMA WEWE PART 1

Asalaam Aleiykum,

Baada ya kusoma sifa za Majina ya Mwenye Enzi Mungu nimeona kuna haja ya kurejea katika Darsa zetu za kawaida ili tuendelee kupata faida za kawaida za matunda ya dini yetu, leo hii tunaitizama Ihsan na fadhila kubwa tuloipata katika dini ya Kiislam kutoka kwa Mtume s.a.w pale alipo wacha kumchagua kiongozi wa kuindeleza Dini hii, alijua hii Dini ya Haki na italindwa na Mwenyewe alomtuma kuufikisha ujumbe huu, isionekane kwamba hakufanya uteuzi laa, alifanya uteuzi lakini ulikua wa Kisiasa kwani yeye alikua ni Mjumbe wa Mwenye Enzi Mungu na pia Mkuu wa Dola ya Kiislam, kama Mkuu wa Dola na kiongozi wa Waumini aliteua Magavana(Governor), lakini kwa upande mwengine kama Mjumbe wa Mwenye Enzi Mungu alikaa kimya na hivyo ndio walivofanya Wajumbe wote kabla yake.
Hakuchagua Khalifa au huyu awe Sheikh wenu, Hakuchagua Mchungaji wala kuwepo na Muangalizi, ila yeye alipewa na kufahamishwa maneno na Mwenye Enzi Mungu kuwajulisha Umma wake yakwamba Dini ni (Indivisual)mtu pekee, huna haja ya kushikiwa dini yako, na kama utayafahamu maneno hayo (In-deep understanding)basi kuanzia leo hutotaka mtu yoyote awe Sheikh wako au kuwa Imam wako, yatosha wewe Mwenyewe kuifanya kazi hiyo, na wala usitafute mtu wakukusomea dua na hivi na vile.
Utayafanya Maombi hayo kwa uchache au kwa wingi bila ya kutegemea yoyote, lakini cha msingi mpaka haya maneno yapasue akili yako huku ukiambiwa(Babu jinga inama ufikiri dini yako unashikiwa), kabla ya kuyagusa maneno hayo(Adhimu)Naomba nikumbushe kitu kuhusiana na Mtume s.a.w alivokua anapenda Usawa, Haki, na Uongofu, ndio  mpaka leo ukaona wale alokua nao pamoja wakati ule hawakuitwa wanafunzi wake, au wafuasi wake bali walikuwa wakiitwa (Masahaba zake)Marafiki zake.
Nani Rafiki?
Rafiki ni mtu ambaye yuko karibu na  akishirikiana na wewe katika mahusiano ya kiroho, Ikiwemo furaha na Misiba, kwenye shida na Raha zote, Rafiki ni Mwenye kukushauri katika mambo yote ya wema, na hana shaka wala wasiwasi juu yako kwenye jambo lolote la Ukweli, Kinyume na hayo anza kutilia wasiwasi Urafiki wenu.
Sasa twende tukahudhurie hayo maneno aloteremshiwa Bwana Mtume s.a.w ili tupate kujua vipi na wewe utakua Sheikh, wacha leo tuondoshe Viburi vya wale wanodhani Dini ni Mali yao, wacha tuwafichue wale wanotumia migongo ya wenzao kuwapanda na kuwadanganya na kuwadharau wenzao, kuendelea kuwabagua na kuwatenga, kuzidi kuwalaza ili wapate kuonekana wao ndio wenye kujua na wanayo mamlaka kamili ya uwezo wa kumpeleka mtu peponi, na maandalizi yote wanayo wao, napenda uelewe katika Uislam hakuna kitu kama hicho,na ukimgundua mtu ana nyendo kama hizo basi mkimbie haraka sana.
Endelea part 2 

HAKUNA SHEIKH-A-KAMA WEWE PART 2

Asalaam Aleiykum,

Al-Hujurat (13) يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّاسُ إِنَّا خَلَقۡنَـٰكُم مِّن ذَكَرٍ۬ وَأُنثَىٰ وَجَعَلۡنَـٰكُمۡ شُعُوبً۬ا وَقَبَآٮِٕلَ لِتَعَارَفُوٓاْ‌ۚ إِنَّ أَڪۡرَمَكُمۡ عِندَ ٱللَّهِ أَتۡقَٮٰكُمۡ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ۬ 
"Enyi Watu hakika tumekuumbeni Wanaume na Wanawake na tumekufanyeni Mataifa na Makabila(Mbali mbali)ili (Mpate)mjuane(Tu)Hakika ahishimiwaye sana(Mwenye cheo na daraja)miongoni mwenu mbele ya Mwenye enzi Mungu ni yule amchaye Mungu zaidi katika nyinyi,(Mwenye mapenzi na Mollah wake) Hakika Mwenye enzi Mungu ni mjuzi, na Mwenye habari."
Huna haja ya kujifanya fanya wewe una msimamo au ndio uko katika usawa, Mollah wako anajua kila kitu anazo habari zote mpaka katika kifua chako kuna kitu gani, huna haja ya kudanganya, wala usimwachie mtu akakudanganya kukwambia wewe ndio pekee unafanya sawa wengine wote sio sawa, kazi hiyo mwachie Mollah wako ndie atakae ifanyia uamuzi, unachotakiwa wewe uombe Imani ikujae kwenye nafsi yako, na Imani ikikujaa unakua huyumbi, unakua ushaupata ukweli, Na ukiujua ukweli hutaki tena kushikiwa Dini yako, unakua hutaki Sheikh yoyote, au mjanja yoyote wa maneno akusogelee, Bali wewe mwenyewe unageuka kuwa huo ukweli, na kila unapokuwepo unauwakilisha huo ukweli, na ukweli wenyewe ni huo Uislam na matendo yake.
Basi Mwenye kuujua ukweli ndio anaambiwa "Enyi Watu" tumekuumbeni Wanaume na Wanawake katika tafauti ya Maumbile tu, lakini katika jumuiko la (Roho)nyote sawa,  Tafauti yenu katika maumbile ambayo yana dhumuni maalum, ama katika mambo ya Nje Mwanamme yeye ndie Mwenye dhamana, na kuhusu mambo ya ndani Mwanamke anachukua madaraka kamili, kama Mwanamme anapigana vita ya Mpakani, Mwanamke anapigana vita ya Moyoni ambayo ndio nzito zaidi kuliko ya mpakani, Mpakani ukipigwa risasi kazi yako imekwisha, lakini ya moyoni kifo chake ni taratibu, machungu yake ni ya muda mrefu, ndio maana utakuta Mwanamke mstahamilivu anabeba mimba na huku mtoto anaumbwa ndani ya tumbo lake kwa muda wa miezi tisa, yote hayo Wanaume tunayajua na ukipata kuyajua hayo basi utafahamu kuwa sisi sote ni viumbe na inapaswa kuheshimiana.
Tukakujaalieni Mataifa na Makabila na hilo kama Muumin unalifahamu ni kwa ajili ya kujuana tu. 
 Kujuana(Knowing) Ipo kwenye Akili, na Akili ni nyenzo ya kutumika kwa mahitaji ya kuishi siku hadi siku, Lakini kipo cha zaidi ambacho kitu hicho nyote mnakutana kwenye (Level)moja, hakuna huyu Mweupe huyu Mweusi, huyu kabila fulani yule kabila hili, huyu ana cheo hichi yule ana utajiri huu, katika (Level) hiyo Muumin wa kweli ambaye kaamini kwa dhati huondosha Kiburi chake, anafahamu pahala hapa niache jeuri zangu, pahala hapa mimi si chochote,pahala hapa niwache kuwadanganya wenzangu, pahala hapa mimi sina madaraka yoyote  ya kumjua nani mwema na nani mbaya, Nani kashika dini na yupi kaichia, Na pahala hapo ndio sote tunapokutana kwenye Mamlaka ya (Kiroho)Na Mfano midogo ipo (Angalia sote tunakula uwe tajiri au maskini, sote tunavuta pumzi, sote tunalala, sote tunaongea, sote tunacheka, sote tunatembea, sote tuna ndoto zetu, sote tunaona na kusikia, sote tuna majina na mengi mengineyo)basi haikujii fikira ewe Mwanaadamu kwamba kuna pahala tunakutana, na pahala hapo ndipo pekee penye Mamlaka ya kujua kwamba kiumbe anatenda kheri au shari, nani mwenye msimamo na yupi hana, Sala yake inakubaliwa au haikubaliwi, dua yake imefika au haijafika, kwa hiyo asizuke mtu akakupeni habari yeye ni mwenye kujua dua au anajua njia za kukupeleka peponi, au yeye yupo kwenye kabila fulani au kikundi fulani ambacho ndicho kinakubalika hakuna kitu kama hicho kabisa, ndio maana aya ikasema dhumuni lake la huo Utaifa na ukabila ni kujuana tu, na wala halina kazi nyengine.
Endelea part 3



HAKUNA SHEIKH-A-KAMA WEWE PART 3

Asalaam Aleiykum

Hakika mbora wenu Mbele ya Mwenye Enzi Mungu ni yule Mwenye vitendo vya Mapenzi juu ya Mollah wake, ni yule mwenye Mapenzi na Mollah wake(Taqwa)Na Ukimpenda Mollah wako unakua si mwenye kumsahau hata dakika moja, na hiyo ndio alama kubwa ya mapenzi ya Mwenye Enzi Mungu, na ikiwa kweli umefika katika daraja ya Mcha Mungu basi kwenye masaa 24 isikupite hata dakika kumsahau Mollah wake, na ukishindwa kufanya hivyo basi wewe umo tu kwenye kundi la wale wenye kujitahidi.
Utakapofikia Daraja hiyo basi jua hakuna Sheikh kama wewe, hakuna Imam kama wewe, lakini ikiwa kinyume na hayo jijue wewe bado na wacha kuwapumbaza wenzako, wacha kuwapa (Boarding Pass)za pepo ya uongo wenzio, unafanya jambo la hatari litakuangamiza, Kwani aliye kipenzi cha Mwenye Enzi Mungu ni yule Amchaye, na Mcha Mungu wa kweli  ndio huyo mwenye kuishi na huo ukweli, ambaye keshakutana na mambo ya Mwenye enzi Mungu, kashaoneshwa Taa ya Mollah wake ambayo inamuongoza akiwa sokoni yeye yupo na Mollah wake, akiwa darasani yuo na Mollah wake, akiwa na family yupo na Mollah wake, akiwa kwenye halaiki za siasa yupo na Mollah wake, kila aendapo yeye ni mwenye Kumkumbuka Mollah wake, huku anakua kavaa taji la sifa ya upole na ukarimu, si mwenye kumbagua yoyote, unapomkuta Wallahi utaona Nuru ya Rahiim inammurika, huyo ndio anofaa kuwa Mwalimu wenu, huyo ndio anofaa kuwa Sheikh wenu, kuwa Imam wenu, kuwa kiongozi wenu, kinyume na hivyo itakua nyote mnapotea.
Hakika Mwenye enzi Mungu ni mjuzi(Wa hayo yote)na ni mwenye habari zote, anakujueni mnavopanga mipango yote ya njama za kujiona nyinyi bora, anafahamu mbinu zenu za kutaka kuwashikia wenzenu dini yao, eti dua lazima uombe wewe ndio iwe kubuli, hakuna kabisa kitu kama hicho katika Uislam.hakuna mwenye kuijua siri hiyo katika dini ndio katika aya ya (11 ya sura hiyo hiyo ya Hujurat)Inasema,
يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا يَسۡخَرۡ قَوۡمٌ۬ مِّن قَوۡمٍ عَسَىٰٓ أَن يَكُونُواْ خَيۡرً۬ا مِّنۡہُمۡ وَلَا نِسَآءٌ۬ مِّن نِّسَآءٍ عَسَىٰٓ أَن يَكُنَّ خَيۡرً۬ا مِّنۡہُنَّ‌ۖ وَلَا تَلۡمِزُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ وَلَا تَنَابَزُواْ بِٱلۡأَلۡقَـٰبِ‌ۖ بِئۡسَ ٱلِٱسۡمُ ٱلۡفُسُوقُ بَعۡدَ ٱلۡإِيمَـٰنِ‌ۚ وَمَن لَّمۡ يَتُبۡ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ 
Enyi Mloamini Wanaume wasiwadharau Wanaume wenzao,Huwenda wakawa bora kuliko wao, Wala Wanawake wasiwadharau Wanawake wenzao, Huwenda wakawa bora kuliko wao,(Na)Wala msitukanane kwa Kabila, wala msiitane kwa majina mabaya,(Na)Jina Baya kabisa kuambiwa Mtu ni asi baada ya kuwa ni Muislam,(Na kufanya hivyo ni Dhanmbi)Na wasotubu basi hao ndio Madhalim,(Wamedhulumu nafsi zao kwa kuipinga amri ya Mollah wao).
Kama mna Imani ya kweli, basi sikieni maneno ya Mollah wenu, na kama husikilizi kaa peke yako ujiulize wewe uko kundi gani?Basi ikiwa unaendelea kumsikiliza Binaadamu mwenzako hilo ni shauri lako, Na huenda hao mnaowadharau mkawaona sio Masheikh wakawa bora kuliko nyinyi, Na wala wanawake wasiwadharau wanawake wenzao huwenda wakawa bora kuliko wao, wala msitukanane kwa kabila, au kikundi fulani wakajiona sisi bora kuliko wale, yote hayo ni maneno msihadaike na maneno hakuna anojua yupi bora, hakuna anoshushiwa (Wahyi)akaambiwa nyinyi ndio mnokwenda Peponi yote hayo ni maneno, usikubali kuyumbishwa na maneno mazuri, kumbuka nyuma ya maneno mazuri kuna ubaya ulojificha, fanya uchunguzi utalijua hilo.
Na hakuna jina baya kama ukipita ukamtangazia mwenzio yule asi, yule si Sheikh, yule kafiri, yule jinsi kadhaa wa kadhaa, ikiwa unayatenda hayo basi jijue wewe mwenyewe ndio asi mkubwa na unataka dawa ili upone, na wala usifikiri huo ni Ucha Mungu, huko ni kuingia hasarani, na unatakiwa utoke kwenye kundi hilo na utubu kwa dhanmbi zako hizo, Rejea kwa Mollah wako Uwe Mcha Mungu upate daraja ya watu wema, Uwe katika watendao mazuri, upate cheo cha hakuna Sheikh kama wewe, hakuna Imam kama wewe, na hicho ndio cheo kikubwa kukipata hapa Ulimwenguni, Na hicho ndio cheo cha Ucha Mungu ambacho sote tunatakiwa tupigane kukipata, na ukisha kukipata wewe utakua umeipata Nuru ya Mwenye enzi Mungu, lakini hivi sas kwa wakati huu bado umo kwenye kuiona Taa, ondoka katika taa ukaione Nur -ala-Nur, Na hayo ndio mafanikio makubwa ambayo sote tunayataraji kuyapata.
Tunamuomba Mollah wetu atuwezeshe kuipata Nur yake.

Sunday, December 1, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(SHAKUR)PART 1

Asalaam Aleiykum,

Hakuna Jina lenye Ibada yenye kumridhisha na Mollah na kumfurahisha Kiumbe kama jina hili la (Shakur)
Mwenye Kushukuru, Ndio Maana hata kwenye ufunguzi wa Sala Unaanza kwa kushukuru(Alhamdulillah)Namshukuru Mollah wa viumbe vyote, Hapana apasae kuabudiwa na kushukuriwa isipokua Mwenye enzi Mungu wa haki. Kila kilichomo katika matendo yako kinastahiki shukran kwa ajili ya Mollah wako, Yeye ndiye aliyekupa Uhai kwa Mapenzi yake, Una nini wewe cha kumlipa isipokua hiyo shukurani ya dhati itokayo kwenye Moyo wako.
Wewe Shukuru kwa wema na Ihsani aliyokufanyia kakupa Afya na Mali, Kakupa Majumba na Magari ushakaa na kuyafikiri hayo halafu ukajaa furaha Moyoni yenye kutambua katika wengi wa viumbe vyake Mollah kanichagua mimi kunipa haya nilonayo, Usipewe hayo basi mengine ambayo unachukulia kwa mzaha kama vile umetoka usingizini mara ngapi unakumbuka umetoa Shukurani kwa kuamka kwako na ukasema(Alhamdulillah).
Jee labda umemaliza kuozesha Mwanao umekumbuka kutoa Shukurani kwa Mollah wako na kusema nakushukuru Mollah wangu kazi yangu ya ulezi ulonipa nimeimaliza salama, Jee siku ulopata hicho cheo umekimbilia Msala peke yako ukamshukuru Mollah wako, usiogope najua umemshukuru (Boss)wako mie nakukumbusha tu Jina la (Shakur).
Sasa una Afya nzuri maradhi yametoweka jee unakumbuka kila wakati kumshukuru Mollah wako, au unasubiri mpaka uanze kuumwa tena ndio uanze (Toba Yarabi), Umekaa peke yako ikakujia kushukuru kwa ajili ya kuumbwa tu kwenye Ulimwengu huu, Ishakujia fikra kuwa hata utakapo kufa basi Mollah wako atakufufua tena akupe Uhai kwa Mapenzi yake, ushawahi kushukuru kwa jambo hilo.
Ushawahi kushukuru kwa ajili ya kupewa Elimu na Akili ya kuyajua mazuri yaliyomo kwenye Ulimwengu huu ukayafurahia. Basi elewa hakuna mwenye kustahiki kushukuriwa kwa haki isipokua Mollah wako aliye Mkarim.Isiwe unasubiri mpaka upate kitu kizuri ndio Ushukuru lazima kila siku iwe siku ya Shukura kutoka kwako kwa ajili ya kupewa kwako maisha haya unayoishi. Mollah wako si mwenye kuhitaji shukurani yako, lakini kila ukishukuru moyo wako unazidi kuelekea kwake Muumba wako na hiyo ndio Ibada kama inavosema aya ya 66 sura ya Zumar,
بَلِ ٱللَّهَ فَٱعۡبُدۡ وَكُن مِّنَ ٱلشَّـٰكِرِينَ 
"Bali Muabudu Mwenye Enzi Mungu na uwe Miongoni mwa wenye kushukuru"
Na ukaendelea kukumbushwa kwenye sura ya Baqarah aya ya 152 inasema:endelea part 2

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(SHAKUR)PART 2

Asalaam Aleiykum,

فَٱذۡكُرُونِىٓ أَذۡكُرۡكُمۡ وَٱشۡڪُرُواْ لِى وَلَا تَكۡفُرُونِ 
"Basi nikumbukeni,(Namie)Nitakukumbukeni, Na Mnishukuru wala msinikufuru"
Ukianza kulitumia jina la (Shakur) au mengine yote unakua unafanya vitendo viwili kwa wakati mmoja kwanza unakumbuka halafu unatumia maana ya hilo neno, kwa hiyo nikumbukeni, nani umkumbuke Mollah wako, nini ukumbuke (Ya Shakur) uwe mwenye kutoa shukurani, Nini kitatokea na yeye atakukumbuka na hakuna fadhila ilo bora, raha isokwisha kama kukumbukwa na Mollah wako.
Yeye Mollah wetu ni mwenye kutukumbuka kwa mapenzi yake, basi anastahiki Shukurani zetu hususan tukikumbuka pale ndugu na jamaa wakishakukufikia ardhini wewe unabaki na nani? Mshukuru Mollah wako yeye ndiye (Shakur). Mshukuru Mollah wako aliyekupa uwezo wa kufikiri, kuona kusikia, na kuzungumza, yeye yuko pamoja na wewe kila wakati kwa hiyo wajibu wako kumshukuru.
Mshukuru yule ambaye bila ya kunyoosha mikono anakupa kila zawadi katika Ulimwengu huu, kuanzia chakula, afya, pumzi na kila kitu, huyo ndiye anayestahiki kushukuriwa na kila kiumbe, kaa kila wakati ukikumbuka fadhila zake kwako zisizokua na kipimo basi kila ukikaa kumbuka yuko alokuumba na anastahiki kushukuriwa.
Na ukitumia Jina hili la (Shakur) litakupeleka kumjua Mollah wako kwa undani zaidi, na furaha ilioje kumjua Mollah wako kupitia sifa hii ya Shukurani.

Sunday, November 24, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(RAZAQ)PART 1

Asalaam Aleiykum,

Mwenye Kuruzuku(Mtoa Riziki) Wanaadamu tumo katika kiza kikubwa hata akitokea Mtu akakushika mkono na kukufahamisha twende upande huu kuna muangaza utatoka kwenye giza basi hutokubali kumfata, Mwenzangu wee mimi nimeshaona alama ya taa waweza kuipata njia na ukatoka kizani basi utatia wasiwasi na hutokubali kumfata abadan. Hiyo ndio desturi ya Imani dhaifu inavokuamrisha ubakie kwenye kiza, Imani hiyo inatufahamisha kuwa kipato kinapatikana kutokana na nguvu zako mwenyewe.
Napenda uelewe hakuna nguvu zako mwenyewe ila yupo alokupangia ikisha akakuonesha na njia za kupita, halafu akakufundisha mipango ya kufanya mpaka ukaipata hiyo (Riziki).
Yeye ndiye ambaye mwenye kusababisha kila kitu katika Ardhi hii, basi kwanza "Na atizame mwanaadamu chakula chake"Abasa 24"فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَـٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِ"
Ukitizama chakula kinaweza kukupeleka safari kubwa ya kufika kwenye ukamilifu wa Imani yako katika jambo la kumjua(Razaq) Kakuwekeeni kila kitu kuanzia chakula chenu mpaka Mali ghafi zenu mnazipata kutoka katika Ardhi yake, kama Petrol,Dhahabu,Shaba,Vyuma,Almasi Maji na kila kinachohitajika katika Uchumi wenu, sasa Jiulize nani Tajiri, Nani mwenye kutoa, Nani anopanga huyu apate kile na huyu apate hiki, ukimjua Mwenye kupanga hayo basi Yeye ndiye (Razaq) Ambaye baada ya hapo akawa Mwenye kuwaonyesha waja wake njia za kuvipata vitu hivyo, Huyu akampa elimu na kumpangia wewe itakua kazi yako Ofisini, wewe utakua mfanya biashara, akawapa maguvu nyinyi mtakua mnatumika kwa njia nyengine kuipata Riziki yenu.
Ikisha baada ya yote hayo akatoa mtihani kuwaangalia waja wake alowapa kwa radhi na mapenzi yake kama jee akiwataka watoe vile alivowapa watamtii, Jee watafanya hivyo kwa ajili ya Imani ya kumpenda Mollah wao na kuvitoa kwa mapenzi? lakini wapi hapo ndipo anasahaulika kabisa Mwenye kuruzuku na mnageuka kuwa wenye"

وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
(Kuipenda)Mnapenda Mali pendo la kupita kiasi.
Unasema kabisa hapa hakitoki kitu, unapata maradhi ukimuona maskini unaanza kupanga uongo wa kujikinga kabla hata hujakutana nae,(Kumbe maskini mkipishana anakutolea salamu tu) Na akitokea Mtu kukumbusha jamani mnatakiwa mtowe mtaanza kumwita husda huyoo wa mali za watu, Na kuna wengi wanasahau kama katika maombi yao chungu nzima kabla ya kupewa hiyo Mali walikua kwenye Sijda au sehemu ya siri katikati ya usiku wanaomba na kusema," وَمِنۡہُم مَّنۡ عَـٰهَدَ ٱللَّهَ لَٮِٕنۡ ءَاتَٮٰنَا مِن فَضۡلِهِۦ لَنَصَّدَّقَنَّ وَلَنَكُونَنَّ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ"(Tawba 75)
Na miongoni mwao wako waliomuahidi Mwenye enzi Mungu kuwa,(Kama)akitupa katika fadhila zake tutatoa Sadaka na tutakuwa miongoni mwa wanaotenda mema.
Nenda ukaombe sasa hivi uone cha mtemakuni, Pengine utamkuta mtu kaweka (Bodyguard) hao kwa madhumuni ya kuwazuia maskini tu wasimkurubie, Basi kumbuka huyo ndio (Razaq)mwenye kumiliki Uchumi wote katika Ulimwengu huu.
Endelea part 2


MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(RAZAQ)PART 2

Asalaam Aleiykum,

Yeye ndiye ambaye akileta msukosuko wa Mvua au Kimbunga Biashara zote husimama, akikutieni mtihani wa vita nchi nzima inafilisika, akikuondosheeni amani kidogo tu Petrol inapanda, mara haiwezi kusafirishwa, vyakula bei juu hichi hakendi kile hakirudi sasa jiulize nani Mwenye kuruzuku.
Ukiyajua hayo basi utagundua hata huko kupewa kwako Mali ni mwenenedo wa kuruzukiwa, Hiyo njia ya kutafuta Riziki pia ni kuruzukiwa, huo Uhai pia ni kuruzukiwa, kakutia yeye fahamu na kukuonesha mipango ya kufanya mpaka ukaweza kuipata hiyo Mali ulonayo. Yeye ndiye anayempa anayemtaka na kumnyima anayemtaka, Na katika viwili hivyo kuna sababu ya undani ikiwa utakua mjuzi wa kutizama, Kwa hiyo ikiwa ushahangaika sana na unaona Utajiri haupatikani basi pumzika jua Mwenyewe mwenye Kuruzuku hataki utajirike, Na ana sababu za kufanya hivyo na hiyo pia ni baraka itokayo kwake ili utumikie mambo mengine, lakini wapi wewe umeshikilia lazima upate utajiri na hayo ndio makosa yako.
Basi litumie Jina hili la Razaq kwa ajili ya kumuomba Mollah wako, Na usije kudhani mapesa yataporomoka kutoka mbinguni ila atakufungulia njia ili uweze kupata hiyo Riziki, Na hata ukinyimwa furahi kwani kuna mengi Mollah wako anayo kuruzuku hayana hesabu, Na kama hujapewa kabisa Furahi jua Mollah wako kakusikia na anakupenda na uko karibu nae na kila ukimuomba hakupi,basi kwa kutamka jina hili litakujulisha kitu kwamba Mollah kakupa mengine yenye thamani kuliko huo utajiri, Na kwa kukunyima huo utajiri anakupenda na kukuepusha na shari yake,
Tunakuomba Mollah, Yaa Razaq, tupe ulotupangia ya kheri na utujaalie kuridhika.

Sunday, November 17, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(HAAFIZ)PART 1

Asalaam Aleiykum,

(Mwenye Kuhifadhi) Vipi utamjua anayehifadhi, Itabidi kwanza uchunguze mwenendo mzima wa kuwepo kwako kwenye Ulimwengu huu, Nani kakuumba na imekuaje akakuleta kwenye dunia hii na kukupa zawadi ya Uhai, Ukisha kulijua hilo ndipo jiulize vipi atashindwa kukuhifadhi.
Halafu fanya maulizo tena kwanini unafikia uamuzi wa kwenda kwa Mganga kutafuta hifadhi, lazima upate Hirizi au akupe kichupa ukaweke ndani ya nyumba au kazini eti iwe Hifadhi yako, ukisha elewa kama huo ni upuuzi mtupu basi achana na kuamini kuwa yupo mwengine atakae kuhifadhi zaidi ya Mollah wako, na ukikubali kuwa Mollah wako pekee ndie mwenye kukuhifadhi basi hiyo ndio Imani na wewe Muumin wa kweli.
Lakini najua tabia za Binaadamu vigumu kuacha Imani walizo zizoea, vipi leo utakubali kinga isiyokua ya Hirizi la Shaba au Pete la Fedha, au kikaratasi uweke chini ya mto, Basi kwa kukidhi haja yako hiyo Mimi leo nitakupa Hirizi langu ambalo hutakiwi kulivaa shingoni, Hirizi hii unatakiwa uivae Akilini, Na ukisha kuivaa utakua huna wasiwasi na chochote, woga wote utaondoka, Hirizi hii itakufahamisha kumbe kwenye Ulimwengu huu hakuna cha kukudhuru, na utajua kwamba mimi nimehifadhiwa kila upande na yoyote yule atotaka kunidhuru lazima apate idhini au Amri ya yule Mwenye kunihifadhi.
Sina haja mimi ya kulindwa na fulani wala fulani, Hakika hifadhi ya (Haafiz)imeenea kila sehemu na kila pahala Hifadhi hii inaendelea kuwapo, Yeye huyo ndio Mwenye kuhifadhi vidogo na hivyo vikubwa vyenye maguvu, Na hata kama haja kuhifadhi ukahisi mbona yamenikuta basi elewa kukufika huko kwa hilo jambo ni kwa sababu maalumu, Na kutokana na yeye kuruhusu hilo jambo likufike, Na kila likufikalo elewa ni kwa Amri yake yeye, Na lile lenye kukuepuka basi pia kaa ukijua yeye ni (Haafiz).
Kamata Hirizi hii ili uiweke moyoni mwako, Ikisha ingia sawasawa utajua kwa yakini liloandikwa likukute litakukuta hali ya kuwa hakuna mlinzi wa kukuhifahi.
Endelea part 2

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(HAAFIZ)PART 2

Asalaam Aleiykum,

Ipokee Hirizi yenyewe ikuvae kwenye mawazo yako uwe unaikumbuka mara kwa mara, Ishibishe ndani ya Akili itakupelekea Aya hii ya ayat (Kursiyu)kumjua nani huyo (Haafiz)kwa upeo mwengine kabisa, itakapo kuingia aya hii basi utakua hutaki tena Mlinzi yoyote isipokua Yeye Yaa (Haafiz).
Nisiseme hivi ukadhani kuwa kumbe kama ni hivyo naweza kulala na begi la Pesa mlango wazi kwenye jiji la dar es salaam yatakayo kukuta mimi simo, kuna kisa katika Injili(Biblia)kinafaa nikitaje ili upate ufahamu mzuri, Nabii Issa a.s (Jesus)"Alichukuliwa na Shetani kwa ajili ya majaribio(Mtihani)kwa muda wa siku arobaini, baada ya kupasi majaribio yote Shetani akamchukua katika jaribio la mwisho, Akampeleka kwenye Mlima mrefu, ikisha akamwambia kama uyasemayo ni kweli basi chupa nikuone, chupa nithibitishe, Nabii Issa a.s(Yesu)akamjibu (Baba Hachezewi),"Kwa hiyo na wewe ukitaka kufanya majaribio ya kulala na godoro lako la pesa kumbuka (Baba Hachezewi).
Sasa tunaingia kwenye aya yenyewe tuichungulie (Sifat ul Haafiz)Baqara 255
ٱللَّهُ لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡحَىُّ ٱلۡقَيُّومُ‌ۚ 
"Mwenye Enzi Mungu ni mmoja hakuna Mollah(Mwengine)na ndiye Mwenye Uhai wa Maisha na Mwenye kusimamia kila jambo"
Wapi unataka hifadhi kwengine hali ushajua Yeye ndie aliyekupa Uhai na Yeye ndie wa Kudumu, hata hao wakikudhur elewa yeye atakupa Uhai tena, ondoa wasiwasi".
 لَا تَأۡخُذُهُ ۥ سِنَةٌ۬ وَلَا نَوۡمٌ۬‌ۚ
"Hakumshiki kusinzia (Kusahau)wala kulala"
Vipi atashindwa kukuhifadhi hali yakua wakati wote ni mwenye kuwaangalia na kuwajua viumbe vyake.
لَّهُ ۥ مَا فِى ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَمَا فِى ٱلۡأَرۡضِ‌ۗ 
Ni vyake (Vyote) viliyomo Mbinguni na vilivyomo katika Ardhi.
Sasa itatokeaje kuwa awe Mlinzi wako asiyekua Yeye Mollah wako, ikiwa kavimiliki vyote vya mbinguni na ardhini atashindwa kukuhifadhi wewe.
مَن ذَا ٱلَّذِى يَشۡفَعُ عِندَهُ ۥۤ إِلَّا بِإِذۡنِهِۦ‌ۚ
"Nani huyo awezaye kuombea mbele yake(Mollah)Bila ya Idhini yake". Hakuna yoyote anayeweza kukudhuru wala ukidhurika hakuna awezaye kukuponya isipokua lazima ipatikane Idhini yake Yeye aliye (Hafiz)Bure kuhangaika na mizimu, Upuuzi mtupu eti mpaka utambike, mizimu imehamaki, Mganga akichukia utaangamia, yote hayo porojo, Jua wewe Umehifadhiwa Na Yeye Mollah wako alokuleta katika Ulimwengu huu, na akitaka jambo likufike litakufika hakuna wa kuzuia, Na akitaka upone utapona bila ya Mganga, hujiulizi mbona Ndege na wanyama wanapona bila ya (Doctor).
يَعۡلَمُ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡ‌ۖ 
"Anayajua yaliyo Mbele yao (Viumbe)na Yaliyo(Nyuma)yao"
Mwenye kuyajua ya mbeleni kabla ya kutokea hayo msoyajua, Na pia anayajua yale mlokwisha kuyasahau ambayo yashatokea vipi leo ashindwe kukuhifadhi."
وَلَا يُحِيطُونَ بِشَىۡءٍ۬ مِّنۡ عِلۡمِهِۦۤ إِلَّا بِمَا شَآءَ‌ۚ
"Na wala(Viumbe)hawalijui lolote katika Ilimu yake(Mwenye enzi Mungu)ila kwa alipendalo(Analolitaka)"
Hakuna kupiga Bao(Ramli)wala kujua utibabu huu na ule, au chochote katika Ulimwengu huu mpaka ujulishwe kutoka kwake Mwenyewe mwenye kuhifadhi.
وَسِعَ كُرۡسِيُّهُ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضَ‌ۖ وَلَا يَـُٔودُهُ ۥ حِفۡظُهُمَا‌ۚ وَهُوَ ٱلۡعَلِىُّ ٱلۡعَظِيمُ
"Enzi yake Imeenea Mbingu na Ardhi, wala hakumshindi kuvilinda, Na yeye Ndiye aliye juu na ndiye aliye Mkuu"
Huo ndio Ufalme wa Mwenye enzi Mungu, umekimiliki kila kitu, Na hiyo ndio hifadhi unotakiwa kuijua, Na hivi ndivo unavotakiwa fikra hii ikuingie katika mawazo yako yende (deep)kuwa kila ukiona Binaadamu, Vinyama, Miti, Mbingu,Nyota,Mwezi,Jua Uwe unakumbuka kuwa vyote hivi ni Enzi ya Mwenye enzi Mungu, Na kwamba yeye ndiye aliyeviumba na yeye ndiye Mwangalizi wake, Na pia ndiye (Hafiz)Mwenye kuvihifadhi, Aliye juu ya kila alichokiumba na ni Mkuu wa kila Jambo, basi litumie Jina hili la (Haafiz)uipate kinga itokayo kwa Mollah wako.






Sunday, November 10, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU (ALIIM) PART 1

Asalaam Aleiykum,

Hakika yeye ni Mwenye kujua kila kitu kwenye Ulimwengu huu,(Aliim) Nini Kujua? Kujua ni Elimu yenye kuhusiana na (Roho), Ndio maana utaona kujua siku zote kunatokea ndani na wala sio nje.
Na mifano ipo chungu nzima ikiwa unataka kuelewa nini kujua, basi hebu jiulize inakua vipi mtoto akizaliwa anajua kutafuta ziwa la mama na kulinyonya, nini kinachomjulisha sasa aanze kutambaa,(Lazima kuna kitu kinamjulisha), Nani anomjulisha mnyama akizaliwa tu anze kusimama na kutembea,,Nani Mwenye kukujulisha wewe sasa hivi uhai na mzima, Nani Mwenye kukujulisha wakati Umelala amka sasa ushamaliza usingizi, Yeye huyo ndie ajuae fulani siku gani ataumwa na lini atakufa, Nani atazaliwa na nchi gani atakayozaliwa, Yeye huyo Mtukufu ndie aliye kienea kila kitu kwa Ujuzi(Muhittun)Kila kitu kimo katika Ufalme wake wa Kujua.
Yeye ambaye kakipanga kila kitu kufata amri za ujuzi wake bila ya upinzani wowote, Na akaufunza ujuzi huo kwa kila kilicho Hai chenye kuishi. Kwanini nikaita ujuzi na nisiite elimu, Sababu elimu ina kikomo lakini ujuzi hauna kikomo, elimu ukijua kidogo wenzio wanajua zaidi, lakini ujuzi au kujua hakuna tafauti wewe unajua hili ua na mwenzio analijua hivyo hivyo hili ua, hakuna tafauti, kujua kama kuona au kusikia hakuna mwenye kuzidi, ukisha kujua ndio ushajua hakuna mbadala, kujua kunatokana na hiyo elimu ya (Ghayib)au siri kama alivosema Mwenye huo Ufalme wa kujua kwenye sura ya (Hashir 22)
هُوَ ٱللَّهُ ٱلَّذِى لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ‌ۖ عَـٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَـٰدَةِ‌ۖ
"Yeye ndiye Mwenye enzi Mungu ambaye, Anayajua yalofichikana na yaliyo dhahiri"
Mafundisho yote yanatokea kwake kwenye enzi ya siri na kufundishwa viumbe vyote, Na kila kiumbe kimefunikwa na ujuzi huu usiokua na mwisho, Jiulize swali la rahisi kwanini kila kiumbe kina dasturi ya kufanya maskani ya kukaa, Nani alomfundisha Ndege kujenga Nyumba yake na kutafuta Riziki, Na ana juaje wapi ataipata. Yeye huyo ndie Mollah Mjuzi mwenye kumfundisha huo ujuzi wake kila kiumbe, Akateremshiwa huyu akawa mwenye kuvumbua kutengeneza Ndege, Na mwengine akaunda Meli, Yule akavumbua kile na huyu akavumbua hichi, Na wote ukiwauliza wapi mumepata (Idea)hizi, imekuaje mpaka mkajua, ilikua vipi hata ukatengeneza gari, atakujibu mimi imenijia tu katika Akili yangu, Ikisha nikaandika kwenye karatasi ndio nikaanza kuifanayia kazi.
Nini Elimu?
Endelea part 2

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU (ALIIM) PART 2

Asalaam Aleiykum,

Naam nini  Elimu? Elimu ni (Gathering of Information) unakusanya huku na kule ikisha una hifadhi kichwani mwako, Na mwanzo wake imetokea kwenye hiyo (Source) na kutiwa katika Roho yako, Halafu tena wewe mwenyewe unafanya (Transfer)  kuipeleka kwenye akili, Na hapo ndio unaanza Ku(Shared) na watu wengine.
Lakini Ujuzi unaweza kubakia peke yako kama hutakai kuugeuza elimu, ikawa unajua mambo hayo ya siri pekee. Na anokupa Ukarim huo wa kujua hakuna Mwengine isipokua Yeye Mwenyewe (Yaa Aliim)Mjuzi wa kila kitu. Yeye ndie anaejua kila kitu kitokeacho Ardhini na Mbinguni, Kifanyike Baharini au Nchi kavu hakitokei bila ya Idhini yake au yeye kukijua.
Basi ikiwa hali yenyewe ndio iko hivyo ajijue kiumbe huko kufichaficha kwake na kufanya siri anajidanganya mwenyewe kwa mambo anayaofanya hali ya kuwa anajua fika Mollah wake anafahamu kila kitu.
Basi Niombeni kwa ajili ya Jina hili la (Aliim) ili mpate ujuzi zaidi wa kumfahamu Mollah wenu na Ulimwengu huu mnaoishi kwa Jumla, Ikiwa kwa Ukarimu wake kakufunzeni bila ya kumuomba, Nini Habari yenu nyinyi kama mtamuomba kwa dhati ya nafsi zenu, Basi kuanzia leo ikiwa mwenye kutaka kujua jambo la kheri utumie jina hili la Yaa Aliim kwa idadi nyingi kabisa huku unataja hilo kusudio lake uone faida zake. Na ulikumbuke jina hili kabla ya kulala, kuwa ukilala na jina hili, kuna mambo mawili yatatokezea ima utaamka ushapata jawabu au ufumbuzi, au utapewa habari kwa njia ya ndoto, Tunamuomba Mollah wetu atuzidishie ujuzi wa kumjua yeye na kumuabudu pasi na makosa, na huku tukitii amri zake.

Sunday, November 3, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(BASIRA) PART 1

Asalaam Aleiykum,

(Basiran) Mwenye kuona, Kabla ya kuendelea na jina hili wacha tujue tafauti ya kuona na kutizama, kutizama ni kitendo cha kuwepo mbali ukawa unaangalia, Kuona ni kitendo cha kuwepo karibu na ukawa unashuhudia, Na shahada ni jambo la yakini halina wasiwasi, kutizama inaweza kuwa yule ndie au siye huna uhakika, lakini kuona unasema moja kwa moja huyu ndie, hiyo ndio tafauti yake, Sasa hii sifa ya kuona imekusanya kila jambo linaonekana (in detail)kuona huku hakuna pazia wala kikomo, tunapo zungumza kuona huku si kule kuona kwa kawaida unavofahamu mimi na wewe, kuona huku kwenye kutajawa hapa kuna muhusu yule ambaye amejaalia huku kuona, kwa hiyo isije kukutuma akili yako ukadhani anaona kama unavoona wewe, hizo zako ni (tashbiha)umeletewa ili upate kutumia hilo jina la kuona kwa ajili ya maombi yako.
Usije ukazuka nakuanza kufikiri anaona kwa macho gani, usifananishe kabisa na kitu chochote, (Basira)Mwenye kuona, Kumekua kuona huko ni alama ya kuwepo na kukienea kila kitu, huna wakati au sehemu ikawa huonekani, ikiwa upo peke yako yeye wapili wako(Na kuna Method ya kulijua hilo ukifikia upeo fulani wa kufahamu utafahamishwa)Yeye ni Mwenye kukiona kila kila kitu kwa undani wake, hakuna chochote kiwezacho kuepuka kutoonekana na Mollah wako.
Yeye ndiye aliyekupa Roho na anakuona ndani ya hiyo Roho, Vipi linakua tukio lenyewe, Napenda ieleweke kuwa kitendo cha kuona ni (Temprory)katika matumizi ya macho, lakini ni cha kuendelea kwenye matumizi ya kiroho ndio maana ukilala unaendelea kuona ndoto zako, kwa hiyo inayoona ni hiyo Roho. Kwa hiyo hilo tendo limeitwa Jaala kwa sababu mara nyingi unaondoshewa hata katika hiyo Roho huoni kitu(Ndio unaamka na kusema leo nimelala fofofo, Kwa hiyo yeye ni mwenye kumiliki huko kuona, ndio maana akakwambia kwenye surat(Mulk 3-4)
مَّا تَرَىٰ فِى خَلۡقِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ مِن تَفَـٰوُتٍ۬‌ۖ فَٱرۡجِعِ ٱلۡبَصَرَ هَلۡ تَرَىٰ مِن فُطُورٍ۬ 
"Tizama katika Uumbaji wa Rahmani huoni tafauti (Yoyote)Rejesha macho (Yako utizame)jee unaona kosa"
ثُمَّ ٱرۡجِعِ ٱلۡبَصَرَ كَرَّتَيۡنِ يَنقَلِبۡ إِلَيۡكَ ٱلۡبَصَرُ خَاسِئً۬ا وَهُوَ حَسِيرٌ۬ 
"Tena rejesha macho(yako)mara nyingi zaidi, jicho lako litarudi hali ya kuwa limehasirika na umechoka"
Tizama, sababu Mbinguni  mbali, kwa hiyo nyanyua jicho utizame kama utaona tafauti yoyote, halafu ukaambiwa tazama tena na hali utarejesha jicho lako ukiwa hasarani, kwa sababu huko kuona kakupa yeye Mwenyewe uwezo huo , Na hizo mbingu saba kazitengeneza yeye, Basi kama unazitafuta.Endelea Part 2


MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(BASIRA)PART 2

Asalaam Aleiykum,

Kwanini kila ukitizama Mbinguni huoni tafauti na wala hizo Mbingu saba , Kwa sababu kuona kwetu viumbe kuna daraja au kikomo, ndio maana ndege ana kiasi chake, kuku ana kiasi chake, samaki ana upeo wake wa kuona, na yote hayo yamemilikiwa na mwenyewe mwenye huo Ufalme wa kuona, Lakini wewe Mwanaadamu kiumbe chake alokufanya Khalifa kwenye Ulimwengu huu kakupa zawadi ya kutizama isiyokua na kikomo.
Na ndio maana kwenye hiyo aya imetajwa tizama na wala sio angalia, Basi kafanye majaribio hayo ya kutizama ukimaliza kusoma, Nenda Nje angalia Mbingu au upande wowote usokua na kizuizi cha Miti au Majumba utajua siri hiyo ya upeo wako usokua na mwisho.
Picha au (Telescope)zinachukua (Still Image) kutokana na mafundisho yako, wewe unaona na kuweka kumbukumbu kutokana na uwezo na mafundisho ya Mollah wako, Yeye pekee ndio Mwenye huo uwezo na Ufalme wa Kuona, Na katika kuona huku kupo kwa aina mbili unaweza kuona Nje na ukipata mafundisho ya kuondoa pazia basi utaona na ndani(au mambo ya siri),  hivi sasa unaona lakini bado pazia limekufunika, labda mpaka siku ya kufa kwako ndio huondoshwa hilo pazia ukawa unaona pasi shaka na hicho unacho kiona, Kwa hiyo fanya hima katika kuona kwako ili utumie jina hili la Basira likuondoshee pazia na uyaone mambo makubwa makubwa yaliyo mazuri katika Ulimwengu huu.

Sunday, October 27, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(ALLAH)PART 1

Asalaam Aleiykum,

Tunaingia katika Darsa ya mzizi wa (Tawhid), Tunagusa nguzo nzima ya jengo la Dini, Tunakamata kitu muhimu sana na kama wewe utakua makini wa kufatilia na kufahamu darsa hii utatoka katika Bahari hii ya (Tawhid)huku umebeba Lulu na wala sio Chaza mwenyewe, Kwanza kabisa napenda kufahamisha hichi tunachokisoma ndio msingi mzima wa hiyo Sala unayosali, Makusudio yote ya Sala nzima yapo hapa. Kwa hiyo ukishindwa kuifahamu Darsa hii utakua umekosa kitu Adhimu sana, na vilevile ukifahamu basi usiwe mchoyo mwambie mwenzio au mfahamishe ili na yeye apate faida atakapo simamisha Sala awe na ufunuo fulani kwa ajili ya Mollah wake, kutokana na hali hiyo napenda uelewe huyo unompa taarifa hizi kila akizidi kukurubia kwa Mollah wake na wewe ukawa ndio sababu basi anazidi kukusukuma kwa darja na ujira mbele ya Mollah wako.
Katika Darsa hizi Inshaa Allah nitajaribu kuchukua majina matatu manne ili kukuonesha njia ili uifate na hayo mengine yalobakia ukayatafute zaidi, Kwa hiyo kila wiki tutakua tunalisoma jina moja na leo tunaanza Darsa hii na Jina la Allah, Katika darsa hii tunakaribishwa na aya 180 iliyomo kwenye sura ya Al-AAraf inayosema "وَلِلَّهِ ٱلۡأَسۡمَآءُ ٱلۡحُسۡنَىٰ فَٱدۡعُوهُ بِہَا‌ۖ"
"Na Mwenye enzi Mungu ana majina mazuri muombeni (Kwa)hayo"(Na mpaka mwisho wa aya inapomalizikia)
Katika hiyo aya yametajwa mambo mawili inatupasa tuyazingatie nayo la mwanzo Uzuri na la pili Ombeni, ukitumia viwili hivyo wewe mwenyewe utakua unaishi ndani ya huo uzuri ulokusudiwa, kutaka kulijua hilo kwanza tuiulize hiyo Sala, Wewe ni kitu gani, Nini Sala?.
Sala ni maombi Maalum unayopeleka kwa Mollah wako ukitumia hayo majina ya Mwenye enzi Mungu, Bila ya kutumia majina hayo utakua bado hujaitekeleza hiyo Sala, Utafanya Rukuu na Sijda lakini itakua bure mpaka upate jina zuri la kuweza kutumia katika vitendo hivyo. Na hapo ndio unakutana na majina 99 yenye (Kushubihisha)sifa za Mwenye enzi Mungu, Nimesema sifa ili usije ukaingia dhana ya kufikiri hivi ndivo alivo na haya ndio majina yake utakua umeingia hasarani, Mwenye enzi Mungu hana jina, Ila kwa kuwa anazungumza na wewe kwa kutumia lugha na kakufundisha kwa kutumia majina, basi hapana budi upewe sifa hizi nzuri(za mfano) Na imekua uzuri majina yenyewe kuwa 99, kutokana na tabia za viumbe tunajiuliza kwanini ikawa 99, lazima hesabu ikae sawa iwepo la 100, na hilo ndio lengo la kuwepo 99 ili ufanye jitihada kulifikia hilo moja ambalo halitajiki, halisomeki, halina lugha, halina mfano, na hilo ndilo lenye kuyakinisha uwepo wake Subhanna, Hilo halina(Shubiha) kama yalivyo hayo 99, huwezi kutoa mfano abadan.
Huwezi kulitamka, ila utakachoweza kufanya kutumia hayo majina 99 yakupeleke kwenye hilo moja, Na ambalo la karibu kabisa ni hili la (Allah) kama ilivotajwa katika sura ya (Ikhlas)قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ .
"Mwenye enzi Mungu ni Mmoja" hapo limetumika neno Allah na Mmoja kwa sentensi moja kuonesha mambo mawili, ili usije ukaanza kufikiri labda yuko vile au yuko hivi, Yeye katika Ufalme wake hana Mshirika. Endelea Part 2


MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(ALLAH)PART 2

Asalaam Aleiykum,

Sababu hana mshirika ndio ikatajwa Umoja kutokana na Allah ina mahusiano na Lugha, na neno la (Ahad)moja lina mashiko yale yale ya kwenye lugha, sasa usije kubabaika ukaona mbona kuna Allah na Ahad, kwanini ikawa viwili hivyo vipo pamoja, kwa sababu vyote vimo ndani ya hilo moja lisilo na lugha, lisoweza kutamkwa, kama Allah ilivokusanya hayo majina 99 hilo moja limekusanya vitu vyote katika Ulimwengu huu, ukiondosha hayo 99 hilo moja linabakia, Moja hili ndilo lenye(Wahid)lenye Ufalme huu wa Ulimwengu, Katika hilo moja sote ndipo tulipotokea na huko dipo tutakaporejea.
Basi kutokana na sababu hiyo, ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ.
"Mwenye enzi Mungu ndiye anastahiki kukusudiwa" 
Na ndio liwe kusudio lako kuyapita kwa maombi hayo yote 99 kufika kwenye hilo lenye dhati yenye yakini, Kila kusudio lako liwe kwa ajili yake, Nani Allahu Ahad? Allah Jina hili kusudio lake ni ule Utukufu Ulotawala Ulimwengu, Utukufu ulokizunguka kila kitu Mbingu na Ardhi(Allahu Akbar) kwa (Zahiri na Batini)Umefichika Utukufu huo na pia uko Wazi kwa Mwenye Akili kuona. Ahad ni Mmoja kwanini isiwe hivyo wakati unajua kila kilichomo katika Ulimwengu huu kimehusiana, wewe na Mti, wewe na Nyota na vyote vilivyomo kwenye Ulimwengu huu vina jinsi moja hakuna tafauti, Mpaka jani liloanguka kutoka kwenye mti au Ua lilochanua lina (Formula ya Dna)kama ulivo wewe, hiyo ndio Ahad, Muumbaji wake nini yeye pekee anokusudiwa na kila kilichomo kati Ulimwengu huu. Hiyo ndio Ahad au (Wahid) ilojificha, vipi sisi leo tutakijua au kulijua jambo linalo onekana na kufichikana kwa wakati mmoja, hatuwezi hata kufikiria upeo wa Allah ukoje, seuze kumfananisha na chochote.
لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ
"Hakuzaa wala kuzaliwa"
Ili kuondosha zana za labda kwamba pengine ni kiumbe ama ana hivi au vile au vyenginevo ndio akatwambia (Hakuzaa wala kuzaliwa) Kilo zaa ama kuzaliwa kinategemea mambo manne, Ardhi,Hewa,Maji,Moto, na vyote hivyo kaviumba yeye Allah vipi leo atakua katika hali ya kuvitegemea vitu hivyo.
وَلَمۡ يَكُن لَّهُ ۥ ڪُفُوًا أَحَدٌ 
"Na wala hana anayefanana naye hata Mmoja" Inaweza mtu kusema ndio hakuzaa wala hakuzaliwa lakini kafanana na (Mtume Fulani) Yeye ni (Formless)hana mfano na yoyote, ikiwa hakuzaa wala kuzaliwa vipi atakua na mfano na yoyote, Anaondosha dhana zenu za kumdhania dhania, Yeye ndiye Allah ambaye mnatakiwa kumuabudu na kumuomba kwa kutumia hayo majina mazuri mazuri, usije ukataka pesa (Ukasoma Tabaytayada-Surat-Massad)utapata moto baada ya pesa, omba kwa majina mazuri upate vilivyo vizuri, na munasaba wake usije ukaishia kwenye hayo majina mkaanza kuleta (Kushubihisha)na hayo majina ukawa unafanya (Image za kila aina) unatakiwa uende (Beyond) ya hizo dhana. Tunamuomba Mollah atufikishe katika hiyo(Tawhid)ya kumjua yeye kwa uwezo  alotupangia wa kumfahamu Mollah wetu Mpenzi.Amin

Sunday, October 20, 2013

LIJUE KUNDI LAKO PART 1

Asalaam Aleiykum,

Jee unataka kujua wewe kundi gani?, Na pia unataka kuelewa ukiwemo kwenye hilo kundi nini kitakufika? Basi hudhuria darsa hii kwa uangalifu mkubwa ili upate kuchagua kundi lako kwa busara. Huna huja ya kusubiri Kiyama au mpaka ufike kaburini, hapahapa Ulimwenguni utajijua mimi ni mtu wa kundi fulani, Na katika hayo makundi yapo ya aina tatu lakini mimi leo nitayazungumza mawili lile la mwanzo la hasara, na lile la pili kundi la kheri.
Kazi yangu mimi ni kukueleza kwanini upo katika kundi fulani na kwa sababu gani, Kitu cha mwanzo unachotakiwa ukifahamu kwamba huu Uhai wako wote ni mtihani, Na hakuna mtihani mkubwa Mwanaadamu unao mshinda kama kusahau, Madhara makubwa sana yanapatikana katika kipindi hichi cha kusahau,Dhanbi zote zinafanyika katika kipindi hicho, Shida zote zipo hapo kwenye kusahau, lau Wanaadamu tungepata theluthi moja ya kukumbuka, basi ungekua wewe Walii, wewe Mcha Mungu, lakini kinyume na hivyo kundi lako litakua la balaa tupu. Na ikiwa utajikuta umo katika kundi baya basi fanya jitihada ukurupuke utoke mbio, na kama umo kwenye kundi la kheri zidi kujipigilia misumari usije ukachomoka.
Sasa kwanza acha tuingie katika kundi la hasara, Kundi la adhabu, kundi la mateso ambalo limewafunika waja kwa moshi mkubwa wa moto wa shetani, Na ndani ya kundi  hili yaweza kuwa umo mwanzoni au katikati au umezama kabisa huonekani hata kichwa. Katika kundi hili la hasara limegubikwa na Matendo ya kusahau ambayo yanapambwa na Vitendo vya Shetani kama alivoahidi mwenyewe( Sad aya ya 82)قَالَ فَبِعِزَّتِكَ لَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ 
"Akasema Naapa kwa haki ya utukufu wako, Nitawapoteza wote"
Sasa vitendo vipi Shetani anakuingia mpaka kukupoteza, ni huko kusahau, anakuondoshea kukumbuka Ufalme wa Mwenye enzi Mungu, na ukisahau Ufalme huo unaingia hasarani, Hapa inabidi kabla sijavitaja vitendo vyenyewe mnipe nafasi nifafanue kidogo, Naomba kukumbusha hujakatazwa kuishi, sio kila kitu haramu, Maisha sio uteseke, ila kinachokutia hasarani ni kitendo cha kusahau, na jambo la mwanzo katika matendo nitayoyataja utashangaa kwamba si chengine ila Taji la Pesa, Pesa ndio Baba la ushaulivu, Penye pesa Mungu hakai kabisa, penye pesa anakaa shetani na kiburi chake, Pesa ni msukosuko, lakini cha ajabu sote tunafukuzia kundi la pesa, Jee wewe kundi gani? Hili la cheo na umaarufu, Hili la (Power and Security)Hili la kunyanyasa na kuwadharau viumbe wenzio, basi ikiwa ndio hivyo fanya haraka iwezekano umlainishe ngamia wako mifupa kwani itakua tabu kubwa kupita kwenye tundu ya shindano lazima utakwama kichwa(1).
La pili(2)Linalo tusahaulisha Ufalme wa Mwenye enzi Mungu ni Matamanio(Sex), hapa tena tukifika mtu ndio hukumbuki chochote, ndio tunalala kabisa, wewe jitizame ukiwa na mpenzi wako unamkumbuka Mollah wako, Hili la (sex) lina visa chungu nzima ndio linakupofua kabisa, na kama utatajiwa mambo ya akhera wakati huo unaweza kumnasa kibao mtu anakuharibia mambo yako ya starehe, inawezekana hapo kuna watu mia mbili wanakuangalia wewe, ukaambiwa watu wanakuona, ukageuka nakujibu wote hawanioni, hao wanadhani tu, na fanya uchunguzi utaona mambo yako yote unafanya kwa ajili ya hayo matamanio, hisani zote nyuma yake imejificha (Sex) chunguza utapata jawabu la jambo hilo.
Na Jambo la(3)Kutusahaulisha ni Macho, haya ndio hatari tupu, Mimi hapa nataja mambo katika maelfu ya majambo ili nitoe mwanga wa kusahau, Basi hata wewe Macho unanisahaulisha mimi, Ndio, kupitia kwangu ndio unaona Ulimwengu, mimi ndiye ninayekuonesha mipira na senema, Ngoma Na manyama nyama yanotingishika, vipi leo wewe utaweza kumkumbuka Mollah wako.
Jambo la (4)Mdomo mimi ndio (Chifu) wa mazungumzo, mimi ndio nasababisha unazungumza mambo yote ya watu ya kweli na ya uongo, vipi uwe katika vikao na ukaweza kumkumbuka Mollah wako.
Na la (5)Ni hilo shikio, kwanini likaitwa shikio, kwa sababu linashika habari za kila mtu, linasikiliza muziki wote, hili ndilo linalo kusahaulisha kwa utamu (wa ngoma kucheza ukizunguka raha zimezidi)za kumsahau Mollah wako, na takriban kuna mambo mengi ila mimi nimeyataja haya machache makubwa  ili nikujulishe mimi na wewe tumo kundi gani. Na kazi yangu mimi na yako ni kufanya jitihada za kuweza kutoka katika kundi hili la hasara, kama alivokumbusha Mwenye enzi Mungu katika sura ya Mujaddilah aya ya 19ٱسۡتَحۡوَذَ عَلَيۡهِمُ ٱلشَّيۡطَـٰنُ فَأَنسَٮٰهُمۡ ذِكۡرَ ٱللَّهِ‌ۚ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ حِزۡبُ ٱلشَّيۡطَـٰنِ‌ۚ أَلَآ إِنَّ حِزۡبَ ٱلشَّيۡطَـٰنِ هُمُ ٱلۡخَـٰسِرُونَ
"Amewatalia Shetani , Akawasahaulisha kumkumbuka Mwenye enzi Mungu, Hao ndio kundi la Shetani, Sikilizeni kwa hakika kundi la Shetani ndilo lenye Kuhasirika(Limo Hasarani)"
Ama kuhusu kundi la pili Endelea Part 2

LIJUE KUNDI LAKO PART 2

Asalaam Aleiykum,

Tunaingia katika kiwanja cha kundi la pili, Kundi hili lilojaa kheri tupu, Tunawauliza ili watupe habari wao wanafanya nini hata wakawemo kwenye kundi hili la kheri, Kundi liloridhiwa na Mwenye enzi Mungu.
Nini Wanafanya?
Wanafanya kitu Rahisi sana, Na wakati huo huo ni kigumu sana, Vipi kitakua rahisi na ugumu kwa wakati mmoja, wafanyacho wao ni kinyume cha kusahau, kama kundi la mwanzo wanasahau wao wanakumbuka, hiyo ndio tafauti yao, Na wewe ukifanya hilo la kukumbuka moja kwa moja unaingia katika kundi hili la kheri.
Sasa Ukumbuke Nini?
Kitu cha mwanzo kukumbuka ambacho ndio Sala yenyewe, Ndio Ibada yenyewe, Hata hao wanosali nyakati zote wanakifanya hicho hicho ni (Kulitaja Jina la Mwenye enzi Mungu) Kama alivotuamrisha katika (Sura ya Muzzamil aya ya 8)
وَٱذۡكُرِ ٱسۡمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلۡ إِلَيۡهِ تَبۡتِيلاً۬
"Litaje jina la Mollah wako, Na Ujitupe (Kwake)Kikweli(Kwa)(Devotion).
Kwanini ikawa Jina? Kwa sababu wewe mwanaadamu huna njia nyengine ya kumjua Mollah wako ila lazima upitie mlango huu wa jina, na Mlango huu wewe ndio ulopitia mwanzo kwa ajili ya mafundisho yako ya Majina, kutokana na Majina wewe ndio ukaona. (وَعَلَّمَ ءَادَمَ ٱلۡأَسۡمَآءَ كُلَّهَا)"Akamfundisha Adam majina ya vitu vyote"(Mpaka inapomalizikia aya) Nimesema unapitia kujua ndio ukaona, nina maana hii, Ingekua kuona ni kujua basi Malaika walipowekewa hivyo vitu wangevijua, Sasa kwanini hawakuvijua, ukijibu kwa urahisi utasema hawakufundishwa, na ukisema hawakufundishwa itabidi unipe  nafasi nifafanue zaidi.
Kutokana na Kadhia hiyo lazima kuwepo Mfundishaji, na hilo litakufanya uzame kwenye elimu ya (Tawhid)ili uweze kufahamu nasema nini kuhusiana na (Fumbo)hili la kufundishwa.
Katika kufundishwa au kujua lazima vipatikane vitu vitatu hivi: Anojua(Knower) Kinachojulikana(Known)Na Kisichojulikana(Unknowable) Hichi kisichojulikana ndio kinachokupa wewe uwezo wa kujua(Mollah wako), vipi leo utaweza kukiona hicho kisichoweza kuonekana, Ndio maana Nabii Musa a.s akaambiwa hutoweza kuniona, kwa hiyo na wewe ondoa itikadi yuko hivi au yuko vile usije ukapotosha Imani yako, Na kwa kuwa huwezi kumuona basi kwa Rehma zake kakupa Mbegu uipande ya kuweza kumjua, (Kwani hata ukipewa uwezo wa kumuona hutoweza kumjua) kwa hiyo chukua Mbegu hii ya kumjua ipande na hakuna anojua nini kitaota, unaweza kuota huo Mti wa majina 99 ambayo Insha Allah wiki zijazo nitakua nayapitia mawili matatu ili tupate maana yake na faida zake. 
Sasa Turejee nyuma katika lile kundi la kheri kundi la Mwenye enzi Mungu. Kundi hili la pili wameambiwa ili na nyinyi msisahau mkashughulika na mambo mengine basi nyie litajeni Jina la Mwenye enzi Mungu, Lishikeni kwa mtajo Jina langu, Nini kitatokea ikiwa mtadumu katika kunikumbuka kupitia moja katika majina hayo 99. Endelea Part 3



LIJUE KUNDI LAKO PART 3

Asalaam Aleiykum,

Litaje jina la Mollah wako, nini kimo ndani ya hilo jina, Elewa ndani ya hilo jina yamefichwa mambo, Ndani ya hilo jina utapata kumjua Mollah wako, Sio Kumuona, Na siri ya kujua haina mwisho, daima utaendelea kufunguliwa maajabu yaliyomo kwenye Ulimwengu huu kama wanasayansi wanavoendelea kuvumbua kila siku mambo mepya mepya, Basi na wewe kama umo katika kundi la Mwenye enzi Mungu unayo nafasi hiyo ikiwa utadumisha kulitaja na kulikumbuka jina la Mollah wako.
Kwani ikiwa utakua unalitaja pekee utaingia katika kusahau, utakua kama kasuku, inatakiwa lazima ulikumbuke kwa hamu kubwa na Shauku, kama unavokumbuka mbona sijasali, ni kitu kimoja ila umebadilisha jina, Sababu unakwenda kutaja hilo hilo jina la Mwenye Enzi Mungu. Jitupe kikamilifu, vipi kujitupa kikamilifu(Devotion) Unakumbuka wakati unashida au jambo baya litakutokea unavomuomba Mollah wako akuvue, hivyo ndio kujitupa, Na huko kujitupa isiwe kwa ajili ya kuonesha watu iwe siri baina ya wewe na Mollah wako, Na Mollah wako ni mwenye kukujua vipi ukweli wa mapenzi yako juu yake, usijali wengine kama wanajua wewe Mcha mungu au sio usiwajali kabisa hawapunguzi wala kuongeza chochote katika dini yako, Kujitupa kwenyewe lazima kuwe kwa Roho yako, Akili yako, na kila tendo lako kwa ajili ya kumkumbuka Mollah wako.Na hiyo ndio maana halisi ya( وَتَبَتَّلۡ إِلَيۡهِ تَبۡتِيلاً۬).
Na hayo ndio makundi mawili ama utakua kushoto au kuliani, lipo la tatu lakini nimeamua nisilizungumze kwa sababu watu wachache sana wanofanikiwa kubakia katika hilo kundi la katikati la (Ashab-Aaraf)ambalo hili kwa viumbe haliko na kwa Mollah wao halitaki.
Inshaa Allah tutalizungumza siku za mbele penye majaaliwa tukipata nafasi. Na mpaka sasa ushapata nafasi ya kujijua wewe mtu wa kundi gani, Basi ikiwa la hasara fanya haraka utoke kwani muda ushamalizika, umekaa siku nyingi katika kundi hilo la hasara, huna faida unayopata ila kuzidi kumsahau Mollah wako.
Na kama umo katika kundi la kheri basi zidisha mapenzi yako kwa Mollah wako na yeye atafungua pazia lake uone mambo hujapata kuyaona ya furaha katika Ulimwengu huu, Hapo utajua Mollah wako kakuridhia na wewe umemridhia, Na kuwemo katika kundi la Mwenye enzi Mungu ni mafanikio yasioelezeka.
Namuomba Mollah atujaalie sote tuwemo katika kundi la kheri aliloliridhia kwa uwezo wake Rahman. Amin.



Sunday, October 13, 2013

MUALIKO WA IMANI PART 1

Asalaam Aleiykum,

Kubali kuna kitu kinakusumbua, Kuna jambo hutaki kulisema, mbona umenyamaza kimya, unadhani nani atakusemea, Na hofu sasa imekuzidi Umri unasonga mbele, Na ndani ya moyo wako una yakini Imani haipo, hujui ufanye nini, Moyo unakutu, kipande hicho cha nyama umekijeruhi kwa mambo chungu nzima ya maasi nk, ndio maana Imani haina nafasi ya kukaa kabisa, Na una wasiwasi pengine hiyo ndio sababu dua hazipokelewi, unakhisi katika mambo ya Dini umekua muflis, hali hiyo inakufanya uwe dua zako mfano wa(Mtu aliye kwenda kwa Tajiri akaomba akopeshwe pesa ya kiwanja, na huyo tajiri akashangaa hii huyu utajenga vipi hiyo nyumba) Na hivi ndivo sote tunavo shangaa  katika jambo hili la Imani, Mbona kwangu haitokezi Imani hii, Hali yangu mimi najijua sina chochote moyoni, Nasoma Quraan, Nasali sana lakini ndani Kifuani(Empty).
Na baya zaidi nikishikwa na dhiki ima namtegemea Mganga au binaadamu mwenzangu kunitatulia matatizo yangu, sasa hapo iwapi Imani yangu, Na kibaya zaidi nakwenda kwa mganga eti kutafuta Utajiri hali najua huyo Mganga mwenyewe anataraji mie ndio nimpe pesa ili apate chakula chake, Inakua vipi namuamini Mganga kuliko Mollah wangu. Haya yote yanatukuta na tumo tunajiuliza lini na mimi nitaipata hiyo Imani niachane na mambo haya, lini nitaipata Imani iwe napeleka sala yangu kikamilifu, Nini tufanye tupate kutoka madhila, Tupate kusafisha Nyoyo zetu ili ije kukaa hiyo Imani.
Midamu umeuliza swali hili unajibiwa kuwa zipo mbinu na njia ukifanya unaweza kuipata hiyo Imani na zaidi ya Imani, ukifanya utafunguliwa mambo ambayo hujayategemea katika maisha yako, basi kama uko tayari chukua Zawadi ya aya iliyopo kwenye sura ya Rad aya ya 28. Inasemaje kuhusiana na kuipata hiyo Imani
Endelea Part 2

MUALIKO WA IMANI PART 2

Asalaam Aleiykum,

 ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَطۡمَٮِٕنُّ قُلُوبُهُم بِذِكۡرِ ٱللَّهِ‌ۗ أَلَا بِذِڪۡرِ ٱللَّهِ تَطۡمَٮِٕنُّ ٱلۡقُلُوبُ 
(Wao)Ni wale waloamini na zikatulia Nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenye enzi Mungu, Kwa kumkumbuka Mwenye enzi Mungu nyoyo hutulia.
Maneno yaliyotajwa hapo juu ni makubwa ikiwa unayajua maana yake kwa undani, lakini kama utapita juu juu hupati kitu, maana imefichika mpaka uwe katika wale wanotaka kujishughulisha kuitafuta.
Kwa wale wanotaka kujua maana basi nitafafanua kidogo ili nikujuze japo kwa uchache maana hiyo, Pata faida mbili hizi uzitumie kuipata hiyo Imani katika moyo wako ugeuke kuwa mtu mwengine kabisa.
Aya Imeanza kwa wale waloamini. Nini Kuamini? Kuamini ni kukubali bila ya pingamizi yoyote kwa lile uliloambiwa, Lakini hiyo haitoshelezi haja, ukikubali bila ya ushahidi (Shaka inabakia) Kwa sababu umeambiwa tu, inaweza kuwa kweli au uongo, unakua na mashaka huna utulivu, mara unafanya makosa, mara unatubu, mara unajiuliza pepo ipo, mara unajipa tamaa moto hakuna, hali hiyo inatokea moyoni mwako kila siku, Ndio maana mtu akikwambia katokea mjini unakubali, unamuamini, lakini ikiwa umemuagizia kitu hajakuletea unabaki na wasiwasi sijui kenda kweli au ananidanganya, lakini wakati huo ushaamini, inakua nusu umeamini nusu una shaka, kutokana na hali hiyo moyo wako unakua (Split)umegawika hauko kwenye Imani wala kwenye kukanusha.
Na unajiona hivi sasa Unakubali Mwenye enzi Mungu yupo, unaogopa adhabu zake, lakini bado unachungulia dirishani huku shaka imekushika, inaweza kuwa kweli inaweza kuwa uongo, Na kama kweli wacha Nisali, Na ikiwa uongo sijapata hasara yoyote, hivi ndio fikra zetu zilivo, zimejaa kila shaka, zimejaa mambo chungu nzima, Unapeleka dua bila ya tamaa, Sala yako inakua kama ya kulazimishwa.
Sasa kwenye aya hii unakumbushwa kitu muhimu sana na kama utakifanyia kazi unaweza kupata manufaa makubwa ya kuipata hiyo Imani. Wale wenye kuamini wanapata utulivu kwa kumkumbuka Mollah wao, Kukumbuka kuko kwa aina mbili, aina ya kwanza hii ni ngumu sana, wachache sana wanoweza kuipata hiyo Imani kupitia njia hii, na hiyo njia ya pili ni rahisi wengi wanaweza kuipata hiyo Imani kama watafata maelekezo yake.
Ama hii ya ugumu unatakiwa Uweke uwepo wa Mwenye enzi Mungu wakati wote (Presence) kila unapokuwepo fikra zako, na wewe mwenyewe uwe kwa Mollah wako, Ukiona Mti, Ukiona Ndege, Ukiona Mbingu, Ukiona Jua, Ukiona mwezi iwe unaviona vyote hivyo na huku unamkumbuka Mollah wako ndie aliyeviumba, ni Vigumu sana huwezi kumkumbuka Mollah kwenye Sala yako, utamkumbuka ukiona Mti, ndio maana nikasema hii ni ngumu wacha sasa tuitizame hiyo ilo rahisi ili tupate kuona kama tutaipata hiyo Imani.
Endelea Part 3

MUALIKO WA IMANI PART 3

Asalaam Aleiykum,

Kwanini utulivu haupatikani kwa sababu huna Imani, Na kama Imani haipo ndio utaona kila ukianza Ibada huyoo unatoka arijojo hurejei mpaka pale Ibada inapotaka kwisha, Sasa hii aina ya Pili ni ya Kutamka iwe taratibu au kwa sauti, hii kidogo ni Rahisi nikisema rahisi nina maana kama utaifanyia mazoezi labda unaweza kuipata hiyo Imani kwa kutumia njia hii ya kukumbuka Majina ya Mwenye enzi Mungu, Na majina hivyo hivyo yako mengine ni magumu kujihusisha nayo kwa njia ya kukumbuka, mie nimekuchagulieni jina hili la Rahisi pengine mtu anaweza kulizoea nalo ni kalima ya Tawhid(Laa Illa Illah Allah) Lifanyie mazoezi ya kulitaja na kulikumbuka Jina hili japo kwa siku nzima uone faida zake, na ukiweza kufanya kwa miezi mitatu utaona faida zake kubwa kubwa zinazopatikana katika jina hili la Mollah wako.
Nini Kinatokea?
Ukiweza kufanya moja katika mawili hayo nilokueleza utaanza kuona Utulivu unakushukia katika Moyo wako, Na huo Utulivu ukija unafatana na hiyo Imani,Na kwa ajili gani ukaja huo utulivu, kwa sababu Fikra zako haziwezi kumudu mambo mawili, Fikra zako zina (Focus)katika jambo moja tu, kwa hiyo Unapo mkumbuka Mollah wako una (Block) vyengine vyote, na ukivizuia hivyo vyengine ndipo unapata huo Utulivu,  Na utulivu ukija unageuka na kuwa Imani, Na Ukiipata Imani unakua ushafanikiwa, watu wanaweza kuchukua utu wako, wanaweza kuchukua heshima yako, wanaweza kuchukua cheo chako na mali yako, Lakini kitu kimoja hawawezi kukichukua ni hiyo Imani yako Adhimu uliyonayo. Na huo utulivu unatokea vipi, kihudhurie kisa hiki cha Mke na Mume(Walipokua wamepanda Jahazi wanasafiri mara kukazuka Kimbunga kikubwa, Yule Mke akaanza kupiga mayowe na kelele huku akimwambia Mumewe fanya maarifa tuokoke au tutakufa, Yule mume alipoona makelele yamezidi alichomoa jambia lake akamuekea mkewe shingoni, yule mke akanyamaza kimya, baada ya muda kupita yule bwana akaondosha kile kisu shingoni, Ikisha akamuuliza Mkewe nini kimetokea mbona umenyamza kimya, Yule bibi akajibu umenijia Utulivu sijapata kuuona, hofu yote ya kimbunga iliniondoka, ikawa naona kwa kimbunga nitakufa na kwa jambia nitakufa sasa kelele za nini. Yule Mume akasema na mimi  nimetulia moyo wangu nikawa najua aloleta Kimbunga hichi yeye ana uwezo akitaka tutakufa na akitaka tuokoke basi atakiondosha kimbunga kama alivofanya sasa hivi).
Na hiyo ndio Imani na utulivu ulokusudiwa, sio ya matatizo kidogo kukimbilia kwa waganga kuomba ufanikiwe, Unamtegemea Mtu mpaka unamuasi Mollah wako, Na sasa turejee nyuma katika yale mambo mawili ya (Dhikiri) au kukumbuka, Nini Kinatokezea?
Ukiweza kudumu kukumbuka, unakua unatumia (Energy)nguvu ambayo inatumika ukiwa kimya au ukitoa sauti, yote hayo ni sawa.
Unapotumia hizo nguvu unakutana na Sheria mbili moja hii inojulikana ya Ulimwengu ambayo inaitwa (Gravitation) na ile ya Pili ya Dunia ya pili ambayo ni ya (Sipiritual)inayoitwa(Levitation) pengine mtu ishawahi kukutokezea lakini huijui, na inatokezea mara nyingi kama umedumu kwenye Ibada au unasoma Quraan utahisi kama unapaa au unanyanyuka kutoka katika ardhi wakati umekaa, Na kama haijakutokezea fanya ujaribu upate faida ya kuijua hiyo (Levitation).
Aya Imesema wale wenye kuamini wanapata utulivu kwa kumkumbuka Mollah wao, Wanapoanza kukumbuka wanakua wanapeleka nguvu hizo za kukumbuka Moyoni, na kama kweli Mja anafanya kwa Ikhlas na kumuhitaji Mollah wake na kumkumbuka kila mara, Basi Mollah wao huwapa nguvu hii ya (Levitation)ikatokea Moyoni na kuwa utulivu wa Imani, Na ukipatikana huo utulivu nguvu hiyo haibakii hapo moyoni bali inapanda juu, Na hapo ndio unapatikana Ucha Mungu, Kwenye moyo umetulia haikubabaishi mali ya mtu, anotaka kukuroga, anotaka kukudhulumu,vyote hivyo havikushitu kabisa, Na  juu kwenye kichwa utaona furaha na mapenzi yanotokea kwenye huo moyo, na hapo tena ndio unaanza kutoa nuru moyoni mwako, wale wanofahamu wanajua sasa ushapanda daraja, unageuka wewe kuwa (Light)Laa illa illlah Allah inakungarisha mbali ya kukupa utulivu, na yoyote atokua karibu na wewe anapata hiyo nuru, macho yako yatakua yanangara kwa nuru ya Mwenye enzi Mungu.
Huo ndio Utulivu ambao unaambatana na Imani, Na hakuna kitu kizuri katika Ulimwengu huu kama Imani, Imani haibadiliki, Imani haisemi uongo, siku zote inatoa uhakika, siku zote iko vilevile haibadiliki, Na ikiingia Imani unakua ushashinda, usha (Surrender) na huo ndio Uislam, kwa hiyo fanya hima ujitahidi kualika hiyo Imani ije kwenye Moyo wako ili upate utulivu, fanya sana bidii ya kukumbuka, kwani ushasikiliza Mawaidha chungu nzima mambo yako vile vile, ushasomewa hadith mabuku kwa mabuku bado hujabadilika, basi hebu jaribu dawa hii yaweza kuwa ndio ponyo lako ukapata hiyo Imani, kinachotakiwa ni kukumbuka tu, sikwambii ni rahisi lakini inawezekana, na Imani ikiingia Moyoni kwako hapo ndio unaipata Sala sawasawa, Dua zako zinapokelewa kwa uhakika. Naomba Baraka za Mollah zitushukie sote tuwe na Imani.

Sunday, October 6, 2013

SIRI NDANI YA SIRI PART 1

Asalaam Aleiykum,

Katika Ulimwengu wa Elimu zipo za aina mbili, ya kwanza ni hii ya Dhahiri, na ya pili ni ile ya siri ilofichika ambayo leo tunaingia japo kidogo tupate kuchungulia tujue faida mbili tatu ambazo zitaweza kutujulisha mambo ya upande wa pili katika hiyo elimu isiyo onekana, Twende tukapajue pahala panapotokea  hiyo siri.
Nitaanza darsa yetu ya leo kwa msemo wa hekima ulo maarufu unaosema hivi"(KAVUNJA UKUTA WA WATU KWA HARUFU YA CHAKULA KITAMU)"
Msemo huu kwa nje unaonekana ni wa kawaida lakini ukizama ndani ya maana ya maneno haya utakutana na Siri kubwa ilofichika ndani ya Ukuta huo.(Kavunja Ukuta wa Watu) tujiulize kwanini akavunja?. Inaonesha labda hajui Mlango ulipo, Na hivi ndivo sote tulivo, hatujui mlango uwapi na kila mtu anapita akivunja ukuta wa mwenzie bila ya faida yoyote. 
Sasa Ukuta kwani una siri gani? Ukitaka kujua siri ya Ukuta kihudhurie kisa cha Msemezwa na Mwenye enzi Mungu Nabii Musa a.s na yule Mja alopewa elimu na Mollah wake kwa jina anaitwa Al Khidhir, Kisa chenyewe kilianzia pale walipofika katika mji wakaomba wapewe chakula na wale watu wa ule mji wakakataa, Ndipo Al Khidhir alipoukuta Ukuta unataka kuanguka akaujenga, Na Nabii Musa a.s akamwambia kwanini umeujenga, Al Khidhir akamjibu.
 وَأَمَّا ٱلۡجِدَارُ فَكَانَ لِغُلَـٰمَيۡنِ يَتِيمَيۡنِ فِى ٱلۡمَدِينَةِ وَكَانَ تَحۡتَهُ ۥ كَنزٌ۬ لَّهُمَا وَكَانَ أَبُوهُمَا صَـٰلِحً۬ا فَأَرَادَ رَبُّكَ أَن يَبۡلُغَآ أَشُدَّهُمَا وَيَسۡتَخۡرِجَا كَنزَهُمَا رَحۡمَةً۬ مِّن رَّبِّكَ‌ۚ
"Na ama(ule)Ukuta, Ulikuwa wa watoto wawili mayatima katika huo mji, Na chini yake(Ya Ukuta)kulikuwa na Hazina yao, Na Baba yao alikuwa (Mtu)mwema, kwa hivyo Mollah wako alitaka wafikie baleghe yao (Ili)wajitolee hazina yao, Hiyo ni Rehma inayotoka kwa Mollah wako" Mpaka inapomalizikia aya.
Naam hizo ndizo habari ya siri za Ukuta, Ukuta ni wenye kuficha Siri na Hazina za kila aina, Sasa huo wa kwenye Quraan ulikua ndio unaanguka ukajengwa, lakini kinyume na Ukuta wetu kenda mtu kuuvunja makusudi, Na sababu yake kubwa kuvunjwa ukuta huu ni hiyo harufu.
Nini Harufu? Nipeni nafasi nifanye ufafanuzi mdogo wa harufu ili tujue Harufu ina mahusiano gani na (Siri ndani ya Siri)pata faida hii uitie kibindoni iwe manufaa  kwako. Harufu kwa upande wa sayansi inapatikana kwenye pua na lazima ipatikane(molecules)kutoka katika hicho kitu ili upate kunusa hiyo harufu, lakini upande wetu wa (Mystic)katika fani ya Dini tunatambua harufu inatokea kulekule inapopatikana hizo (Senses)tano kubwa ikiwemo na kunusa, zipo za ziada lakini leo tutazitaja hizi tano ili kufupisha uchambuzi, nazo ni (Kuona, Kusikia, Kunusa, Kugusa na Kuhisi) yote hayo yanamilikiwa na hiyo Siri, Na hiyo Siri inakaa kwenye huo Mwili lakini cha ajabu haigusani na huo Mwili(Siri ndani ya Siri) Na kwenye hiyo siri ndipo inapopatikana Harufu, Na hiyo harufu yenyewe inaendelea kuwa siri, Mwana sayansi anaweza kulikamata Ua akatwambia kuna kitu kinatoka katika hilo ua kinaitwa (esters)kinatokea kwenye Ua ukimuuliza afafanue hajui ni kitu gani, au akujibu nini,ila atakwambia livamie upate (DNA)zake, lakini utapata (DNA)huwezi kupata harufu na hiyo ndio haja yako, kwa hiyo Utavunja ukuta wake lakini hupati harufu yake, Sasa ufanye nini kuijua hiyo harufu? Endelea part 2